Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo Ambayo Kazi Yake Itafanikisha

Kwanza, hebu tuuimbe wimbo wa kumsifu Mungu: Wimbo wa Ufalme (I) Ufalme Unashuka Duniani.

Kiambata: Umati unanishangilia Mimi, umati wananisifu Mimi; vinywa vyote vinamtaja Mungu mmoja wa kweli. Ufalme unashuka juu ya ulimwengu wa wanadamu.

1 Umati unanishangilia, umati unanisifu; watu wote wanalitaja jina la Mungu mmoja wa kweli, watu wote wanayainua macho yao kuviangalia vitendo Vyangu. Ufalme unashuka duniani mwa wanadamu, nafsi Yangu ni ya fahari na yenye neema. Nani asingesherehekea kwa ajili ya hili? Ni nani asingecheza kwa furaha? Ee Sayuni! Inua bendera yako ya ushindi unisherehekee! Imba wimbo wako wa ushindi ili ulieneze jina Langu takatifu!

2 Viumbe wote duniani kote! Harakisheni kujitakasa ili muweze kufanywa kuwa sadaka Kwangu! Nyota juu mbinguni! Rudini kwenye maeneo yenu kwa haraka ili muonyeshe nguvu Yangu kuu katika anga! Nazisikiliza sauti za watu duniani, wanaomimina upendo na uchaji wao mwingi kwa ajili Yangu katika wimbo! Katika siku hii, huku viumbe wote wakirudishiwa uhai, Nashuka katika dunia ya wanadamu. Katika wakati huu, mambo yalivyo, maua yanachanua kwa wingi, ndege wote wanaimba kwa sauti moja, vitu vyote vinajawa na furaha! Kwa sauti ya saluti ya ufalme, ufalme wa Shetani unaanguka, ukiangamizwa katika mngurumo wa wimbo wa ufalme, usiinuke tena!

3 Nani duniani anathubutu kuinuka na kupinga? Ninaposhuka duniani Naleta kuchoma, Naleta ghadhabu, Naleta maafa ya aina yote. Falme za dunia sasa ni ufalme Wangu! Juu angani, mawingu yanagaagaa na kujongea kama mawimbi; chini ya anga, maziwa na mito yanatapakaa na kutoa muziki wa kusonga kwa furaha. Wanyama wanaopumzika wanaibuka kutoka kwenye matundu yao, na watu wote ambao wamelala wanaamshwa nami. Siku ambayo watu wote wameingojea hatimaye imefika! Wananiimbia nyimbo nzuri sana!

Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Ni nini mnachofikiria kuhusu kila wakati mnapouimba wimbo huu? (Ukiwa umechangamka; nasisimkwa; nafikiria namna ambavyo utukufu wa ufalme ulivyo mrembo, na mwanadamu na Mungu wataunganishwa daima dawamu.) Je, yupo yeyote aliyefikiria kuhusu umbo ambalo binadamu lazima achukue ili kuweza kuwa na Mungu? Katika kufikiria kwenu, mtu anafaa kuwa vipi ili kuweza kujiunga na Mungu na kufurahia maisha yenye utukufu yanayofuata katika ufalme? (Wanafaa kuwa wamebadilisha tabia.) Wanafaa kuwa wamebadilisha tabia, lakini kubadilisha hadi kiwango gani? Watakuwa vipi baada ya kubadilishwa tabia? (Watakuwa watakatifu.) Ni nini kipimo cha utakatifu? (Fikira na utiliaji maanani wao wote unalingana na Kristo.) Sasa ni vipi ambavyo hali hii ya kuingiliana inavyojionyesha? (Hawamzuii Mungu, wala kumsaliti Mungu, lakini wanajitolea kuwa wenye utiifu kabisa kwa Mungu na kumcha Mungu katika mioyo yao.) Baadhi ya majibu yenu yako katika njia sawa. Fungueni mioyo yenu, nyinyi nyote, na msemezane kile ambacho mioyo yenu inawaambia. (Watu wanaoishi na Mungu katika ufalme wanaweza kutekeleza wajibu wao, kutekeleza kwa uaminifu wajibu wao, kwa kutafuta ukweli na kutozuiliwa na mtu yeyote, hafla yoyote, au kifaa chochote. Na inawezekana kujiondoa kwenye ushawishi wa giza na kulinganisha mioyo yao na Mungu, na kumcha Mungu na kujiepusha na uovu.) (Mtazamo wetu wa kuangalia mambo unaweza kulinganishwa na ule wa Mungu, na tunaweza kujitenga na ushawishi wa giza. Kiwango cha chini zaidi ni kutotumiwa vibaya na Shetani, kutupa nje tabia yoyote ya upotoshaji, na kutimiza utiifu wa Mungu. Tunasadiki kwamba kuwa huru dhidi ya ushawishi wa giza ndiyo hoja kuu. Kama mtu hawezi kujitenga na ushawishi wa giza, hawezi kujipa uhuru kutoka kwenye minyororo ya Shetani, basi hajapata wokovu wa Mungu.) (Kiwango cha kufanywa kuwa mtimilifu na Mungu ni binadamu akiwa na moyo mmoja na akili na Mungu. Binadamu hamzuii Mungu tena; anaweza kujua Mungu mwenyewe, kuweka ukweli katika matendo, kupata uelewa wa Mungu, kumpenda Mungu, na kulingana na Mungu. Hayo ndiyo yote ambayo mtu anahitaji kufanya.)

Uzito wa Matokeo katika Mioyo ya Watu

Yaonekana mnavyo vitu katika mioyo yenu kuhusu njia mnayofaa kutembea na mmeimarisha mmeimarisha kiwango cha kuielewa au kufahamu. Hata hivyo, iwapo maneno yote ambayo mmeyanena ni maneno matupu au halisi inategemea lengo lenu la matendo yenu ya kila siku. Mmepata mavuno kutoka kwenye dhana zote za ukweli kupitia miaka hii, kwenye falsafa na kwenye maudhui ya ukweli. Hii inathibitisha kwamba watu siku hizi wanatilia mkazo kule kutafuta ukweli. Na kutokana na hayo, kila dhana na kila kipengele cha ukweli kwa hakika kimeweka mizizi kwenye mioyo ya baadhi ya watu. Hata hivyo, ni nini hasa Ninachoogopa sana? Kwamba ingawa wahusika wa ukweli, na nadharia hizi, yameweza kunakili mizizi yao, maudhui halisi bado hayana uzito mkubwa katika mioyo yenu. Wakati mnapokumbana na masuala, mnapopitia majaribio, mnapopitia chaguo—ni kwa kiwango kipi utumiaji wa vitendo wa ukweli huu utakuwa wa manufaa kwenu? Je, inawezekana yatawasaidia kupita ugumu wenu na kuwafanya kuibuka kutoka kwenye majaribio yenu baada ya kutosheleza nia za Mungu? Je, mtasimama imara katika majaribio yenu na kushuhudia kwa sauti na waziwazi kwake Mungu? Je, mmewahi kuwa na kivutio katika masuala haya awali? Mniruhusu kuuliza: Katika mioyo yenu, kwenye fikira na tafakari zenu za kila siku, ni nini hicho ambacho ni muhimu sana kwenu? Mmewahi kuja kwenye hitimisho? Ni nini mnachosadiki kuwa kitu muhimu zaidi? Baadhi ya watu husema “ni kuweka ukweli katika matendo, bila shaka”; baadhi ya watu husema “bila shaka ni kulisoma neno la Mungu kila siku”; baadhi ya watu husema “ni kujiweka mbele ya Mungu na kuomba Mungu kila siku, bila shaka”; na kisha kunao wale wanaosema “bila shaka ni kutekeleza wajibu wangu kwa njia bora kila siku”; kunao baadhi ya watu pia ambao wanasema wanafikiria wakati wote tu kuhusu namna ya kumtosheleza Mungu, namna ya kumtii Yeye katika mambo yote, na namna ya kuchukua hatua kulingana na mapenzi Yake. Je, hivi ndivyo ilivyo? Je, hivi ndivyo kila kitu kinavyohitajika kufanywa? Kwa mfano, kunao baadhi wanaosema: “Mimi ninataka tu kumtii Mungu, lakini kitu kinapofanyika siwezi kumtii Yeye.” Baadhi ya watu husema: “Nataka tu kumtosheleza Mungu. Hata kama ningemtosheleza Yeye mara moja tu, hilo lingetosha, lakini sitoweza kumtosheleza Yeye.” Na baadhi ya watu husema: “Ninataka tu kumtii Mungu. Katika nyakati za majaribio nataka kunyenyekea katika mipango Yake, huku nikitii ukuu na mipangilio Yake, bila ya malalamiko au maombi yoyote. Ilhali karibu kila wakati ninashindwa kuwa mtiifu.” Baadhi ya watu wengine husema: “Ninapokabiliwa na uamuzi, siwezi kamwe kutia ukweli katika matendo. Siku zote nataka kutosheleza mwili, siku zote nataka kutosheleza matamanio yangu ya kibinafsi ninayojitakia.” Ni nini sababu ya haya? Kabla ya jaribio la Mungu kufika, je, mmewahi kujipa changamoto nyinyi wenyewe mara nyingi, na kujijaribu nyinyi wenyewe mara nyingi? Oneni kama kweli mnaweza kumtii Mungu, kuweza kwa kweli kumtosheleza Mungu, na kuwa na hakika kutomsaliti Mungu. Tazameni kama hamwezi kujitosheleza, kutojitosheleza matamanio yenu ya kibinafsi, lakini kumtosheleza Mungu tu, bila ya chaguo lenu la kibinafsi. Je, yupo aliye hivi? Kwa hakika, kunayo hoja moja tu ambayo imewekwa mbele ya macho yenu nyinyi wenyewe. Ni kile ambacho kila mmoja wenu anavutiwa nacho, kile ambacho mnachotaka kujua zaidi, na hilo ni suala la matokeo na hatima ya kila mmoja wenu. Huenda msitambue, lakini hili ni jambo ambalo hakuna anayeweza kulikataa. Ninajua kwamba kunao baadhi ya watu ambao, tunapokuja katika ukweli wa matokeo ya binadamu, ahadi ya Mungu kwa ubinadamu, na aina gani ya hatima ambayo Mungu ananuia kumleta binadamu katika, tayari wamefanyia uchunguzi neno la Mungu katika masuala haya mara kadhaa. Kisha kunao ambao kila mara wanalitafuta na kulifikiria kwenye akili zao, na bado hawapati matokeo, au pengine wanafikia katika hitimisho fulani isiyoeleweka. Hatimaye bado hawana hakika kuhusu ni aina gani ya matokeo yanayowasubiri. Wanapotekeleza wajibu wao, baadhi ya watu siku zote wanataka kujua majibu dhahiri kwa maswali yafuatayo: Matokeo yangu yatakuwa yapi? Ninaweza kutembelea njia hii hadi mwisho wake? Mwelekeo wa Mungu kwake binadamu ni upi? Baadhi ya watu huwa hata na wasiwasi: Nimefanya baadhi ya mambo siku zilizopita, nimesema baadhi ya mambo, sikumtii Mungu, nimefanya mambo fulani ambayo yamemsaliti Mungu, kulikuwa na masuala fulani ambapo sikumtosheleza Mungu, niliuumiza moyo wa Mungu, nilimfanya Mungu kunikasirikia, nilimfanya Mungu kunichukia na kuniona kwamba ninachukiza, hivyo basi pengine matokeo yangu hayajulikani. Ni haki kusema kwamba watu wengi zaidi wanahisi wasiwasi kuhusu matokeo yao wenyewe. Hakuna anayethubutu kusema: “Nahisi kwa uhakika wa asilimia mia moja kwamba nitaishi Ninao uhakika wa asilimia mia moja kwamba ninaweza kuzitosheleza nia za Mungu; mimi ni mtu anayefuata moyo wa Mungu; mimi ni mtu anayesifiwa na Mungu.” Baadhi ya watu hufikiria ni vigumu hasa kufuata njia ya Mungu, na kwamba kutia ukweli katika matendo ndilo jambo gumu zaidi la kufanya. Kwa hivyo, watu hawa hufikiria hawawezi kusaidika, na hawathubutu kuwa na matumaini ya kuwa na matokeo mazuri. Au pengine wanasadiki kwamba hawawezi kutosheleza nia za Mungu, na kuweza kuishi; na kwa sababu ya haya watasema kwamba hawana matokeo, na hawawezi kufikia hatima nzuri. Licha ya jinsi watu hufikiria, kila mmoja anastaajabu kuhusu matokeo yao mara nyingi. Kuhusu masuala ya siku zao za usoni, kuhusu maswali ya kile watakachopata wakati Mungu atakapomaliza kazi Yake, watu hawa siku zote wanapiga hesabu, siku zote wanapanga. Baadhi ya watu wanalipia bei mara dufu; baadhi ya watu wanaacha familia zao na kazi zao; baadhi wanakata tamaa katika ndoa zao; baadhi yaowanakubali bila kulalamika kujitumia kwa ajili ya Mungu; baadhi ya watu huacha nyumba zao ili kutenda wajibu wao; baadhi ya watu huchagua ugumu, na kuanza kufanya kazi ambazo ni chungu zaidi na zinachosha zaidi; baadhi ya watu huchagua kuutoa utajiri wao, kujitolea kila kitu chao; na bado baadhi ya watu huchagua kufuata ukweli na kufuatilia kumjua Mungu. Haijalishi namna mnavyochagua kutenda, namna mnavyotenda ndiyo muhimu zaidi? (Si muhimu.) Ni vipi tunavyoelezea kwamba si muhimu, basi? Kama namna hiyo si muhimu, basi ni nini muhimu? (Tabia nzuri kwa nje si wakilishi wa kutia ukweli katika matendo.) (Kile ambacho kila mmoja anafikiria si muhimu. Cha msingi hapa ni kama tumeweza kutia ukweli katika matendo, na kama tunampenda Mungu.) (Maangamizi ya wapinga Kristo na viongozi bandia hutusaidia kuelewa kwamba tabia ya nje si jambo muhimu zaidi. Kwa nje wanaonekana kuwa wamejinyima mengi, na wanaonekana kuwa radhi kulipa bei, lakini kwa kuchambua tunaweza kuona kwamba hawana moyo kabisa unaomcha Mungu; kwa mitazamo yote wanampinga Yeye. Siku zote wanasimama pamoja na Shetani katika nyakati za hatari, na kuingilia kazi ya Mungu. Hivyo basi, utiliaji maanani mkuu hapa ni upande gani tutasimama wakati ukiwadia, na mitazamo yetu.) Nyote mnaongea vyema, na yaonekana kwamba tayari mnao msingi wa uelewa wa na kiwango cha kuweza kutia ukweli wenu katika matendo, nia za Mungu, na kile Mungu anahitaji kutoka kwa binadamu. Kwamba mnaweza kuongea hivi ni jambo la kugusa kweli. Ingawa kuna maneno machache yasiyofaa hapa na pale, kauli zenu tayari zinakaribia ufafanuzi unaostahili ukweli Hii inathibitisha kwamba mmeimarisha uelewa wenu halisi wa watu matukio, na vifaa vilivyo karibu nanyi, mazingira yenu yote ambayo Mungu amepanga, na kila kitu mnachoweza kuona. Uelewa huu unakaribia ukweli. Hata ingawa kile mnachosema si pana kabisa, na maneno machache hayafai sana, uelewa wenu tayari unakaribia uhalisi wa ukweli. Kuwasikiliza mkiongea kwa njia hii kunanifanya Mimi kuhisi vizuri sana. 

Imani za Watu Haziwezi Kubadilishwa na Ukweli

Kunao baadhi ya watu wanaoweza kuvumilia ugumu; wanaweza kulipia bei; tabia yao ya nje ni nzuri sana; wanaheshimika sana; na wanatamaniwa na wengine. Mnafikiria nini: Je, tabia kama hii ya nje inaweza kuchukuliwa kama ya kutia ukweli katika matendo? Mnaweza kusema kwamba mtu huyu anatosheleza nia za Mungu? Kwa nini mara kwa mara watu wanamwona mtu wa aina hii na kufikiria kwamba wao wanamtosheleza Mungu, wanafikiria kwamba wanatembelea njia ile ya kutia ukweli katika matendo, kwamba wanatembea katika njia ya Mungu? Kwa nini baadhi ya watu hufikiria kwa njia hii? Upo ufafanuzi mmoja tu kwa haya. Na ufafanuzi huu ni upi? Sababu ni kwamba kwa kiasi kikubwa cha watu, maswali kama kutia ukweli katika matendo ni nini, kutosheleza Mungu ni nini, ni nini kuwa na uhalisia wa ukweli—maswali haya hayako wazi sana. Hivyo basi kunao baadhi ya watu ambao mara nyingi wanadanganywa na wale ambao kwa nje wanaonekana wa kiroho, wanaonekana wa kilodi, wanaonekana kuwa na taswira za ukuu. Kuhusiana na watu hao wanaoweza kuzungumzia barua na falsafa, na ambao hotuba na vitendo vyao vinaonekana kuwa vyenye kustahili uvutiwaji, wale wanaodanganywa nawao hawajawahi kuangalia kiini halisi cha vitendo vyao, kanuni zinazoendesha vitendo vyao, au shabaha zao ni nini. Na hawajawahi kuangalia kama watu hawa wanatii Mungu kwa kweli, na kama wao ni watu wanaomcha Mungu kwa kweli na kujiepusha na uovu au la. Hawajawahi kutambua kile kiini halisi cha ubinadamu cha watu hawa. Badala yake, kutoka kwenye hatua ya kwanza ya kujua na kuzoeana nao, hatua kwa hatua wanaanza kuwapenda watu hawa, kuwatukuza watu hawa, na hatimaye watu hawa wanakuwa sanamu zao. Aidha, katika akili za baadhi ya watu, sanamu hizi wanazoziabudu, wanaosadiki wanaweza kuacha familia na kazi zao, na kulipa ile bei kwa juujuu—sanamu hizi ndizo ambazo kwa kweli zinatosheleza Mungu, ndizo zile zinazoweza kupokea kwa kweli matokeo mazuri na hatima nzuri. Katika akili zao, sanamu hizi ndizo wale watu ambao Mungu husifu. Ni nini husababisha watu kuwa na aina hii ya kusadiki? Ni nini kiini halisi cha suala hili? Ni nini matokeo hali hii inaweza kuleta? Hebu na tuzungumzie kwanza suala la kiini chake halisi.

Masuala haya kuhusiana na mitazamo ya watu, vitendo vya watu, ni kanuni gani ambazo watu wanachagua kutenda, na kile ambacho kwa kawaida kila mtu anatilia mkazo, kimsingi haya yote hayahusu mahitaji ya Mungu kwa mwanadamu hata kidogo. Bila kujali kama watu wanazingatia masuala ya juujuu au yale ya kina, wanazingatia barua na falsafa au uhalisia, watu hawatii yale ambayo wanafaa kutii zaidi, na hawajui kile wanachofaa kujua zaidi. Sababu ya hali hii kuwa hivi ni kwamba watu hawaupendi ukweli kamwe. Hivyo basi, watu hawako radhi kutumia muda na jitihada zao katika kutafuta na kuendeleza kanuni katika neno la Mungu. Badala yake, wanapendelea kutumia njia za mkato, na kujumlisha kile wanachoelewa, kile wanachojua, kuwa vitendo vizuri na tabia nzuri. Muhtasari huu nao huwa shabaha yao ya binafsi ya kufuata, unakuwa ukweli wa kutendwa. Athari ya moja kwa moja ya haya yote ni kwamba watu wanatumia tabia nzuri ya kibinadamu kama kisawazisho cha kutia ukweli katika matendo yao, hali ambayo inatosheleza pia matamanio ya watu ili kupata fadhila na Mungu. Hii inawapa watu mtaji wa kushindania ukweli, ambao pia wao hutumia kutoa sababu na kushindana na Mungu. Wakati uo huo, watu wanamweka Mungu kando kwa njia za ufidhuli, na kuiweka ile sanamu ya mioyo yao katika nafasi ya Mungu. Kunayo sababu moja tu ya chanzo cha haya ambayo huwafanya watu kuwa na vitendo wasivyovijua, mitazamo wasiyoijua, au mitazamo na vitendo vya upande mmoja, na leo Nitawaelezea kuhusu haya. Sababu ni kwamba ingawa watu wengi wanaweza kumfuata Mungu, kumwomba Yeye kila siku, na kusoma neno la Mungu kila siku, hawaelewi kwa hakika nia za Mungu. Hiki ndicho chanzo cha tatizo. Kama mtu huelewa moyo wa Mungu, huelewa kile anachopenda Mungu, kile humchukiza Mungu, kile anachotaka Mungu, kile anachokataa Mungu, ni mtu wa aina gani ambaye Mungu humpenda, ni mtu wa aina gani ambaye Mungu hampendi, ni kiwango kipi ambacho Mungu hutumia katika kutoa mahitaji Yake kwa binadamu, ni mtazamo gani ambao Anauchukua katika kumfanya binadamu kuwa mtimilifu, je, mtu huyu anaweza bado kuwa na mawazo yake ya kibinafsi? Wanaweza tu kuenda na kumwabudu mtu mwingine? Mtu wa kawaida anaweza kuwa sanamu yao? Kama mtu anaelewa nia za Mungu, mtazamo wake ni wenye kirazini zaidi kuliko hapo. Hawatamwabudu kama Mungu kiongozi aliyepotoka kiholela, wala hawataweza, huku wakitembea njia ya kutia ukweli katika matendo, kusadiki kwamba kutii kiholela katika sheria au kanuni chache rahisi ni sawa na kutia ukweli katika matendo.

Kunayo Maoni Mengi Yanayohusu Kiwango Ambacho Mungu Hutumia Kuasisi Matokeo ya Binadamu

Hebu na turudi katika mada hii na tuendelee kuzungumzia suala la matokeo.

Kwa sababu kila mmoja anajali matokeo yake, je, mnajua namna ambavyo Mungu huamua matokeo hayo? Na ni kwa njia gani ambayo Mungu huanzisha matokeo ya mtu? Na ni kiwango gani ambacho Mungu hutumia kuasisi matokeo ya mtu? Na wakati ambapo matokeo ya mtu yangali bado hayajaasisiwa, ni nini anachofanya Mungu ili kufichua matokeo haya? Je, yupo anayejua haya? Kama Nilivyosema tu, kunao baadhi ambao tayari wamefanyia uchunguzi neno la Mungu kitambo sana. Watu hao wanatafuta dalili fulani kuhusu matokeo ya mwanadamu, kuhusu kategoria ambazo matokeo haya yamegawanywa, na kuhusu matokeo tofauti yanayosubiria aina tofauti ya watu. Wanataka pia kujua namna neno la Mungu linavyoanzisha matokeo ya binadamu, aina za kiwango ambacho Mungu hutumia, na njia ambayo Yeye huasisi matokeo ya binadamu. Ilhali mwishowe watu hawa hawafanikiwi kupata chochote. Kwa hakika, yapo mambo machache yenye thamani yanayozungumzwa kuhusu suala hili miongoni mwa neno la Mungu. Kwa nini hali iko hivi? Ili mradi matokeo ya binadamu yangali hayajafichuliwa, Mungu hataki kumwambia yeyote kuhusu kile kitakachofanyika mwishowe, wala Hataki kumfahamisha yeyote kuhusu hatima yao kabla ya wakati kufika. Sababu ya kufanya hivi ni kwamba Mungu kufanya hivyo hakutaleta manufaa yoyote kwa binadamu. Sasa hivi, Nataka kuwaambia tu kuhusu namna Mungu huasisi matokeo ya binadamu, kuhusu kanuni Anazotumia katika kazi Yake ili kuyaasisi matokeo ya binadamu, na kuonyesha matokeo haya, pamoja na kiwango Anachotumia ili kuanzisha kama mtu ataweza kuishi au la. Hiki sicho kile ambacho mnajali zaidi kuhusu? Hivyo basi, ni vipi ambavyo watu hufahamu njia ambayo Mungu anaanzisha matokeo ya binadamu? Mlizungumzia kidogo kuhusu suala hili muda mfupi uliopita. Baadhi yenu mlisema kwamba ni swali la kutenda wajibu wao kwa uaminifu, kugharamika kwa ajili ya Mungu; baadhi ya watu walisema kumtii Mungu na kutosheleza Mungu; baadhi ya watu walisema kudhibitiwa na Mungu; na baadhi ya watu walisema kuishi maisha ya hadhi ya chini…. Wakati mnapotia ukweli huu katika matendo, wakati mnapotenda kanuni za kufikiria kwenu, je mnajua kile Mungu anachofikiria? Mmewahi kufikiria kama kuendelea hivi ni kutosheleza nia za Mungu au la? Kama kunatilia maanani kiwango cha Mungu? Kama kunatilia maanani mahitaji ya Mungu? Ninasadiki kwamba watu wengi zaidi hawalifikirii suala hili kwa undani. Wanatumia tu bila kutilia maanani sehemu ya neno la Mungu, au sehemu ya mahubiri, au viwango vya watu fulani wa kiroho ambao wanawaabudu, na kujilazimisha kufanya hivi na vile. Wanasadiki kwamba hii ndiyo njia sahihi, na hivyo basi wanaendelea kuitii, kuifanya, liwalo liwe hatimaye. Baadhi ya watu hufikiria: “Nimesadiki kwa miaka mingi siku zote nimetenda mambo kwa njia hii; nahisi kuwa nimemtosheleza kabisa Mungu; ninahisi pia kuwa nimejifunza mengi kutoka kwa haya. Kwani nimekwishaelewa ukweli mwingi katika kipindi hiki, na nimeelewa mambo mengi ambayo sikuyaelewa awali—hasa, wingi wa fikira na mitazamo yangu imebadilika, maadili ya maisha yangu yamebadilika sana, na ninao uelewa mzuri sana wa ulimwengu huu.” Watu kama hao wanasadiki kwamba haya ni mavuno, na ndiyo matokeo ya mwisho ya kazi ya Mungu kwa binadamu. Kwa maoni yenu, kwa viwango hivi na vitendo vyenu nyote vimewekwa pamoja—je, mnatosheleza nia za Mungu? Baadhi ya watu watasema kwa uhakika wote, “Bila shaka! Tunatenda kulingana na neno la Mungu; tunatenda kulingana na kile ambacho yule aliye juu Alihubiri na kuwasilisha. Sisi siku zote tunafanya wajibu wetu na tunamfuata Mungu bila kukoma, hatujawahi kumwacha Mungu. Hivyo basi tunaweza kusema kwa imani kamili kwamba tunamtosheleza Mungu. Haijalishi ni kiasi kipi tunachoelewa kuhusu nia za Mungu, haijalishi ni vipi tunavyoelewa neno la Mungu, siku zote tumekuwa kwa njia ya kutafuta kuweza kutangamana na Mungu. Kama tutachukua hatua kwa usahihi, na kutenda kwa usahihi, basi matokeo yatakuwa sahihi.” Je, mnafikiria nini kuhusu mtazamo huu? Je, ni kweli? Pengine wapo wale wanaosema: “Sijawahi kufikiria kuhusu mambo haya awali. Mimi nafikiria tu kwamba nikiendelea kutimiza wajibu wangu na kuendelea kutenda kulingana na mahitaji ya neno la Mungu, basi nitasalia. Sijawahi kufikiria swali la kama ninaweza kutosheleza moyo wa Mungu, na sijawahi kufikiria kama ninatimiza kiwango kinachohitajika na Yeye. Kwa sababu Mungu hajawahi kuniambia, wala kunipatia maagizo yoyote kwa uwazi, ninasadiki kwamba mradi tu niendelee kupiga hatua mbele, Mungu atatosheka na Yeye hafai kuwa na mahitaji yoyote ya ziada kwangu mimi.” Je, kusadiki huku ni sahihi? Kulingana na Ninavyojua, njia hii ya kutenda, njia hii ya kufikiria, na mitazamo hii—yote yanakuja na madoido fulani na kiasi kidogo cha upofu. Ninaposema hivi, pengine wapo baadhi yenu mnaohisi kuvunjika moyo: “Yaani upofu? Kama ni ‘upofu,’ basi tumaini letu la wokovu, tumaini letu la kuishini dogo mno, na halina uhakika, hapo ni kweli? Je, wewe kulitamka hivyo lilivyo si sawa na kutumwagilia maji baridi?” Haijalishi kile mnachosadiki, mambo Ninayoyasema na kufanya hayanuii kukufanya ninyi kuhisi kama mnamwagiliwa maji baridi. Badala yake, yananuia kuboresha uelewa wenu wa nia za Mungu, na kuboresha ung’amuzi wenu kuhusu kile ambacho Mungu anafikiria, kile ambacho Mungu anataka kukamilisha ni mtu wa aina gani ambaye Mungu anapenda, nini kinachukiza Mungu, nini Mungu anadharau, ni mtu wa aina gani ambaye Mungu anataka kumpata, na ni mtu wa aina gani ambaye Mungu anatupilia mbali. Yananuia kupatia akili zenu uwazi, kuwasaidia kujua wazi ni kiwango kipi vitendo na fikira za kila mmoja wenu yamepotea kutoka kwa kiwango kinachohitajika na Mungu. Je, inahitajika kuzungumzia mada hii? Kwa sababu Ninajua mmesadiki kwa muda mrefu, na mmesikiliza mahubiri mengi, lakini kwa hakika haya ndiyo mambo yanayokosekana zaidi. Mmerekodi kila ukweli katika daftari zenu, mmerekodi pia kile ambacho nyie wenyewe mnasadiki kibinafsi kuwa muhimu katika akili zenu na ingawa mnapanga kutumia haya kumridhisha Mungu wakati wa kutenda kwenu, kuyatumia mnapojipata mkihitaji msaada, kuyatumia kupitia nyakati ngumu zilizo mbele yenu, au mnaacha ukweli huu uandamane na ninyi mnapoishi maisha yenu tu. Lakini kulingana na Ninavyojua, iwapo mnatenda tu, namna mnavyotenda hasa si muhimu. Nini, basi, ndicho kitu cha muhimu sana? Ni kwamba wakati unatenda, moyo wako hujua kwa uhakika wote kama kila kitu unachofanya, kila kitendo, ndicho kile anachotaka Mungu au la; kama kila kitu unachofanya ni sahihi au la, kila kitu unachofikiria ni sahihi au la, na matokeo na shabaha katika moyo wako yanatosheleza nia za Mungu au la, kama yanatilia maanani mahitaji ya Mungu au la, na kama Mungu anayaidhinisha au la. Haya ni mambo muhimu.

Tembea katika Njia ya Mungu: Mche Mungu na Kuepuka Maovu

Kunao msemo ambao mnafaa kutilia maanani. Ninasadiki msemo huu ni muhimu sana, kwa sababu kwangu Mimi unakuja akilini mara nyingi kila siku. Kwa nini hivyo? Kwa sababu kila wakati Ninapokumbana na mtu, kila wakati Ninaposikia hadithi ya mtu, kila wakati Ninaposikia kile alichopitia mtu au ushuhuda wake wa kusadiki Mungu, siku zote Ninatumia msemo huu kuweza kupima kama mtu huyu binafsi ni mtu wa aina ambayo Mungu anataka au la, mtu wa aina ambayo Mungu anapenda. Hivyo msemo huu ni upi, basi? Sasa nyinyi nyote mnasubiri kwa hamu. Nitakapoufichua msemo huu, pengine mtakasirika kwa sababu wapo baadhi yenu ambao mmekuwa mkijifanya kuwa mnakubaliana nao kwa miaka mingi. Lakini Kwangu Mimi, Sijawahi kujifanya kuwa nakubaliana nao. Msemo huu umo moyoni Mwangu. Hivyo basi msemo huu ni upi? Msemo ni “tembea katika njia ya Mungu: mche Mungu na kuepuka maovu.” Je, huoni kwamba kauli hii ni rahisi kupindukia? Ilhali ingawa msemo huu unaweza kuwa rahisi, mtu ambaye anao uelewa wa ndani na wa kweli wa msemo huu atahisi kwamba ni wenye uzito mkubwa; kwamba unao thamani nyingi ya kutenda; kwamba ni lugha ya uzima iliyo na uhalisia wa ukweli; ambayo ni lengo la maishani katika kulenga wale wanaotafuta kutosheleza Mungu; na hiyo ni njia ya maisha marefu itakayofuatwa na mtu yeyote anayejali nia za Mungu. Hivyo basi mnafikiria nini: Je, msemo huu sio ukweli? Je, unao umuhimu kama huo au la? Pia, pengine baadhi yenu mnafikiria kuhusu msemo huu, wakijaribu kuuelewa, na wapo baadhi ambao bado wanautilia shaka. Je, msemo huu ni muhimu sana? Je, ni muhimu sana? Unahitajika sana na unastahili kutiliwa mkazo? Pengine wapo baadhi ya watu ambao hawapendi sana msemo huu kwa sababu wanafikiria kwamba kuchukua njia ya Mungu na kuitiririsha ndani ya msemo huu mmoja ni urahisishaji wa kupindukia. Kuyachukua yale yote ambayo Mungu alisema na kuyafanya yawe msemo mmoja—je, hivi si kumfanya Mungu kuwa yule asiyekuwa na umuhimu sana? Hivi ndivyo ilivyo? Inaweza kuwa kwamba wengi wenu nyinyi hamwelewi kabisa maana kuu ya maneno haya. Ingawa mmeyanakili na kuyatilia maanani, hamnuii kuuweka msemo huu katika mioyo yenu; mnaunakili tu katika vitabu vyenu, na kuudurusu tu, na kuufikiri katika muda wenu wa ziada. Wapo baadhi ya watu ambao hata hawatashughulika kuutia kwenye kumbukumbu msemo huu, sikuambii hata kujaribu kuutumia vizuri. Lakini kwa nini Nikauzungumzia msemo huu? Licha ya mtazamo wenu, au kile mtakachofikiria, lazima Nizungumzie msemo huu kwa sababu unafaa ajabu namna ambavyo Mungu huasisi matokeo ya binadamu. Bila kujali kama uelewa wenu wa sasa wa msemo huu upo, namna mnavyouchukulia, bado Nitawaeleza: kama watu wanaweza kuyaweka maneno ya msemo huu katika vitendo na kuyapitia, na kutimiza kiwango cha kumcha Mungu na kujiepusha na maovu, basi atahakikishiwa kuishi kisha atahakikishiwa kuwa mtu mwenye matokeo mazuri. Kama huwezi kutimiza kiwango kilichowekwa wazi katika msemo huu, basi inaweza kusemekana kwamba matokeo yako hayajulikani. Hivyo basi Ninaongea kwenu kuhusu msemo huu kwa matayarisho yenu ya kiakili, na ili mjue ni kiwango aina gani ambacho Mungu anatumia kuwapima. Kama Nilivyozungumza tu muda mfupi uliopita, msemo huu unafaa pakubwa kwa wokovu wa Mungu kwa binadamu na namna ambavyo Aliyaasisi matokeo ya binadamu. Uhusiano huu unapatikana wapi? Mngependa kwa kweli kujua, hivyo basi tutauzungumzia leo.

Mungu Hutumia Majaribio Tofauti ili Kupima Kama Watu Humcha Mungu na Kujiepusha na Maovu

Katika kila enzi, Mungu huwapa binadamu baadhi ya maneno Anapofanya kazi ulimwenguni, huku akimwambia mwanadamu kuhusu baadhi ya ukweli. Ukweli huu unahudumu kama njia ambayo binadamu anafaa kuitii, njia ya kutembelewa na binadamu, njia ambayo humwezesha binadamu kumcha Mungu na kujiepusha na uovu, na njia ambayo watu wanafaa kuweka katika vitendo na kuitii katika maisha yao na kwenye mkondo wa safari zao za maisha. Ni kwa sababu hizi ambapo Mungu anampa binadamu maneno haya. Binadamu anafaa kuyatii maneno haya yanayotoka kwa Mungu, na kuyatii ni kupokea uzima. Kama mtu hataweza kuyatii, na hayatii kwenye matendo, na haishi kwa kudhihirisha maneno ya Mungu katika maisha yake, basi mtu huyo hautilii ukweli katika matendo. Na kama hawatilii ukweli katika matendo, basi hawamchi Mungu na hawaepuki uovu, wala hawawezi kumtosheleza Mungu. Kama mtu hawezi kumtosheleza Mungu, basi hawezi kupokea sifa ya Mungu; mtu wa aina hii hana matokeo. Hivyo basi ni vipi katika mkondo wa kazi ya Mungu ndipo Anapoasisi matokeo ya mtu? Ni mbinu gani anayoitumia Mungu kuasisi matokeo ya binadamu? Pengine nyinyi hamlielewi suala hili sasa hivi, lakini Nitakapowaambia mchakato jambo hili litakuwa wazi kabisa. Hii ni kwa sababu watu wengi tayari wamelipitia suala hili wenyewe.

Katika mkondo wa kazi ya Mungu, kuanzia mwanzo hadi sasa, Mungu Amepanga majaribio kwa kila mtu—au mnaweza kusema, kila mtu anayemfuata Yeye—na majaribio haya yanakuja kwa ukubwa tofauti. Wapo wale ambao wamepitia jaribio la kukataliwa na familia zao; wapo wale ambao wamepitia jaribio la mazingira mabovu; wapo wale ambao wamepitia majaribio ya kukamatwa na kuteswa; wapo wale ambao wamepitia majaribio ya kukumbwa na chaguo; na wapo wale ambao wamekumbwa na majaribio ya pesa na hadhi. Nikizungumza kwa ujumla, kila moja wenu amekabiliwa na aina zote za majaribio. Kwa nini Mungu anafanya kazi hivyo? Kwa nini Mungu Anamtenda hivi kila mtu? Ni matokeo aina gani Anayotaka kuyaona? Hii ndiyo hoja muhimu kuhusu kile Ninachotaka kuwaambia: Mungu anataka kuona kama mtu huyu ni yule anayemcha Mungu na kujiepusha na uovu. Maana ya haya ni kwamba wakati Mungu anakupa jaribio, na kukufanya kukabiliwa na baadhi ya hali, Anataka kukupima na kujua kama wewe ndiye yule mtu anayemcha Mungu, mtu huyo anayejiepusha na uovu au la. Kama mtu amekumbwa na wajibu wa kutunza sadaka, na anakutana na sadaka ya Mungu, basi unadhani kwamba hiki ni kitu ambacho Mungu amepanga? Bila shaka! Kila kitu unachokumbana nacho ni kitu ambacho Mungu amepanga. Unapokumbwa na suala hili, Mungu atakuangalia kwa siri, namna ulivyochagua, namna unavyotenda, na kile unachofikiria. Matokeo yake ya mwisho ndiyo ambayo Mungu anayajali zaidi, sababu ni matokeo ambayo yatamruhusu Yeye kupima kama umetimiza kiwango cha Mungu katika jaribio hilo au la. Hata hivyo, wakati watu wanapokumbwa na baadhi ya masuala haya, mara nyingi hawafikirii kuhusu ni kwa nini wanakumbwa na mambo hayo, au kile kiwango ambacho kinahitajika na Mungu. Hawafikirii kuhusu kile Mungu anachotaka kutoka kwao, kile Anachotaka kupata kutoka kwao. Wakati wanapokumbwa na suala hili, mtu wa aina hii anafikiria tu: “Hili ni jambo ambalo nimekumbwa nalo; lazima niwe makinifu, wala si mzembe! Haijalishi ni nini, hii ni sadaka ya Mungu na siwezi kuigusa.” Mtu huyo anasadiki kwamba anaweza kutimiza jukumu lake kupitia kufikiria huko sahili. Je, Mungu ataweza kutosheka na matokeo ya jaribio hili? Au Hatatosheka? Mnaweza kuzungumzia suala hili. (Kama mtu anamcha Mungu katika moyo wake, kisha anapokumbwa na wajibu unaomruhusu kukutana na sadaka ya Mungu, anaweza kufikiria namna ilivyo rahisi kukosea tabia ya Mungu, ili wawe na hakika ya kuendelea kwa tahadhari.) Mwitikio wako u katika njia sahihi, lakini bado haujafika. Kutembea katika njia ya Mungu hakuhusu kuangalia sheria juujuu. Badala yake, kunamaanisha kwamba unapokabiliwa na suala, kwanza kabisa, unaliangalia kama ni hali ambayo imepangwa na Mungu, wajibu uliopewa wewe na Yeye, au kitu ambacho Amekuaminia wewe, na kwamba unapokabiliana na suala hili, unapaswa kuliona kama jaribio kutoka kwa Mungu. Wakati unapokabiliwa na suala hili, lazima uwe na kiwango, lazima ufikirie kwamba suala hilo limetoka kwa Mungu. Lazima ufikirie ni vipi ambavyo utashughulikia suala hili kiasi cha kwamba unaweza kutimiza wajibu wako, na kuwa mwaminifu kwa Mungu; namna ya kulifanya bila ya kumghadhabisha Mungu; au kukosea tabia Yake. Tumetoka tu kuzungumzia kutunza sadaka. Swala hili linahusu sadaka, na linahusisha pia wajibu wako, jukumu lako. Unahitajika kuwajibikia jukumu hili. Ilhali unapokabiliwa na suala hili, kunalo jaribio lolote? Lipo! Jaribio hilo linatoka wapi? Jaribio hilo linatoka kwa Shetani, na linatoka pia kwa tabia potovu na ya uovu ya binadamu. Kwa sababu kunalo jaribio, hili linahusisha kuwa shahidi; kuwa shahidi ni jukumu na wajibu wako pia. Baadhi ya watu husema: “Hili ni suala dogo; kwa kweli linahitajika kulifanya suala hili dogo kuwa kubwa hivyo?” Ndiyo pana haja! Kwa sababu ili kutembea katika njia ya Mungu, hatuwezi kuwachilia chochote kinachotuhusu sisi wenyewe, au kinachofanyika karibu nasi, hata yale mambo madogo madogo. Haijalishi kama tunafikiria tunafaa kumakinika au la, mradi tu suala lolote linatukabili hatufai kuliacha. Lote linafaa kuonekana kama jaribio la Mungu kwetu. Mwelekeo aina hii uko vipi? Kama unao mwelekeo aina hii, basi unathibitisha hoja moja: Moyo wako unamcha Mungu, na moyo wako uko radhi kujiepusha na maovu. Kama unalo tamanio hili la kumtosheleza Mungu, basi kile unachotia katika matendo hakiko mbali na kiwango cha kumcha Mungu na kujiepusha na maovu.

Kunao mara nyingi wale wanaosadiki kwamba masuala ambayo hayatiliwi maanani na watu, masuala ambayo kwa kawaida hayatajwi—haya ni mambo madogo tu, na hayana chochote kuhusiana na kutia ukweli katika matendo. Wakati watu hawa wanakabiliwa na suala kama hilo, hawalifikirii sana na wanaliachilia tu. Lakini ukweli wa mambo ni kwamba, suala hili ni funzo ambalo unafaa kulidadisi, funzo kuhusu namna ya kumcha Mungu, namna ya kujiepusha na maovu. Zaidi, kile unachofaa kujali hata zaidi ni kujua kile Mungu anachofanya wakati suala hili linapoibuka kukabiliana na wewe. Mungu yuko kando yako, anaangalia kila mojawapo ya maneno na vitendo vyako, anaangalia hatua zako, mabadiliko ya akili zako—hii ni kazi ya Mungu. Baadhi ya watu husema: “Basi kwa nini siihisi?” Huihisi kwa sababu namna ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu haijawa ndiyo njia muhimu zaidi kwako kushughulikiwa. Hivyo basi, huwezi kuhisi kazi ngumu ya Mungu katika binadamu, inayojionyesha kulingana na fikira tofauti na vitendo tofauti vya watu. Wewe u makini! Suala kubwa ni lipi? Swala dogo ni lipi? Masuala yanayohusu kutembea katika njia ya Mungu hayagawanywi katika masuala makuu au madogo, yote ni yenye umuhimu—je, mnaweza kulikubali hilo? (Tunaweza kulikubali). Kuhusiana na masuala ya kila siku, kunayo yale ambayo watu wanayaona kuwa makubwa sana na muhimu, na mengine yanaonekana kuwa mambo madogo madogo tu. Mara nyingi watu huyaona masuala haya makubwa kuwa ndiyo muhimu zaidi, na wanayachukulia kwamba yametumwa na Mungu. Hata hivyo, kwenye mkondo wa masuala haya makubwa kujitokeza, kutokana na kimo finyu cha binadamu, na kutokana na kiwango cha binadamu kisichotosha, mara nyingi binadamu haendani sawa na nia za Mungu, hawezi kupata ufunuo wowote, na hawezi kufaidi maarifa yoyote halisi yenye thamani. Kuhusu masuala madogo, haya yanapuuzwa tu na binadamu, kuachwa kuponyoka kidogokidogo. Hivyo basi, wamepoteza fursa nyingi sana za kuchunguzwa mbele ya Mungu, kujaribiwa na Yeye. Je unafaa kuwapuuza watu, masuala na hali hizi siku zote ambazo Mungu anakupangilia wewe, hii itamaanisha nini? Inamaanisha kwamba kila siku, hata kila wakati, siku zote unakana ukamilifu wa Mungu kwako, na uongozi wa Mungu. Kila Mungu anapopanga hali hizi kwako wewe, Yeye anakuangalia kwa siri, Anauangalia moyo wako, Anaziangalia fikira na hali zako, Anaangalia namna unavyofikiria wewe, Anaangalia namna unavyochukua hatua. Kama wewe ni mtu asiyejali—mtu ambaye hajawahi kujali kuhusu njia ya Mungu, neno la Mungu, au ukweli—basi hutajali, hutatilia maanani kile ambacho Mungu anataka kukamilisha, na yale ambayo Mungu anakuhitaji wewe kufanya wakati Anapopanga hali hizi kwako wewe. Wala hutajua jinsi watu, matukio na vitu ambavyo unakumbana navyo vinavyohusiana na ukweli au mapenzi ya Mungu. Baada ya kukabiliana na hali nyingi kama hizi na majaribio mengi kama haya, huku naye Mungu haoni mafanikio yoyote kutokana na wewe, ataweza kuendelea vipi? Baada ya kukabiliwa na majaribio mara kwa mara, humkuzi Mungu katika moyo wako, na hushughulikii zile hali ambazo Mungu anakupangia wewe kama zilivyo—kama majaribio ya Mungu au mitihani ya Mungu. Badala yake unakataa fursa ambazo Mungu amekupa wewe moja baada ya nyingine, na unaziacha kutokomea mara kwa mara. Je huku si kutotii kwa hali ya juu ambako watu huonyesha? (Naam, ni kutotii.) Je, Mungu atahuzunishwa na mambo haya? (Naam, Atahuzunika). Sivyo, Mungu hatahuzunishwa! Mkinisikia Nikiongea hivi mnashtuka kwa mara nyingine tena. Kwani umesahau, ilisemekana hapo awali kwamba Mungu huhuzunika siku zote? Mungu hatahuzunika? Ni lini basi Mungu atahuzunika? Usijali, Mungu hatahuzunika na hali hii. Basi mwelekeo wa Mungu kwa aina hii ya tabia iliyoelezwa kwa muhtasari hapo juu ni upi? Wakati watu wanapokataa majaribio, mitihani, ambayo Mungu anawapa, wakati wanapoikwepa, kunao mwelekeo mmoja tu ambao Mungu anao kwa watu kama hawa. Mwelekeo huu ni upi? Mungu husukumia mbali aina hii ya watu kutoka kina cha moyo Wake. Kunazo safu mbili za maana ya kauli “sukumia mbali”. Ninawezaje kuzielezea? Ndani kabisa ya moyo, kauli hii inao mkazo wa kuchukiza, wa chuki. Na je, safu ya pili ya maana? Sasa hiyo ndiyo sehemu inayoashiria kukata tamaa dhidi ya kitu. Nyote mnajua “kukata tamaa” kunamaanisha nini, ni kweli? Kwa ufupi, kusukumia mbali kunamaanisha uamuzi na mwelekeo wa mwisho wa Mungu kwa watu wanaokuwa na mwenendo huu. Ni chuki ya kupindukia dhidi yao, maudhi, na hivyo basi uamuzi wa kuwaacha. Huu ndio uamuzi wa mwisho wa Mungu kwa mtu ambaye hajawahi kutembea katika njia ya Mungu, ambaye hajawahi kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Je, nyote mnaweza kuona sasa umuhimu wa msemo huu Niliouzungumzia?

Sasa mnaelewa mbinu ambayo Mungu hutumia kuasisi matokeo kwa binadamu? (Kupanga hali tofauti kila siku.) Kupangilia hali tofauti—hivi ndivyo watu wanavyoweza kuhisi na kugusa. Basi nia ya Mungu kwa haya yote ni nini? Nia ni kwamba Mungu anataka kumpa kila mmoja wetu majaribio katika njia tofauti, katika nyakati tofauti, na katika sehemu tofauti. Ni dhana zipi za binadamu zinazopimwa katika jaribio? Haijalishi kama wewe ni mtu wa aina ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu katika kila suala unalokabiliwa nalo, unalosikia kuhusu, unaloliona, na unalolipitia wewe binafsi au la. Kila mmoja atakabiliwa na aina ya jaribio, kwa sababu Mungu ni mwenye haki kwa watu wote. Baadhi ya watu husema: “Nimesadiki Mungu kwa miaka mingi; inakuaje kwamba sijawahi kabiliwa na jaribio?” Unahisi hujakabiliwa na jaribio kwa sababu kila wakati Mungu amepanga hali kwako wewe, hujazichukulia hali hizo kwa umakinifu, na hujataka kutembea kwa njia ya Mungu. Hivyo basi huna kamwe hisia zozote za majaribio ya Mungu. Baadhi ya watu husema: “Nimekabiliwa na majaribio machache, lakini sijui njia bora ya kufanya mazoezi. Hata ingawa nilitenda, bado sijajua kama nilisimama imara wakati huo wa majaribio.” Watu walio na aina hii ya hali bila shaka hawamo katika kundi la walio wachache. Hivyo basi ni nini kiwango ambacho Mungu hupimia watu? Ni vile tu Nilivyosema muda mfupi uliopita: Kila kitu unachofanya, kila kitu unachofikiria, na kila kitu unachoelezea—ni kumcha Mungu na kujiepusha na uovu? Hivi ndivyo inavyobainika kama wewe ni mtu unayemcha Mungu na kujiepusha na maovu au la. Hii ni dhana rahisi? Ni rahisi mno kusema, lakini ni rahisi pia kutia katika matendo? (Si rahisi mno.) Kwa nini si rahisi mno? (Kwa sababu watu hawamjui Mungu, hawajui namna ambavyo Mungu humfanya binadamu kuwa mtimilifu, na hivyo basi wanapokabiliwa na masuala hawajui namna ya kutafuta ukweli ili kutatua tatizo lao; watu lazima wapitie majaribio mbalimbali, usafishaji, kuadibu, na hukumu kabla ya kuwa na uhalisia wa kumcha Mungu.) Mnasema hivyo, lakini kulingana na vile mnavyojua, kumcha Mungu na kujiepusha na maovu kunaonekana rahisi kufanywa kwa sasa. Kwa nini Nasema hivi? Kwa sababu mmesikiliza ibada nyingi, na umepokea kiwango kingi cha kunyunyiziwa kwa uhalisia wa ukweli. Hii imewaruhusu kuelewa namna ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu kwa mujibu wa nadharia na kufikiria. Kuhusiana na matendo yenu ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu, haya yote yamekuwa yenye manufaa na kuwafanya kuhisi kwamba kitu kama hicho kinaweza kutimizika. Basi ni kwa nini katika uhalisia wa mambo watu hawajawahi kukitimiza? Hii ni kwa sababu kiini halisi cha asili ya binadamu hakimchi Mungu na kinapenda maovu. Hiyo ndiyo sababu halisi.

Kutomcha Mungu na Kutojiepusha na Maovu ni Kumpinga Mungu

Hebu tuanze kuangazia ni wapi ambapo msemo huu “kumcha Mungu na kujiepusha na maovu” ulitokea. (Kitabu cha Ayubu.) Sasa kwa vile mmetaja Ayubu, hebu tumzungumzie. Katika nyakati za Ayubu, Mungu alikuwa akishughulikia kushinda na wokovu wa binadamu? Alikuwa hafanyi hivyo, kweli? Na kuhusiana na Ayubu, ni maarifa kiwango gani alikuwa nayo kumhusu Mungu wakati huo? (Si mengi.) Je, Ayubu alikuwa na maarifa mengi au machache ya Mungu kuliko mliyo nayo ninyi sasa hivi? Kwa nini hamwezi kuthubutu kujibu? Hili ni swali rahisi sana kujibu. Machache! Hiyo ni bila shaka! Sasa hivi mnaangaliana uso kwa uso na Mungu, uso kwa macho na neno la Mungu. Maarifa yenu ya Mungu ni mengi zaidi kuliko yale ya Ayubu. Kwa nini Naleta suala hili? Kwa nini Ninaongea hivi? Ningependa kuwaelezea hoja moja, lakini kabla Sijafanya hivyo, Ningependa kuwauliza swali: Ayubu alijua machache sana kumhusu Mungu, ilhali angeweza kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Hivyo basi kwa nini watu siku hizi wanashindwa kufanya hivyo? (Wamepotoka sana.) “Wamepotoka sana”—hili ni jambo la kijuujuu linalosababisha tatizo hili, lakini siwezi kulitazama kwa namna hiyo kamwe. Mara nyingi ninyi huchukua mafundisho na maneno yanayotumiwa mara kwa mara, kama vile "upotovu mkubwa,” “kuasi dhidi ya Mungu,” “kutotii Mungu,” “kutotii,” “kutopenda ukweli,” na mnatumia vidahizo kama hivi kuelezea kiini halisi cha kila swali. Hii ni njia isiyofaa ya kufanya mazoezi. Kutumia jibu moja kuelezea maswali yaliyo na asili tofauti mara moja huibua shaka ya kuukufuru ukweli na Mungu. Sipendi kusikia aina hii ya jibu. Hebu fikiria! Hakuna yeyote kati yenu amefikiria kuhusu suala hili, lakini kila siku Mimi Ninaliona, na kila siku Mimi Ninalihisi. Hivyo basi, mnafanya, na Mimi Ninatazama. Wakati mnapolifanya, hamwezi kuhisi kiini halisi cha suala hili. Lakini wakati Ninapoliona, Ninaweza kuona kiini halisi chake, na Ninaweza kuhisi kiini chake halisi vilevile. Hivyo basi kiini hiki ni nini basi? Kwa nini watu siku hizi hawamchi Mungu na hawaambai maovu? Majibu yenu yako mbali na kuweza kueleza kiini halisi cha swali hili, na haziwezi kutatua kiini halisi cha swali hili. Hiyo ni kwa sababu kunacho chanzo hapa ambacho nyinyi hamna habari kukihusu. Chanzo hiki ni kipi? Ninajua mnataka kusikia kukihusu, hivyo basi Nitawaambia kuhusu chanzo cha swali hili.

Hapo mwanzo kabisa wa kazi ya Mungu, Alichukulia vipi binadamu? Mungu alimwokoa binadamu; Alimchukulia binadamu kama mmoja wa familia Yake, kama mlengwa wa kazi Yake, kama kile ambacho Alitaka kukishinda, kuokoa, na kile ambacho Alitaka kufanya kuwa kitimilifu. Huu ndio uliokuwa mwelekeo wa Mungu kwa binadamu mwanzoni mwa kazi Yake. Lakini mwelekeo wa binadamu kwa Mungu wakati huo ulikuwa upi? Mungu alikuwa haeleweki kwa binadamu na binadamu alimchukulia Mungu kuwa mgeni. Inaweza kusemwa kwamba mtazamo wao kwa Mungu haukuleta matokeo sahihi, na kwamba hawakuelewa wazi jinsi wanastahili kumshughulikia Mungu. Hivyo basi Alimshughulikia alivyopenda yeye, na akafanya kile alichopenda yeye. Je, binadamu alikuwa na mtazamo kuhusu Mungu? Hapo mwanzoni, binadamu hakuwa na mtazamo wowote kuhusu Mungu. Mtazamo wa binadamu kama ulivyojulikana, ulikuwa tu baadhi ya dhana na fikira kumhusu Mungu. Kile ambacho kiliingiliana na dhana za watu kilikubalika; kile ambacho hakikuingiliana kiliitikiwa juujuu, lakini katika mioyo yao watu waligongana pakubwa nacho na wakakipinga. Huu ndio uliokuwa uhusiano wa binadamu na Mungu hapo mwanzoni: Mungu alimwona binadamu kama mwanachama wa familia, ilhali binadamu alimchukulia Mungu kama mgeni. Lakini baada ya kipindi cha kazi ya Mungu, binadamu alielewa hatimaye kile ambacho Mungu alikuwa akijaribu kutimiza. Watu hatimaye walijua kwamba Mungu ndiye aliyekuwa Mungu wa kweli, na hatimaye wakajua kile ambacho binadamu angepokea kutoka kwa Mungu. Binadamu alimchukulia Mungu wakati huu kuwa nini? Binadamu alichukulia Mungu kuwa tegemeo kuu, akitumai kupokea neema, kupokea baraka, kupokea ahadi. Naye Mungu alimchukulia binadamu wakati huu kuwa nini? Mungu alimchukulia binadamu kuwa mlengwa wa ushindi Wake. Mungu alitaka kuyatumia maneno ili kumhukumu binadamu, kumjaribu binadamu, kumpa majaribio binadamu. Lakini kwa wanadamu wakati huu hasa, Mungu alikuwa kifaa ambacho angetumia kutimiza shabaha zake binafsi. Watu waliona kwamba ukweli uliotolewa na Mungu ungeweza kushinda na kuwaokoa, na kwamba walikuwa na fursa ya kupokea vitu walivyotaka kutoka kwa Mungu, hatima ambayo walikuwa wakitaka. Kwa sababu ya haya, chembechembe ya uaminifu kajitunga katika mioyo yao, na walikuwa radhi kumfuata Mungu huyu. Muda ukapita na watu wakawa na maarifa fulani ya juujuu na ya kifalsafa kuhusu Mungu. Inaweza kusemekana kwamba walikuwa wameanza “kuzoeana” zaidi na zaidi na Mungu. Neno likitamkwa na Mungu, mahubiri Yake, ukweli Aliokuwa ameutoa awali, na kazi Yake—watu walikuwa “wamezoea” zaidi na zaidi. Hivyo basi, watu walidhania kimakosa kwamba Mungu hakuwa tena mgeni, na kwamba tayari walikuwa wakitembea njia ya uwiano na Mungu. Tangu hapo mpaka sasa, watu wamesikiliza mahubiri mengi ya ukweli, na wamepitia kazi nyingi ya Mungu. Ilhali kwenye uingiliaji kati na uzuiaji wa mambo mengi tofauti na hali, watu wengi hawawezi kufikia hali ya kutia ukweli katika matendo, na hawawezi kufikia hali ya kumtosheleza Mungu. Watu wanazidi kuwa goigoi, wanazidi kuikosa imani. Wanazidi kuhisi ni kana kwamba matokeo yao binafsi hayajulikani. Hawathubutu kuwa na mawazo yoyote ya kupita kiasi, na hawatafuti kupiga hatua yoyote ya maendeleo; wanafuata tu shingo upande, wakienda mbele hatua kwa hatua. Kuhusiana na hali ya sasa ya binadamu, mwelekeo wa Mungu kwa binadamu ni upi? Tamanio tu la Mungu ni kuukabidhi ukweli huu kwa binadamu, na kutia moyoni mwa binadamu njia Yake, na kupangilia hali mbalimbali ili kujaribu binadamu katika njia tofauti. Shabaha yake ni kuweza kuchukua maneno haya, ukweli huu, na kazi Yake, na kusababisha matokeo ambapo binadamu anaweza kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Watu wengi ambao Nimewaona wanalichukua tu neno la Mungu na kuliona kuwa falsafa, kuliona kuwa barua, kuliona kuwa kanuni za kufuatwa. Wanapoendelea na shughuli zao na kuongea au kukabiliwa na majaribio, hawachukulii njia ya Mungu kama njia ambayo wanafaa kuifuata. Hali hii hasa ni kweli wakati watu wanapokabiliwa na majaribio makuu; Sijamwona yeyote ambaye alikuwa anatia katika matendo kwa mwelekeo wa kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Kwa sababu ya hili, mwelekeo wa Mungu kwa binadamu umejaa chuki na chukizo ya kupindukia. Baada ya Mungu kuwapa watu majaribio kadhaa, hata mara mia, bado hawana mwelekeo wazi wa kuonyesha bidii yao—ninataka kumcha Mungu na kujiepusha na maovu! Kwa sababu watu hawana bidii hii, na hawaonyeshi ishara kama hii, mwelekeo wa sasa wa Mungu kwao si kama ule wa hapo nyuma, Alipotoa rehema Yake, akatoa uvumilivu wake, akatoa ustahimilivu na subira yake. Badala yake, Amesikitishwa mno na binadamu. Ni nani aliyesababisha masikitiko haya? Aina hii ya mwelekeo ambao Mungu anao kwa binadamu, unamtegemea nani? Unategemea kila mtu anayemfuata Mungu. Kwenye mkondo wa miaka Yake mingi ya kazi, Mungu ametaja mahitaji mengi kwa binadamu, na kupangilia hali nyingi kwa binadamu. Lakini haijalishi ni vipi binadamu ametenda, na haijalishi ni mwelekeo upi ambao binadamu anao kwa Mungu, binadamu hawezi kutenda kwa njia wazi kulingana na shabaha ya kumcha Mungu na kujiepusha na uovu. Hivyo basi, Nitajumlisha yote haya kwa msemo mmoja, na kuweza kutumia msemo huu kuelezea kila kitu ambacho tumeweza kuzungumzia kuhusiana na ni kwa nini watu hawawezi kutembea kwa njia ya Mungu—mche Mungu na kujiepusha na maovu. Msemo huu ni upi? Msemo huu ni: Mungu humchukulia binadamu kama kifaa cha wokovu Wake, kifaa cha kazi Yake; binadamu humchukulia Mungu kama adui wake, kama tabaini yake. Je, unalielewa suala hili sasa? Kile ambacho ndicho mwelekeo wa binadamu; kile ambacho ndicho mwelekeo wa Mungu; kile ambacho ni uhusiano wa binadamu na Mungu—hivi vyote viko wazi sana sasa. Haijalishi ni kiwango kipi cha mahubiri ambayo mmeyasikiliza, yale mambo ambayo mliyoyatolea muhtasari nyinyi wenyewe—kama vile kuwa mwaminifu kwa Mungu, kumtii Mungu, kutafuta njia ya uwiano na Mungu, kutaka kuishi daima dawamu kwa ajili ya Mungu, kuishi kwa ajili ya Mungu—kwangu Mimi mambo hayo hayajumuishi kutembea kwa njia ya Mungu kwa nadhari, ambako ni kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Badala yake, ni njia mbalimbali kupitia kwazo mnaweza kufikia shabaha fulani. Ili kutimiza shabaha hizi, mnaangalia shingo upande baadhi ya taratibu. Na ni taratibu hizi hasa ambazo huwapeleka watu mbali zaidi kutoka katika njia ile ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu, na kumweka Mungu katika upinzani na binadamu kwa mara nyingine.

Swali tunalolizungumzia leo ni zito kidogo, lakini licha ya chochote bado Natumai kwamba mtakapopitia yale yote yajayo, na kwenye nyakati zijazo, mnaweza kufanya kile ambacho Nimewaambia mfanye. Msipuuze Mungu na kumchukulia Yeye kama hewa tupu, kuhisi kwamba Anakuwepo tu nyakati zile Anapokuwa Mwenye manufaa kwako, lakini wakati ule ambao humhitaji unahisi kwamba Yeye hayupo. Unaposhikilia uelewa huu katika bila ufahamu, tayari umemghadhabisha Mungu. Pengine kunao watu wanaosema: “Mimi sichukulii Mungu kama hewa tupu, mimi siku zote humwomba Mungu, siku zote mimi humtosheleza Mungu, na kila kitu ninachokifanya huwa katika ule upana na kiwango na kanuni zinazohitajika na Mungu. Bila shaka siendelei kulingana na mawazo yangu binafsi.” Ndiyo, namna ambayo unafanya mambo ni sahihi. Lakini unafikiria vipi wakati unakumbana macho kwa macho na suala? Unakuwa na matendo gani unapokabiliwa na suala? Baadhi ya watu huhisi kwamba Mungu yupo wakati wanapomwomba Yeye, na Kumsihi kuwasikiliza. Lakini wakati wanapokabiliwa na suala wanakuja na fikira zao binafsi na wanataka kuzitii. Hapa Mungu huchukuliwa kama hewa tupu. Aina hii ya hali humfanya Mungu kutokuwepo. Watu hufikiria kwamba Mungu anafaa kuwepo wakati wanapomhitaji Yeye, na wakati hawamhitaji Mungu Hafai kuwepo. Watu hufikiria kwamba kufanya mambo kulingana na mawazo yao katika matendo ya maisha ni tosha. Wanasadiki wanaweza kufanya mambo vyovyote vile wapendavyo. Wanafikiria tu kwamba hawahitaji kutafuta njia ya Mungu. Watu ambao kwa sasa wamo katika aina hii ya hali, hali hii ya namna—huoni kwamba karibu wataingia hatarini? Baadhi ya watu husema: “Haijalishi kama karibu nitaingia hatarini au la, nimesadiki kwa miaka mingi sana, na ninasadiki kwamba Mungu hataniacha kwa sababu Asingeweza kustahimili kuniacha mimi.” Watu wengine husema: “Hata tangu nilipokuwa kwenye tumbo la mama yangu, nilimsadiki Bwana, tangu hapo mpaka sasa, jumla ya miaka arubaini au hamsini hivi. Kwa mujibu wa muda, mimi ndimi nimefuzu zaidi kuokolewa na Mungu; mimi ndimi nimefuzu zaidi kuwepo. Kwenye kipindi hiki cha muda cha miongo minne au mitano, niliiacha familia yangu na kazi yangu. Nilijitolea kila kitu nilichokuwa nacho kwa Mungu, kama pesa, ardhi, anasa na muda wa familia; sijala vyakula vingi vitamu; sijafurahia vitu vingi vya kusisimua; sijatembelea sehemu nyingi za kuvutia; nimeweza hata kupitia mateso ambayo hata watu wa kawaida wasingevumilia. Kama Mungu hawezi kuniokoa mimi kwa sababu ya haya yote, basi mimi nashughulikiwa kwa njia isiyo ya haki na siwezi kuamini kwa aina hii ya Mungu.” Je, kunao watu wengi walio na aina hii ya mtazamo? (Kunao wengi sana.) Basi leo Nitawasaidia kuelewa hoja moja: Kila mmoja wa hao anayeshikilia aina hii ya maoni anachukua hatua zitakazomdhuru mwenyewe. Hii ni kwa sababu wanatumia maoni yao binafsi katika kuyafunika macho yao. Ni kufikiria kwao hasa, na hitimisho yao binafsi zinazochukua nafasi ya kiwango cha kile Mungu anahitaji kutoka kwa binadamu, ndizo zinazowashikilia dhidi ya kukubali nia za kweli za Mungu, na kuwafanya kutoweza kuhisi uwepo wa kweli wa Mungu, na kuwafanya pia kupoteza fursa yao kufanywa kuwa watimilifu na Mungu na kutokuwa na sehemu au mgao katika ahadi ya Mungu. 

Namna Ambavyo Mungu Huanzisha Matokeo Ya Binadamu na Kiwango Ambacho Hutumia Kuasisi Matokeo ya Binadamu

Kabla ya kuwa na mitazamo au hitimisho zako binafsi, unafaa kwanza kuelewa mwelekeo wa Mungu kwako, kile ambacho Mungu anafikiria, na kuamua kama kufikiria kwako ni sahihi au la. Mungu hajawahi kutumia vipimo vya muda katika kuasisi matokeo ya mtu, na Hajawahi kutumia kiwango cha mateso yaliyovumiliwa na mtu katika kuasisi matokeo yake. Basi Mungu hutumia kiwango gani katika kuasisi matokeo ya binadamu? Kutumia vipimo vya muda katika kuasisi matokeo ya binadamu—hii ndiyo inaingiliana zaidi na dhana za watu. Na pia kuna hao watu binafsi ambao mara nyingi mnawaona, wale ambao katika wakati fulani walijitolea kabisa, wakatumia muda mwingi kabisa, wakagharamika kabisa, wakateseka kabisa. Hawa ndio, kwa maoni yenu, wanaweza kuokolewa na Mungu. Kile tu ambacho watu hawa wanaonyesha, yote wanayoishi kwa kudhihirisha, ndiyo hasa dhana ya wanadamu kuhusu kiwango ambacho Mungu anaanzisha kuhusiana na matokeo ya binadamu. Bila kujali ni nini unachosadiki, Sitaorodhesha mifano hii mmoja baada ya mwingine. Nikiongea kwa ujumla, mradi tu si kiwango cha kufikiria binafsi kwa Mungu, basi kinakuja kutoka kwenye kufikiria kwa binadamu na ni dhana tu ya binadamu. Ni nini athari za kusisitiza bila mwelekeo dhana na kufikiria kwako binafsi? Bila shaka, athari inaweza kuwa tu Mungu akikusukuma mbali. Hii ni kwa sababu siku zote unaringa kuhusu sifa zako mbele ya Mungu, unashindana na Mungu, na kuleta mzozo dhidi ya Mungu, na hujaribu hata kufahamu kwa kweli kufikiria kwa Mungu, wala hujaribu kuzifahamu nia za Mungu na mwelekeo wa Mungu kwa binadamu. Kuendelea mbele hivi ni kujiheshimu kuliko yote na wala si kumheshimu Mungu. Unajisadiki; husadiki Mungu. Mungu hataki mtu wa aina hii, na Mungu hatamwokoa mtu wa aina hii. Kama huwezi kuachilia aina hii ya mtazamo, na kisha kuirekebisha mitazamo hii ya kale isiyokuwa sahihi; kama ungeweza kuendelea mbele kulingana na maagizo ya Mungu; anza kutenda njia ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu kwa sasa na kusonga mbele; kuweza kuheshimu Mungu na kumwona kuwa mkubwa katika mambo yote; usitumie ndoto zako za kibinafsi, mitazamo au imani katika kujifafanua, kumfafanua Mungu. Na badala yake, unazitafuta nia za Mungu kwa hali zote, unatimiza utambuzi na uelewa wa mwelekeo wa Mungu kwa binadamu, na unatumia kiwango cha Mungu kutosheleza Mungu—kufanya hivi kungependeza! Huku kungemaanisha karibu unaanza katika njia ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu.

Kwa sababu Mungu hatumii namna ambavyo watu hufikiria kwa njia hii au njia ile mawazo na mitazamo yao, kama kiwango cha kuanzisha matokeo ya binadamu, basi ni aina ipi ya kiwango Anayoitumia? Mungu hutumia majaribio kuanzisha matokeo ya binadamu. Kunavyo viwango viwili vya kutumia katika majaribio yanayoasisi matokeo ya binadamu: Kiwango cha kwanza ni idadi ya majaribio ambayo watu hao wanapitia, na kiwango cha pili ni matokeo ya watu hawa katika majaribu haya. Ni viashirio hivi viwili vinavyoasisi matokeo ya binadamu. Sasa tutaweza kufafanua viwango hivi viwili. 

Kwanza kabisa, unapokabiliwa na jaribio kutoka kwa Mungu (Inawezekana kwamba katika macho yako jaribio hili ni dogo sana na halifai kutajwa), Mungu atakufanya kuwa na ufahamu kabisa kwamba huu ni mkono wa Mungu juu yako, na kwamba ni Mungu ambaye amepangilia hali hizi zote kwako. Wakati kimo chako hakijakomaa, Mungu atapanga majaribio ili kuweza kukupima. Majaribio haya yatalingana na kimo chako, yale ambayo unaweza kuelewa, na yale ambayo unaweza kustahimili. Kujaribu sehemu yako gani? Kujaribu mwelekeo wako kwa Mungu. Je, mwelekeo huu ni muhimu sana? Bila shaka ni muhimu! Zaidi ya hayo, ni muhimu hasa! Kwa sababu mwelekeo huu wa binadamu ndiyo matokeo anayotaka Mungu, ndicho kitu muhimu zaidi kulingana na Mungu. Ama sivyo Mungu asingetumia jitihada Zake kwa watu kwa kujihusisha na aina hizi za kazi. Mungu hutaka kuuona mwelekeo wako kwake Yeye, kupitia kwa majaribio haya; Anataka kujua kama uko kwenye njia sahihi na Anataka kujua kama unamcha Mungu na kujiepusha na maovu. Hivyo basi, bila kujali kama unaelewa ukweli mwingi au kidogo wakati huo, bado utakabiliwa na majaribio ya Mungu, na kufuatia ongezeko lolote katika kiwango chochote cha ukweli unaouelewa, Mungu ataendelea kupangilia majaribio sawa na hayo kwako. Wakati unapokabiliwa kwa mara nyingine tena na jaribio, Mungu anataka kuona iwapo mtazamo wako, mawazo yako, na mwelekeo wako kwa Mungu umekuwa na ukuaji wowote mpaka sasa. Baadhi ya watu husema: “Kwa nini siku zote Mungu anataka kuiona mielekeo ya watu? Kwani Mungu hajaona namna wanavyouweka ukweli katika matendo? Kwa nini Atake tena kuiona mielekeo ya watu?” Huku ni kupayuka kwa upuuzi! Kwa sababu Mungu anaendelea hivi, basi nia za Mungu lazima ziwe mumohumo. Siku zote Mungu huwaangalia watu kutoka pembeni mwao, akiangalia kila neno na tendo lao, kila kitendo na kusonga kwao, na hata kila fikira na wazo lao. Kila kitu kinachowafanyikia watu: vitendo vyao vizuri, makosa yao, dhambi zao, na hata kuasi na kusaliti kwao, Mungu atazirekodi zote kama ithibati katika kuasisi matokeo yao. Kwa kadri kazi ya Mungu inavyoendelea kuimarika hatua kwa hatua, unasikia ukweli zaidi na zaidi, unakubali mambo mazuri zaidi na zaidi, taarifa nzuri, na uhalisia wa kweli. Kwenye mkondo wa mchakato huu, mahitaji ya Mungu kwako wewe yataongezeka pia. Wakati uo huo, Mungu atapanga majaribio makubwa zaidi kwako. Shabaha yake ni kuchunguza kama mwelekeo wako kwa Mungu umekomaa mpaka sasa. Bila shaka, kwenye kipindi hiki, mtazamo ambao Mungu anahitaji kwako unaingiliana na uelewa wako wa uhalisia wako wa ukweli.

Huku kimo chako kinapoendelea kuimarika kwa utaratibu, kile kiwango ambacho Mungu anahitaji kutoka kwako wewe kitaendelea kuimarika kwa utaratibu pia. Kama utakuwa hujakomaa, Mungu atakupa kiwango kidogo sana; wakati kimo chako kitakapokuwa kikubwa kidogo, Mungu atakupa kiwango cha juu zaidi kidogo. Lakini Mungu atakuwa vipi baada ya wewe kuuelewa ukweli wote? Mungu atahakikisha kuwa unakabiliana na hata majaribio makubwa zaidi. Katikati ya majaribio haya, kile Mungu anachotaka kupata, kile Mungu anachotaka kuona, ni maarifa yako ya kina zaidi ya Mungu na kumcha kwako Kwake kwa njia ya kweli. Wakati huu, mahitaji ya Mungu kwako wewe yatakuwa ya juu zaidi “makali zaidi” kuliko wakati ambapo kimo chako kilikuwa kidogo zaidi (watu huona kwamba hali hii ni kali, lakini Mungu kwa hakika Huiona kuwa ya kustahimilika). Wakati Mungu anawapa watu majaribio, ni uhalisia gani ambao Mungu anataka kuunda? Mungu anauliza kila mara kwamba watu wampe Yeye moyo wao. Baadhi ya watu watasema: “Mtu anawezaje kufanya hivyo? Natekeleza wajibu wangu, niliacha nyumba yangu na riziki yangu, niligharamika kwa sababu ya Mungu. Hii yote si mifano ya kuutoa moyo wangu kwa Mungu? Ni vipi vingine nitakavyoutoa moyo wangu kwa Mungu? Yaweza kuwa kwamba, hii si mifano ya kuutoa moyo wangu kwa Mungu? Mahitaji mahususi ya Mungu ni yapi?” Mahitaji haya ni mepesi mno. Kwa hakika, kunao baadhi ya watu ambao tayari wameitoa mioyo yao kwa Mungu katika viwango tofauti na awamu mbalimbali za majaribio yao. Lakini wengi wa watu huwa hawapi Mungu mioyo yao. Wakati Mungu anapokupa jaribio, Mungu hutaka kujua kama moyo wako uko pamoja Naye, pamoja na mwili au pamoja na Shetani. Wakati Mungu anapokupa jaribio, Mungu anataka kujua kama unasimama katika upinzani na Yeye au kama unasimama katika hali ambayo inalingana na Yeye, na kutaka kuona moyo wako kama uko na Yeye. Wakati hujakomaa na wakati wa kukabiliwa na majaribio, kiwango cha imani yako kiko chini, na huwezi kujua hasa ni nini unachohitaji ili kutosheleza nia za Mungu kwa sababu unao uelewa finyu wa ukweli. Licha ya haya yote, bado unaweza kumwomba Mungu kwa dhati na uaminifu, kuwa radhi kuutoa moyo wako kwa Mungu, kumfanya Mungu kuwa mkuu wako, na kuwa radhi kumpa Mungu yale mambo unayosadiki kuwa yenye thamani zaidi. Hii ndiyo maana ya wewe kuwa tayari umempa Mungu moyo wako. Unaposikiliza mahubiri mengi zaidi na zaidi, na kuelewa ukweli zaidi na zaidi kimo chako kitaanza kukomaa kwa utaratibu. Kiwango ambacho Mungu huhitaji kutoka kwako si sawa na kile ambacho ulikuwemo wakati ulikuwa hujakomaa; Anahitaji kiwango cha juu zaidi kuliko hicho. Wakati moyo wa binadamu unapewa Mungu kwa utaratibu, unaanza kuwa karibu zaidi na karibu zaidi na Mungu; wakati binadamu anaweza kuwa karibu na Mungu kweli, wanaanza kuwa na moyo ambao sanasana unamcha Yeye. Mungu anataka aina hii ya moyo. 

Wakati Mungu anataka kuumiliki moyo wa mtu, Atawapa majaribio mengi. Kwenye majaribio haya, kama Mungu hatauchukua moyo wa mtu huyu, wala Haoni kama mtu huyu anao mwelekeo wowote—hivi ni kusema Havioni vitu ambavyo mtu huyu anapitia au anafanya mambo kwa njia ambayo ni ya kumcha Mungu, na Haoni mwelekeo au suluhisho ambalo linajiepusha na maovu kutoka kwa mtu huyu. Kama hivi ndivyo ilivyo, basi baada ya majaribio mengi, subira ya Mungu kwa mtu huyu binafsi itaondolewa, na Hatamvumilia mtu huyu tena. Hataweza kuwapa watu kama hawa majaribio, na Hataweza tena kuwashughulikia. Basi hiyo inamaanisha nini kwa matokeo ya mtu huyu? Inamaanisha kwamba hawatakuwa na matokeo. Yawezekana kwamba mtu huyu hajafanya maovu yoyote. Yawezekana pia kwamba watu hawa hawajafanya chochote cha kukatiza au kutatiza. Yawezekana kuwa watu hawa hawajampinga Mungu waziwazi. Hata hivyo, moyo wa mtu huyu umefichwa kutoka kwa Mungu. Hawajawahi kuwa na mwelekeo na mtazamo wazi kwa Mungu, na Mungu hawezi kuona waziwazi kwamba moyo wake amekabidhiwa Yeye, na Yeye Hawezi kuona waziwazi kwamba mtu huyu anatafuta kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Mungu hana subira tena kwa watu hawa, Hatawagharamia tena, Hatatoa tena rehema Yake kwao, na Hatawafanyia kazi wao tena. Maisha ya imani ya mtu huyu katika Mungu tayari hayapo tena. Hii ni kwa sababu katika majaribio yote mengi ambayo Mungu amempa mtu huyu, Mungu hajapata matokeo Anayotaka. Hivyo basi, kunayo idadi ya watu ambao ndani yao Sijawahi kuuona mwangaza na kupata nuru kwa Roho Mtakatifu. Inawezekanaje kuona haya? Mtu wa aina hii huenda aliamini katika Mungu kwa miaka mingi, na kwenye sehemu ya juujuu wamekuwa amilifu. Wamevisoma vitabu vingi, wameyashughulikia masuala mengi, wameandika nakala nyingi, wamekuwa na ujuzi wa barua na falsafa nyingi. Hata hivyo, hakuna ukuaji wowote unaonekana kamwe, na wala kuwa na mtazamo wowote wa kuonekana kwa Mungu kutoka kwa mtu huyu, wala hakuna mwelekeo wowote wazi. Hivi ni kusema kwamba huwezi kuona moyo wa mtu huyu. Moyo wao siku zote umesetiriwa, moyo wao umefumikwa—Umefunikwa kutoka kwa Mungu, hivyo basi Mungu hajauona moyo wa kweli wa mtu huyu, Hajaona kumcha Mungu kwa mtu huyu, na hata zaidi Hajaona namna ambayo mtu huyu anatembea katika njia za Mungu. Kama mpaka sasa Mungu hajampata mtu wa aina hii, Anaweza kuwapata katika siku za usoni? Hawezi! Je, Mungu ataendelea kusukumiza mbele mambo ambayo hayawezi kupatikana? Hatafanya hivyo! Mwelekeo wa Mungu kwa watu kama hawa, hivyo basi ni nini? (Anawasukumia mbali, Hawasikilizi.) Yeye hawasikilizi! Mungu hasikilizi mtu wa aina hii; Anawasukumia mbali. Mmetia kwenye kumbukumbu maneno haya kwa haraka sana, kwa usahihi sana. Inaonekana mmeelewa kile mlichosikia!

Kunao baadhi ya watu ambao, punde wanapoanza kumfuata Mungu wao hawana ukomavu na hawajui chochote; hawaelewi nia za Mungu; hawajui pia maana ya kusadiki Mungu, kuchukua njia iliyoundwa na binadamu na inayokosewa na wengi ya kusadiki Mungu, kufuata Mungu. Wakati mtu wa aina hii anakabiliwa na majaribio hawana habari na hawajali kuhusu mwongozo na nuru ya Mungu. Hawajui maana ya kuutoa moyo wao kwa Mungu na maana ya kusimama imara wakati wa jaribio. Mungu atampa mtu huyu kiwango finyu cha muda na katika kipindi hiki, Atawaacha kuelewa jaribio la Mungu ni nini, na nia za Mungu ni nini. Baadaye mtu huyu atahitaji kuonyesha mtazamo wao. Kuhusiana na watu wale walio katika awamu hii, Mungu angali anasubiri. Kuhusiana na watu wale ambao mitazamo yao ingali inayumbayumba, wale wanaotaka kumpa Mungu mioyo yao lakini hawajawa na maridhiano ya kufanya hivyo, ambao, ingawa wameweza kutenda ukweli fulani, wakati wanapokumbwa na jaribio kuu, wanaokwepa na wanataka kukata tamaa—mwelekeo wa Mungu kwa watu kama hawa ni upi? Mungu angali bado ana matarajio kidogo kwa watu kama hawa. Matokeo yanategemea na mielekeo na utendakazi wao. Mungu anaitikia vipi kama watu si amilifu katika kuwa na maendeleo? Yeye hukata tamaa. Hii ni kwa sababu kabla Mungu hajakata tamaa kwako, tayari wewe mwenyewe umekata tamaa. Kwa hivyo, huwezi kumlaumu Mungu kwa kufanya hivyo. Ni makosa kwako kuwa na manung’uniko kwa Mungu.

Swali la Kiutendaji Huleta Aina Zote za Aibu kwa Watu

Kunayo aina nyingine ya mtu aliye na matokeo mabaya zaidi kati ya yote. Hawa ndio Nisiopenda kutaja sana. Hali si mbaya kwa sababu mtu huyu hupokea adhabu ya Mungu, au kwamba mahitaji ya Mungu kwao ni makali na wana matokeo mabaya. Badala yake, hali ni mbaya kwa sababu wanajifanyia wenyewe, kama inavyosemwa mara kwa mara: Wanajichimbia kaburi lao. Mtu kama huyu ni aina gani? Mtu huyu hatembei kwenye njia inayofaa, na matokeo yake yanafichuliwa mapema. Mungu humwona mtu wa aina hii kama lengo Lake kubwa zaidi la chuki Yake. Kama watu wanavyosema hawa ndio wa huzuni kuliko wote. Mtu wa aina hii ni mwenye shauku anapoanza kumfuata Mungu; wanalipia bei nyingi; wanayo maoni mazuri kuhusu mtazamo wa kazi ya Mungu; kufikiria kwao ni kwingi kuhusu mustakabali wao binafsi; wao hasa wanayo imani katika Mungu, wanasadiki kwamba Mungu anaweza kumfanya binadamu kuwa kamili, na kumfanya huyo binadamu kufikia hatima yenye utukufu. Ilhali kwa sababu isiyoeleweka, mtu huyu kisha hukimbia akiwa katika harakati ya kazi ya Mungu. Ni nini maana ya mtu huyu kukimbia? Maana yake ni kwamba wanatoweka bila kwaheri, bila sauti yoyote. Wanaondoka bila kutaja neno lolote. Ingawa mtu wa aina hii anadai kuwa anasadiki Mungu, huwa haweki kamwe mizizi yoyote kwenye njia ya kusadiki Mungu. Hivyo basi, haijalishi ni kwa muda upi wamesadikia, bado wanaweza kumgeuka Mungu. Baadhi ya watu huondoka ili kufanya biashara, baadhi ya watu huondoka ili kuishi maisha yao, baadhi ya watu huondoka ili kutajirika, baadhi ya watu huondoka kuoa au kuolewa, kuwa na watoto…. Miongoni mwa wale wanaondoka, kunao wanaopata shambulizi la nadhari na wanataka kurudi, na wengine wanaoendelea vibaya sana kimaisha, wanaishi maisha tu na kuyasukuma kwa miaka na miaka. Wasukuma maisha hawa wamepitia mateso mengi, na wanasadiki kwamba kuwa ulimwenguni kuna maumivu mno, na hawawezi kutenganishwa na Mungu. Wanataka kurudi nyumba ya Mungu ili kupokea tulizo, amani, furaha, na kuendelea kusadiki katika Mungu ili kukwepa janga, au kuokolewa na kupata hatima nzuri. Hii ni kwa sababu watu hawa wanasadiki kwamba upendo wa Mungu hauna mipaka, kwamba neema ya Mungu haiwezi kuisha na kwamba haiwezi kutumika yote. Wanasadiki kwamba haijalishi ni nini mtu amefanya, Mungu anafaa kumsamehe na kuvumilia maisha yao ya kale. Watu hawa wanasema mara kwa mara ya kwamba wanataka kurudi na kufanya wajibu wao. Kuna wale ambao hata hupa baadhi ya mali yao kanisa, wakitumai kwamba hii ndiyo njia yao ya kurudi katika nyumba ya Mungu. Mwelekeo wa Mungu kwa watu aina hii ni upi? Mungu anafaa kuanzisha vipi matokeo yao? Kuwa huru kuongea. (Ulifikiri kwamba Mungu angewakaribisha watu wa aina hii, lakini baada ya kusikia kwamba sasa hivi, pengine hawatakaribishwa tena.) Na wewe unafikiria vipi? (Mtu wa aina hii huja mbele ya Mungu ili matokeo yao yasije yakawa yale ya kifo. Hawafanyi hivyo kutokana na uaminifu wa kweli. Badala yake, kutokana na maarifa kwamba kazi ya Mungu itakamilika hivi karibuni, wanadanganyika kuwa watapata baraka.) Unasema kwamba mtu huyu kwa kweli hasadiki katika Mungu, na hivyo basi Mungu hawezi kumkubali? Ndivyo ilivyo? (Ndiyo.) (Uelewa wangu ni kwamba mtu wa aina hii ni yule wa kujali maslahi yake kuliko uhaki wa jambo, na kwamba hamsadiki Mungu kwa dhati.) Hajapata kumsadiki Mungu; yeye ni mtu mwenye kuangalia maslahi yake kuliko haki. Yamesemwa vizuri! Watu hawa wanaojali maslahi yao ni wale ambao kila mmoja anawachukia. Wanaenda na mkondo tu, na hawawezi kusumbuliwa ili kufanya kitu isipokuwa kama watafaidi kwa jambo hilo. Bila shaka wanastahili dharau! Je, kati ya ndugu zangu wengine kunaye anayo maoni? (Mungu hatawakubali tena kwa sababu kazi ya Mungu karibu inakamilika na sasa ndipo matokeo ya watu yanaandaliwa. Ni wakati huu ambapo watu hawa wanataka kurudi. Si kwa sababu kwa kweli wanataka kufuata ukweli; wanataka kurudi kwa sababu wanayaona majanga yakishushwa, au wanashawishiwa na mambo ya nje. Kama kweli walikuwa na moyo uliokuwa ukifuatilia ukweli, wasingewahi kukimbia wakiwa katikati ya safari.) Je, yapo maoni mengine? (Hawatakubaliwa. Kwa kweli Mungu aliwapa fursa lakini mwelekeo wao kwake Mungu ulikuwa siku zote kutomsikiliza. Bila kujali nia za mtu huyu ni zipi, na hata kama atatubu, Mungu bado hatamkubali. Hii ni kwa sababu Mungu tayari aliwapa fursa nyingi ajabu ilhali wao walionyesha mtazamo wao: Walitaka kumwacha Mungu. Hivyo basi, watakaporudi sasa, Mungu hatawakaribisha.) (Ninakubali pia kwamba Mungu hatamkaribisha mtu wa aina hii, kwa sababu kama mtu ameona njia ya kweli, akapitia kazi ya Mungu kwa kipindi kirefu kama hicho, na bado anaweza kurudi kwa ulimwengu, kurudi kwa kumbatio la Shetani, basi huu ni usaliti mkuu kwa Mungu. Licha ya hoja kwamba kiini cha Mungu ni rehema, ni upendo, inategemea ni mtu wa aina gani ambaye kiini hicho kinaelekezwa kwake. Kama mtu huyu atakuja mbele ya Mungu akitafuta faraja, kitu cha kuwekea tumaini lake, basi mtu wa aina hii kwa kweli si mtu anayemsadiki Mungu kwa dhati, na rehema za Mungu kwake zinafika hapo.) Kiini halisi cha Mungu ni rehema, kwa hivyo ni kwa nini Hampatii mtu wa aina hii rehema zaidi kidogo tu? Kwa rehema kidogo, hawapati fursa? Awali, mara nyingi ilisemekana: Mungu anamtaka kila mmoja kuokolewa, na hataki mtu yeyote kuangamia. Kama kondoo mmoja miongoni mwa kondoo mia moja atapotea, Mungu atawaacha wale kondoo tisini na tisa kumtafuta yule kondoo aliyepotea. Siku hizi, kuhusiana na mtu wa aina hii, kama ni kwa minajili ya kusadiki kwao kwa Mungu, je, Mungu anafaa kuwakaribisha na kuwapa fursa ya pili? Kwa kweli hilo si swali gumu; ni rahisi mno! Kama kwa kweli mnamtambua Mungu na mnao uelewa halisi wa Mungu, basi hamna ufafanuzi mwingi unaohitajika; hamna kukisia kwingi kunahitajika vilevile, kweli? Majibu yenu yamo katika njia sahihi, lakini bado upo umbali fulani kati yao na mwelekeo wa Mungu. 

Sasa hivi tu kulikuwepo na baadhi yenu mliokuwa na hakika kwamba Mungu asingeweza kumkubali mtu wa aina hii. Wengine hawakuwa na hakika sana kuwa Mungu anaweza kuwakubali, na huenda asiwakubali—mwelekeo huu ndio ule wa wastani; na kisha kulikuwa na wale ambao mtazamo wao ulikuwa kwamba wanatumai kwamba Mungu atamkaribisha mtu wa aina hii—huu ndio mwelekeo ule usioeleweka. Wale walio na mwelekeo hakika wanasadiki kuwa Mungu ameshughulika mpaka sasa, na shughuli Yake imekamilika, hivyo basi Mungu hahitaji kuwa mvumilivu na watu hawa, na kwamba Hatawakaribisha tena. Wale watu wa wastani wanasadiki kwamba masuala haya yanafaa kushughulikiwa kulingana na hali inayoyazunguka: Kama moyo wa mtu huyu hauwezi kutenganishwa na wa Mungu, na bado wao ni watu wanaomsadiki Mungu kwa kweli, mtu anayefuatilia ukweli, basi Mungu hafai kukumbuka udhaifu na makosa yao ya awali; Anafaa kuwasamehe, na kuwapa fursa nyingine, kuwaruhusu kurudi katika nyumba ya Mungu, na kukubali wokovu wa Mungu. Hata hivyo, kama mtu huyu atatoroka kwa mara nyingine, hapo ndipo Mungu hatataka mtu huyu na kitendo hiki hakitachukuliwa kuwa cha ukiukaji wa haki. Kunalo kundi jingine ambalo linatumaini kwamba Mungu anaweza kumkaribisha mtu huyu. Kundi hili halina uhakika sana kama Mungu anawakaribisha au la. Kama wanaamini kwamba Mungu anafaa kuwakaribisha, lakini Mungu asiwakaribishe, basi yaonekana kwamba wamepotoka kidogo na mtazamo wa Mungu. Kama watasadiki kwamba Mungu hafai kuwakaribisha, naye Mungu atokee kusema kwamba upendo Wake kwa binadamu hauna kikomo na kwamba Yuko radhi kumpa mtu fursa nyingine, basi huu si mfano wa kutojua kwa binadamu ukimulikwa waziwazi? Kwa vyovyote vile, nyinyi nyote mna mitazamo yenu binafsi. Mitazamo hii ni maarifa katika fikira zenu binafsi; ni onyesho pia ya kina cha uelewa wenu wa kweli na uelewa wenu wa nia za Mungu. Imesemwa vyema, sio? Ni jambo la kupendeza kwamba mnayo maoni katika suala hili! Lakini suala kuhusu kama maoni yenu ni sahihi au si sahihi, kunayo alama ya kiulizo. Je, nyinyi nyote hamna wasiwasi kidogo? “Basi ni gani sahihi? Siwezi kuona vizuri, na sijui hasa kile anachofikiria Mungu. Mungu hakuniambia chochote. Nawezaje kujua anachofikiria Mungu? Mtazamo wa Mungu kwake binadamu ni upendo. Kulingana na mwelekeo wa kale wa Mungu, Anafaa kumkubali mtu huyu. Lakini sina hakika kuhusu mwelekeo wa sasa wa Mungu—ninaweza kusema tu kwamba pengine Atamkaribisha mtu huyu na pengine Hatamkaribisha.” Je, waona vile jambo hili lilivyo la mzaha? Jambo hili limewakoroga. Kama hamna msimamo bora wa suala hili basi ni nini mtakachofanya endapo kanisa lenu litakumbana kwa kweli na mtu wa aina hii? Kama hamtalishughulikia kwa njia bora, basi pengine mtamkosea Mungu. Je, hamuoni kwamba suala hili ni hatari mno?

Kwa nini Ninataka kuulizia maoni yenu kuhusu kile Nilichokuwa Nazungumzia? Nataka kupima mitazamo yenu, kupima ni maarifa kiasi kipi ya Mungu mliyo nayo, ni uelewa kiasi kipi mlio nao katika nia za Mungu na mwelekeo wa Mungu. Jibu ni gani? Jibu limo kwenye mitazamo yenu. Baadhi yenu mnashikilia sana ukale, na baadhi yenu mnatumia kufikiria kwenu katika kukisia. “Kukisia” ni nini? Ni wakati ule ambao hamna wazo lolote namna ambavyo Mungu anafikiria, hivyo basi mnakuja na mawazo yasiyo na msingi kuhusu namna ambavyo Mungu anafaa kufikiria kwa namna hii au namna ile. Hamjui kwa hakika kama kukisia kwenu ni sahihi au si sahihi, na hivyo basi mnatoa mtazamo usioleweka. Mkikumbwa na hoja hii mnaona nini? Wakati wakimfuata Mungu, ni nadra sana kwa watu kutilia maanani makusudi ya Mungu, na ni nadra wao kutilia maanani mawazo ya Mungu na mtazamo Wake kwa wanadamu. Watu hawaelewi fikira za Mungu, kwa hivyo mnapoulizwa maswali yanayohusisha nia za Mungu, yanayohusisha tabia ya Mungu, mnaingia katika hali ya kutokuwa na hakika; mnakuwa kwa kweli hamna uhakika, na mnakisia au kubahatisha. Mwelekeo huu ni upi? Unathibitisha hoja hii: kwamba watu wengi wanaomwamini Mungu wanamchukulia kuwa kifungo cha hewa tupu na kama kitu kinachoonekana kuishi dakika moja na hakipo tena dakika ifuatayo. Kwa nini Nasema hivyo? Kwa sababu kila wakati mnapokumbwa na suala, hamzijui nia za Mungu. Kwa nini hamzijui? Si kwamba hamzijui tu kwa sasa. Badala yake kuanzia mwanzo hadi mwisho hamjui mwelekeo wa Mungu katika suala hili. Kwenye nyakati zile ambazo huwezi kuona na hujui mwelekeo wa Mungu, umewahi kuutafakaria? Umeutafuta? Umewasiliana ili kuupata? La! Hii inathibitisha hoja: Mungu unayemsadiki na Mungu wa kweli hawajaunganika. Wewe, unayemsadiki Mungu, unafikiria Mungu kuhusu mapenzi yako, unafikiria tu kuhusu mapenzi ya kiongozi wako, na unafikiria tu yale mambo ya juujuu na maana ya kifalsafa ya neno la Mungu, lakini hujaribu kwa kweli kujua na kutafuta mapenzi ya Mungu kamwe. Sivyo ndivyo hali ilivyo? Kiini halisi cha suala hili hakipendezi! Kwa miaka na mikaka Nimeona watu wanaomsadiki Mungu. Kusadiki huku kunachukua mfumo gani? Baadhi ya watu wanasadiki katika Mungu ni kana kwamba Yeye ni hewa tupu. Watu hawa hawana majibu ya maswali kuhusu uwepo wa Mungu kwa sababu hawawezi kuhisi au kuwa na ufahamu uwepo au kutokuwepo kwa Mungu, sikuambii hata kuuona waziwazi au kuuelewa. Kwa nadharia yao, watu hawa wanafikiria kwamba Mungu hayupo. Baadhi wanasadiki katika Mungu ni kana kwamba Yeye ni binadamu. Watu hawa wanasadiki kwamba Mungu hawezi kufanya mambo yale ambayo wao hawawezi kufanya, na kwamba Mungu anafaa kufikiria namna wanavyofikiria. Ufafanuzi wa mtu huyu kuhusu Mungu ni “mtu asiyeonekana na asiyegusika.” Kunalo pia kundi la watu wanaosadiki katika Mungu kana kwamba Yeye ni kikaragosi; watu hawa wanasadiki kwamba Mungu hana hisia. Wanafikiria kwamba Mungu ni sanamu ya matope, na kwamba wanapokabiliwa na jambo, Mungu hana mwelekeo, hana mtazamo, hana mawazo; Anatawaliwa na binadamu. Watu wanasadiki tu wanavyotaka kusadiki. Wakimfanya kuwa mkubwa, Yeye ni mkubwa; wakimfanya kuwa mdogo, Yeye ni mdogo. Wakati wanapotenda dhambi na wanahitaji rehema ya Mungu, wanahitaji uvumilivu wa Mungu, wanahitaji upendo wa Mungu, basi Mungu anafaa kutoa rehema Zake. Watu hao wanafikiria kuhusu Mungu kwenye akili zao binafsi na kumfanya Mungu kutimiza mahitaji yao na kutosheleza matamanio yao yote. Haijalishi ni lini na ni wapi, na haijalishi hata mtu huyu anafanya nini, watakubali mvuto huu katika matendo yao kwa Mungu na kusadiki kwao katika Mungu. Kuna hata wale wanaosadiki katika Mungu kuweza kuwaokoa baada kuikera tabia ya Mungu. Hii ni kwa sababu wanasadiki kuwa upendo wa Mungu hauna mipaka, tabia ya Mungu ni haki, na kwamba bila kujali ni vipi ambavyo watu wanakosea Mungu, Hatakumbuka chochote. Kwa sababu makosa ya binadamu, dhambi za binadamu na kutotii kwa binadamu ni maonyesho ya mara moja ya tabia ya mtu huyo, Mungu atawapatia watu fursa, kuvumilia na kuwa na subira nao. Mungu angali atawapenda kama awali. Kwa hivyo tumaini la wokovu wao lingali kubwa. Kwa hakika, haijalishi ni vipi mtu anavyosadiki Mungu, mradi tu hafuatilii ukweli basi Mungu anashikilia mwelekeo mbaya kwake. Hii ni sababu wakati unamsadiki Mungu, labda unakithamini kile kitabu cha neno la Mungu unakichambua kila siku, unakisoma kila siku, lakini unamweka Mungu halisi pembeni, unamchukulia kama hewa tupu, unamchukulia Yeye kama mtu, na baadhi yenu mnamchukulia kuwa kikaragosi. Kwa nini Nasema hivi? Kwa sababu kutokana na vile Ninavyoona, licha ya kama unakabiliwa na suala au kukumbana na hali, yale mambo yanayopatikana katika nadharia yako, yale mambo ambayo yameimarishwa ndani kwa ndani—hakuna kati ya haya ambayo yana uunganisho wa neno la Mungu au yanafuatilia ukweli. Unajua tu kile wewe mwenyewe unatafuta, maoni yako wewe binafsi, na kisha mawazo yako binafsi, mitazamo yako binafsi inalazimishiwa Mungu. Inakuwa mitazamo ya Mungu. Akilini mwako hii inakuja kuwa mitazamo ya Mungu, na unafanya hii mitazamo kuwa viwango ambavyo unavishikilia bila kutetereka. Kwa muda, kuendelea namna hii kunakufanya uwe mbali na mbali kutoka kwa Mungu.

Elewa Mwelekeo wa Mungu na Utupilie Mbali Dhana zote Potovu Kumhusu Mungu

Mungu huyu ambaye kwa sasa mnasadiki, mmewahi kufikiria kuhusu Yeye ni Mungu wa aina gani? Anapomwona mtu mwovu akifanya mambo maovu, je Anayachukia? (Anayachukia.) Anapoona makosa ya mtu asiyejua, mwelekeo Wake ni upi? (Huzuni.) Anapowaona watu wakiiba sadaka Yake, mwelekeo Wake ni upi? (Anawachukia.) Haya yote yako wazi, sivyo? Anapoona mtu akiwa mzembe katika kusadiki kwake Mungu, na mtu huyo akikosa kufuatilia ukweli kwa namna yoyote, mwelekeo wa Mungu ni upi? Bado hamjaelewa jambo hili, sivyo? Uzembe ni mwelekeo ambao si dhambi, na humkosei Mungu. Watu husadiki kwamba haupaswi kuchukuliwa kama kosa. Basi mnafikiria mwelekeo wa Mungu ni nini? (Hayuko radhi kujibu swali hili.) Hayuko radhi kulijibu—mwelekeo huu ni upi? Ni kwamba Mungu huwa anawadharau watu hawa, anawabeza watu hawa! Mungu hushughulikia watu hawa kwa kutowathamini. Mtazamo wake ni kuwaweka pembeni, kutojihusisha na kazi yoyote inayowahusu, ikiwemo kuwapa nuru, mwangaza, kuwarudi au kuwafundisha nidhamu. Mtu wa aina hii kwa kweli si wa thamani kwa kazi ya Mungu. Mwelekeo wa Mungu kwa watu wanaozikera tabia Yake, na kuzikosea amri Zake za kiutawala ni upi? Chuki mno kwa kupindukia! Kwa kweli Mungu hupandwa na hasira kali na watu ambao hawaghairi kuhusu kukera tabia Yake! “Hasira Kali” ni hisia tu, hali ya moyo; haiwezi kuwakilisha mwelekeo kamili. Lakini hisia hii, hali hii ya moyo, itasababisha matokeo kwa mtu huyu: Itamjaza Mungu na chukizo la kupindukia! Ni nini matokeo ya kuchukia huku kwa kupindukia? Ni kwamba Mungu atamweka pembeni mtu huyu, na kutomwitikia kwa sasa. Kisha atasubiri sasa kuwashughulikia “baada ya msimu wa kupukutika kwa majani.” Hali hii inaashiria nini? Mtu huyu angali anayo matokeo? Mungu hakuwahi kunuia kumpa mtu wa aina hii matokeo! Hivyo basi si jambo la kawaida endapo Mungu kwa sasa hamwitikii mtu wa aina hii? (Ndiyo.) Mtu wa aina hii anafaa kujitayarisha vipi sasa? Wanafaa kujitayarisha kukabiliana na zile athari mbaya zilizosababishwa na tabia zao na maovu waliofanya. Huu ndio mwitikio wa Mungu kwa mtu wa aina hii. Hivyo basi Nasema waziwazi kwa mtu wa aina hii: Usishikilie imani za uwongo tena, na usijihusishe katika kufikiria makuu tena. Mungu hatavumilia watu siku zote bila kikomo; Hatastahimili dhambi zao au kutotii kwao bila kukoma. Baadhi ya watu watasema: “Nimeweza pia kuona watu wachache kama hawa. Wanapoomba wanaguswa hasa na Mungu, na wanalia kwa machungu. Kwa kawaida wao pia wanakuwa na furaha sana; wanaonekana kuwa na uwepo wa Mungu, na mwongozo wa Mungu.” Usiseme huo upuzi! Kulia kwa machungu si lazima iwe kwamba umeguswa na Mungu au unao uwepo wa Mungu, acha hata mwongozo wa Mungu. Kama watu watamghadhabisha Mungu, je, bado Mungu atawaongoza? Nikiongea kwa ujumla, wakati Mungu ameamua kumwondoa mtu, kuwaacha watu hao, tayari mtu huyo hana matokeo. Haijalishi ni vipi wanavyohisi kutosheka kujihusu wao wenyewe wakati wanapoomba, na imani kiwango kipi walichonacho katika Mungu mioyoni mwao; tayari hii si muhimu. Kitu cha muhimu ni kwamba Mungu hahitaji aina hii ya imani kwamba Mungu tayari amemsukumia mbali mtu huyu. Namna ya kuwashughulikia baadaye pia si muhimu. Kilicho muhimu ni kwamba katika muda ule ambao mtu huyu atamghadhabisha Mungu, matokeo yao tayari yameanzishwa. Kama Mungu ameamua kutomwokoa mtu wa aina hii, basi ataachwa na kuadhibiwa. Huu ndio mwelekeo wa Mungu.

Ingawa sehemu ya kiini halisi cha Mungu ni upendo, na Anaitoa rehema yake kwa kila mtu, watu hupuuza na kusahau hoja kwamba kiini Chake halisi ni heshima vilevile. Kwamba Anao upendo haimaanishi kwamba watu wanaweza kumkosea Yeye wapendavyo na kwamba Yeye hana hisia zozote, au mijibizo yoyote. Kwamba Anayo rehema haimaanishi kwamba Hana kanuni zozote kuhusiana na namna Anavyoshughulikia watu. Mungu yu hai; kwa kweli Yupo. Yeye si kikaragosi kilichofikiriwa au kitu kingine tu. Kwa sababu Yeye yupo, tunafaa kusikiliza kwa makini sauti ya moyo Wake siku zote, kutilia makini mwelekeo Wake, na kuzielewa hisia Zake. Hatufai kutumia kufikiria kwa watu ili kumfafanua Mungu, na hatufai kulazimisha fikira na matamanio ya watu kwa Mungu, kumfanya Mungu kutumia mtindo na fikira za binadamu katika namna Anavyomshughulikia binadamu. Ukifanya hivyo, basi unamghadhabisha Mungu, unaijaribu hasira ya Mungu, na unapinga heshima ya Mungu! Hivyo basi, baada ya kuelewa ukali na uzito wa suala hili, Ninasihi kila mmoja wenu mlio hapa kuwa makini na wenye busara katika vitendo vyenu. Kuwa makini na wenye busara katika kuongea kwenu. Na kuhusiana na namna mnavyoshughulikia Mungu, mnapokuwa makini zaidi na wenye busara zaidi, ndivyo ilivyo bora zaidi! Wakati huelewi mwelekeo wa Mungu ni nini, usizungumze kwa uzembe, usiwe mzembe katika vitendo vyako, na usipachike majina ovyo ovyo. Na hata zaidi, usikimbilie hitimisho kiholela. Badala yake, unafaa kusubiri na kutafuta; hili pia ndilo dhihirisho la kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Kama unaweza kutimiza hoja hii kati ya zote, na kumiliki mwelekeo huu kati ya yote, basi Mungu hatakulaumu wewe kwa upumbavu wako, kutojua kwako, na ukosefu wa kuelewa kwa sababu zinazosababisha vitu. Badala yake, kutokana na hofu yako ya kumkosea Mungu, heshima yako kwa nia za Mungu, na mwelekeo wako wa kuwa radhi kumtii Yeye, Mungu atakukumbuka, atakuongoza na kukuangaza wewe, au kustahimili kutokuwa mkomavu kwako na kutojua kwako. Kinyume chake, endapo mwelekeo wako kwake Yeye utakuwa usioheshimu—kuhukumu Mungu kiholela, kukisia kiholela, na kufafanua maana ya Mungu—Mungu atakupa hukumu, nidhamu, au hata adhabu; au Atakupa taarifa. Pengine kauli hii inahusisha matokeo yako. Hivyo basi, Ningali bado nataka kutilia mkazo jambo hili kwa mara nyingine: Unapaswa uwe makini na mwenye busara katika kila kitu kinachotoka kwa Mungu. Usiongee kwa uzembe, na usiwe mzembe katika matendo yako. Kabla ya kusema chochote, unafaa kufikiria: Je, kufanya hivi kutamghadhabisha Mungu? Kufanya hivi ni kumcha Mungu? Hata katika masuala mepesi, bado unafaa kujaribu kuelewa hakika maswali haya, yafikirie kwa kweli. Kama unaweza kwa kweli kutenda haya kulingana na kanuni hizi kila pahali, katika hali zote, katika vitu vyoye, nyakati zote, na kushikilia mtazamo wa aina hiyo hasa wakati huelewi kitu basi Mungu siku zote atakuongoza wewe, na kukupa na hata njia ya kufuata. Bila kujali ni nini ambacho watu wanaonyesha, Mungu anaona yote waziwazi, dhahiri, na Atakupa utathmini sahihi na unaofaa kwa maonyesho haya. Baada ya kupitia jaribio la mwisho, Mungu atachukua tabia yako yote na kuijumlisha ili kuasisi matokeo yako. Matokeo haya yatashawishi kila mmoja bila shaka lolote. Kile ambacho Ningependa kuwaambia ni kwamba kila kitendo chenu, kila hatua yenu, na kila fikira yenu vyote vitaamua majaliwa yenu.

Ni Nani Hupanga Matokeo ya Binadamu

Kunalo jambo jingine muhimu zaidi, na hilo ni mwelekeo wenu kwa Mungu. Mwelekeo huu ni muhimu sana! Huamua kama hatimaye mtatembea kuelekea katika maangamizo, au kwenye hatima nzuri na ya kupendeza ambayo Mungu amewatayarishia. Katika Enzi ya Ufalme, Mungu tayari amefanya kazi kwa zaidi ya miaka 20 na kwenye kipindi cha miaka hii 20 pengine mioyo yenu imekuwa na tashwishi kuhusu utendakazi wenu. Hata hivyo, katika moyo wa Mungu, Ameweka rekodi halisi na ya kweli kwa kila mmoja wenu. Kuanzia wakati ule ambao kila mtu anaanza kumfuata Yeye na kusikiliza mahubiri Yake, kuelewa zaidi na zaidi kuhusu ukweli, hadi pale ambapo wanatekeleza wajibu wao—Mungu anayo rekodi ya kila mojawapo ya maonyesho haya. Wakati mtu anapofanya wajibu wake, wakati anapokabiliwa na kila aina ya hali, kila aina ya majaribio, mwelekeo wa mtu huyo ni upi? Wanatenda kazi vipi? Wanahisi vipi kwa Mungu katika mioyo yao? … Mungu ameweka rekodi ya yote haya, rekodi yote kwa hakika. Pengine kutokana na mtazamo wenu, masuala haya yanakanganya. Hata hivyo, kutoka pale ambapo Mungu yupo, yote yako wazi kabisa, na hakuna hata dalili yoyote ya kutokuwa wazi. Hili ni suala linalohusisha matokeo ya kila mmoja, na majaliwa yao na matarajio yao ya siku za baadaye vilevile. Hata zaidi, hapa ndipo ambapo Mungu anatumia jitihada Zake zote alizomakinikia. Hivyo basi Mungu hathubutu kuipuuza hata kidogo, na hatavumilia kutomakinika kokote. Mungu anarekodi haya yote kuhusu wanadamu, anarekodi mambo kuhusu mkondo mzima wa binadamu anayefuata Mungu, kuanzia mwanzo hadi mwisho. Mwelekeo wako kwa Mungu wakati huu utaamua hatima yako. Je, haya si kweli? Kutoka hapo mpaka sasa, mnasadiki kwamba Mungu ni mwenye haki? Vitendo vya Mungu vinafaa? Bado mnayo picha yoyote ya Mungu vichwani mwenu? (La.) Basi mnasema kwamba matokeo ya binadamu ni kwa ajili ya Mungu kuweza kupanga au kwa ajili ya binadamu mwenyewe kupanga? (Ni kwa Mungu kupanga.) Ni nani basi anayeyapanga? (Mungu.) Hamna hakika, sivyo? Ndugu kutoka makanisa ya Hong Kong, ongeeni—ni nani anayeyapanga? (Binadamu anayapanga mwenyewe.) Mwanadamu anayapanga? Hivyo basi haimaanishi kwamba haina chochote kuhusu Mungu? Ndugu kutoka Korea Kusini, ongeeni. (Mungu huanzisha matokeo ya binadamu kutokana na hatua na vitendo vyake vyote na kutokana pia na njia wanayotembelea.) Hili ni jibu halisi sana. Kunayo hoja hapa ambayo lazima Niwafahamishe nyinyi: Kwenye mkondo wa kazi ya wokovu wa Mungu, Yeye huweka kiwango kwa binadamu. Kiwango hiki ni kwamba binadamu anaweza kutii neno la Mungu, na kutembea kwa njia ya Mungu. Ndicho kiwango kinachotumika kupima matokeo ya binadamu. Kama utafanya mazoezi kwa mujibu wa kiwango hiki cha Mungu, basi unaweza kupata matokeo mazuri; kama hutafanya hivyo, basi huwezi kupokea matokeo mazuri. Basi ni nani unayesema kwamba anayapanga matokeo haya? Si Mungu pekee anayeyapanga, lakini badala yake Mungu na binadamu pamoja. Hiyo ni sahihi? (Ndiyo.) Kwa nini hivyo? Kwa sababu ni Mungu ambaye anataka kujishughulisha na kujihusisha katika kazi ya wokovu wa wanadamu, na kutayarisha hatima nzuri kwa ajili ya binadamu; binadamu ndiye mlengwa wa kazi ya Mungu, na matokeo haya, hatima hii, ndiyo ambayo Mungu humtayarishia binadamu. Kama kusingekuwa na kilengwa cha kazi Yake, basi Mungu asingehitaji kazi hii; kama Mungu asingefanya kazi hii, basi binadamu asingekuwa na fursa ya wokovu. Binadamu ndiye mlengwa wa wokovu, na ingawa binadamu yumo kwenye upande wa kimya katika mchakato huu, ni mwelekeo wa upande huu ambao unaamua kama Mungu atafanikiwa katika kazi Yake ya kuwaokoa wanadamu au la. Kama si mwongozo ambao Mungu anakupa wewe, basi usingejua kiwango Chake, na usingekuwa na lengo lolote. Kama unacho kiwango hiki, lengo hili, ilhali hushirikiani, hulitilii kwenye matendo, hulipii gharama, basi bado hutapokea matokeo haya. Kwa sababu hii, Ninasema kwamba matokeo haya hayawezi kutenganishwa na Mungu, na pia hayawezi kutenganishwa na binadamu. Na sasa unaweza kujua ni nani anayepanga matokeo ya binadamu. 

Watu Huishia Kumfafanua Mungu Kutokana na Uzoefu Wao

Wakati wa kuwasilisha mada ya kumjua Mungu, mmegundua kitu? Mmegundua kwamba mwelekeo wa sasa wa Mungu umepitia mabadiliko? Je, mwelekeo wa Mungu kwa wanadamu hauwezi kubadilika? Je, siku zote Mungu atavumilia hivi, huku akimpa upendo Wake wote na rehema kwa binadamu bila kikomo? Suala hili pia linahusu kiini halisi cha Mungu. Hebu turejelee swali la yule mtoto wa kiume mbadhirifu kama aitwavyo kutoka awali. Baada ya swali hili kuulizwa, majibu yenu hayakuwa wazi sana. Kwa maneno mengine, bado hamwelewi vizuri nia za Mungu. Punde tu watu wanapojua kwamba Mungu anawapenda wanadamu, wanamfafanua Mungu kama ishara ya upendo: Haijalishi kile wanachofanya watu, haijalishi namna wanavyotenda mambo, haijalishi vipi wanavyomshughulikia Mungu na haijalishi ni vipi wasivyotii, hakuna chochote kinachojalisha kwa sababu Mungu ni upendo na upendo wa Mungu hauna mipaka na haupimiki. Mungu anao upendo, hivyo basi Anaweza kuvumilia watu; Mungu anao upendo, hivyo basi Anaweza kuwa mwenye rehema kwa watu, mwenye rehema kwa kutokomaa kwao, mwenye rehema kwa kutojua kwao, na mwenye rehema kwa kutotii kwao. Hivi ndivyo ilivyo kwa kweli? Kwa baadhi ya watu, wakati wamepitia subira ya Mungu mara moja, au mara chache, watashughulikia suala hili kama mtaji katika uelewa wao wa Mungu, wakisadiki kwamba Mungu atakuwa mara moja na milele mwenye subira kwao, atakuwa mwenye rehema kwao, na kwenye mkondo wa maisha yao watachukua subira ya Mungu na kuichukulia kama kiwango cha ni vipi ambavyo Mungu anawashughulikia. Kunao pia watu ambao, wakati wamepitia uvumilivu wa Mungu mara moja, daima watamfafanua Mungu kuwa uvumilivu, na uvumilivu huu hauna mipaka, hauna masharti, na hata usio na kanuni zozote. Je, kusadiki huku ni sahihi? Kila wakati mambo kuhusu kiini cha Mungu au tabia ya Mungu yanapozungumziwa, mwaonekana mmekanganywa mno. Kuwaona mkiwa hivi kunanifanya Mimi kuwa na wasiwasi. Mmeusikia mambo mengi ya ukweli kuhusiana na kiini halisi cha Mungu; mmeweza pia kusikiliza mada mengi kuhusiana na tabia ya Mungu. Hata hivyo, katika akili zenu masuala haya, na ukweli wa dhana hizi, ni kumbukumbu tu kutokana na nadharia na maneno yaliyoandikwa. Hakuna kati yenu anaweza kupitia kile ambacho tabia ya Mungu inamaanisha katika maisha yenu halisi, wala hamwezi kuona tu tabia ya Mungu ni nini. Hivyo basi, nyote mmechanganyikiwa katika kusadiki kwenu, nyote mnasadiki bila kujua, hadi kufikia kiwango ambacho mnao mwelekeo usiofaa kwa Mungu, kwamba mnamweka pembeni. Mwelekeo kama huu kwa Mungu unawaongoza wapi? Mnaongozwa katika hali ya kutoa hitimisho siku zote kuhusu Mungu. Punde unapopata maarifa kidogo, unahisi umetosheka kweli, unahisi ni kana kwamba umempokea Mungu kwa uzima Wake wote. Baadaye unahitimisha kwamba hivi ndivyo Mungu Alivyo, na humruhusu kuendelea mbele na shughuli Zake kwa furaha zaidi. Na kila Mungu anapofanya jambo jipya, hukubali kwamba Yeye ni Mungu. Siku moja, wakati Mungu atakaposema: “Simpendi binadamu tena; Sitoi rehema kwa binadamu tena; Sina uvumilivu au subira yoyote kwa binadamu tena; Nimejaa chuki na uhasama kupindukia kwa binadamu,” watu watakinzana na aina hii ya taarifa kutoka kwenye ndani ya mioyo yao. Baadhi yao wataweza hata kusema: “Wewe si Mungu wangu tena; Wewe si Mungu ninayetaka kufuata tena. Kama hivi ndivyo Unavyosema, basi Hujafuzu tena kuwa Mungu wangu, na sitaki kuendelea kukufuata Wewe. Kama Hunipi rehema, hunipi upendo, hunipi uvumilivu, basi nami sitakufuata Wewe tena. Kama Utakuwa mvumilivu tu kwangu bila kikomo, utakuwa mwenye subira kwangu mimi, na kuniruhusu mimi kuona kwamba Wewe ni upendo, kwamba Wewe ni subira, kwamba Wewe ni uvumilivu, hapo tu ndipo nitakapoweza kukufuata Wewe, na hapo tu ndipo nitakapoweza kuwa na ujasiri kukufuata mpaka mwisho. Kwa sababu ninapata subira na rehema Yako, kutotii kwangu na dhambi zangu zinaweza kusamehewa bila kikomo, kuondolewa bila kikomo, na ninaweza kutenda dhambi wakati wowote na mahali popote, kutubu na kusamehewa wakati wowote na mahali popote, na kukughadhabisha wakati wowote na mahali popote. Hufai kuwa na fikira au hitimisho Zako binafsi kuhusiana na mimi.” Ingawa huenda usifikirie kuhusu aina hii ya swali kwa namna ya kibinafsi na ya kufahamu kama hiyo, kila unapomchukulia Mungu kuwa zana ya dhambi zako kusamehewa na kifaa cha kutumika cha kupata hatima nzuri, tayari unamweka kwa njia isiyoeleweka Mungu aliye hai na katika hali ya kukupinga wewe, kuwa adui yako. Hivi ndivyo Ninavyoona. Unaweza kuendelea kusema, “Ninasadiki Mungu”; “Ninafuatilia ukweli”; “Ninataka kubadilisha tabia yangu”; “Ninataka kuwa huru dhidi ya ushawishi wa giza”; “Ninataka kumtosheleza Mungu”; “Nataka kumtii Mungu”; “Ninataka kuwa mwaminifu kwa Mungu, na kufanya wajibu wangu vizuri”; na kadhalika. Hata hivyo; haijalishi ni vipi utakavyosema kinasikika kuwa kizuri, haijalishi ni nadharia kiasi kipi unayojua, haijalishi ni vipi nadharia hiyo inavyovutia, ni vipi nadharia hiyo ilivyo na heshima, hoja ya mambo ni kwamba kunao wengi wenu ambao tayari wamejifunza namna ya kutumia taratibu, falsafa, nadharia mlizojifunza katika kuhitimisha mambo kuhusu Mungu, na kumweka yeye katika upinzani na nyinyi wenyewe kwa njia ambayo ni ya kimaumbile kabisa. Ingawa umejifunza barua na kujifunza falsafa, bado hujaingia kwa hakika katika uhalisia wa ukweli, hivyo basi ni vigumu sana kwako kuwa karibu na Mungu, kumjua Mungu, na kumwelewa Mungu. Hali hii inasikitisha!

Niliiona picha hii kwenye video: Akina dada wachache walikuwa wameshikilia kitabu cha Neno Laonekana katika Mwili, na walikuwa wamekishikilia juu sana. Walikuwa wamekishikilia kitabu hiki kikiwa katikati yao, na juu zaidi kuliko vichwa vyao. Ingawa hii ni picha tu, kile kilichoamshwa ndani Yangu si picha. Badala yake, hiyo picha ilinifanya kufikiria kwamba kile ambacho kila mtu hushikilia juu angani kwenye mioyo yao si neno la Mungu, lakini ni kitabu cha neno la Mungu. Hili ni suala la kusikitisha moyo sana. Njia hii ya kutenda mambo si njia kwa kweli ya kumshikilia Mungu kwa heshima. Ni kwa sababu hammwelewi Mungu kiasi cha kwamba swali wazi, swali dogo sana, linawafanya kuja na mawazo yenu binafsi. Wakati Ninapowauliza maswali, wakati Ninapomakinika na ninyi, mnajibu kwa kubahatisha na kwa kutumia kufikiria kwenu binafsi; baadhi yenu hata huchukua sauti ya shaka na kuuliza tena swali hilo kwangu. Hii inathibitisha hata waziwazi kwangu Mimi kwamba yule Mungu mnayemsadiki si Mungu wa kweli. Baada ya kulisoma neno la Mungu kwa miaka mingi sana, mnalitumia neno la Mungu, kutumia kazi ya Mungu, na falsafa nyingi zaidi katika kuhitimisha mengi kuhusu Mungu kwa mara nyingine. Aidha, hamjawahi kujaribu kumwelewa Mungu; hamjawahi kujaribu kupata kuelewa nia za Mungu; hufanyi jaribio la kuelewa mwelekeo wa Mungu kwa binadamu ni nini; au ni vipi ambavyo Mungu anafikiria, kwa nini Anayo huzuni, kwa nini Anayo ghadhabu, kwa nini Yeye husukumia watu mbali, na maswali mengine kama hayo. Na kwa kuongezea hayo, watu wengi zaidi wanasadiki kwamba Mungu siku zote amekuwa kimya kwa sababu Anaangalia tu vitendo vya wanadamu, kwa sababu Hana mwelekeo wowote kwao, wala Hana fikira zozote Zake binafsi. Kundi jingine linasukumiza mbele zaidi suala hili. Watu hawa wanaamini kwamba Mungu hatamki neno kwa sababu Amekubali, Mungu hatamki neno kwa sababu Anasubiria, Mungu hatamki neno kwa sababu Hana mwelekeo, kwa sababu mwelekeo wa Mungu tayari umefafanuliwa kwa kina ndani ya vitabu, tayari umeelezewa kwa uzima wake kwa wanadamu, na hauhitajiki kurudiwa kwa watu mara kwa mara. Ingawa Mungu yuko kimya, bado Anao mwelekeo, anao mtazamo, na anacho kiwango ambacho Anahitaji kutoka kwa watu. Ingawa watu hawajaribu kumwelewa Yeye, na hawajaribu kumtafuta Yeye, mwelekeo Wake uko wazi sana. Fikiria mtu ambaye aliwahi kumfuata Mungu kwa shauku, lakini wakati fulani akaacha kumfuata Yeye na akaondoka. Mtu huyu akitaka kurudi sasa, jambo la kushangaza ni kwamba, hamjui mtazamo wa Mungu utakuwa upi, na mwelekeo wa Mungu utakuwa upi. Hili si jambo ovyo? Kwa hakika, hili ni suala ambalo kwa kiasi fulani ni la juujuu. Kama kweli mngeelewa moyo wa Mungu, mngejua mwelekeo Wake kwa mtu wa aina hii, na msingelitoa jibu la juujuu. Kwa sababu hamjui, Niruhusu kuwafafanulia pale msipoelewa.

Mwelekeo wa Mungu kwa Wale Wanaotoroka Wakati Kazi Yake Inaendelea

Utampata mtu wa aina hii kila pahali: Baada ya kuwa na hakika kuhusu njia ya Mungu, kwa sababu mbalimbali, wanaondoka kimyakimya bila ya neno la kwaheri na kufanya chochote kile ambacho moyo wao unatamani. Huku haya yakiendelea, hatutaingilia kwa nini mtu huyu anaondoka. Kwanza tutaangalia mwelekeo wa Mungu ni upi kwa mtu wa aina hii. Iko wazi sana! Tangu muda ule ambao mtu huyu huondoka, machoni mwa Mungu, kile kipindi cha imani yao kimekwisha. Si mtu huyu aliyekimaliza, bali ni Mungu. Kwamba mtu huyu alimwacha Mungu inamaanisha kwamba tayari amemkataa Mungu, kwamba tayari hamtaki Mungu. Inamaanisha kwamba tayari hakubali wokovu wa Mungu. Kwa sababu mtu huyu hamtaki Mungu, Mungu naye anaweza bado kumtaka? Aidha wakati mtu huyu anao mwelekeo huu, mtazamo huu, na anayo azma ya kumwacha Mungu, tayari ameikera tabia ya Mungu. Hata ingawa hawakujipata wakiwa na hasira na wakalaani Mungu, hata ingawa hawakujihusisha katika uovu wowote au tabia au utovu wa nidhamu, na hata ingawa mtu huyu hafikirii: Kama kutawahi kuwepo na siku nitakapokuwa nimeshiba anasa zangu kwa nje, au nitakapokuwa bado nahitaji kitu kutoka kwa Mungu, nitarudi. Au kama Mungu ataniita, nitarudi. Au wanasema: Kama nitajeruhiwa kwa nje, nikiuona ulimwengu wa nje una giza sana na una maovu sana na sitaki tena kujishirikisha nao, nitarudi kwa Mungu. Hata ingawa mtu huyu amepiga hesabu katika akili zake ni wakati gani anarudi, hata ingawa wanauacha mlango ukiwa wazi wa kurudi kwao, hawatambui kwamba bila kujali ni namna gani wanavyofikiria na namna gani wanavyopanga, hii ni ndoto tu. Kosa lao kubwa zaidi ni kutokuwa wazi kuhusu namna ambavyo Mungu anahisi wakati wanapotaka kuondoka. Kuanzia muda ule ambao mtu huyu anaamua kumwacha Mungu, Mungu amemwacha kabisa; tayari Mungu ameanzisha matokeo katika moyo Wake. Matokeo hayo ni yapi? Kwamba mtu huyu ni mmoja wa buku, na ataangamia pamoja nao. Hivyo basi, watu mara nyingi huona aina hii ya hali: Mtu anamwacha Mungu, lakini hapokei adhabu yoyote. Mungu hufanya kazi kulingana na kanuni Zake binafsi. Watu wanaweza kuona baadhi ya mambo, na baadhi ya mambo yanahitimishwa tu katika moyo wa Mungu, kwa hivyo watu hawawezi kuyaona matokeo. Kile ambacho watu huona si lazima kiwe ndio upande wa ukweli wa mambo; lakini upande ule mwingine, ule upande usiouona—hizi ndizo fikira na hitimisho la kweli kuhusu moyo wa Mungu.

Watu Wanaotoroka Wakati wa Kazi ya Mungu ni Wale Wanaoiacha Njia ya Kweli

Mungu anawezaje kuwapa watu wanaokimbia wakati wa kazi Yake adhabu kali kama hiyo? Kwa nini Mungu anakuwa na hasira kali kwao? Kwanza kabisa tunajua kwamba tabia ya Mungu ni adhama, ni hasira. Yeye si kondoo ili achinjwe na yeyote; na hata zaidi Yeye si kikaragosi ili adhibitiwe na watu vyovyote vile wanavyotaka. Yeye pia si hewa tupu ili kuamrishwa huku na kule na watu. Kama kweli unasadiki kwamba Mungu yupo, unafaa kuwa na moyo unaomcha Mungu, na unafaa kujua kwamba kiini halisi cha Mungu hakifai kughadhabishwa. Ghadhabu hii inaweza kusababishwa na neno; pengine fikira; pengine aina fulani ya tabia bovu; pengine tabia ya upole tabia inayoweza kuruhusiwa kwenye macho na maadili ya binadamu; au pengine inasababishwa na falsafa, nadharia. Hata hivyo, punde unapomghadhabisha Mungu, fursa yako inapotea na siku zako za mwisho zinakuwa zimewasili. Hili ni jambo baya! Kama huelewi kwamba Mungu hawezi kukosewa, basi pengine humchi Mungu, na pengine unamkosea Yeye kila wakati. Kama hujui namna ya kumcha Mungu, basi huwezi kumcha Mungu, na hutaweza kujua namna ya kujiweka kwenye njia ya kutembelea kwa njia ya Mungu—kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Punde unapokuwa na habari, unaweza kuwa na ufahamu kwamba Mungu hawezi kukosewa, kisha utajua ni nini maana ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu.

Kutembea katika njia ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu si lazima kuumaanishe ni kiwango kipi cha ukweli unachojua, ni majaribio mangapi ambayo umepitia, au ni mitihani mingapi ambayo umepitia na kutiwa adabu. Badala yake, kunategemea aina ya mtazamo ulio nao kwa Mungu moyoni mwako, na kiini unachokionyesha. Kiini halisi cha watu na mielekeo yao ya kibinafsi—mambo haya ni muhimu sana, muhimu kabisa. Kuhusiana na wale watu ambao wamemkana na kumwacha Mungu, mwelekeo wao wa dharau kwa Mungu na mioyo yao inayodharau ukweli ulikera tabia ya Mungu, hivyo basi kulingana na Mungu hawatawahi kusamehewa. Wamejua kuhusu uwepo wa Mungu, wamekuwa na taarifa kwamba Mungu tayari amewasili, wameweza hata kupitia kazi mpya ya Mungu. Kuondoka kwao si kutokana na kudanganywa, wala si suala kwamba wao wamechanganyikiwa kulihusu. Hata si suala hata kidogo la wao kulazimishwa kuondoka. Lakini kwa nadhari yao, na kwa akili iliyo wazi, wamechagua kumwacha Mungu. Kuondoka kwao si kupotea kwao; si hata kutupwa kwao nje. Hivyo basi, katika macho ya Mungu, wao si kondoo aliyepotea njia kutoka kwenye kondoo wale wengine, sikuambii hata mtoto wa kiume mbadhirifu aliyepotea njia yake. Waliondoka bila hofu ya kuadhibiwa, na hali kama hiyo, mfano kama huo unaikera tabia ya Mungu na ni kutokana na kero hili ambapo Yeye huwapa matokeo yasiyo na matumaini. Je, huoni kwamba matokeo kama haya yanatisha? Hivyo basi kama watu hawamjui Mungu, wanaweza kumkosea Mungu. Hilo ni suala dogo! Kama mtu hatachukulia mwelekeo wa Mungu kwa umakinifu, na bado anasadiki kwamba Mungu angali anatarajia kurudi kwake—kwa sababu wao ni mojawapo wa kondoo wa Mungu waliopotea na kwamba Mungu angali anawasubiria kubadilisha moyo wao—basi mtu huyu hayupo mbali sana na kuweza kuondolewa kwenye siku yake ya adhabu. Mungu hatakataa tu kumkaribisha. Hii ndiyo mara yake ya pili ya kuikera tabia ya Mungu; hivyo basi suala hili ni baya zaidi! Mwelekeo wa mtu huyu usioheshimu vitu vitakatifu tayari umekosea agizo la kiutawala la Mungu. Bado Mungu atawakaribisha? Kwa moyo Wake, kanuni za Mungu kuhusiana na suala hili ni kwamba mtu amefikia uhakika kuhusu ni ipi ndiyo njia ya kweli, ilhali anaweza bado kwa nadhari yake na kwa akili wazi kumkataa Mungu, na kuondoka kutoka kwa Mungu, basi Mungu atazuia kabisa barabara iendayo katika wokovu wake, na hata lango la kuingia kwenye ufalme watafungiwa. Wakati mtu huyu atakapokuja kubisha kwa mara nyingine, Mungu hatamfungulia lango. Mtu huyu atafungiwa milele. Pengine baadhi yenu mmeisoma hadithi hii ya Musa kwenye Biblia. Baada ya Musa kupakwa mafuta na Mungu, viongozi 250 walionyesha ukosefu wa utiifu kwa Musa kwa sababu ya hatua zake na sababu nyinginezo mbalimbali. Ni nani waliyekataa kumtii? Hakuwa Musa. Walikataa kutii mipango ya Mungu; walikataa kutii kazi ya Mungu katika suala hili. Walisema yafuatayo: “Ninyi mnachukua mengi kwenu, kwa sababu mkusanyiko wote ni mtakatifu, kila mmoja wao, naye Yehova yuko miongoni mwao….” Katika macho yenu, maneno haya ni mazito? Si mazito! Angaa maana ya moja kwa moja ya maneno haya si mazito. Katika mkondo wa kisheria, hawavunji sheria zozote, kwa sababu kwenye sehemu ya juu kabisa si lugha katili, au msamiati, isitoshe, hayana maana yoyote ya kukufuru. Sentensi ya kawaida ndiyo iliyo hapo, hamna cha ziada. Ilhali inakuwaje kwamba maneno haya yanaweza kuanzisha hasira kali kama hiyo kutoka kwa Mungu? Ni kwa sababu hayasemwi kwa watu, mbali kwa Mungu. Mwelekeo na tabia iliyoelezewa na wao ndicho hasa kinachoikera tabia ya Mungu, na wao wanaikosea tabia ya Mungu ambayo haipaswi kukosewa. Sote tunajua matokeo yao hatimaye yalikuwa yapi. Kuhusiana na wale waliomwacha Mungu, mtazamo wao ni upi? Mwelekeo wao ni upi? Na ni kwa nini mtazamo na mwelekeo wao unasababisha Mungu kuwashughulikia kwa njia hiyo? Sababu ni kwamba wanajua waziwazi Yeye ni Mungu ilhali bado wanachagua kumsaliti Yeye. Na ndiyo maana wanaondolewa kabisa fursa yao ya wokovu. Kama vile Biblia inavyosema: “Kwa sababu tukitenda dhambi makusudi baada ya sisi kupokea maarifa ya ukweli, hakuna tena dhabihu ya dhambi” (Waebrania 10:26). Je, mmelielewa suala hili sasa?

Majaliwa ya Binadamu Yanaamuliwa na Mwelekeo Wake Kwa Mungu

Mungu ni Mungu aliye hai, na kama vile tu watu wanavyotenda tofauti katika hali tofauti, ndivyo mwelekeo wa Mungu ulivyo katika utendakazi huu na unavyotofautiana kwa sababu Yeye si kikaragosi, wala Yeye si hewa tupu. Kupata kuujua mwelekeo wa Mungu ni jambo lenye thamani kwa wanadamu. Watu wanafaa kujifunza vipi, kwa kuujua mwelekeo wa Mungu, wanaweza kuijua tabia ya Mungu na kuuelewa moyo Wake kidogo kidogo. Unapouelewa moyo wa Mungu kidogo kidogo hutahisi kwamba kumcha Mungu na kujiepusha na maovu ni jambo gumu la kutimiza. Kilicho zaidi ni kwamba, unapomwelewa Mungu, hakuna uwezekano wa wewe kufanya hitimisho kuhusu Yeye. Unapoacha kufanya hitimisho kuhusu Mungu, hakuna uwezekano wa wewe kumkosea Yeye, na bila kujua Mungu atakuongoza kuwa na maarifa Yake, na hivyo basi utamcha Mungu katika moyo wako. Utaacha kumfafanua Mungu kwa kutumia falsafa, zile barua, na nadharia ambazo umejifunza. Badala yake, kwa kutafuta nia za Mungu katika mambo yote na siku zote utaweza bila kufahamu kuwa mtu anayefuata moyo wa Mungu.

Kazi ya Mungu haionekani wala kugusika na wanadamu, lakini kulingana na Mungu, hatua za kila mmoja, pamoja na mwelekeo wake kwake Yeye—haya hayatambuliki tu na Mungu, lakini pia kuonekana vilevile. Hili ni jambo ambalo kila mmoja anafaa kutambua na kuwa wazi kulihusu. Unaweza kuwa ukijiuliza siku zote: “Je, Mungu anajua kile ninachofanya hapa? Je, Mungu anajua kile ninachofikiria sasa hivi? Pengine Anajua, pengine Hajui.” Kama utakuwa na aina hii ya mtazamo, kufuata na kusadiki Mungu ilhali unatia shaka katika kazi Yake na uwepo Wake, basi hivi karibuni au baadaye siku itawadia ambapo utamghadhabisha, kwa sababu tayari unayumbayumba pembezoni pa jabali hatari. Nimewaona watu ambao wamesadiki katika Mungu kwa miaka mingi lakini bado hawajapata uhalisia wa ukweli, wala hawaelewi hata mapenzi ya Mungu. Maisha yao na kimo chao havipigi hatua yoyote, ukitii tu falsafa zile za kiwango cha chini zaidi. Hii ni kwa sababu watu hawa hawajawahi kuchukulia neno la Mungu kama maisha yao binafsi, na hawajawahi kukabiliana na kukubali uwepo Wake. Je, unafikiri kwamba Mungu huwaona watu kama hawa na kujawa na furaha? Je, wanamtuliza Yeye? Katika jinsi hiyo, ni mbinu ya imani ya watu katika Mungu ambayo inaamua majaliwa yao. Kuhusu jinsi watu humtafuta na jinsi wanavyomweleka Mungu, mitazamo ya watu ni ya umuhimu wa kimsingi. Usimwache Mungu kana kwamba yeye ni fungu la hewa kavu tu linaloelea karibu na nyuma ya kichwa chako. Usikose kumjali Mungu ni kana kwamba Yeye ni hewa tupu nyuma ya kichwa chako. Siku zote fikiria kuhusu Mungu wa imani yako kama Mungu hai, Mungu halisi. Yeye hayupo kule juu kwenye mbingu ya tatu bila chochote cha kufanya. Badala yake, siku zote bila kusita Anaangalia kwenye mioyo ya kila mmoja, Akiangalia ni nini unachofanya, akichunguza kila neno dogo na kila tukio dogo, akiangalia mwenendo wako na mwelekeo wako kwa Mungu. Kama uko radhi kujitolea kwa Mungu au la, tabia yako yote na fikira zako na mawazo yako ya ndani zaidi ziko mbele ya Mungu, na yanaangaliwa na Yeye. Ni kulingana na tabia yako, kulingana na vitendo vyako, na kulingana na mwelekeo wako kwa Mungu, ambapo maoni Yake kwako, na mwenendo Wake kwako, vinaendelea vikibadilika. Mimi Ningependa kutoa ushauri fulani kwa baadhi ya watu. Msijiweke kwenye mikono ya Mungu kama watoto wachanga, kana kwamba Yeye Anapaswa kukupenda sana, kana kwamba Asingewahi kukuacha, na kana kwamba mwelekeo Wake kwako ni imara na usingeweza kubadilika, na Ninawashauri muache kuota ndoto! Mungu ni mwenye haki katika kutendea kila mtu. Anakabiliana na kazi ya ushindi wa wanadamu na wokovu kwa bidii. Huo ndio usimamizi Wake. Anashughulikia kila mmoja kwa umakinifu, na wala si kama kiumbe cha kufugwa cha kucheza nacho. Upendo wa Mungu kwa binadamu si ule wa kudekeza au kupotosha; rehema na uvumilivu Wake kwa wanadamu si dokezi au ya kutotilia maanani. Kinyume cha mambo, upendo wa Mungu kwa wanadamu ni wa kutunza, kusikitikia, na kuheshimu maisha; rehema na uvumilivu Wake vyote vinaonyesha matarajio Yake kwa binadamu; rehema na uvumilivu Wake ndivyo ambavyo binadamu anahitaji ili kuishi. Mungu yuko hai, na kwa hakika Mungu yupo; mwelekeo Wake kwa wanadamu unafuata kanuni, si yenye kutangazwa kama imani ya dini, na unaweza kubadilika. Mapenzi Yake kwa binadamu yanabadilika kwa utaratibu na kurekebishwa kwa muda, hali na mwelekeo wa kila mtu. Kwa hiyo, unafaa kujua rohoni mwako na uwazi wote kwamba kiini halisi cha Mungu hakibadiliki, na kwamba tabia Yake itajitokeza katika nyakati tofauti, na muktadha tofauti. Huenda usifikirie kwamba hili si suala muhimu, na wewe unatumia dhana zako za kibinafsi katika kufikiria namna ambavyo Mungu anafaa kufanya mambo. Lakini zipo nyakati ambapo kinyume kabisa cha mtazamo wako ni kweli, na kwa kutumia dhana zako za kibinafsi katika kujaribu na kumpima Mungu, tayari umemghadhabisha. Hii ni kwa sababu Mungu hafanyi kazi kama unavyofikiria wewe, Naye Mungu hatalishughulikia suala hili kama vile unavyosema Atalishughulikia. Na hivyo basi Nakukumbusha kuwa makini na mwenye hekima katika mtazamo wako katika kila kitu, na ujifunze namna ya kufuata kanuni ya kutembea kwenye njia ya Mungu katika mambo yote—kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Lazima uimarishe uelewa dhabiti katika masuala ya mapenzi ya Mungu na mwelekeo wa Mungu; kutafuta watu walio na nuru kuuwasilisha kwako, na kutafuta kwa dhati. Usimwone Mungu wa imani yako kama kikaragosi—kuhukumu kiholela, kufikia hitimisho kiholela, kutomshughulikia Mungu kwa heshima Anayostahili. Katika mchakato wa wokovu wa Mungu Anapofafanua matokeo yako, bila kujali kama Yeye atakupa rehema, au uvumilivu, au hukumu na kuadibu, mwelekeo Wake kwako wewe unabadilika. Inategemea na mwelekeo wako kwa Mungu, na uelewa wako wa Mungu. Usiache dhana moja ya kupita ya maarifa au uelewa wako katika Mungu kumfafanua Yeye daima. Usisadiki katika Mungu aliyekufa; amini kwa yule aliye hai. Kumbuka hili! Ingawa Nimezungumzia ukweli fulani hapa, ukweli mliohitaji kusikia, kwa mujibu wa hali yenu ya sasa na kimo chenu cha sasa, Sitatoa mahitaji yoyote makubwa zaidi ili nisije nikaiondoa shauku yenu. Kufanya hivyo kutajaza mioyo yenu na huzuni na simanzi, na kuwafanya nyinyi kuhisi masikitiko mengi mno kwa Mungu. Badala yake Natumai kwamba mnaweza kutumia upendo wa Mungu katika mioyo yenu, na kutumia mwelekeo ambao ni wa heshima kwa Mungu wakati mnapotembea kwenye njia iliyo hapo mbele. Usimalizie suala la jinsi ya kushughulikia imani ya Mungu kwa kubahatisha. Lishughulikie kama mojawapo ya maswali makubwa zaidi yaliyopo. Liwekeni kwenye mioyo yenu, litieni kwenye matendo, unganeni nalo kupitia kwa maisha halisi—msikubaliane nalo kwa maneno pekee. Kwani hili ni suala la uzima na mauti, na ndilo ambalo litaamua hatima yako. Usilichukulie kama mzaha, kama mchezo wa mtoto! Baada ya kuwaambia maneno haya leo, Najiuliza mavuno ya uelewa yamekuwa nini katika akili zenu? Kunayo maswali yoyote ambayo ungependa kuuliza kuhusu kile Nilichokisema leo?

Ingawa mada hizi ni mpya kidogo, na zimeondolewa kidogo kutoka kwenye mitazamo yenu na kile ambacho kwa kawaida mnafuatilia na kutilia maanani, Nafikiria kwamba baada ya mada hizi kuwasilishwa kwa kipindi cha muda, mtaimarisha uelewa mzuri wa kila kitu Nilichosema hapa. Kwa sababu hizi ni mada mpya, mada ambazo hujawahi kufikiria awali, Ninatumai kwamba hazitaongezea mzigo kwako. Ninaongea maneno haya leo si kwa sababu ya kuwatishia nyinyi, wala Sijaribu kukushughulikia wewe; badala yake, nia Yangu ni kukusaidia kuelewa ukweli wa hoja. Kwa vyovyote vile, kunao umbali kati ya wanadamu na Mungu. Ingawa binadamu anaamini katika Mungu, hajawahi kumwelewa Mungu; hajawahi kujua mitazamo ya Mungu. Binadamu pia hajawahi kuwa na shauku katika kuujali mwelekeo wa Mungu. Badala yake, amesadiki kwa kutojua, ameendelea mbele kwa kutojua na amekosa kumakinika katika maarifa na uelewa wake wa Mungu. Hivyo basi Nahisi mshawasha wa kuyafumbua masuala haya kwa niaba yenu na kuwasaidia kuelewa huyu Mungu unayemsadiki hasa ni Mungu wa aina gani; kile Anachofikiria; mwelekeo Wake ni nini katika kushughulikia Kwake kwa watu wa aina tofauti; uko mbali kiasi gani kukamilisha mahitaji Yake; na tofauti iliopo kati ya hatua zako na kiwango anachohitaji Yeye. Shabaha katika kujua kwako haya ni kuwapa kigezo cha kupimia kwenye mioyo yenu ambacho mtaweza kupimia dhidi ya na kujua barabara mnayotembelea imewaelekeza katika mavuno aina gani, kile ambacho hamjapata kwenye barabara hii, na sehemu zile ambazo hamjajihusisha kwazo. Wakati mnawasiliana miongoni mwa nyinyi wenyewe, kwa kawaida mnazungumzia mada chache zinazungumziwa kwa kawaida; upana huo wa kazi ni mwembamba, na maudhui ni ya juujuu sana. Kunao umbali, nafasi, kati ya kile ambacho mnazungumzia na nia za Mungu, katikati ya mazungumzo yenu na upana na kiwango cha mahitaji ya Mungu. Kuendelea hivi baada ya muda kutawafanya kupotoka zaidi na zaidi kutoka kwenye njia ya Mungu. Mnayachukua tu maneno yaliyopo kutoka kwa Mungu na kuyageuza kuwa vifaa vya kuabudu, kuwa kaida za dini na utaratibu. Hayo tu ndiyo maana yake! Kwa hakika, Mungu hana nafasi kamwe katika mioyo yenu, na Mungu hajawahi kuipata mioyo yenu. Baadhi ya watu hufikiria kwamba kumjua Mungu ni vigumu sana—huu ndio ukweli. Ni vigumu! Kama watu wataambiwa kutekeleza wajibu wao na kuhakikisha kwamba mambo yanatendeka kwa nje, kama wataulizwa kutia bidii, basi watu watafikiria kwamba kusadiki Mungu ni jambo rahisi sana, kwa sababu haya yote yanapatikana katika ule upana wa uwezo wa binadamu. Ilhali punde tu mada hizo zinaposonga kuelekea kwenye maeneo ya nia za Mungu na mwelekeo wa Mungu kwa binadamu, basi mambo yanapata kuwa magumu zaidi kwa watu wote. Hiyo ni kwa sababu yote haya yanahusisha uelewa wa ukweli na kuingia kwao katika uhalisia; bila shaka kuna kiwango cha ugumu. Lakini baada ya wewe kuingia kupitia mlango wa kwanza, baada ya wewe kuanza kuingia ndani yake, mambo yanaanza kuwa rahisi na rahisi kwa utaratibu.

Sehemu ya Mwanzo ya Kumcha Mungu ni Kumtendea Kama Mungu

Mtu fulani amelizua swali hivi punde: Inakuwaje kwamba tunajua zaidi kuhusu Mungu kuliko alivyojua Ayubu, ilhali bado hatuwezi kumcha Mungu? Tuliligusia suala hili hapo awali kidogo, sivyo? Kwa hakika, kiini halisi cha swali hili kimeweza pia kuzungumziwa awali kwamba ingawa Ayubu hakumjua Mungu wakati huo, alimshughulikia Yeye kama Mungu, na kumchukulia Yeye kama Bwana wa mambo yote mbinguni na nchini. Ayubu hakumchukulia Mungu kuwa adui. Badala yake, alimwabudu Yeye kama Muumba wa viumbe vyote. Watu siku hizi wanampinga Mungu sana kwa nini? Kwa nini hawawezi kumcha Mungu? Sababu moja ni kwamba wamepotoshwa pakubwa na Shetani. Wakiwa na asili yao ya kishetani ikiwa imekita mizizi ndani, watu wanageuka na kuwa adui wa Mungu. Hivyo basi, hata ingawa wanasadiki katika Mungu na kumtambua Mungu, bado wanaweza kumpinga Mungu na kujiweka katika nafasi ya upinzani na Yeye. Hili linaamuliwa na asili ya binadamu. Sababu nyingine ni kwamba ingawa watu wanasadiki Mungu, hawamchukulii Yeye tu kama Mungu. Badala yake, wanamchukulia Mungu kuwa ndiye anayempinga binadamu, wakimwona Yeye kuwa adui wa binadamu, na hawawezi kupatanishwa na Mungu. Ni rahisi hivyo. Je, jambo hili halikuzungumziwa kwenye kikao cha awali? Hebu fikiria: Hiyo ndiyo sababu? Ingawa unayo maarifa kidogo ya Mungu, maarifa haya hasa ni nini? Haya siyo yale kila mtu anazungumzia? Haya si yale ambayo Mungu alikuambia? Unajua tu zile dhana za kinadharia na kifalsafa; umewahi kupitia dhana halisi ya Mungu? Je, unayo maarifa ya kibinafsi? Je, unayo maarifa na uzoefu wa kimatendo? Kama Mungu asingekuambia, ungelijua hili? Maarifa yako katika nadharia hayawakilishi maarifa halisi. Kwa ufupi, bila kujali ni kiwango kipi unachojua na ni vipi ulivyokijua hatimaye, kabla ya wewe kufikia uelewa halisi wa Mungu, Mungu ndiye adui wako, na kabla ya wewe kumshughulikia Mungu hivyo, Amewekwa kuwa mpinzani wako, kwani wewe ni mfano halisi wa Shetani.

Unapokuwa pamoja na Kristo, pengine unaweza kumhudumia kwa milo mitatu kwa siku, pengine kumhudumia Yeye kwa chai, kuyashughulikia mahitaji Yake ya maisha, ni kana kwamba unamshughulikia Kristo kama Mungu. Kila wakati jambo linapofanyika, mitazamo ya watu siku zote inakuwa kinyume cha mtazamo wa Mungu. Siku zote wanashindwa kuelewa mtazamo wa Mungu, na wanashindwa kuukubali. Ingawa watu wanaweza kupatana na Mungu juujuu, hii haimaanishi kwamba wanalingana na Yeye. Punde tu jambo linapofanyika, ukweli wa kutotii kwa binadamu unaibuka, na kuthibitisha ukatili uliopo kati ya binadamu na Mungu. Ukatili huu si wa Mungu kumpinga binadamu; si Mungu kutaka kuwa katili kwa binadamu, na si Mungu kumweka binadamu katika upinzani na kumshughulikia binadamu hivyo. Badala yake, ni hali ya upinzani huu wa kiini halisi kwa Mungu ambao unajificha katika mapenzi ya kibinafsi ya binadamu, na katika akili ya kutofahamu ya binadamu. Kwa sababu binadamu anachukulia kila kitu kinachotoka kwa Mungu kama kifaa cha utafiti wake, mwitikio wake kwa hiki ambacho kinatoka kwa Mungu na kile ambacho kinamhusisha Mungu ni, zaidi ya yote, kukisia, na kushuku, na kisha haraka sana kuingia katika mwelekeo ambao unakinzana na Mungu, na unapingana na Mungu. Baada ya hapo, binadamu atachukua hali hizi za moyo za kimyakimya na kuzua mjadala na Mungu au kushindana na Mungu hadi kufikia kiwango ambacho atatia shaka kama Mungu wa aina hii anastahili kufuatwa. Licha ya hoja kwamba urazini wa binadamu unamwambia asiendelee hivi, bado atachagua kufanya hivyo licha ya kutotaka kufanya hivyo, kiasi kwamba ataendelea bila kusita hadi mwisho. Kwa mfano, ni nini mwitikio wa kwanza kwa baadhi ya watu wanaposikia uvumi fulani au matusi fulani kumhusu Mungu? Mwitikio wa kwanza ni: Sijui kama uvumi huu ni kweli au la, kama upo ama haupo, hivyo basi nitasubiri na kuona. Kisha wanaanza kutafakari: Hakuna njia ya kuthibitisha haya; ipo kweli? Uvumi huu ni kweli au la? Ingawa mtu huyu haonyeshi juujuu, moyo wake tayari umeanza kutia shaka, tayari umeanza kumkataa Mungu. Ni nini kiini halisi cha aina hii ya mwelekeo, aina hii ya mtazamo? Je huu si usaliti? Kabla ya wao kukumbwa na suala, huwezi kuona mtazamo wa mtu huyu ni nini—yaonekana ni kana kwamba wao hawakinzani na Mungu, ni kama hawamchukulii Mungu kuwa adui. Hata hivyo, punde wanapokumbwa na suala hilo, wanasimama mara moja na Shetani na kumpinga Mungu. Hali hii inapendekeza nini? Inapendekeza kwamba binadamu na Mungu wanapingana! Si kwamba Mungu anamchukulia binadamu kama adui, lakini kwamba kile kiini halisi chenyewe cha binadamu ni kikatili kwa Mungu. Haijalishi ni kwa muda mrefu vipi ambapo mtu humfuata Mungu, ni kiwango kipi anacholipia; haijalishi vipi ambavyo mtu anamsifu Mungu, anavyojihifadhi dhidi ya kumpinga Mungu, hata akijisihi kumpenda Mungu, hatawahi kufaulu kumshughulikia Mungu kama Mungu. Si hali hii inaamuliwa na kiini halisi cha mwanadamu? Kama Utamshughulikia kama Mungu, unaweza kwa kweli kusadiki kwamba Yeye ni Mungu, unaweza bado kuwa na shaka lolote kwake Yeye? Bado kunaweza kuwa na maswali yoyote yanayomhusu Yeye katika moyo wako? Hakuwezi. Mitindo ya ulimwengu huu ni miovu kweli, na wanadamu wa kizazi hiki pia, hivyo, inawezekanaje kwamba huna fikira zozote kuzihusu? Wewe mwenyewe umejaa uovu, hivyo inakuwaje kwamba huna fikira zozote kuhusu hayo? Ilhali uvumi mchache tu, matusi fulani yanaweza kusababisha dhana kubwa mno kumhusu Mungu, zinaweza kuleta mawazo mengi mno, hali inayoonyesha vile ambavyo kimo chako kilivyo bado kichanga! “Mnong’ono” tu wa mbu wachache, nzi wachache wabaya, hilo tu ndilo linalokupotosha? Huyu ni mtu wa aina gani? Je, unajua anachofikiria Mungu kuhusu mtu wa aina hii? Mwelekeo wa Mungu kwa hakika uko wazi sana kuhusiana na ni vipi Anavyowashughulikia watu hawa. Ni kwa sababu tu kwamba ushughulikiaji wa Mungu kwa watu hawa ni kuwapuuza—mwelekeo Wake ni kutowatilia maanani, na kutomakinikia watu hawa wasiojua. Kwa nini hivyo? Kwa sababu katika moyo Wake Hakuwahi kupangilia kuhusu kupata watu hao ambao wameahidi kuwa wakatili kwake Yeye hadi mwisho, na ambao hawajawahi kupangilia kutafuta njia ya uwiano na Yeye. Pengine maneno haya Niliyoyaongea yamewaumiza watu wachache. Kwa kweli, mko radhi kuniruhusu Mimi kuwadhuru siku zote namna hii? Bila kujali kama mko radhi au la, kila kitu Ninachosema ni ukweli! Kama siku zote Ninawadhuru namna hii, siku zote Nafichua makovu yenu, je, itaathiri taswira za majivuno kuhusu Mungu katika mioyo yenu? (Haitaathiri.) Ninakubali kwamba haitaathiri kwani kwa ufupi hakuna Mungu katika mioyo yenu. Yule Mungu wa majivuno anayepatikana ndani ya mioyo yenu, yule mnayemtetea kwa dhati na kulinda, kwa ufupi si Mungu. Badala yake ni ndoto ya kufikiria kwa binadamu; kwa ufupi haipo. Hivyo basi ni bora zaidi kama Nitafichua jibu la kitendawili hiki. Je, huu si ukweli wote? Mungu halisi hatokani na kufikiria kwa binadamu. Natumai kwamba nyote mnaweza kukabiliana na uhalisia huu, na utawasaidia katika maarifa yenu ya Mungu.

Wale Watu Wasiotambuliwa na Mungu

Kunao baadhi ya watu ambao imani yao haijawahi kutambuliwa katika moyo wa Mungu. Kwa maneno mengine, Mungu hatambui kwamba watu hawa ni wafuasi Wake, kwa sababu Mungu haisifu imani yao. Kwa watu hawa, haijalishi wamemfuata Mungu kwa miaka mingapi, mawazo na mitazamo yao haijawahi kubadilika. Wao ni kama wasioamini, wanatii kanuni na njia ambayo wasioamini wanafanya mambo yao, kutii sheria zao za kusalia na imani. Hawakuwahi kukubali neno la Mungu kama maisha yao, hawakuwahi kusadiki kwamba neno la Mungu ni ukweli, hawakuwahi kunuia kukubali wokovu wa Mungu, na hawakuwahi kutambua Mungu kama Mungu wao. Wanachukulia kusadiki Mungu kuwa uraibu fulani wa wanagenzi, wakishughulikia Mungu kama riziki ya kiroho, hivyo basi hawafikirii kwamba ipo thamani ya kujaribu na kuelewa tabia ya Mungu, au kiini halisi cha Mungu. Unaweza kusema kwamba kila kitu kinacholingana na Mungu wa kweli hakihusiani kwa vyovyote vile na watu hawa. Hawana hamu yoyote, na hawawezi kusumbuliwa kutilia maanani. Hii ni kwa sababu ndani kabisa ya mioyo yao kunayo sauti ya nguvu ambayo siku zote inawaambia: Mungu haonekani na hagusiki, na Mungu hayupo. Wanasadiki kwamba kujaribu kumwelewa Mungu wa aina hii hakutastahili jitihada zao; itakuwa sawa na wao kujidanganya. Wao wanaamini tu kwa kumtambua Mungu kwa maneno tu bila kuchukua msimamo wowote halisi au kujiweka ndani yao kupitia vitendo halisi, wao wanakuwa werevu sana. Mungu anachukulia vipi watu kama hawa? Anawachukulia kuwa wasioamini. Baadhi ya watu huuliza: “Je, wasioamini wanaweza kulisoma neno la Mungu? Je, wanaweza kutekeleza wajibu wao? Je, wanaweza kuyasema maneno haya: ‘Nitaishi kwa ajili ya Mungu’?” Kile ambacho binadamu huona mara nyingi ni maonyesho ya juujuu tu ya watu, na wala si kiini chao halisi. Ilhali Mungu haangalii maonyesho haya ya juujuu; Yeye huona tu kiini chao halisi cha ndani. Hivyo basi, Mungu anao mwelekeo wa aina hii, ufafanuzi wa aina hii, kwa watu kama hawa. Kuhusiana na kile ambacho watu hawa husema: “Kwa nini Mungu hufanya hivi? Kwa nini Mungu hufanya vile? Siwezi kuelewa haya; siwezi kuelewa yale; haya hayaingiliani na fikira za binadamu; Lazima unielezee haya; …” Jibu langu ni: Inahitajika kuelezea suala hili kwako? Je, suala hili lina chochote kuhusiana na wewe? Unafikiria wewe ni nani? Ulitokea wapi? Umefuzu kumwelekeza Mungu? Je, unamwamini Yeye? Je, Anatambua imani yako? Kwa sababu imani yako haina chochote kuhusiana na Mungu, matendo Yake yana uhusiano gani na wewe? Hujui pale ulipo katika moyo wa Mungu, ilhali umefuzu kuzungumza na Mungu?

Maneno ya Maonyo

Hamhisi vibaya baada ya kusikia matamshi haya? Ingawa huenda msiwe radhi kusikiliza maneno haya, au msiwe radhi kuyakubali, yote ni uhakika. Kwa sababu awamu hii ya kazi ni ya Mungu kutenda, kama hujali nia za Mungu, hujali mwelekeo wa Mungu na huelewi kiini halisi na tabia ya Mungu, basi hatimaye wewe ndiwe utakayekosa kufaidi. Msiyalaumu maneno yangu kwa kuwa magumu kusikiliza, na msiyalaumu kwa kupunguza majivuno ya shauku yenu. Mimi naongea ukweli; na wala Sinuii kuwavunja moyo. Haijalishi ni nini Ninachowauliza ninyi, na haijalishi ni vipi mnavyohitajika kukifanya, Ninatumai kwamba mtatembelea njia sahihi, na ninatumai kwamba mtafuata njia ya Mungu na wala msipotoke katika njia hii. Kama hutaendelea kulingana na neno la Mungu, na hufuati njia Yake, basi hakutakuwa na shaka kwamba unaasi dhidi ya Mungu na umepotea kutoka kwa njia sahihi. Hivyo basi Nahisi kwamba yapo masuala fulani ambayo lazima Niwabainishie, na kuwafanya kusadiki dhahiri shairi, waziwazi, bila ya tone la mashaka na kuwasaidia waziwazi kujua mwelekeo wa Mungu, nia za Mungu, namna Mungu anavyomfanya binadamu kuwa mtimilifu, na ni kwa njia gani Yeye Hupanga matokeo ya binadamu. Endapo kutakuwa na siku ambayo hutaweza kuanza katika njia hii, basi Sitahitajika kuwajibika kwa vyovyote vile kwa sababu maneno haya tayari yamezungumzwa kwako waziwazi. Kuhusiana na matokeo ya aina tofauti ya watu Mungu Anayo mitazamo tofauti. Anazo njia Zake binafsi za kuwapima, vile vile kama kiwango Chake binafsi cha mahitaji kwao. Kiwango Chake cha kupima matokeo ya watu ni kile ambacho ni chenye haki kwa kila mmoja—hakuna shaka kuhusu hilo. Hivyo basi, woga wa watu fulani hauhitajiki. Je, umepata tulizo la moyo sasa? Ndivyo hivyo kwa leo. Kwaheri!

Oktoba 17, 2013

Iliyotangulia: Dibaji

Inayofuata: Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp