Unasema kwamba watu wanaomwamini Mungu wanapaswa kuikubali kazi ya hukumu ya Mungu katika siku za mwisho, na ni hapo tu ndipo wanapoweza kutakasiwa tabia yao potovu na wao wenyewe kuokolewa na Mungu. Lakini sisi, kwa mujibu wa mahitaji ya Bwana, hutenda unyenyekevu na uvumilivu, kuwapenda adui zetu, kuibeba misalaba yetu, kuviacha vitu vya dunia, na sisi hufanya kazi na kuhubiri kwa ajili ya Bwana na kadhalika. Hivyo si haya yote ni mabadiliko yetu? Daima tumetafuta kwa njia hii, kwa hiyo hatuwezi kupata utakaso, unyakuo na kuingia katika ufalme wa mbinguni?

07/06/2019

Jibu:

Tunaweza kuwapenda adui zetu, kubeba msalaba, kushinda mwili wetu, na kueneza injili ya Bwana. Hizi ni tabia chanya zinazotokana na imani yetu kwa Bwana, na kuweza kutenda kwa njia hii kunaashiria kuwa imani yetu kwa Bwana ni ya kweli. Tabia hizi nzuri zinaweza kuonekana kuwa sahihi kwa wengine na kana kwamba ziko sambamba na neno la Mungu, lakini haimaanishi kwamba tunayaweka maneno ya Mungu katika vitendo na kufuata mapenzi ya Baba wa mbinguni, wala haimaanishi kwamba tumeacha asili yetu ya dhambi na kutakaswa. Tunapokuwa tunaangalia tabia nzuri za wengine hatuwezi tu kuangalia kuonekana kwao kwa nje; lazima pia tuangalie nia zao na madhumuni ya hatimaye. Ikiwa nia za mtu ni kumtii, kumpenda, na kumridhisha Mungu, basi aina hii ya tabia njema ni kutenda ukweli na kutii mapenzi ya Baba wa mbinguni. Kwa upande mwingine, kama tabia nzuri ya mtu ni kwa ajili tu baraka, kutuzwa na kupewa taji, na si kwa ajili ya moyo wa upendo kwa Mungu, basi aina hii ya “tabia nzuri” ni kama unafiki wa Mafarisayo wala si kutenda mapenzi ya Baba ya mbinguni. Ikiwa kuonyesha tabia njema pekee kunamaanisha kwamba tunayafuata mapenzi ya Baba wa mbinguni na kwamba tumetakaswa, basi kwa nini mara nyingi tunatenda dhambi na kumpinga Mungu? Kwa nini bado tunaishi maisha ya kutenda dhambi mchana na kukiri dhambi usiku? Hii inaonyesha vya kutosha kuonyesha tabia njema pekee haimaanishi kuwa tunautenda ukweli na kuishi kwa kudhihirisha uhalisi wa neno la Mungu wala haimaanishi kwamba tunamjua Mungu au tuna moyo wa uchaji Kwake, sembuse kuwa na uwezo wa kumpenda na kumtii Yeye. Kama maneno ya Mwenyezi Mungu yasemavyo: “Mabadiliko katika tabia tu hayawezi kudumu. Kama hakuna mabadiliko katika tabia ya maisha ya watu, basi siku moja upande wao wa uovu utajionyesha. Kwa sababu kiini cha mabadiliko katika mienendo yao ni bidii, pamoja na kazi ya Roho Mtakatifu wakati huo, ni rahisi sana kwao kuwa na bidii, ama kuonyesha ukarimu kwa muda. Kama wasioamini wanavyosema, ‘kufanya tendo moja zuri ni rahisi, kilicho kigumu ni kufanya matendo mazuri maishani.’ Watu hawana uwezo wa kufanya matendo mazuri katika maisha yao yote. Mienendo yao inaongozwa na maisha hayo; maisha yao yalivyo, ndivyo mwenendo wao ulivyo, na kile tu kinachofichuliwa kwa asili kinawakilisha maisha hayo, na asili ya mtu. Vitu vilivyo vya bandia haviwezi kudumu. … Kuwa na tabia nzuri si sawa na kumtii Mungu, hasa si sawa na kulingana na Kristo. Mabadiliko katika tabia yanategemea mafundisho, na kuzaliwa na juhudi—hayategemei maarifa ya kweli kumhusu Mungu, ama juu ya ukweli, hasa hayategemei uongozi wa Roho Mtakatifu. Ingawa kuna nyakati ambapo baadhi ya yale watu wanayofanya yanaongozwa na Roho Mtakatifu, haya si maonyesho ya maisha, sembuse kuwa sawa na kumjua Mungu; haijalishi mienendo ya mtu ni mizuri kiasi gani, haithibitishi kwamba anamtii Mungu, ama kwamba anauweka ukweli katika matendo(“Tofauti Kati Ya Mabadiliko Ya Nje Na Mabadiliko Katika Tabia” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). Maneno ya Mwenyezi Mungu yanatuelezea wazi kuhusu asili na chanzo cha tabia njema. Tabia njema ya mwanadamu inatokana na shauku na ni tendo lenye msingi katika mafundisho na sheria, si kwa ufahamu wa kanuni za matendo baada ya kuelewa ukweli mwingi, au kutoka kwa tamaa ya kumpenda na kumridhisha Mungu kwa sababu ya kuelewa mapenzi Yake. Tabia njema inatokana na mawazo na fikra za mtu, na hivi vinatokana na maoni ya mtu binafsi na asili yake potovu. Kwa hiyo bila afanyacho mwanadamu, maumivu yoyote anayoyapitia au gharama yoyote anayolipa, sio kutenda ukweli. Sio kumtii Mungu haitoki kwa kazi ya Roho Mtakatifu. Hata tunapoonyesha tabia njema na tunaweza kufuata sheria fulani, tukionekana kuwa wacha Mungu na wa dini, bado tuna uwezekano wa kutenda dhambi na kumpinga Mungu kwa sababu ya tabia yetu ya zamani ya kishetani, asili yetu ya dhambi ambayo haijaondolewa, na ukosefu wa uelewa wa kweli wa Mungu. Tumewaona watu wengi wenye tabia njema ambao bado hutenda dhambi mara nyingi na kukiri dhambi zao baada ya kumwamini Mungu. Huu ni ukweli usiopingika. Kutenda kwa tabia njema kama bado wanatenda dhambi na kumpinga Mungu ni ithibati ya kutosha kwamba hawafuati mapenzi ya Baba wa mbinguni, na hawawezi kupata sifa ya Mungu. Mafarisayo wa Kiyahudi walikuwa watii sheria waliokuwa na tabia isiyokuwa na kosa kwa juujuu. Hata hivyo, Bwana Yesu alipokuja kufanya kazi, kwa nini walimpinga, kumshutumu, kula njama, na kumsulubisha Bwana Yesu vikali? Hii inaonyesha kwamba asili ya kumpinga Mungu ilikuwa ya kimaumbile ndani yao. Haijalishi jinsi walivyotenda wema vizuri, haikumaanisha kwamba walielewa, walitii au walilingana na Mungu, sembuse kufuata mapenzi ya Mungu na kupata utakaso. Ikiwa tunataka kuondoa asili yetu ya dhambi na kupata utakaso, tunapaswa kupitia kazi ya Mungu ya hukumu na kuadibu katika siku za mwisho, kuelewa ukweli kamili ulioko ndani yake na kupata ujuzi wa kweli wa Mungu, hivyo kupata na utii wa kweli na uchaji wa Mungu. Vinginevyo tabia potovu ya Shetani iliyojikita ndani yetu haiwezi kamwe kutakaswa na kubadilishwa, na kamwe hatutaupendeza moyo wa Mungu au kukubaliwa katika ufalme wa Mungu.

Bwana Yesu ametoka kutenda tu kazi ya ukombozi. Hivyo basi, wakati wa Enzi ya Neema, binadamu hawakuweza kujiondoa katika dhambi zao na kupata utakaso, licha ya namna walivyojaribu au walivyosoma Biblia. Katika siku za mwisho, Mungu anaanza kazi Yake ya hukumu kutoka kwa nyumba Yake kulingana na hatua za mpango Wake wa usimamizi wa kuwaokoa binadamu; kupitia kazi hii, Atawatakasa na kuwabadilisha binadamu, huku akiwaruhusu kuondolewa dhambi zao na kupata utakaso. Ni kama tu vile Mwenyezi Mungu akasema, “Hata ingawa Yesu Alifanya kazi nyingi miongoni mwa wanadamu, Yeye Alimaliza tu ukombozi wa wanadamu wote na akawa sadaka ya dhambi ya mwanadamu, na Hakumwondolea mwanadamu tabia yake yote ya upotovu. Kumwokoa mwanadamu kikamilifu kutokana na ushawishi wa Shetani hakukumlazimu Yesu kuchukua dhambi zote za mwanadamu kama sadaka ya dhambi tu, lakini pia kulimlazimu Mungu kufanya kazi kubwa zaidi ili kumwondolea mwanadamu tabia yake kikamilifu, ambayo imepotoshwa na Shetani. Na kwa hivyo, baada ya mwanadamu kusamehewa dhambi zake, Mungu Amerudi katika mwili kumwongoza mwanadamu katika enzi mpya, na kuanza kazi ya kuadibu na hukumu, na kazi hii imemleta mwanadamu katika ulimwengu wa juu zaidi. Wote wanaonyenyekea chini ya utawala Wake watapata kufurahia ukweli wa juu na kupata baraka nyingi mno. Wataishi katika mwanga kwa kweli, na watapata ukweli, njia na uzima(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Dibaji). “Kupitia kwa sadaka ya dhambi, mwanadamu amesamehewa dhambi zake, kwani kazi ya kusulubisha imefika mwisho na Mungu Ametawala juu ya Shetani. Lakini tabia potovu ya wanadamu bado imebaki ndani yao na mwanadamu anaweza kutenda dhambi na kumpinga Mungu; Mungu hajampata mwanadamu. Hiyo ndio sababu katika hatua hii ya kazi Mungu Anatumia neno kutangaza tabia potovu ya mwanadamu na kumuuliza mwanadamu kutenda kulingana na njia sahihi. Hatua hii ni ya maana zaidi kuliko zile za awali na pia yenye mafanikio zaidi, kwani wakati huu ni neno ambalo linatoa maisha moja kwa moja kwa mwanadamu na linawezesha tabia ya mwanadamu kubadilishwa kabisa; ni hatua ya kazi ya uhakika kabisa. Kwa hivyo, Mungu kupata mwili katika siku za mwisho imekamilisha umuhimu wa Mungu kupata mwili wa Mungu na kukamilisha usimamizi wa Mungu katika mpango wa kuokoa mwanadamu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Fumbo la Kupata Mwili (4)). Kutoka kwa maneno ya Mungu, tunaweza kuona kwamba Kazi ya ukombozi ya Bwana Yesu iliweka msingi wa kazi ya wokovu ya Mungu katika siku za mwisho na kazi ya hukumu katika siku za mwisho ndiyo kiini, kitovu, cha kazi ya wokovu ya Mungu. Ndiyo kipaumbele, sehemu muhimu zaidi ya wokovu wa wanadamu. Kwa kupitia kazi ya Mungu katika Enzi ya Neema, tunasamehewa dhambi zetu, lakini hatuwezi kuwekwa huru kutokana nazo, wala hatuwezi kupata utakaso. Kazi ya Mungu ya hukumu pekee katika siku za mwisho ndiyo inayoweza kushughulikia umuhimu unaohitajika kwa wanadamu, kuwaruhusu kumjua Mungu kwa kweli, kubadilisha tabia zao za maisha kutii na kumwabudu Mungu, na kuwa mwenye kuupendeza moyo wa Mungu. Hivyo ndivyo Mungu ataukamilisha mpango Wake wa usimamizi ili kuwaokoa wanadamu.

Kimetoholewa kutoka katika Maswali na Majibu Bora zaidi Kuhusu Injili ya Ufalme

Kama binadamu wataikubali kazi ya ukombozi pekee ya Bwana Yesu katika Enzi ya Neema, lakini wasikubali kazi ya hukumu na kuadibu ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho, hawataweza kujiweka huru kutokana na dhambi, kutenda mapenzi ya Baba wa mbinguni, na kuingia katika ufalme wa Mungu. Hali hii haina shaka yoyote! Hii ni kwa sababu wakati wa Enzi ya Neema, Bwana Yesu alifanya kazi Yake ya ukombozi. Kwa sababu ya kimo cha watu wakati huo, Bwana Yesu aliwapa njia ya kutubu pekee, na akawaomba watu kufahamu ukweli na njia chache muhimu za kuutenda. Kwa mfano: Aliwaambia watu kukiri dhambi zao na kutubu na kuubeba msalaba. Aliwafunza kuhusu unyenyekevu, ustahimilivu, upendo, kufunga, ubatizo, n.k. Huu ni ukweli mchache sana na finyu ambao watu wa wakati huo waliweza kufahamu na kufikia. Bwana Yesu hakuwahi kuonyesha ukweli mwingine wa kina ambao unahusu kubadilisha tabia ya maisha, kuokolewa, kutakaswa, kufanywa kuwa mtimilifu, n.k., kwa sababu wakati huo, watu walikosa kimo kinachohitajika kushuhudia ukweli huo. Lazima binadamu asubiri mpaka Bwana Yesu arudi kuifanya kazi Yake katika siku za mwisho. Atawapatia wanadamu wapotovu ukweli wote wanaohitaji ili kuokolewa na kufanywa kuwa watimilifu kulingana na mpango wa usimamizi wa Mungu wa kuwaokoa wanadamu na mahitaji ya wanadamu wapotovu. Ni kama tu vile Bwana Yesu alivyosema, “Bado ningali nayo mengi ya kuwaambieni, lakini hivi sasa hamwezi kuyavumilia. Hata hivyo, wakati yeye, Roho wa ukweli, atakapokuja, atawaongoza hadi kwenye ukweli wote: kwa maana hatazungumza juu yake mwenyewe; bali chochote atakachosikia, atakinena: na atawaonyesha mambo yajayo(Yohana 16:12-13). Maneno ya Bwana Yesu yako wazi sana. Wakati wa Enzi ya Neema, Bwana Yesu hakuwahi kuwapatia wanadamu wapotovu ukweli wote waliouhitaji ili kuokolewa. Kunao bado ukweli mwingi zaidi wa kina, na wa juu zaidi, yaani, kunao ukweli mwingi ambao Bwana Yesu hakuwaambia wanadamu ambao utawaruhusu watu kuwekwa huru kutokana na tabia zao potovu za kishetani na kufikia utakaso, pamoja na ukweli ambao binadamu wanahitaji ili kutii na kumjua Mungu, Hivyo basi, katika siku za mwisho, Mwenyezi Mungu anauonyesha ukweli wote unaohitajika kuwaokoa wanadamu. Anautumia ukweli huu kuhukumu, kuadibu, na kuwafanya kuwa watimilifu wote wanaoukubali wokovu wa Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho. Mwishowe, watu hawa watafanywa kuwa watimilifu na kuwa katika ufalme wa Mungu. Hivi ndivyo mpango wa usimamizi wa Mungu wa kuwaokoa wanadamu utakamilishwa. Kama watu wataikubali kazi ya ukombozi ya Bwana Yesu pekee, lakini hawaikubali kazi ya hukumu ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho, hawatawahi kuweza kupata ukweli na kubadilisha tabia zao. Hawatawahi kuwa wale wanaotenda mapenzi ya Mungu na bila shaka hawatawahi kustahili kuingia katika ufalme wa Mungu.

Watu wa siku za mwisho wamepotoshwa sana na Shetani; wamejaa sumu ya Shetani. Mitazamo yao, kanuni za kuishi, namna ya kuangalia maisha, maadili, n.k. yote inaenda kinyume na ukweli na vinampinga Mungu. Watu wote wanaabudu maovu na wamekuwa adui wa Mungu. Kama binadamu aliyejaa tabia potovu ya kishetani, hapitii hukumu na kuadibu kwa Mwenyezi Mungu pamoja na uteketezaji na utakaso wa maneno, atawezaje kuasi dhidi ya Shetani na kujiondoa katika ushawishi wake? Watawezaje kumcha Mungu, na kuepuka maovu, na kuyafanya mapenzi ya Mungu? Tunaweza kuona kwamba watu wengi wamemwamini Bwana Yesu kwa miaka, lakini licha ya wao kushuhudia kwa shauku kubwa kwamba Bwana Yesu ni Mwokozi na kutia bidii kwa miaka mingi, kushindwa kwao kuijua tabia ya haki ya Mungu na kumcha Mungu bado kunawafanya kuhukumu na kushutumu kazi ya Mungu na kutokubali na kukataa kurudi kwa Mungu wakati Mwenyezi Mungu anapotekeleza kazi Yake katika siku za mwisho. Hata wanamsulubisha tena Yesu Kristo msalabani wakati Anaporudi katika siku za mwisho. Hili linatosha kuonyesha kwamba kama binadamu hawaikubali kazi ya hukumu na kuadibu kwa Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho, chanzo cha dhambi za binadamu na asili ya kishetani hakitawahi kutatuliwa. Upinzani wao kwa Mungu utawafanya kuangamia. Huu ni ukweli ambao hakuna anayeweza kuukataa! Miongoni mwa waumini, wale wanaokubali kwa uaminifu hukumu na kuadibu kwa Mungu pekee katika siku za mwisho ndio watakaopata ukweli kama maisha, watakuwa wale wanaotenda mapenzi ya Baba wa mbinguni na kuwa wale ambao wanamjua Mungu na wanalingana na Yeye, Wao ndio watakaostahili kushiriki ahadi za Mungu na kupelekwa katika ufalme Wake.

Kimetoholewa kutoka katika Maswali na Majibu Bora zaidi Kuhusu Injili ya Ufalme

Je, utakaso huu ambao watu wa dini huzungumzia, na utakaso ambao Mungu hudai ni kitu sawa? Si sawa, kwa hivyo utakaso ambao mwanadamu anazungumzia si utakaso wa kweli. Iwapo katika kumwamini Yesu kwa kweli wewe unatakaswa, Mungu bado anahitaji kufanya kazi ya siku za mwisho? Hujamwamini Yesu kwa miaka kadhaa, lakini unasema kwamba umebadilika na kwamba unaweza kutakaswa ukizidi kufuatilia njia hii; basi angalia wahubiri wote wanaomwamini Yesu, Wakristo ambao wamemwamini Mungu maisha yao yote, wao ni wametakaswa? Ni yupi kati yao ametakaswa? Nani kati yao anathubutu kusema kwamba, baada ya kumwamini Mungu maisha yake yote, yeye ametakaswa, na ameokolewa kikamilifu? Hutapata mtu mmoja kama huyu. Wamemwamini Mungu maisha yao yote na bado hawathubutu kusema kwamba wao wametakaswa. Je, inaleta maana kusema kwamba utafikia utakaso kwa kutenda imani kwa njia hii? Iwapo mwana wa kiume ama binti angesema “Nimekuwa kwa jamii kwa miaka kadhaa na nimebaini jamii,” je hii haingekuwa ujinga? Unaweza kumwuliza baba ama mama yako na wale walio wazee zaidi kukuliko, je, wamebaini jamii? Iwapo hakuna kati yao ambaye amebaini jamii, je, unaweza kuibaini? Kwa hivyo, mwanadamu haelewi ukweli, na hajui utakaso wa kweli ni nini. Anaamini kwamba anatenda vyema katika njia kadhaa chache, ana imani katika Mungu na hajihusishi katika mapigano, haibi vitu, hawatukani watu, hanywi pombe na hivyo yeye ametakaswa. Hii haiwakilishi utakaso. Je utakaso wa kweli unahusu nini? Huu pia unahusisha ukweli. Utakaso wa kweli unahusu kuwa huru dhidi ya sumu za Shetani. Mantiki ya kishetani katika mioyo ya wanadamu, falsafa ya Shetani, aina zote za uwongo wa Shetani, sheria za Shetani kwa maisha ya mwanadamu, mtazamo wa maisha na maadili ya maisha ambayo ni ya Shetani, je hizi si sumu za Shetani? Nini hutawala kutenda dhambi kwa mwanadamu na upinzani kwa Mungu? Ni sumu za Shetani ndani ya mwanadamu zinazosababisha mwanadamu kutenda dhambi, zinazomwongoza mwanadamu kuhukumu, kuelewa vibaya, na kuasi. Chanzo cha kutenda dhambi kwa mwanadamu ni asili ya Shetani iliyoko ndani ya mwanadamu. Vitu vyote ambavyo ni vya Shetani machoni pa Mungu ni vichafu, viovu, na kwa hivyo mwanadamu ambaye ana aina zote za sumu za Shetani ndani yake amekuwa mpotovu mchafu na mwovu. Sumu hizi ambazo ni za Shetani zimekita mizizi ndani ya mwanadamu, kuchanua, na kuzaa matunda, na mwanadamu amekuwa mwanadamu mpotovu, mwanadamu mchafu, mwanadamu mwovu. Ni ukweli, kwa hivyo, kwamba mwanadamu humpinga Mungu na ni adui wa Mungu. Kulingana na ukweli huu, tunaona shida gani ambayo mwanadamu lazima atatue ili kufikia utakaso wa kweli? Anahitaji kutatua sumu za Shetani, kutatua mtazamo wa Shetani wa maisha na maadili ya maisha, mantiki ya Shetani, sheria za Shetani, aina zote za uwongo wa Shetani. Vitu hivi vikiondolewa kikamilifu kutoka kwa mioyo ya wanadamu, huku ni kutakaswa kwa kweli. Vitu hivi visipoondolewa kutoka kwa mioyo ya wanadamu, mwanadamu bado ataweza kumpinga Mungu, kumhukumu Mungu, kuwa adui wa Mungu, na kumsaliti Mungu. Kwa hivyo, wanadamu wanaweza tu kufikiriwa kuwa wametakaswa kweli wakati vitu vya Shetani vimeondolewa, na kutatuliwa. Haya, kwa kumwamini Yesu inawezekana kutatua sumu za Shetani? Je, imani katika Yesu inaweza kubadili mtazamo wa mwanadamu wa maisha na maadili ya maisha? Inaweza kumwongoza mwanadamu kumtii Mungu kwa kweli na kutompinga Mungu? Inaweza kumwongoza mwanadamu kumjua Mungu kwa kweli, kumwabudu Mungu? Kwa kumwamini Yesu umefanya dhambi zako zisamehewe karibuni; kufikia utatuzi wa kweli wa upotovu wa mwanadamu na kutakaswa, mwanadamu anahitaji Mungu kutekeleza kazi Yake ya hukumu na kuadibu katika siku za mwisho. Bila kazi ya siku za mwisho, wanadamu wapotovu hawawezi kupata utakaso. Utakaso haupatikani tu kupitia kusamehewa dhambi, lakini utakaso wa kweli unapatikana kupitia kumwondolea mwanadamu tabia potovu kupitia hukumu na kuadibu. Wakati tabia potovu ya mwanadamu imetatuliwa, hampingi Mungu tena, anaweza kumtii Mungu, anaweza kumpenda Mungu katika moyo wake, na anaweza kupenda ukweli; ni mwanadamu wa aina hii tu ndiye mwanadamu aliyetakaswa. Wengine wanakosa kuelewa kinachoitwa utakaso, wakiamini kwamba kutakaswa ni kutoiba, kutopora, kutovunja, kwamba kutakaswa ni kutowapiga wengine na kutowatusi wengine. Je hili ni sahihi? Hili si sahihi hata kidogo na wanaangalia tu shida kutoka kwa mwonekano wake wa nje. Kwa sababu watu wa dini hawana ukweli, wote wanafikiri hivi. Wana maoni rahisi sana kuhusu vitu, hawaoni chanzo, hawaoni dutu; hivyo, si ajabu sana kwamba watu hawa wangeweza kufikiri kwa njia hii.

Kimetoholewa kutoka katika Ushirika kutoka kwa Aliye Juu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp