Sura ya 11

Je, Mimi ni Mungu wako? Je, Mimi ni Mfalme wako? Je, kweli umeniruhusu Mimi kutawala kama Mfalme ndani yako? Unapaswa kutafakari kujihusu kabisa. Je, hukuchunguza na kukataa mwanga mpya na hata kuthubutu kuacha bila kuufuata ulipokuwa ukija? Kwa sababu ya hili utapitia hukumu na kuanguka hadi kifo chako, utahukumiwa na kutandikwa kiboko na kiboko cha chuma na hutahisi kazi ya Roho Mtakatifu. Kwa haraka utalia na kupiga magoti katika ibada wakati huo ukiomboleza. Nimewaambia daima na daima Nimewaeleza na Nimewaambia kila kitu. Fikirieni nyuma kulihusu kwa makini, ni wakati upi Nimewahi kukosa kuwaambia kitu? Hata hivyo, kuna watu fulani ambao wanashikilia kufanya mambo kwa njia ambayo si sahihi. Wamepotea katika ukungu wa shaka ambao unazuia jua na kamwe hawauoni mwanga. Je, hii si kwa sababu dhamira yao ya “nafsi” ni yenye nguvu sana ama mawazo yao wenyewe ni makubwa sana? Tangu lini wewe ukanifikiria Mimi? Tangu lini ukawa na nafasi kwa ajili Yangu katika moyo wako? Wakati umefeli, wakati huna uwezo, na wakati umeishiwa na uchaguzi, hapo tu ndipo unaomba Kwangu. Basi, mbona usifanye mambo wewe mwenyewe sasa? Enyi watu! Ni nafsi zenu nzee ambazo zimewaharibu!

Watu wengine hawawezi kupata njia, na hawawezi kufuata mwanga mpya. Wanashiriki tu kuhusu kile ambacho wameona awali, hakuna kitu kipya kwao. Mbona hivyo? Mnaishi ndani yenu na mmeniacha Mimi nje ya mlango. Unapoona mbinu za kazi ya Roho Mtakatifu zikibadilika, moyoni mwako, daima wewe huwa mwangalifu kuhusu kuwa mwenye makosa. uchaji wako kwa Mungu uko wapi? Je, umelitafuta katika ukimya wa uwepo wa Mungu? Unatafakari tu: “Je, Roho Mtakatifu kweli anafanya kazi hivyo?” Watu wengine wameshuhudia kwamba ni kazi ya Roho Mtakatifu, lakini bado wana mambo kusema kuihusu. Watu wengine wanakiri kwamba ni neno la Mungu, lakini hawalikubali. Dhana tofauti zinafurika kuhusu kila mmoja wao, na hawaelewi kazi ya Roho Mtakatifu, wakiwa wazembe na wa ovyoovyo, bila hiari ya kulipa gharama na kuwa wenye bidii katika uwepo Wangu. Roho Mtakatifu amewapa nuru, lakini hawatakuja mbele Yangu kuwasiliana kwa karibu na kunitafuta. Badala yake, wanafuata tamaa zao wenyewe, wakifanya chochote wapendacho; ni nini nia yao?

Iliyotangulia: Sura ya 10

Inayofuata: Sura ya 12

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp