Sura ya 36

Mwenyezi Mungu wa kweli, Mfalme katika kiti cha enzi, hutawala ulimwengu mzima, Anakabiliana na mataifa yote na watu wote, na kila kitu chini ya mbingu hung'aa kwa utukufu wa Mungu. Viumbe vyote hai katika ulimwengu na hadi miisho ya dunia vitaona. Milima, mito, maziwa, ardhi, bahari, na viumbe vyote viishivyo, katika nuru ya uso wa Mungu wa kweli, na wamesisimka kana kwamba wameamka kutoka ndotoni, kana kwamba wao ni chipuko zinazochipuka kutoka mchangani!

Ah! Mungu mmoja wa kweli, Huonekana mbele ya dunia. Je, nani anathubutu kumtendea kwa upinzani? Kila mmoja hutetemeka kwa hofu. Hakuna ambao hawajaridhishwa kabisa, mara kwa mara kuomba msamaha, wote kwa magoti yao mbele Yake, vinywa vyote vikimuabudu! Mabara na bahari, milima, mito, vitu vyote kumsifu bila kikomo! Vuguvugu la upepo mwanana wa masika huja na masika kuleta mvua mzuri wa masika. Kama watu wote, mikondo ya mito hutiririka kwa huzuni na furaha, ikitoa machozi ya kuwiwa na kujilaumu. Mito, maziwa, chafuko na mawimbi, yote yanaimba, yakihimidi jina takatifu la Mungu Wa kweli! Sifa hizi zinavuma kwa wazi sana! Mambo yote ya zamani ambayo kwa wakati mmoja yalikuwa yamepotoshwa na Shetani, kila mmoja atafanyia upya, atabadilika, na kuingia katika hali mpya kabisa …

Hili ni tarumbeta takatifu linasikika! Sikiliza. Sauti hiyo, tamu sana, ni kiti cha enzi kinatoa mlio, kutangaza kwa mataifa yote na watu, wakati umefika, hatima ya mwisho imefika. Mpango Wangu wa usimamizi umemalizika. Ufalme Wangu huonekana hadharani duniani. Falme za duniani zimekuwa ufalme—wa Mungu—Wangu. Matarumbeta Yangu saba yanasikika kutoka kwenye kiti cha enzi, na ni maajabu gani yatatokea! Watu katika miisho ya dunia watakurupuka pamoja kutoka kila upande kwa nguvu ya lundo na uwezo wa radi, baadhi yao baharini, baadhi yao wakiendesha ndege, baadhi yao watakuja kwa magari ya kila muundo na ukubwa, baadhi yao watakuja mgongoni mwa farasi. Angalia kwa karibu. Sikiliza kwa makini. Hawa wapandao farasi wa kila rangi, pepo kuchochewa, wenye majivuno na waadhimu, kama kuchukua uwanja wa vita, wao hawajali kifo. Katikati ya milio ya farasi na makelele ya watu ya kupiga mayowe wakimwita Mungu wa kweli, wanaume, wanawake na watoto wengi watakanyagwa na kwato zao mara moja. Baadhi yao watakufa, baadhi yao watakuwa wakivuta pumzi yao ya mwisho, baadhi yao watapondwa, pasipo na mtu wa kuwatunza, wakipiga kelele kwa kupagawa, wakilia kwa uchungu. Wana wa uasi! Je, hizi si hatima zenu za mwisho?

Hufurahia kuona watu Wangu, ambao husikia sauti Yangu, na kukusanyika kutoka kila taifa na nchi. Watu wote, uhifadhi Mungu wa kweli daima katika midomo yao, kusifu na kuruka kwa furaha bila kukoma! Wao huushuhudia kwa ulimwengu, na sauti ya ushuhuda wao kwa Mungu wa kweli ni kama sauti ya ngurumo ya maji mengi. Watu wote watasongamana katika ufalme Wangu.

Matarumbeta Yangu saba yatapaza sauti, kuamsha walio lala! Shughulika kwa haraka, muda hujakwisha. Angalia maisha yako! Fungua macho yako na uone ni wakati upi sasa. Ni nini unatafuta? Kuna nini ya kufikiri? Na ni nini kilicho cha kushikilia? Je, inawezekana kuwa bado hujafikiria tofauti katika thamani kati ya kupata maisha Yangu na mambo yote unayopenda na kushikilia? Acha kuwa makaidi na kucheza kila mahali. Usikose nafasi hii. Wakati huu hautakuja tena! Simama mara moja, tenda kufanyisha roho yako mazoezi, kutumia zana mbalimbali kukuwezesha na kuzuia kila njama na hila za Shetani, na umshinde Shetani, ili kwamba uzeofu wako wa maisha uweze kuwa wa kina zaidi na uweze kuishi kwa kudhihirisha tabia Yangu, ili maisha yako yaweze kukomaa na yawe yenye tajriba na ili uweze daima kufuata nyayo Zangu. Ukiwa bila hofu, ukiwa usiye udhaifu, daima ukisonga mbele, hatua kwa hatua, moja kwa moja hadi mwisho wa njia!

Wakati matarumbeta saba zitatoa sauti tena, itakuwa mwito wa hukumu, hukumu ya wana wa uasi, hukumu ya mataifa yote na watu wote, na kila taifa litajisalimisha mbele ya Mungu. Uso wa utukufu wa Mungu hakika utaonyeshwa mbele ya mataifa yote na watu wote. Kila mtu atakuwa ameridhishwa kabisa, kupiga kelele kwa Mungu wa kweli bila kikomo. Mwenyezi Mungu Atakuwa Mtukufu zaidi, na wanangu watashiriki katika utukufu, kushiriki ufalme nami, kuhukumu mataifa yote na watu wote, kuadhibu maovu, kuokoa na kuwa na huruma juu ya watu ambao ni Wangu, kuleta uthabiti na utulivu kwa ufalme. Kupitia sauti ya matarumbeta saba, kundi kubwa la watu litaokolewa, kurudi mbele Yangu kupiga magoti na kuabudu, kwa sifa daima!

Wakati matarumbeta saba zitatoa sauti mara nyingine tena, hilo litakuwa tukio la hitimisho la mwisho wa enzi, mlipuko wa sauti wa tarumbeta ya ushindi dhidi ya ibilisi Shetani, saluti katika mwanzo wa maisha ya wazi wa ufalme duniani! Sauti hii ya kifahari sana, sauti hii inayonguruma pande zote za kiti cha enzi, mlipuko wa sauti ya tarumbeta inayotikisa mbingu na dunia, ni ishara ya mpango Wangu wa usimamizi, na hukumu ya Shetani, kuadhibu duniani hii ya zamani kwa kifo kabisa, jahanamu! Huu mlipuko wa sauti ya tarumbeta unaashiria kwamba lango la neema ni linafungika, kwamba uhai wa ufalme utaanza duniani, ambayo ni kamilifu kabisa. Mungu Huokoa wale wanaompenda. Mara tu watakaporudi kwa ufalme Wake, watu duniani watakabili njaa, ndwele ya kufisha, na mabakuli saba ya Mungu, tauni saba zitaanza kutumika kwa mfululizo. Mbingu na dunia zitapita, lakini neno Langu halitapita!

Iliyotangulia: Sura ya 35

Inayofuata: Sura ya 37

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp