Christian Video "Bwana Anabisha" | Welcoming the Second Coming of the Lord Jesus (Skit)

03/06/2020

Igizo fupi la kuchekesha Bwana Anagonga linaelezea namna ambavyo, katika siku za mwisho, Bwana anagonga kwenye mlango wa mioyo yetu kwa maneno Yake, na kwamba wanawali wenye hekima wanaweza kusikia sauti ya Mungu na kula karamu na Mwanakondoo.

Mchungaji Chang Shoudao amekuwa wakati wote akingoja kurudi kwa Bwana, lakini wakati Ndugu Zhei anamshuhudia kwamba Bwana tayari amerudi, kwa ubishi anang'ang'ania fikra na mawazo yake, akiamini kwamba Bwana atarudi juu ya wingu, na akiacha mlango wa moyo wake umefungwa dhidi ya njia ya kweli. Safari hii, hata hivyo, Ndugu Zhen anajadili pamoja naye vifungu vya Maandiko vinavyohusiana na kurudi kwa Bwana, na anagundua kuwa Biblia ina unabii kwamba katika siku za mwisho Bwana atarudi kwa siri, katika mwili wenye nyama, ili kuongea maneno mapya na kumtakasa mwanadamu, na baada ya hapo tu ndipo atatokea wazi kulipa wema na kuadhibu uovu. Wakati huohuo, anafikia kuelewa maana ya kweli ya Bwana kugonga kwenye milango yetu, na kwamba cha muhimu katika kukaribisha kurudi kwa Bwana ni kuweza kusikia sauti ya Mungu. Mwishowe anaposikia sauti ya Mungu katika neno la Mwenyezi Mungu, hatimaye anafungua mlango wa moyo wake na anakaribisha kurudi kwa Bwana.

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp