Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VI

Utakatifu wa Mungu (III)

Mada tuliyoishiriki wakati uliopita ilikuwa utakatifu wa Mungu. Ni kipengele kipi cha Mungu Mwenyewe kinahusisha utakatifu wa Mungu? Je, kinahusisha kiini cha Mungu? (Ndiyo.) Kwa hivyo ni nini mada inayohusiana na kiini cha Mungu katika ushirika wetu? Je, ni utakatifu wa Mungu? Utakatifu wa Mungu: hiki ni kiini cha kipekee cha Mungu. Ni nini ilikuwa dhamira kuu tuliyoshiriki wakati uliopita? (Utambuzi wa uovu wa Shetani. Yaani, jinsi Shetani anampotosha mwanadamu; anatumia maarifa, sayansi, desturi ya kitamaduni, ushirikina, na mitindo ya kijamii kupotosha mwanadamu.) Hii ndiyo ilikuwa mada kuu tuliyojadili wakati uliopita. Shetani hutumia maarifa, sayansi, ushirikina, desturi ya kitamaduni, na mitindo ya kijamii kumpotosha mwanadamu; hizi ndizo njia ambazo Shetani anampotosha mwanadamu. Hizi ni njia tano kwa jumla. Mnafikiri Shetani anatumia nini zaidi kumpotosha mwanadamu, kitu ambacho kinampotosha kwa kina zaidi? (Desturi ya kitamaduni. Hii ni kwa sababu falsafa za kishetani kama vile mafundisho ya Confucius na Mencius zimetopea sana katika akili zetu.) Baadhi ya ndugu wanafikiri ni desturi za kitamaduni. Mwingine yeyote? (Maarifa. Maarifa hayawezi kuturuhusu kumwabudu Mungu. Yanapinga kuwepo kwa Mungu, na yanapinga kanuni ya Mungu. Yaani, Shetani hutuambia tusome kuanzia umri mdogo, na kwamba ni kupitia tu kusoma na kupata maarifa ndipo siku zetu za baadaye na kudura zetu zinahakikishwa.) Shetani anatumia maarifa kudhibiti siku zako za baadaye na kudura yako, kisha anakuongoza kuendelea kupitia pua lako; hivi ndivyo unavyofikiria Shetani anampotosha mwanadamu kwa kina zaidi. Kwa hivyo wengi wenu wanafikiri Shetani anatumia maarifa kumpotosha mwanadamu kwa kina. Kuna yeyote aliye na maoni tofauti? Je, sayansi na mitindo ya kijamii, kwa mfano? Kuna yeyote anayekubaliana na haya? (Ndiyo.) Leo Nitashiriki tena kuhusu njia tano ambazo Shetani anampotosha mwanadamu, na, baada ya Mimi kumaliza, Nitawauliza baadhi ya maswali ili kuona ni katika kipengele kipi hasa Shetani anampotosha mwanadamu kwa kina zaidi.

Njia Tano Ambamo Shetani Humptosha Mwanadamu

a. Shetani Hutumia Maarifa Kumpotosha Mwanadamu, na Yeye Hutumia Umaarufu na Faida Kumdhibiti

Kati ya njia tano ambazo Shetani anatumia kumpotosha mwanadamu ni njia tano anavyompotosha mwanadamu, ya kwanza tano tuliyotaja ni maarifa, kwa hivyo wacha kwanza tuchukue maarifa kama mada ya kushiriki. Shetani hutumia maarifa kama chambo. Sikiza kwa makini: Ni aina tu ya chambo. Watu wanavutiwa “kusoma kwa bidii na kuboreka kila siku,” kujihami kwa maarifa, kama silaha, kisha kutumia maarifa kufungua njia ya sayansi; kwa maneno mengine, kadri unapopata maarifa zaidi, ndivyo utakavyoelewa zaidi. Shetani huwaambia watu haya yote. Shetani huwaambia watu kuwa na fikira za juu pia, kwa wakati sawa wanaposoma maarifa, akiwaambia kuwa na matarajio na mawazo. Bila kujua kwa watu, Shetani anasambaza ujumbe mwingi kama huu, na kuwafanya watu kuhisi bila kujua kwamba vitu hivi ni sahihi, ama ni vya manufaa. Bila kujua, watu wanaitembea njia hii, bila kujua wanaongozwa mbele na matarajio na mawazo yao. Hatua kwa hatua, kwa kutojua wanajifunza kutoka kwa maarifa waliyopewa na Shetani njia ambazo watu wakubwa ama maarufu wanafikiria. Wanajifunza pia mambo fulani kutoka kwa matendo ya wengine ambao wanafikiriwa kuwa mashujaa. Shetani anatetea nini kwa mwanadamu katika matendo ya hawa mashujaa? Ni nini anachotaka kuingiza kwa mwanadamu? Mwanadamu lazima awe mzalendo, awe na uadilifu wa kitaifa, na awe shujaa. Ni yapi ambayo mwanadamu anajifunza kutoka kwa baadhi ya hadithi za kihistoria ama kutoka kwa wasifu wa mashujaa? Kuwa na hisia ya uaminifu wa kibinafsi, ama kufanya lolote kwa ajili ya rafiki ya mtu ama kwa rafiki. Miongoni mwa maarifa haya ya Shetani, mwanadamu bila kujua anajifunza mambo mengi hasi. Katikati ya kutojua huku, mbegu zilizotayarishwa kwa ajili yao na Shetani zinapandwa katika akili zao zisizokomaa. Mbegu hizi zinawafanya kuhisi kwamba wanapaswa kuwa watu wakubwa, wanapaswa kuwa maarufu, wanapaswa kuwa mashujaa, kuwa wazalendo, kuwa watu wanaopenda familia zao, ama kuwa watu wanaoweza kufanya chochote kwa ajili ya rafiki na kuwa na hisia za uaminifu wa kibinafsi. Baada ya kushawishiwa na Shetani, bila kujua wanatembea njia ambayo amewatayarishia. Wanapotembea njia hii, wanalazimika kukubali kanuni za Shetani za kuishi. Bila kujua na bila wao kuwa na uelewa kabisa, wanakuwa na kanuni zao za kuishi, wakati hizi si chochote ila kanuni za Shetani ambazo zimeingizwa kwao kwa nguvu. Wakati wa mchakato wa kujifunza, Shetani anawasababisha kukuza malengo yao wenyewe, kuamua malengo yao ya maisha wenyewe, kanuni za kuishi, na mwelekeo wa maisha, wakati huo wote anawaingizia mambo ya Shetani, kwa kutumia hadithi, kwa kutumia wasifu, kwa kutumia mbinu zote zinazowezekana kuwapata watu, kuchukua chambo polepole. Kwa njia hii, katika mkondo wa kujifunza kwao, wengine wanakuja kupenda fasihi, wengine uchumi, wengine unajimu ama jiografia. Kisha kuna wengine wanaokuja kupenda siasa, wengine wanaopenda fizikia, wengine kemia, na hata wengine wanaopenda teolojia. Haya yote ni sehemu ya maarifa. Katika mioyo yenu, kila mmoja wenu anajua yalivyo na mambo haya, kila mmoja amepatana nayo awali. Kuhusiana na maarifa ya aina hii, yeyote anaweza kuzungumza bila kikomo kuhusu moja yao fulani. Na hivyo ni wazi jinsi maarifa haya yameingia kwa kina katika akili ya mwanadamu, pia inaonyesha nafasi iliyochukuliwa na maarifa haya katika akili ya mwanadamu na jinsi yalivyo na athari ya kina kwa mwanadamu. Punde tu mtu anapenda sehemu ya maarifa, wakati katika moyo wake mtu amependa kwa dhati mojawapo, basi bila kujua anaendeleza mawazo: Watu wengine wanataka kuwa watunzi, wengine wanataka kuwa waandishi, wengine wanataka kuwa na kazi kutokana na siasa, na wengine wanataka kushiriki katika uchumi na kuwa wanabiashara. Kisha kuna kundi la watu ambao wanataka kuwa mashujaa, kuwa wakubwa ama maarufu. Bila kujali mtu anataka kuwa mtu wa aina gani, lengo lake ni kuchukua mbinu hii ya kujifunza maarifa na kuitumia kwa ajili yake, kufikia matamanio yake, mawazo yake mwenyewe. Haijalishi inasikika kuwa nzuri namna gani—anataka kufikia ndoto yake, asiishi katika maisha haya bure, ama anataka kushiriki katika kazi—anakuza haya mawazo na matarajio ya juu lakini, kimsingi, yote ni ya nini? Je, mmeyafikiria haya awali? Mbona Shetani anataka kufanya hivi? Madhumuni ya Shetani ni yapi katika kuyaweka mambo haya kwa mwanadamu? Mioyo yenu lazima ielewe vizuri swali hili.

Sasa wacha tuzungumze kuhusu jinsi Shetani hutumia maarifa kumpotosha mwanadamu. Kwanza, tunapaswa kuwa na ufahamu wazi wa haya mambo: Kwa maarifa, ni kipi ambacho Shetani Anataka kumpa mwanadamu? Anataka kumfanyia nini mwanadamu kwa kutumia maarifa? Kumwongoza mwanadamu kufuata njia ya aina gani? (Kumpinga Mungu.) Bila shaka ni kumpinga Mungu. Hii ni matokeo unayoweza kuyaona kutoka kwa watu kupata maarifa—kumpinga Mungu. Hivyo ni nini malengo husuda ya Shetani? Hujayaelewa, sio? Katika mchakato wa mwanadamu kujifunza maarifa, Shetani atatumia mbinu zozote, iwe kufafanua hadithi, akimpa tu kipande kimoja cha maarifa, au kumruhusu aridhishe tamaa zake au aridhishe mawazo. Shetani anataka kukuongoza katika njia gani? Watu wanafikiri kwamba hakuna chochote kibaya na kujifunza maarifa, kwamba ni mkondo wa kiasili. Kuisema bila kutia chumvi, kukuza mawazo ya juu ama kuwa na matarajio ni kuwa na hamu ya kupata, na hii inapaswa kuwa njia sawa katika maisha. Iwapo watu wanaweza kufanikisha mawazo yao wenyewe, ama kuwa na kazi maishani mwao—je, si ni adhimu zaidi kuishi namna hii? Kwa kufanya mambo haya, mtu anaweza kuheshimu babu zake na pia ana nafasi ya sifa yake katika historia—si hili ni jambo zuri? Hili ni jambo zuri katika macho ya watu wa kidunia na kwao linapaswa kuwa la kufaa na njema. Je, Shetani, hata hivyo, na malengo yake husuda, anawapeleka tu watu kwa njia ya aina hii na kisha kuamua amemaliza? Bila shaka la. Kwa kweli, haijalishi jinsi yalivyo juu mawazo ya mwanadamu, haijalishi matamanio ya mwanadamu ni ya uhalisi jinsi gani ama jinsi yote yanaweza kuwa ya kufaa, yote ambayo mwanadamu anataka kufikia, yote ambayo mwanadamu anatafuta yameunganishwa bila kuchangulika na maneno mawili. Haya maneno mawili ni muhimu sana kwa maisha ya kila mtu, na haya ni mambo ambayo Shetani ananuia kuingiza ndani ya mwanadamu. Maneno haya mawili ni yapi? Ni “umaarufu” na “faida”: Shetani anatumia njia ya hila sana, njia ambayo iko pamoja sana na dhana za watu; si aina ya njia kali. Katikati ya kutoelewa, watu wanakuja kukubali njia ya Shetani ya kuishi, kanuni zake za kuishi, kuanzisha malengo ya maisha na mwelekeo wao katika maisha, na kwa kufanya hivyo wanakuja pia bila kujua kuwa na mawazo katika maisha. Haijalishi mawazo haya yanaonekana kusikika kuwa ya juu kiasi gani katika maisha, ni kisingizio tu ambacho kinahusiana kwa kutochangulika kwa umaarufu na faida. Mtu yeyote aliye mkubwa ama maarufu, watu wote kwa hakika, chochote wanachofuata maishani kinahusiana tu na haya maneno mawili: “umaarufu” na “faida.” Watu hufikiri kwamba punde tu wanapata umaarufu na faida, wanaweza basi kuyatumia kwa faida yao kufurahia hadhi ya juu na utajiri mwingi, na kufurahia maisha. Baada ya wao kuwa na umaarufu na faida, wanaweza basi kuyatumia kwa faida yao katika kutafuta kwao raha na kufurahia kwao kwa fidhuli mwili. Watu kwa hiari, lakini bila kujua, wanachukua miili na akili zao na vyote walivyonavyo, siku zao za baadaye, na kudura zao na kuzikabidhi zote kwa Shetani ili kupata umaarufu na faida wanayotaka. Watu kweli hufanya hivi kamwe bila kusita kwa muda, kamwe bila kujua haja ya kupata tena yote. Je, watu bado wanaweza kujidhibiti baada ya wao kumkimbilia Shetani na kuwa mwaminifu kwake kwa njia hii? Bila shaka, la. Wanadhibitiwa na Shetani kikamilifu na kabisa. Pia kikamilifu na kabisa wamezama katika bwawa na hawawezi kujinusuru. Baada ya mtu kukwama katika umaarufu na faida, hatafuti tena kile kilichong’aa, kile chenye haki ama yale mambo ambayo ni mazuri na mema. Hii ni kwa sababu nguvu za ushawishi ambazo umaarufu na faida yanayo juu ya watu ni kubwa mno, na vinakuwa vitu vya watu kutafuta katika maisha yao yote na pia milele bila kikomo. Hili si ukweli? Watu wengine watasema kwamba kujifunza maarifa si chochote zaidi ya kusoma vitabu ama kujifunza mambo kadhaa ambayo hawajui tayari, ili wasiwe nyuma ya nyakati ama wasiwachwe nyuma na dunia. Maarifa yanafunzwa tu ili waweze kuweka chakula mezani, kwa sababu ya siku zao za baadaye ama kwa sababu ya mahitaji ya kimsingi. Kuna mtu yeyote ambaye atastahimili mwongo wa kusoma kwa bidii kwa mahitaji ya kimsingi tu, ili kutatua swala la chakula tu? Hakuna watu kama hawa. Kwa hivyo ni nini anatesekea matatizo haya na kutesekea miaka hii yote? Ni kwa sababu ya umaarufu na faida: Umaarufu na faida yanamngoja mbele, yanamwita, na anaamini tu kwa kupitia bidii yake mwenyewe, matatizo na mapambano ndiyo anaweza kufuata ile njia na hivyo kupata umaarufu na faida. Lazima ateseke matatizo haya kwa sababu ya njia yake ya siku za baadaye, kwa sababu ya raha yake ya siku za baadaye na kwa sababu ya maisha bora. Mnaweza kuniambia—haya maarifa kwa hakika ni nini? Je, si kanuni na falsafa za kuishi ambazo Shetani hutia ndani ya mwanadamu, kama vile “Penda Chama, penda nchi, na penda dini yako” na “Mtu mwenye hekima hutii hali”? Je, si “maadili ya hali ya juu” ya maisha yaliyoingizwa kwa mwanadamu na Shetani? Chukua, kwa mfano, mawazo ya watu wakubwa, uadilifu wa watu maarufu ama roho jasiri ya watu mashujaa, ama chukua uungwana na wema wa nguli na wenye panga katika riwaya za kareti—je, si hizi zote ni njia ambamo Shetani anatia mawazo haya? Mawazo haya hushawishi kizazi kimoja baada ya kingine, na watu wa kila kizazi wanaletwa kuyakubali mawazo haya. Wao huhangaika sikuzote wakifuatilia “maadili ya hali ya juu” ambayo hata watayatoa maisha yao kafara kwa ajili yake. Hii ndiyo njia na namna ambayo Shetani hutumia maarifa kuwapotosha watu. Hivyo baada ya Shetani kuwaelekeza watu kwenye njia hii, je, wanaweza kumtii na kumwabudu Mungu? Na, je, wanaweza kuyakubali maneno ya Mungu na kufuatilia ukweli? La hasha—kwa sababu wamepotoshwa na Shetani. Hebu tuangalie tena maarifa, mawazo, na maoni yaliyotiwa polepole ndani ya watu na Shetani: Je, mambo haya yana ukweli wa utii kwa Mungu na kumwabudu Mungu? Je, kuna ukweli wa kumcha Mungu na kuepuka maovu? Je, kuna maneno yoyote ya Mungu? Je, kuna chochote ndani yao kinachohusiana na ukweli? Hakuna chochote kabisa—vitu hivi havipo kabisa. Je, mnaweza kuwa na uhakika kwamba mambo yaliyotiwa polepole ndani ya watu na Shetani hayana ukweli wowote? Hamwezi kuthubutu—lakini haijalishi. Alimradi mtambue kwamba “umaarufu” na “faida” ni maneno mawili muhimu ambayo Shetani hutumia kuwashawishi watu kuingia njia ya uovu, basi hilo limetosha.

Acha turejelee tena kwa ufupi: Shetani hutumia nini kuendelea kumfungia mwanadamu na kumdhibiti? (Umaarufu na faida.) Kwa hivyo Shetani hutumia umaarufu na faida kudhibiti fikira za mwanadamu hadi anachofikiria tu ni umaarufu na faida. Wanapambana kwa sababu ya umaarufu na faida, wanateseka matatizo kwa sababu ya umaarufu na faida, wanastahimili udhalilishaji kwa sababu ya umaarufu na faida, wanatoa kila kitu walichonacho kwa sababu ya umaarufu na faida, na watafanya maoni au uamuzi wowote kwa ajili ya umaarufu na faida. Kwa njia hii, Shetani humfunga mwanadamu kwa pingu zisizoonekana. Pingu hizi zinabebwa na watu, na hawana nguvu ama ujasiri wa kuzirusha mbali. Kwa hivyo, bila kujua, watu huvumilia pingu hizi na kutembea kwenda mbele kwa ugumu mkubwa. Kwa ajili ya umaarufu huu na faida hii, binadamu humwepuka Mungu na kumsaliti, na wanazidi kuwa waovu zaidi na zaidi. Kwa njia hii, hivyo kizazi kimoja baada ya kingine kinaharibiwa katika umaarufu na faida ya Shetani. Tukiangalia sasa vitendo vya Shetani, nia zake husuda ni za kuchukiza? Pengine leo bado hamwezi kuona kupitia nia husuda za Shetani kwa sababu mnafikiri hakuna maisha bila umaarufu na faida. Mnafikri kwamba, iwapo watu wataacha umaarufu na faida nyuma, basi hawataweza tena kuona njia mbele, hawataweza tena kuona malengo yao, siku zao za baadaye zawa giza, zilizofifia na za ghamu. Lakini, polepole, nyote siku moja mtatambua kwamba umaarufu na faida ni pingu za ajabu ambazo Shetani hutumia kumfunga mwanadamu. Hadi ile siku utakuja kutambua hili, utapinga kabisa udhibiti wa Shetani na utapinga kabisa pingu anazoleta Shetani kukufunga. Wakati utakapofika wa wewe kutaka kutupilia mbali vitu vyote ambavyo Shetani ameingiza ndani yako, utakuwa basi umejiondoa kwa Shetani na pia utachukia kwa kweli vyote ambavyo Shetani amekuletea. Hapo tu ndipo utakuwa na upendo na shauku ya kweli kwa Mungu.

b. Shetani Hutumia Sayansi Kumpotosha Mwanadamu

Tumetoka tu kuongea kuhusu jinsi Shetani hutumia maarifa kumpotosha mwanadamu, basi kinachofuata wacha tushiriki kuhusu jinsi Shetani hutumia sayansi kumpotosha mwanadamu. Kwanza, Shetani hutumia jina la sayansi kuridhisha hamu ya mwanadamu kutafiti sayansi na kuchunguza siri. Kwa jina la sayansi, Shetani huridhisha haja ya mwili na mahitaji ya mwanadamu kuendelea kuinua ubora wao wa maisha. Shetani hivyo, katika jina hili, hutumia njia ya sayansi kumpotosha mwanadamu. Je, ni kufikiria tu kwa mwanadamu ama akili za mwanadamu ambazo Shetani anapotosha kwa kutumia njia hii ya sayansi? Miongoni mwa watu, matukio na mambo katika mazingira yetu ambayo tunaweza kuona na ambayo tunakutana nayo, ni yapi mengine ambayo Shetani anatumia sayansi kupotosha? (Mazingira ya kiasili.) Mko sahihi. Inaonekana kwamba mmedhuriwa sana na hili, na pia mmeathirika sana na yeye. Mbali na kutumia matokeo yote ya utafiti na mahitimisho mbalimbali ya sayansi kumdanganya mwanadamu, Shetani pia hutumia sayansi kama mbinu ya kutekeleza maangamizi na unyonyaji tele wa mazingira ya kuishi aliyopewa mwanadamu na Mungu. Anafanya hivi chini ya kisingizio kwamba iwapo mwanadamu anatekeleza utafiti wa kisayansi, mazingira ya kuishi ya mwanadamu yatakuwa bora na bora zaidi na viwango vya kuishi vya mwanadamu daima vitaboreka, na zaidi ya hayo kwamba maendeleo ya kisayansi yanafanywa ili kuhudumia mahitaji ya mwili ya mwanadamu yanayozidi kila siku na haja yao ya kuendelea kupandisha ubora wao wa maisha. Huu ni msingi wa kidhahania wa maendeleo ya Shetani ya sayansi. Hata hivyo, sayansi imemletea binadamu nini? Je, mazingira yetu ya kuishi—na mazingira ya kuishi ya binadamu wote—hayajachafuliwa? Je, si hewa anayopumua mwanadamu imechafuliwa? Je, si maji tunayokunywa yamechafuliwa? Je, chakula tunachokula bado ni cha ogani na asilia? Nafaka na mboga nyingi zimebadilishwa vinasaba, zimekuzwa kwa mbolea, na nyingine ni aina zilizoundwa kwa kutumia sayansi. Mboga na matunda tunayokula sio asili tena. Hata mayai ya asili si rahisi kupata tena, na mayai hayaonji yalivyokuwa yakionja awali, baada ya kusindikwa na inayoitwa sayansi na Shetani. Kwa kuangalia taswira kubwa, anga nzima imeharibika na kuchafuliwa; milima, maziwa, misitu, mito, bahari, na kila kitu juu na chini ya ardhi vyote vimeharibiwa na inayoitwa mafanikio ya kisayansi. Kwa maneno mengine, mazingira yote ya kiikolojia, mazingira ya kuishi yaliyopewa mwanadamu na Mungu yameangamizwa na kuharibiwa na inayodaiwa kuwa sayansi. Ingawa kuna watu wengi waliopata walichotarajia katika suala la ubora wa maisha wanaotafuta, kuridhisha tamaa na miili yao, mazingira ambayo mwanadamu anaishi kimsingi yameharibiwa na kuangamizwa na “mafanikio” mbalimbali yaliyoletwa na sayansi. Sasa, hatuna tena haki ya kupumua pumzi moja ya hewa safi. Hii ni huzuni ya mwanadamu? Bado kuna furaha yoyote ya kuzungumzia kwa mwanadamu kuishi katika nafasi hii ya kuishi? Mwanadamu anaishi katika nafasi hii ya kuishi na, kutoka mwanzoni, haya mazingira ya kuishi yaliumbwa na Mungu kwa ajili ya mwanadamu. Maji ambayo watu hunywa, hewa ambayo watu hupumua, vyakula mbalimbali ambavyo watu hula, na vilevile mimea na viumbe hai, na hata milima, maziwa, na bahari—kila sehemu ya mazingira haya ya maisha alipewa mwanadamu na Mungu;; ni asili, na hutekeleza kulingana na amri asili iliyotolewa na Mungu. Bila sayansi, watu bado wangefuata mbinu walizopewa na Mungu, wangeweza kufurahia yote yaliyo safi na ya asili, na wangekuwa wenye furaha. Sasa, hata hivyo, haya yote yameangamizwa na kuharibiwa na Shetani; nafasi ya kimsingi ya kuishi ya mwanadamu haipo tena katika hali yake asili zaidi. Lakini hakuna anayeweza kutambua kilichosababisha matokeo ya aina hii ama jinsi haya yalikuja kuwa, na zaidi ya hapo hata watu zaidi wanaelewa na kukaribia sayansi kwa kutumia mawazo waliyoingiziwa na Shetani Je, hii si ya kuchukiza sana na ya kusikitisha? Kwa kuwa Shetani sasa amechukua nafasi ambamo wanadamu wapo na mazingira yao ya kuishi na kuwapotosha kuwa katika hali hii, na kwa kuwa wanadamu wanaendelea kwa njia hii, kuna haja yoyote ya mkono wa Mungu kuwaangamiza wanadamu hawa duniani? Iwapo wanadamu watazidi kuendelea kwa njia hii, watachukua mwelekeo upi? (Wataangamizwa.) Wataangamizwa kwa njia gani? Zaidi ya mwanadamu kutafuta kwa tamaa umaarufu na faida, daima anaendelea kutekeleza uchunguzi wa sayansi na utafiti wa kina, kisha bila kikomo huridhisha mahitaji yake ya mwili na tamaa; yapi tena ni matokeo ya mwanadamu? Kwanza kabisa hakuna tena usawa wa ikolojia na, pamoja na hili, miili ya wanadamu yote imetiwa doa na kuharibiwa na mazingira ya hali hii, na magonjwa mbalimbali ya kuambukiza na mapigo kusambaa kila mahali. Hii ni hali ambayo mwanadamu sasa hawezi kudhibiti, sivyo? Sasa kwa sababu mnaelewa hili, iwapo wanadamu hawamfuati Mungu, lakini daima wanamfuata Shetani kwa njia hii—kutumia maarifa daima kujitajirisha, kutumia sayansi kuchunguza bila kikomo siku za baadaye za maisha ya binadamu, kutumia mbinu ya aina hii kuendelea kuishi—unaweza kutambua jinsi hii itawaishia binadamu? Binadamu watatoweka wasikuwepo tena kiasili: Hatua kwa hatua, binadamu wanazidi kuukaribia uharibifu, wakielekea maangamizi yao wenyewe! Je, huku si kujiletea maangamizi wenyewe? Na, je, si hili ni tokeo la maendeleo ya kisayansi? Inaonekana sasa kama sayansi ni aina ya ushombwe ambao Shetani amemwandalia mwanadamu, ili wakati mnapojaribu kupambanua mambo mnafanya hivyo katika hali ya ukungu; haijalishi mnaangalia kwa ugumu aje, hamwezi kuona mambo kwa wazi, na haijalishi mnajaribu sana vipi, hamwezi kuyatambua. Hata hivyo, Shetani bado anatumia jina la sayansi kuzidisha hamu yako na kukuongoza kwa pua, mguu mmoja mbele ya mwingine, kuelekea shimo na kuelekea kifo. Na hali ikiwa hivi, watu wataona wazi kwamba kwa kweli, maangamizo ya mwanadamu yanaletwa na mkono wa Shetani—Shetani ndiye kiongozi. Sivyo? (Naam, ndivyo.) Hii ndiyo njia ya pili ambayo Shetani humpotosha mwanadamu.

c. Shetani Hutumia Desturi ya Kitamaduni Kumpotosha Mwanadamu

Njia ya tatu ni jinsi Shetani hutumia desturi ya kitamaduni kumpotosha mwanadamu. Kuna usawa mwingi kati ya desturi ya kitamaduni na ushirikina, ni tu kuwa desturi ya kitamaduni ina hadithi fulani, vidokezo, na vyanzo fulani. Shetani ametunga na kuunda ngano ama hadithi nyingi katika vitabu vya historia, na kuacha watu na hisia za kina za desturi ya kitamaduni ama watu wa kishirikina. Chukua kwa mfano Watu Wanane Wasiokufa Wanaovuka Bahari, Safari ya kwenda Magharibi, Mfalme Mkuu Jade, Nezha Anamshinda Joka Mfalme, na Uchunguzi wa Miungu, zote za Uchina. Haya hayajakita mizizi katika akili za mwanadamu? Hata iwapo baadhi yenu hawajui maelezo yote, bado mnajua hadithi za jumla, na yaliyomo kwa jumla ndiyo yanayokwama katika moyo wako na yanakwama katika akili yako, na huwezi kuyasahau. Hizi ni dhana au hadithi ambazo Shetani alimwandalia mwanadamu kitambo sana, na ambazo zimesambazwa katika nyakati tofauti. Haya mambo yanadhuru moja kwa moja na kumomonyoa nafsi za watu na kuweka watu chini ya fingo moja baada ya jingine. Hiyo ni kusema kwamba baada ya wewe kukubali aina hii ya desturi ya kitamaduni, hadithi ama vitu vya ushirikina, mara tu mambo haya yanawekwa kwa akili yako, na mara tu yanakwama katika moyo wako, basi ni kama umeduwazwa—unakamatwa na kushawishika na hizi mitego ya kitamaduni, haya mawazo na hadithi za kitamaduni. Yanashawishi maisha yako, mtazamo wako wa maisha na pia yanashawishi maoni yako ya mambo. Hata zaidi yanashawishi ufuataji wako wa njia sahihi ya maisha: Hii bila shaka ni apizo. Unajaribu lakini huwezi kuyatupilia mbali; unayakatakata lakini huwezi kuyakata chini; unayapiga lakini huwezi kuyapiga chini. Zaidi ya hayo, baada ya mwanadamu bila kujua kuwekwa chini ya aina hii ya apizo, bila kujua, anaanza kumwabudu Shetani, kukuza taswira ya Shetani katika moyo wake. Kwa maneno mengine, anamweka Shetani kama sanamu, kifaa cha yeye kuabudu na kutazamia, hata kwenda mbali kiasi cha kumchukulia kama Mungu. Bila kujua, mambo haya yako katika mioyo ya watu yakidhibiti maneno na matendo yao. Aidha, kwanza unachukulia hadithi na hekaya hizi kuwa uongo, na kisha bila kujua unakubali kuwepo kwa hadithi hizi, kuzitengenezea sanamu halisi na kuzibadili kuwa mambo halisi yaliyopo. Katika kutojua, unapokea haya mawazo bila kufahamu na kuwepo kwa vitu hivi. Pia unapokea bila kufahamu mashetani, Shetani na sanamu ndani ya nyumba yako na ndani ya moyo wako—hii bila shaka ni apizo. Je, mnahisi sawa? (Ndiyo.) Kuna yeyote miongoni mwenu ambao wamechoma ubani na kuabudu Budha? (Ndiyo.) Kwa hivyo madhumuni ya kuchoma ubani na kumwabudu Budha yalikuwa yapi? (Kuombea amani.) Kwa kuifikiria sasa, ni ujinga kuombea amani kutoka kwa Shetani? Shetani analeta amani? (La.) Je, mlikuwa wajinga hapo nyuma? Namna ya aina hiyo ni ya upuuzi, jinga na nyofu, siyo? Shetani anafikiria tu jinsi ya kukupotosha na hawezi kukupa amani; anaweza tu kukupa nafasi ya kupumua ya muda mfupi. Lakini lazima uchukue kiapo na ukivunja ahadi yako ama ukivunja kiapo ulichofanya, basi utaona jinsi anavyokuadhibu. Kwa kukufanya uchukue kiapo, kwa kweli anataka kukudhibiti. Wakati mlipoombea amani, mlipata amani? (La.) Hamkupata amani, lakini kinyume na hayo alileta bahati mbaya, majanga yasiyoisha kweli bahari isiyo na mipaka ya uchungu. Amani haiko miongoni mwa miliki ya Shetani, na hili ni ukweli. Haya ndiyo matokeo kwa wanadamu ya ushirikina wa kikabila na desturi ya kitamaduni.

d. Shetani Hutumia Mienendo ya Kijamii Kumpotosha Mwanadamu

Njia ya mwisho ambayo kwayo Shetani humpotosha na kumtawala mwanadamu ni kupitia mitindo ya kijamii. Mitindo ya kijamii inajumuisha vipengele mengi, ikiwa ni pamoja na maeneo mbalimbali kama vile kuabudu watu mashuhuri na wenye kusifika, na vilevile waigizaji filamu na wanamuziki mashuhuri, kuwaabudu watu mashuhuri, michezo ya mtandaoni, n.k.—hizi zote ni sehemu ya mitindo ya kijamii, na hakuna haja ya kuingia katika maelezo mengi hapa. Tunataka tu kuzungumza kuhusu mawazo ambayo mitindo ya kijamii inaleta kwa watu, jinsi inasababisha watu kutenda duniani, malengo ya maisha na mtazamo ambao inaleta kwa watu. Hii ni muhimu sana; wanaweza kudhibiti na kushawishi mawazo na maoni ya watu. Mitindo hii huibuka mmoja baada ya mwingine, na yote huwa na ushawishi mbaya unaoendelea kumdhalilisha mwanadamu na kuwafanya watu kupoteza dhamiri, ubinadamu na akili, kudhoofisha zaidi maadili yao na ubora wa tabia zao, kiasi kwamba tunaweza hata kusema kwamba watu wengi sasa hawana uadilifu, hawana ubinadamu, na wala hawana dhamiri yoyote, sembuse kuwa na akili yoyote. Kwa hivyo mienendi hii ya kijamii ni ipi? Ni mienendo ambayo huwezi kuona kwa macho. Wakati mtindo mpya unapoenea duniani kote, pengine ni idadi ndogo tu ya watu ndio walio na ufahamu wa juu, wakitenda kama waanzishaji mitindo. Wao huanza kwa kufanya jambo jipya, kisha kukubali aina fulani ya wazo au aina fulani ya mtazamo. Hata hivyo, watu wengi, wataendelea kuambukizwa, kuvutiwa na kustaarabishwa na mtindo huu katika hali ya kutofahamu, hadi wote bila kujua na bila kupenda wanamkubali na wanazama ndani yake na kudhibitiwa na yeye. Moja baada ya nyingine, mitindo ya aina hii inawafanya watu ambao si wa mwili na akili timamu, wasiojua ukweli, na hawawezi kutofautisha kati ya vitu vyema na hasi, mitindoinawafanya kukubali mitindokwa furaha vilevile mtazamo wa maisha, na maadili yatokayo kwa Shetani. Wanakubali anachowaambia Shetani kuhusu jinsi ya kukaribia maisha na jinsi ya kuishi ambayo Shetani “amewapa.” Na hawana nguvu, wala uwezo, wala ufahamu wa kupinga. Kwa hivyo, utaitambuaje mitindo kama hii? Nimechagua mfano rahisi ambao mnaweza kuja kuelewa polepole. Kwa mfano, watu wa kale waliendesha biashara zao kwa njia ambayo haikudanganya wazee wala vijana, na ambayo iliuza bidhaa kwa bei sawa bila kujali aliyekuwa akinunua. Je, dokezo la dhamiri na ubinadamu haliwasilishwi hapa? Wakati watu walitumia aina hii ya imani walipokuwa wakifanya biashara zao, inaonyesha kwamba bado walikuwa na baadhi ya dhamiri, baadhi ya ubinadamu wakati huo. Lakini na mahitaji ya mwanadamu ya kiasi kinachopanda daima cha pesa, watu bila kujua walikuja kupenda pesa, hupenda faida na hupenda raha zaidi na zaidi. Kwa hivyo watu walikuja kuona pesa kuwa muhimu zaidi? Wakati watu wanaona pesa kuwa muhimu zaidi, bila kujua wanapuuza sifa, umashuhuri wao, ufahari, na uadilifu wao, sivyo? Unapojihusisha katika biashara, unawaona wengine wakiwa matajiri kwa kuwahadaa wengine. Ingawa pesa zinazochumwa si halali, wanazaidi kuwa matajiri. Unapoona yote ambayo familia zao zinafurahia hukukasirisha: “Sote wawili tuko katika biashara lakini walikuwa matajiri. Kwa nini nisiweze kuchuma pesa nyingi? Siwezi kuvumilia hili—lazima nitafute njia ya kupata pesa zaidi.” Baada ya hayo, unachofikiria ni jinsi ya kutengeneza utajiri wako tu. Mara tu unapoacha kuamini kwamba “fedha inapaswa kupatikana kwa dhamiri, bila kumdanganya mtu yeyote,” basi, ukiongozwa na maslahi yako mwenyewe, kufikiri kwako kunabadilika polepole, na vile vile maadili ya matendo yako. Unapomhadaa mtu kwa mara ya kwanza, unahisi ukishutumiwa na dhamiri yako, na moyo wako unakuambia, “Hili linapokamilika, hii ni mara ya mwisho ambayo nitamdanganya mtu. Kuwadanganya watu siku zote kutasababisha adhabu!” Hii ndiyo kazi ya dhamiri ya mwanadamu—kukufanya uhisi aibu na kukushutumu, ili ihisi kuwa siyo asili wakati unamdanganya mtu. Lakini baada ya wewe kufanikiwa kumdanganya mtu unaona kwamba sasa una pesa zaidi kuliko awali, na unafikiria mbinu hii inaweza kuwa ya manufaa sana kwako. Licha ya maumivu madogo ndani ya moyo wako, bado unahisi kujipongeza kwa mafanikio yako, na unahisi kuridhika mwenyewe kiasi. Kwa mara ya kwanza, unakubali tabia yako mwenyewe, njia zako mwenyewe za uwongo. Punde mwanadamu amechafuliwa na kudanganywa huku, ni sawa na mtu ambaye anahusika na kamari na kisha anakuwa mchezaji kamari. Katika kutoelewa, anapenda tabia yake ya kudanganya na anaikubali. Katika hali yako ya kutoelewa, unakubali udanganyifu. Katika hali yako ya kutoelewa unachukua udanganyifu kuwa tabia halali ya kibiashara, na unachukua kudanganya kuwa mbinu ya manufaa zaidi ya kusalimika kwako na riziki yako; unafikiria kwamba kwa kufanya hivi anaweza kutengeneza mali nyingi haraka. Huu ni mchakato: Mwanzoni mwa mchakato huu watu hawawezi kukubali tabia ya aina hii, wanadharau tabia hii na njia hii ya kufanya mambo, kisha wanajaribu tabia hii wao wenyewe, na kuijaribu kwa njia yao wenyewe, na kisha mioyo yao inaanza kubadilika polepole. Kwa hivyo mabadiliko haya ni yapi? Ni kukubali na kukiri mwenendo huu, kukiri na kukubali wazo hili lililoingizwa kwako na mwenendo wa jamii. Kwa kutojua, unahisi kwamba usipodanganya watu katika kufanya biashara nao, unahisi umebaki nyuma sana; usipodanganya watu unahisi kuwa umepoteza kitu. Bila kujua, kudanganya huku kunakuwa nafsi yako, tegemeo kuu kwako, na kunakuwa aina ya tabia ya lazima ambayo ni kanunimaishani mwako. Baada ya mwanadamu kukubali tabia hii na kufikiria huku, je, moyo wa mwanadamu unapitia mabadiliko? Moyo wako umebadilika, basi uadilifu wako umebadilika? Ubinadamu wako umebadilika? Dhamiri yako imebadilika? Nafsi yako nzima, kutoka moyoni mwako hadi mawazoni mwako, kutoka ndani hadi nje, imebadilika, na haya ni mabadiliko ya ubora. Badiliko hili linakuvuta mbali zaidi na zaidi kutoka kwa Mungu, na unakuwa karibu na Shetani zaidi na zaidi; unamfanana Shetani zaidi na zaidi, na matokeo yake ni kwamba kupotoshwa na Shetani kunakufanya uwe pepo.

Unapotazama mitindo hii ya kijamii, je, unaweza kusema kuwa ina ushawishi mkubwa kwa watu? Je, ina athari inayodhuru kwa kina kwa watu? Mitindo hii ina athari ya kudhuru kwa kina kwa watu. Je, ni vipengele vipi vya mwanadamu ambavyo Shetani hutumia kila mojawapo ya mitindo hii kupotosha? Kwa kiwango cha juu, Shetani hupotosha dhamiri, hisia, ubinadamu, maadili na mitazamo ya maisha ya mwanadamu. Na, je, mitindo hii ya kijamii haiwashushi na kuwapotosha watu hatua kwa hatua? Shetani hutumia hii mitindo ya kijamii kuvuta watu hatua moja baada ya nyingine hadi katika kiota cha mashetani, ili watu walionaswa katika mitindo ya kijamii bila kujua wanatetea pesa na tamaa za mwili, na pia kutetea uovu na ukatili. Punde mambo haya yameingia moyoni mwa mwanadamu, ni nini basi mwanadamu anakuwa? Mwanadamu anakuwa ibilisi Shetani! Hii ni kwa sababu ya mwelekeo kisaikolojia upi katika moyo wa mwanadamu? Ni kipi ambacho mwanadamu anatetea? Mwanadamu huanza kupenda uovu na ukatili. Hawapendi uzuri ama wema, wala hata amani. Watu hawako radhi kuishi maisha rahisi ya ubinadamu wa kawaida, lakini badala yake wanataka kufurahia hadhi ya juu na utajiri mkubwa, kufurahia raha za mwili, na kutumia juhudi zote kuridhisha miili yao, bila vizuizi, hakuna vifungo vya kuwashikilia nyuma, kwa maneno mengine kufanya chochote wanachotaka. Hivyo wakati mwanadamu ametumbukizwa katika mitindo ya aina hii, maarifa ambayo mmefunzwa yanaweza kuwasaidia kuwa huru? Je, desturi ya kitamaduni na ushirikina mnayojua yanaweza kuwasaidia kutupilia mbali hii hatari ya kutisha? Je, maadili ya desturi na sherehe za desturi ambazo mwanadamu huelewa zinaweza kumsaidia kujizuia? Kwa mfano, chukua riwaya ya Analects na Tao Te Ching. Je, vinaweza kuwasaidia watu kujikwamua miguu yao kutoka katika tope la mitindo hii miovu? Bila shaka hapana. Hivyo, mwanadamu anakuwa mwovu zaidi na zaidi, mwenye kiburi, mwenye kushusha hadhi, mwenye ubinafsi, na mwenye kijicho. Hakuna tena upendo kati ya watu, hakuna tena upendo wowote kati ya wanafamilia, hakuna tena uelewa wowote miongoni mwa jamaa na marafiki; mahusiano ya binadamu yamejawa ukatili. Kila mtu anataka kutumia mbinu katili kuishi miongoni mwa wanadamu wenzake; wanakamata riziki zao kwa kutumia ukatili; wanashinda vyeo vyao na kupata faida zao wenyewe kwa kutumia ukatili na wanafanya chochote watakacho kwa kutumia njia mbovu na katili. Si ubinadamu huu unatisha? Unatisha sana: Sio tu kwamba walimsulubisha Mungu, bali pia wangewachinja wote wanaomfuata—kwa sababu mwanadamu ni mwovu sana. Baada ya kusikia vitu hivi vyotenimetoka kuongea kuhusu, hamfikiri kwamba inatisha kuishi katika mazingira haya, katika ulimwengu huu, na miongoni mwa aina hii ya umati, ambayo Shetani hupitia kupotosha watu? (Ndiyo.) Kwa hivyo mmewahi kujihisi kuwa wenye kusikitisha? Lazima mnaihisi kiasi sasa, siyo? (Ndiyo.) Kwa kusikiza sauti zenu, inaonekana kana kwamba mnafikiria “Shetani hutumia njia nyingi mbalimbali kumpotosha mwanadamu. Anakamata kila fursa na yupo kila mahali tunageukia. Mwanadamu bado anaweza kuokolewa?” Mwanadamu bado anaweza kuokolewa? Wanadamu wanaweza kujiokoa? (La.) Je, Mfalme Mkuu wa Jade anaweza kumwokoa mwanadamu? Je, Confucius anaweza kumwokoa mwanadamu? Je, Guanyin Bodhisattva anaweza kumwokoa mwanadamu? (La.) Kwa hivyo ni nani anayeweza kumwokoa mwanadamu? (Mungu.) Watu wengine, hata hivyo, wataibua katika mioyo yao maswali kama: “Shetani anatudhuru kwa kiasi kikubwa sana, kwa hasira sana basi hatuna matumaini ya kuishi, wala imani katika kuishi. Sote tunaishi miongoni mwa upotovu na kila mtu anampinga Mungu hata hivyo, na sasa mioyo yetu imezama chini kadri iwezavyo. Kwa hivyo wakati Shetani anatupotosha, Mungu yuko wapi? Mungu anafanya nini? Chochote Mungu anatufanyia kamwe hatukihisi!” Watu wengine bila kuepukika wanahisi kuhuzunika na bila kuepukika wanahisi kuvunjika moyo kiasi, siyo? Kwenu, hisia hii ni ya kina sana kwa sababu vyote ambavyo Nimekuwa nikisema vimekuwa kuwafanya watu kuja kuelewa polepole, kuhisi zaidi na zaidi kwamba hawana matumaini, kuhisi zaidi na zaidi kwamba wameachwa na Mungu. Lakini usijali. Mada yetu ya kushiriki leo, “uovu wa Shetani,” siyo dhamira yetu ya kweli. Kuongea kuhusu kiini cha utakatifu wa Mungu, hata hivyo, lazima kwanza tuongee kuhusu jinsi Shetani anampotosha mwanadamu na uovu wa Shetani ili kuifanya kuwa wazi zaidi kwa watu mwanadamu sasa yuko katika hali ya aina gani. Lengo moja la kuongea juu ya hili ni kuruhusu watu kujua uovu wa Shetani, ilhali jingine ni kuwaruhusu watu kuelewa kwa kina zaidi utakatifu ni nini.

Je, haya mambo ambayo Nimeongea kuhusu hivi karibuni ni ya kina zaidi kuliko ya wakati uliopita? Hivyo uelewa wenu sasa basi ni wa kina zaidi? (Ndiyo.) Najua kwamba sasa watu wengi wananitarajia kusema ni nini hasa utakatifu wa Mungu, lakini Ninapozungumza kuhusu utakatifu wa Mungu Nitaongea kwanza kuhusu matendo ambayo Mungu anafanya. Nyinyi nyote mnapaswa kusikiza kwa makini, kisha nitawauliza utakatifu wa Mungu ni nini hasa. Sitawaeleza moja kwa moja, lakini badala yake nitawaacha mjaribu kuutambua, kuwapa nafasi ya kuutambua. Mnafikiri nini kuhusu mbinu hii? (Ni nzuri.) Kwa hivyo sikizeni kwa makini.

Kuelewa Utakatifu wa Mungu Kupitia Kile Anachomfanyia Mwanadamu 

Wakati wowote Shetani anampotosha mwanadamu ama anashughulika na madhara yasiyodhibitiwa, Mungu hasimami bila kazi, wala haweki kando ama kupuuza wale ambao amechagua. Yote ambayo Shetani anafanya ni wazi kabisa na yanaeleweka na Mungu. Haijalishi anachofanya Shetani, haijalishi mwenendo anaosababisha kuibuka, Mungu anajua yote ambayo Shetani anajaribu kufanya, na Mungu hawawachi wale ambao amechagua. Badala yake, bila kuvuta macho hata kidogo, kwa siri, kwa ukimya, Mungu anafanya yote yanayohitajika. Mungu Anapoanza kufanya kazi kwa mtu, wakati amemchagua mtu, Haambii yeyote, wala Hamwambii Shetani, wala hata kufanya maonyesho makubwa. Anafanya tu kwa ukimya, kwa asili kile ambacho kinahitajika. Kwanza, Anakuchagulia familia; usuli ambao hiyo familia inao, wazazi wako ni nani, mababu zako ni nani—haya yote tayari yaliamuliwa na Mungu. Kwa maneno mengine, haya hayakuwa uamuzi wa mvuto wa ghafla yaliyofanywa na Yeye, lakini badala yake hii ilikuwa kazi iliyoanza kitambo. Baada ya Mungu kukuchagulia familia, pia Anachagua tarehe ambayo utazaliwa. Kwa sasa, Mungu anaangalia unapozaliwa katika dunia hii ukilia, Anatazama kuzaliwa kwako, Anatazama unapotamka maneno yako ya kwanza, Anatazama unapoanguka na kutembea hatua zako za kwanza, ukijifunza kutembea. Kwanza unachukua hatua moja na kisha unachukua nyingine … sasa unaweza kukimbia, sasa unaweza kuruka, sasa unaweza kuongea, sasa unaweza kuonyesha hisia zako. Mwanadamu anavyokuwa, macho ya Shetani yamewekwa kwa kila mmoja wao, kama chui mkubwa mwenye milia anavyomwangalia nyara wake. Lakini kwa kufanya kazi Yake, Mungu hajawahi kuteseka mapungufu yoyote ya watu, matukio ama mambo, ya nafasi ama wakati; Anafanya kile anachopaswa kufanya na Anafanya kile Anacholazimika kufanya. Katika mchakato wa kukua, unaweza kukutana na mambo mengi ambayo hupendi, kukutana na magonjwa na kuvunjika moyo. Lakini unapotembea njia hii, maisha yako na bahati zako ziko chini ya ulinzi wa Mungu kabisa. Mungu anakupa hakikisho halisi litakalodumu maisha yako yote, kwani Yeye yuko kando yako, anakulinda na kukutunza. Bila kujua haya, unakua. Unaanza kukutana na mambo mapya na unaanza kujua dunia hii na wanadamu hawa. Kila kitu ni kipya kwako. Unapenda kufanya kile unachopenda. Unaishi katika ubinadamu wako mwenyewe, unaishi katika nafasi yako ya kuishi na huna hata kiasi kidogo cha mtazamo kuhusu kuwepo kwa Mungu. Lakini Mungu anakulinda katika kila hatua ya njia unapokua, na Anakutazama unapoweka kila hatua mbele. Hata unapojifunza maarifa, ama kusoma sayansi, Mungu hajawahi toka upande wako kwa hatua hata moja. Wewe ni sawa na watu wengine kwamba, katika harakati za kuja kujua na kukutana na dunia, umeanzisha mawazo yako mwenyewe, una mambo yako mwenyewe ya kupitisha muda, mambo unayopenda mwenyewe, na pia unayo matamanio ya juu. Wakati mwingi unafikiria siku zako za baadaye, wakati mwingi ukichora muhtasari wa jinsi siku zako za baadaye zinapaswa kuwa. Lakini haijalishi kitakachofanyika njiani, Mungu anaona vyote na macho wazi. Labda wewe mwenyewe umesahau siku zako za nyuma, lakini kwa Mungu, hakuna anayeweza kukuelewa bora kuliko Yeye. Unaishi chini ya macho ya Mungu, unakua, unapevuka. Wakati huu, jukumu muhimu la Mungu ni kitu ambacho hakuna yeyote kamwe hufahamu, kitu ambacho hakuna yeyote anajua. Mungu hakika hakuambii kukihusu. Basi kitu hiki cha muhimu zaidi ni kipi? Inaweza kusemwa kwamba ni hakikisho kuwa Mungu atamwokoa mtu. Hii inamaanisha kwamba Mungu anataka kumwokoa mtu huyu, kwa hivyo lazima Afanye hivi, na kazi hii ni muhimu sana kwa mwanadamu na Mungu. Je, mnajua ni nini? Inaonekana kwamba hamna hisia yoyote kuhusu hili, ama dhana yoyote kuhusu hili, kwa hivyo nitawaambia. Kutoka ulipozaliwa hadi sasa, Mungu amefanya kazi nyingi sana kwako, lakini Hakupi maelezo moja baada ya nyingine ya kila kitu Amefanya. Mungu hakukuruhusu kujua, na Hakukwambia. Hata hivyo, kwa mwanadamu, kila kitu anachofanya Mungu ni muhimu. Kwa Mungu, ni kitu ambacho lazima Afanye. Katika moyo wake kuna kitu muhimu Anapaswa kufanya ambacho kinazidi yoyote ya mambo haya. Yaani, kutoka alipozaliwa mwanadamu hadi sasa, Mungu lazima ahakikishe usalama wao. Baada ya kusikia maneno haya, mnaweza kuhisi kana kwamba hamwelewi kikamilifu, kusema “usalama huu ni muhimu sana?” Kwa hivyo ni nini maana halisi ya “usalama”? Labda mnauelewa kumaanisha amani ama pengine mnauelewa kumaanisha kutopitia maafa ama msiba wowote, kuishi vyema, kuishi maisha ya kawaida. Lakini katika mioyo yenu lazima mjue kwamba si rahisi hivyo. Kwa hivyo ni nini hasa kitu hiki ambacho Nimekuwa nikizungumzia, ambacho Mungu anapaswa kufanya? Usalama unamaanisha nini kwa Mungu? Kuna hakikisho lolote la usalama wenu? La. Kwa hivyo ni nini hiki ambacho Mungu anafanya? Usalama huu unamaanisha humezwi na Shetani. Je, jambo hili ni muhimu? Wewe humezwi na Shetani, kwa hivyo hili linahusisha usalama wako, au la? Hili linahusisha usalama wako binafsi, na hakuwezi kuwa na lolote muhimu zaidi. Baada ya wewe kumezwa na Shetani, nafsi yako wala mwili wako si vya Mungu tena. Mungu hatakuokoa tena. Mungu huacha nafsi kama hiyo na huacha watu kama hao. Kwa hivyo Nasema kitu muhimu sana ambacho Mungu anapaswa kufanya ni kuhakikishia usalama wako, kuhakikisha kwamba hutamezwa na Shetani. Hili ni muhimu kiasi, silo? Kwa hivyo mbona hamwezi kujibu? Inaonekana kwamba hamwezi kuhisi wema mkubwa wa Mungu!

Mungu anafanya mengi kando na kuhakikisha usalama wa watu, kuhakikisha kwamba hawatamezwa na Shetani; pia hufanya kazi nyingi sana kwa kutayarisha kumchagua mtu na kumwokoa. Kwanza, una tabia gani, utazaliwa kwa familia ya aina gani, wazazi wako ni nani, una kaka na dada wangapi, na hali, hadhi ya kiuchumi na tabia za familia ambayo unazaliwa ndani ni gani—haya yote yanapangiwa wewe kwa uangalifu na Mungu. Je, unajua ni familia ya aina gani watu waliochaguliwa na Mungu wanazaliwa ndani mara nyingi, kama inavyohusu watu wengi? Ni familia mashuhuri? Hatuwezi sema kwa uhakika hakuna yoyote. Kunaweza kuwa na nyingine, lakini kuna chache sana. Ni familia za utajiri wa kupindukia, kama yenye mabilioni ama yenye mamilioni nyingi? Mara nyingi huwa si aina hii ya familia. Kwa hivyo Mungu anapangia watu hawa familia za aina gani zaidi? (Familia za kawaida.) Kwa hivyo ni familia zipi ambazo zinaweza kufikiriwa za kawaida? Familia hizi ni pamoja na zile zinazofanya kazi—zinategemea mishahara yao kuishi na zinaweza kumudu mahitaji ya kimsingi na si wenye mali nyingi; pia ni pamoja na familia za ukulima. Wakulima hutegemea kupanda mazao kwa chakula chao, na wana nafaka za kula na nguo za kuvaa, hawataona njaa au kuhisi. Kisha kuna familia zingine zinazoendesha biashara ndogondogo, na zingine ambazo wazazi ni wenye akili, na hizi zinaweza kuhesabika kama familia za kawaida. Kuna baadhi ya wazazi ambao ni wafanyakazi wa ofisi ama maafisa wadogo wa serikali kwa kiwango zaidi, ambazo haziwezi kuhesabika kama familia mashuhuri pia. Watu wengi zaidi wanazaliwa katika familia za kawaida, na haya yote yanapangiliwa na Mungu. Kusema kwamba, kwanza kabisa mazingira haya unayoishi si familia ya uwezo mkubwa ambayo unaweza kufikiria, lakini badala yake ni familia uliyoamuliwa na Mungu, na watu wengi wataishi katika mipaka ya aina hii ya familia. Kwa hivyo je, hadhi ya kijamii? Hali ya uchumi ya wengi wa wazazi ni wastani na hawana hadhi ya juu ya kijamii—kwao ni vizuri tu kuwa na kazi. Je, inajumuisha magavana? Au maraisi wa mataifa? La, sivyo? Kwa zaidi ni watu kama mameneja wa biashara ndogo ama wakubwa wa muda mfupi. Hadhi zao za kijamii ni kuwa katikati, na hali zao za uchumi ni wastani. Sababu nyingine ni mazingira ya kuishi ya familia. Kwanza kabisa, hakuna wazazi ambao wanaweza kushawishi kwa wazi watoto wao kutembea njia ya uaguzi na kupiga ramli; hawa pia ni wachache. Wazazi wengi ni wa kawaida kiasi. Mungu anaweka mazingira ya aina hii kwa ajili ya watu wakati sawa na kuwachagua, na ni kwa manufaa sana ya kazi Yake ya kuokoa watu. Kwa nje, inaonekana kwamba Mungu hajafanya chochote kikuu kwa mwanadamu; Anafanya kila kitu kwa siri tu, kwa unyenyekevu na kwa kimya. Lakini kwa hakika, vyote ambavyo Mungu anafanya vinafanywa kuweka msingi wa wokovu wako, kuandaa njia mbeleni na kuandaa hali zote muhimu za wokovu wako. Halafu, Mungu anawarudisha mbele Yake, kila mtu kwa wakati wake: Ni wakati huo ndipo unaposikia sauti ya Mungu; ni wakati huo ndipo unapokuja mbele Yake. Kufikia wakati hilo linafanyika, watu wengine wamekuwa wazazi tayari wenyewe, ilhali wengine bado ni watoto wa mtu tu. Kwa maneno mengine, watu wengine wameoa na kupata watoto ilhali wengine bado hawajaoa, na hawajaanza bado familia zao. Lakini licha ya hali za watu, Mungu tayari ameweka nyakati utakapochaguliwa na injili na maneno Yake yatakapokufikia. Mungu ameweka hali, ameamulia mtu fulani ama muktadha fulani ambamo injili itapitishwa kwako, ili uweze kusikia maneno ya Mungu. Mungu tayari amekuandalia hali zote muhimu ili, bila kujua, unakuja mbele Yake na unarudishwa kwa familia ya Mungu. Pia, bila kujua, unafuata Mungu na kuingia katika kazi Yake ya hatua kwa hatua, kuingia katika kila hatua ya njia ya Mungu ya kazi ambayo ameiandalia mwanadamu. Ni njia za aina gani ambazo Mungu hutumia wakati Anapofanya mambo kwa ajili ya mwanadamu wakati huu? Kwanza, angalau kabisa ni utunzaji na ulinzi ambao mwanadamu hufurahia. Kando na hayo, Mungu huweka watu, matukio, na vitu mbalimbali ili mwanadamu aweze kuona kuwepo Kwake na matendo Yake miongoni mwao. Kwa mfano, kuna watu wengine wanaomwamini Mungu kwa sababu mtu katika familia yao ni mgonjwa. Wakati wengine wanawahubiria injili, wanaanza kumwamini Mungu, na imani hii kwa Mungu imekuja kwa sababu ya hali hii. Kwa hivyo ni nani aliyepangilia hali hii? (Mungu.) Kwa njia ya maradhi haya, kuna familia zingine ambamo wote ni waumini, vijana na wazee, ilhali kuna familia zingine ambamo imani ni ya kibinafsi. Inavyoonekana, mtu katika familia yako ana maradhi, lakini kwa hakika ni hali uliyopewa ili uje mbele ya Mungu—huu ni wema wa Mungu. Kwa sababu maisha ya familia ya watu wengine ni magumu na hawawezi kupata amani yoyote, fursa ya bahati inakuja ambapo mtu anapitisha injili na kusema, “Mwamini Bwana Yesu na utakuwa na amani.” Bila fahamu, basi anakuja kumwamini Mungu katika hali asili, kwa hivyo hii si aina ya hali? Na je, familia yake kuwa na amani si neema aliyopewa na Mungu? Kisha kuna wengine wanaokuja kumwamini Mungu kwa sababu zingine. Kuna sababu tofauti na njia tofauti za imani, lakini licha ya sababu inakuleta kumwamini Yeye, yote hakika yamepangwa na kuongozwa na Mungu. Kwanza, Mungu hutumia njia kadhaa ili kukuchagua na kukuleta katika familia Yake. Hii ndiyo neema Mungu anayompa kila mwanadamu.

Sasa na kazi ya Mungu katika siku za mwisho, Hampi tena mwanadamu neema na baraka tu kama Alivyofanya awali, wala halazimishi watu kwenda mbele. Wakati wa hatua hii ya kazi, ni nini mwanadamu ameona kutoka kwa vipengele hivi vyote vya kazi ya Mungu ambavyo wamepitia? Wameona upendo wa Mungu, na hukumu na kuadibu kwa Mungu. Kwa wakati huu, Mungu zaidi ya hayo, anamtegemeza, tia nuru, na kumwongoza mwanadamu, ili aje kujua nia Zake polepole, kujua maneno Anayozungumza na ukweli Anaompa mwanadamu. Wakati mwanadamu ni mnyonge, wakati amevunjika roho, wakati hana popote pa kugeukia, Mungu atatumia maneno Yake kufariji, kushauri na kuwatia moyo, ili mwanadamu wa kimo kidogo aweze kupata nguvu polepole, kuinuka kwa wema na kuwa radhi kushirikiana na Mungu. Lakini wakati wanadamu hawamtii Mungu ama wanampinga Yeye, ama wanapofichua upotovu wao, Mungu hataonyesha huruma kuwarudi na kuwafundisha nidhamu. Kwa ujinga, kutojua, unyonge, na uchanga wa mwanadamu, hata hivyo, Mungu ataonyesha uvumilivu na ustahimilivu. Kwa njia hii, kupitia kazi yote Mungu anamfanyia mwanadamu, mwanadamu anapevuka, anakua na anakuja kujua nia za Mungu polepole, kujua baadhi ya ukweli, kujua ni nini mambo mema na ni nini mambo hasi, kujua uovu ni nini na kujua giza ni nini. Mungu hamrudi na kumfundisha nidhamu mwanadamu siku zote wala Haonyeshi uvumilivu na ustahimilivu siku zote. Badala yake anampa kila mtu kwa njia tofauti, katika hatua zao tofauti na kulingana na kimo na ubora wa tabia yao tofauti. Anamfanyia mwanadamu mambo mengi na kwa gharama kubwa; mwanadamu hafahamu lolote la gharama hii ama mambo haya Mungu anafanya, ilhali yote ambayo anafanya kwa kweli inafanywa kwa kila mtu. Upendo wa Mungu ni wa kweli: Kupitia neema ya Mungu mwanadamu anaepuka janga moja baada ya jingine, ilhali kwa unyonge wa mwanadamu, Mungu anaonyesha ustahimili wake muda baada ya muda. Hukumu na kuadibu kwa Mungu yanaruhusu watu kuja kujua polepole upotovu wa wanadamu na kiini chao cha kishetani. Kile ambacho Mungu anapeana, kutia nuru Kwake kwa mwanadamu na uongozi Wake yote yanawaruhusu wanadamu kujua zaidi na zaidi kiini cha ukweli, na kujua zaidi kile ambacho watu wanahitaji, njia wanayopaswa kuchukua, kile wanachoishia, thamani na maana ya maisha yao, na jinsi ya kutembea njia iliyo mbele. Haya mambo yote ambayo Mungu anafanya hayatengwi na lengo Lake la awali. Ni nini, basi lengo hili? Mbona Mungu anatumia njia hizi kufanya kazi Yake kwa mwanadamu? Anataka kutimiza matokeo gani? Kwa maneno mengine, ni nini ambacho anataka kuona kwa mwanadamu na kupata kutoka kwake? Kile ambacho Mungu anataka kuona ni kwamba moyo wa mwanadamu unaweza kufufuliwa. Njia hizi ambazo anatumia kufanya kazi kwa mwanadamu ni za kuamsha bila kikomo moyo wa mwanadamu, kuamsha roho ya mwanadamu, kumwacha mtu kujua alipotoka, ni nani anayemwongoza, kumsaidia, kumkimu, na ni nani ambaye amemruhusu mwanadamu kuishi hadi sasa; ni ya kuwacha mwanadamu kujua ni nani Muumbaji, ni nani wanapaswa kuabudu, ni njia gani wanapaswa kutembelea, na mwanadamu anapaswa kuja mbele ya Mungu kwa njia gani; yanatumika kufufua moyo wa mwanadamu polepole, ili mwanadamu ajue moyo wa Mungu, aelewe moyo wa Mungu, na aelewe utunzaji mkuu na wazo nyuma ya kazi Yake kumwokoa mwanadamu. Wakati moyo wa mwanadamu umefufuliwa, hataki tena kuishi maisha ya uasherati, tabia potovu, lakini badala yake kutaka kufuatilia ukweli kwa kuridhishwa kwa Mungu. Wakati moyo wa mwanadamu umeamshwa, anaweza basi kujinusuru kutoka kwa Shetani, kutoathiriwa tena na Shetani, kutodhibitiwa na kudanganywa na yeye. Badala yake, mwanadamu anaweza kushiriki kwa makini katika kazi ya Mungu na maneno Yake ili kuridhisha moyo wa Mungu, na hivyo kupata uchaji wa Mungu na kuepuka uovu. Hili ndilo lengo la awali la kazi ya Mungu.

Kuzungumza kuhusu uovu wa Shetani hivi sasa kulimfanya kila mtu kuhisi kana kwamba watu huishi kwa huzuni sana na kwamba maisha ya mwanadamu yamejaa bahati mbaya. Lakini mnahisi vipi sasa kwani Nimezungumza kuhusu utakatifu wa Mungu na kazi ambayo anafanya kwa mwanadamu? (Furaha sana.) Tunaweza kuona sasa kwamba kila kitu Mungu anafanya, kila kitu ambacho anapanga kwa uangalifu kwa mwanadamu ni safi kabisa. Kila kitu anachofanya Mungu ni bila kasoro, kumaanisha ni bila dosari, hakihitaji yeyote kukosoa, kutoa mawaidha ama kufanya mabadiliko yoyote. Kila kitu ambacho Mungu anafanya kwa kila mtu hakina shaka; Anaongoza kila mtu kwa mkono, Anakuchunga kwa kila muda na Hajawahi kuondoka upande wako. Watu wanapokua katika mazingira haya na kukua na usuli wa aina hii, tunaweza kusema kwamba watu kwa kweli wanakua katika kiganja cha mkono wa Mungu? (Ndiyo.) Kwa hivyo sasa bado mnahisi hisia za hasara? Je, kuna yeyote anayehisi kuvunjika moyo bado? Kuna yeyote anayehisi kwamba Mungu amewaacha wanadamu? (La.) Kwa hivyo ni nini hasa Mungu amefanya? (Anawahifadhi wanadamu.) Wazo na utunzaji mkuu nyuma ya kila anachofanya Mungu hayapingwi. Hata zaidi, wakati Mungu anapofanya kazi Yake, hajawahi kuweka sharti ama mahitaji yoyote kwa yeyote kati yenu kujua gharama anayokulipia, kwa hivyo uhisi shukrani kwake kwa kina. Je, Mungu amewahi kufanya chochote kama hiki kabla? (La.) Katika miaka yenu mirefu yote, kimsingi kila mtu amekutana na hali nyingi hatari na kupitia majaribu mengi. Hii ni kwa sababu Shetani yupo kando yako, macho yake yakikutazama kila wakati. Anapenda janga linapokupata, wakati maafa yanakupata, wakati hakuna chochote kinaenda sawa kwako, na anapendelea unaponaswa na wavu wa Shetani. Kuhusu Mungu, anakulinda kila wakati, kukuweka mbali na bahati moja mbaya baada ya nyingine na kutokana na janga moja baada ya jingine. Hii ndiyo maana Nasema kwamba kila kitu ambacho mwanadamu anacho—amani na furaha, baraka na usalama wa kibinafsi—yote hakika yanadhibitiwa na Mungu, na Anaongoza na kuamua hatima ya kila mtu. Lakini, je, Mungu ana dhana iliyovimbishwa ya cheo chake, kama wanavyosema watu wengine? Kukuambia “Mimi ni mkuu kabisa wa wote, ni Mimi ninayechukua watamu wenu, lazima nyote mniombe huruma na kutotii kutaadhibiwa na kifo.” Je, Mungu amewahi kutishia wanadamu kwa njia hii? (La.) Ashawahi kusema “Wanadamu ni wapotovu kwa hivyo haijalishi Ninavyowashughulikia, utendeaji wowote holela utatosha; Sihitaji kupanga mambo vizuri sana kwa sababu yao.” Je, Mungu anafikiria kwa njia hii? Mungu ametenda kwa njia hii? (La.) Kinyume na haya, utendeaji wa Mungu wa kila mtu ni wenye ari na ambao umewajibika, umewajibika zaidi hata kuliko vile ulivyo kwa wewe mwenyewe. Sivyo hivi? Mungu haongei bure, wala hasimami juu akijifanya kuwa muhimu wala hadanganyi watu. Badala yake, Anafanya vitu ambavyo Yeye Mwenyewe anapaswa kufanya kwa uaminifu na kwa ukimya. Mambo haya yanaleta baraka, amani na furaha kwa mwanadamu. Yanamleta mwanadamu kwa amani na kwa furaha katika macho ya Mungu na ndani ya familia Yake; kisha wanaishi mbele ya Mungu na kukubali wokovu wa Mungu na fikira na mawazo ya kawaida. Kwa hivyo Mungu amewahi kuwa mdanganyifu kwa mwanadamu katika kazi Yake? Ashawahi kuonyesha maonyesho ya uongo ya ukarimu, Akimpumbaza mwanadamu na mazungumzo ya kufurahisha, kisha kumpuuza mwanadamu? (La.) Je, Mungu ashawahi kusema kitu kimoja na kisha kufanya kingine? Je, Mungu ashawahi kupeana ahadi tupu na kujigamba, Akikuambia kwamba Anaweza kukufanyia hili ama kukusaidia kufanya lile, na kisha kutoweka? (La.) Hakuna udanganyifu ndani ya Mungu, hakuna uongo. Mungu ni mwaminifu na kila kitu Anachofanya ni halisi. Ni Yeye pekee ambaye watu wanaweza kutegemea na Mungu ambaye watu wanaweza kuaminia maisha yao na yote wanayo Kwake. Kwa vile hakuna udanganyifu ndani ya Mungu, tunaweza kusema kwamba Mungu ndiye wa kweli zaidi? (Ndiyo.) Bila shaka tunaweza, siyo? Ingawa, kuzungumza kuhusu maneno haya sasa, likitumika kwa Mungu ni dhaifu sana, cha ubinadamu sana, hakuna lolote tunaloweza kufanya kulihusu kwa vile hii ni mipaka ya lugha ya binadamu. Si sahihi sana hapa kumwita Mungu wa kweli, lakini tutatumia neno hili kwa sasa. Mungu ni mwaminifu. Kwa hivyo tunamaanisha nini kwa kuongea kuhusu vipengele hivi? Je, tunamaanisha tofauti kati ya Mungu na mwanadamu na tofauti kati ya Mungu na Shetani? Tunaweza kusema hivi. Hii ni kwa sababu mwanadamu hawezi kuona chembe cha tabia potovu ya Shetani kwa Mungu. Je, Niko sahihi kusema hivi? Ninaweza kupata Amina kwa sababu ya hili? (Amina!) Hatuoni uovu wowote wa Shetani ukifichuliwa kwa Mungu. Yote ambayo Mungu hufanya na kufichua ni muhimu sana na ya msaada sana kwa mwanadamu, yanafanywa kumkimu mwanadamu kabisa, yamejaa uhai na yanampa mwanadamu njia ya kufuata na mwelekeo wa kuchukua. Mungu hajapotoka, na zaidi ya hayo, kuangalia sasa kila kitu Mungu hufanya, tunaweza kusema kwamba Mungu ni mtakatifu? Kwa kuwa Mungu hana tabia yoyote potovu ya mwanadamu, wala chochote kifananacho kiini cha kishetani cha binadamu waliopotoka, kutoka katika mtazamo huu tunaweza kusema kikamilifu kwamba Mungu ni mtakatifu. Mungu haonyeshi upotovu wowote, na wakati huo huo Mungu anapofanya kazi, Mungu hufichua kiini Chake Mwenyewe, ambacho kinathibitisha kikamilifu kwamba Mungu Mwenyewe ni mtakatifu. Je, mnaona hili? Sasa, kujua asili takatifu ya Mungu, kwa sasa wacha tuangalie hivi vipengele viwili: 1) Hakuna tabia potovu ndani ya Mungu; 2) kiini cha kazi ya Mungu kwa mwanadamu kinamruhusu mwanadamu kuona kiini cha Mungu mwenyewe na kiini hiki ni kizuri kabisa. Kwa kuwa vitu ambavyo kila namna ya kazi ya Mungu inamletea mwanadamu ni vitu vizuri. Kwanza, Mungu anamhitaji mwanadamu kuwa mwaminifu—hili si zuri? Mungu anampa mwanadamu maarifa—hili si zuri? Mungu anamfanya mwanadamu aweze kutambua kati ya mema na maovu—hili si zuri? Anamruhusu mwanadamu kuelewa maana na thamani ya maisha ya binadamu—hili si zuri? Anamruhusu mwanadamu kuona ndani ya kiini cha watu, matukio na mambo kulingana na ukweli—si hili ni jambo zuri? Ndiyo ni zuri. Na matokeo ya haya yote ni kwamba mwanadamu hadanganywi tena na Shetani, haendelei kudhuriwa na Shetani ama kudhibitiwa na yeye. Kwa maneno mengine, yanawaruhusu watu kujinusurisha kabisa kutoka upotovu wa Shetani, na hivyo kutembea polepole njia ya kumcha Mungu na kuepuka maovu. Mmetembea umbali gani katika njia hii sasa? Ni vigumu kusema, sivyo? Lakini angalau sasa mna uelewa wa mwanzo wa jinsi Shetani anampotosha mwanadamu, vitu vipi ni ovu na vitu vipi ni hasi? Nyinyi angalau mnatembea sasa njia sahihi maishani. Je, ni sahihi kusema hivyo? Ni sahihi kabisa.

Kuna kitu kinachopaswa kushirikiwa kuhusu utakatifu wa Mungu. Kulingana na yote ambayo mmesikia na kupokea, ni nani kati yenu anayeweza kusema utakatifu wa Mungu ni nini? Utakatifu wa Mungu ninaozungumzia unarejelea nini? Lifikirie kidogo. Je, ukweli wa Mungu ni utakatifu Wake? Je, uaminifu wa Mungu ni utakatifu Wake? Je, kutokuwa na ubinafsi kwa Mungu ni utakatifu Wake? Je, unyenyekevu wa Mungu ni utakatifu Wake? Je, upendo wa Mungu kwa mwanadamu ni utakatifu Wake? Mungu humpa mwanadamu ukweli na uhai bure—huu ni utakatifu Wake? Naam, yote ni sahihi. Yote haya ambayo Mungu anafichua ni wa kipekee; hayapo katika binadamu potovu, wala hayawezi kuonekana hapo. Hakuna hata chembe ya hayo yanaweza kuonekana katika mchakato wa upotovu wa Shetani wa mwanadamu, wala katika tabia potovu ya Shetani wala katika kiini ama asili ya Shetani. Chote ambacho Mungu Anacho na Alicho ni ya kipekee na Mungu tu Mwenyewe anacho kiini cha aina hii, ni Mungu Mwenyewe tu anamiliki kiini cha aina hii. Baada ya kuzungumza hili hadi sasa, kuna yeyote kati yenu ambaye ameona yeyote mtakatifu hivi miongoni mwa wanadamu? (La.) Kwa hivyo, kuna yeyote mtakatifu hivi miongoni mwa watu mashuhuri, walio marufu, au watu walio wakuu kati ya binadamu mnaowaabudu? (La.) Kwa hivyo sasa tunasema kwamba utakatifu wa Mungu ni wa kipekee, je anadhihirisha hili katika jina na vile vile katika ukweli? Anadhihirisha. Zaidi ya hayo, kuna pia sehemu yake ya utendaji. Je, kuna tofauti zozote kati ya utakatifu ninaozungumzia sasa na utakatifu ambao mlifikiria na kudhania awali? (Ndiyo.) Kuna tofauti kubwa sana. Watu humaanisha nini sanasana wanapoongea kuhusu utakatifu huu? (Baadhi ya tabia ya nje.) Tabia, ama kama njia ya kuelezea kitu, wanasema kwamba ni takatifu. Ni kitu tu kinachoonekana kuwa safi na kizuri, kitu kinachoonekana ama kusikika kuwa kizuri kwa watu, si chochote cha asili yoyote halisi ya utakatifu. Hii ni dhahania. Kando ya hili, kipengele cha utendaji cha “utakatifu” ambacho watu wanafikiria kinarejelea nini hasa? Je hasa ni kile wanachokifikiria ama kudhania kuwa? Kwa mfano, Wanabudhaa wengine hufariki wakati wanatia vitendoni, wanaaga wakiwa wamekaa pale wakilala. Watu wengine husema kwamba wamekuwa watakatifu na kuruka mbinguni. Hii pia ni aina ya ubunifu. Pia kuna wengine ambao wanafikiria kwamba kichimbakazi anayeelea chini kutoka mbinguni ni mtakatifu. Kwa kweli, wazo la watu la neno “takatifu” limekuwa tu kama fikira tupu na dhahania ambayo kimsingi haina kiini, na zaidi ya hayo haina chochote kuhusu kiini cha utakatifu. Kiini cha utakatifu ni upendo wa kweli, lakini hata zaidi ya hili ni kiini cha ukweli, cha haki na mwanga. Neno “takatifu” linafaa tu linapotumika kwa Mungu; hakuna chochote katika uumbaji kinachostahiki kuitwa takatifu. Mwanadamu lazima aelewe hilo. Kuanzia sasa kuendelea, tunatumia neno “takatifu” kwa Mungu pekee. Hii ni ya kufaa? (Ndiyo, inafaa.)

Ujanja Anaotumia Shetani  Kumpotosha Mwanadamu

Hebu turudi kuzungumza kuhusu mbinu ambazo Shetani hutumia kumpotosha mwanadamu. Tumeongea karibuni kuhusu mbinu mbalimbali ambazo Mungu anafanya kazi kwa mwanadamu na ambazo kila mmoja wenu anaweza kupitia mwenyewe, kwa hivyo sitatoa maelezo zaidi. Lakini katika mioyo yenu pengine mmechanganyikiwa kuhusu mbinu ambazo Shetani hutumia kumpotosha mwanadamu, ama kwa kiwango cha chini zaidi ana upungufu wa maelezo. Ni ya manufaa kwenu kwa Mimi kuzungumzia hili tena? Je, mnataka kumwelewa? Pengine wengine wenu watauliza: “Mbona tuzungumze kuhusu Shetani tena? Punde tunapoongea kuhusu Shetani, tunakuwa na hasira, na tunaposikia jina lake tunahisi kutotulia kila mahali.” Bila kujali jinsi anavyokufanya kutotulia, lazima ukubali ukweli, na mambo haya yanapaswa kuzungumziwa kwa uwazi na kufanywa dhahiri kwa manufaa ya ufahamu wenu: kama sivyo hamwezi kweli kuepukana na ushawishi wa Shetani.

Tumezungumza hapo awali njia tano ambazo Shetani anatumia kumpotosha mwanadamu. Ndani ya hizi njia tano kuna mbinu anazotumia. Njia ambazo Shetani anampotosha mwanadamu ni aina ya kifuniko tu; ya kudhuru kwa siri zaidi ni mbinu zinazojificha nyuma ya sura hii ya kinafiki na anataka kutumia mbinu hizi kufikia malengo yake. Mbinu hizi ni zipi? Nipeni muhtasari. (Anadanganya, anashawishi na anatishia.) Kadri mnavyoendelea kutaja ndivyo mnavyokaribia. Inaonekana kana kwamba mmedhuriwa kwa kina na yeye na mna hisia kali kuhusu mada hii. (Anatumia pia maneno matamu, anashawishi, na anamiliki kwa nguvu.) Anamiliki kwa nguvu—hii inatoa fikra ya kina. Watu wanaogopa umiliki wa nguvu wa Shetani, siyo? Kuna mengine? (Huwadhuru watu kikatili, hutumia vitisho na vivutio, na hudanganya.) Uongo ni kiini cha matendo yake na hudanganya ili kukulaghai. Ni nini asili ya kudanganya? Je, kudanganya si sawa na kulaghai? Lengo la kusema uongo kwa kweli ni kukudanganya wewe. Je, kuna ujanja mwingine? Niambieni njia zote ujanja wa Shetani mnazojua. (Yeye hushawishi, hudhuru, hupofusha na hudanganya.) Wengi wenu mnahisi sawa kuhusu uongo huu, sivyo? (Yeye humdhibiti mwanadamu, humkamata mwanadamu, humtishia sana mwanadamu na humzuia mwanadamu kumwamini Mungu.) Ninajua vizuri kiasi mnachomaanisha na yote ni mazuri. Nyote mnajua kitu kuhusu hili, kwa hivyo wacha sasa tufanye muhtasari.

Kuna Njia Sita za Msingi Ambazo Shetani Hutumia Kumpotosha Mwanadamu.

Ya kwanza ni kudhibiti na kulazimisha. Yaani, Shetani atafanya vyovyote vile kudhibiti moyo wako. “Kulazimisha” kunamaanisha nini? Kunamaanisha kutumia mbinu za kutishia na kulazimisha kukufanya umtii, kukufanya kufikiria matokeo usipomtii. Unaogopa na huthubutu kumpinga, kwa hivyo basi unamtii.

Ya pili ni kudanganya na kulaghai. “Kudanganya na kulaghai” yanahusisha nini? Shetani hutunga baadhi ya hadithi na uongo, kukulaghai wewe kuziamini. Hakwambii kamwe kwamba mwanadamu aliumbwa na Mungu, wala hasemi pia moja kwa moja kwamba hukuumbwa na Mungu. Hatumii jina “Mungu” kabisa, lakini badala yake hutumia kitu kingine mbadala, akitumia kitu hiki kukudanganya ili kimsingi usiwe na wazo la kuwepo kwa Mungu. Huu ulaghai bila shaka unahusisha vipengele vingi, sio tu hiki kimoja.

Ya tatu ni kufunza kwa nguvu. Watu wanafunzwa nini kwa nguvu? Je, kufunzwa kwa nguvu kunafanywa kwa hiari ya mwanadamu mwenyewe? Je, kunafanywa na idhini ya mwanadamu? Bila shaka sivyo. Hata usipokubali, hakuna unachoweza kufanya kuhusu hilo. Katika kutokujua kwako, Shetani anakutia mafundisho, akitia fikira zake ndani mwako, kanuni zake za maisha na kiini chake.

Ya nne ni vitisho na vivutio. Yaani, Shetani hutumia hila mbalimbali kukusababisha umkubali, umfuate na ufanye kazi katika Huduma yake. Atafanya chochote kufikia malengo yake. Wakati mwingine yeye hukupa fadhili ndogo, wakati wote akikushawishi utende dhambi. Usipomfuata, atakufanya uteseke na kukuadhibu, na hutumia njia mbalimbali kukushambulia na kukulia njama.

Ya tano ni uongo na kiharusi. “Uongo na kiharusi” ni wakati ambapo Shetani hutia ndani ya watu maneno na mawazo yanayolingana na dhana zao na yanayoonekana ya kuaminika, kufanya ionekane kwamba anajali hali za kimwili za watu, kuhusu maisha yao na siku zao za baadaye, wakati kwa kweli lengo lake la kweli ni kukudanganya tu. Kisha anakupooza ili usijue kile kilicho sahihi na kile kilicho makosa, ili udanganywe bila kujua na hivyo kuja chini ya udhibiti wake.

Ya sita ni maangamizi ya mwili na akili. Ni sehemu gani ya mwanadamu ambayo Shetani huharibu? Shetani huharibu akili yako, kukufanya kutokuwa na nguvu za kupinga, kumaanisha kuwa polepole sana moyo wako unageuka kwa Shetani licha ya wewe mwenyewe. Huingiza mambo haya ndani yako kila siku, kila siku akitumia mawazo na utamaduni huu kukushawishi na kukuelimisha, polepole akiharibu utashi wako, kukufanya kutotaka kuwa mtu mzuri tena, kukufanya kutotaka tena kuvumilia katika kutetea kile unachoita cha haki. Bila kujua, huna tena utashi wa kuogelea kinyume na mkondo dhidi ya bamvua, lakini badala yake kububujika chini pamoja nayo. “Maangamizi” yanamaanisha kwamba Shetani hutesa watu sana hadi wanakuwa vivuli vya wao wenyewe, sio wanadamu tena. Hapa ndipo Shetani huwapiga, kuwashika na kuwameza.

Kila ya hizi njia zote Shetani hutumia kumpotosha mwanadamu inaweza kumfanya mwanadamu kutokuwa na nguvu ya kupinga; yoyote inaweza kuwa ya kufisha kwa watu. Kwa maneno mengine, chochote anachofanya Shetani na njia yoyote anayotumia inaweza kukufanya kupotoka, inaweza kukuleta chini ya udhibiti wa Shetani na inaweza kukuzamisha katika bwawa la uovu. Hizi ndizo njia Shetani hutumia kumpotosha mwanadamu.

Tunaweza kusema Shetani ni mwovu, lakini ili kuthibitisha hili ni lazima bado tuangalie matokeo ya upotovu wa Shetani wa mwanadamu ni yapi na ni tabia gani na viini vipi anamletea mwanadamu. Nyote mnajua kitu kuyahusu, kwa hivyo ongeeni. Matokeo ya upotoshaji wa Shetani kwa watu ni yapi? Wao hufichua tabia gani potovu? (Kiburi na majivuno, ubinafsi na kustahili dharau, uovu na udanganyifu, kudhuru kwa siri na kijicho, na utovu wa ubinadamu.) Kwa ujumla, tunaweza kusema hazina ubinadamu, siyo? Wacha kaka na dada wengine wazungumze. (Punde mwanadamu anapopotoshwa na Shetani, wakati mwingi hasa huwa mwenye kiburi na wa kujidai, wa kujigamba na mwenye majivuno, mwenye tamaa na mwenye ubinafsi. Haya ndiyo mazito sana.) (Baada ya mwanadamu kupotoshwa na Shetani, anafanya chochote ili kupata mali na utajiri. Kisha wanakua wakatili kwa Mungu, wanampinga Mungu, hawamtii Mungu, na anapoteza dhamiri yake na akili ambayo mwanadamu anapaswa kumiliki.) Yale ambayo mmesema yote kimsingi ni sawa na ijapokuwa na tofauti kidogo tu; wengine wenu mmeongeza maelezo madogo kiasi. Kwa muhtasari, mambo yanayojitokeza kuhusu binadamu wapotovu ni kiburi, udanganyifu, kuwa mwenye kijicho na ubinafsi. Hata hivyo, nyote mmepuuza kitu sawa. Watu hawana dhamiri, wamepoteza akili zao na hawana ubinadamu—lakini kitu kingine muhimu zaidi ambacho hamjataja, ambacho ni “usaliti”. Matokeo ya mwisho ya tabia hizi ambazo zipo kwa mwanadamu yeyote baada ya kupotoshwa na Shetani ni kusaliti kwao Mungu. Licha ya kile Mungu anamwambia mwanadamu ama licha ya kazi anayomfanyia, hatilii maanani kile ambacho anajua kuwa ukweli, yaani, hamtambui Mungu tena na anamsaliti: Haya ndiyo matokeo ya upotovu wa Shetani wa mwanadamu. Ni sawa kwa tabia zote potovu za mwanadamu. Miongoni mwa njia ambazo Shetani hutumia kumpotosha mwanadamu—maarifa ambayo mwanadamu hujifunza, sayansi anayojua, ushirikina, utamaduni wa jadi, na mitindo ya kijamii anayoelewa—kuna yoyote ambayo mwanadamu anaweza kutumia kusema kile kilicho haki na kile kisicho haki? Kuna chochote kinachoweza kumsaidia mwanadamu kujua kilicho takatifu na kilicho ovu? Kuna viwango vyovyote? (La.) Hakuna viwango na hakuna msingi ambao unaweza kumsaidia mwanadamu. Hata kama watu wanajua neno “takatifu,” hakuna yeyote anayejua kweli kile kilicho takatifu. Kwa hivyo mambo haya ambayo Shetani anamletea mwanadamu yanaweza kumruhusu kujua ukweli? Je, yanaweza kumruhusu mwanadamu kuishi na ubinadamu unaoongezeka? Je, yanaweza kumruhusu mwanadamu kuishi maisha ambamo anaweza zaidi na zaidi kumwabudu Mungu? (La.) Ni dhahiri kwamba hayawezi kumruhusu mwanadamu kumwabudu Mungu, au kuelewa ukweli, wala hayawezi kumruhusu mwanadamu kujua utakatifu na uovu ni nini. Kinyume chake, mwanadamu anakuwa zaidi na zaidi mwenye uasherati, mbali na mbali zaidi na Mungu. Hii ndiyo sababu ya mbona tunasema Shetani ni mwovu. Baada ya kuchangua asili ovu nyingi za Shetani, je, mmeona Shetani kuwa na dalili yoyote ya utakatifu katika sifa zake ama katika uelewa wenu wa kiini chake? (La.) Hiyo ni ya hakika. Kwa hivyo mmeona kiini chochote cha Shetani ambacho kinashiriki usawa wowote na Mungu? (La.) Je, kuna maonyesho ya Shetani ambayo yanashiriki usawa na Mungu? (La.) Kwa hivyo sasa Nataka kuwauliza, kwa kutumia maneno yenu, utakatifu wa Mungu ni nini hasa? Kwanza kabisa, utakatifu wa Mungu unasemwa kwa uhusiano na nini? Je, unasemwa kwa uhusiano na kiini cha Mungu? Ama unasemwa kwa uhusiano na vipengele fulani vya tabia Yake? (Inasemwa kwa uhusiano na kiini cha Mungu.) Lazima tupate kidato wazi katika mada yetu tunayopenda. Inasemwa kwa uhusiano wa kiini cha Mungu. Kwanza kabisa, tumetumia uovu wa Shetani kama foili[a] ya kiini cha Mungu, kwa hivyo umeona kiini chochote cha Shetani katika Mungu? (La, hatujaona. Mungu si fidhuli, si mchoyo na hasaliti, na kutokana na kipengele hiki kiini kitakatifu cha Mungu kinaonekana kufumbuliwa.) Kunacho kingine cha kuongeza? (Mungu hana dalili za tabia potovu ya Shetani. Chochote Shetani anacho ni hasi kabisa, wakati kile ambacho Mungu anacho ni kizuri. Tunaweza kuona kwamba Mungu amekuwa upande wetu daima, Akitulinda na kutuhifadhi kutoka wakati tulipokuwa wachanga, katika maisha yetu yote hadi sasa, na hasa wakati ambapo tumechanganyikiwa na kupotea njia. Hamna udanganyifu ndani ya Mungu, hamna kusema uongo. Yeye hunena kwa udhahiri na uwazi, na hii pia ni asili ya kweli ya Mungu.) Vizuri sana! (Hatuwezi kuona tabia yoyote potovu ya Shetani kwa Mungu, hamna udanganyifu, hamna kujisifu, hamna ahadi tupu na hamna udanganyifu. Ni Mungu pekee ambaye mwanadamu anaweza kuamini na Mungu ni mwaminifu na mkweli. Kutoka kwa kazi ya Mungu, tunaweza kuona Mungu akiwaambia watu wawe waaminifu, wawe na hekima, wawe na uwezo wa kung’amua kati ya mema na mabaya na kuwa na utambuzi wa watu, matukio, na mambo mbalimbali. Kwa haya tunaweza kuona utakatifu wa Mungu.) Je, mmemaliza? Je, mmeridhika na mliyoyasema? Ni kiasi gani cha uelewa cha Mungu kweli upo mioyoni mwenu? Na mnaelewa kiasi kipi utakatifu wa Mungu? Najua kwamba kila mmoja kati yenu katika moyo wake ana baadhi ya kiwango cha ufahamu wa utambuzi, kwa sababu kila mtu anaweza kuhisi kazi ya Mungu kwao na, katika viwango tofauti, wao hupata vitu vingi kutoka kwa Mungu; wao hupata neema na baraka, wao hutiwa nuru na kuangaziwa, na wao hupokea hukumu na kuadibu kwa Mungu ili kwamba mwanadamu aweze kuwa na uelewa rahisi wa kiini cha Mungu.

Ingawa utakatifu wa Mungu tunaojadili leo unaweza kuonekana geni kwa watu wengi, bila kujali jinsi unaweza kuonekana tumeanza mada hii, na mtakuwa na ufahamu zaidi mnapotembea katika njia yenu kwenda mbele. Itawalazimu kuja kuhisi na kuelewa kutoka kwa uzoefu wenu wenyewe kwa utaratibu. Sasa uelewa wenu wa utambuzi kuhusu kiini cha Mungu bado unahitaji kipindi cha muda mrefu kujifunza, kuthibitisha, kuhisi na kuipitia, hadi siku moja mtajua utakatifu wa Mungu kutoka katikati ya moyo wenu kuwa kiini cha Mungu ambacho hakina dosari, upendo wa Mungu usio na ubinafsi, kwamba haya yote Mungu humpa mwanadamu hayana ubinafsi, na mtakuja kujua ya kwamba utakatifu wa Mungu hauna dosari wala haushutumiki. Hivi viini vya Mungu si maneno tu ambayo Yeye hutumia kuonyesha utambulisho Wake, bali Mungu hutumia kiini Chake kwa kimya na kwa dhati kushughulika na kila mtu. Kwa maneno mengine, kiini cha Mungu si tupu, wala si cha nadharia au mafundisho ya dini na hakika si aina ya maarifa. Si aina ya elimu kwa mwanadamu, lakini badala yake ni ufunuo wa kweli wa matendo ya Mungu mwenyewe na ni kiini ambacho kimefichuliwa cha kile Mungu anacho na alicho. Binadamu anapaswa kujua kiini hiki na kukifahamu, kwa kuwa kila kitu Mungu hufanya na kila neno Yeye husema ni la thamani kubwa na umuhimu mkubwa kwa kila mtu. Unapokuja kuelewa utakatifu wa Mungu, basi unaweza kweli kumwamini Mungu; unapokuja kuelewa utakatifu wa Mungu, basi unaweza kweli kutambua maana halisi ya maneno haya “Mungu Mwenyewe, wa Kipekee.” Hutafikiria tena kwamba unaweza kuchagua kutembea njia zingine, na hutakuwa tena radhi kusaliti kila kitu ambacho Mungu amekupangia. Kwa sababu kiini cha Mungu ni takatifu, hiyo ina maana kwamba kupitia tu Mungu ndipo unaweza kutembea njia yenye kung’aa na sahihi katika maisha; ni kupitia tu Mungu unaweza kujua maana ya maisha, ni tu kupitia Mungu unaweza kuishi kwa kudhihirisha ubinadamu halisi, kumiliki ukweli, kujua ukweli, na ni kupitia tu Mungu unaweza kupata maisha kutoka kwa kweli. Ni Mungu Mwenyewe tu anaweza kukusaidia kuepuka maovu na kukuokoa kutoka kwa madhara na udhibiti wa Shetani. Kando na Mungu, hakuna mtu au kitu kinaweza kukuokoa kutoka kwa bahari ya mateso, ili usiteseke tena: Hili linaamuliwa na kiini cha Mungu. Ni Mungu Mwenyewe tu hukuokoa bila ubinafsi wowote, ni Mungu pekee anayehusika na maisha yako ya baadaye, na hatima yako na maisha yako, na Yeye anapanga mambo yote kwa ajili yako. Hili ni jambo ambalo hakuna kitu ambacho kimeumbwa au hakijaumbwa kinaweza kutimiza. Kwa sababu hakuna kitu ambacho kimeumbwa au hakijaumbwa kina kiini cha Mungu kama hiki, hakuna mtu au kitu kina uwezo wa kukuokoa au kukuongoza wewe. Huu ndio umuhimu wa kiini cha Mungu kwa mwanadamu. Labda mnahisi kuwa maneno haya Niliyoyasema yanaweza kweli kusaidia kimsingi katika kanuni. Lakini kama wewe unafuatilia ukweli, kama wewe unapenda ukweli, katika uzoefu wako wa baada ya hapa maneno haya hayataleta tu mabadiliko katika hatima yako, lakini zaidi ya hayo yatakuleta kwa njia sahihi ya maisha. Je, unafahamu hili, siyo? (Ndiyo.) Kwa hivyo sasa mna moyo wa kupenda katika kujua kiini cha Mungu? (Ndiyo.) Ni vizuri kuwa na moyo wa kupenda. Tutamalizia hapa kujadili mada yetu ya leo juu ya kujua utakatifu wa Mungu.

***

Ningependa kuwazungumzia kuhusu kitu mlichofanya kilichonishangaza mwanzoni mwa mkusanyiko wetu leo. Wengine wenu pengine mlikuwa na hisia za shukrani hivi karibuni, ama kuhisi shukrani, na hivyo mlitaka kuonyesha kimwili kile mlichokuwa nacho akilini mwenu. Hili si la kushutumiwa, na si sahihi wala makosa. Lakini ningependa muelewe kitu. Ni nini hiki? Kwanza Ningetaka kuwauliza kuhusu mlichokifanya hivi sasa. Je, kulikuwa ni kusujudu ama kupiga magoti kuabudu? Kuna yeyote anayeweza kuniambia? (Tunaamini ilikuwa kusujudu.) Mnaamini kulikuwa kusujudu, kwa hivyo ni nini maana ya kusujudu? (Kuabudu.) Kwa hivyo ni nini kupiga magoti kuabudu basi? Sijashiriki hili na ninyi awali, lakini leo nahisi ni muhimu kushiriki mada hii na ninyi. Je, mnasujudu katika mikusanyiko yenu ya kawaida? (La.) Je, mnasujudu mnaposema sala zenu? (Ndiyo.) Je, mnasujudu kila wakati mnaposema sala zenu, hali zinaporuhusu? (Ndiyo.) Hivyo ni vizuri sana. Lakini kile Ningependa nyinyi muelewe leo ni kwamba Mungu hukubali tu kupiga magoti kwa aina mbili za watu. Hatuhitaji kutafuta maoni katika Biblia ama tabia za watu wa kiroho, na Nitawaambia kitu kweli hapa na sasa. Kwanza, kusujudu na kupiga magoti kuabudu si kitu sawa. Mbona Mungu anakubali kupiga magoti kwa wale wanaosujudu wenyewe? Ni kwa sababu Mungu humwita mtu Kwake na humwita mtu huyu kukubali agizo la Mungu, kwa hivyo anasujudu mwenyewe mbele ya Mungu. Huyu ni mtu wa aina ya kwanza. Aina ya pili ni kupiga magoti kuabudu kwa mtu anayemcha Mungu na kuepukana na maovu. Kuna watu hawa wa aina mbili tu. Kwa hivyo mko katika aina gani? Mnaweza kusema? Huu ni ukweli kabisa, ingawa unaweza kuumiza hisia zenu kidogo. Hakuna kitu cha kusema kuhusu kupiga magoti kwa watu wakati wa sala—hii ni sahihi na ndivyo inavyopaswa kuwa, kwa sababu wakati watu wanasali wakati mwingi ni kuombea kitu, kufungua mioyo yao kwa Mungu na kukutana Naye uso kwa uso. Ni mawasiliano na mazungumzo, moyo kwa moyo na Mungu. Mkiifanya kama urasmi tu, basi haipaswi kufanya hivyo. Simaanishi kuwashutumu kwa yale ambayo mmefanya leo. Mnajua kwamba nataka tu kuweka wazi kwenu ili muelewe kanuni hii, mnajua? (Tunajua.) Ili msiendelee kufanya hili. Je, watu basi wana fursa yoyote ya kusujudu na kupiga magoti mbele ya uso wa Mungu? Daima kutakuwa na fursa. Hatimaye siku itakuja lakini wakati sio sasa. Mnaona? Je, hili linawafanya kuhisi vibaya? (La.) Hivyo ni vizuri. Labda maneno haya yatawatia moyo ama kuwashawishi ili muweze kujua katika mioyo yenu taabu ya sasa kati ya Mungu na mwanadamu na aina ya uhusiano uliopo sasa kati yao. Ingawa tumeongea na kuzungumza sana hivi karibuni, uelewa wa mwanadamu kuhusu Mungu bado uko mbali na kutosha. Mwanadamu bado ana umbali mrefu wa kwenda katika njia hii ya kutafuta kumwelewa Mungu. Si nia yangu kuwafanya mfanye hivi kwa dharura, ama kuwaharakisha kuonyesha matamanio na hisia za aina hizi. Yale mliyofanya leo yanaweza kufichua na kuonyesha hisia zenu za kweli, na Niliyafahamu. Kwa hivyo wakati mlipokuwa mkiyafanya, nilitaka tu kusimama na kuwatakia mema, kwa sababu Nataka nyote muwe wazima. Kwa hivyo katika maneno na vitendo vyangu vyote ninafanya yote ninayoweza kuwasaidia, kuwaongoza, ili muwe na uelewa sahihi na mtazamo sahihi wa mambo yote. Mnaweza kuelewa haya, sivyo? (Ndiyo.) Hivyo ni vizuri sana. Ingawa watu wana baadhi ya uelewa wa tabia mbalimbali za Mungu, kipengele cha kile anacho Mungu na alicho na kazi Mungu anafanya, wingi wa uelewa huu hauendi mbali na kusoma maneno kwenye ukurasa, ama kuyaelewa katika kanuni, ama tu kuyafikiria. Yale wanayoyakosa sana watu ni uelewa na mtazamo wa kweli unaotoka kwa uzoefu halisi. Ingawa Mungu hutumia njia mbalimbali kuamsha mioyo ya wanadamu, bado kuna njia ndefu ya kutembea kabla mioyo ya wanadamu iamshwe kikamilifu. Sitaki kumwona yeyote akihisi kana kwamba Mungu amemwacha nje kwa baridi, kwamba Mungu amemwacha ama amempuuza. Ningetaka tu kuona kila mtu katika njia ya kufuatilia ukweli na kutafuta kumwelewa Mungu, akiendelea mbele kwa ujasiri na utashi usiosita, bila wasiwasi, bila kubeba mizigo. Haijalishi umefanya makosa gani, haijalishi umepotoka aje ama vile ulivyotenda dhambi, usiwache haya yawe mizigo ama vikorokoro ziada kubeba katika ufuataji wako wa kumwelewa Mungu: Endelea kutembea mbele. Nyakati zote, Mungu hushikilia wokovu wa mwanadamu moyoni Mwake; hili halibadiliki kamwe. Hii ni sehemu ya thamani sana ya kiini cha Mungu. Mnahisi vizuri kiasi sasa? (Ndiyo.) Ninatumai kwamba mnaweza kuchukua mtazamo sahihi katika mambo yote na maneno ambayo Nimezungumza. Wacha tukomeshe ushirika wetu hapa, basi. Kwaheri!

Januari 11, 2014

Tanbihi:

a. Mtu/kitu kinachodhihirisha uzuri/ubora wa kingine kwa kuvilinganisha.

Iliyotangulia: Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee V

Inayofuata: Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VII

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp