Onyo kwa Wale Wasiotenda Ukweli
Wale ambao daima hutoa uhasi miongoni mwa akina ndugu ni watumishi wa Shetani, na wao ni wasumbufu wa kanisa. Watu kama hao lazima siku moja watimuliwe na waondoshwe. Katika imani yao katika Mungu, ikiwa watu hawana mioyo imwogopayo Mungu, ikiwa hawana mioyo ya utii kwa Mungu, basi si tu kwamba hawataweza kumfanyia kazi yoyote, bali kinyume chake, watakuwa wale wanaosumbua kazi Yake na wanaompinga Yeye. Kumwamini Mungu lakini kutomtii au kumwogopa Yeye, na badala yake kumpinga Yeye, ndiyo aibu kubwa kabisa kwa mwumini. Waumini wakiwa tu wazembe na wasiojizuia katika usemi na mwenendo wao kama vile watu wasio na dini walivyo, basi wao ni waovu hata zaidi kuliko watu wasio na dini; wao ni vielelezo asili vya mapepo waovu. Wale wanaotoa maneno yao yenye sumu na yenye nia mbaya ndani ya kanisa, wanaosambaza uvumi usio na msingi, wanaochochea migawanyiko, na wanaounda magenge miongoni mwa akina ndugu—walipaswa kutimuliwa kutoka kanisani. Hata hivyo kwa sababu sasa ni enzi tofauti ya kazi ya Mungu, watu hawa wanazuiwa, kwani hakika wataondoshwa. Wote ambao wamepotoshwa na Shetani wana tabia potovu. Hata hivyo, wengine wana tabia potovu tu, huku wengine wakiwa tofauti: Si tu kwamba wana tabia potovu za kishetani, bali asili yao pia ni yenye nia mbaya kupita kiasi. Maneno na matendo ya watu hawa yanavuka mipaka ya kufunua tu tabia potovu za kishetani; wao ni ibilisi na Mashetani wa kweli. Yote wanayofanya ni kuvuruga na kusumbua kazi ya Mungu, wanasumbua kuingia katika uzima kwa akina ndugu, na wanaharibu maisha ya kawaida ya kanisa. Ipo siku, mbwa mwitu hawa waliovalia ngozi ya kondoo wataondolewa; mtazamo usio na huruma, mtazamo wa kuwakataa, unapaswa kuchukuliwa kuelekea watumishi hawa wa Shetani. Huku tu ndiko kusimama upande wa Mungu, na wale wanaoshindwa kufanya hivyo wanagaagaa matopeni pamoja na Shetani. Watu wanaomwamini Mungu kwa kweli daima wanaye mioyoni mwao, na daima wanabeba ndani yao moyo umwogopao Mungu, moyo umpendao Mungu. Wale wanaomwamini Mungu wanapaswa kufanya mambo kwa uangalifu na busara, na yote wanayofanya yanapaswa kulingana na matakwa ya Mungu na kuweza kuridhisha moyo Wake. Hawapaswi kuwa wakaidi, wakifanya chochote wanachopenda; hilo halifai kwa adabu ya mtakatifu. Watu hawapaswi kucharuka, wakitamba na kutapeli kila mahali, huku wakipeperusha bendera ya Mungu; hii ndiyo aina ya mwenendo wa uasi kabisa. Familia zina sheria zake, na mataifa yana sheria zake—na, je, si hivyo zaidi katika nyumba ya Mungu? Je, haina viwango vikali hata zaidi? Je, haina amri za utawala hata zaidi? Watu wako huru kufanya wanachotaka, lakini amri za utawala za Mungu haziwezi kubadilishwa wapendavyo. Mungu ni Mungu asiyestahimili kukosewa na wanadamu; Yeye ni Mungu anayewapiga watu. Je, kweli watu hawajui hili tayari?
Kila kanisa lina watu wanaosababisha usumbufu kwa kanisa au wanaovuruga kazi ya Mungu. Wao wote ni Mashetani ambao wamepenya katika nyumba ya Mungu kwa kujificha. Watu kama hao ni hodari sana katika kuigiza: Wanakuja mbele Yangu kwa heshima kubwa, wakiinama na kujipendekeza, mfano halisi wa mbwa wenye upele, na kujitolea “yote” waliyo nayo ili kufikia malengo yao wenyewe—lakini mbele ya akina ndugu, wanaonyesha upande wao mbaya. Wanapowaona watu wanaotenda ukweli, wanawashambulia na kuwasukuma kando; wanapowaona watu wa kutisha zaidi kuliko wao wenyewe, wanawasifu na kujipendekeza kwao. Wanafanya fujo kanisani. Inaweza kusemwa kwamba “waonevu wa hapo” kama hao, “vibaraka” kama hao, wapo katika mengi ya makanisa. Wanatenda kwa siri pamoja, wakikonyezana na kupeana ishara za siri, na hakuna hata mmoja wao anayetenda ukweli. Yeyote aliye na sumu nyingi kabisa ndiye “ibilisi mkuu,” na yeyote aliye na hadhi ya juu kabisa huwaongoza, akipeperusha bendera yao juu. Watu hawa wanafanya ghasia kanisani, wakieneza uhasi, wakiachilia kifo, wakifanya wapendavyo, wakisema wapendavyo, na hakuna anayethubutu kuwazuia. Wamejaa tabia za kishetani. Pindi tu wanaposababisha usumbufu, hewa ya kifo inaingia kanisani. Wale walio ndani ya kanisa wanaotenda ukweli wanakataliwa, wakishindwa kufanya kila wanachoweza, huku wale wanaosumbua kanisa na kueneza kifo wanafanya fujo ndani—na, zaidi ya hayo, watu wengi kabisa huwafuata. Makanisa kama hayo hakika yanatawaliwa na Shetani, huku ibilisi akiwa mfalme wao. Watu katika makanisa kama hayo wasiposimama na kuwakataa mapepo wakuu, basi wao pia, ipo siku, wataangamia. Kuanzia sasa na kuendelea, hatua lazima zichukuliwe dhidi ya makanisa kama hayo. Ikiwa wale wenye uwezo wa kutenda ukweli kidogo hawatafuti, basi kanisa hilo litafutiliwa mbali. Ikiwa kanisa halina mtu yeyote aliye tayari kutenda ukweli na hakuna mtu anayeweza kusimama imara katika ushuhuda wake kwa Mungu, basi kanisa hilo linapaswa kutengwa kabisa, na mahusiano yake na makanisa mengine lazima yakatwe. Hili linaitwa “kuzika kifo”; hii ndiyo maana ya kumkataa Shetani. Kanisa likiwa na waonevu kadhaa wa hapo, na wanafuatwa na “nzi wadogo” ambao hawana utambuzi kabisa, na ikiwa watu katika kanisa kama hilo, hata baada ya kuona ukweli, bado hawawezi kukataa vifungo na utawala wa hila wa waonevu hawa, basi watu hao wote waliokanganyika wataondoshwa mwishoni. Nzi hawa wadogo wanaweza kuwa hawajafanya uovu wowote mkuu, lakini wao ni wadanganyifu hata zaidi, wajanja hata zaidi, na kila mtu kama huyu ataondoshwa. Hakuna hata mmoja atakayesalia! Wale walio wa Shetani watarudishwa kwa Shetani, huku wale waliochaguliwa na Mungu hakika watatafuta ukweli; hili linaamuliwa na asili zao. Acha wale wote wanaomfuata Shetani waangamie! Hakuna huruma itakayoonyeshwa kwa watu kama hao. Acha wale wanaotafuta ukweli waruzukiwe, na wapate kufurahia neno la Mungu kadiri ya matamanio ya mioyo yao. Mungu ni mwenye haki; Yeye haonyeshi upendeleo kwa mtu yeyote. Ikiwa wewe ni ibilisi, basi huwezi kutenda ukweli; ikiwa wewe ni mtu anayetafuta ukweli, basi ni hakika kwamba hutatekwa nyara na Shetani. Hili halina shaka yoyote.
Wale wasiotafuta maendeleo daima wanataka wengine wawe hasi na watepetevu kama wao wenyewe. Wale wasiotenda ukweli wanawaonea wivu wale wanaotenda, na daima wanajaribu kuwapotosha wale waliokanganyika na wasio na utambuzi. Vitu ambavyo watu hawa wanatoa vinaweza kukufanya upotoke, uteleze kwenda chini, uanguke katika hali isiyo ya kawaida, na ujawe na giza. Vinaweza kukufanya uwe mbali na Mungu, uthamini mwili na ujiendekeze. Watu ambao hawapendi ukweli na ambao daima wanafanya mambo kwa kijuujuu tu kuelekea kwa Mungu hawana hali ya kujitambua, na tabia ya watu kama hao huwashawishi wengine watende dhambi na wampinge Mungu. Hawatendi ukweli, wala hawawaruhusu wengine kuutenda. Wanathamini dhambi na hawajichukii. Hawajijui, na wanawazuia wengine kujijua; pia wanawazuia wengine kuwa na kiu ya ukweli. Wale wanaopotoshwa nao hawawezi kuona mwanga—wanaanguka gizani, hawajijui, hawaelewi ukweli waziwazi, na wanazidi kuwa mbali na Mungu. Hawatendi ukweli na wanawazuia wengine kutenda ukweli, wakiwaleta watu hao wote waliokanganyika mbele yao. Badala ya kusema kwamba wanamwamini Mungu, ingekuwa bora kusema kwamba wanawaamini mababu zao, au kwamba kile wanachoamini ni sanamu zilizo mioyoni mwao. Ingekuwa bora zaidi kwa watu hao wanaodai kumfuata Mungu kufungua macho yao na kutazama vizuri ili waone ni nani hasa wanayemwamini: Je, kweli ni Mungu unayemwamini, au Shetani? Ikiwa unajua kwamba kile unachoamini si Mungu, bali sanamu zako mwenyewe, basi ingekuwa bora zaidi kama hungedai kuwa muumini. Ikiwa kweli hujui unamwamini nani, basi, tena, ingekuwa bora zaidi kama hungedai kuwa muumini. Kusema hivyo kungekuwa kukufuru! Hakuna anayekulazimisha kumwamini Mungu. Msiseme mnaniamini Mimi; Nimesikia maneno kama hayo ya kutosha, na sitaki kuyasikia tena, kwa sababu kile mnachoamini ni sanamu zilizo mioyoni mwenu na waonevu wa hapo walio miongoni mwenu. Wale ambao wanatikisa vichwa vyao wanaposikia ukweli, ambao nyuso zao hujaa tabasamu pana wanaposikia maneno ya kifo, wote ni uzao wa Shetani, na wao ndio watakaoondoshwa. Wengi kanisani hawana utambuzi. Mtu anapojaribu kuwapotosha wengine, wao kinyume chake wanasimama upande wa Shetani; hata wanahisi kukosewa sana wanapoitwa watumishi wa Shetani. Ingawa watu wanaweza kusema hawana utambuzi, daima wao husimama upande usio wa ukweli, hawasimami kamwe upande wa ukweli katika wakati muhimu sana, hawasimami kamwe ili kutetea ukweli. Je, kweli hawana utambuzi? Kwa nini kinyume chake wanachukua upande wa Shetani? Kwa nini hawasemi kamwe neno moja ambalo ni la haki na la busara kwa ajili ya ukweli? Je, hali hii kweli imetokea kutokana na kuchanganyikiwa kwao kwa muda? Kadiri watu wanavyokuwa na utambuzi kiasi kidogo, ndivyo wanavyoshindwa kusimama upande wa ukweli. Hili linaonyesha nini? Je, halionyeshi kwamba watu wasio na utambuzi wanapenda dhambi? Je, halionyeshi kwamba wao ni uzao mtiifu wa Shetani? Kwa nini daima wanaweza kusimama upande wa Shetani na kuzungumza lugha yake? Kila neno na tendo lao, sura za nyuso zao, yote yanatosha kuthibitisha kwamba wao si wapenzi wa ukweli wa aina yoyote; badala yake, wao ni watu wanaochukia ukweli. Ukweli kwamba wanaweza kusimama upande wa Shetani unatosha kuthibitisha kwamba Shetani anawapenda sana ibilisi hawa wadogo wanaotumia maisha yao kupigana kwa ajili ya Shetani. Je, ukweli huu wote hauko wazi kabisa? Ikiwa kweli wewe ni mtu anayependa ukweli, basi kwa nini huna heshima kwa wale wanaotenda ukweli, na kwa nini unawafuata mara moja wale wasiotenda ukweli wanapokutupia jicho kidogo tu? Hili ni tatizo la aina gani? Sijali kama una utambuzi au la. Sijali umelipa gharama kubwa kiasi gani. Sijali nguvu zako ni kubwa kiasi gani, na Sijali kama wewe ni mwonevu wa hapo au kiongozi anayepeperusha bendera. Ikiwa nguvu zako ni kubwa, basi hilo ni kwa msaada wa nguvu za Shetani tu. Ikiwa hadhi yako iko juu, basi hiyo ni kwa sababu tu kuna watu wengi mno karibu nawe ambao hawatendi ukweli. Ikiwa hujatimuliwa, basi hiyo ni kwa sababu sasa si wakati wa kazi ya kutimua; badala yake, ni wakati wa kazi ya kuondosha. Hakuna haraka ya kukutimua sasa. Ninasubiri tu siku ambayo Nitakuadhibu baada ya wewe kuondoshwa. Yeyote asiyetenda ukweli ataondoshwa!
Watu wanaomwamini Mungu kwa kweli ni wale walio tayari kutia neno la Mungu katika vitendo na walio tayari kutenda ukweli. Watu ambao kwa kweli wanaweza kusimama imara katika ushuhuda wao kwa Mungu pia ni wale walio tayari kutia neno Lake katika vitendo na wanaoweza kwa kweli kusimama upande wa ukweli. Watu wanaojihusisha na matendo mapotovu na yasiyo ya haki wote hawana ukweli, na wote humletea Mungu aibu. Wale wanaosababisha mabishano kanisani ni watumishi wa Shetani, wao ni mfano halisi wa Shetani. Watu kama hao ni wenye nia mbaya sana. Wale wasio na utambuzi lakini ambao hawana uwezo wa kusimama upande wa ukweli wote ni watu wanaohifadhi nia mbovu na kuchafua ukweli. Wao ni wawakilishi halisi zaidi wa Shetani. Ni wasioweza kukombolewa, na bila shaka wataondoshwa. Nyumba ya Mungu hairuhusu wale wasiotenda ukweli kusalia, wala hairuhusu kusalia kwa wale wanaobomoa kanisa kwa makusudi. Hata hivyo, sasa si wakati wa kufanya kazi ya kufukuza; watu kama hao watafunuliwa tu na kuondoshwa mwishoni. Hakuna kazi nyingine ya bure itakayofanywa juu ya watu hawa; wale ambao ni Mashetani hawawezi kusimama upande wa ukweli, ilhali wale wanaotafuta ukweli wanaweza. Watu wasiotenda ukweli hawastahili kusikia Neno la ukweli na hawastahili kuwa mashahidi wa ukweli. Kimsingi ukweli si kwa ajili ya masikio yao; badala yake, unaelekezwa kwa wale wanaoutenda. Kabla matokeo ya kila mtu hayajafunuliwa, wale wanaosumbua kanisa na wanaovuruga kazi kwanza watawekwa kando na kuachwa bila kushughulikiwa kwa sasa. Pindi tu kazi itakapokamilika, watu hawa kila mmoja atafunuliwa, na kisha wataondoshwa. Kwa sasa, wakati ukweli unatolewa, watapuuzwa. Ukweli wote utakapofunuliwa kwa binadamu, watu wataanza kuondoshwa; huo ndio utakuwa wakati ambapo watu wote wataainishwa kulingana na aina zao. Ujanja mdogo wa wale wasio na utambuzi utasababisha maangamizi yao mikononi mwa waovu, watashawishiwa nao na kupelekwa mbali, na hawatarudi kamwe. Na kushughulikiwa huku ndiko wanakostahili, kwa sababu hawaupendi ukweli, kwa sababu hawana uwezo wa kusimama upande wa ukweli, na kwa sababu wanawafuata watu waovu, wanasimama upande wa watu waovu, na wanashirikiana na watu waovu kumpinga Mungu. Wanajua fika kwamba kile ambacho watu hao waovu wanafunua ni uovu, lakini wanashupaza shingo na wanaupa kisogo ukweli ili kuwafuata. Je, watu hawa wasiotenda ukweli lakini wanaofanya mambo ya uharibifu na ya chukizo wote hawafanyi maovu? Ingawa kuna wale miongoni mwao wanaotenda kama “wafalme” na wengine wanaowafuata, je, asili yao ya kumpinga Mungu si sawa? Wanaweza kuwa na kisingizio gani kudai kwamba Mungu hawaokoi? Wanaweza kuwa na kisingizio gani kudai kwamba Mungu si mwenye haki? Je, si uovu wao wenyewe ndio unaowaangamiza? Je, si uasi wao wenyewe ndio unaowavuta chini hadi jahanamu? Watu wanaotenda ukweli, mwishowe, wataokolewa na kufanywa kuwa timilifu kwa sababu ya ukweli. Wale wasiotenda ukweli, mwishowe, watajiletea maangamizi kwa sababu ya ukweli. Haya ndiyo matokeo yanayowasubiri wale wanaotenda ukweli na wale wasioutenda. Ninawashauri wale ambao hawapangi kutenda ukweli waondoke kanisani haraka iwezekanavyo ili waepuke kutenda dhambi nyingi hata zaidi. Wakati utakapofika, itakuwa imechelewa sana kujuta. Hasa, wale wanaounda magenge na wanaosababisha migawanyiko, na wale waonevu wa hapo ndani ya kanisa, lazima waondoke mapema hata zaidi. Watu kama hao, walio na asili ya mbwa mwitu waovu, hawana uwezo wa kubadilika. Ingekuwa bora kama wangeondoka kanisani katika fursa ya kwanza kabisa, wasisumbue tena kamwe maisha ya kawaida ya akina ndugu, wasije wakaadhibiwa na Mungu. Wale miongoni mwenu ambao mmewafuata mtafanya vema kutumia fursa hii kujitafakari. Je, mtaondoka kanisani pamoja na waovu, au mtasalia na kufuata kwa utiifu? Mnapaswa kufikiria jambo hili kwa makini. Ninawapa ninyi fursa hii moja zaidi ya kuchagua, na Ninasubiri jibu lenu.