259 Mimi ni Kiumbe Mdogo Sana tu Aliyeumbwa

1

Ee Mungu! Kama nina hadhi au la,

sasa ninajielewa mwenyewe.

Hadhi yangu ikiwa juu ni kwa sababu ya kuinuliwa na Wewe,

na ikiwa iko chini ni kwa sababu ya mpango Wako.

Ee Mungu! Sina chaguzi au malalamishi yoyote.

Kila kitu ki mikononi Mwako.

Ulipanga kwamba ningezaliwa

katika nchi hii na miongoni mwa watu hawa,

na ninapaswa tu kuwa mtiifu kabisa chini ya utawala Wako.

Mimi si chochote zaidi ya kiumbe mdogo

sana aliyeumbwa na Bwana wa uumbaji,

Ni Wewe uliyeniumba, na sasa kwa mara nyingine tena Umeniweka

katika mikono Yako ili niwe chini ya rehema Yako.

Niko tayari kuwa chombo Chako na foili Yako

kwa sababu vyote ni vile Umepanga.

Hakuna anayeweza kubadili jambo hilo.

Vitu vyote na matukio yote yako katika mikono Yako.

2

Ee Mungu! Silengi hadhi; hata hivyo,

mimi ni mmoja tu miongoni mwa uumbaji.

Ungeniweka kuzimu,

katika ziwa la moto wa jahanamu, mimi si chochote isipokuwa kiumbe.

Mimi si chochote zaidi ya kiumbe mdogo

sana aliyeumbwa na Bwana wa uumbaji,

Ni Wewe uliyeniumba, na sasa kwa mara nyingine tena Umeniweka

katika mikono Yako ili niwe chini ya rehema Yako.

Niko tayari kuwa chombo Chako na foili Yako

kwa sababu vyote ni vile Umepanga.

Hakuna anayeweza kubadili jambo hilo.

Vitu vyote na matukio yote yako katika mikono Yako.

3

Ukinitumia, mimi ni kiumbe.

Ukinikamilisha, mimi bado ni kiumbe.

Usiponikamilisha, bado nitakupenda

kwa sababu mimi si zaidi ya kiumbe.

Mimi si chochote zaidi ya kiumbe mdogo

sana aliyeumbwa na Bwana wa uumbaji,

Ni Wewe uliyeniumba, na sasa kwa mara nyingine tena Umeniweka

katika mikono Yako ili niwe chini ya rehema Yako.

Niko tayari kuwa chombo Chako na foili Yako

kwa sababu vyote ni vile Umepanga.

Hakuna anayeweza kubadili jambo hilo.

Vitu vyote na matukio yote yako katika mikono Yako.

Iliyotangulia: 258 Nimeamua Kumpenda Mungu

Inayofuata: 260 Natafuta tu Kumpenda Mungu Moyoni Mwangu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp