21. Kujiweka Huru Kutoka katika Mtego wa Uvumi

Na Xiaoyun, China

Awali nilikuwa afisa kike wa jeshi. Siku moja mnamo mwaka wa 1999, mchungaji Mkorea alinihubiria injili ya Bwana Yesu. Kwa sababu ya ufuatiliaji wangu wa ari, punde niligeuka kuwa lengo la mafunzo ya mchungaji huyo na msaidizi wake mkuu. Katika majira ya joto ya mwaka wa 2000, mchungaji alikuja Yunnan katika safari fupi ya misheni ya majira ya joto akiwa na zaidi ya wanafunzi kumi na wawili wa chuo cha elimu kutoka Kanisa la Injili la Korea. Bila kutarajiwa, hili liliiogofya serikali ya CCP. Tulikamatwa tulipokuwa tukihudhuria mkutano katika nyumba ya mchungaji na kisha kuletwa katika Idara ya Usalama wa Umma ya Jimbo la Yunnan ili kuhojiwa. Wanafunzi hao Wakorea wa chuo kikuu walifukuzwa nchini usiku huo huo na huyo mchungaji Mkorea pia alifukuzwa kutoka nchi. Kanisa liliteswa na serikali ya CCP na waumini wengi wakawa na woga na hawakuthubutu kuamini. Sehemu fulani ya waumini pia walilazimishwa kwenda katika Kanisa la Kanuni Tatu za Binafsi, na hivi ndivyo jinsi kanisa lilivunjwa na serikali ya CCP. Nilikuwa mfanyakazi mwenza mkuu katika kanisa na mateso ya serikali ya CCP wakati huu pia yalinisababisha kupoteza kazi yangu.

Mnamo Machi mwaka wa 2005, nilisikia injili ya ufalme ya Mwenyezi Mungu. Niliposikia kwamba Bwana Yesu alikuwa amerudi, nilisisimka sana kiasi kwamba machozi ya furaha yalijaza macho yangu na nilihisi shukrani isiyoweza kuelezeka. Nilitaka tu kuwaleta ndugu zangu mbele ya Mungu haraka kadiri nilivyoweza. Chini ya mwongozo wa Mungu, mmoja baada ya mwingine, ndugu waliikubali kazi ya Mungu ya siku za mwisho. Lakini bila kutarajiwa, mfanyakazi mwenza mmoja wa kanisa aliyekuwa na kipaji zaidi alitangaza baada ya kusikia ushuhuda wa kazi ya siku za mwisho ya Mwenyezi Mungu: “Mafundisho haya yanaonekana kuwa sahihi, lakini tunahitaji kumwuliza mchungaji kwanza na kuona atakachosema.” Punde baadaye, mchungaji alinipigia simu na kusema, “Kuna vurugu sana nje sasa. Hujamwamini Mungu kwa muda mrefu na kimo chako ni kidogo. Chochote utakachofanya, usisikilize mahubiri kutoka nje ya kanisa, na hivyo basi hutapotoka. Tunaweza tu kukubali uchungaji wa kanisa hili. Usisikilize njia zinazohubiriwa na makanisa mengine.” Baada ya kusikiliza, nilisema kwa utulivu, “Kupitia wakati huu wa kuchunguza kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho, nimegundua kwamba kila kitu wanachohubiri kinakubaliana na Biblia, kina nuru na mwangaza wa Roho Mtakatifu na ndiyo njia ya kweli.” Mchungaji wangu akasema, “Bila kujali jinsi wanavyohubiri vizuri, lazima tuelewe kwamba Bwana Yesu pekee ndiye Mungu wa kweli. Hatupaswi kumwacha Bwana!” Nilisema kwa uthabiti, “Sijamwacha Bwana, lakini nafuata nyayo za Mwanakondoo. Bwana Yesu tayari amerudi. Ni vema tu kwamba tunapaswa kumkaribisha Bwana kama walivyofanya wanawali wenye busara.” Mchungaji akasema kwa ukali, “Kanisa la Injili la Korea linawezaje kukosa kujua kwamba Bwana amerudi?” Nilisema, “Hili silo jambo ambalo linaweza kuelezwa kwa maneno machache.” Mchungaji akasema kwa lugha ya kushawishi, “Wanaloliamini ni Umeme wa Mashariki, ambalo lilichukuliwa hatua kali na serikali ya CCP. Imeelezwa wazi sana mtandaoni. Nenda mtandaoni, na utaona. Lazima uende mtandaoni kuangalia….” Baada ya kuweka simu chini, moyo wangu haukuweza kutulia kwa muda mrefu. Maneno ya mchungaji yaliendelea kuvuma masikioni mwangu. Hasa nilitaka kujua kile kilichokuwa kikisemwa mtandaoni.

Ili kujua, nilienda katika chumba cha mtandao haraka. Punde nilipofungua tovuti, nilipigwa na bumbuazi. Katika tovuti kulikuwa na kufuru na shutuma nyingi ya serikali ya CCP dhidi ya Mungu, na pia kashfa na kufuru kutoka kwa watu wa dini wenye mamlaka. Nilikuwa na mashaka kiasi: Maneno ya Mwenyezi Mungu hayawezi kunenwa na yeyote tu. Ni maonyesho ya Roho wa ukweli. Huu ni ukweli unaotambuliwa na watu wengi kutoka madhehebu mbalimbali ambao wanamwamini Bwana kwa kweli na wanatamani ukweli. Lakini kwa nini tovuti zinaanza uvumi ili kuwafanya watu wamkatae Mwenyezi Mungu? Pia kuna wachungaji wengi maarufu ambao pia wanamshutumu na kumkufuru Mungu pamoja na serikali ya CCP. Ni nini kinachoendelea hapa? Baada ya kuona propaganda hizi hasi, nilihisi kuhangaishwa na mashaka. Baada ya hapo, niliona shambulizi dhidi ya mtu aliyetumiwa na Roho Mtakatifu mtandaoni. Nilisikitika tena. Kweli nilimwamini mwanadamu? Nilipoendelea kupitiapitia habari mtandaoni, nilitiwa msukosuko zaidi na kuhisi kutatizwa na kukanganywa sana, kiasi kwamba mwishowe, sikujua jinsi nilivyotoka katika chumba hicho cha mtandao.

Njiani kuelekea nyumbani, nilikumbuka nyakati zote nilizotumia kutafuta na kuchunguza kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho. Wakati wowote nilipouliza maswali kiasi, ndugu kutoka Kanisa la Mwenyezi Mungu walinisomea maneno ya Mungu. Kila suala lilitatuliwa moja baada ya jingine, na nikashawishika kabisa. Ilichukua siku kumi na moja kamili za mjadala na uchunguzi kabla niamini kwa uthabiti kwamba Mwenyezi Mungu alikuwa Bwana Yesu aliyerudi. Pia nilisoma maneno kiasi ya Mwenyezi Mungu. Mungu amefichua siri zote za hatua tatu za kazi na mpango wa usimamizi wa miaka elfu sita, na pia Ameeleza wazi ukweli kama vile maelezo ya ndani na asili ya Biblia, ambayo ni maneno ya Mungu na ambayo ni maneno ya watu katika Biblia, na jinsi ambavyo watu wanapaswa kuichukulia Biblia. Niliposoma vitu hivi, kila kitu kikawa dhahiri na nilipata faida kubwa. Kutoka katika maneno haya ya Mungu, niliona kwamba Mwenyezi Mungu anapaswa kuwa Bwana Yesu aliyerudi. Lakini kwa nini propaganda yote mtandaoni ilikuwa hasi? Nilivyozidi kufikiria kuhusu uvumi huu, ndivyo nilivyohuzunika zaidi na ndivyo moyo wangu ulivyohisi mzito zaidi, na nilikuwa karibu nigongwe na gari nilipokuwa nikivuka barabara.

Baada ya kurudi nyumbani, moyo wangu haukuweza kabisa kutulia na uvumi huo wa mtandao ulikuwa wa mstari wa mbele akilini mwangu mara kwa mara na kukawia hapo. Moyo wangu ulihisi kuzidiwa nilipokuwa nikifikiria jambo moja baada ya jingine. Sikuweza kulala usiku huo, na nikafikiri: “Nikichukua njia isiyo sahihi, basi si imani yangu itakuwa bure? La, lazima nirudi mara moja. Lakini, je, ikiwa Mwenyezi Mungu ni Bwana Yesu aliyerudi? Basi si nitapoteza nafasi yangu ya kumkaribisha Bwana na kupoteza fursa yangu ya kuokolewa?” Nilipokuwa nikiyumbayumba mbele na nyuma, nilikuja mbele ya Mungu katika sala: “Ee Mungu! Tangu nikubali hatua hii ya kazi, moyo wangu daima umehisi mtulivu, nimefurahia sana kusoma maneno ya Mungu na roho yangu imehisi kustawishwa sana. Lakini baada ya kuona propaganda fulani hasi mtandaoni, siwezi kutulia. Tafadhali ulinde moyo wangu. Ee Mungu! Kimo changu ni kidogo na sijui jinsi ya kutambua vitu hivi. Ikiwa Mwenyezi Mungu kweli ni Wewe ambaye amerudi, basi nakuomba Uniongoze niwe na uhakika kuhusu kazi Yako bila kusumbuliwa na yeyote ama chochote. Ikiwa sivyo, basi nakuomba Uniongoze nikuze utambuzi….” Baada ya kuomba, wazo lilinijia moyoni: Kumaliza kusoma maneno ya Mwenyezi Mungu haraka ili kuamua ikiwa ni sauti ya Mungu au la. Usiku huo, nilisoma maneno ya Mungu usiku kucha na sijui nilipolala mezani.

Mapema asubuhi iliyofuata, niliamshwa na hodi mlangoni na nikaenda kuufungua nikisinzia. Ilitokea kuwa alikuwa Dada Wu ambaye alikuwa ameninyunyizia. Aliniona nikionekana mwenye usingizi na kuniuliza kilichokuwa kimetokea kwa namna ya kujali. Nilisema, “Nilikuwa mtandaoni jana na nikaona mambo mengi ambayo yalimpinga na kumkufuru Mungu, na sasa nahisi kukanganywa sana….” Baada ya kusikia hili, Dada Wu alishiriki nami: “Dada, unajua vyema sana mtazamo wa serikali ya CCP kwa Wakristo. Wamewakamata na kuwatesa Wakristo wengi. Huu ni ukweli mtupu. Uvumi wote ulio mtandaoni umebuniwa na serikali ya CCP ili kulitesa Kanisa la Mwenyezi Mungu. Lengo lao ni kukandamiza kazi ya Mungu na kufanya China kuwa eneo likanalo Mungu na kutowaruhusu watu kumfuata ama kumwabudu Mungu. Dada, CCP ni serikali imkanayo Mungu. Tunaweza kuamini wanachosema?” Maneno ya dada huyo yalikuwa kumbusho la wakati ufaao. Kweli! CCP inamkana Mungu. Wao ndio wale wanaomchukia na kumpinga Mungu zaidi. Mtu anawezaje kuamini wanachosema? Serikali ya CCP inatumia kisingizio cha bango la “uhuru wa dini,” lakini kwa siri, wanawalazimisha na kuwakamata watu wanaomwamini Mungu kwa utukutu. Nilifikiria kuhusu jinsi serikali ya CCP ilivyokuwa imewalazimisha na kuwakandamiza wale kutoka kanisa letu awali na jinsi ndugu wengi walivyopoteza imani na hawakuthubutu kuamini, na nilifikiria pia kuhusu jinsi nilivyopoteza kazi yangu kwa sababu ya hili—je, huu haukuwa mtazamo wa serikali ya CCP kwa watu wanaomwamini Mungu? Ili kuzuia imani ya dini, serikali ya CCP ilianzisha Kanisa la Kanuni Tatu za Binafsi na kuwataka watu “wapende nchi” kwanza kisha “wapende dini.” Lengo lao ni kuwadhibiti watu kwa uthabiti mikononi mwao na kuzuia uhuru wa watu wa imani. Nilipofikiri kuhusu hili, nilipata kuwa na utambuzi kiasi kuhusu makusudi yenye kustahili dharau ya serikali ya CCP. Serikali ya CCP daima imetesa imani za dini na kushutumu njia ya kweli, Kwa hivyo kubuni kwao uvumi na kushutumu kazi ya siku za mwisho ya Mwenyezi Mungu sio ufunuo mkubwa wa asili yao ya kishetani ya kumchukia Mungu na kumpinga Mungu?

Dada Wu aliendelea kushiriki nami: “Serikali ya CCP ni utawala wa kishetani unaomkana Mungu na ni adui wa Mungu. Ili kufikia nia yao kali ya kudhibiti watu kwa kudumu, wanageuza mambo kwa ukaidi ili kushutumu na kuaibisha Kanisa la Mwenyezi Mungu. Tunaweza kubainisha hili vizuri sana. Lakini wachungaji wa dini na wazee wanawezaje kufuata utawala unaomkana Mungu katika kumpinga, kumshutumu na kumkufuru Mungu? Watu wengi hawawezi kuelewa shida hii. Kwa kweli, hili linahusiana na asili ya viongozi wa dini na kiini cha kumpinga Mungu na kuchukia ukweli. Kufikiria nyuma miaka elfu mbili iliyopita, wakati Bwana Yesu alifanya kazi ya kuwakomboa wanadamu, Alikumbana na upinzani na mateso makubwa kutoka kwa wakuhani wakuu, waandishi na Mafarisayo. Hii ilikuwa kwa sababu njia ambayo Bwana Yesu alihubiri na miujiza Aliyofanya wakati huo yalisababisha kioja katika Yudea nzima. Watu wengi wa kawaida walivutiwa na maneno ya Bwana na mmoja baada ya mwingine walimgeukia Bwana Yesu. Makuhani wakuu, waandishi na Mafarisayo waliona hili kama tishio kwa hadhi na riziki zao, na walikula njama na serikali ya Kirumi kumpinga na kumshutumu Bwana Yesu. Walieneza uvumi, kuikashifu kazi ya Bwana na kumsulubisha Bwana Yesu msalabani. Sasa historia ya miaka elfu mbili iliyopita inajirudia. Viongozi wa dini wanaona kazi ya siku za mwisho ya Mwenyezi Mungu ikikubaliwa na idadi inayoongezeka ya watu na wanaanza kuwa na wivu mara moja na kuungana na serikali ya CCP katika kupinga na kuishutumu kazi ya siku za mwisho ya Mungu. Hili linaonyesha kabisa kwamba viongozi wengi wa dini ni wapinga Kristo wasiopenda ukweli na wanaopenda tu hadhi. ‘Tangu nyakati za kale, njia ya kweli daima imekandamizwa.’ Kwa hivyo haishangazi kwamba kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho inaweza kupingwa na kushutumiwa vikali na nguvu ovu za serikali ya CCP na jamii ya dini.” Ndiyo, Mafarisayo, makuhani wakuu na waandishi wote walikuwa watu wenye mamlaka katika jumuiya ya watawa, lakini hawakuwa waumini wa kweli wa Mungu na hawakupenda ukweli. Walijua kwamba maneno ya Bwana Yesu yalikuwa na mamlaka na nguvu, lakini hawakutafuta ama kuchunguza hata kidogo. Badala yake, ili kudumisha hadhi na riziki zao, walimshutumu na kumkufuru Bwana. Asili yao kweli ilikuwa kumpinga Mungu na kuwa maadui wa Mungu. Siku hizi, jinsi ambavyo wachungaji na wazee wa jamii ya dini wanatenda kuhusiana na kuja kwa mara ya pili kwa Bwana ni sawa na kile walichofanya Mafarisayo. Inatukia kwamba wao ni wapinga Kristo wanaomchukia Mungu na kuchukia ukweli! Wakati kurudi kwa Bwana Yesu kunatabiriwa katika Biblia, inasema, “Bali kwanza lazima apitie mambo mengi, na akataliwe na kizazi hiki(Luka 17:25). Sasa Mwenyezi Mungu amekuja kufanya kazi Yake, lakini Anapingwa na kushutumiwa najamii ya dini na utawala ukanao Mungu wa CCP. Je, huu sio utimizo wa unabii wa Bwana? Wakati huo, moyo wangu ulitiwa nuru. Dada Wu aliendelea na ushirika wake: “Propaganda hasi inayoenezwa na serikali ya CCP najamii ya dini mtandaoni kimsingi inanuiwa kuharibu na kuvuruga kazi ya Mungu. Shetani daima ametumia uongo kuwadanganya na kuwakanganya watu na kuwafanya watu wamshuku, kumkataa na kumsaliti Mungu. Mwishowe, wataadhibiwa na Mungu na kutumwa kuzimu, na watapoteza nafasi ya kuokolewa na Mungu milele. Lazima tuweze kutambua uvumi wao na kujua makusudi yao mabaya na nia inayostahili dharau katika kueneza uvumi. Vinginevyo, tutadanganywa na kupoteza nafasi ya kuokolewa na Mungu.” Nilikubali kwa kichwa na kuhisi kwamba ushirika na msaada wa dada huyo ulikuwa umekuja katika wakati ufaao hasa. Sikuweza kusubiri kuendelea kusikiza…

Dada Wu alitoa kitabu cha maneno ya Mungu na kuniambia: “Dada, hebu tusome kifungu cha maneno ya Mwenyezi Mungu! Mwenyezi Mungu alisema: ‘Katika mpango Wangu, Shetani amewahi kushindana na kila hatua, na, kama foili[a] ya hekima Yangu, amejaribu siku zote kutafuta njia na namna za kuvuruga mpango Wangu wa awali. Lakini Ningeweza kushindwa na njama zake danganyifu? Vyote mbinguni na duniani vinanitumikia—njama danganyifu za Shetani zingeweza kuwa tofauti? Huku ndiko hasa kukutana kwa hekima Yangu, ndiyo hasa yaliyo ya ajabu kuhusu matendo Yangu, na ni kanuni ya utendaji ya mpango Wangu mzima wa usimamizi. Katika enzi ya ujenzi wa ufalme, bado Mimi siepuki njama danganyifu za Shetani, ila Naendelea kufanya kazi ambayo lazima Nifanye. Kati ya ulimwengu na vitu vyote, Nimechagua matendo ya Shetani kama foili Yangu. Je, hii si hekima Yangu? Je, si haya ndiyo hasa yaliyo ya ajabu kuhusu kazi Yangu?(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima, Sura ya 8).”

Baada ya kusoma maneno ya Mungu, Dada Wu alisema katika ushirika: “Tunaona kutoka katika maneno ya Mwenyezi Mungu kwamba kila hatua ya kazi ya Mungu inajumuisha mapenzi, hekima na ajabu ya Mungu. Kutoka mwanzo hadi mwisho, kazi ya Mungu haiepi hila za Shetani, lakini hutumia hila ya Shetani kwa manufaa ya kazi ya Mungu, ili kuwakamilisha wale wanaomwamini Mungu kwa kweli na ili kukamilisha mpango wa Mungu wa usimamizi wa kuwaokoa wanadamu. Juujuu, Shetani anaonekana kujawa na majivuno katika kumpinga kwake Mungu, lakini hekima ya Mungu hutumika kwa msingi wa hila ya Shetani. Mwanzoni, Shetani aliwapotosha wanadamu, lakini Mungu hakumwangamiza moja kwa moja. Badala yake, Mungu hutumia hatua tatu za kazi Yake kuwaokoa wanadamu, na huku akiwaokoa wanadamu, Mungu humruhusu Shetani kusababisha vurugu na vipingamizi, nia Yake ikiwa kuonyesha asili ovu ya kweli ya Shetani ya kuwapotosha na kuwakanganya wanadamu, ya kumpinga Mungu kwa ukali na kuwa adui wa Mungu, ili wanadamu waone kwa kweli sura mbaya ya Shetani na asili ovu. Kwa kufanya hivyo, watu wanaweza kumkataa Shetani kwa ari na kumwacha na kumrudia Mungu, na Shetani ataaibishwa na kushindwa kabisa. Huu ndio ushuhuda wenye nguvu kabisa dhidi ya Shetani, na unafichua hekima na uweza wa Mungu. Jinsi tu Ayubu alikuwa mtu mcha Mungu ambaye aliepuka uovu, lakini Mungu alimruhusu Shetani amtese Ayubu na hatimaye Alitumia ushuhuda wa Ayubu katika majaribu kumfedhehesha Shetani na kuthibitisha kwamba tathmini ya Mungu ya Ayubu ilikuwa sahihi kabisa. Hii ilikuwa hekima ya Mungu. Aidha, kile anachofanya Mungu katika siku za mwisho ni kazi ya kuwaokoa na kuwakamilisha watu. Pia ni kazi ya kuwatenga watu kulingana na aina zao na kukamilisha enzi. Mungu hutumia mateso ya serikali ya CCP najamii ya dini kuwafanya watu wapitie majaribu na dhiki mbalimbali. Wale wanaomwamini Mungu kwa kweli wanaweza kuelewa ukweli na kukuza utambuzi kwa kupitia dhiki, wanaweza kujua uweza na hekima ya Mungu, wabaini uovu wa Shetani, na mwishowe wamkatae Shetani kabisa na kupata wokovu wa Mungu. Lakini wale ambao ni waoga, wale wasio na imani ya kweli, wale waliochoshwa na ukweli na wale waovu wanaochukia ukweli wanafunuliwa wote kupitia majaribu na dhiki, na wanakuwa walengwa wa kuondolewa. Hivyo mbuzi wanatengwa kutoka kwa kondoo, magugu kutoka kwa ngano, watumishi waovu kutoka kwa watumishi wazuri, na wanawali wapumbavu kutoka kwa wanawali wenye busara, kwani wote wanatengwa kulingana na aina zao. Hii ni hekima na uweza wa Mungu.” Baada ya kusikia ushirika wa Dada Wu, sikuweza kujizuia kufikiria nyuma kwa miaka elfu mbili iliyopita ambapo Bwana Yesu alisulubiwa na Mafarisayo wa Kiyahudi na serikali ya Kirumi. Kutoka kwa mtazamo wa mwanadamu, kazi ya Bwana Yesu ilikuwa imefeli, lakini Bwana Yesu alisema, “Imekwisha.” Ilikuwa hasa kupitia mateso ya Shetani na usulubisho ndiyo Mungu alikamilisha kazi ya kuwakomboa wanadamu. Leo katika siku za mwisho, shutuma na kukashifu kwa serikali ya CCP najamii ya dini kwa usahihi kumetoa huduma kwa Mungu kuwakamilisha wale wanaomwamini kwa kweli, na pia wamekuwa ushuhuda wa Mungu kuwatia hatiani. Mwenyezi Mungu asema: “Hekima Yangu hutumiwa kutegemea njama za Shetani(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ukweli wa Ndani wa Kazi ya Ushindi (1)). Imerekodiwa katika Biblia: “Ee ukuu wa utajiri wa hekima na maarifa ya Mungu! hukumu zake haziwezi kuchunguzwa, na njia zake haziwezi kutafutika!” (Romans 11:33). Nilipofikiria hili, niliona kwamba kazi ya Mungu ilikuwa ya hekima sana na ya ajabu sana, na nilimsifu Mungu kwa dhati.

Kupitia ushirika wa Dada Wu, nilipata kuwa na ufahamu kiasi wa kazi ya Mungu na pia ningeweza kubainisha kiasi kiini cha upinzani wa serikali ya CCP najamii ya dini dhidi ya Mungu, lakini bado sikuelewa kilichosemwa mtandaoni kuhusu sisi kumwamini mwanadamu, yaani, kumwamini mwanadamu anayetumiwa na Roho Mtakatifu. Nilimwuliza Dada Wu: “Mtandaoni kunasemwa kwamba tunamwamini mwanadamu. Hii ni kweli?” Dada Wu akasema katika ushirika kuhusu swali hili: “Shida yako ni kwamba huelewi ukweli unaohusu tofauti kati ya kazi ya Mungu na kazi ya mwanadamu. Hebu kwanza tusome vifungu viwili vya maneno ya Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu asema: ‘Kazi ya Mungu Mwenyewe inahusisha kazi ya wanadamu wote, na pia inawakilisha kazi ya enzi nzima. Hii ni kusema kwamba, kazi ya Mungu mwenyewe inawakilisha harakati na mwelekeo wa kazi yote ya Roho Mtakatifu, ilhali kazi ya mitume inafuata kazi ya Mungu na wala haiongozi enzi, na wala haiwakilishi mitindo ya kazi ya Roho Mtakatifu katika enzi nzima. Huwa wanafanya tu kazi ambayo mwanadamu anapaswa kufanya, ambayo haihusishi kabisa kazi ya usimamizi. Kazi ya Mungu ni mradi ndani ya kazi ya usimamizi. Kazi ya mwanadamu ni wajibu tu wa wanadamu kuweza kutumika na wala haina uhusiano na kazi ya usimamizi(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kazi ya Mungu na Kazi ya Mwanadamu). ‘Kazi ambayo Mungu anafanya haiwakilishi uzoefu wa mwili Wake; kazi ambayo mwanadamu anafanya inawakalisha uzoefu wa mwanadamu. Kila mtu anazungumza kuhusu uzoefu wake binafsi. Mungu anaweza kuonyesha ukweli moja kwa moja, wakati mwanadamu anaweza tu kuonyesha uzoefu unaolingana na huo baada ya kupata uzoefu wa ukweli. … Unatakiwa tu kulinganisha tofauti baina yao ili kuonyesha kama ni kazi ya Mungu mwenyewe au kazi ya mwanadamu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kazi ya Mungu na Kazi ya Mwanadamu). Maneno ya Mwenyezi Mungu huturuhusu kuelewa kwamba kazi ya Mungu ni kazi ya kuanzisha enzi mpya. Ni kazi inayookoa wanadamu wote. Mwanadamu hawezi kuanzisha enzi yoyote, wala hawezi kufanya kazi ya kuwaokoa wanadamu. Kazi ya mwanadamu ni kufanya tu wajibu wa mwanadamu juu ya msingi wa kazi ya Mungu. Ni kufanya kazi fulani kuwanyunyiza, kuwaruzuku na kuwaongoza watu kuingia katika uhalisi wa maneno ya Mungu na inafanywa kwa ushirikiano na Mungu, lakini kazi ya mwanadamu haiwezi kuchukua nafasi ya kazi ya Mungu Mwenyewe hata kidogo, wala haiwezi kuchukuliwa kuwa katika kundi moja na kazi ya Mungu. Chukua mfano wa Enzi ya Neema, wakati Bwana Yesu alianza Enzi ya Neema na kukamilisha Enzi ya Sheria, akiwaongoza wanadamu kuingia katika enzi mpya. Baada ya Bwana Yesu kumaliza kazi Yake, mtume Petro na wengine walianza kuendeleza kazi ya Bwana Yesu, kuliongoza na kulichunga kanisa na kuwaongoza ndugu kufuata njia ya Bwana. Hili lilifanywa katika ushirika na kazi ya Bwana Yesu kabisa. Wakati huo, watu wa kanisa walikubali uchungaji na uongozi wa Petro, lakini hakuna mtu aliyesema kwamba alikuwa akimwamini Petro ama mitume wengine. Huu ni ukweli. Katika namna iyo hiyo, Mwenyezi Mungu wa siku za mwisho amekuja na amekamilisha Enzi ya Neema na kuanzisha Enzi ya Ufalme; Anatekeleza kazi ya hukumu kuanzia na nyumba ya Mungu na kuonyesha ukweli wote ili kuwatakasa na kuwaokoa wanadamu, Ikiwa tunaweza kuelewa, kutenda na kuingia katika ukweli huu, basi sisi ndio wale tutakaopata wokovu wa kweli na kukamilishwa. Hata hivyo, kwa sababu ya ubora wetu duni wa tabia, kupitia kusoma maneno ya Mungu sisi wenyewe na kupitia maneno ya Mungu, kupata wokovu wa kweli ni mchakato mgumu na wa polepole sana. Kwa hivyo, Mungu alimwandikisha mwanadamu anayetumiwa na Roho Mtakatifu kutuongoza. Mwanadamu anayetumiwa na Roho Mtakatifu ametayarishwa na kukamilishwa na Mungu mapema. Ana uzoefu wa kupata wokovu na ukamilisho kupitia kazi ya Mungu. Anatumia uzoefu wake wa maneno ya Mungu kutuongoza kujua maneno ya Mungu na kuingia maneno ya Mungu. Hili linatusaidia tusipotoke sana kutoka katika njia. Alimradi tukubali na kutii uongozi na unyunyizaji wa mwanadamu anayetumiwa na Roho Mtakatifu, basi tunaweza kuchukua njia sahihi ya kumwamini Mungu na kupata wokovu wa kweli. Huu ni wema na baraka wa Mungu kwetu kabisa. Kazi ambayo mwanadamu anayetumiwa na Roho Mtakatifu hufanya ni kumtukuza na kumshuhudia Mungu na kutuongoza kutii na kumwabudu Mungu. Hajawahi kututaka tumchukulie kama Mungu, wala hajadai kwamba tumwamini. Wateule wote wa Mungu wanaelewa sana hili: Mwanadamu anayetumiwa na Roho Mtakatifu ni ndugu yetu na kiongozi wetu tu, na tunamwamini Kristo wa siku za mwisho, Mwenyezi Mungu, si mwanadamu ambaye Roho Mtakatifu hutumia. Imevumishwa mtandaoni kwamba tunamwamini mwanadamu anayetumiwa na Roho Mtakatifu. Huku ni kugeuzwa kabisa kwa ukweli na mkanganyo wa lililo sahihi na lisilo sahihi. Ni dhana ya Shetani yenye kosa na ni uongo wa kuwadanganya watu. Unaweza pia kwenda katika Kanisa la Mwenyezi Mungu kujionea mwenyewe, utembee miongoni mwa ndugu, uwasikilize na uelewe kwa kweli. Kisha utaona kwamba tunasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, tunaomba katika jina la Mwenyezi Mungu na tunamwamini Mungu mwenye mwili Mwenyewe, yaani, Mwenyezi Mungu, Kristo wa siku za mwisho. Kristo anatawala Kanisa la Mwenyezi Mungu kabisa. Ni maneno ya Mungu yanayotawala. Kwa hivyo niambie, tunamwamini mwanadamu ama Mungu? Je, hili si dhahiri?” Baada ya kusikiza ushirika wa dada huyo, nilikuja kujua kiasi kuhusu kazi ya Mungu na kazi ya mwanadamu, na pia nilielewa kiasi kuhusu nia ya Mungu katika kumtumia mwanadamu anayetumiwa na Roho Mtakatifu. Nilijua pia kwamba tulimwamini Mwenyezi Mungu mwenye mwili, si mwanadamu. Sikuweza kuzuia kujiwazia: Tulichopokea ni kazi ya Mungu na ruzuku ya maneno ya Mungu. Tunamwamini Mwenyezi Mungu; hatufuati ama kumwamini mwanadamu. Inaonekana kwamba uvumi huo mtandaoni kweli ni uongo wa Shetani, uongo unaonuiwa kuwadanganya watu. Mwanzoni, mababu zetu wa kwanza, Adamu na Hawa, walidanganywa na hila za Shetani; walitenda dhambi na kufukuzwa kutoka Bustani ya Edeni kwa sababu walisikiliza uongo wa Shetani. Watu wa Kiyahudi walioungana na Mafarisayo katika kumsulubisha Bwana Yesu pia walisikiliza uvumi na wakadanganywa na hila za Shetani na kuwa watenda dhambi wa milele dhidi ya Mungu. Lazima nijifunze kutoka kwa mafunzo ya kutofaulu kwa awali. Sipaswi kudanganywa tena na Shetani!

Dada Wu alipoondoka, aliniambia nisome maneno ya Mungu zaidi na pia akaniachia ushirika wa mwanadamu anayetumiwa na Roho Mtakatifu nisome. Siku moja niliona kifungu cha ushirika: “Katika wakati huu muhimu wa mwisho, watu wanapaswa kufanya yafuatayo yawe kipaumbele katika utendaji wao: kula na kunywa maneno ya Mungu, kufanya chochote kile ambacho Mungu amewaaminia kufanya, kutekeleza wajibu wao, kumridhisha Mungu, na kumtukuza Mungu—ni kwa kutenda kwa njia hizi pekee ndiyo watu wanaweza kuwa waaminifu kwa Mungu. Watakatifu wa zamani mara nyingi walisema, ‘Tunachopata au kupoteza hakijalishi; tunapaswa kuzingatia mapenzi ya Mungu.’ Hii inapaswa kuwa kauli mbiu ya watu wote. Utendaji maalumu ni kama ufuatao: mtu akiteswa na mashambulio ya Shetani, basi kazi ya kwanza ni kutetea ushuhuda wa Mungu na kazi ya Mungu na kutumia ukweli kumshinda Shetani; mtu akikabili dhambi au jaribio, basi kumtukuza Mungu huwa jambo la kwanza, na lazima mtu asitende dhambi na kumfedhehesha Mungu; watu, maswala, au vitu vikizuia kutimizwa kwa wajibu wa mtu, basi kile ambacho Mungu humwaminia mtu huwa jambo la kwanza na mtu lazima ajitenge na matatizo yote na kuwa mwaminifu kwa Mungu; ikiwa na wakati ambapo mambo yanayohusu masilahi ya mtu binafsi yanatokea, basi masilahi ya familia ya Mungu huwa jambo la kwanza. Kutelekeza masilahi ya mtu binafsi na kuudhukuru moyo wa Mungu ni muhimu. Mambo ya kidunia yakimtatiza na kumzuia mtu, basi kutimiza wajibu wake na kumridhisha Mungu lazima kuwe jambo la kwanza na mtu lazima atelekeze mambo mengine yote na ajitumie kwa ajili ya Mungu” (Ushirika kutoka kwa Aliye Juu). Nilikuja kujua wazi kabisa kutoka kwa ushirika wa mwanadamu anayetumiwa na Roho Mtakatifu jinsi ninavyopaswa kutenda katika maisha halisi ili kuyaridhisha mapenzi ya Mungu na kile cha kufanya ili kuwa mwaminifu kwa Mungu. Nilihisi kwamba mwanadamu anayetumiwa na Roho Mtakatifu kweli alikuwa akituongoza tumtii Mungu, tuingie katika ukweli na kutimiza mapenzi ya Mungu. Nilikuja kufahamu kwamba yule “mkalimani” ambaye Mungu ametupangia kweli ni hodari sana! Nilihisi dhahiri hata zaidi kwamba Mungu ametutayarishia mapema mtu anayetumiwa na Roho Mtakatifu kutuongoza kuelewa ukweli haraka zaidi na kuja kumjua Mungu. Huu ni upendo wa kweli wa Mungu kwetu! Wakati huu, nilibaini na kutupa kabisa uvumi huo uliokuwa umeenezwa mtandaoni ulioshutumu kazi ya siku za mwisho ya Mungu na kushambulia mwanadamu anayetumiwa na Roho Mtakatifu. Baada ya kuhisi mwenye wasiwasi, hatimaye niliweza kutulia. Kweli nilikuja kuamini kwamba Mwenyezi Mungu ndiye Bwana Yesu aliyerudi. Kwa kukubali kazi ya siku za mwisho ya Mwenyezi Mungu, naenda sambamba na nyayo za Mwanakondoo, nahudhuria karamu ya harusi ya Mwanakondoo na nainuliwa mbele ya kiti cha Mungu cha enzi!

Baada ya kupitia usumbufu huu wa Shetani, nilishawishika hata zaidi kuhusu kazi ya siku za mwisho ya Mwenyezi Mungu. Sasa nimemfuata Mwenyezi Mungu kwa zaidi ya muongo mmoja. Nakumbuka fikira zote nilizokuwa nazo nilipokuwa nimetoka tu kukubali kazi ya siku za mwisho ya Mungu, hadi kuelewa ukweli kiasi na kubaini uvumi wa serikali ya CCP najamii ya dini, kuweka kando fikira zangu na kutodanganywa tena, hadi kujitahidi kufuatilia ukweli na kufanya wajibu wangu kama kiumbe aliyeumbwa na kulipiza upendo wa Mungu, na kumfuata Mwenyezi Mungu kwa uthabiti. Haya yote yamenifanya nithamini sana ukweli wa maneno haya ya Mungu: “Katika uhusiano wake na Mungu mwenye mwili, mwanadamu huwa anapiga hatua kutoka katika upinzani na kuwa mtii, kutoka katika mateso na kukubaliwa, kutoka katika mitazamo na kuwa na maarifa, na kutoka kukataliwa hadi upendo. Haya ni matokeo ya kazi ya Mungu mwenye mwili(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mwanadamu Aliyepotoka Anahitaji Zaidi Wokovu wa Mungu Mwenye Mwili). Shukrani ziwe kwa Mungu!

Tanbihi:

a. Mtu/kitu kinachodhihirisha uzuri/ubora wa kingine kwa kuvilinganisha.

Iliyotangulia: 20. Nabaini Uwongo wa Serikali ya CCP na Upendo wa Mungu Unanirudisha Kwake

Inayofuata: 22. Kukimbia Kutoka katika “Tundu la Chui”

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

4. Mwamko wa Roho Aliyedanganywa

Na Yuanzhi, BraziliNilizaliwa katika mji mdogo huko Kaskazini mwa China na mnamo 2010, nikafuata jamaa kwenda Brazili. Hapa nchini Brazili,...

43. Kupotea na Kurejea Tena

Na Xieli, MarekaniNilikuja Marekani kufanya kazi kwa bidii kama vile ningeweza kutafuta maisha yenye furaha na hali ya juu ya maisha....

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp