150 Mwenyezi Mungu, Moyo Wangu ni Wako

1

Maneno ya nani ni matamu zaidi na huilisha roho yangu?

Upendo wa nani ni mzuri zaidi na huushika moyo wangu?

Kazi ya nani ni ya ajabu zaidi, inayoutakasa upotovu wa binadamu?

Nani anayenipa wokovu mkuu, na kunileta mbele ya kiti cha enzi?

Nani anayeonyesha ukweli kumwokoa mwanadamu?

Nani huniruhusu nione mwanga tena?

Nani ndiye mtu anayependeka?

Ni nani nitakayemfikiria kila wakati?

Mwenyezi Mungu, mpendwa wangu, Wewe uko moyoni mwangu.

Mwenyezi Mungu, mpendwa wangu, moyo wangu ni Wako.

2

Umemsimamia binadamu kwa miaka elfu sita, bila kusitisha kazi Yako kamwe.

Leo Umepata mwili tena, ili kuwapata watu.

Unatanafusi sana kati ya mawingu, upotovu wa binadamu ni wa kina.

Unakaa mbinguni ukiangalia harakati za watu.

Unatembea miongoni mwa watu na kuingiliana nao,

Ukikabiliwa na matatizo ya dunia.

Unanena na kufanya kazi, kutoa damu ya moyo Wako

ili kuwakamilisha wale wanaokupenda.

Mwenyezi Mungu, mpendwa wangu, Wewe uko moyoni mwangu.

Mwenyezi Mungu, mpendwa wangu, moyo wangu ni Wako.

3

Watu wanapaswa kupata nini hatimaye kwa kumwamini Mungu?

Ujuzi wa Mungu na ukweli.

Ni taabu gani ya maana sana?

Iletayo mabadiliko katika tabia ya mwanadamu.

Ni njia gani katika maisha iletayo mafanikio? Njia ya Petro ya upendo kwa Mungu.

Upendo wa aina gani kwa Mungu ndio wa kweli sana? Kumtunza kwa moyo na akili yote ya mtu.

Mungu anatumaini kwamba mwanadamu anaweza kubadilishwa katika tabia ya maisha na kupatwa naye.

Nitafanya kila Niwezalo kumridhisha, na kuutuliza moyo Wake.

Mwenyezi Mungu, mpendwa wangu, Wewe uko moyoni mwangu.

Mwenyezi Mungu, mpendwa wangu, moyo wangu ni Wako.

Iliyotangulia: 149 Nitaukaribisha Uso Wako Unaotabasamu Utakapoonekana Mbele Yangu

Inayofuata: 151 Kukusanyika katika Sayuni

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp