Ingawa wachungaji na wazee wa kanisa wanashikilia mamlaka katika ulimwengu wa kidini na wanaitembea njia ya Mafarisayo wanafiki, tunamwamini Bwana Yesu, sio wachungaji na wazee wa kanisa, kwa hiyo unawezaje kusema kwamba sisi pia tunaitembea njia ya Mafarisayo? Je, hatuwezi kuokolewa kwa kumwamini Mungu ndani ya dini?

09/06/2019

Jibu:

Kuna watu wengi katika dini ambao wanaamini na kuabudu bila kufikiria na kufuata Mafarisayo. Kwa hiyo kama njia wanayoenda ni njia ya Mafarisayo ni dhahiri mara tu unapofikiri juu yake. Unathubutu kusema kuwa unaabudu na kuwalinda Mafarisayo katika moyo wako lakini huna uhusiano na dhambi zao? Unathubutu kusema kuwa unawafuata Mafarisayo wanafiki, lakini wewe si kama wao, mtu anayepinga Mungu? Je, bado hatuwezi kung’amua swali rahisi kama hilo? Aina ya mtu unayefuata ni aina ya njia unayotembea. Ikiwa unawafuata Mafarisayo basi uko kwenye njia ya Mafarisayo. Ukitembea njia ya Mafarisayo basi wewe kiasili ni aina hiyo ya mtu kama Mafarisayo. Yule ambaye mtu anamfuata na njia ambayo anachagua vyote vinawhusiana na asili yake moja kwa moja. Yeyote anayefuata Mafarisayo ana asili na kiini sawa na Mafarisayo. Huu ni ukweli usiopingika! Kiini cha Mafarisayo ni unafiki. Wanaamini katika Mungu lakini hawapendi ukweli au kutafuta maisha. Wanamwamini tu katika Mungu asiye dhahiri juu mbinguni na mawazo yao wenyewe na dhana zao, lakini hawamwamini au kumkubali Kristo mwenye mwili. Kusema kweli, wote ni wasioamini. Kumwamini kwao Mungu ni kuifanyia utafiti teolojia na kuchukulia imani kwa Mungu kama aina ya maarifa ya kufanya utafiti. Riziki yao inategemea kuifanyia utafiti Biblia na teolojia. Katika mioyo yao, Biblia ni riziki yao. Wanafikiri jinsi walivyo bora zaidi katika kueleza ujuzi wa kibiblia na nadharia ya kiteolojia, ndivyo kutakuwa na watu zaidi ambao wanawaabudu na ndivyo wanavyoweza kusimama juu zaidi na kuwa imara zaidi kwenye jukwaa, na ndivyo hadhi zao zitakavyokuwa imara zaidi. Ni hasa kwa sababu Mafarisayo ni watu ambao wanaishi tu kwa ajili ya hadhi zao na riziki yao, na ni watu ambao wamechoshwa na kudharau ukweli, kwamba wakati Bwana Yesu alikuwa mwili na kuja kufanya kazi, walishikilia kwa utundu mawazo yao na dhana zao na ujuzi wa kibiblia kwa ajili ya kulinda hadhi zao na riziki yao, kufanya kila kitu ili kupinga na kumshutumu Bwana Yesu na kumpinga Mungu. Kutoka kwa maneno ya Mwenyezi Mungu tunaweza kabisa kuona ukweli wa asili ya Mafarisayo wanaochukia ukweli na mizizi ya upinzani wao kwa Mungu. Mwenyezi Mungu anasema, “Je, mngependa kujua kiini cha sababu ya Mafarisayo kumpinga Yesu? Je, mnataka kujua dutu ya Mafarisayo? Walikuwa wamejawa na mawazo makuu kuhusu Masiha. Kilicho zaidi, waliamini tu kuwa Masiha angekuja, ilhali hawakutafuta ukweli wa uzima. Na hivyo, hata leo bado wanamngoja Masiha, kwani hawana maarifa ya njia ya uzima, na hawajui ukweli ni nini. Ni vipi, hebu nielezeni, watu wapumbavu, wakaidi na washenzi kama hawa wangeweza kupata baraka za Mungu? Wangewezaje kumwona Masiha? Walimpinga Yesu kwa sababu hawakujua mwelekeo wa kazi ya Roho Mtakatifu, kwa sababu hawakuijua njia ya ukweli uliozungumziwa na Yesu, na zaidi, kwa sababu hawakumwelewa Masiha. Na kwa kuwa hawakuwa wamewahi kumwona Masiha na hawakuwa wamewahi kuwa pamoja na Masiha, walifanya kosa la kuning’inia bila mafanikio kwa jina la Masiha huku wakipinga dutu ya Masiha kwa kila njia iwezekanayo. Mafarisayo hawa kwa dutu walikuwa wakaidi, wenye kiburi na hawakutii ukweli. Kanuni ya imani yao kwa Mungu ni: Haijalishi mahubiri Yako ni makubwa vipi, haijalishi mamlaka Yako ni makubwa vipi, Wewe si Kristo iwapo Huitwi Masiha. Je, maoni haya si ya upuuzi na ya kudhihaki?(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kufikia Utakapouona Mwili wa Kiroho wa Yesu, Mungu Atakuwa Ametengeneza Upya Mbingu na Dunia). “Hapo zamani, wakati Mungu alikuwa hajawa mwili, inawezekana ulikuwa mtu wa dini, au msahilina. Baada ya Mungu kuwa mwili, wasahilina wengi kama hao waligeuka bila kujua na kuwa wapinga Kristo. Unajua ni nini kinachoendelea hapa? Katika imani yako kwa Mungu, hujikiti katika uhalisi au kuufuatilia ukweli, bali unashikilia sana uongo—je, si hiki ndicho chanzo wazi cha uadui wako na Mungu mwenye mwili? Mungu mwenye mwili anaitwa Kristo, hivyo sio kwamba wote ambao hawamwamini Mungu mwenye mwili ni wapinga Kristo?(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ni Wale tu Wanaomjua Mungu na Kazi Yake Ndio Wanaoweza Kumridhisha Mungu). Hii inaonyesha kwamba kwa asili Mafarisayo wa kidini wamechoshwa na ukweli na huchukia ukweli. Wanaamini tu katika dhana zao na mawazo yao. Wanaamini tu katika nadharia za kiteolojia zilizotafitiwa na zilizoundwa na wao wenyewe, lakini hawaamini katika Kristo mwenye mwili au ukweli ulioonyeshwa na Kristo. Wote ni maadui wa Mungu mwenye mwili. Wao ni wapinga Kristo waliofunuliwa na kazi ya Mungu mwenye mwili katika siku za mwisho! Wale wanaowafuata ni sawa na wao, pia kwa ukaidi wanashikilia dhana zao na mawazo kama vile ujuzi wa Biblia na nadharia ya kiteolojia. Wanazifuata katika kumkana Kristo, kumpinga na kumhukumu Kristo, wakikataa kukubali ukweli na kumchukulia Kristo kama adui! Ukweli unatosha kuthibitisha kwamba, kwa asili na kiini, mtu yeyote anayefuata Mafarisayo pia amechoshwa na ukweli na anachukia ukweli! Njia wanayotembea hasa ni njia ya Mafarisayo. Wao ni katika kikundi sawa na Mafarisayo na wote ni watu wanaompinga Kristo! Huu ni ukweli ambao wote wanaweza kuona. Tayari umefunuliwa kabisa na kazi ya Mungu ya siku za mwisho!

Katika dini, watu wote wanaamini katika Mungu chini ya udhibiti wa Mafarisayo, wakiwafuata kikamilifu na kuwasikiliza. Kama wao, wanajifunza Biblia tu na teolojia, wakiwa makini tu kuelewa ujuzi wa kibiblia na nadharia ya kiteolojia, na kamwe kutolenga kutafuta ukweli au kutenda maneno ya Bwana. Kama Mafarisayo, wanaamini tu katika Mungu asiye dhahiri mbinguni, lakini hawaamini katika Kristo mwenye mwili wa siku za mwisho—Mwenyezi Mungu. Haijalishi jinsi ukweli ulioonyeshwa na Mwenyezi Mungu ulivyo na mamlaka na nguvu, bado wanaendelea kushikilia dhana na mawazo yao kwa ukaidi, na kufuata wachungaji na wazee katika kumpinga na kumshutumu Mwenyezi Mungu. Ni wazi kuwa, watu kama hao ni aina sawa na Mafarisayo, na wanatembea njia ya kumpinga Mungu ya Mafarisayo! Hata kama watu kama hao hawawafuati Mafarisayo, bado ni aina moja ya watu kama Mafarisayo na pia ni vizazi vya Mafarisayo kwa sababu asili yao na kiini ni sawa. Wao ni wasioamini ambao wanajiamini tu wenyewe lakini hawapendi ukweli! Wao ni wapinga Kristo ambao hudharau ukweli na kupinga Kristo! Kama tu Alivyofichua Mwenyezi Mungu: “Kuna watu wengi kanisani ambao hawana ufahamu, na jambo la uongo linapotendeka wanasimama tu upande wa Shetani. Wanapoitwa vibaraka wa Shetani wanahisi kuwa wamekosewa sana. Wanasemekana kuwa hawana ufahamu, lakini daima wanasimama upande usiokuwa na ukweli. Hakujakuwa na wakati muhimu ambapo wamesimama upande wa ukweli, hakuna wakati mmoja ambapo hawasimami na kutetea mjadala juu ya ukweli. Je, kweli hawana ufahamu? Kwa nini daima wao husimama upande wa Shetani isipotarajiwa? Kwa nini hawasemi neno lolote la haki ama lenye mantiki kwa ukweli? Je, hali hii kweli imetokana na kuchanganyikiwa kwao kwa ghafla? Kadri mtu anapokuwa na ufahamu mdogo, ndivyo anavyozidi kushindwa kusimama upande wa ukweli. Je, hili linaonyesha nini? Je, halionyeshi kuwa wale wasio na ufahamu wanapenda uovu? Je, halionyeshi kuwa wale wasio na ufahamu ni watoto waaminifu wa Shetani? Je, ni kwa nini daima wanaweza kusimama upande wa Shetani na kuzungumza lugha moja naye? Kila neno na tendo lao, na maonyesho yao yanathibitisha vya kutosha kuwa wao sio wapenzi wa ukweli kwa namna yoyote, lakini badala yake wao ni watu wanaochukia ukweli(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Onyo kwa Wale Wasiotenda Ukweli). Je, huu si ukweli? Wakati watu wengine wa dini wanawafuata wachungaji na wazee, wao hawawasikilizi tu bali wanafanya kila wawezalo kuwalinda; mara tu wanaposikia mtu akiwafunua wachungaji wa kidini na wazee, watu hawa watahisi wasiwasi na kuja nje kuwatetea wachungaji na wazee. Tatizo hapa ni lipi? Je, hii haitoshi kuthibitisha kwamba watu hawa wana wachungaji na wazee pekee yao katika mioyo yao lakini hakuna mahali pa Mungu? Katika mioyo ya watu hawa, wachungaji wa kidini na wazee wote ni wa juu zaidi kuliko Mungu. Hii inaonyesha tatizo gani? Mwanadamu anapompinga Mungu, hakuna wengi wanaokuja kumtetea Mungu. Hakuna wengi ambao wanaweza kusimama na kuwa na ushuhuda kwa Mungu! Lakini mara tu kiini cha Mfarisayo cha wachungaji wa kidini na wazee kinapofunuliwa, kwa nini kuna watu wengi ambao hulilia haki kwa niaba yao na kuja kuwatetea? Hii inatosha kuthibitisha kuwa watu hawa ni wazao watiifu wa Mafarisayo wa kidini. Wao ni washirika na vibaraka wa wapinga Kristo! Hii ni kweli hakuna mtu anayeweza kukataa!

Kimetoholewa kutoka katika Maswali na Majibu Bora zaidi Kuhusu Injili ya Ufalme

Dini ni mahali pa aina gani? Ni ulimwengu wa Mafarisayo, kiota cha zamani cha wapinga Kristo! Kufikiri kwamba unaweza kuokolewa kwa kumwamini Mungu huko ni ndoto tu! Kwa nini mtu hawezi kuokolewa kama anamwaamini Mungu katika dini? Sababu kuu ni kwamba, Mungu alipofanya kazi mpya katika siku za mwisho, kazi ya Roho Mtakatifu imehamishwa pamoja na kazi mpya ya Mungu, na ulimwengu wa kidini hivyo ulipoteza kazi ya Roho Mtakatifu, ukawa kame. Zaidi ya hayo, ulimwengu wa kidini umedhibitiwa kabisa na Mafarisayo wanafiki na wapinga Kristo, na kwa muda mrefu pamekuwa mahali ambapo panampinga Mungu. Sio tu kwamba Roho Mtakatifu hafanyi kazi katika dini, Mungu mwenye mwili pia haji katika dini kufanya kazi. Kwa hiyo, mtu hawezi kupitia kazi ya Mungu ya siku za mwisho kwa kumwamini Mungu katika dini. Hawawezi kula, kunywa na kufurahia maneno ya Mungu katika siku za mwisho, na hivyo kwa kawaida huanguka katika giza. Kama watu hawatafuti na kuchunguza njia ya kweli sasa, itakuwa rahisi sana kuanguka katika uharibifu na kutopokea wokovu wa Mungu! Watu ambao wameanguka katika uharibifu wa ulimwengu wa kidini hushikilia tu kwenye Biblia wakati wa mikutano na hawawezi kufurahia maneno ya sasa ya Mungu. Bila kazi na mwongozo wa Roho Mtakatifu, Mungu ambaye mwanadamu anaamini kwake ni asiye dhahiri. Mawasiliano yao yote katika mikutano ni kuhusu rekodi za kazi na maneno ya Mungu katika Biblia kutoka zamani. Watu kama hao wanawezaje kupata wokovu wa Mungu wa siku za mwisho na kupokea ahadi ya Mungu? Ni kama hapo nyuma wakati Bwana Yesu alianza kufanya kazi nje ya hekalu. Hekalu likawa nchi bure yenye machafuko, pango la wezi. Kwa sababu hawakufuata kazi ya Bwana Yesu, wale waliobaki katika hekalu walikuwa bado wanashikilia sheria na kanuni za zamani, kwa kawaida wakipotelewa na wokovu wa Bwana. Vivyo hivyo, sasa katika siku za mwisho, Mwenyezi Mungu amefanya kazi Yake ya hukumu kuanzia katika nyumba ya Mungu, kuonyesha ukweli ili kumhukumu na kuwatasa wanadamu, kumfanya mwanadamu ajinasue kutoka kwa tabia mbaya ya Shetani na mvuto ili kupata wokovu wa Mungu, na kukamilishwa na Mungu kuwa mshindi na moja kwa moja kuchukuliwa katika ufalme Wake. Hii ni fursa kubwa! Kama mwanadamu hafuati kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho, hataweza kupokea wokovu na kuingia ufalme wa mbinguni. Hebu tusome baadhi kutoka kwa maneno ya Mwenyezi Mungu. “Wale wasioikubali kazi mpya ya Mungu hawana uwepo wa Mungu na, zaidi, wanakosa baraka na ulinzi wa Mungu. Maneno na matendo yao mengi yanashikilia matakwa ya zamani ya kazi ya Roho Mtakatifu; ni mafundisho ya kidini, si ukweli. Mafundisho na taratibu kama hizo ni thibitisho la kutosha kuwa kukutana pamoja kwa watu hawa si linguine ila dini; si watu walioteuliwa au vyombo vya kazi ya Mungu. Mkutano wa wale wote walio miongoni mwao unaweza tu kuitwa mkutano mkubwa wa watu wa dini, na bali hauwezi kuitwa kanisa. Huu ni ukweli usioweza kubadilishwa. Hawana kazi mpya ya Roho Mtakatifu; wakifanyacho kinaonekana chenye kunuka dini, wanachoishi kwa kudhihirisha katika maisha yao kinaonekana kimejaa dini; hawana uwepo na kazi ya Roho Mtakatifu, sembuse kustahiki kupokea nidhamu au nuru ya Roho Mtakatifu. Watu hawa wote ni miili isiyo na uhai, na funza wasio na mambo ya kiroho. Hawana ufahamu wa uasi na pingamizi wa mwanadamu, hawana ufahamu wa uovu wote wa mwanadamu, sembuse kujua kazi yote ya Mungu na mapenzi ya sasa ya Mungu. Wote ni watu wapumbavu, waovu, ni watu duni wasiostahili kuitwa waumini!(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kazi ya Mungu na Utendaji wa Mwanadamu). “Wale ambao wanataka kupata uzima bila kutegemea ukweli wa neno la Kristo ni watu wafidhuli mno duniani, na wale ambao hawawezi kukubali njia ya maisha inayoletwa na Kristo wamepotea ndotoni. Na hivyo nasema kwamba watu ambao hawakubali Kristo wa siku za mwisho watadharauliwa milele na Mungu. Kristo ni lango la binadamu kwa ufalme katika siku za mwisho, ambayo hakuna anayeweza kupita bila Yeye. Hakuna anayeweza kukamilishwa na Mungu ila kwa njia ya Kristo. Unaamini katika Mungu, na hivyo ni lazima ukubali neno Lake na kutii njia Yake. Lazima usifikiri juu ya kupata baraka tu bila kupokea ukweli, au kukubali utoaji wa maisha. Kristo Anakuja katika siku za mwisho ili wale wote ambao kweli wanaamini katika Yeye waweze kupata maisha. Kazi Yake ni kwa ajili ya kuhitimisha enzi ya zamani na kuingia enzi mpya, na ni njia ambayo lazima ichukuliwe na wale wote ambao wataingia enzi mpya. Kama huna uwezo wa kumtambua Yeye, na badala yake kumhukumu, kulikufuru jina Lake au hata kumtesa Yeye, basi wewe umefungwa kuchomwa milele, na kamwe hutaingia katika ufalme wa Mungu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ni Kristo wa Siku za Mwisho Pekee Ndiye Anayeweza Kumpa Mwanadamu Njia ya Uzima wa Milele). Hii inaonyesha kwamba wote ambao hawakubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na wale ambao hawatii kazi ya Mungu ya sasa na maneno ni walengwa wa chukizo la Mungu. Kwa njia hii, wale ambao wanabaki katika maeneo ya kidini kwa kawaida wamepoteza uongozi wa Mungu na hawawezi kupata ruzuku ya maneno halisi ya Mungu. Wanaweza tu kuanguka katika giza na kuondolewa, wakipoteza wokovu wa Mungu wa siku za mwisho. Kama ilivyokuwa katika Enzi ya Neema, watu bado waliendelea kushikilia kazi na kanuni kutoka kwa Enzi ya Sheria, kwa kawaida kupotelewa na wokovu wa Bwana Yesu. Katika Enzi ya Ufalme, kama watu bado wanashikilia kazi na kanuni kutoka kwa Enzi ya Neema, kwa kawaida wataachwa na kuondolewa na Mungu na hawataokolewa katika ufalme wa mbinguni! Huu ni ukweli ambao hakuna mtu anayeweza kubadilisha!

Kumwamini Mungu katika dini, wanataka kumpendeza Shetani na wapinga Kristo kwa upande mmoja na kwa upande mwingine wanataka kupokea wokovu wa Mungu—je, hiyo inawezekana? Dunia ya kidini inadhibitiwa na Mafarisayo wanafiki na kudhibitiwa na wachungaji wa kidini na wazee. Ukweli ni kwamba inadhibitiwa na wapinga Kristo hawa wapinzani wa Mungu. Huu ni ukweli ulio imara! Wachungaji na wazee wanapofanya kazi na kuhubiri, hawatilii maanani kueleza au kushuhudia maneno ya Bwana, au kushuhudia kazi ya Mungu na tabia Yake katika Biblia. Wanatilia maanani tu kueleza maneno ya mwanadamu katika Biblia na kutumia maneno ya mwanadamu katika Biblia kuchukua nafasi ya maneno ya Mungu na kufanya maneno ya Mungu yasiwe na maana, kuwafanya watu wote wafuate maneno ya mwanadamu huku wakikaa mbali na maneno ya Mungu. Zaidi ya hayo, pia wanalenga kueleza ujuzi wa Biblia na nadharia ya kiteolojia, wakifafanua wahusika katika Biblia, historia yao, na kadhalika. Wao wanaeleza mambo haya ili kujionyesha na kuwafanya wengine wawaabudu, kuchukua watu kwenye njia ya kumfuata mwanadamu, kumwabudu mtu na kumpinga Mungu. Hasa wakati Mwenyezi Mungu anapokuja kufanya kazi Yake ya siku za mwisho, wao hupinga na kumshutumu Mwenyezi Mungu kwa ghadhabu, na kufanya yote wanayoweza kuwakinga na kuwawekea watu mipaka kutotafuta na kuchunguza njia ya kweli, kuwazuia watu kukubali ukweli ulioonyeshwa na Mwenyezi Mungu na kutowaruhusu wapokee ruzuku ya maneno ya Mwenyezi Mungu. Wanaruhusu tu watu kukubali udanganyifu wao mbalimbali na nadharia za kiitikadi. Kwa hivyo, watu wanapomwamini Mungu katika maeneo ya kidini yaliyosimamiwa na Mafarisayo na wapinga Kristo, na kukubali mafundisho ya Mafarisayo wa kidini, mawazo yao na mitazamo, uamuzi, na uwezo wa kupokea wote hushawishiwa na kuathirika nao. Wao kawaida huwa wenye giza ndani zaidi na zaidi na kutengwa kutoka kwa Mungu! Mwenyezi Mungu anapokuja kufanya kazi Yake katika siku za mwisho, wao hufungwa na kudhibitiwa na Mafarisayo wa kidini na wapinga Kristo, na hivyo hawataweza kusikia matamshi ya kweli ya Mungu au kufurahia ruzuku ya maji yaliyo hai ya uzima yanayotiririka kutoka kwenye kiti cha enzi cha Mungu. Kwa njia hiyo, hawataweza kupokea wokovu wa Mungu wa siku za mwisho. Cha kutia hofu zaidi ni kwamba, ingawa watu wanamwamini Mungu katika dini, kile wanachofuata ni wanadamu, wapinga Kristo, na njia wanayoitembea ni hasa ile ya Mafarisayo na wapinga Kristo. Baada ya muda, wao pia watageuka kuwa Mafarisayo. Basi wanawezaje kuwa watu wanaofuata mapenzi ya Mungu na kuingia katika ufalme wa mbinguni? Hiyo hakika haiwezekani! Sasa, kiini cha ulimwengu wa dini kimefunuliwa kabisa kupitia kazi ya Mwenyezi Mungu wa siku za mwisho. Dunia ya dini sio ufalme wa mbinguni; ni kiota cha zamani cha wapinga Kristo. Ni ngome imara ambayo inampinga Mungu, ufalme wa kishetani unaompinga Mungu! Kwa hiyo, watu hawawezi kufikia wokovu kwa kumwamini Mungu katika dini. Hata kama ni mtu anayependa ukweli, kwa kuwa hawakubali kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho, hawataweza kupata ruzuku ya maneno yaliyotolewa na Kristo wa siku za mwisho na pia hawataweza kupokea wokovu wa Mungu!

Kimetoholewa kutoka katika Maswali na Majibu Bora zaidi Kuhusu Injili ya Ufalme

Iliyotangulia: Unafiki ni nini?

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp