Kuahidi Maisha Yangu kwa Moyo wa Ibada

16/01/2018

Zhou Xuan Mkoa wa Shandong

Mnamo Aprili 3, mwaka wa 2003, niliambatana na dada mmoja kumtembelea muumini mpya. Muumini huyu mpya hakuwa na uhakika kuhusu kazi ya Mungu katika siku za mwisho na aliishia kuturipoti. Kwa sababu hiyo, askari wanne waovu wenye nguo za raia walikuja na kwa ugomvi kutuingiza sisi wawili katika gari lao na kutupeleka kwa kituo cha polisi. Njiani, moyo wangu ulikuwa na wasiwasi mno, kwa sababu mwilini mwangu nilikuwa na peja ya mawasiliano, orodha isiyo kamili ya majina ya wanajumuiya wa kanisa letu, na daftari dogo. Niliogopa kwamba wale askari waovu wangeweza kugundua vitu hivi na niliogopa zaidi kwamba ndugu zangu wa kiume na wa kike wangeniita kupitia peja yangu ya mawasiliano, kwa hiyo mimi kwa mfululizo nilimwomba Mungu kwa haraka moyoni mwangu: “Mungu, ninapaswa kufanya nini? Ninakuomba Unipe suluhisho na usiruhusu vitu hivi viingie mikononi mwa askari hawa waovu.” Baada ya hili, nilichukua vitu hivi kutoka kwa mkoba wangu na kwa kimya kuviweka kiunoni mwangu na kusema kwamba tumbo langu liliuma na nilihitaji kutumia msala. Wale askari waovu wakaniapizia wakisema: “Wewe umejaa upuuzi!” Baada ya maombi yangu ya mara kwa mara, walimtaka askari mmoja wa kike anichunge nilipokwenda msalani. Nilipouondoa mshipi wangu, kifaa changu cha mawasiliano kilianguka na kwa urahisi nikakiokota na kukitupa katika bomba la maji taka. Kwa sababu niliogopa wakati huo kwamba huyo afisa wa kike angegundua mkoba kiunoni mwangu, sikuutupa katika bomba, lakini badala yake niliutia katika pipa la taka; nilidhani kwamba ningetumia msala tena usiku na kisha kuutupa ndani ya choo. Ilivyotukia, sikurudi kwa msala huo kamwe. Ilitukia kuwa wale askari waovu waliupata ule mkoba niliokuwa nimeutupa katika jaa la taka.

Wale askari waovu wakatufungia yule dada na mimi katika chumba kimoja na kutulazimisha tuvue nguo zetu zote ili waweze kutupekua. Walipekua hata kwa nywele zetu kuona kama tulificha chochote. Baada ya kumaliza kutafuta, walitutia pingu na kutufungia katika kile chumba. Ilipofika usiku, wale askari waovu walitutenganisha ili tuhojiwe kwa makini; waliniuliza: “Unatoka wapi? Jina lako ni nani? Ulikuja hapa lini? Unafanya nini hapa? Unaishi wapi? Unaamini nini? Jina la mtu uliye naye ni nani?” Kwa sababu hawakuridhishwa na majibu yangu, wale askari waovu walisema hivi kwa hasira: “Sisi huonyesha upole kwa wale wanaokiri na ukali kwa wale wanaobisha. Usiposema ukweli, utajilaumu mwenyewe! Sema! Ni nani anayekusimamia? Unafanya nini? Sema na tutakutendea kwa upole.” Nilivyoona jinsi walivyoonekana wakali kishetani, nilifanya uamuzi kwa kimya: kabisa sitakuwa Yuda, sitawasaliti ndugu zangu wa kiume na wa kike na sitazisaliti nia za familia ya Mungu. Walipoona kwamba hawakuweza kupata chochote kutoka kwangu, waliingiwa na wasiwasi na kuanza kunigonga na kunipiga mateke kwa ukali wakisema: “Kwa kuwa husemi chochote, tutakuadhibu kwa kukunyosha mikono na miguu!” Kisha ghafla kulikuwa na mlipuko mwingine wa kupigwa ngumi na mateke kwa ukali sana. Baadaye, mmoja wao akaniamuru niketi chini, na akanitia pingu na kuipinda mikono yangu kwelekea nyuma yangu kwa kukaza alivyoweza. Kisha akaweka kiti nyuma yangu na kutumia kamba kuifunga mikono yangu nyuma ya kiti. Alitumia mikono yake na akawekea nguvu zake zote kwelekea chini, akiweka shinikizo juu ya mikono yangu. Mara moja, mikono yangu ikahisi kama ingevunjika; iliumia vibaya sana hivi kwamba nilitoa yowe kali. Walikwenda mbele na nyuma jinsi hii kwa mikono yangu wakiniumiza bila kukoma kwa muda wa saa kadhaa. Baadaye, sikuweza kuvumilia na nilitikisika kutoka utosini hadi kidoleni. Walipoona hayo, wakasema: “Usijifanye kana kwamba wewe ni wazimu, tumeona hili mara nyingi kabla. Je, unadhani unamshtua nani? Je, unadhani kuwa kufanya hivi kutakuondoa kwa tatizo hili?” Waliona kwamba bado nilikuwa nikitikisika na askari mmoja mwovu akasema: “Nenda naye msalani na kumtia kinyesi kiasi kinywani mwake, angalia kama atakila au la.” Walitumia kijiti kuchotea kinyesi kiasi na kukifikicha ndani ya kinywa changu na kunifanya nikile; nilikuwa bado nikitoa pofu kwa kinywa na waliona kwamba bado nilikuwa nikitikisika, kwa hiyo waliniacha nishuke kutoka kwa kiti. Mwili wangu mzima uliumia bila kuvumilika kama kwamba nilikuwa na mito kutoka utosini hadi kidoleni na nilitoa yowe kwa maumivu nilipolala sakafuni nikiwa nimeduwaa. Baada ya muda mrefu, viganja vyangu na mikono viliaanza kusogea tena. Polisi hao waovu waliogopa kwamba ningegonga kichwa changu kwa ukuta na kujiua, kwa hiyo walinipa helmeti. Baadaye, waliniburuta na kunirudisha kwa kile chumba kidogo cha chuma. Nililia na kumwomba Mungu: “Ewe Mungu, mwili wangu ni dhaifu sana. Natamani kuwa Unilinde. Bila kujali jinsi Shetani anavyonitesa, ningependelea kufa kuliko kukusaliti Wewe kama Yuda. Sitawasaliti ndugu zangu wa kiume na wa kike au maslahi ya familia ya Mungu. Niko tayari kuwa shahidi Kwako ili kumuaibisha yule Shetani mzee.”

Siku ya tatu, wale askari waovu walichukua ile daftari dogo na orodha ya majina ya wanajumuiya wa kanisa niliyokuwa nimeitupa katika jaa la taka na kunihoji. Nilipoona vitu hivi, nilihisi hasa kutokuwa na raha na kujaa kujilaumu na majuto. Nilichukia kwamba nilikuwa na hofu sana na mwoga na kwamba sikuwa na ujasiri wa kutosha wakati huo wa kutupa mkoba ndani ya bomba la maji taka, jambo lililosababisha matokeo haya ya hatari. Nilichukia hata zaidi kwamba sikusikiliza mipango ya familia ya Mungu na kuleta vitu hivi wakati wa kutimiza wajibu wangu, jambo ambalo limelisababishia kanisa tatizo hili kubwa. Wakati huo, nilitamani kumtegemea tu Mungu kukabiliana na yaliyokuwa mbele yangu. Zaidi ya hayo, nilitamani kumtegemea Mungu kumshinda Shetani. Wakati huu nilifikiri juu ya wimbo “Kutembea kwenye Njia ya Kumpenda Mungu”: “Sijali jinsi njia ya imani katika Mungu ilivyo ngumu, natekeleza tu mapenzi ya Mungu kama wito wangu; sembuse kujali ikiwa nitapokea baraka au kuteseka katika siku zijazo. Sasa kwa kuwa nimeamua kumpenda Mungu, nitakuwa mwaminifu hadi mwisho. Bila kujali ni hatari au dhiki gani zinazojificha nyuma yangu, bila kujali mwisho wangu utakuwa upi, ili kukaribisha siku ya Mungu ya utukufu, nafuata kwa makini nyayo za Mungu na kujitahidi kuendelea mbele” (Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Niliuimba wimbo huu kimya kimya na moyo wangu ulikuwa na imani na nguvu tena. Wale askari waovu wakaniuliza: “Je, vitu hivi ni vyako? Sema ukweli nasi, hatutakutendea bila haki. Wewe ni mwathirika na umedanganywa. Mungu mnayemwamini ni Mungu asiye dhahiri na yu mbali, ni ndoto za mchana. Chama cha Kikomunisti ni kizuri, na unapaswa kutegemea hicho chama na serikali. Ukiwa na shida yoyote, unaweza kuja kwetu na tutakusaidia kuitatua. Ukihitaji usaidizi kupata kazi, tunaweza kukusaidia pia. Kiri tu kila kitu juu ya kanisa lako; tuambie kile watu hawa walio kwa orodha yako wanachofanya. Wanaishi wapi? Ni nani mkuu wenu?” Nilitambua hila zao za uwongo na kusema: “Vitu hivi si vyangu, sijui.” Walipoona kwamba singefichua chochote, basi ilifichuka ni watu wa aina gani kamili na walinipiga kikatili na kuniangusha chini na kuendelea kunipiga kwa ukali sana na kutumia nguvu zao zote kuniburuta huku na huko wakitumia pingu zangu. Jinsi walivyozidi kuniburuta, ndivyo pingu zilivyozidi kujikaza na kuukata mwili wangu. Niliumia vibaya sana kiasi cha kulia kwa sauti kubwa na wale askari waovu wakasema kwa ukali: “Tutakufanya uonge, tutakuminya kidogo kidogo kama dawa ya meno ili kukufanya uzungumze!” Hatimaye, walichukua mikono yangu miwili na kuifunga ikielekea nyuma kwa kiti na kunifanya nikalie sakafu. Walinigonga na kuwekea nguvu zao na kugandamiza kwelekea chini juu ya mikono yangu; nilihisi maumivu yasiyovumilika na uchungu uliochoma kana kwamba mikono yangu ingevunjika. Wale askari waovu walinitesa na kunikemea: “Sema wazi!” Bila kusita nikasema: “Sijui!” “Usiposema wazi tutakuua; usiposema wazi basi usitarajie kuishi; tutakufunga jela kwa miaka kumi, miaka ishirini, maisha yako yote; usitarajie kutoka jela kamwe!” Niliposikia hivi, wazo fulani likanijia akilini mwangu ghafla: ni lazima niamue kuwa tayari kwenda jela maisha. Baadaye nilifikiri juu ya wimbo wa uzoefu “Natamani Kuiona Siku ya Utukufu wa Mungu”: “Nitatoa upendo na uaminifu wangu kwa Mungu na kukamilisha misheni yangu ya kumtukuza Mungu. Nimedhamiria kusimama imara katika ushuhuda kwa Mungu, wala kamwe sitashindwa na Shetani. Eh, kichwa changu kinaweza kupasuka na damu itiririke, lakini ujasiri wa watu wa Mungu hauwezi kupotea. Ushawishi wa Mungu umo moyoni, naamua kumwaibisha Shetani Ibilisi” (Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Mungu alinipa nuru, akinifanya niwe imara na kuwa na ujasiri na akinipa imani na uamuzi kupitia kila kitu na kuwa shahidi kwa Mungu. Kwa sababu hiyo, hila za hao askari waovu hazikushinda; walinitesa mpaka wakachoka, kisha wakanirudisha kwa chumba cha chuma.

Siku chache baadaye, niliteswa na hao askari waovu mpaka nikawa sina nguvu. Nilikuwa katika mpagao wa usahaulifu kabisa na mikono yangu ilikuwa na ganzi. Katika kukabiliana na mateso haya katili na ya kinyama, niliogopa hasa kwamba hao askari waovu wangerudi na kunihoji. Mara tu nilivyofikiria hili, moyo wangu haukuweza kujizuia kutetemeka kwa hofu. Kwa kweli sikujua ni nini kingine wangetumia kunitesa, na sikujua ni lini masaili haya yangeisha. Niliweza tu kuendelea kuomba ndani ya moyo wangu kwa Mungu na kumwomba Mungu kuulinda moyo wangu na kunipa hiari na nguvu za kuvumilia mateso ili ningeweza kuwa shahidi kwa Mungu na kumfanya Shetani ashindwe kwa fedheha kamili.

Wakati wale askari waovu walipoona kuwa singekiri, waliungana na Brigedi ya Usalama wa Taifa na Shirika la Usalama wa Umma ili kunihoji. Kulikuwa na watu zaidi ya ishirini huko wakishika zamu kunihoji mchana na usiku wakijaribu kunilazimisha kukiri. Siku hiyo, askari wawili waovu kutoka kwa Brigedi ya Usalama wa Taifa ambao tayari walikuwa wamenihoji mara moja kabla walinijia na mwanzoni walizungumza kwa huruma wakisema: “Ukikiri ukweli, basi tutakuacha uende na tutahakikisha usalama wako. … Ni chama cha Kikomunisti tu kinachoweza kukuokoa, na Mungu hawezi kukuokoa ….” Wakati mmoja wao alipoona kwamba singetamka neno, aliingiwa na wasiwasi na kuanza kunipigia yowe kwa maneno machafu, akinilazimisha niketi sakafuni. Alinipiga teke kwa miguuni kwa nguvu alivyoweza akitumia viatu vya ngozi akisababisha maumivu yasiyoweza kustahimilika. Askari mwingine muovu akamwuliza: “Kunaendaje, anazungumza?” Alisema: “Yeye ni mkaidi sana, bila kujali unampiga kiasi gani na hatazungumza.” Huyo mtu akasema kwa ukali: “Kama hazungumzi, basi mpige hadi afe!” Yule askari muovu akanitishia akisema: “Hutazungumza? Basi tutakuua!” Nikasema: “Nimesema kila kitu ambacho nilihitaji kusema, sijui!” Alikasirika sana kiasi kwamba alionekana kuwa wazimu kabisa, kisha akanguruma kama mnyama wa mwitu na kuanza kunichapa na kunipiga mateke. Hatimaye alipata uchovu kwa kunipiga na kupata kamba kiasi cha unene wa kidole na kuiviringishia mkononi mwake mara chache. Kwa ukatili aliupiga uso wangu mijeledi tena na tena akisema: “Je, wewe humwamini Mungu? Wewe unateseka, kwa nini Mungu wako haji na kukuokoa? Kwa nini Yeye haji na kukufungua pingu? Mungu wako yuko wapi?” Niliyakereza meno yangu na kuvumilia maumivu. Niliomba kwa utulivu moyoni mwangu kwa Mungu: “Ee Mungu! Hata wakinipiga hadi kufa leo, kamwe sitakuwa kama Yuda. Nataka Uwe pamoja nami na kuulinda moyo wangu. Niko tayari kutoa maisha yangu ili kuwa shahidi Kwako na kumfedhehesha Shetani mzee.” Nilifikiria kuhusu wimbo “Ninaomba tu Kwamba Mungu Aridhike”: “Nimejitoa kabisa na kikamilifu, kujitoa kwa Mungu bila hofu ya kifo. Mapenzi Yake daima yako juu ya yote. Bila kujali mustakabali wangu, bila kufikiria faida au hasara, Natamani tu Mungu aridhike. Nashuhudia ushuhuda mkubwa sana na kumwaibisha Shetani kwa ajili ya utukufu wa Mungu. Naahidi kabisa kulipa upendo wa Mungu. Namsifu bila pingamizi moyoni mwangu. Nimeona Jua la haki, ukweli unadhibiti vitu vyote vilivyo duniani. Tabia ya Mungu ni ya haki (na inastahili sifa za wanadamu). Moyo wangu utampenda Mwenyezi Mungu milele, na nitaliinua jina Lake juu” (Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Nilifunga macho yangu na kuvumilia mateso ya Shetani na kupigwa. Wakati huo, ilikuwa ni kama nilisahau kuhusu maumivu yangu. Sikujua ni wakati upi mateso hayo yangeisha. Sikuthubutu kulifikiria, na sikuweza hata kutafakari juu ya hilo. Kitu pekee ambacho niliweza kufanya ni kusali bila kukoma na kumlilia Mungu. Maneno ya Mungu pia yalinipa imani ya mfululizo: “Msiogope, Mwenyezi Mungu wa majeshi hakika atakuwa pamoja nawe; Yeye anawasaidia na Yeye ni ngao yenu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Matamko ya Kristo Mwanzoni, Sura ya 26). “Msiwe na hofu ya wao wanaoua mwili, lakini hawana uwezo wa kuifisha roho: ila heri uwe na hofu ya yeye anayeweza kuiangamiza roho pamoja na mwili katika kuzimu(Mathayo 10:28). Nilifikiri kuhusu jinsi joka kubwa jekundu lilikuwa tishio la bure tu lililoandikiwa kushindwa na mikono ya Mungu. Kama Mungu hakuyaruhusu, mauti hayangenijia; bila ruhusa ya Mungu, hakuna hata unywele wangu mmoja ungepotea. Pia nilifikiria kuhusu maneno haya ya Mungu: “Mmewahi kuzikubali baraka mlizopewa? Mmewahi kuzitafuta ahadi mlizofanyiwa? Hakika, chini ya mwongozo wa mwangaza Wangu, mtapenya katika utawala wa nguvu za giza. Hakika, katikati ya giza, hamtaupoteza mwangaza unaowaongoza. Hakika mtakuwa bwana wa viumbe vyote. Hakika mtakuwa washindi mbele ya Shetani. Hakika, wakati wa maangamizi ya ufalme wa joka kubwa jekundu, mtasimama miongoni mwa umati mkubwa kushuhudia ushindi Wangu. Hakika mtasimama imara na thabiti katika nchi ya Sinimu. Kupitia katika mateso mnayoyavumilia, mtarithi baraka zinazotoka Kwangu, hakika mtaonyesha utukufu Wangu katika ulimwengu mzima(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima, Sura ya 19). Nguvu ya neno la Mungu haina mipaka na imesababisha imani yangu kuongezeka; nilikuwa na azimio la kupambana na Shetani hadi mwisho. Yule askari muovu alipochoka kunipiga, aliniuliza tena: “Je, utasema?” Nilisema kikiki: “Hata ukinipiga hadi nife, bado sitajua!” Yule askari muovu aliposikia hayo, hakuweza kufanya chochote. Akatupa kamba na kusema: “Wewe ni mkaidi kweli, kama nyumbu. Kwa kweli wewe ni mzuri, huwezi kusema chochote hata ukifa. Ulipata kutoka wapi nguvu na imani nyingi jinsi hii? Wewe kwa kweli ni Liu Hulan zaidi ya Liu Hulan” Nilipomsikia akisema haya, ilikuwa ni kama nilimwona Mungu ameketi kwenye kiti Chake cha enzi kwa ushindi, akimwangalia Shetani akifedheheshwa. Nililia nusu na kumtukuza Mungu nusu: Ee Mungu, kwa kuitegemea nguvu Yako, ninaweza kumshinda Shetani, yule pepo! Kwa sababu ya ukweli huo, naona kwamba Wewe ni mwenye kudura na Shetani hana nguvu; Shetani daima atashindwa chini ya udhibiti Wako. Usipomruhusu, Shetani hataweza kunitesa hadi nife. Wakati huu, maneno ya Mungu yalinipa nuru tena: “Tabia ya Mungu ni ile ambayo inamilikiwa na Mtawala wa vitu vyote na viumbe vyote vyenye uhai…. Tabia Yake ni ishara ya mamlaka … ni ishara ya Yeye ambaye hawezi[a] kushindwa au kushambuliwa na giza na nguvu yoyote ya adui …(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ni Muhimu Sana Kuelewa Tabia ya Mungu). Baada ya kupitia mateso katili ya joka kubwa jekundu, kwa kweli niliona upendo wa Mungu na wokovu kwangu na nilipitia nguvu na mamlaka ya neno la Mungu. Bila neno la Mungu kuniongoza kila hatua ya njia na kwa kutegemea tu nguvu yangu mwenyewe, haingewezekana kwangu kuyashinda mateso na kupigwa kwa joka kubwa jekundu. Vivyo hivyo, lilinifanya nione taswira yenyekuweza kudhuruiwa na iliyopondwapondwa ya joka kubwa jekundu. Nilikielewa kiini cha pepo cha unyama walo na kutojali kwalo kwa uhai na nililichukia na kulilaani ndani ya moyo wangu. Nilipenda kuvunja kabisa uhusiano wote nalo na kumfuata Kristo na kumtumikia Kristo milele.

Siku iliyofuata, askari waovu walikuja na kunihoji tena, kwa kweli walishangaa na kusema: “Ni nini kibaya na uso wako?” Nilipotazama katika kioo, sikuweza kujitambua; askari muovu alikuwa ameupiga uso wangu mijeledi kwa kamba siku iliyopita na ulikuwa umevimba sana na kuwa mweusi na bluu na kuwa kama panda. Nilipoona kuwa uso wangu ulikuwa umebadilika kabisa mpaka kutotambulika, nilihisi chuki kali kwa joka kubwa jekundu na nikafanya azimio langu kuwa shahidi. Sikuweza kabisa kuruhusu njama yake ishinde! Miguu yangu ilikuwa imepigwa vibaya sana kiasi kwamba sikuweza kutembea na wakati nilipokwenda msalani, niliweza kuona kwamba miguu yangu yote haikuwa na hali ya kawaida iliyobaki, kila kitu kilikuwa cheusi na bluu. Mmoja wa askari waovu akasema: “Hakuna haja ya wewe kuteswa hivi; ukiongea basi hutahitaji kuteseka; unajifanyia hivi mwenyewe! Lifikirie; kiri na tutakutuma nyumbani kwa mumeo na binti yako.” Baada ya kumsikia akisema haya, nilimchukia kabisa. Baadaye, walibadilisha mbinu zao na wakaanza kushika zamu kwa kutoniruhusu nilale mchana kutwa na usiku kucha. Nilipoanza kulala, wangepiga yowe na kupiga kelele kubwa ili kuniamsha; walijaribu kuivunja dhamira yangu kwa kutoniruhusu kulala ili nizungumze kwa usahaulifu, katika hali ya akili isiyobainika. Nilimshukuru Mungu kwa kunilinda. Ingawa wale askari waovu waliniweka kwa muda wa siku nne mchana na usiku, haikujalisha jinsi walivyonihoji, nilimtegemea Mungu kwa ustahimilivu na imani, na sio tu kwamba sikuwa na usahaulifu, lakini nilikuwa macho mno. Askari waovu waliponihoji tena na tena, wakasononeka zaidi na zaidi na wakawa wenye kukata tamaa. Walianza kutekeleza masaili ya shingo upande; walitoa matusi na kulalamika, walikasirikia kwamba nilikuwa nimewasababisha kupoteza hamu yao ya kula, kutopata mapumziko mazuri, na kuteswa na mimi, walihisi kuwa walikuwa na bahati mbaya sana. Hatimaye, yote waliyofanya yalikuwa kuniuliza maswali ya kawaida na hawakuwa tena na utashi wa kunihoji. Katika duru hii ya vita Shetani aliishia kushindwa tena.

Askari waovu hawakuachia hapo, walijaribu kunitongoza. Askari mmoja muovu alikuja na kuweka vidole chini ya kidevu changu, akachukua mkono wangu na kusema jina langu. Kwa sauti ya “upendo” akasema: “Wewe ni mzuri sana; haina thamani kuteseka sana hapa. Matatizo yoyote uliyo nayo, naweza kukusaidia kuyatatua. Imani yako kwa Mungu haijakupatia kitu. Nina nyumba mbili, siku moja, nitakuleta huko ili uwe na burudani; sisi wawili tunaweza kutengeneza ubia. Ukikiri, basi utakuwa huru. Chochote unachotaka, naweza kukusaidia. Sitakutendea bila haki….” Niliposikia uongo wake mbaya, mchafu sana, nilijihisi kuchafuka moyo na kwa nguvu zote nilimkataa. Hakuwa na chaguo jingine bali kuondoka kwa aibu. Hili lilinifanya niwaelewe kabisa hawa watu waliolaaniwa na wasio na aibu wanaodaiwa kuwa “polisi wa watu.” Ili kupata malengo yao wenyewe, wao hutumia mbinu zilizolaaniwa na za kishenzi bila aibu yoyote; hawana heshima yoyote au uadilifu; kwa kweli wao ni pepo wabaya na wachafu!

Hao askari waovu walikuwa na njama moja ya ujanja baada ya nyingine na waliitumia vibaya watu wa familia yangu kujaribu kunishurutisha, wakisema: “Unamwamini Mungu tu, hufikirii juu ya mume wako, binti, wazazi, na watu wengine wa familia; binti yako atakwenda shuleni siku fulani na kutafuta kazi. Ukishikilia imani yako, hili litaathiri moja kwa moja matarajio yake ya mustakabali. Je, utaruhusu hili lifanyike kwake? Wewe humfikirii; Je, una moyo mgumu wa kumruhusu ahusike katika hili?” Kufuatia hili, walimleta mume wangu, binti, na shangazi ndani ili kuwaacha wajaribu kunishawishi. Nilipomwona binti yangu ambaye sikuwa nimemwona kwa miaka kadhaa, machozi yangu yalitiririka bila kuzuilika. Wakati huu, niliomba kwa nguvu zangu zote kwa Mungu: “Ee Mungu, nakuomba Uulinde moyo wangu, kwa sababu mwili wangu ni dhaifu mno. Wakati huu, siwezi kukamatwa na hila za Shetani na siwezi kujaribiwa na Shetani kuanguka katika hisia zangu; Siwezi kumsaliti Mungu au kuwasaliti ndugu zangu wa kiume na wa kike; namwomba tu Mungu awe pamoja nami na kunipa imani na nguvu.” Shangazi akaniambia: “Fanya haraka na uzungumze, kwa nini wewe ni mjinga hivi? Ina thamani yoyote kupitia hili kwa sababu ya imani yako kwa Mungu? Ni nani atakayekushughulikia iwapo chochote kitatokea? Mama yako na baba yako wanahangaika juu yako, wana wasiwasi kila siku kukuhusu, hawawezi kula au kulala vizuri. Ni lazima utufikirie na urudi na kuishi maisha na sisi. Usimwamini Mungu. Angalia ni shida gani ulizopitia kwa sababu ya imani yako kwa Mungu; kwa nini unajisumbua?” Ingawa nilikuwa dhaifu, nililindwa na Mungu na nilitambua kuwa hili lilikuwa pambano la kiroho na niliweza kugundua hila za Shetani; maneno ya Mungu yalinikumbusha moyoni mwangu kwamba: “… lazima umridhishe Mungu, ingawa unaweza kulia kwa uchungu au uhisi kusita kuhusu kuacha kitu unachopenda(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Wale Wanaopaswa Kukamilishwa Lazima Wapitie Usafishaji). Wakati huo, nilimwambia: “Shangazi, usijaribu kunishawishi, nimesema kila kitu ninachopaswa kuwaambia. Sijui nini kingine ninachopaswa kuwaambia. Wanaweza kunitendea kwa hali yoyote wanayotaka, ni juu yao. Hupaswi kujali kunihusu. Unapaswa kurudi!” Wakati wale askari waovu walipoona mwelekeo wangu imara, hawakuwa na uchaguzi mwingine bali kuiruhusu familia yangu irudi. Njama na mipango ya hao polisi waovu zilikuwa zimeshindwa, na walikuwa na hasira sana kwambawalisaga meno yao na kusema: “Kwa kweli wewe ni mkatili! Wewe una ubinafsi sana. Kwa hakika huna asili ya binadamu. Mungu wako yuko wapi? Kama Yeye ni mwenyezi sana, basi kwa nini Anaruhusu uteswe hapa? Kwa nini Mungu wako haji na kukuokoa? Kama kwa kweli kuna Mungu, basi kwa nini Yeye haji na kufungua pingu zako na kukuokoa? Mungu yuko wapi? Usidanganywe na uongo huu, usiwe mjinga. Hujachelewa mno kuamka na kuuona ukweli. Usipokiri, basi tutakupeleka gerezani kwa miaka mingi!” Uongo wa askari hawa waovu ulinifanya nifikirie kuonekana kwa Bwana Yesu akisulubishwa msalabani. Mungu mwenyewe alikuja na kuwa mwili ili kuwakomboa wanadamu wote; kila kitu Alichokifanya kilikuwa ni kwa manufaa ya mwanadamu; hata hivyo, alidhihakiwa, kukashifiwa, kushtakiwa, kukufuriwa, kutukanwa, na kuuawa na Mafarisayo na wale waliokuwa na mamlaka. Mungu alipitia fedheha mno ili kuwaokoa wanadamu, na hatimaye alitundikwa msalabani kwa ajili ya wanadamu. Maumivu yote ambayo Mungu alipitia ni kwa ajili ya wanadamu na leo maumivu ninayoyapitia ni maumivu ninayohitaji kuyapitia. Kwa sababu nina sumu ya joka kubwa jekundu, Mungu anatumia mazingira haya kwa upande mmoja ili kunipima, na kwa upande mwingine ili kuniruhusu kuelewa kwa hakika asili mbaya ya joka kubwa jekundu na, kulidharau na kulisaliti joka kubwa jekundu, na kumfuata Mungu kikamilifu. Kama vile tu neno la Mungu linavyosema: “Mungu anakusudia kutumia sehemu ya kazi ya pepo wachafu ili kuikamilisha sehemu ya mwanadamu, ili watu hawa waweze kufahamu matendo ya mapepo, na kuwawezesha watu wote wawafahamu kwa kweli mababu zao. Ni kwa njia hii pekee wanadamu wanaweza kujinasua kabisa, sio tu kutoroka kizazi cha mapepo, lakini hata zaidi mababu wao. Hili ndilo kusudi la asili la Mungu kulishinda kabisa joka kubwa jekundu, kufanya hivyo ili wanadamu wote wajue umbo halisi la joka kubwa jekundu, Aambue kinyago chake kabisa, na kuona umbo lake halisi. Hili ndilo Mungu anataka kutimiza, nalo ni lengo Lake la mwisho duniani ambalo Amefanyia kazi nyingi sana; Ananuia kulifanikisha hili ndani ya watu wote. Hili linajulikana kama ushawishi wa vitu vyote kwa ajili ya kusudi la Mungu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ufafanuzi wa Mafumbo ya “Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima”, Sura ya 41).

Hatimaye, wale askari waovu walinipeleka kwa kituo cha kizuizi na kunizuia kama mhalifu kwa mwezi mmoja. Katika mwezi huu, walinihoji mara moja zaidi. Kwa siku mbili mchana na usiku, hawakuniacha nilale na hawakunipa chakula cha kutosha. Wakati mwingine hawakunipa chakula chochote, lakini bado ilikuwa bure. Joka kubwa jekundu huwatesa na kuwaumiza watu jinsi hii bila kikomo! Wakati kuzuiliwa kwangu kulipofikia kikomo, walinihukumu miaka miwili ya marekebisho kupitia kwa kazi kwa “kuamini katika Xie Jiao na kuvuruga utaratibu wa jamii” bila ushahidi wowote. Kabla ya kwenda kambi ya kazi, familia yangu ilinitumia yuan 2,000 kwa ajili ya gharama za maisha, lakini zote zilibadhiriwa nao. Pepo hawa walikuwa kweli Shetani na pepo wabaya ambao walikuwa na kiu ya damu na uhai wa binadamu. Ulikuwa ni uovu kabisa! Katika nchi ya joka kubwa jekundu, hakuna sheria; chochote linachopinga, linaweza kuchinja na kunyonya lipendavyo; linaweza kuanzisha mashtaka ya jinai linavyotaka ili kuwadhibiti watu na kuwatesa watu. Joka kubwa jekundu huwasingizia na kuwanasa watu, huwaua watu wasio na hatia, hufanya kitu duni kuwa muhimu, na bila haki huwapachika watu sifa. Wao ni dhehebu halisi na la kweli, wao ni kikundi cha wahalifu wenye utaratibu na majambazi ambao huleta majanga na maafa kwa wanadamu. Kwa miaka miwili katika kambi ya kazi, niliona askari waovu wa serikali ya Kichina kimsingi huwadhulumu vibaya na kuwaamrishaamrisha wafanya kazi kama watumwa. Waliwalazimisha watu kula skonzi zilizookwa kwa mvuke na mchuzi wa mboga kila siku; mchana na usiku, walitulazimisha tufanye kazi ya ziada. Nilichoka kwa namna isiyovumilika kila siku na sikupokea fidia yoyote. Nilipokosa kufanya kazi nzuri, ningepata ukosoaji mkali na adhabu (vifungo virefu, kunyimwa chakula, kulazimishwa kusimama kimya). Wakati huu, hao askari waovu bado hawangeniruhusu niende, walinihoji wakijaribu kunilazimisha kukiri mazingira ya kanisa. Nililichukia vikali, nikitegemea imani na nguvu kutoka kwa Mungu, nikasema kwa hasira: “Mmenipiga na kuniadhibu; mnataka nini kingine? Nimesema kila kitu ninachopaswa kusema; mnaweza kunihoji kwa miaka kumi, miaka ishirini, na bado sitajua chochote. Mnaweza kusahau kuhusu hilo!” Waliposikia hili, wakasema kwa ghadhabu: “Huwezi kuponyeka, unaweza kusubiri hapa tu!” Hatimaye, hao askari waovu waliondoka kwa aibu na kushindwa.

Baada ya kupitia mateso ya kinyama ya joka kubwa jekundu na matendo ya kikatili pamoja na kuishi bila haki gerezani kwa miaka miwili, niliona kwa dhahiri kwamba tabia ya joka kubwa jekundu ni uongo, uovu, kiburi, na ukali. Ni chini ya mifugo. Wao hufikia kiwango cha kuweka mabango yakisema “uhuru wa kidini,” kisha wanakwenda huku na huko wakiwafuatilia na kuwatesa wateule wa Mungu kwa kila njia iwezekanayo. Wao kwa wayowayo huivuruga na kuivunja kazi ya Mungu. Wao ni wauaji ambao huua bila kupepesa jicho, wao ni majambazi ambao hupora kwa kisingizio cha “sadaka, haki, amani, na uadilifu.” Mwishowe, barakoa zao zimeambuliwa kabisa kupitia hekima ya kazi ya Mungu, na nyuso zao mbaya za pepo zimefunuliwa katika mwanga ili niweze kufungua mawanda yangu ya maono na kuamka kutoka katika ndoto yangu. Kama vile tu neno la Mungu linavyosema: “Kwa maelfu ya miaka hii imekuwa ni nchi ya uchafu, ni chafu sana, shida zimejaa, mizimu wanakimbia kila mahali, wakihadaa na kudanganya, wakitoa tuhuma zisizokuwa na msingi,[1] wakiwa katili na waovu, wakikandamiza mji huu ulio mahame na kuuacha ukiwa umetapakaa maiti; harufu ya uozo inaijaza nchi na kuenea hewani, na inalindwa isivyo kawaida.[2] Nani awezaye kuuona ulimwengu kupita anga? Ibilisi anaufunga mwili wote wa mwanadamu, anafumba macho yake yote, na kufunga kinywa chake kwa nguvu. Mfalme wa pepo amefanya ghasia kwa maelfu kadhaa ya miaka, hadi leo hii, wakati bado anaangalia kwa karibu mji ulio mahame kana kwamba ulikuwa kasiri la pepo lisilopenyeka; kundi hili la walinzi, wakati uo huo, wakiangalia kwa macho yanayong’aa, wakiogopa sana kwamba Mungu atawakamata bila wao kujua na kuwafutilia wote mbali, Akiwaacha wakiwa hawana sehemu ya amani na furaha. Inawezekanaje watu wa mji wa mahame kama huu wawe wamewahi kumwona Mungu? Je, wamekwishawahi kufurahia uzuri na upendo wa Mungu? Wanathamini vipi masuala ya ulimwengu wa kibinadamu? Ni nani miongoni mwao anayeweza kuelewa matakwa ya kina ya Mungu? Haishangazi, basi, kwamba Mungu mwenye mwili abaki kuendelea kuwa Amefichwa: Katika jamii ya giza kama hii, ambapo pepo hawana huruma na ni katili, inawezekanaje mfalme wa pepo anayeua watu bila hisia yoyote, avumilie uwepo wa Mungu ambaye ni mwenye upendo, mpole, na mtakatifu? Anawezaje kushangilia na kufurahia ujio wa Mungu? Vikaragosi hawa! Wanalipa upole kwa chuki, wanamtweza Mungu kwa muda mrefu, wanamtukana Mungu, ni washenzi kupita kiasi, hawamjali Mungu hata kidogo, wanapora na kuteka nyara, wamepoteza dhamiri yote, wanaenda kinyume na dhamiri yote, na wanawajaribu watu wasiokuwa na hatia kuwa watu wasiokuwa na uwezo wa kuhisi. Wazazi wa kale? Viongozi Wapendwa? Wote wanampinga Mungu! Udukuzi wao umeacha wote walio chini ya mbingu katika hali ya giza na machafuko! Uhuru wa dini? Haki halali na matakwa ya wananchi? Zote hizo ni njama za kufunika dhambi!(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kazi na Kuingia (8)).

Mwenyezi Mungu milele ni mwenye hekima, mwenye kudura na wa ajabu, na Shetani, joka kubwa jekundu, milele ni wa kusikitisha, mchafu na asiyeweza. Bila kujali jinsi alivyo mshenzi na mkosa nidhamu, na bila kujali jinsi hujitahidi na kuasi, daima atakuwa chombo cha Mungu kuwafundishia watu Wake wateule. Aidha, limehukumiwa kubagwa kuzimu na Mungu kama adhabu ya milele. Linajaribu kuvunja dhamira ya watu kupitia mateso yake ya kinyama ili watu waweze kujitenga na Mungu na kumtelekeza Mungu. Lakini limekosea! Mateso yake hutufanya tuone kwa usahihi kiini cha pepo. Ni jambo linalotuamsha kabisa kulisaliti kabisa na kuwa na imani na ujasiri kumfuata Mungu kwenye njia sahihi ya uzima. Daima nitamtegemea Mungu mwenye busara na mwenyezi. Kuanzia sasa kwendelea, bila kujali ni hatari zipi kemkem na shida zilizo kwa njia iliyo mbele, nitamfuata Mungu kwa uthabiti mpaka mwisho na kuwa na ushuhuda wa nguvu Kwake ili kuliaibisha joka kuu jekundu.

Tanbihi:

1. “Wakitoa tuhuma zisizokuwa na msingi” inahusu mbinu ambazo ibilisi hutumia huwadhuru watu.

2. “Inalindwa isivyo kawaida” inaonyesha kuwa mbinu ambazo ibilisi hutumia huwatesa watu ni mbovu hasa, na kuwadhibiti watu sana kiasi kwamba hawana nafasi ya kusogea.

a. Maandishi asilia yanasema “ni ishara ya kutoweza.”

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Ujana Usio na Majuto Yoyote

Xiaowen Jijini Chongqing“‘Upendo,’ kama unavyoitwa, unaashiria hisia safi isiyo na dosari, ambapo unatumia moyo wako kupenda, kuhisi,...

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp