Ufalme wa Mbinguni Kwa Kweli Upo Duniani

24/12/2019

Na Chen Bo, China

Tunachotamani zaidi sisi waumini ni kuweza kuingia katika ufalme wa mbinguni na kufurahia furaha ya milele aliyopewa mwanadamu na Mungu. Kila wakati nilipomsikia mchungaji akihubiri kwamba pahali ambapo Bwana atatutayarishia katika siku za mbele pako mbinguni, na kutakuwa na nyanja za dhahabu na kuta za mawe ya thamani ya kijani kibichi, vito vitameremeta kila mahali, na tunaweza kula tunda la mti wa uzima na kunywa maji ya mto wa uzima, kwamba hakutakuwa na uchungu, machozi na huzuni tena, na sote tutakuwa huru na kukombolewa, ningehisi mfuro wa hisia kubwa na furaha kubwa. Hapa ni pahali nilipopatamani sana, na maisha yangu duniani ya kazi ya taabu na huzuni kweli yalinifanya kuhisi mchovu sana. Kisha ningeharakisha kila mahali na kujitumia kwa shauku kwa sababu ya Bwana; ningeeneza injili na kuanzisha makanisa, na sikuwahi kukoma bila kujali jinsi hali ilivyogeuka kuwa ya uchungu ama ngumu. Hasa sasa kwa kuwa tuko katika siku za mwisho na Bwana atarudi karibuni na kutupeleka sote nyumbani mbinguni, nilifanya kazi na kujitumia kwa jitihada hata zaidi.

Siku moja, nilienda nyumbani kwa dadangu ili kumwangalia mama yetu. Kabla ya kuondoka, dadangu alinipa kitabu, akinisisitiza kuwa na hakika nikisome kwa makini. Nilifikiria mwenyewe: Kitabu hiki ambacho dadangu alinipa hakika ni kazi ya roho. Ilitukia tu kwamba roho yangu inahisi kavu kabisa sasa hivi, haihisi kana kwamba Bwana yu nami, na sihisi kuangaziwa kutokana na kusoma Biblia. Nitakaporudi, napaswa kusoma kitabu hiki kwa makini. Pengine kitanipa kitu. Baada ya kurudi nyumbani, nilifungua kitabu hicho na kuanza kusoma, na kabla sijajua nilivutiwa na maneno katika kitabu hicho. Kadri nilivyozidi kukisoma ndivyo nilivyozidi kukifurahia, kadiri nilivyozidi kukisoma ndivyo nilivyozidi kuhisi kwamba kulikuwa na mwanga katika maneno haya, kwamba yalitiwa nuru na Roho Mtakatifu, kuwa hakukuwa na njia kwamba maneno haya yangeweza kuzungumzwa na mwanadamu wa kawaida. Tangu kukisoma kitabu hiki, nimekuja kuelewa ukweli kiasi ambao sikuwa nimeelewa awali kutoka kusoma Biblia, na katika akili yangu nahisi uwazi na raha. Niko tayari kuomba ili kumkaribia Bwana, na imani yangu imekua. Hali yangu ya kiroho imekuwa nzuri zaidi na zaidi. Nilifikiri: Ni kazi ya Roho Mtakatifu pekee inaweza kumpa mwanadamu imani na nguvu, na kukimu na kustawisha roho ya mwanadamu. Maneno katika kitabu hiki hakika yanatoka kwa Roho Mtakatifu. Matokeo ni, kitu cha kwanza mimi hufanya kila asubuhi ninapoamka ni kusoma kitabu hiki.

Siku moja, nilifungua kitabu hicho na kusoma fungu lifuatalo: “Mungu kuingia rahani kunamaanisha kwamba Hatafanya tena kazi Yake ya wokovu wa binadamu. Binadamu kuingia rahani kunamaanisha kwamba binadamu wote wataishi ndani ya mwangaza wa Mungu na chini ya baraka Zake; hakutakuwa na upotovu wowote wa Shetani, wala maovu yoyote kutokea. Binadamu wataishi kama kawaida duniani, na wataishi chini ya ulinzi wa Mungu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mungu na Mwanadamu Wataingia Rahani Pamoja). Nilikoma hapo. Moyo wangu ulishtuka, na nilifikiria mwenyewe: Katika siku za baadaye mwanadamu ataishi duniani? Je, Bwana Yesu hakuahidi kwamba katika siku za baadaye tungeishi mbinguni? Maneno haya yanazungumza vipi kuhusu kuwa duniani? Hili linawezekanaje? Je, nasoma hili visivyo? Kwa hivyo nilisoma tena fungu hilo kwa makini, na maneno hayo kwa kweli yalikuwa yakisema kwamba katika siku za baadaye mwanadamu angeishi duniani. Basi hilo kwa kweli linamaanisha nini? Hili halifai. Ilinilazimu kuelewa hili lilimaanisha nini kwa kweli. Hivyo, niliendelea kusoma: “Mungu ana hatima ya Mungu na mwanadamu ana hatima ya mwanadamu. Apumzikapo, Mungu ataendelea kuwaongoza binadamu wote kwa maisha yao duniani. Akiwa kwa mwangaza wa Mungu, mwanadamu atamwabudu Mungu wa kweli aliye mbinguni. … Binadamu wanapoingia rahani, kunamaanisha kwamba mwanadamu amekuwa kiumbe halisi; binadamu watamwabudu Mungu wakiwa duniani na kuwa na maisha ya kawaida ya wanadamu. Watu hawatakuwa tena wasiomtii Mungu ama kumpinga Mungu; watarudia maisha asili ya Adamu na Hawa(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mungu na Mwanadamu Wataingia Rahani Pamoja). Kadiri nilivyozidi kusoma ndivyo nilivyozidi kuhisi kuchanganyikiwa: Mwanadamu atamwabudu Mungu akiwa duniani? Hili litafanyika vipi? Katika Biblia haisemwi kwamba hili litafanyika mbinguni? Linawezaje kuwa duniani? Nilikimbilia Biblia yangu, kuifungua kwa Yohana 14:2-3, na kusoma mahali Bwana Yesu anasema: “Katika nyumba ya Babangu kuna majumba mengi: ingalikuwa sivyo, ningaliwajulisha. Naenda kuwatayarishia mahali. Na nikienda kuwatayarishia mahali, nitarudi tena na kuwapokea kwangu; ili mahali nipo, muweze kuwa pia.” Bwana Yesu anasema dhahiri kwamba ufufuo Wake na kupaa mbinguni ilikuwa ili kutuandalia mahali, kwa hivyo hatima yetu inapaswa kuwa mbinguni. Hii ni ahadi ya Bwana! Nilifikiria mwenyewe: Kile ambacho kitabu hiki kinasema ni tofauti na kile ambacho Bwana anasema, kwa hivyo siwezi kuendelea kukisoma. Baada ya kufunga kitabu hicho nilikuwa katika hali ya kuchanganyikiwa sana, sikujua kile kilichokuwa sahihi, kwa hivyo nikaendelea kumwomba Bwana: “Ee Bwana, tafadhali niongoze na unielekeze. Nifanye nini? Napaswa kusoma kitabu hiki au la? Ee Bwana, tafadhali nipe nuru, niongoze….” Baada ya kuomba nilifikiri kuhusu jinsi baada ya kusoma kitabu hiki nilihisi karibu zaidi katika uhusiano wangu kwa Bwana, mwenye shauku zaidi kuhusu imani yangu katika Bwana, na kwamba roho yangu ilikuwa ikikimiwa. Ningeweka kitabu hiki chini na kuacha kukisoma basi ningerudi katika hali yangu ya awali ambapo roho yangu ilihisi kavu Kwa kuwa kitabu hiki kilinifanyia mengi, kwa kuwa ningeweza kuwa na uhakika kwamba kilitoka kwa Roho Mtakatifu, kwamba hakingeweza kukosea kwa vile kilitoka kwa Roho Mtakatifu, ingawa maneno haya hayakufuatana na dhana zangu sipaswi kuyakana kwa sababu hii na kutoyasoma. Nilipokuwa nikifikiri kuhusu hili, niliamua ingekuwa bora kuendelea kusoma kabla ya kukata ushauri.

Kwa hiyo nilichukua tena kitabu hicho na kuendelea kusoma: “Pahali pa pumziko pa mwanadamu ni duniani, na pahali pa Mungu pa pumziko ni mbinguni. Wakati binadamu wanamwabudu Mungu katika pumziko, wataishi duniani, na wakati Mungu anaongoza sehemu iliyobaki ya binadamu katika pumziko, Atawaongoza kutoka mbinguni, sio kutoka duniani(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mungu na Mwanadamu Wataingia Rahani Pamoja). Niliendelea kutafakari hili tena na tena akilini mwangu: Fungu hili sasa linasema kwamba mahali pa Mungu pa mapumziko ni mbinguni, na kwamba wakati mwanadamu anapumzika atamwabudu Mungu duniani. Inawezekana kuwa kwamba mahali pa mwanadamu pa mapumziko kweli ni duniani kama maneno haya yanavyosema? Haiwezekani! Bwana Yesu tayari amesema kwamba tutakuwa mahali popote Bwana yuko, na Bwana Yesu alifufuka na kupaa mbinguni, kwa hivyo hakika pia sisi tutapaa mbinguni! Nilifikiri nyuma kwa miaka iliyopita, jinsi nilivyokuwa nimetembelea njia nyingi kwa ajili ya Bwana, jinsi nilivyohimili mateso mengi, Je, haikuwa ili nipae mbinguni na kutohimili tena mateso duniani? Kama kweli ni vile kitabu hiki kinasema, kwamba katika siku za baadaye mwanadamu bado atakuwa akiishi duniani, basi si matumaini yangu hayatafanikishwa? Nililala nikiwa nimepooza juu ya kitanda changu cha kang. Nilihisi mdhaifu kutoka kichwani hadi kidole cha mguu. Kadiri nilivyozidi kufikiri juu ya hili ndivyo nilivyoshindwa kutulia. Kwa hivyo, ili kuelewa hili, nilikimbia hadi nyumbani kwa dadangu.

Nilipowasili nyumbani kwa dadangu, nilikutana na mwanamke wa makamo, na kupitia dadangu kututambulisha dadangu nilipata kujua kwamba huyu alikuwa Dada Li. Baada ya muda mfupi, nilizungumza nao kuhusu mawazo yangu baada ya kusoma kitabu hiki. Baada ya kusikiza, Dada Li alishirikiana nami, akisema: “Dada, sote ambao tunamwamini Bwana tunafikiri kwamba Bwana Yesu ameahidi kumwandalia mwanadamu mahali, na kwamba popote Alipo Atatuomba tukuje hapo. Bwana amepaa mbinguni, kwa hivyo katika siku za baadaye wakati Bwana atarudi hakika Atatupokea mbinguni kuishi pamoja naye. Lakini kuna yeyote kati yetu ambaye amewaza kuhusu iwapo fikira na mawazo ya aina hii yanaweza kutetewa? Kama ingekuwa jinsi tunavyofikiri kwamba Bwana angerudi na kutuleta kuishi mbinguni, basi si maneno katika sala ya Bwana ‘Ufalme wako ufike, Mapenzi yako yafanywe duniani, kama ilivyo mbinguni(Mathayo 6:10) na unabii katika Ufunuo ‘Tazama, hema takatifu la Mungu liko pamoja nao watu, na yeye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Na yeye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, na kuwa Mungu wao(Ufunuo 21:3) haukutimika? Mambo haya yangetimika vipi kama yalivyotabiriwa? Iwapo hatima ya mwisho ambayo Mungu hutupa ilikuwa mbinguni, basi wakati Mungu alimuumba mwanadamu kwanza, umuhimu wa Yeye hutufanya tuishi duniani ulikuwa upi?” Sikuridhishwa hata kidogo, na kujibu vikali: “Hata ingawa vifungu hivi vitakatifu vinasema vitu hivi, Bwana Mwenyewe alisema: ‘Naenda kuwatayarishia mahali. Na nikienda kuwatayarishia mahali, nitarudi tena na kuwapokea kwangu; ili mahali nipo, muweze kuwa pia(Yohana 14:2-3). Baada ya Bwana Yesu kufufuka, Alipaa mbinguni, na hapa Bwana anasema kwamba Ataenda kutuandalia mahali. Anasema kwamba Alipo, sisi pia tutakuwepo. Kwa hivyo hili linathibitisha kwamba Mungu alituahidi kwamba tutapaa mbinguni kupata uzima wa milele, sio kwamba tutapata uzima wa milele duniani. Hili ni jambo ambalo hakuna anayeweza kulikana!” Dada Li aliendelea kuzungumza kwa subira: “Dada, ni kweli kwamba Bwana anawaandalia mahali wale wanaomwamini, lakini mahali hapa kweli papo duniani au mbinguni? Bwana hasemi hivyo katika maneno haya, kwa hivyo tunategemeza kwa kipi tunaposema kwamba mahali Anatuandalia papo mbinguni? Je, kweli hii ni ahadi ya Mungu au ni dhana na mawazo yetu wenyewe? Kwa wale wetu wanaomwamini Mungu, mambo yote yanapaswa kutegemezwa kwa neno la Bwana, hatupaswi kuchanganya dhana na mawazo yetu wenyewe na neno la Bwana na kisha tuseme kwamba hii ndiyo maana ya Bwana. Je, huku si kutegemea mawazo yetu wenyewe kuelezea neno la Mungu? Je, huku si kupotosha neno la Bwana? Hivyo, hatuwezi kutegemea fikira zilizo kichwani mwetu na mawazo yetu wenyewe na upendeleo kuelezea neno la Bwana. Iwapo ni hivyo, tutakosea. Katika Mwanzo 2:7-8 inasema: ‘Na Yehova Mungu akamwumba mwanadamu kupitia mavumbi yaliyo ardhini na kupuliza pumzi ya uhai ndani ya pua yake; na mwanadamu huyo akawa nafsi iishiyo. Na bustani ikapandwa mashariki mwa Edeni na Yehova Mungu; na ndani hapo akamweka mwanadamu huyo ambaye alikuwa amemuumba.’ Ni dhahiri kwamba mwanzoni Mungu alimwumba mwanadamu duniani, na kabla ya Mungu kumwumba mwanadamu kwanza Aliumba vitu vyote ili kuandalia mwanadamu mazingira mazuri ya kuishi ndani yake. Kwa hivyo tunaweza kuona kwamba ni mapenzi ya Mungu kutufanya tuishi duniani. Aidha, katika sala ya Bwana, Bwana anatufanya tumwombe Mungu kwamba ufalme Wake ufike duniani. Imetabiriwa katika kitabu cha Ufunuo: ‘Falme za ulimwengu zimekuwa falme za Bwana wetu, na za Kristo wake(Ufunuo 11:15) na ‘Hema takatifu la Mungu liko pamoja nao watu, na yeye atakaa pamoja nao(Ufunuo 21:3). Kutoka kwa mistari hii ya Maandiko na unabii tunaweza kuona kwamba mahali ambapo Mungu anatuandalia yapo duniani, na kwamba hatima yetu ya mwisho katika siku za baadaye iko duniani na si mbinguni….” Ushirika wa Dada Li ulipingana kabisa na dhana zangu. Sikusikiza alichosema kabisa. Nilisimama na kumwambia kwa hasira: “Acha kuzungumza! Kwa miaka kadhaa nimekimbia, kutumia na kuteseka kwa ajili ya Bwana ili niweze kupaa mbinguni! Wakati huu wote nimekuwa nikingojea kwa hamu Bwana kunirudisha nyumbani mbinguni, ili nisiteseke tena duniani. Unasema kwamba hatima yetu ya mwisho iko duniani. Siwezi kukubali hili.” Baada ya kusema hili niligeuka kuondoka. Dadangu mdogo alikimbia kujaribu kuniongelesha: “Dada, unawezaje kuwa mkaidi hivyo? Je, mtazamo huu unaoshikilia ni sahihi? Bwana asema ‘nikienda kuwatayarishia mahali,’ hujui maana ya kweli ya maneno haya, na unashikilia mawazo yako mwenyewe, Je, huko si kuwa mpumbavu? Huu sio mtazamo watu wanaotafuta ukweli wanapaswa kuwa nao! Bwana Yesu ambaye tunamngoja kwa hamu tayari amerudi, Mwenyezi Mungu ni Bwana Yesu aliyerudi! Kitabu hicho ambacho nilikupa kusoma ni matamshi ya binafsi na maneno ya Mungu! Bwana, ambaye kila siku tumemtarajia aje kutuchukua, sasa amerudi. Ni lazima tusikize kwa makini. Hatupaswi kabisa kuvuruga nafasi hii adimu mno!”

Nilishangazwa kumsikia dadangu akisema maneno haya. Singeweza kabisa kuthubutu kuamini kile nilichokuwa nimesikia: Bwana amerudi? Hii ni kweli? Kisha dadangu akasema: “Haikuwa wewe uliyesema awali kwamba maneno katika kitabu hiki yanatoka kwa Roho Mtakatifu? Ulipokisoma, ulihisi ulikuwa umepewa mengi, ulikuwa na kazi ya Roho Mtakatifu, na uhusiano wako na Bwana ulikuwa wa karibu zaidi. Sasa fikiria: Kando na neno la Bwana, nani mwingine huzungumza kwa njia inayotimiza matokeo ya aina hii? Sasa Bwana amerudi kutekeleza kazi na kuonyesha maneno mapya, na tunaweza kufurahia utamu wa maneno ya Mungu. Tusipotafuta na kuchunguza, tukishikilia tu dhana na mawazo yetu bila kufikiria, na kushikilia maana halisi ya Biblia bila kuachilia, basi hatimaye tutajiharibu. Wakati wao, Mafarisayo ambao walikuwa hodari katika Biblia walishikilia maneno ndani ya Biblia kwa upofu, hawakujaribu hata kidogo kuuliza iwapo ufahamu wao wa Biblia ulikuwa sahihi au la, au iwapo ulifuata mapenzi ya Mungu au la. Badala yake walifikiri mwanadamu huyo asiyeitwa Masiya hakuwa Mwokozi ambaye angekuja, hawakuchunguza kabisa iwapo njia ya Bwana Yesu ingekimu maisha ya mwanadamu au la, au iwapo ingemwonyesha mwanadamu njia ya kutenda. Walishikilia dhana na mawazo yao kwa ukaidi tu na bila kufikiria wakakataa wokovu wa Bwana Yesu, hatimaye kutenda uhalifu mbaya sana wa kumsulubisha Bwana msalabani. Hatuwezi kufuata katika nyayo za Mafarisayo na kutembelea njia yao ya kumpinga Mungu!” Baada ya kusikiza maneno ya dadangu nilifikiri mwenyewe: Kile anachosema dadangu ni cha maana. Neno la Bwana ni suluhisho la pekee wakati roho ya mwanadamu ni kavu. Nilifikiri nyuma kwa jinsi tangu nilipoanza kusoma maneno katika kitabu hiki, hali ya roho yangu kweli ilikuwa nzuri zaidi na zaidi, jinsi kilivyonipa imani katika Mungu, na jinsi kilivyonifanya kuhisi kwamba Mungu yuko nami. Hata nilihisi kama nilielewa ukweli kiasi. Inaweza kuwa kwamba maneno katika kitabu hiki kweli yalikuwa matamshi ya Bwana aliyerudi? Bwana kurudi ni jambo kubwa sana. Ingekuwa bora kama singekataa na kuhukumu bila kufikiria, lazima niweke juhudi kuchunguza na kutafuta, siwezi kuwa kama wao Mafarisayo ambao hawakutafuta ukweli, walioshikilia dhana zao katika kumpinga Mungu! Wakati huu nilihisi mshangao wa kufurahisha na pia hofu. Nilikuwa na mshangao wa kufurahisha kwa sababu nilimwamini Bwana na kutazamia kwa hamu kurudi Kwake kunikubali katika ufalme wa mbinguni, ambapo ningeishi maisha pasi na wasiwasi, nisihitaji tena kupitia nyakati ngumu duniani, na leo nilisikia habari ya kurudi kwa Bwana. Huu kweli ni wasaa mkubwa mno na wa furaha. Niliogopa kwa sababu iwapo Mwenyezi Mungu ni Bwana aliyerudi basi ndoto yangu ya kumsubiri Bwana kunikubali katika ufalme wa mbinguni ingevunjika…. Moyoni mwangu nilihisi kila aina ya jazba, sikujua jinsi ya kuhisi. Nilihisi nisiyejiweza. Yote niliyoweza kufanya ilikuwa kumgeukia Bwana katika sala: “Ee Bwana! Kila siku nimengoja kwa hamu Wewe kuja kunileta nyumbani Kwako mbinguni, lakini wanasema kwamba mahali Umeandalia hatima yangu ya mwisho papo hapa duniani. Kweli siwezi kuukabili ukweli huu. Kweli sitaki kupitia nyakati ngumu za aina hii duniani. Ee Bwana! Nahisi mateso makubwa moyoni mwangu sasa, tafadhali nisaidie, na uniongoze kwa njia iliyo mbele.” Baada ya kuomba nilifikiri kuhusu maneno ya Bwana Yesu ambapo Anasema: “Wamebarikiwa wao walio maskini kiroho: kwa kuwa ufalme wa mbinguni ni wao(Mathayo 5:3). Ni kweli! Bwana anapenda na kuwaruhusu tu wale ambao ni maskini wa roho na ambao wanatafuta ukweli kuingia ufalme wa mbinguni. Napaswa kuwa mtu ambaye ni maskini wa roho. Ni kwa kusikiza ushirika wao kwa makini tu ndipo nitafuata mapenzi ya Bwana.

Wakati huu, Dada Li alisema: “Bwana alisema: ‘Heri wenye moyo safi; kwa kuwa hao watamwona Mungu(Mathayo 5:8). Tunapaswa kusikiza neno la Bwana, na kutenda kama watu walio na moyo safi ili kupokea kurudi kwa Bwana. Ingawa kazi ambayo Mungu anatekeleza leo haifuati dhana na mawazo yetu, bado kila kitu ambacho Mungu hufanya ni chema, chote ni kwa ajili ya mwanadamu, na miongoni mwa vitu hivyo kuna mapenzi ya Mungu, ambapo ukweli unaweza kutafutwa. Kama hatukielewi kikamilifu basi kwanza lazima tujiweke kando na kuweka juhudi kutafuta ukweli, ili tuweze kupokea nuru ya Mungu na kuelewa mapenzi ya Mungu. Dada, fungua moyo wako na kuzungumza kuhusu vitu ambavyo bado huelewi, na tunaweza kutafuta pamoja kupitia kushiriki.” Nilihisi kama kile Dada Li alikuwa amesema kilikuwa na maana, napaswa kutulia na kutafuta, hivyo, nilisema: “Dada, kuna jambo moja sielewi. Mbona hatima yetu ya mwisho haiko mbinguni lakini badala yake hapa duniani?” Dada Li alipata Yohana 3:13: “Na hakuna mwanadamu amepaa hadi mbinguni, isipokuwa yeye ambaye alishuka chini kutoka mbinguni, ambaye ni Mwana wa Adamu aliye mbinguni” na Isaya 66:1 “Kiti changu cha enzi ni mbingu, na dunia ndipo niwekapo miguu yangu” na kunipa mafungu haya mawili kusoma. Kisha alishiriki kuhusu maana ya mafungu haya mawili. Kupitia ushirika wa dada huyo nilihisi akili yangu ghafla ilikuwa wazi. Pia nilijua mafungu haya mawili kutoka kwa Maandiko, hivyo kwa nini sikuwahi kutafakari kuyahusu awali? Bwana anasema wazi kwamba kando na Mwana wa Adamu aliyekuja chini kutoka mbinguni hakuna mwanadamu anaweza kupaa mbinguni, kwa kuwa mbinguni ni kiti cha Mungu cha enzi na dunia ni mahali pa miguu ya Mungu, kwa hivyo mwanadamu angestahili vipi kupaa mbinguni? Mungu alimwumba mwanadamu duniani, na kumfanya aishi duniani. Kutoka siku Mungu alimwumba mwanadamu, mwanadamu ameishi duniani kizazi baada ya kizazi, akiongezeka taratibu kwa idadi. Kazi yote ambayo Mungu ametekeleza kumwokoa mwanadamu pia imekuwa duniani. Hiki kilikuwa kitu ambacho Mungu aliamua kabla kitambo. Ni kitu ambacho hakuna mwanadamu anaweza kukibadili. Kisha dada huyo alishiriki kuhusu Biblia, kuhusu jinsi Bwana alivyosema Angetutayarishia mahali. Alieleza kwamba hili lilimaanisha kuwa kuonekana na kazi ya Mungu mwenye mwili duniani katika siku za mwisho, na kwamba Alikuwa ameamua kabla kuwa tungezaliwa katika siku za mwisho, kwamba tungesikia sauti ya Mungu, tuletwe mbele ya kiti cha Mungu cha enzi, tukubali hukumu na utakaso wa Mungu wa siku za mwisho, na hatimaye tuongozwe katika ufalme wa Mungu. Hii ndiyo maana ya kweli ya maneno, “mahali nipo, muweze kuwa pia(Yohana 14:3). Inaonekana kwamba ufalme wa Mungu kweli uko duniani, na kwamba hatima ya mwisho ya wanadamu iko duniani na sio mbinguni! Wakati huu wote nilikuwa nimeishi ndani ya dhana na mawazo yangu mwenyewe, nilikuwa nimeweka mipaka kwamba Mungu angerudi kunileta mbinguni kuishi, lakini hili kweli halikubaliani na mapenzi ya Mungu, hili halikubaliani na ukweli! Hata hivyo, bado sikuwa radhi kuishi maisha ya aina hii duniani ambapo niliteswa na Shetani. Kwa hivyo muda mfupi baadaye, nilieleza mawazo niliyokuwa nayo kwa Dada Li.

Bada ya kunisikiza, Dada Li alifungua kitabu cha Neno Laonekana katika Mwili, na kunisomea fungu kutoka kwa neno la Mwenyezi Mungu: “Maisha ya pumziko ni yale bila vita, bila uchafu, bila udhalimu unaoendelea. Hii ni kusema kwamba hayana unyanyasaji wa Shetani (hapa ‘Shetani’ inamaanisha nguvu za uhasama), upotovu wa Shetani, na pia uvamizi wa nguvu yoyote inayompinga Mungu. Kila kitu kinafuata aina yake na kuabudu Bwana wa uumbaji. Mbingu na dunia ni shwari kabisa. Haya ni maisha matulivu ya binadamu. … Baada ya Mungu na mwanadamu kuingia rahani, Shetani hatakuweko tena, na kama Shetani, wale watu waovu pia hawatakuweko tena. Kabla ya Mungu na mwanadamu kuingia rahani, wale watu waovu waliomtesa Mungu wakati mmoja duniani na adui waliokuwa hawamtii duniani watakuwa tayari wameangamizwa; watakuwa wameangamizwa na majanga makubwa ya siku za mwisho. Baada ya hao watu waovu kuangamizwa kabisa, dunia haitajua tena unyanyasaji wa Shetani. Binadamu watapata wokovu kamili, na hapo tu ndipo kazi ya Mungu itaisha kabisa. Haya ndiyo masharti ya Mungu na mwanadamu kuingia rahani(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mungu na Mwanadamu Wataingia Rahani Pamoja).

Kupitia kusoma maneno ya Mwenyezi Mungu nilikuja kuelewa kwamba, ingawa katika siku za baadaye maisha yetu bado yako duniani, punde Mungu atamaliza hatua Yake ya mwisho ya kazi katika kuwaokoa wanadamu Shetani ataangamizwa, na maisha yetu duniani hayatasumbuliwa tena na Shetani, wala hatutakuwa na wasiwasi au kufanya kazi ya sulubu, wala kulia, wala kuhema kwa majonzi. Itakuwa tu kama wakati ambapo Adamu na Hawa waliishi katika Bustani ya Edeni. Tutakuwa huru kumwabudu Mungu, tukuishi maisha mazuri na yaliyobarikiwa ambapo Mungu yupo pamoja na mwanadamu. Hii ni hatima ya mwisho ya wanadamu, na hiki ndicho kitu cha mwisho ambacho Mungu atafanikisha katika kazi Yake katika siku za mwisho. Kweli ni kuu! Wakati uo huo nilishusha pumzi: “Ni nani angezungumza kwa njia wazi hivi kuhusu hatima ya mwisho ya wanadamu? Nani angepanga mwisho wa wanadamu? Mungu pekee angefanya hili!” Ndani ya neno la Mwenyezi Mungu nilitambua sauti ya Mungu, na kuona kwamba kazi ya Mwenyezi Mungu ni Mungu kuonekana kutekeleza kazi! Hatimaye nilikuwa nimeondoa dhana zilizokuwa akilini mwangu, na kwa furaha kukubali kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho, kurudi mbele ya kiti cha Mungu cha enzi.

Iliyotangulia: Nimerudi Nyumbani

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Nimeunganishwa Tena na Bwana

Mwenyezi Mungu anasema, “Kristo wa siku za mwisho huleta uzima, na huleta kudumu kwa njia ya kweli na ya milele. Ukweli huu ni njia ambayo...

Kufuata Nyayo za Mwanakondoo

“Kwa kuwa mwanadamu anamwamini Mungu, ni sharti afuate kwa ukaribu nyayo Zake, hatua kwa hatua; anapaswa ‘kumfuata Mwanakondoo popote...

Fumbo la Utatu Linafichuliwa

Na Jingmo, MalaysiaNilikuwa na bahati katika mwaka wa 1997 kukubali injili ya Bwana Yesu na nilipobatizwa, mchungaji aliomba na kunibatiza...

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp