Unashuhudia kwamba Mungu amekuwa mwili na kuwa Mwana wa Adamu ili kufanya kazi ya hukumu katika siku za mwisho, na bado wengi wa wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa wanakiri kwamba Bwana atarudi akija na mawingu, na wanategemeza hili hasa aya za Biblia: “Huyu Yesu … atakuja kwa namna hiyo hiyo ambayo mmemuona akienda mbinguni(Matendo 1:11). “Tazama, anakuja na mawingu; nalo kila jicho litamwona yeye(Ufunuo 1:7). Na zaidi ya hayo, wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa pia hutufundisha kwamba Bwana Yesu yeyote asiyekuja na mawingu ni wa uongo na lazima aachwe. Kwa hiyo hatuna uhakika kama mtazamo huu unakubaliana na Biblia; ni sahihi kuchukua huu kama ukweli au la?

07/06/2019

Jibu:

Ikija kwa kungoja kushuka kwa Bwana na mawingu, lazima tusitegemee mawazo ya mwanadamu na fikira! Mafarisayo walifanya kosa kubwa kwa kungoja kufika kwa Masiha. Walitumia kabisa mawazo na fikira ya mwanadamu kumtathmini Bwana Yesu ambaye alisharudi tayari. Mwishowe, walimsulubisha Bwana Yesu msalabani. Je, huu sio ukweli? Je, kungoja kufika kwa Bwana ni rahisi kama tufikiriavyo? Ikiwa Bwana atarudi na kufanya kazi kati ya binadamu kama jinsi Bwana Yesu kwa mwili Alikuwa Amefanya, na hatumtambui Yeye, basi pia sisi tutamhukumu na kumshutumu Yeye kama vile Mafarisayo walivyofanya na kumsulubisha Yeye mara nyingine? Je, huu ni uwezekano? Bwana Yesu alitabiri kuwa Atarudi na Akasema maneno mengi kuihusu, lakini nyinyi mnashikilia tu unabii kuwa Bwana atashuka na mawingu na hamtafuti na kuchunguza nabii zingine muhimu zilizoongelewa na Bwana. Hii inafanya kutembea katika njia mbaya kuwa rahisi na kuachwa na Bwana! Kweli sio tu unabii wa “kushuka na mawingu” ndiyo upo katika Biblia. Kuna unabii mwingi kama huo kuwa Bwana atakuja kama mwizi na kushuka kwa siri. Kwa mfano, Ufunuo 16:15, “Tazama, mimi nakuja kama mwizi.” Mathayo 25:6, “Na kukawa na kelele saa sita ya usiku, Tazama, anakuja bwana arusi; ondokeni nje ili kumkaribisha.” Na Ufunuo 3:20, “Tazama, nimesimama mlangoni, na kupiga hodi: mtu yeyote akisikia sauti yangu, na aufungue mlango, Mimi nitaingia kwake, na nitakula na yeye, na yeye na Mimi.” Unabii huu wote unarejelea Mungu kuwa mwili kama Mwana wa Adamu na kushuka kwa siri. “Kama mwizi” kunamaanisha kuja kwa upole, kwa siri. Watu hawatajua kuwa Yeye ni Mungu hata kama watamwona au kumsikia, kama tu ilivyokuwa awali wakati Bwana Yesu alitokea na kufanya kazi Yake wakati wa kupata mwili Kwake kama Mwana wa Adamu. Kutoka nje, Bwana Yesu alikuwa tu Mwana wa Adamu wa kawaida na hakuna yeyote alijua Yeye ni Mungu, ndiyo sababu Bwana Yesu alitumia “kama mwizi” kama analojia ya kutokea na kazi ya Mwana wa Adamu. Hii ni inastahili sana! Wale ambao hawapendi ukweli, bila kujali jinsi Mungu katika mwili anavyoongea au kufanya kazi, au ukweli ngapi Anaoonyesha, hawakubali. Badala yake, wanamchukulia Mungu mwenye mwili kama mtu wa kawaida na kumshutumu na kumwacha Yeye. Hiyo ndiyo sababu Bwana Yesu alitabiri kuwa Atarudi: “Kwani kama umeme, unavyomulika chini ya mbingu kutoka sehemu moja, huangaza hadi sehemu nyingine chini ya mbingu; vivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakuwa katika siku yake. Bali kwanza lazima apitie mambo mengi, na akataliwe na kizazi hiki(Luka 17:24-25). Kulingana na unabii wa Bwana, kurudi Kwake kutakuwa “kuja kwake Mwana wa Adamu.” “Mwana wa Adamu” inarejelea Mungu katika mwili, sio mwili wa kiroho uliofufuka wa Bwana Yesu ukishuka na mawingu kuonekana wazi mbele ya watu wote. Mbona hali ni hii? Ikiwa ungekuwa mwili wa kiroho uliofufuka wa Bwana Yesu ambao ungekuwa unashuka kwa watu wote na mawingu, ingekuwa nguvu ya ajabu na ya kushtua ulimwengu. Kila mtu angeanguka chini na hakuna yeyote atathubutu kukataa. Kwa hali hiyo, je, Bwana Yesu aliyerudi bado Atastahimili mateso mengi na kukataliwa na kizazi hiki? Bila shaka hapana! Hiyo ndiyo sababu Bwana Yesu alitabiri kuwa kurudi Kwake kutakuwa “kuja kwake Mwana wa Adamu” na “kama mwizi.” Kwa kweli, inarejelea Mungu mwenye mwili kama Mwana wa Adamu kufika kwa siri.

Basi ni nini uhusiano kati ya Mwana wa Adamu anayeshuka kwa siri kuonekana na kufanya kazi Yake na Mungu kuonekana kwa wazi akishuka na mawingu? Je, mchakato huu unahusisha nini? Hebu tuwasiliane kuhusu hilo tu. Katika siku za mwisho, Mungu anapata mwili na kushuka kwa siri kati ya binadamu kutamka na kuongea, Akifanya kazi ya hukumu Akianzia na nyumba ya Mungu, Akiwatakasa na kuwakamilisha wote ambao wanao sikia sauti Yake na kurudi mbele ya kiti Chake cha enzi. na kuwafanya katika kikundi cha washindi. Kisha Mungu analeta maafa makubwa, Akiwasafisha na kuwaadibu wale wote ambao hawakukubali hukumu ya Mungu ya siku za mwisho. Baadaye, Mungu atashuka na mawingu Akionekana kwa wazi mbele ya binadamu wote. Hiyo basi itatimiza kikamilifu unabii katika Ufunuo 1:7: “Tazama, anakuja na mawingu; nalo kila jicho litamwona yeye, na pia wale waliomdunga: na makabila yote ya ulimwengu yatalia kwa huzuni kwa sababu ya yeye.” Wakati Bwana atashuka na mawingu, wale waliomchoma watamwona Yeye bado? Ni akina nani hasa ndio walimchoma? Wengine wanasema ni waliomsulubisha Bwana Yesu msalabani. Je, hiyo ndiyo hali? Je, si watu waliomsulubisha Bwana Yesu walilaaniwa na kuangamizwa na Mungu kitambo sana? Kwa kweli, wale ambao walimchoma Yeye ni wale ambao, katika wakati ambao Mungu mwenye mwili ameshuka kwa siri katika siku za mwisho kufanya kazi, hawatafuti sauti ya Mungu na kumshutumu na kumkataa Mwenyezi Mungu. Kwa wakati huo, watamwona Mwenyezi Mungu ambaye walimkataa na kumshutumu ni hasa Yule Mwokozi Yesu waliyekuwa wakimngoja kwa uchungu kwa miaka hii zote. Watapiga vifua vyao, watoe machozi na kusaga meno yao, na matokeo yao yanaweza tu kuwa adhabu. Kitabu cha Ufunuo hakisemi kama watu wa aina hii wataishi ama watakufa mwishowe, hivyo basi hatuwezi kujua kwa kweli. Ni Mungu pekee Ajuaye. Kila mtu anafaa kuwa wazi. Bikira wenye busara tu ambao wanasikia sauti ya Mungu ndio wanaweza kupata nafasi ya kukaribisha kurudi kwa Bwana, waletwe mbele ya kiti cha enzi cha Mungu kuhudhuria chajio ya ndoa ya Mwanakondoo, na kukamilishwa na Mungu kuwa washindi. Hii inatimiza unabii katika Ufunuo 14:4, “Hao ndio wale hawakunajisiwa na wanawake; kwani wao ni bikira. Hao ndio wale wanaomfuata Mwanakondoo popote aendapo. Hawa walikombolewa kutoka miongoni mwa wanadamu, wakiwa matunda ya kwanza kwa Mungu na Mwanakondoo.” Kwa wale ambao walishikilia tu wazo kuwa Bwana atashuka na mawingu lakini hawatafuti na kuchunguza kazi ya Bwana ya siku za mwisho, wanachukuliwa kuwa bikira wajinga. Hasa wale ambao wanamkataa kwa nguvu na kumshutumu Mwenyezi Mungu, hao ni Mafarisayo na maadui wa Kristo wanaowekwa wazi na kazi ya Mungu katika siku za mwisho. Ni watu wote ambao wamesulubisha Mungu tena. Hawa watu wote wataanguka kwenye maafa makubwa na kupokea adhabu.

Hebu tuone jinsi Mafarisayo walingoja kufika kwa Masiha na kwa nini walimsulibisha Bwana Yesu msalabani. Mwanzoni, Mafarisayo wa Kiyahudi walikuwa wenye wingi wa dhana na fikira ikija kwa Masiha. Waliuona unabii wa biblia: “Kwani mtoto amezaliwa kwa sababu yetu, sisi tumepewa mwana wa kiume: na mamlaka ya serikali yatakuwa juu ya bega lake(Isaya 9:6). “Lakini ewe, Bethlehemu Efrata, ingawa wewe ni mdogo miongoni mwa maelfu ya Yuda, hata hivyo kutoka kwako atanitokea yule ambaye atakuwa mtawala katika Israeli; ambaye asili yake ni ya kutoka zamani za kale, tangu milele(Mika 5:2). Kulingana na maneno ya unabii katika Biblia na njozi zao mbalimbali za muda mrefu na mambo yaliyofasiriwa kuhusu kufika kwa Masiha, Mafarisayo walibainisha kuwa Bwana bila shaka Ataitwa Masiha na kwa hakika Atazaliwa kwa familia tajiri. Zaidi ya hayo, Atakuwa kama Daudi na kuwa Mfalme wa Uyahudi, kuwaongoza kutoroka utawala wa serikali ya Warumi. Wayahudi wengi labda walifikiria kwa njia hii. Lakini Mungu hakutimiza unabii huu kulingana na dhana na fikira zao, hivyo Mafarisayo wakajaribu kutafuta kila aina ya mashtaka dhidi ya Bwana Yesu na kumshutumu na kumkufuru Bwana Yesu. Hata kama wakati huo Bwana Yesu alionyesha ukweli mwingi na kumshutumu na kumkufuru Bwana Yesu. Akidhihirisha kikamilifu mamlaka na nguvu za Mungu, Mafarisayo hawakujali jinsi maneno ya Bwana Yesu yalikuwa ya maana sana au jinsi mamlaka Yake yalikuwa kubwa. Mradi tu haikupatana na dhana na fikira zao, mradi tu Hakuzaliwa kwa familia tajiri na sura Yake sio ya kilodi na ya kutukuzwa, mradi tu jina Lake halikuwa Masiha, wangeshutumu na kukataa. Kwa sababu ya hali yao asili ya kuchukia ukweli, mwishowe walimsulubisha Bwana Yesu, ambaye Alionyesha ukweli na kufanya kazi ya wokovu, msalabani! Je, Mafarisayo ni wa kuchukiza? Wanafaa kulaaniwa? Dhambi za Mafarisayo kukataa na kushutumu Bwana Yesu kwa kikamilifu zilifichua hali yao asili ya kishetani ya kuchukia ukweli na kukuwa na kinyongo na ukweli. Hii inaonyesha kuwa nyoyo zao kwa kweli hazikuwa zinatarajia Masiha kuwaokoa kutoka dhambini, lakini Walitarajia Mfalme wa Wayahudi kuwasaidia kutoroka utawala wa serikali ya Warumi, ili wasilazimike kuteseka tena kama watumwa! Waliamini katika Mungu na wakatazamia kufika kwa Masiha yote kwa sababu walitaka kuridhisha maombi yao ya kibinafsi na kuhifadhi hali zao. Ni kosa gani Mafarisayo walitenda wakingoja kuja kwa Masiha? Kwa nini walilaaniwa na kuadhibiwa na Mungu? Hii kweli inasababisha fikira! Kwa nini Mafarisayo walikataa na kumshutumu Bwana Yesu wakati Alionekana kufanya kazi Yake? Ni asili na dutu zipi za Mafarisayo zimeonyeshwa hapa? Hizi ni shida watu wanaotamani kuonekana kwa Mungu wanafaa kuzielewa! Ikiwa hatuwezi kuelewa shida hizi, basi ikija kwa kumpokea Bwana Yesu aliyerudi, tunaweza pia kuishia njia sawa ya kumkataa Mungu kama Mafarisayo!

Mafarisayo walingoja kufika kwa Masiha jinsi gani? Kwa nini walimsulubisha Bwana Yesu? Je, ni nini chanzo cha maswali haya? Hebu tuangalie ni nini Mwenyezi Mungu anasema! Mwenyezi Mungu Anasema, “Je, mngependa kujua kiini cha sababu ya Mafarisayo kumpinga Yesu? Je, mnataka kujua dutu ya Mafarisayo? Walikuwa wamejawa na mawazo makuu kuhusu Masiha. Kilicho zaidi, waliamini tu kuwa Masiha angekuja, ilhali hawakutafuta ukweli wa uzima. Na hivyo, hata leo bado wanamngoja Masiha, kwani hawana maarifa ya njia ya uzima, na hawajui ukweli ni nini. Ni vipi, hebu nielezeni, watu wapumbavu, wakaidi na washenzi kama hawa wangeweza kupata baraka za Mungu? Wangewezaje kumwona Masiha? Walimpinga Yesu kwa sababu hawakujua mwelekeo wa kazi ya Roho Mtakatifu, kwa sababu hawakuijua njia ya ukweli uliozungumziwa na Yesu, na zaidi, kwa sababu hawakumwelewa Masiha. Na kwa kuwa hawakuwa wamewahi kumwona Masiha na hawakuwa wamewahi kuwa pamoja na Masiha, walifanya kosa la kuning’inia bila mafanikio kwa jina la Masiha huku wakipinga dutu ya Masiha kwa kila njia iwezekanayo. Mafarisayo hawa kwa dutu walikuwa wakaidi, wenye kiburi na hawakutii ukweli. Kanuni ya imani yao kwa Mungu ni: Haijalishi mahubiri Yako ni makubwa vipi, haijalishi mamlaka Yako ni makubwa vipi, Wewe si Kristo iwapo Huitwi Masiha. Je, maoni haya si ya upuuzi na ya kudhihaki?(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kufikia Utakapouona Mwili wa Kiroho wa Yesu, Mungu Atakuwa Ametengeneza Upya Mbingu na Dunia). Baada ya kusoma maneno ya Mwenyezi Mungu, kiini na chanzo cha upinzani wa Mafarisayo wa Bwana Yesu kwa kumngojea Masiha. Hivyo kuhusu kupokea kurudi kwa Bwana, ikiwa mwanadamu anategemea dhana zake na fikira, na kungoja tu kwa Bwana kushuka na mawingu kama mpumbavu, badala ya kutafuta ukweli na kusikiliza sauti ya Mungu, basi si watakuwa wanatembea njia sawa na Mafarisayo ya kumkataa Mungu? Basi matokeo yake yatakuwa nini? Inaonekana kila mtu amekuwa wazi kuhusu hii.

Sasa, injili ya ufalme ya Mwenyezi Mungu imekuwa ikienezwa Bara Uchina kote kwa zaidi ya miaka 20. Imeenea kwa kina hadi madhehebu na vikundi mbalimabali. Katika wakati huu, kwa sababu ya ukandamizaji wa hasira na kuchukuliwa hatua za kinidhamu na serikali ya CCP, pamoja na kampeni ya propaganda ya vyombo vya habari ya CCP, Mwenyezi Mungu tayari ni jina ya kaya ambao kila mtu anaijua. Baadaye, ukweli wote ulioonyeshwa na Mwenyezi Mungu na video na filamu mbalimbali za Kanisa la Mwenyezi Mungu zimekuwa zikitolewa hatua kwa hatua mtandaoni, ikienezwa kote ulimwenguni. Watu katika ulimwengu wa kidini wote wamesikia kuihusu utaratibu wa ushuhuda mbalimbali za Kanisa la Mwenyezi Mungu. Watu wengi sana wametoa ushuhuda kuwa Mungu Amerejea. Hii kwa kikamilifu inatimiza unabii wa Bwana Yesu: “Na kukawa na kelele saa sita ya usiku, Tazama, anakuja bwana arusi; ondokeni nje ili kumkaribisha(Mathayo 25:6). Basi kwa nini wachungaji na wazee wa kanisa wa kidini bado kwa hasira wanashutumu na kukataa kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho? Kuna unabii mwingi sana kuhusu kurudi kwa Bwana katika Biblia, hivyo kwa nini wamekazia macho unabii kuhusu Bwana kushuka na mawingu? Kwa nini hawatafuti kabisa wanaposikia kuna ushuhuda ingine kuhusu kuja kwa Bwana? Kwa nini, wakati wanajua kuwa Mwenyezi Mungu ameonyesha ukweli mwingi na wameona halisi ya kazi ya Mungu, je, bado kwa ukaidi wameshikilia dhana na fikira zao za kukataa na kushutumu kazi ya Mungu ya siku za mwisho? Je, watu hawa wanapenda ukweli na kwa kweli kutarajia kurudi kwa Bwana au la? Je, hao ni bikira wenye busara au bikira wapumbavu? Ikiwa hao ni bikira wenye busara na kwa kweli wanatarajia kurudi kwa Bwana, basi mbona, wanaposikia sauti ya Mungu na kuona injili ya ufalme ikisitawi, bado kwa ukaidi wanashutumu na kukataa? Je, huu unaweza kuwa uaminifu wao wa kutamani na kutarajia Bwana aonekane? Je, hii inaweza kuwa ishara yao halisi ya kufurahia kurudi kwa Bwana? Hatimaye, kwa kweli, imani yao katika Bwana na kutarajia kurudi kwa Bwana Yesu ni buni, lakini kutarajia kwao kubarikiwa na kuingia katika ufalme wa mbinguni ni kweli! Wanaamini kwa Bwana sio kwa ajili ya kutafuta ukweli na kupata uzima, sio kwa ajili ya kupata ukweli na kwenda mbali ya dhambi. Ni nini wanachojali zaidi kuhusu? Ni wakati Bwana Atashuka kuwachukua moja kwa moja juu katika ufalme wa mbinguni na kuwafanya waepuke mateso ya mwili na kufurahia baraka za ufalme wa mbinguni. Hili ni kusudi lao halisi la kumwamini Mungu! Mbali na sababu hii, ni sababu gani waliyo nayo ya kukana Mwenyezi Mungu, Anayeonyesha ukweli kuokoa binadamu? Kila mtu anaweza kufikiria kuihusu. Ikiwa mtu anapenda ukweli na kwa kweli anatamani Mungu Aonekane, watafanyaje wakati wanaposikia kuwa Bwana Amekuja? Hawatasikiliza, hawataangalia, hawatawasiliana nayo? Je, watakana kwa upofu, kushutumu na kukataa? Bila shaka hapana! Kwa sababu mtu ambaye kwa dhati anatamani kuonekana kwa Mungu na anakaribisha kufika kwa Mungu anatarajia mwanga wa kweli kuonekana, ukweli na haki zikitawala moyoni mwake. Anatarajia kuja kwa Mungu kuwaokoa binadamu na kuwasaidia watu kuepuka dhambi kabisa ili kutakaswa na kupatwa na Mungu. Lakini wale ambao wanangoja tu Bwana kushuka na mawingu bado wanakataa na kumkana Mwenyezi Mungu, hasa wale viongozi wa kidini ambao kwa hasira wanashutumu na kumkataa Mwenyezi Mungu kwa ajili ya kuhifadhi hali na maisha yao—hao ni watu wote ambao wanadharau ukweli na kuchukia ukweli. Wote ni wasioamini na wapinga Kristo waliofichuliwa na kazi ya Mungu wa siku za mwisho. Baada ya Mungu katika mwili kumaliza kazi Yake ya wokovu, hawa watu wataanguka ndani ya maafa hayo ya mmoja kati ya miaka milioni, wakilia na kusaga meno yao. Basi unabii wa Bwana kushuka na mawingu kuonekana wazi utakuwa umetimizwa kikamilifu: “Tazama, anakuja na mawingu; nalo kila jicho litamwona yeye, na pia wale waliomdunga: na makabila yote ya ulimwengu yatalia kwa huzuni kwa sababu ya yeye(Ufunuo 1:7).

Hebu tuangalie ni nini maneno ya Mwenyezi Mungu yanasema: “Watu wasioukubali ukweli, ilhali wanangoja kufika kwa Yesu juu ya wingu jeupe kwa upofu, kwa hakika watamkufuru Roho Mtakatifu, na ni kundi ambalo litaangamizwa. Mnatamani tu neema ya Yesu, na kutaka tu kufurahia ulimwengu wa mbinguni wenye raha, ilhali hamjawahi kutii maneno yaliyonenwa na Yesu, na hamjawahi kupokea ukweli utakaoonyeshwa na Yesu atakaporudi katika mwili. Mtashikilia nini badala ya ukweli wa kurejea kwa Yesu juu ya wingu jeupe? Je, ni ukweli ambao ndani yake mnashinda mkitenda dhambi, na kisha kuzikiri, tena na tena? Mtatoa nini kama kafara kwa Yesu Anayerejea juu ya wingu jeupe? Je, ni miaka ya kazi ambayo mnajiinua nayo? Ni nini mtakachoinua kumfanya Yesu Anayerejea kuwaamini? Je, ni hiyo asili yenu ya kiburi, ambayo haitii ukweli wowote?

… Nawaambieni, wale wanaoamini katika Mungu kwa sababu ya ishara hakika ni kikundi ambacho kitapata kuangamizwa. Wale wasio na uwezo wa kukubali maneno ya Yesu Ambaye Amerudi kwa mwili kwa hakika ni vizazi vya kuzimu, vizazi vya malaika mkuu, kikundi ambacho kitakabiliwa na kuangamizwa kwa milele. Watu wengi wanaweza kukosa kujali kuhusu kile Ninachosema, lakini bado Nataka kumwambia kila anayedaiwa kuwa mtakatifu wa Mungu anayemfuata Yesu kwamba, mtakapoona Yesu Akishuka kutoka juu mbinguni juu ya wingu jeupe kwa macho yenu wenyewe, huu ndio utakuwa mwonekano wa umma wa Jua la haki. Pengine huo utakuwa wakati wa furaha kubwa kwako, ilhali lazima ujue kuwa wakati utakaposhuhudia Yesu Akishuka kutoka mbinguni ndio pia wakati ambapo utaenda chini kuzimu kuadhibiwa. Huo ndio utakuwa wakati wa mwisho wa mpango wa Mungu wa usimamizi na ndio utakuwa wakati ambapo Mungu atawatunukia wazuri na kuwaadhibu waovu. Kwani hukumu ya Mungu itakuwa imeisha kabla ya mwanadamu kuona ishara, wakati kuna onyesho la ukweli tu. Wale wanaokubali ukweli na hawatafuti ishara, na hivyo wametakaswa, watakuwa wamerudi mbele za kiti cha enzi cha Mungu na kuingia katika kumbatio la Muumba. Ni wale tu ambao wanashikilia imani kwamba “Yesu Asiyeshuka juu ya wingu jeupe ni Kristo wa uongo” watakabiliwa na adhabu ya milele, kwani wanaamini tu katika Yesu ambaye Anaonyesha ishara, lakini hawamkubali Yesu Anayetangaza hukumu kali na Anatoa njia ya kweli ya uzima. Na hivyo itakuwa tu kuwa Yesu Atawashughulikia tu Atakaporejea wazi wazi juu ya wingu jeupe. Ni wakaidi sana, wanajiamini sana, wenye kiburi sana. Wapotovu kama hawa watatunukiwa vipi na Yesu?(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kufikia Utakapouona Mwili wa Kiroho wa Yesu, Mungu Atakuwa Ametengeneza Upya Mbingu na Dunia).

Kimetoholewa kutoka katika Maswali na Majibu Bora zaidi Kuhusu Injili ya Ufalme

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp