Kuwa na Tabia Isiyobadilika Ni Kuwa katika Uadui na Mungu

Baada ya miaka elfu kadhaa ya upotovu, mwanadamu amekuwa asiyehisi na mpumbavu, pepo anayempinga Mungu, kwa kiasi kwamba uasi wa mwanadamu kwa Mungu umeandikwa katika vitabu vya historia, na hata mwanadamu mwenyewe hana uwezo wa kutoa ripoti kamili ya tabia zake za uasi wake—kwa kuwa mwanadamu amepotoshwa sana na Shetani, na amehadaiwa na Shetani kiasi kwamba hajui ni wapi pa kugeukia. Hata wa leo, mwanadamu bado anamsaliti Mungu: Wakati mwanadamu anamwona Mungu, anamsaliti, na wakati yeye hawezi kumwona Mungu, bado anamsaliti. Kuna hata wale ambao, baada ya kushuhudia laana ya Mungu na ghadhabu ya Mungu, bado wanamsaliti. Na hivyo Nasema kwamba hisia ya mwanadamu imepoteza kazi yake ya awali, na kwamba dhamiri ya mwanadamu, pia, imepoteza kazi yake ya awali. Mwanadamu Ninayemtazamia ni mnyama katika mavazi ya binadamu, yeye ni nyoka mwenye sumu, haijalishi jinsi anavyojaribu kuonekana mwenye kuhurumiwa machoni Pangu, Sitawahi kamwe kuwa na huruma kwake, kwa kuwa mwanadamu hana ufahamu wa kutofautisha kati ya nyeusi na nyeupe, tofauti kati ya ukweli na yasiyo ya kweli. Hisia ya mwanadamu ni usiohisi chochote, ilhali bado anataka apate baraka; ubinadamu wake si wa kuheshimika lakini bado anataka kumiliki ukuu wa mfalme. Ataweza kuwa mfalme wa nani, na hisia kama hiyo? Jinsi gani yeye na ubinadamu kama huo ataweza kukaa kwenye kiti cha enzi? Mwanadamu kwa kweli hana aibu! Yeye ni mdhalili wa kujivuna tu! Kwa wale kati yenu mnaotaka kupokea baraka, Ninawashauri kwanza mtafute kioo na kuangalia picha zenu mbaya—je, una kile kinachohitajika kuwa mfalme? Je, una uso wa mwanadamu ambaye anaweza kupata baraka? Hakujawa mabadiliko hata madogo katika tabia yako na wewe hujaweka ukweli wowote katika vitendo, ilhali bado unatamani kuona siku ifuatayo ikiwa ya ajabu. Unajihadaa mwenyewe! Kwa sababu ya kuzaliwa katika nchi ya uchafu vile, mwanadamu ameangamizwa kabisa na jamii, amekuwa akishawishiwa na maadili ya kikabaila, na amefundisha katika “taasisi za elimu ya juu.” Fikra zilizo nyuma kimaendeleo, maadili potovu, mtazamo mbaya juu ya maisha, falsafa za kudharauliwa za kuishi, uwepo usio na thamani, na hali potovu za maisha na desturi—mambo yote haya yameuingilia moyo wa mwanadamu, na kudhoofisha na kushambuliwa dhamiri yake pakubwa. Matokeo yake, mwanadamu kamwe yuko mbali kutoka kwa Mungu, na kila mara anampinga. Tabia ya mwanadamu inakuwa matata zaidi kila siku, na hakuna hata mmoja ambaye kwa hiari yake atatoa chochote kwa ajili ya Mungu, hakuna hata mmoja ambaye kwa hiari atamtii Mungu, wala, zaidi ya hayo, mwanadamu mmoja ambaye kwa hiari yake atatafuta uso wa Mungu. Badala yake, chini ya umiliki wa shetani, mwanadamu hafanyi kitu ila kukimbiza anasa, kujitoa mwenyewe kwa upotovu wa mwili katika nchi ya matope. Hata wanaposikia ukweli, wale wanaoishi gizani hawafikiri kuuweka katika vitendo, na wala kuelekea kumtafuta Mungu hata kama wameuona mwonekano Wake. Jinsi gani wanadamu wapotovu kiasi hiki wawe na nafasi yoyote ya wokovu? Jinsi gani wanadamu waovu kiasi hiki kuishi katika mwanga?

Kubadilisha tabia ya mwanadamu huanza na maarifa ya kiini chake na kupitia mabadiliko katika mawazo yake, asili, na mtazamo wa akili—kwa njia ya mabadiliko ya msingi. Ni kwa njia hii tu ndio mabadiliko ya kweli yatapatikana katika tabia ya mwanadamu. Tabia ya upotovu ya mwanadamu inatokana na hali yake ya kupewa sumu na kukanyagwa na Shetani, kutokana na madhara mabaya sana ambayo Shetani ameweka katika mawazo yake, maadili, ufahamu, na hisia. Ni hasa kwa sababu mambo ya msingi ya mwanadamu yamepotoshwa na Shetani, na ni tofauti kabisa na jinsi Mungu aliwaumba kwa asili, kwamba mwanadamu humpinga Mungu na haelewi ukweli. Hivyo, mabadiliko katika tabia za mwanadamu lazima yaanze na mabadiliko katika mawazo yake, ufahamu na hisia ambayo yatabadilisha maarifa yake ya Mungu na maarifa yake ya ukweli. Wale waliozaliwa katika nchi potovu zaidi ndio wasiojua zaidi kumhusu kile Mungu Alicho, au kunamaanisha nini kumwamini Mungu. Jinsi watu walivyo wapotovu zaidi, ndivyo wanavyokosa kujua kuwepo kwa Mungu na ndivyo hisia zao na utambuzi huwa duni. Chanzo cha upinzani wa mwanadamu na uasi dhidi ya Mungu ni kupotoshwa kwake na Shetani. Kwa sababu amepotoshwa na Shetani, dhamiri ya mwanadamu imekuwa bila hisia, yeye ni mwovu, mawazo yake yamepotoka, na ana mtazamo duni. Kabla ya kupotoshwa na Shetani, mwanadamu kawaida alimfuata Mungu na alitii maneno Yake baada ya kuyasikia. Alikuwa kawaida mwenye akili timamu na dhamiri, na wa ubinadamu wa kawaida. Baada ya kupotoshwa na Shetani, hali yake ya awali, dhamiri, na ubinadamu vilidhoofika sana na viliharibiwa na shetani. Hivyo, yeye amepoteza utii wake na upendo kwa Mungu. Akili ya mwanadamu imekuwa potovu, tabia yake imekuwa sawa na ile ya mnyama, na uasi wake kwa Mungu kabisa umekuwa wa mara kwa mara na wa kuhuzunisha zaidi. Hata hivyo mwanadamu bado hajui wala kutambua hili, na kwa upofu anapinga na kuasi. Ufunuo wa tabia ya mwanadamu ni udhihirisho wa hisia zake, utambuzi na dhamiri, na kwa sababu hisia yake na utambuzi si timamu, na dhamiri yake imezidi kuwa ndogo zaidi, hivyo tabia yake ni ya uasi dhidi ya Mungu. Kama hisia ya mwanadamu na utambuzi hauwezi kubadilika, basi mabadiliko katika tabia yake hayawezekani, sawa na kuwa baada ya moyo wa Mungu. Kama hisia ya mwanadamu sio timamu, basi hawezi kumhudumia Mungu na hafai kutumiwa na Mungu. “Hisia za Kawaida” inaashiria kutii na kuwa mwaminifu kwa Mungu, kuwa mwenye imani kamili kwa Mungu, na kwa kuwa na dhamiri kwa Mungu. Inamaanisha kuwa na moyo mmoja na akili kwa Mungu, na si kwa kumpinga Mungu kwa makusudi. Wale ambao ni wa akili potovu hawako hivi. Tangu mwanadamu aharibiwe na Shetani, ametunga dhana kuhusu Mungu, na yeye hajakuwa na uaminifu au kumtamani Mungu, pia hana dhamiri kwa Mungu. Mwanadamu kwa makusudi anapinga na huweka hukumu juu ya Mungu, na, zaidi ya hapo, anatupa shutuma Kwake nyuma Yake. Mwanadamu anajua vizuri kuwa Yeye ni Mungu, lakini bado humhukumu nyuma ya mgongo wake, hana nia ya kumtii, na hufanya madai ya kipofu na maombi kwa Mungu. Watu wa aina hii—watu walio na akili potovu—hawana uwezo wa kujua tabia zao za kudharauliwa au ya kujuta uasi wao. Kama watu wana uwezo wa kujijua wenyewe, basi wao wamerudisha kiasi kidogo cha akili zao; Zaidi ya vile watu wanavyomuasi Mungu lakini hawajui wenyewe, ndivyo walivyo zaidi wenye akili isiyo timamu.

Chanzo cha ufunuo wa upotovu wa tabia ya mwanadamu ni dhamiri yake iliyofifia, asili yake mbovu na akili yake isiyo timamu; kama dhamiri ya mwanadamu na hisia vinaweza kurudi kawaida, basi atafaa kwa matumizi mbele ya Mungu. Ni kwa sababu tu kuwa dhamiri ya mwanadamu daima imekuwa isiyosikia, akili ya mwanadamu haijawahi kuwa timamu, na inazidi kuwa hafifu ndio mwanadamu amezidisha uasi wake kwa Mungu, hata akampiga Yesu misumari juu ya msalaba na kumkataa Mungu mwenye mwili wa siku za mwisho kuingia katika nyumba yake, na analaani mwili wa Mungu, na anaona mwili wa Mungu kuwa wa hali ya chini. Kama mwanadamu angekuwa na ubinadamu kidogo, hangekuwa mkatili kiasi hicho katika utendeaji wake wa mwili wa Mungu mwenye mwili; kama angekuwa na akili hata kidogo tu, hangekuwa hivyo katika utendeaji wake wa mwili wa Mungu mwenye mwili; kama angekuwa na dhamiri hata kidogo, hangekuwa mwenye “shukrani” kwa Mungu mwenye mwili kwa njia hii. Mwanadamu anaishi katika enzi ya Mungu kuwa katika mwili, lakini yeye hawezi kumshukuru Mungu kwa kumpatia nafasi nzuri kiasi hicho, na badala yake analaani kuja kwa Mungu, au kupuuza kabisa ukweli wa Mungu aliyepata mwili, na inaonekana anapinga hali hii na anachoshwa nayo. Haijalishi jinsi mwanadamu anachukua kuja kwa Mungu, Mungu, kwa ufupi, daima ameendeleza kazi yake kwa uvumilivu—hata kama mwanadamu hajawahi kumkaribisha, na bila kujua yeye hufanya maombi kwa Mungu. Tabia ya mwanadamu imekuwa mbaya zaidi, akili yake imekuwa hafifu zaidi, na dhamiri yake imekanyagwa kabisa na yule muovu na kwa muda mrefu imekoma kuwa dhamiri ya awali ya mwanadamu. Mwanadamu hajakosa tu shukrani kwa Mungu mwenye mwili kwa kukabidhi maisha na neema nyingi juu ya wanadamu, bali pia anachukia Mungu kwa kumpatia ukweli; ni kwa sababu mwanadamu hana haja ya kujua ukweli hata kidogo ndio maana anamchukia Mungu. Haitoshi kwamba mwanadamu hawezi kuutoa uhai wake kwa ajili ya Mungu mwenye mwili tu, lakini pia anajaribu kutoa neema kutoka kwa Mungu, na anafanya madai kwa Mungu yaliyo mara kadhaa kubwa kuliko kile mwanadamu ametoa kwa Mungu. Watu wa dhamiri na hisia kama hizo hufikiria kwamba hili si jambo kubwa, na bado wanaamini kuwa wao wamefanya mengi sana kwa ajili ya Mungu, na kwamba Mungu amewapa kidogo sana. Kuna watu ambao wamenipa bakuli la maji na kisha kunyosha mikono yao na kudai kwamba nilipie bakuli mbili za maziwa, au kunipa chumba kwa usiku mmoja lakini walijaribu kunilipisha mara nyingi zaidi katika ada ya makazi. Ukiwa na ubinadamu kama huo, na dhamiri ya aina hii, ni jinsi gani bado mnatarajia kupata uzima? Nyinyi ni fukara wa kudharauliwa mlioje! Ni kwa sababu ya ubinadamu huu na dhamiri ya mwanadamu ndio maana Mungu mwenye mwili anatembea katika ardhi yote, asipate mahali pa makazi. Wale ambao kwa kweli wanayo dhamiri na ubinadamu wanapaswa kumuabudu na kwa moyo wote kumhudumia Mungu mwenye mwili si kwa sababu ya kiasi cha kazi aliyofanya, lakini hata kama Yeye hangefanya kazi yoyote kamwe. Hili ndilo linafaa kufanywa na wale walio na akili timamu, na ndio wajibu wa mwanadamu. Watu wengi hata huzungumza juu ya masharti katika huduma yao kwa Mungu: Hawajali kama yeye ni Mungu au mwanadamu, na wao huzungumza juu ya masharti yao tu, na kutafuta kuridhisha tamaa zao wenyewe tu. Mnaponipikia, mnadai malipo ya huduma, wakati mnakimbia kwa ajili Yangu, mnadai pesa za mkimbiaji, mkinifanyia kazi mnadai ada ya kazi, mkifua nguo Zangu, mnadai ada ya kufua, wakati mnatoa kwa ajili ya kanisa mnadai malipo ya kurudisha nguvu, mkizungumza, mnadai malipo ya msemaji, mkipeana vitabu mnadai ada ya usambazaji, na wakati mnaandika mnadai malipo ya kuandika. Wale Nimehusiana nao hata hudai malipo kutoka Kwangu, na wale waliotumwa nyumbani hudai fidia kwa uharibifu wa majina yao; wale ambao hawajaoa au kuolewa hudai mahari, au fidia kwa ujana wao waliopoteza, wale wanaochinja kuku wanadai ada ya uchinjaji, wale wanaokaanga chakula wanadai ada ya kukaanga, na wale ambao hupika supu wanadai malipo pia…. Huu ndio ubinadamu wenu mkuu na wenye majivuno, na haya ndiyo matendo yanayoamrishwa na dhamiri yenu yenye joto. Hisia zenu ziko wapi? Ubinadamu wenu uko wapi? Wacha Niwaambie! Mkiendelea hivi Nitakoma kufanya kazi miongoni mwenu. Sitafanya kazi miongoni mwa wanyama waliovalia mavazi ya binadamu, Sitateseka hivyo kwa ajili ya kundi la watu ambao nyuso zao nzuri zimeficha nyoyo za uhasama, Sitavumilia kwa ajili ya kundi la wanyama ambao hawana uwezekano hata kidogo wa kuokolewa. Siku Nitakayowapa mgongo ndiyo siku mtakayokufa, ndiyo siku ambayo giza litakuja juu yenu, na ni siku mtakayoachwa na mwanga. Hebu Niwaambie! Sitakuwa mwema kamwe kwa kundi kama lenu, kundi ambalo liko chini ya hata wanyama! Kuna mipaka katika maneno na matendo Yangu, na vile ubinadamu wenu na dhamiri zilivyo, Sitafanya kazi zaidi, kwani mmekosa dhamiri, umenisababishia maumivu mengi sana, na tabia yenu ya kudharauliwa inanichukiza Mimi sana. Watu wanaokosa utu na dhamira kamwe hawatakuwa na nafasi ya wokovu; Mimi kamwe Sitawaokoa watu kama hao wasio na utu wala shukurani. Siku Yangu itakapofika, Nitanyesha mvua ya moto Wangu mkali milele juu ya wana waasi walioiamsha hasira na ghadhabu yangu kali hapo awali, Nitalazimisha adhabu yangu milele juu ya wanyama wale ambao wakati mmoja waliupa lugha chafu Kwangu na wakaniacha, Nitawachoma wakati wote kwa moto wa hasira Yangu wana wa uasi waliokula na kuishi pamoja Nami lakini hawakuniamini, na wakanitukana na kunisaliti. Nitawatia wote walionikasirisha kwa adhabu Yangu, Nitanyesha ghadhabu Yangu kwa ukamilifu juu ya wanyama hao waliotamani wakati mmoja kusimama kando Yangu kama visawe Vyangu ilhali hawakuniabudu wala kunitii, fimbo Ninayotumia kumgonga mwanadamu itaanguka juu ya wanyama hao waliofurahia utunzaji Wangu na siri Nilizonena, na waliojaribu kuchukua starehe ya mali ya dunia kutoka Kwangu. Sitamsamehe mtu yeyote anayejaribu kuchukua nafasi Yangu; Sitamsamehe yeyote anayejaribu kupokonya chakula na nguo kutoka Kwangu. Kwa sasa, mnabaki huru kutokana na madhara na kuendelea kujiharibia kwa kuzidi katika mahitaji mnayotaka kutoka Kwangu. Siku ya ghadhabu inapofika hamtafanya madai yoyote zaidi Kwangu; wakati huo, Nitawaruhusu “kujifurahia” hadi mtakaporidhika, Nitalazimisha nyuso zenu kuingia mchangani, na kamwe hamtaweza kuinuka tena! Wakati mmoja au mwingine, Ninaenda “kulipiza” madeni hayo kwenu na Natumaini mnasubiri kwa uvumilivu kuwasili kwa siku hii.

Kama viumbe hawa wa kudharauliwa wanaweza kweli kuweka kando tamaa zao kuu na kurudi kwa Mungu, basi wao bado wana nafasi ya wokovu; kama mwanadamu ana moyo ambao kwa kweli unamtamani Mungu, basi yeye hataachwa na Mungu. Mwanadamu anashindwa kumpata Mungu sio kwa sababu Mungu ana hisia, au kwa sababu Mungu hataki kupatikana na mwanadamu, bali ni kwa sababu mwanadamu hataki kumpata Mungu, na kwa sababu mwanadamu hana haraka kumtafuta Mungu. Jinsi gani mmoja wa wale ambao kweli wanamtafuta Mungu alaaniwe na Mungu? Ni jinsi gani mwenye akili timamu na dhamiri nzuri anaweza laaniwa na Mungu? Ni vipi yule anayemwabudu kwa kweli na kumhudumia Mungu ataangamizwa na moto wa ghadhabu yake? Ni jinsi gani mwanadamu aliye na furaha ya kumtii Mungu kutupwa nje ya nyumba ya Mungu kwa mateke? Jinsi gani mwanadamu ambaye hawezi kumpenda Mungu vya kutosha aishi katika adhabu ya Mungu? Jinsi gani mwanadamu ambaye ana furaha ya kuacha kila kitu kwa ajili ya Mungu kuachwa bila chochote? Mwanadamu hana nia ya kumfuata Mungu, hana nia ya kutumia mali yake kwa Mungu, hana nia ya kutoa juhudi za milele kwa Mungu, na badala yake anasema kwamba Mungu amepita kiasi, kwamba mengi kuhusu Mungu yanakinzana na dhana za mwanadamu. Na ubinadamu kama huu, hata kama mngekuwa wakarimu katika juhudi zenu bado hamngeweza kupata kibali cha Mungu, bila kutaja kuwa hamumtafuti Mungu. Je, hamjui kwamba ninyi ni bidhaa mbovu za binadamu? Je, hamjui kwamba hakuna ubinadamu ulio mnyenyekevu zaidi kuliko wenu? Je, hamjui “cheo” chenu ni kipi? Wale ambao kweli wanampenda Mungu wanawaita baba wa mbweha, mama wa mbweha, mwanambweha, na mjukuu wa mbweha; nyinyi ni vizazi vya mbweha, watu wa mbweha, na mnapaswa kujua utambulisho wenu na kamwe msiwahi kuusahau. Msidhani kwamba nyinyi ni kiumbe mkubwa zaidi: Nyinyi ni kundi mojawapo la wasio-wanadamu wabaya zaidi miongoni mwa wanadamu. Je, hamjui lolote kuhusu haya? Je, mnajua ni kiasi gani cha hatari Nimechukua kwa kufanya kazi miongoni mwenu? Kama akili yenu haiwezi kurudi kawaida, na dhamiri yenu haiwezi kufanya kazi kwa kawaida, basi kamwe hamtawahi kuwa huru kutokana na jina “mbwa mwitu”, kamwe hamtaitoroka siku ya laana, kamwe hamtaitoroka siku ya adhabu yenu. Mlizaliwa mkiwa duni, kitu kisicho na thamani yoyote. Kwa hivyo nyinyi ni kundi la mbwa mwitu wenye njaa, rundo la uchafu na takataka, na, tofauti na nyinyi, Mimi Sifanyi kazi kwenu ili nipate chochote, lakini kwa sababu ya haja ya kazi. Mkiendelea kuwa waasi kwa njia hii, basi Nitakomesha kazi Yangu, na kamwe sitafanya kazi kwenu tena; badala yake, Nitahamisha Kazi yangu kwa kundi lingine linalonipendeza, na kwa njia hii kuondoka kwenu milele, kwa sababu Mimi sina nia ya kuwaangalia walio katika uadui na Mimi. Hivyo basi, je, mnataka kulingana na Mimi, au katika uadui dhidi Yangu?

Iliyotangulia: Je, Wewe ni Mtu Ambaye Amepata Uzima?

Inayofuata: Watu Wote Wasiomjua Mungu Ni Watu Wanaompinga Mungu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp