Wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa wana elimu dhabiti ya Biblia, kuieleza Biblia kinaganaga mara kwa mara kwa watu wakiwafanya washikilie Biblia, kwa hiyo kuieleza Biblia kinaganaga na kuiinua kwa kweli ni kumshuhudia na kumtukuza Bwana? Kwa nini inasemwa kwamba wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa ni Mafarisayo wa uongo? Bado hatuwezi kulielewa jambo hili, kwa hiyo unaweza kutujibu hili tafadhali?

09/06/2019

Jibu:

Kwa watu, kueleza Biblia hakupaswi kuwa makosa, lakini wakati huo huo kama kueleza Biblia, kile wanachofanya hasa ni vitendo ambavyo vinavyopinga Mungu. Hawa ni watu wa aina gani? Je, si Mafarisayo wanafiki? Je, si wao ni wapinga Kristo wanaompinga Mungu? Kueleza Biblia ni kumpinga Mungu vipi? Kwa nini ni kumhukumu Mungu? Hata kuwasiliana kwa njia hii bado kuna watu ambao hawaelewi na bado wanadhani kuwa kuieleza Biblia ni kumwinua na kumshuhudia Mungu. Makuhani wakuu wa Kiyahudi, waandishi na Mafarisayo wakati huo wote walikuwa wasomi wa maandiko na wataalamu ambao mara nyingi walieleza maandiko kwa watu. Kama kueleza Biblia ni kumwinua na kumshuhudia Mungu, basi kwa nini wakati Bwana Yesu alikuja kuhubiri na kufanya kazi, wao badala yake walimpinga kwa hasira na kumhukumu Bwana Yesu, na hatimaye walishikamana na serikali kumpiga Bwana Yesu msumari msalabani? Wachungaji na wazee wa kidini wa kisasa wote ni watu ambao wanaifahamu Biblia na wameieleza Biblia kwa miaka mingi. Kama kuieleza Biblia ni kumwinua na kumshuhudia Mungu, basi kwa nini ni kwamba Mwenyezi Mungu alipokuja kuonyesha ukweli na kufanya kazi Yake ya hukumu, wao hawakushindwa tu kutafuta na kuchunguza, lakini badala yake walipinga na kuhukumu? Tatizo ni nini hapa? Je, hili si tatizo kubwa ambalo waumini wote wanapaswa kulitafakari? Zaidi ya hayo, kama viongozi wa kidini kueleza Biblia ni sawa na kumwinua na kumshuhudia Mungu, basi katika Enzi ya Neema, kwa nini Bwana Yesu hakufanya kazi hekaluni Alipokuja? Kwa nini Mwenyezi Mungu wa siku za mwisho hafanyi kazi kanisani Alipokuja? Ni kwa sababu viongozi wa dini hawamwinui na kuwa na ushuhuda kwa Mungu hata kidogo na wote ni Mafarisayo wanafiki, wenye kiburi. Wao ni wapinga Kristo ambao hudhibiti dini na kumpinga Mungu! Je, wanawezaje kumruhusu Mungu awepo au kuruhusu ulimwengu wa dini kuwa na sauti zilizo na ushuhuda kwa Mungu? Kama Kristo mwenye mwili alikuja katika dini kufanya kazi na kuhubiri kanisani, basi bila shaka Angekamatwa na kupelekwa kwa chama tawala na kusulubiwa. Kama watu wangeenda kwa makanisa ya kidini ili kumshuhudia Mungu, basi bila shaka wangekamatwa na kuteswa. Kama Bwana Yesu alivyosema, “Tazameni, Nawatuma ninyi kama kondoo katikati ya mbwa mwitu(Mathayo 10:16). Je, watu bado hawawezi kuona ukweli huu? Kulingana na ukweli wa Mafarisayo wa dini kupinga na kumshutumu Mungu, tunapaswa kuwa na uwezo wa kuona wazi kama kuinua Biblia kunamshuhudia Mungu. Je, watu wanaomwinua na kumshuhudia Mungu kwa kweli humpinga Mungu? Je, wanaweza kumwona Mungu kuwa adui wao? Zaidi ya hayo, tunapaswa sote kujua kwamba Biblia haina maneno ya Mungu tu bali pia ina maneno mengi ya mwanadamu. Kwa hiyo, kuinua Biblia na kuinua Mungu sio kitu kimoja. Kutetea Biblia na kutetea amri za Bwana sio kitu kimoja. Wakati Mafarisayo wa kidini wanaeleza Biblia, wanazingatia tu kueleza maneno ya mwanadamu katika Biblia, wakieleza ujuzi wa Biblia na nadharia ya kiteolojia, na kuhubiri na kushuhudia maneno ya mwanadamu, lakini hawazingatii kueneza na kushuhudia maneno ya Mungu na ukweli ulioonyeshwa na Mungu katika Biblia. Je, Huku bado kunaweza kusemwa kuwa kuinua na kuwa na ushahidi kwa Mungu? Je, huku si kumpinga na kumdharau Mungu? Kwa hiyo, wote wanaofikiri kueleza Biblia ni kumwinua na kumshuhudia Mungu hawaelewi mambo ya kiroho na hawawezi kung'amua kiini cha tatizo. Wote ni watu waliochanganyikiwa, watu wanaoabudu na kuamini bila kutambua na kufuata viongozi wa kidini. Je, huu sio ukweli?

Hapo zamani, Mafarisayo hao wa Kiyahudi walilenga tu kueleza maarifa ya Biblia na mafundisho, pamoja na kushiriki katika mila za kidini na kufuata sheria za kidini na mila ya wanadamu, lakini badala yake waliziacha amri za Mungu na kuiacha njia ya Mungu, kwamba Bwana Yesu alipofika, walipinga kwa fujo, wakamshutumu Bwana Yesu na kumsulubisha msalabani. Matokeo yake, walilaaniwa na kuadhibiwa na Mungu. Ingawa wachungaji wa dini wa leo na wazee mara nyingi huieleza Biblia na kuishuhudia Biblia kwa watu, hawatilii maanani kueneza na kushuhudia neno la Mungu, au kuwa makini kuhubiri mapenzi ya Bwana Yesu na mahitaji Yake kwa mwanadamu, na pia mara chache kushuhudia kiini kitakatifu cha Bwana Yesu na uzuri. Hawawaongozi watu kutenda na kupitia neno la Bwana, aidha, hawatilii maanani jinsi ya kuzingatia amri za Bwana na kufuata mapenzi ya Mungu. Wanalenga tu kueleza na kuinua maneno ya mwanadamu katika Biblia, kuwaambia wengine wayachukulie maneno ya mwanadamu katika Biblia kama maneno ya Mungu na kama ukweli wa kutenda na kuyashikilia. Wanapotatua shida pia hutegemea maneno ya mwanadamu katika Biblia badala ya maneno ya Mungu katika Biblia. Wanatumia maneno ya mwanadamu katika Biblia kukataa na kupinga maneno ya Mungu. Katika suala la kuingia katika ufalme wa mbinguni, kwa mfano, Bwana Yesu aliwaambia watu waziwazi: “Siye kila mmoja ambaye aliniambia, Bwana, Bwana, ataingia ufalme wa mbinguni, ila yeye atendaye mapenzi ya Baba yangu ambaye yuko mbinguni(Mathayo 7:21) Lakini wachungaji na wazee badala yake waliweka kando maneno ya Bwana Yesu na kuyachukulia maneno ya mwanadamu katika Biblia kama ukweli na kama kiwango cha kuingia kwa mwanadamu katika ufalme wa mbinguni, kuwafundisha watu kwamba wanahitaji tu kujitahidi na kumfanyia Bwana kazi ili kuingia katika ufalme wa mbinguni. Wanatumia maneno ya mwanadamu kuchukua nafasi ya maneno ya Mungu na kukataa maneno ya Mungu, na matokeo yake wanawapotosha watu. Hii ndiyo hali ya uongo zaidi, na ya uovu zaidi ya upinzani wa wachungaji na wazee wa kidini kwa Mungu! Wao hutafsiri Biblia nje ya muktadha, wakitumia maneno ya mwanadamu katika Biblia kupinga na kumhukumu Mwenyezi Mungu, na kufanya kila kitu ili kudanganya, kufunga, na kuwadhibiti waumini, na kuwazuia kuchunguza na kukubali kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho, kuwaweka wote imara chini ya udhibiti wao wenyewe. Ni kama Mwenyezi Mungu anavyosema, “Tazama tu viongozi wa kila madhehebu—wote ni wa kujigamba na kujidai, na wanafafanua Biblia nje ya muktadha na kulingana na ubunifu wao wenyewe. Wote wanategemea zawadi na maarifa kufanya kazi yao. Kama hawangekuwa na uwezo wa kuhubiri chochote, wale watu wangewafuata? Wao, hata hivyo, wanamiliki ufahamu fulani, na wanaweza kuhubiri kuhusu mafundisho fulani, au wanajua jinsi ya kuwashawishi wengine na jinsi ya kutumia ustadi kadhaa. Wanatumia haya kuwaleta watu mbele yao wenyewe na kuwadanganya. Kwa jina, watu hao humwamini Mungu, lakini katika uhalisi wanafuata viongozi wao. Wakikutana na mtu akihubiri njia ya kweli, baadhi yao husema, ‘Lazima tutafute ushauri kwa kiongozi wetu imani.’ Imani yao lazima impitie mwanadamu; hilo si tatizo? Viongozi hao wamekuwa nini, basi? Hawajakuwa Mafarisayo, wachungaji waongo, wapinga Kristo, na vikwazo kwa kukubali kwa watu njia ya kweli?(“Ukimbizaji wa Ukweli Tu Ndiyo Imani ya Kweli katika Mungu” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). Kulingana na ukweli huu, tunawezaje kusema kwamba wachungaji wa kidini na wazee kueleza Biblia ni kumwinua na kutoa ushahidi kwa Mungu? Je, hawatumii fursa ya kueleza Biblia kueleza Biblia visivyo na kufanya mambo nje ya muktadha kumpinga Mungu? Kwa muda mrefu wamekuwa vizuizi na vikwazo kwa watu kukubali njia ya kweli na kurudi kwa Mungu, na ni hasa wapinga Kristo waliowekwa wazi na kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho. Je, watu bado hawawezi kuona ukweli huu wazi?

Kulingana na mawazo ya watu, kueleza Biblia ni sawa na kumwinua na kumshuhudia Mungu, lakini kutoka kwa Mafarisayo na viongozi wa dini kueleza Biblia, tunaweza kuona kwamba hali sio hivi kwa kweli. Kile ambacho Mafarisayo wa dini wanainua na kushuhudia ni Biblia na sio Mungu. Mahubiri yao kimsingi ni kueleza maneno ya mwanadamu katika Biblia na si maneno ya Mungu. Wanatumia maneno ya mwanadamu katika Biblia kuchukua nafasi ya Mungu na kupinga maneno ya Mungu, na kuyachukua maneno ya mwanadamu katika Biblia nje ya muktadha ili kupinga na kufanya mahitimisho juu ya Mungu. Kusudi la kueleza kwao Biblia sio kuinua na kutoa ushuhuda kwa Mungu, lakini kudanganya na kuwadhibiti watu na kufikia madhumuni yao ya kudharauliwa. Kufafanua Biblia vile ni kumpinga Mungu na kufanya uovu! Ndiyo sababu, Mungu anakapokuja kufanya kazi, wanatumia Biblia ili kuwashika watu kuwafanya waamini bila kufikiria katika Biblia na kushikilia Biblia, kuwachukua wote kwenye njia ya kumpinga Mungu. Hii inaonyesha kwamba kueleza Biblia kwa viongozi wa kidini na Mafarisayo ni njia ya kupinga Mungu. Wao wanayatoa kabisa maneno ya mwanadamu katika Biblia nje ya muktadha ili kupinga na kumkataa Mungu, kuanzisha utawala wao wenyewe wa kujitegemea. Kisha mtu anawezaje kueleza Biblia kuwa ya kumwinua na kumshuhudia Mungu? Kile ambacho Biblia inarekodi ni kazi ya Mungu na ushuhuda wa Mungu. Kuieleza Biblia kunamaanisha kuinua na kushuhudia Mungu kwa mujibu wa maneno ya Mungu katika Biblia na ukweli katika Biblia. Ni kueneza na kushuhudia maneno ya Mungu katika Biblia. Ni kuwasiliana nia za Mungu kwa mujibu wa mahitaji ya Mungu na kulingana na maneno ya Mungu na kuwasilisha ukweli katika maneno ya Mungu. Ni kuwaletea watu ushuhuda wa kazi ya Mungu na tabia Yake, na kushuhudia kiini cha Mungu na uzuri Wake. Ni kuwaongoza watu kutenda na kupitia maneno ya Mungu, hivyo kuwawezesha kufanikisha kuingia katika ukweli wa maneno ya Mungu. Ni kumtukuza Bwana Yesu na kuwa na ushuhuda Kwake katika kila kitu. Ni kwa kueleza Biblia kwa njia hizo tu ndio mtu atakuwa anamwinua na kuwa na ushuhuda kwa Mungu, kuupendeza moyo wa Mungu, na kumtumikia Mungu kwa kweli. Maneno ya mwanadamu katika Biblia yanaweza kutumika tu kama kumbukumbu na nyongeza, na hayawezi kamwe kulinganishwa na maneno ya Mungu. Hata hivyo wachungaji wa kidini na wazee wanajali tu kuhusu kueleza maneno ya mwanadamu katika Biblia. Wanayachukua maneno ya mwanadamu katika Biblia kama maneno ya Mungu, kama ukweli, kuyatumia kama mwongozo wa tabia zao na mienendo yao, kama msingi wa njia ambayo wao hushughulikia matatizo. Lakini mara chache hutaja maneno ya Mungu, na hutumia maneno ya mwanadamu katika Biblia kuchukua nafasi ya maneno ya Mungu na kuyaacha maneno ya Mungu nyuma. Je, kueleza Biblia namna hiyo ni kumshuhudia Mungu? Je, si huku tu ni kumwinua na kumtolea mwanadamu ushahidi? Zaidi ya hayo, wanapoeleza Biblia wanalenga tu kueleza nadharia za kiteolojia, kueleza wahusika, maeneo, na asili za kihistoria katika Biblia ili kujionyesha. Huku sio tu kuwadanganya na kuwatega watu? Huku sio kufanya watu wawaabudu na kuwafuata wao? Hapo zamani, hao Mafarisayo wanafiki walitumia fursa yao ya kueleza Biblia kwa kueleza Biblia vibaya ili kuwadanganya na kuwadhibiti watu, na hatimaye waliwachukua waumini kwenye njia ya kumfuata mwanadamu na kumpinga Mungu, na kugeuza Uyahudi kuwa ufalme wa kujitegemea wa kumpinga Mungu. Katika siku za mwisho, wachungaji wa kidini na wazee pia wanachukua fursa ya kueleza Biblia ili kuwafanya watu waiamini na kuiabudu Biblia bila kufikiria, na wanatumia Biblia kuchukua nafasi ya Mungu katika mioyo ya watu, bila kujua wanawapeleka waumini katika njia ya kusaliti neno la Bwana na kumpinga Mungu, pia kugeuza ulimwengu wa kidini kuwa ufalme wa kujitegemea wa kumpinga Mungu, msingi thabiti wa upinzani dhidi ya kazi ya Mungu. Je, si kueleza Biblia kama wanavyofanya kupinga na kumkufuru Mungu? Je, huu sio udanganyifu wa Mafarisayo wapinga Kristo katika kupinga Mungu na kuanzisha ufalme wao wenyewe wa kujitegemea? Inawezaje kusemwa kuwa ni kumwinua na kumtolea Mungu ushuhuda? Ujanja wa Mafarisayo wa kidini katika kumpinga Mungu uko katika kutumia fursa yao kuieleza Biblia kwa kuitafsiri Biblia vibaya ili kudanganya na kuwadhibiti watu. Biblia ilikuwa awali ushuhuda wa Mungu. Kulingana na mawazo ya mwanadamu, daima wanatoa ushahuda kwa Mungu bila kujali jinsi wanavyoeleza Biblia, lakini Mafarisayo wanafiki wanafaidika na dhana hii ya mwanadamu, kufanya wawezavyo katika kuinua na kushuhudia Biblia. Wanaitumia Biblia kuchua nafasi ya Mungu na kumpinga Mungu na kuwadanganya watu. Hii huwafanya watu wote kuamini bila kufikiria na kuabudu Biblia, na huwafanya watu waabudu na kufuata wasomi wa Biblia kama wao na hivyo kumsaliti Mungu. Huu ndio uongo, udanganyifu zaidi wa Shetani wa kumpinga Mungu na kuwadanganya watu, na kipengele ambacho ni vigumu sana kwa watu kuona na rahisi kwao kudanganywa nacho.

Hebu tuangalie maneno ya Mwenyezi Mungu: “Wale wanaosoma Biblia katika makanisa makubwa hukariri Biblia kila siku, lakini hakuna yeyote anayeelewa madhumuni ya kazi ya Mungu. Hakuna hata mmoja anayeweza kumwelewa Mungu; juu ya hayo, hakuna yeyote anayekubaliana na moyo wa Mungu. Wote hawana thamani, wanadamu waovu, kila mmoja akisimama juu kufundisha kuhusu Mungu. Ingawa wanalionyesha hadharani jina la Mungu, wanampinga kwa hiari. Ingawa wanajiita waumini wa Mungu, wao ni wale wanaokula mwili na kunywa damu ya mwanadamu. Wanadamu wote kama hao ni mashetani wanaoteketeza nafsi ya mwanadamu, pepo wakuu wanaowasumbua kimakusudi wanaojaribu kutembea katika njia iliyo sawa, na vizuizi vinavyozuia njia ya wanaomtafuta Mungu. Inagawa wao ni wenye ‘mwili imara,’ wafuasi wao watajuaje kwamba wao ni wapinga Kristo wanaomwongoza mwanadamu katika upinzani kwa Mungu? Watajuaje kwamba hao ni mashetani hai wanaotafuta hasa nafsi za kuteketeza?(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Watu Wote Wasiomjua Mungu Ni Watu Wanaompinga Mungu). “Kama umemwamini Mungu kwa miaka mingi, lakini hujawahi kumtii ama kuyakubali maneno Yake, na badala yake umemwuliza Mungu anyenyekee kwako na kufuata dhana zako, basi wewe ni mtu mwasi zaidi ya wote, na wewe si muumini. Mtu kama huyu anawezaje kutii kazi na maneno ya Mungu ambayo hayafuati fikira za mwanadamu? Mtu mwasi zaidi ni yule anayemkataa na kumpinga Mungu makusudi. Yeye ni adui wa Mungu na ni mpinga Kristo. Mtu kama huyu daima anakuwa na mtazamo wa kikatili kwa kazi mpya ya Mungu, hajawahi kuonyesha nia hata ndogo ya kutii, na hajawahi kuonyesha utii ama kujinyenyekeza kwa furaha. Anajisifu mbele ya wengine na kamwe haonyeshi utii kwa mwingine. Mbele ya Mungu, anajiona kuwa hodari zaidi katika kuhubiri neno na mwenye ujuzi zaidi katika kufanya kazi kwa wengine. Kamwe hatupi ‘hazina’ anazomiliki tayari, lakini anazichukua kama vitu vinavyorithiwa kwa familia vya kuabudiwa, vya kuhubiri kuhusu wengine, na huvitumia kuhutubia wale wapumbavu wanaomwabudu. Hakika kuna baadhi ya watu kama hawa kanisani. Inaweza kusemwa kwamba wao ni ‘mashujaa wasioshindwa,’ kizazi baada ya kizazi kinachokaa kwa muda mfupi ndani ya nyumba ya Mungu. Wanachukua kuhubiri neno (mafundisho ya dini) kama wajibu wao wa juu zaidi. Mwaka baada ya mwaka na kizazi baada ya kizazi, wao huenenda kwa nguvu wakitekeleza wajibu wao ‘mtakatifu na usiokiukwa’. Hakuna anayethubutu kuwaguza na hakuna mtu hata mmoja anayethubutu kuwashutumu kwa uwazi. Wanakuwa ‘wafalme’ katika nyumba ya Mungu, wakienea kote wakiwaonea wengine kutoka enzi hadi enzi. Hili kundi la mapepo linataka kuungana mikono na kuharibu kazi Yangu; Nawezaje kuwaruhusu ibilisi hawa waishio kuwepo mbele Yangu?(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Wale Wanaomtii Mungu kwa Moyo wa Kweli Hakika Watapatwa na Mungu). Kwa kweli, ingawa wachungaji wa kidini na wazee mara nyingi hueleza Biblia, wao si watu ambao wanaelewa ukweli na kumjua Mungu. Wao hasa ni Mafarisayo wanafiki. Wao ni wachungaji wa uongo na wafanyakazi ambao hudanganya, kudhibiti, kuwafunga na kuwadhuru watu. Wanaongoza watu kumkana Kristo, kumhukumu Kristo, kwa kiwango cha hata kupinga na kumuasi Mungu, kuwafanya wote kuwa washirika wa Shetani na vikaragosi. Mtu yeyote mwenye macho anaweza kuona kwamba hii ndiyo hali.

Kimetoholewa kutoka katika Maswali na Majibu Bora zaidi Kuhusu Injili ya Ufalme

Kwa kuwa wachungaji na wazee wakanisa daima hufafanua na kushuhudia kuhusu maneno ya watu kutoka kwenye Biblia na kuwaomba wafuasi wao kuyafuata maneno haya? Wanawezaje kumtukuza Bwana au kutoa ushuhuda kwa Bwana na kufafanua Biblia kwa njia hii? Kweli kushuhudia Bwana na kutukuza Bwana si kuhusu jinsi watu hufafanua Biblia. Jambo la muhimu ni ikiwa tunaweza kutenda maneno ya Mungu, kupitia kazi Yake, na kupata maarifa ya kweli kumhusu Mungu au la. Watu wakipenda ukweli, wao watapata nuru ya Roho Mtakatifu na uzoefu wa kweli na ufahamu wa neno la Mungu. Maarifa haya yanaanzishwa na kutenda na kupitia maneno ya Mungu. Ni maana ya kweli ya kumjua Mungu. Kuwasiliana kuhusu huu uzoefu halisi na ushuhuda ndiyo maana kweli ya kumtukuza Mungu na kushuhudia Kwake! Maarifa ya kweli ya Mungu ambayo wale wamtukuzae na kushuhudia Kwake husema kuyahusu hayachimbuki kutoka kwa dhana, mawazo au mantiki yao wenyewe; bila shaka hayatokani na ufafanuzi wao halisi ya maneno ya Mungu au nadharia tupu za kiteolojia. Wale wanaotukuza na kuwa na ushuhuda kwa Mungu hulenga kuwasiliana maneno ya Mungu katika Biblia, kuwasiliana mapenzi ya Mungu, mahitaji Yake kwa watu, tabia Yake na chote Alicho na Anacho, wakiwaruhusu watu kuelewa mapenzi ya Mungu na tabia na kumjua Mungu kweli. Hivi ndivyo watu wanaweza kweli kumcha na kumtii Mungu. Aina hizi za ufafanuzi wa kibiblia na mawasiliano kuhusu maneno ya Mungu ni jinsi wanavyoweza kweli kumtukuza Mungu na kutoa ushuhuda kwa Mungu. Hata hivyo, wachungaji na wazee wa kanisa wanapofafanua Biblia, kweli wanaweza kuwasiliana kiini cha ukweli wa maneno ya Mungu? Wanaweza kuwasiliana mapenzi ya Mungu? Wanaweza kutoa ushuhuda kwa tabia ya Mungu? Wanaweza kufanya wengine kumjua, kumtii au kumcha Mungu? Ukweli umetuonyesha kwamba wengi wa wachungaji na wazee wa kanisa katika jumuiya ya dini huchukia ukweli na kumpinga Mungu; hiyo ni asili yao halisi. Hawatendi maneno ya Mungu au kupitia kazi Yake. Hawaelewi mapenzi au matakwa Yake kamwe, na hakika hawaelewi tabia Yake yote, Alicho na Anacho. Kwa hivyo, hawawezi kuwasiliana maarifa yoyote ya kweli ya Mungu, na hawawezi kutoa ushuhuda kwa asili tukufu ya Bwana Yesu au sifa zinazopendeka. Wao hufafanua tu maarifa ya kibiblia na nadharia ya kiteolojia au hadithi ya wahusika fulani katika Biblia, pamoja na usuli ya kihistoria ili kuwafanya watu kuwastahi na kuwaheshimu sana. Hawatukuzi au kutoa ushuhuda kwa Bwana asilani.

Si hayo tu, lakini mara nyingi wachungaji na wazee wa kanisa wanafafanua maneno ya mtu, kama maneno ya Paulo katika Biblia. Kulingana na Paulo, “Andiko lote limetolewa kwa msukumo wa Mungu” (2 Timotheo 3:16), wanachukulia maneno ya Biblia kama kwamba yalikuwa maneno ya Mungu. Hii imesababisha jumuiya nzima ya dini kuchukua maneno ya mitume kama maneno ya Mungu na kuwaambia waumini kuyatenda na kuyazingatia. Wananukuu maneno ya mitume mara nyingi zaidi na zaidi wanapotoa mahubiri, kuwasiliana au kushuhudia. Hata hivyo, wanayanukuu maneno ya Mungu na Bwana Yesu kwa uchache sana. Je, hili linaleta matokeo gani? Matokeo ya mwisho ni kwamba maneno ya Mungu na Bwana Yesu katika Bibilia yote yamebadilishwa na kubatilishwa. Nafasi ya Bwana Yesu katika mioyo ya watu daima inapungua, wakati nafasi ya Paulo na wengine katika mioyo yao inendelea kuongezeka. Hii imeruhusu maneno ya Paulo, pamoja na maneno ya mtu mwingine katika Biblia, kujaza mioyo ya watu. Watu wanaamini katika Bwana Yesu kwa jina, lakini katika hali halisi wanaendelea tu kulingana na maneno ya mtu katika Biblia, kama maneno ya Paulo. Tunasafiri kwenye njia yetu wenyewe ya imani katika Mungu, na maneno ya wanadamu, hasa maneno ya Paulo, yakichukua nafasi ya maneno ya Bwana Yesu. Watu ambao wanaamini katika Mungu kwa njia hii wanawezaje kukosa kupotea kwenye njia ya Bwana? Aina hii ya huduma inawezaje kulingana na mapenzi ya Mungu? Kwa mfano, Bwana Yesu alisema hapo kale haya kuhusu kuingia katika ufalme wa Mbinguni: “Ila yeye atendaye mapenzi ya Baba yangu ambaye yuko mbinguni(Mathayo 7:21). Hata hivyo, wachungaji na wazee wa kanisa huzungumzia wokovu na kuingia katika ufalme wa Mbinguni kulingana na maneno ya Paulo badala yake: “Nimepigana vita vizuri, nimeutimiza mwendo wangu, nimeihifadhi imani: Kutoka sasa kuendelea taji la haki limewekwa kwangu” (2 Timotheo 4:7-8). Wanatufundisha kwamba almradi wanafanya kazi kwa ajili ya Bwana kama alivyofanya Paulo na kuvumilia mateso, wao wanaweza kuingia katika ufalme wa mbinguni. Huu ni usaliti kamili wa maneno ya Bwana Yesu. Matokeo yake ni kwamba waumini wengi hawajui jinsi ya kufuata mapenzi ya Mungu. Wao hata hawana uhakika sana wa aina ya watu wanaoweza kuingia katika ufalme wa Mbinguni. Watu hutumia maneno ya Paulo kama kauli-mbiu yao. Wachungaji na wazee hubadalisha maneno ya watu na maneno ya Mungu; wao hutoa maneno ya Mungu. Matokeo yake ni kwamba wao huwapotosha watu. Wanapofafanua Biblia hivi, je, wanatusaidia kuelewa maneno ya Bwana? Je, wanamtukuza Mungu au kutoa ushuhuda kwa Mungu? Je, wanatuongoza kuingia katika uhalisi wa maneno ya Mungu? Nadhani wako katika upinzani wa moja kwa moja na Mungu! Tatizo hili ni kubwa sana! Wachungaji na wazee wa kanisa wa dini mara nyingi hubadilisha maneno ya watu katika Biblia na maneno ya Mungu. Sasa tunapaswa kuwa na hakika juu ya matokeo ya haya, siyo? Watu wengi wanawezaje kuamini katika Bwana kwa miaka mingi na bado wasimjue? Kwa nini kamwe hawapitii maneno ya Bwana kwa kweli? Jinsi gani wale ambao wanaamini katika Bwana kwa njia hii wanaweza kupata ukweli au uzima? Je, si ni kwa sababu wachungaji na wazee wakanisa daima hufafanua na kushuhudia kuhusu maneno ya watu kutoka kwenye Biblia na kuwaomba wafuasi wao kuyafuata maneno haya?

Kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho ilifunua hawa achungaji na wazee wa kanisa, pepo hawa wanaompinga Kristo katika jumuiya ya dini. Vinginevyo, hakuna yeyote ambaye angeweza kuona kwamba kutukuza kwao na ufafanuzi wao wa Biblia kweli ni njia zao za kudhuru za siri za kuwadanganya na kuwadhibiti watu, wala mtu yeyote hangeweza kuona ukweli: Wanaanzisha ufalme wao wenyewe, huru kama maadui wa Mungu. Sote tunajua, Wakati huo, Mafarisayo walitukuza na kutoa ushuhuda kwa Biblia; walimzuia Mungu ndani ya Biblia. Kamwe hawakutafuta ukweli au kutazamia kufuata nyayo za Mungu. Matokeo yake ni kwamba walisulubisha Bwana Yesu msalabani, wakitumia kukataa Kwake kufuata Agano la Kale kama sababu ya uhalali wao. Wachungaji na wazee wa kanisa katika siku za mwisho ni kama tu Mafarisayo walivyokuwa. Wao hutukuza na kushuhudia kwa Biblia; walimfafanua Mungu katika Biblia. Pia husambaza dhana za uwongo, wakisema, “Hakuna maneno ya Mungu na kazi zilizo nje ya Biblia” “Kuamini katika Biblia ni kuamini katika Mungu. Biblia inamwakilisha Mungu; ukiacha Biblia, huamini tena katika Mungu.” Wao hutumia misemo hii kuwapotosha watu kumwamini na kumwabudu Biblia. Wachungaji na wazee wa kansa wanatumia siri hii, mbinu za hila kuwaiba watu kutoka kwa Mungu, na kuwaleta mbele ya Biblia. Hii inawasababisha watu kupoteza uhusiano wao na Mungu bila kujua. Watu ambao wakati mmoja waliamini katika Mungu sasa wanaamini tu katika Biblia. Biblia inakuwa Bwana katika mioyo yao, Mungu mioyoni mwao. Nafasi ya Mungu katika mioyo ya waumini inapungua bila kujua, na kwa hivyo, imani yao ya kijinga na kuabudu kwa Biblia kunawasababisha kuabudu na kufuata wanazuoni wa kibiblia, wachungaji na wazee wa kanisa. Je, kutukuza na kushuhudia kwa Biblia kwa wachungaji na viongozi wa dini kuna tofauti yoyote na kule kwa makuhani wakuu, waandishi na Mafarisayo wa Kiyahudi? Hapana, hakuna kabisa. Wachungaji na wazee wa kanisa, hutumia Biblia kama chombo cha kudhibiti jumuiya ya dini na kufikia malengo yao wenyewe. Wao hutukuza Biblia na kuifafanua nje ya muktadha ili kuwadanganya, kushawishi na kudhibiti watu. Wao huwaongoza watu kwenye njia ya kuabudu watu, kuwafyata watu, kumpinga Mungu na kuwa adui wa Mungu akili mwao mlipofichika. Wao huwapotosha watu ili wafikirie kwamba kuabudu Biblia na kufuata Biblia ni kuamini katika Mungu, na kuwa na uwepo wa Mungu. Kwa hivyo, watu hawa hawatafuti au kuchunguza kazi ya Mungu katika siku za mwisho, na wanakosa nafasi yao ya mwisho katika wokovu. Hii kweli ni mpango wa kudhuru sirini na wa hila wa Shetani. Kwa hivyo, tunaweza kuona kwamba wachungaji na wazee wa kansia katika jumuiya ya dini ni kundi la Mafarisayo na matapeli halisi! Wao ni wachungaji wa uongo na wapinga Kristo ambao huwapotosha na kuwadhibiti wateule wa Mungu! Jumuiya ya dini inadhibitiwa na kundi la Mafarisayo na pepo wanaompinga Kristo ambao hupinga Mungu. Paliacha kuwa mahali ambapo Mungu angefanya kazi Yake muda mrefu uliopita. Imekuwa kambi ya kishetani ambayo inamchukulia Mungu kama adui yake. Ilikuwa mji mkuu wa Babeli kitambo! Je, Babeli ya dini inawezaje kutoangamia chini ya ghadhabu ya Mungu?

Kimetoholewa kutoka katika Maswali na Majibu Bora zaidi Kuhusu Injili ya Ufalme

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp