Majani Yaangukayo Yatakaporudi kwa Mizizi Yake, Utajuta Maovu Yote Ambayo Umefanya

Nyote mmeshuhudia wenyewe kazi ambayo Nimefanya miongoni mwenu, ninyi wenyewe mmesikia maneno ambayo Nimenena, nanyi mnajua mtazamo Wangu kuelekea kwenu, kwa hiyo mnapaswa kujua kwa nini Ninafanya kazi hii miongoni mwenu. Nitawaambia ukweli—ninyi ni vifaa tu vya kazi Yangu ya ushindi katika siku za mwisho; ninyi ni vyombo vya kupanua kazi Yangu miongoni mwa nchi za Mataifa. Mimi huzungumza kupitia kwa udhalimu wenu, uchafu wenu, upinzani na uasi wenu ili kupanua bora zaidi kazi Yangu ili jina Langu lienee miongoni mwa nchi za Mataifa, yaani, kuenea miongoni mwa nchi yoyote nje ya Israeli. Ni kusudi kwamba jina Langu, vitendo Vyangu, na sauti Yangu viweze kusambaza kotekote katika nchi za Mataifa, hivyo nchi hizo zote ambazo si za Israeli ziweze kushindwa na Mimi na ziweze kuniabudu Mimi, kuwa nchi Zangu takatifu nje ya nchi za Israeli na Misri. Kuipanua kazi Yangu ni kuipanua kwa kweli kazi Yangu ya ushindi, kuipanua nchi Yangu takatifu. Ni kupanua mahali Pangu pa usalama duniani. Mnapaswa kuelewa kwamba ninyi ni viumbe tu miongoni mwa nchi za Mataifa ambazo Mimi huzishinda. Ninyi kwa asili hamkuwa na hali wala thamani yoyote ya kutumia, hakuna matumizi kabisa. Ni kwa sababu tu Niliinua mabuu kutoka kwa rundo la samadi kuwa sampuli za Mimi kuushinda ulimwengu, kuwa “vifaa vya marejeo” pekee vya Mimi kuushinda nchi nzima, ndio mmekuwa na bahati ya kutosha kuwasiliana na Mimi, na kukusanyika na Mimi sasa. Ni kwa sababu ya hadhi yenu ya chini ndiyo Nimewachagua ninyi kuwa sampuli, mifano wa kazi Yangu ya ushindi. Ni kwa sababu hii tu ndiyo Nafanya kazi na kunena miongoni mwenu, na kwamba Naishi na kukaa kwa muda na ninyi. Mnapaswa kujua kwamba ni kwa sababu tu ya usimamizi Wangu na karaha Yangu mno ya ninyi mabuu ndani ya lundo la samadi ndio Nanena miongoni mwenu, na hata ni kwa kiwango cha Mimi kuwa mwenye hasira. Kufanya kazi Kwangu miongoni mwenu sio kabisa sawa na Yehova kufanya kazi katika Israeli, na hasa si sawa na Yesu kufanya kazi Uyahudi. Ni kwa uvumilivu mkuu ndio Nanena na kufanya kazi, na ni kwa hasira na vilevile hukumu ndio Nawashinda wapotovu hawa. Si chochote kama Yehova kuwaongoza watu Wake katika Israeli. Kazi Yake katika Israeli ilikuwa kutoa chakula na maji ya uzima, na Alijawa huruma na upendo kwa watu Wake katika utoaji Wake wa vitu kwao. Kazi ya leo hufanywa katika taifa ambalo halijachaguliwa, ambalo limelaaniwa. Hakuna chakula tele, wala hakuna ustawishaji wa maji ya uzima ya kukata kiu sembuse utoaji wa bidhaa za mwili za kutosha; kunao tu utoaji wa hukumu, laana, na kuadibu vya kutosha. Hawa mabuu katika lundo la samadi hawastahili kwa uthabiti kupata vilima vya ng’ombe na kondoo, utajiri mwingi, na watoto wazuri zaidi kotekote katika nchi ambavyo Nilitoa kwa Israeli. Israeli ya siku hizi hutoa juu ya madhabahu ng’ombe na kondoo na vitu vya dhahabu na fedha ambavyo Mimi huwastawisha navyo, kushinda sehemu moja ya kumi inayotakiwa na Yehova chini ya sheria, na kwa hiyo Nimewapa hata zaidi, zaidi ya mara mia moja ya kile ambacho Israeli ilikuwa ipate chini ya sheria. Kile ambacho Nastawisha Israeli nacho kinashinda kile ambacho Abrahamu na Isaka walipata. Nitaifanya familia ya Israeli kuzaa na kuongezeka, na Nitawafanya watu Wangu wa Israeli kuenea kutoka upande mmoja hadi upande mwingine wa ulimwengu mzima. Wale ambao Mimi hubariki na kutunza bado ni wateule wa Israeli, yaani, watu ambao hutoa kila kitu Kwangu, ambao wamepata kila kitu kutoka Kwangu. Ni kwa sababu wao huniweka Mimi mawazoni ndiyo wao hutoa sadaka ya ndama na wanakondoo waliozaliwa karibuni juu ya madhabahu Yangu takatifu na hutoa mbele Yangu kila kitu walicho nacho, hata kwa kiwango cha kutoa wana wao wa kwanza waliozaliwa karibuni kwa matarajio ya kurudi Kwangu. Na ninyi je? Ninyi huamsha hasira Yangu, ninyi huwa na matakwa mengi kutoka Kwangu, ninyi huiba sadaka za wale wanaotoa vitu Kwangu na hamjui kwamba mnanikosea Mimi, hivyo mnachopata ni kutoa machozi na adhabu katika giza. Ninyi mmechochea hasira Yangu mara nyingi na Nimenyesha moto Wangu wa kuchoma, kiasi kwamba kumekuwa na wengi waliopatwa na mwisho wa majonzi, ambao makazi yao ya furaha yalikuwa makaburi ya kuhuzunisha. Yote Niliyo nayo kwa mabuu hawa ni hasira isiyoisha, na sina kusudi la baraka. Ni kwa ajili ya kazi Yangu tu ndiyo Nimefanya kinzano na kuwatia ninyi moyo, na kwamba Nimevumilia fedheha kuu kufanya kazi miongoni mwenu. Isingekuwa mapenzi ya Baba Yangu, Ningewezaje kuishi katika nyumba moja na mabuu wanaobingirika kutoka upande mmoja hadi mwingine ndani ya rundo la samadi? Nahisi chuki mno kwa vitendo na maneno yenu yote, na vyovyote vile, kwa sababu Nina “shauku” kiasi katika uchafu na uasi wenu, huu umekuwa mkusanyiko mkubwa wa maneno Yangu. La sivyo Mimi bila shaka singebaki miongoni mwenu kwa muda mrefu hivi. Kwa hiyo, mnapaswa kujua kwamba mtazamo Wangu kuelekea kwenu ni wa upole na huruma tu, mmoja ambao kwao hakuna upendo, ila stahamala tu kwenu, kwa sababu Mimi hufanya hili kwa ajili ya kazi Yangu tu. Na mmeyaona matendo Yangu tu kwa sababu Nimechagua uchafu na uasi kama “mali ghafi.” La sivyo Mimi bila shaka singeyafichua matendo Yangu kwa mabuu hawa; Nafanya tu kazi ndani yenu na usitaji; si chochote kama wepesi na hiari ya kazi Yangu katika Israeli. Nazungumza miongoni mwenu kwa kusita, Nikiibeba hasira Yangu. Isingekuwa kazi Yangu kuu zaidi, Ningewezaje kuvumilia mtazamo wenye kuendelea wa mabuu hawa? Isingekuwa kwa ajili ya jina Langu Ningekuwa Nimepanda vilele vya juu zaidi kitambo na kuwateketeza kabisa hawa mabuu na lundo la samadi! Isingekuwa kwa ajili ya utukufu Wangu, Ningewezaje kuwakubalia pepo hawa waovu kunipinga Mimi waziwazi na vichwa vyao vikitikiswa mbele ya macho Yangu? Isingekuwa kusababisha kazi Yangu kutekelezwa kwa urahisi bila kizuizi hata kidogo, Ningewezaje kuwakubalia hawa watu wanaofanana mabuu kunitusi Mimi kwa utukutu? Kama watu mia moja kijijini mwa Israeli wangeinuka kunipinga Mimi hivi, hata kama wangetoa sadaka Kwangu bado Ningewafutilia mbali chini ya nyufa zilizo ardhini ili watu katika miji mingine hawangeasi tena. Mimi ni moto uteketezao na Sivumilii kosa. Kwa sababu wanadamu wote waliumbwa na Mimi, chochote Nisemacho na kufanya, watu lazima watii na hawawezi kukiasi. Watu hawana haki ya kuingilia kazi Yangu, na wao hasa siyo wenye sifa zinazostahili kuchambua kilicho cha kweli au chenye makosa katika kazi Yangu na maneno Yangu. Mimi ni Bwana wa uumbaji, na viumbe wanapaswa kutimiza kila kitu Ninachohitaji kwa moyo wa kunicha Mimi; hawapaswi kutoa sababu ili kunishawishi Mimi na wao hasa hawapaswi kunipinga. Ninatumia mamlaka Yangu kuwatawala watu Wangu, na wale wote ambao ni sehemu ya uumbaji Wangu wanapaswa kuyatii mamlaka Yangu. Ingawa leo ninyi ni, jasiri na wenye kiburi mbele Yangu, ninyi hukaidi maneno ambayo Nawafunzia, na hamwogopi, Mimi hukumbana tu na uasi wenu na uvumilivu. Singekasirika na kuathiri kazi Yangu kwa sababu mabuu wadogo sana walipindua uchafu katika rundo la samadi. Mimi huvumilia kuendelea kuwepo kwa kila kitu ambacho Mimi huchukia kabisa na mambo ambayo Mimi huchukia kabisa kwa ajili ya mapenzi ya Baba Yangu, mpaka matamshi Yangu yawe kamili, mpaka dakika Yangu ya mwisho kabisa. Usijali! Siwezi kuzama katika kiwango sawa na buu asiyefaa kutajwa, na Sitafananisha kiwango cha ujuzi na wewe. Nakuchukia kabisa, ilhali Naweza kuvumilia. Wewe hunikaidi Mimi, ilhali huwezi kuepuka siku ya Mimi kukuadibu ambayo Baba Yangu ameniahidi Mimi. Je, buu aliyeumbwa anaweza kufananishwa na Bwana wa uumbaji wote? Katika majira ya kupukutika kwa majani, majani yaangukayo hurudi kwa mizizi yake, wewe hurudi kwa nyumba ya “baba” yako, na Mimi hurudi ubavuni pa Baba Yangu. Mimi huandamana na upendo mwema wa Baba Yangu, na wewe hufuatwa na kuvyogwa kwa baba Yako. Nina utukufu wa Baba Yangu, na wewe una aibu ya baba yako. Mimi hutumia kuadibu ambako Nimeshikilia kwa muda mrefu kuandamana na wewe, na wewe hukutana na kuadibu Kwangu na mwili wako uliooza ambao tayari umekuwa mpotovu kwa makumi ya maelfu ya miaka. Nimehitimisha kazi Yangu ya maneno ndani yako, ikiandamana na uvumilivu, na umeanza kutimiza wajibu wa kupitia msiba kutoka kwa maneno Yangu. Mimi hufurahia sana na kufanya kazi katika Israeli; wewe hulia na kusaga meno yako na huishi na kufa matopeni. Nimepata tena umbo Langu la asili na Sibaki tena ndani ya uchafu na wewe, huku umepata tena ubaya wako wa asili na bado unafukua kila mahali katika lundo la samadi. Wakati ambapo kazi na maneno Yangu yatakamilika, itakuwa siku ya furaha Kwangu. Wakati ambapo upinzani na uasi wako utakwisha, itakuwa siku ya kulia kwako machozi. Sitakuonea huruma, na hutaniona Mimi tena. Sitakuwa tena na mazungumzo na wewe, na hutakutana na Mimi tena. Nitachukia uasi wako, na utakosa kupendeza Kwangu. Nitakupiga wewe, na utanikosa Mimi. Nitaondoka kwako kwa furaha, na utafahamu deni lako Kwangu. Sitakuona wewe tena, lakini wewe kila mara utanitarajia Mimi. Nitakuchukia kwa sababu unanipinga Mimi sasa, na utanikosa Mimi; kwa sababu Nakuadibu sasa. Siko radhi kuishi ubavuni pako, lakini utalitamani sana kwa uchungu na kulia machozi katika milele, kwa sababu utajuta kila kitu ambacho umenifanyia Mimi. Utajuta uasi wako na upinzani wako, na hata utaulaza uso wako juu ya ardhi kutokana na kujuta, na utaanguka chini mbele Yangu na kuapa kutonikaidi Mimi tena. Lakini ndani ya moyo wako wewe hunipenda Mimi tu na hutaweza kamwe kuisikia sauti Yangu, lazima Nikufanye ujionee haya.

Naona sasa mwili wako usiozuiwa ambao umenibembeleza Mimi, na Nina onyo kidogo tu kwako. Mimi bila shaka sichukui hatua kupitia kuadibu “kukutumikia” wewe. Unapaswa kujua ni wajibu gani ambao wewe huchukua katika kazi Yangu, na kisha Nitaridhika. Kuongezea kwa hili, ukinipinga Mimi au kutumia pesa Zangu, au kula sadaka za Mimi, Yehova, au ninyi mabuu mnaumana, au kuna ugomvi au kuingiliana kati ya ninyi viumbe mfano wa mbwa—Sihusiki na yoyote kati ya hayo. Mnahitaji tu kujua ninyi ni vitu vya aina gani, na Nitaridhika. Mbali na vitu hivi, ni sawa kama mko radhi kuvutiana panga au mikuki au kupigana kwa maneno yenu. Sina tamaa ya kuingilia mambo hayo, na Mimi sihusiki hata kidogo katika mambo ya binadamu. Sio kwamba Sijali kuhusu ugomvi kati yenu, lakini ni kwa sababu Mimi si mmoja wenu, hivyo, Sishiriki katika mambo yaliyo kati yenu. Mimi Mwenyewe si mmoja wa uumbaji na si wa dunia hii, kwa hiyo, Nachukia kabisa maisha ya kuharakisha miongoni mwa watu na hayo mahusiano yasiyofaa, yasiyofaa kati ya watu. Mimi hasa Nachukia kabisa hayo makundi ya makelele ya watu. Hata hivyo, Najua kwa kina uchafu ndani ya mioyo ya kila kiumbe, na kabla ya Mimi kuwaumba ninyi, Nilijua tayari udhalimu uliokuwepo ndani ya kina cha mioyo ya binadamu, na Niliujua udanganyifu na uhalifu wote katika mioyo ya binadamu. Kwa hiyo, hata ingawa hakuna kabisa dalili zozote wakati ambapo watu hufanya mambo ya udhalimu, bado Najua kwamba udhalimu uliowekwa ndani ya mioyo yenu hushinda utajiri wa vitu vyote Nilivyoumba. Kila mmoja wenu amepanda vilele vya juu zaidi vya umati; ninyi mmepanda kuwa mababu wa umati. Ninyi ni wadhalimu mno, na mnacharuka miongoni mwa mabuu wote, mkitafuta mahali pa amani na mkijaribu kuwameza mabuu walio wadogo kuwaliko ninyi. Ninyi ni wenye kijicho na wa husuda katika mioyo yenu, kuwashinda wale pepo ambao wamezama chini ya bahari. Mnaishi chini ya samadi, mkiwasumbua mabuu kutoka juu hadi chini ili wasiwe na amani, mkipigana wenyewe kwa wenyewe kwa muda mfupi na kisha kutulia. Ninyi hamjui hali yenu wenyewe, ilhali bado ninyi hupigana wenyewe kwa wenyewe ndani ya samadi. Ni nini ambacho mnaweza kupata kutokana na mapambano hayo? Kama ninyi kweli mngekuwa na moyo wa kunicha Mimi, mngewezaje kupigana wenyewe kwa wenyewe bila Mimi kujua? Haijalishi vile hali yako ilivyo juu, je, bado wewe si mnyoo mdogo mwenye uvundo ndani ya samadi? Utaweza kuota mbawa na kuwa njiwa angani? Ninyi, minyoo wadogo wenye uvundo mnaiba sadaka kutoka kwa madhabahu ya Mimi, Yehova; kwa kufanya hivyo, mnaweza kuokoa majina yenu yaliyoharibika, yenye kasoro kuwa wateule wa Israeli? Ninyi ni mafukara wasio na haya! Hizo sadaka juu ya madhabahu zilizotolewa Kwangu na watu, kuonyesha hisia karimu kutoka kwa wale ambao hunicha Mimi. Ni za udhibiti Wangu na za matumizi Yangu, kwa hiyo inawezekanaje wewe kuniibia Mimi hua wadogo waliotolewa na watu? Je, huogopi kuwa Yuda? Je, huogopi nchi yako kuwa “konde la damu”? Wewe kitu kisicho na haya! Unadhani kwamba hua waliotolewa na watu wote ni wa kustawisha tumbo la wewe buu? Kile ambacho Nimekupa ni kile ambacho Nimefurahia na kuwa radhi kukupa wewe; kile ambacho Sijakupa kiko chini ya Mamlaka Yangu, na huwezi tu kuiba sadaka Yangu. Yule Anayefanya kazi ni Mimi, Yehova—Bwana wa uumbaji, na sababu ya watu kutoa sadaka ni Mimi. Unadhani kwamba ni fidia ya kukimbia kila mahali ambako wewe hufanya? Wewe kwa kweli ni usiye haya! Ni nani ambaye unamkimbilia kila mahali? Je, si kwa ajili yako mwenyewe? Kwa nini wewe huiba sadaka Zangu? Kwa nini wewe huiba pesa kutoka kwa mfuko Wangu wa pesa? Je, wewe si mwana wa Yuda Iskariote? Sadaka Zangu, za Yehova, ni za kufurahiwa na makuhani. Je, wewe ni kuhani? Wewe huthubutu kula kwa kujisikia sadaka Zangu na hata unazitandaza juu ya meza; huna thamani yoyote! Wewe fukara asiye na thamani! Moto Wangu, wa Yehova, utakuteketeza wewe!

Iliyotangulia: Unajua Nini Kuhusu Imani?

Inayofuata: Hakuna Aliye wa Mwili Anayeweza Kuepuka Siku ya Ghadhabu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp