Kutazama Kuonekana kwa Mungu katika Hukumu na Kuadibu Kwake

Kama mamilioni ya watu wanaomfuata Bwana Yesu Kristo, tunafuata sheria na amri za Biblia, kufurahia neema tele ya Bwana Yesu Kristo, na kukusanyika pamoja, kuomba, kusifu, na kuhudumu kwa jina la Bwana Yesu Kristo—na haya yote sisi tunafanya chini ya utunzaji na ulinzi wa Bwana. Mara nyingi, sisi tunakuwa dhaifu, na mara nyingi sisi tunakuwa pia wenye nguvu. Tunaamini kwamba matendo yetu yote yanaambatana na mafundisho ya Bwana. Na basi, ni dhahiri kwamba sisi pia tunajiamini kuwa kwenye njia ya kufanya mapenzi ya Baba aliye mbinguni. Tunatamani kurudi kwa Bwana Yesu, kushuka Kwake kwa utukufu, mwisho wa maisha yetu hapa duniani, kuonekana kwa ufalme, na kila kitu kama kilivyotabiriwa katika Kitabu cha Ufunuo: Bwana anakuja, Analeta maafa, Anawathawabisha walio wema na kuwaadhibu walio waovu, na Anawachukua wale wote wanaomfuata na kukaribisha kurudi Kwake juu kumlaki angani. Wakati wowote tunapowaza kuhusu haya, hatuwezi kujia kwa kujawa na hisia na kujawa na shukrani kwa kuwa tulizaliwa siku za mwisho na tuna bahati nzuri ya kushuhudia kuja kwake Bwana. Ingawa tumepitia mateso, tumepata badala yake “utukufu mkubwa na wa daima ambao unazidi kuwa mkuu kabisa.” Ni baraka iliyoje! Hamu hii yote, na neema inayotolewa na Bwana hutufanya kuingia kwenye maombi kwa kawaida, na kutufanya tuwe na bidii zaidi katika kukusanyika pamoja. Labda mwaka ujao, labda kesho, na tena, labda kwa muda mfupi zaidi kuliko binadamu anavyoweza kufahamu, Bwana atashuka ghafula, akionekana kati ya kundi la watu ambao wamekuwa wakimsubiri kwa shauku kubwa. Tunaharakisha ili tuwe mbele ya wenzetu, hakuna anayetaka kubaki nyuma, yote kwa ajili ya kuwa kundi la kwanza la kutazama kuonekana kwa Bwana, ya kuwa miongoni mwa wale watakaonyakuliwa kwenda mbinguni. Tumetoa kila kitu, bila kujali gharama, kwa ajili ya kuwadia kwa siku hii, wengine wakiacha kazi zao, wengine wakiacha familia zao, wengine wakiacha ndoa zao, na baadhi hata wakitoa akiba zao zote. Ni vitendo vya upendo usio na ubinafsi kweli! Uaminifu na utiifu kama huu bila shaka hata unashinda ule wa watakatifu wa nyakati za zamani! Kwa kuwa Bwana anampa neema yeyote yule ambaye Anamtaka, na kumwonyesha huruma yeyote ambaye Anataka, vitendo vyetu vya kujitolea na vya kujitumia, tunaamini, vimetazamika machoni Pake kitambo. Kwa hivyo, pia, sala zetu za dhati zimeyafikia masikio Yake, na tunaamini kuwa Bwana atatulipa kwa ajili ya kujitolea kwetu. Aidha, Mungu alikuwa mwenye neema kwetu kabla hajauumba ulimwengu, na baraka na ahadi Ambazo ametupa hakuna anayeweza kuziondoa. Sote tunapanga kwa ajili ya siku za usoni, na bila shaka tumefanya kujitolea na kujitumia kwetu kuwa vitu vya madai au raslimali za mabadilishano kwa ajili ya kunyakuliwa ili kupatana na Bwana hewani. Isitoshe, bila kusita hata kidogo, sisi tumejiweka kwenye kiti cha enzi cha siku za baadaye, ili tutawale mataifa na watu wote kwa ujumla, ama kutawala kama wafalme. Yote haya, sisi huchukulia kama jambo la lazima, kama kitu cha kutarajiwa.

Tunadharau wale wote walio kinyume na Bwana Yesu; wote wataishia kuangamizwa. Nani aliwaambia wasiamini kwamba Bwana Yesu ni Mwokozi? Bila shaka, kuna nyakati ambapo tunamwiga Bwana Yesu katika kuwa na huruma kwa watu wa dunia, kwa kuwa hawaelewi, na ni sahihi kwamba tuwe wavumilivu na kuwasamehe. Kila kitu tufanyacho ni kwa mujibu wa maneno ya Biblia, kwani kila kitu ambacho hakifuatani na Biblia ni chenye kufuata imani tofauti na ni uzushi, Imani ya aina hii imekita mizizi katika akili ya kila mmoja wetu. Bwana wetu yumo katika Biblia, na tusipoiacha Biblia hatutamwacha Bwana; tukiishi katika kanuni hii, tutapata wokovu. Tunahimizana, kila mmoja akimsaidia mwenzake, na kila wakati tunapokusanyika pamoja tunatumaini kwamba kila jambo tunalosema na kufanya ni sawa na mapenzi ya Bwana, na litakubaliwa na Bwana. Licha ya uhasama mkali ulioko kwenye mazingira yetu, mioyo yetu imejaa furaha. Tunapowaza kuhusu baraka hizi tunazoweza kupata kwa urahisi, je, kuna kitu ambacho hatuwezi kukitenga kando? Je, kuna kitu ambacho hatuko tayari kuachana nacho? Yote haya hayapingwi, na haya yote yako chini ya macho angalifu ya Mungu. Sisi, wachache hawa wa wahitaji ambao wameinuliwa kutoka kwenye jaa, ni sawa na wafuasi wote wa kawaida wa Bwana Yesu, wenye ndoto za kunyakuliwa, kubarikiwa, na kutawala mataifa yote. Upotovu wetu umewekwa wazi machoni pa Mungu, na matamanio na uchoyo wetu vimeshutumiwa machoni pa Mungu. Hata hivyo, haya yote yanatokea kwa njia isiyo ya kushangaza, na tena kwa mantiki sana, na hakuna hata mmoja wetu anayejiuliza kama matamanio yetu ni sahihi, sembuse hata mmoja wetu anayeshuku usahihi wa kila kitu tunachoshikilia. Ni nani anayeweza kujua mapenzi ya Mungu? Ni nini hasa njia hii ambayo mwanadamu anaitembea, hatujui kutafuta au kuchunguza, sembuse hata kujishughulisha nayo. Kwa maana sisi tunajali tu kuhusu kama tutaweza kunyakuliwa, kama tunaweza kubarikiwa, kama kuna pahali tumetengewa katika ufalme wa mbinguni, na kama sisi tutaweza kupata mgawo wa maji ya mto wa uzima na matunda ya mti wa uzima. Je, si ni kwa ajili ya kupata vitu hivi ndiyo tunamwamini Bwana na kuwa wafuasi Wake? Dhambi zetu zimesamehewa, tumetubu, tumekunywa kikombe kichungu cha diavi, na tumeuweka msalaba migongoni mwetu. Ni nani anayeweza kusema kwamba Bwana hatapendezwa kukubali gharama ambayo tumelipa? Ni nani anayeweza kusema kuwa hatujatayarisha mafuta ya kutosha? Hatungependa kuwa wale mabikira wapumbavu, ama mmoja wa wale ambao wameachwa. Aidha, tunaomba mara kwa mara, tukimwomba Bwana atuepushe kutokana na kudanganywa na Kristo wa uongo, kwa maana imeandikwa kwenye Biblia: “Wakati huo mtu akiwaambia, Tazama, Kristo yupo hapa, au yuko kule msisadiki. Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule” (Mathayo 24:23-24). Sisi sote tumeweka mistari hii ya Biblia kwenye kumbukumbu, tunaijua vyema sana, na tunaiona kama hazina ya thamani, kama hati ya muamana ambayo inaamua ikiwa tunaweza kuokolewa au kunyakuliwa …

Kwa maelfu ya miaka, wanaoishi wamefariki, wakibeba tamaa zao na ndoto zao, lakini kuhusu iwapo wameenda kwa ufalme wa mbinguni, hakuna anayejua kwa hakika. Wafu wanarudi, wakiwa wamesahau hadithi zote zilizowahi kutokea wakati mmoja, na bado wanafuata mafundisho na njia za mababu. Na kwa njia hii, kadiri miaka inavyosonga na siku zinavyosonga, hakuna anayejua ikiwa Bwana wetu Yesu, Mungu wetu, anakubali kweli kila jambo tunalofanya. Yote tuwezayo kufanya ni kutarajia tu kuwa na matokeo na kubashiri kuhusu yale yote ambayo yatakuja kutokea. Hata hivyo Mungu amenyamaza kimya siku zote, hajawahi kututokea, wala hazungumzi nasi. Na kwa hivyo, kwa kufuata Biblia na kulingana na ishara tunahukumu mapenzi na tabia ya Mungu kwa hiari yetu. Sisi tumezoea ukimya wa Mungu; tumekuwa na mazoea ya kupima usahihi na makosa ya mwenendo wetu kwa kutumia njia zetu wenyewe za mawazo: tumekuwa na mazoea ya kutegemea elimu yetu, dhana, na maadili yetu badala ya matakwa anayotuwekea Mungu; tumekuwa na mazoea ya kufurahia neema ya Mungu; tumekuwa na mazoea ya Mungu kutoa msaada wakati sisi tunahitaji msaada huo; tumekuwa na mazoea ya kunyosha mikono yetu kwa Mungu ili tupate mambo yote, na kumuagiza Mungu; na pia tumekuwa na mazoea ya kufuata kanuni, kutotilia maanani jinsi Roho Mtakatifu hutuongoza; na, hata zaidi, tumekuwa na mazoea ya siku ambazo sisi ni bwana zetu wenyewe. Tunamwamini Mungu wa namna hii, ambaye hatujawahi kukutana naye uso kwa uso. Maswali kama namna tabia Yake ilivyo, kile Anacho na Alicho, mfano Wake ulivyo, kama tutamjua ama hatutamjua wakati Atakaporudi, na kadhalika—haya yote hayana umuhimu. Jambo la muhimu ni kuwa Yeye yupo mioyoni mwetu na kuwa tunamsubiri, na inatosha kuwa tunaweza kufikiria kwamba Yuko jinsi hii au jinsi ile. Tunathamini imani yetu, na kuthamini hali yetu ya kiroho. Tunaona kila kitu kikiwa kama samadi, na kukanyaga vitu vyote kwa nyayo zetu. Kwa sababu sisi ni wafuasi wa Bwana mwenye utukufu, bila kujali jinsi safari yetu ilivyo ndefu na ngumu, bila kujali shida na hatari zinazotukumba, hakuna kitu kitakachosimamisha nyayo zetu tunapomfuata Bwana. “Mto safi wa maji ya uhai, ung’aao kama kioo, ulitoka katika kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo. Na kila upande wa mto huo, palikuwa na mti wa uzima, uzaao matunda ya namna kumi na mbili, na kuzaa matunda yake kila mwezi; na majani ya mti huo yalikuwa ya uponyaji wa mataifa. Wala hapatakuwa na laana tena, bali kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kitakuwa ndani yake; na watumishi wake watamtumikia: nao wataona uso wake; na jina lake litakuwa katika vipaji vya nyuso zao. Na hakutakuwa na usiku pale; wala hawahitaji mshumaa, wala mwanga wa jua; kwa sababu Bwana Mungu huwapa mwanga: na wao watatawala daima na milele” (Ufunuo 22:1-5). Kila wakati tunapoimba maneno haya, mioyo yetu inajaa furaha isiyo na kikomo na kutosheka, na machozi hutiririka kutoka kwa macho yetu. Ashukuriwe Bwana kwa kutuchagua, ashukuriwe Bwana kwa neema yake. Ametupa mara mia katika maisha haya, ametupa uzima wa milele katika ulimwengu ujao. Ikiwa Angetuomba tufe sasa, tungefanya hivyo bila malalamiko hata kidogo. Ee Bwana! Tafadhali njoo hivi karibuni! Kwa kuwa sisi tunakutamani sana, na tumeacha kila kitu kwa ajili Yako, usikawie hata dakika moja, sekunde moja tena.

Mungu amenyamaza, na kamwe hawajawahi kujionyesha kwetu, ilhali kazi Yake haijawahi kusimama. Anaichunguza dunia nzima, na kuamuru vitu vyote, na kuona maneno yote na matendo yote ya mwanadamu. Anaendesha usimamizi Wake, kwa hatua zilizopimwa na kulingana na mpango Wake, kimya kimya, na bila athari ya kushangaza, bado hatua Zake husonga mbele, moja baada ya nyingine, karibu zaidi na wanadamu, na kiti Chake cha hukumu kimeenezwa katika ulimwengu kwa kasi ya umeme, na baada yake kiti Chake cha enzi kinashuka mara moja katikati yetu. Hilo ni tukio la fahari kama nini, ni mandhari ya fahari yaliyoje! Kama njiwa, na kama simba angurumaye, Roho anakuja kati yetu. Yeye ni hekima, Yeye ni haki na uadhama, na Anakuja kwa siri katikati yetu, akiwa na mamlaka na amejaa upendo na huruma. Hakuna anayefahamu kuwasili Kwake, hakuna anayekaribisha kuwasili Kwake, na, zaidi ya hayo, hakuna anayejua yote ambayo Anakaribia kuyafanya. Maisha ya mwanadamu yanaendelea kama zamani, moyo wake hauna tofauti, na siku zinakwenda kama kawaida. Mungu anaishi kati yetu, mtu kama wanadamu wengine, kama mmoja wa wafuasi wasio na maana na kama mwamini wa kawaida. Ana shughuli Zake Mwenyewe, malengo Yake Mwenyewe, na, zaidi ya hayo, Ana uungu usiomilikiwa na wanadamu wa kawaida. Hakuna mtu ambaye ameona kuwepo kwa uungu Wake, na hakuna mtu ambaye ametambua tofauti ya kiini Chake na kile cha binadamu. Sisi tunaishi pamoja Naye, bila mipaka au kuogopa, kwa kuwa katika macho yetu, Yeye ni muumini asiye wa maana tu. Yeye huona matukio yetu yote, na fikra na mawazo yetu yote yanawekwa wazi mbele Yake. Hakuna anayependezwa na kuwepo Kwake, hakuna anayewazia chochote kuhusu kazi Yake, na, zaidi ya hayo, hakuna aliye na shauku hata kidogo kuhusu utambulisho Wake. Tunachofanya ni kuendelea na shughuli zetu, kana kwamba Yeye hana uhusiano wowote nasi …

Kwa bahati, Roho Mtakatifu huonyesha kifungu cha maneno “kupitia” Kwake, na ingawa inahisi kuwa haikutarajiwa sana, hata hivyo tunalitambua kama tamko linalotoka kwa Mungu, na tunalikubali kwa urahisi kutoka kwa Mungu. Hii ni kwa sababu, bila kujali ni nani anayeonyesha maneno haya, ilimradi yanatoka kwa Roho Mtakatifu tunapaswa kuyakubali, na hatufai kuyakana. Tamko linalofuata linaweza kuja kupitia mimi, au wewe, ama kupitia yeye. Yeyote yule, yote ni neema ya Mungu. Ilhali bila kujali mtu huyo ni nani, hatufai kumwabudu mtu huyu, kwa kuwa bila kujali chochote, mtu huyu hawezi kuwa Mungu, wala hatuwezi kwa njia yoyote ile kumchagua mtu wa kawaida kama huyu kuwa ndiye Mungu wetu. Mungu wetu ni mkuu na mwenye kuheshimika sana; mtu asiye na maana kama huyu anawezaje kusimama katika nafasi Yake? Zaidi ya hayo, tunamsubiri Mungu aje na kuturudisha kwa ufalme wa mbinguni, na kwa hivyo mwanadamu asiye na umuhimu hivyo anawezaje kuwa na sifa zinazostahili kufanya kazi ngumu na muhimu kama hiyo? Bwana akirudi tena, ni lazima iwe juu ya wingu jeupe, ambalo halaiki ya watu wanaweza kuliona. Huo utakuwa utukufu ulioje! Itawezekanaje kwamba Anaweza kujificha kwa siri kati ya kundi la watu wa kawaida?

Na bado ni mtu huyu wa kawaida, Aliyejificha kati ya watu, ndiye anayefanya kazi hii mpya ya kutuokoa. Yeye hatupi maelezo yoyote, wala Hatuambii kwa nini amerudi, lakini Yeye anafanya tu kazi Anayokusudia kufanya kulingana na mpango Wake na utaratibu Wake. Maneno Yake na matamshi Yake yanazidi kuwa ya mara kwa mara. Kuanzia kufariji, kuhimiza, kukumbusha, na kuonya mpaka kukaripia na kutia adabu; kuanzia kutumia toni ya upole na laini mpaka kutumia maneno makali na ya adhama—yote hayo humfanya mwanadamu ahisi rehema kuu na hofu kabisa. Kila kitu Anachosema kinalenga siri zilizofichwa ndani yetu; maneno Yake huchoma mioyo yetu, huchoma nafsi zetu, na kutuacha tukiwa tumejaa aibu isiyovumilika, tusijue pa kujificha. Tunaanza kuwa na shaka kama Mungu aliye ndani ya moyo wa mtu huyu Anatupenda kweli; na ni nini hasa Anachokusudia. Pengine tunaweza tu kunyakuliwa baada ya kuvumilia mateso haya? Vichwani mwetu, tunafanya hesabu … kuhusu hatima inayokuja na kuhusu majaliwa yetu ya baadaye. Bado, kama awali, hakuna hata mmoja wetu anayeamini kwamba Mungu amechukua mwili tayari ili kufanya kazi kati yetu. Hata ingawa Ameandamana nasi kwa muda mrefu sana, ingawa tayari Yeye amesema maneno mengi uso kwa uso nasi, bado tunabaki bila utayari wa kumkubali mtu wa kawaida kama huyo kuwa Mungu wa mustakabali wetu, na bado hatuko tayari kukabidhi udhibiti wa maisha yetu ya usoni na hatima zetu kwa mtu huyu asiye na maana. Kutoka Kwake tunafurahia ugavi usioisha wa maji ya uzima, na kupitia Kwake tunaishi maisha ya mwanadamu na Mungu kuwa ana kwa ana. Lakini tunashukuru tu kwa neema ya Bwana Yesu aliye mbinguni, na hatujawahi kamwe kutilia maanani hisia za mtu huyu wa kawaida ambaye Ana uungu. Bado, kama hapo awali, Anafanya kazi Yake kwa unyenyekevu Akiwa amejificha katika mwili, Akitoa maonyesho kwa sauti ya moyo Wake, kana kwamba Hana hisia kwa wanadamu kumkataa Yeye, kana kwamba Anasamehe milele uchanga na ujinga wa mwanadamu, na Anavumilia milele mtazamo wa mwanadamu usiomheshimu Yeye.

Bila sisi kujua, mtu huyu asiye na umuhimu Ametuelekeza katika hatua moja baada ya nyingine ya kazi ya Mungu. Tunapitia majaribu mengi, na kuadibu kusikohesabika, na tunajaribiwa na kifo. Tunapata kujua kuhusu tabia ya Mungu ya haki na uadhama, kufurahia pia, upendo na huruma Zake, tunakuja kufahamu nguvu za Mungu ambazo ni kubwa na hekima Yake, tunashuhudia uzuri wa Mungu, na kutazama shauku Yake ya kumwokoa mwanadamu. Kwa maneno ya huyu mtu wa kawaida, tunakuja kujua tabia na kiini cha Mungu, kufahamu mapenzi ya Mungu, kujua asili ya mwanadamu na kiini cha mwanadamu, na tunapata kuona njia ya wokovu na ukamilifu. Maneno Yake yanafanya sisi “tufe,” na yanatufanya “tuzaliwe upya”; maneno Yake hutufariji, lakini pia yanatuacha tukiwa tumejawa na hatia na hisia ya kuwa wadeni; maneno Yake hutuletea furaha na amani, lakini pia maumivu makubwa sana. Wakati mwingine sisi ni kama wanakondoo wa kuchinjwa mikononi Mwake; wakati mwingine sisi ni kama vipenzi vya roho Yake na tunafurahia upendo Wake wenye upole; wakati mwingine sisi ni kama maadui Wake, na chini ya macho Yake tunageuzwa kuwa majivu kwa ghadhabu Yake. Sisi ni jamii ya wanadamu waliookolewa Naye, sisi ni funza machoni Pake, na sisi ni wanakondoo waliopotea ambao, usiku na mchana, Yeye hunuia kuwapata. Yeye ni mwenye huruma kwetu, Anatudharau, Anatuinua, Anatufariji na kutuhimiza, Anatuongoza, Anatupa nuru, Anaturudi na kutufundisha nidhamu, na Yeye hata hutulaani. Usiku na mchana, Yeye haachi kamwe kuwa na wasiwasi juu yetu, na Anatulinda na kututunza usiku na mchana, Haondoki kamwe upande wetu. Anamwaga damu yote ya moyo Wake kwa ajili yetu na kulipa gharama zozote kwa ajili yetu. Ndani ya matamshi ya mwili huu usio na maana na wa kawaida, tumefurahia ukamilifu wa Mungu na kuona hatima ambayo Mungu ametupa. Licha ya haya, ubatili bado unachochea matatizo ndani ya mioyo yetu, na bado hatuko tayari kabisa kumkubali mtu kama huyu kama Mungu wetu. Ingawa Yeye ametupa mana nyingi sana, nyingi sana ya kufurahia, hakuna hata moja kati ya hizi ambayo inaweza kuchukua nafasi ya Bwana katika mioyo yetu. Tunaheshimu utambulisho maalum na hadhi ya huyu mwanadamu kwa kusita sana. Maadamu hafungui mdomo Wake kututaka tukiri kwamba Yeye ni Mungu, sisi kamwe hatuwezi kukata kauli wenyewe na kukiri Yeye ni Mungu ambaye yuko karibu kuja na bado amekuwa Akifanya kazi kati yetu kwa muda mrefu sana.

Mungu huendelea na matamshi Yake, akitumia mbinu mbalimbali na mitazamo kutuonya kuhusu kile tunachopaswa kufanya, wakati huo huo Anaeleza sauti ya moyo Wake. Maneno Yake yanabeba nguvu za maisha, yanatuonyesha njia tunayopaswa kuitembea, na kutuwezesha kufahamu ukweli ni nini. Tunaanza kuvutiwa na maneno Yake, tunaanza kuzingatia sauti Yake na jinsi Anavyoongea, na bila hiari tunaanza kuvutiwa na hisia za ndani kabisa za mwanadamu huyu asiye wa ajabu. Anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yetu, Anapoteza usingizi na hamu ya kula kwa ajili yetu, Analia kwa ajili yetu, Anashusha pumzi kwa ajili yetu, Anaugulia katika ugonjwa kwa ajili yetu, Anadhalilishwa kwa ajili ya wokovu na hatima zetu; na uasi wetu na kufa ganzi kwetu kunatoa machozi na damu kutoka moyoni Mwake. Hakuna mtu wa kawaida mweye nafsi hii au miliki hizi, wala haiwezi kumilikiwa au kufikiwa na mtu yeyote aliyepotoka. Anaonyesha uvumilivu na subira isiyomilikiwa na mtu wa kawaida, na upendo Wake si kitu ambacho kiumbe chochote kimepewa. Hakuna mtu mbali na Yeye anayeweza kujua mawazo yetu yote, au kufahamu asili yetu na kiini chetu kwa uwazi na kwa ukamilifu, ama kuhukumu uasi na upotovu wa binadamu, ama kusema nasi na kufanya kazi kati yetu kama hivi kwa niaba ya Mungu aliye mbinguni. Hakuna mtu isipokuwa Yeye ambaye amepewa mamlaka, hekima, na heshima ya Mungu; tabia ya Mungu na kile ambacho Mungu anacho na alicho vinatoka, kwa ukamilifu wao, ndani Yake. Hakuna mtu mbali na Yeye ambaye anaweza kutuonyesha njia na kutuletea mwangaza. Hakuna yeyote ila Yeye anayeweza kutufichulia siri ambazo Mungu hajatufunulia tangu uumbaji hadi leo. Hakuna yeyote isipokuwa Yeye ambaye anaweza kutuokoa kutoka kwenye utumwa wa Shetani na tabia zetu potovu. Anamwakilisha Mungu; Anaonyesha sauti ya moyo wa Mungu, ushawishi wa Mungu, na maneno ya hukumu ya Mungu kwa wanadamu wote. Ameifungua enzi mpya, nyakati mpya, na kuleta mbingu na nchi mpya na kazi mpya, Ametuletea matumaini na kukomesha maisha yaliyosababisha hali isiyo dhahiri, na Amewezesha nafsi zetu zote kuiona njia ya wokovu kikamilifu. Ameshinda nafsi zetu zote na kupata mioyo yetu. Tangu wakati huo na kuendelea, mioyo yetu imepata kutambua, na roho zetu zinaonekana kuhuishwa: Mtu huyu wa kawaida, asiyekuwa mwenye umuhimu, mtu huyu anayeishi miongoni mwetu na Aliyekataliwa na sisi kwa muda mrefu sana—je, huyu si Bwana Yesu, ambaye daima yupo katika mawazo yetu, tunapoamka au tunapoota, na ambaye tunamtamani usiku na mchana? Ni Yeye! Ni Yeye kweli! Yeye ni Mungu wetu! Yeye ndiye ukweli, njia, na uzima! Yeye ametuwezesha kuishi tena na kuona nuru na Amekomesha mioyo yetu kuhangaika. Tumerudi nyumbani mwa Mungu, tumerejea mbele ya kiti Chake cha enzi, tuko uso kwa uso pamoja na Yeye, tumeshuhudia uso Wake, na tumeona njia iliyo mbele. Wakati huu, mioyo yetu imeshindwa kabisa na Yeye; hatuna shaka kuhusu Yeye ni nani tena, hatupingi tena kazi Yake na neno Lake, na tunasujudu, mbele Yake. Hakuna tunachotaka zaidi ya kufuata nyayo za Mungu kwa maisha yetu yote, na kufanywa wakamilifu na Yeye, na kulipa neema Yake, na kulipa upendo Wake kwetu, na kutii matayarisho na mipangilio Yake, na kushirikiana na kazi Yake, na kufanya kila kitu tunachoweza ili kukamilisha kile Anachotuaminia.

Kushindwa na Mungu ni kama mashindano ya kareti.

Kila neno la Mungu hugonga eneo letu moja la kufisha, likituacha tukiwa na uchungu na kujawa na hofu. Yeye anafichua dhana zetu, mawazo yetu, na tabia zetu potovu. Kutoka kwa kwa kila neno na tendo letu, kila hatua zetu, hadi kwa kila wazo na fikra zetu, asili na kiini chetu kinafichuliwa katika maneno Yake, yakituweka katika hali ya hofu na kutetemeka na bila mahali pa kuficha aibu yetu. Moja baada ya nyingine, Anatueleza kuhusu matendo yetu yote, malengo yetu na nia, hata tabia potovu ambazo hatujawahi kuzigundua sisi wenyewe, na kutufanya tuhisi kwamba tumewekwa wazi katika hali yetu ya kutokamilika na, hata zaidi kushindwa kikamilifu. Yeye hutuhukumu kwa sababu ya upinzani wetu Kwake, Anatuadibu kwa kumkufuru na kumshutumu, na kutufanya tuhisi kwamba, machoni Pake, hatuna sifa hata moja inayoweza kutuokoa, kwamba sisi ndio Shetani wanaoishi. Matumaini yetu yanavunjika, na hatuthubutu tena kumpa madai yoyote yasiyo na maana au kuweka matumaini yoyote Kwake, na hata ndoto zetu hutoweka mara moja. Huu ni ukweli ambao hakuna yeyote kati yetu anayeweza kuufikiria, na ambao hakuna yeyote kati yetu anayeweza kuukubali. Ndani ya muda mfupi, tunapoteza usawa wetu wa ndani, na hatujui jinsi ya kuendelea kwenye njia iliyo mbele, au jinsi ya kuendelea katika imani zetu. Inaonekana ni kana kwamba imani zetu zimerudi kama zilivyokuwa mwanzoni, na tena ni kana kwamba hatujawahi kukutana na Bwana Yesu au kupata kumjua. Kila kitu machoni petu hutujaza mkanganyiko, na kutufanya tukose msimamo kwa kutokuwa na uhakika, na ndani ya mioyo yetu kuna ghadhabu isiyozuilika na aibu. Tunajaribu kujieleza, kupata suluhisho, na, zaidi ya hayo, sisi tunaendelea kumsubiri Mwokozi Yesu, ili tuweze kujieleza kwa dhati Kwake. Ingawa kuna nyakati zingine ambazo sisi tunaonekana kuwa sawa kwa nje, si wenye majivuno wala wanyenyekevu, mioyoni mwetu tunatatizwa na hisia ya hasara ambayo hatujawahi kuihisi hapo awali. Ingawa wakati mwingine tunaweza kuonekana watulivu isivyo kawaida kwa nje, akili zetu zinavurugika kwa mateso kama bahari yenye dhoruba. Hukumu Yake na kuadibu Kwake kumechukua matumaini na ndoto zetu zote, kukomesha tamaa zetu kuu na kutuacha tusitake kuamini kuwa Yeye ndiye Mwokozi wetu na Anayeweza kutuokoa. Hukumu na kuadibu Kwake kumefungua pengo kati yetu na Yeye, pengo kubwa sana kiasi kwamba hakuna mtu aliye tayari kulivuka. Hukumu na kuadibu Kwake ni mara ya kwanza ambapo tumepatwa na pingamizi kubwa kama hilo, fedheha kubwa kama hio katika maisha yetu. Hukumu na kuadibu Kwake kumetufanya sisi kweli kuhisi heshima ya Mungu na kutovumilia Kwake kosa la binadamu, ambazo tukilinganishwa nazo, sisi ni waovu sana, wachafu sana. Hukumu na kuadibu Kwake kumetufanya tutambue kwa mara ya kwanza jinsi ambavyo tuna kiburi na wenye majivuno, na jinsi ambavyo mwanadamu kamwe hataweza kulingana na Mungu, ama kuwa sawa na Mungu. Hukumu na kuadibu Kwake kumetufanya tutamani kutoishi tena katika tabia potovu kama hiyo, kujiondoa wenyewe kwa asili na kiini hiki haraka iwezekanavyo, na kuacha kuwa waovu na kuchukiwa na Yeye. Hukumu na kuadibu Kwake kumetufanya kuwa tayari kunyenyekea na kutii maneno Yake, na tusiasi matayarisho na mipangilio Yake tena. Hukumu na kuadibu Kwake kwa mara nyingine tena kumetuwezesha sisi tuwe na tamanio la kuendelea kuwepo na kumetuwezesha kufurahia kumkubali Yaye kama Mwokozi wetu…. Sisi tumetoka nje ya kazi ya ushindi, nje ya kuzimu, tumetoka nje ya bonde la uvuli wa mauti…. Mwenyezi Mungu ametupata, kundi hili la watu! Ameshinda dhidi ya Shetani, na kuwashinda adui Zake wengi!

Sisi ni kundi la watu wa kawaida tu, waliomilikiwa na tabia potovu ya kishetani, wale waliochaguliwa na Mungu kabla ya enzi, na wahitaji ambao Mungu amewainua kutoka jaani. Kuna wakati tulimkataa na kumshutumu Mungu, lakini sasa tumeshindwa na Yeye. Kutoka kwa Mungu tumepokea uzima, njia ya uzima wa milele. Licha ya mahali ambapo tunaweza kuwa duniani, licha ya mateso na dhiki tunazovumilia, hatuwezi kuwa mbali na wokovu wa Mwenyezi Mungu. Kwa kuwa Yeye ndiye Muumba wetu, na ukombozi wetu pekee!

Upendo wa Mungu unaenea kama maji ya chemchemi, na unatolewa kwako, na kwangu, na kwa wengine, na kwa wale wote wanaotafuta ukweli kwa dhati na kungoja kuonekana kwa Mungu.

Kama vile tu mwezi unavyofuata jua kwa kubadilishana bila mwisho, vile vile ndivyo kazi ya Mungu haikomi kamwe, na inatekelezwa kwako, kwangu, kwake, na kwa wale wote ambao wanafuata nyayo za Mungu na kukubali hukumu Yake na kuadibu Kwake.

Machi 23, 2010

Iliyotangulia: Kumjua Mungu Ndiyo Njia ya Kumcha Mungu na Kuepuka Maovu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp