246 Mungu Anawataka Watu Zaidi Wapate Wokovu Wake
1
Mungu anatumaini wengi watachunguza kwa makini
wakikabiliwa na maneno ya Mungu na kazi Yake,
wakiendea maneno haya muhimu kwa moyo wa kimungu.
Usifuate nyayo za wale ambao wanaadhibiwa.
Msiwe kama Paulo, aliyejua wazi njia ya kweli
bali alikataa makusudi, akapoteza sadaka ya dhambi.
Kubali kazi Yake mpya, pokea ukweli Anaotoa.
Kisha unaweza kupata wokovu wa Mungu!
2
Mungu hawataki zaidi waadhibiwe, bali atumaini zaidi waokolewe,
ili watu wengi kushika kasi, zaidi wafuate nyayo Zake,
ili zaidi waingie katika ufalme wa Mungu!
Kubali kazi Yake mpya, pokea ukweli Anaotoa.
Kisha unaweza kupata wokovu wa Mungu!
3
Mungu hutendea wote haki, bila kujali umri wako,
bila kujali jinsi ulivyo mkuu, au mateso ulostahimili.
Tabia Yake inabaki milele haibadiliki,
yenye haki mbele ya mambo haya.
Hampendelei yeyote, bali hujali kama mwanadamu akikubali
ukweli Wake na kazi mpya, akitupa vingine vyote mbali.
Kubali kazi Yake mpya, pokea ukweli Anaotoa.
Kisha unaweza kupata wokovu wa Mungu!
Kubali kazi Yake mpya, pokea ukweli Anaotoa.
Kisha unaweza kupata wokovu wa Mungu!
Umetoholewa kutoka katika Hitimisho wa Mifano Maarufu ya Adhabu kwa Kumpinga Mwenyezi Mungu