Nyongeza: Sura ya 1

Ninachotaka mfanye si nadharia isiyo dhahiri na tupu ambayo Naizungumzia, wala si kitu cha kutofikirika na akili ya mwanadamu au kisichoweza kutimizwa na mwili wa mwanadamu. Ni nani anayeweza kuwa mwaminifu kabisa ndani ya nyumba Yangu? Na ni nani anayeweza kutoa nafsi yake yote ndani ya ufalme Wangu? Kama si ufunuo wa mapenzi Yangu, je, mngeweza kujitilia matakwa ambayo mnaridhisha moyo Wangu? Hakuna yeyote ambaye amewahi kuufahamu moyo Wangu, na hakuna yeyote ambaye amewahi kutambua mapenzi Yangu. Ni nani amewahi kuuona uso Wangu au kuisikia sauti Yangu? Petro alifanya hivyo? Au Paulo? Au Yohana? Au Yakobo? Ni nani amewahi kuvishwa na Mimi, au kumilikiwa na Mimi, au kutumiwa na Mimi? Ijapokuwa mara ya kwanza Nilipoupata mwili ilitendeka ndani ya uungu, mwili ambao Nilijivika haukujua mateso ya mwanadamu, kwa sababu Sikuwa mwili katika mfano, kwa hiyo haingeweza kusemwa kwamba mwili ulifanya mapenzi Yangu kikamilifu. Ni wakati tu ambapo uungu Wangu unaweza kufanya jinsi Ningetenda na kunena jinsi Ningenena katika nafsi ya ubinadamu wa kawaida, bila kipingamizi au kizuizi, ndipo inaweza kusemwa kwamba mapenzi Yangu yamefanyika katika mwili. Kwa vile ubinadamu Wangu wa kawaida unaweza kuukinga uungu Wangu, hivyo lengo Langu la kuwa mnyenyekevu na Aliyefichika linatimizwa. Wakati wa hatua ya kazi katika mwili, ingawa uungu unatenda moja kwa moja, si rahisi kwa watu kuona vitendo kama hivyo, ambalo ni kwa sababu tu ya maisha na vitendo vya ubinadamu wa kawaida. Kupata mwili huku hakuwezi kufunga kwa siku 40 kama kupata mwili kwa mara ya kwanza, lakini Anafanya kazi na kunena kwa kawaida, na ingawa Anafichua siri, Yeye ni wa kawaida kabisa; Yeye ni wa kawaida kabisa; sivyo jinsi watu wanavyodhani—sauti Yake sio kama radi, uso Wake haumemetuki kwa nuru, na mbingu hazitetemeki Anapotembea. Ingelikuwa hivyo, basi hakungekuwa na hekima Yangu yoyote katika jambo hili, na haingewezekana kumwaibisha na kumshinda Shetani.

Wakati ambapo Ninaonyesha uungu Wangu chini ya ulinzi wa ubinadamu wa kawaida, Ninatukuzwa kabisa, kazi Yangu kuu inatimizwa, na hakuna chochote kinachosababisha matatizo yoyote. Hii ni kwa sababu lengo la kupata mwili Kwangu hasa ni kuwaruhusu wale wote wanaoniamini wayaone matendo ya uungu Wangu katika mwili, na kumwona Mungu Mwenyewe wa vitendo, hivyo kuondoa katika mioyo ya watu nafasi ya Mungu asiyeonekana na Asiyeshikika. Kwa kuwa Nala, Najivisha nguo, Nalala, Naishi, na kutenda kama mtu wa kawaida, kwa kuwa Nazungumza na kucheka kama mtu wa kawaida, nami Nina mahitaji ya mtu wa kawaida, na pia Nina dutu ya uungu kamili, Ninaitwa “Mungu wa vitendo.” Jambo hili si dhahania, nalo ni rahisi kuelewa; linaweza kuonekana katika sehemu ambayo kiini cha Kazi Yangu kimo, na katika awamu ya kazi ambamo lengo Langu liko. Kufichua uungu Wangu kupitia kwa ubinadamu wa kawaida ni lengo kuu la kupata mwili Kwangu. Si vigumu kuona kwamba kiini cha kazi Yangu kiko katika sehemu ya pili ya enzi ya hukumu.

Ndani Yangu, hakujawahi kuwa na maisha ya binadamu au dalili ya binadamu. Maisha ya binadamu hayajawahi kushikilia nafasi ndani Yangu, na hayajawahi kukomesha ufichuzi wa uungu Wangu. Hivyo, kadri Mtu anavyoionyesha sauti Yangu mbinguni na mapenzi ya Roho Wangu, ndivyo Anavyoweza kumwaibisha Shetani zaidi, na ndivyo inavyokuwa rahisi zaidi kufanya mapenzi Yangu katika ubinadamu wa kawaida. Hili pekee limemshinda Shetani, na tayari Shetani ameaibishwa kabisa. Ingawa Nimefichika, hili halizuii matamshi na vitendo vya uungu Wangu—ambalo linatosha kuonyesha kwamba Nimekuwa mshindi, na Nimetukuzwa kabisa. Kwa kuwa kazi Yangu katika mwili haina kipingamizi, na kwa kuwa Mungu wa vitendo sasa Ana nafasi ndani ya mioyo ya watu na Amekita mizizi ndani ya mioyo yao, inathibitishwa kabisa kwamba Shetani ameshindwa na Mimi. Na kwa kuwa Shetani hawezi kufanya lolote zaidi miongoni mwa wanadamu, na ni vigumu kuifunda sifa ya Shetani katika mwili wa mwanadamu, mapenzi Yangu yanaendelea bila kipingamizi. Maudhui ya kazi Yangu, hasa, ni kuwasababisha watu wote wayatazame matendo Yangu ya ajabu na kuuona uso Wangu halisi: Mimi si asiyeweza kufikika, Siendi juu sana katika anga, Mimi si asiye na umbo wala sura maalum. Mimi si asiyeonekana kama hewa, wala si kama wingu linaloelea, linaloweza kupeperushwa kwa urahisi; badala yake, ingawa Naishi miongoni mwa wanadamu, na kupitia utamu, uchachu, uchungu, na ukali miongoni mwa wanadamu, mwili Wangu unatofautiana kimsingi na ule wa mwanadamu. Watu wengi hushindwa kushirikiana na Mimi, lakini wengi pia hutamani kushirikiana na Mimi. Ni kana kwamba kuna siri kubwa, zisizoeleweka ndani ya Mungu aliyepata mwili. Kwa sababu ya ufunuo wa wazi wa uungu, na kwa sababu ya ulinzi wa kuonekana kwa mwanadamu, watu hukaa mbali sana nami, wakiamini kwamba Mimi ni Mungu mwenye huruma na upendo, lakini pia wanauogopa uadhama na ghadhabu Yangu. Hivyo, ndani ya mioyo yao, wanataka kuzungumza nami kwa dhati, lakini hawawezi kufanya watakavyo—kile ambacho mioyo yao inatamani, wanakosa nguvu. Hivyo ndivyo zilivyo hali za kila mtu katika hali hii—na kadri watu walivyo namna hii, ndivyo thibitisho la ufunuo wa hali mbalimbali za tabia Yangu lilivyo kuu zaidi, hivyo kutimiza lengo la watu kujua kuhusu Mungu. Lakini hili ni la baadaye; kilicho muhimu ni kuwafanya watu wayajue matendo Yangu ya ajabu kutokana na shughuli za mwili Wangu, zikiwasababisha kujua dutu ya Mungu: Kama wanavyodhani watu, Mimi si asiye wa kawaida na wa mwujiza; badala yake, Mimi ni Mungu wa vitendo aliye wa kawaida katika mambo yote. Nafasi “Yangu” katika dhana za watu imeondolewa, na wao huja kunijua kwa kweli. Ni wakati huo tu ndipo Mimi huchukua nafasi Yangu ya kweli katika akili zao.

Mbele ya watu wote, Sijawahi kufanya tu kitu chochote cha ajabu ambacho kimethaminiwa na watu, bali pia Mimi ni wa kawaida mno; Siwaruhusu watu kuona chochote kilicho na dalili ya Mungu katika mwili Wangu kwa makusudi. Lakini kwa sababu ya maneno Yangu, watu wanashindwa kabisa, na wanautii ushuhuda Wangu. Ni hivyo tu ndivyo watu huja kujua, bila wasiwasi, Mimi niliye katika mwili juu ya msingi wa kuamini kabisa kwamba Mungu yupo kweli. Kwa njia hii, ufahamu wa watu kunihusu huwa halisi zaidi, dhahiri zaidi, na hautiwi doa hata kidogo kwa mwenendo wao mzuri; yote ni matokeo ya uungu Wangu kutenda moja kwa moja, ukiwapa watu ufahamu mkuu zaidi wa uungu Wangu, kwani uungu pekee ndiyo sura halisi ya Mungu na sifa ya asili ya Mungu—watu wanapaswa kuona hili. Nitakacho ni maneno, vitendo, na matendo yaliyo katika uungu—Sijali kuhusu maneno na vitendo katika ubinadamu. Lengo Langu ni kuishi na kutenda katika uungu—Sitaki kukita mizizi na kuchipua katika ubinadamu, Sitaki kuishi katika ubinadamu. Je, mnaelewa Ninachosema? Ijapokuwa Mimi ni mgeni katika ubinadamu, Sitaki hili; Natenda katika uungu kamili, na ni kwa njia hii tu ndiyo watu wanaweza kuufahamu uso Wangu halisi vizuri zaidi.

Iliyotangulia: Sura ya 9

Inayofuata: Sura ya 10

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp