807 Unapaswa Kumwiga Petro

1 Punde tu anapotajwa Petro, kila mtu anajawa na sifa. Petro alikuwa na busara nyepesi, alipewa akili asili, kupendwa sana kutoka utotoni na wazazi wake; baada ya kukua, hata hivyo, akawa adui zao, kwani daima alitaka kunijua, na hii ilimfanya kuwapuuza wazazi wake. Hii ilikuwa kwa sababu, kwanza kabisa, aliamini kwamba mbingu na dunia na mambo yote yako mikononi mwa Mwenyezi, na kwamba mambo yote mazuri yanatoka kwa Mungu na yanakuja moja kwa moja kutoka Kwake, bila kupitia usindikaji wowote na Shetani. Na mfano usiofaa wa wazazi wake kuwa kama kikwazo, hii ilimwezesha kwa urahisi kutambua upendo na huruma Yangu, na hivyo kuchochea ndani yake hamu kubwa zaidi ya kunitafuta.

2 Alikuwa makini sana sio tu kula na kunywa maneno Yangu, lakini hata zaidi kufahamu nia Zangu, na daima alikuwa na busara na tahadhari katika mawazo yake, kwa hivyo daima alikuwa mwerevu kwa makini ndani ya roho yake, na hivyo aliweza kuniridhisha kwa vyote alivyofanya. Kwa maisha ya kawaida, alikuwa makini kuunganisha katika maisha masomo ya wale walioshindwa katika siku za nyuma ili kujichochea mwenyewe kufanya juhudi kubwa zaidi, akihofia sana kwamba anaweza kuanguka ndani ya nyavu za ushinde. Alikuwa pia makini kupata imani na upendo wa wote ambao kupitia enzi nyingi walikuwa wamempenda Mungu. Kwa njia hii, aliharakisha maendeleo ya ukuaji wake sio tu kwa masuala hasi, lakini hasa kwa masuala chanya, hadi akawa katika uwepo Wangu mwanadamu pekee aliyenijua bora kabisa.

3 Kwa sababu hii, si vigumu kuwazia jinsi alivyoweza kuweka yote aliyokuwa nayo mikononi Mwangu, kukosa kuwa tena bwana wake mwenyewe hata kwa kula, kuvaa, ama mahali aliishi, lakini alifanya kuniridhisha kwa mambo yote msingi ambao alifurahia fadhila Yangu. Mara nyingi Nilimweka chini ya jaribio, ambalo hakika lilimwacha nusu mfu, lakini hata katikati ya haya mamia ya majaribio, hakupoteza imani Kwangu hata mara moja ama kusikitishwa nami. Hata Niliposema nimemtupa kando, hakufa moyo wala kukata tamaa, lakini aliendelea kama mbeleni akitekeleza kanuni zake ili kunipenda kwa njia ya vitendo. Kwa sababu ya uaminifu wake mbele Yangu, na kwa sababu ya baraka Zangu juu yake, amekuwa mfano mwema na mfano wa kuigwa kwa mwanadamu kwa maelfu ya miaka. Je, huui si hasa mfano unaopaswa kufuata?

Umetoholewa kutoka katika “Sura ya 6” ya Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 806 Matokeo ya Kutojua Tabia ya Mungu

Inayofuata: 808 Petro Alimjua Mungu Vyema Zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp