656 Maumivu ya Majaribio ni Baraka Kutoka Mungu

1 Usivunjike moyo, usiwe dhaifu, Nitakufichulia. Njia ya kwenda kwa ufalme sio laini hivyo, hakuna kitu kilicho rahisi hivyo! Unataka baraka zije kwa urahisi rahisi. Leo kila mtu atakuwa na majaribio machungu ya kukumbana nayo, vinginevyo moyo wa upendo ulio nao Kwangu hautakuwa wenye nguvu zaidi na hutakuwa na upendo wa kweli Kwangu. Hata kama majaribu haya yanajumuisha hali ndogo tu, kila mtu lazima ayapitie; ni kwamba tu ugumu wa majaribu utakuwa tofauti kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine. Majaribu ni Baraka kutoka Kwangu, na ni wangapi kati yenu ambao huja mbele Yangu na kupiga magoti mkiomba baraka Zangu? Wewe daima huhisi kwamba maneno machache ya bahati huhesabika kama baraka Yangu, lakini huhisi kuwa uchungu ni moja ya baraka Zangu.

2 Wale wanaoshiriki katika uchungu Wangu bila shaka watashiriki utamu Wangu. Hiyo ni ahadi Yangu na baraka Zangu kwenu. Usisite kula na kunywa na kufurahia. Wakati giza litapotea hapa kutakuwa na nuru. Huwa kuna giza kuu kabla ya alfajiri; baada ya wakati huu kutakuwa na mwangaza zaidi polepole, na baadaye jua litainuka. Usiogope au kuwa mwepesi kutishwa. Watiifu na wanyenyekevu watapata baraka nyingi. Kanisani, mtasimama imara katika ushuhuda wenu Kwangu, mshikilie ukweli—haki ni haki na mabaya ni mabaya—wala msichanganye nyeusi na nyeupe. Mtakuwa vitani na Shetani na lazima mumshinde kabisa ili asiinuke kamwe.

3 Lazima mtoe kila kitu kulinda ushuhuda Wangu. Hili litakuwa lengo la matendo yenu, usisahau jambo hili. Lakini sasa, mmepungukiwa katika imani na uwezo wa kutofautisha vitu na ninyi daima hamuwezi kuelewa neno Langu na nia Zangu. Hata hivyo, usiwe na wasiwasi; kila kitu kinaendelea kulingana na hatua Zangu na wasiwasi huzaa shida tu. Shinda kwa muda zaidi mbele Yangu na usitilie maanani chakula na nguo kwa mwili wa asili. Tafuta nia Zangu mara nyingi, na Nitakuonyesha wazi ni nini. Pole pole utapata nia Zangu katika kila kitu, ili kwamba nitakuwa na njia ya kwenda ndani ya kila mtu bila vizuizi. Itauridhisha moyo Wangu na mtapata baraka pamoja na Mimi milele na milele!

Umetoholewa kutoka katika “Sura ya 41” ya Matamko ya Kristo Mwanzoni katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 655 Kile Anachokamilisha Mungu ni Imani

Inayofuata: 657 Majaribu Yanahitaji Imani

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp