Juu ya Hatima

Wakati wowote hatima inatajwa, muichukulie kwa uzito maalumu; nyinyi nyote ni mahususi hasa kuhusu jambo hili. Baadhi ya watu hawawezi kusubiri kumsujudia Mungu ili hatimaye kuwa na hatima nzuri. Naweza kutambua hamu yenu, ambayo haihitaji kuonyeshwa katika maneno. Kabisa hamtaki miili yenu ianguke katika maafa, na hata zaidi, hamtaki kushuka katika adhabu ya muda mrefu hapo baadaye. Mnatarajia tu kujiruhusu muishi kwa uhuru zaidi kidogo, kwa urahisi zaidi kidogo. Na hivyo unahisi mwenye wasiwasi hasa wakati wowote hatima inatajwa, ukiwa na hofu kubwa kwa undani kwamba, usipokuwa mwangalifu vya kutosha, unaweza kumkosea Mungu na hivyo upate adhabu unayostahili. Hamjasita kufanya maafikiano kwa ajili ya hatima zenu, na wengi wenu ambao wakati mmoja walikuwa wa kuzunguka na wapuuzi hata kwa ghafla wamegeuka hususa wapole na wa dhati; unyofu wenu hata una mzizimo. Pasipo kutilia maanani, nyinyi nyote mna mioyo “minyoofu”, na kutoka mwanzo hadi mwisho mmejifungua wazi Kwangu bila kuficha siri zozote katika mioyo yenu, yawe lawama, udanganyifu, au ibada. Kwa jumla, “mmekiri” kwa uwazi Kwangu yale mambo muhimu katika pahali pa siri yenye kina kwenu. Mambo kama yalivyo, Sijawahi kuepuka mambo kama haya, kwa sababu yamekuwa ya kawaida Kwangu. Afadhali muingie katika bahari la moto kwa hatima yenu ya mwisho kuliko kupoteza mlia mmoja wa nywele ili kupata kibali cha Mungu. Sio kwamba Ninakuwa wa kulazimishia imani kwenu; ni kwamba mioyo yenu ya ibada ni pungufu hasa kwa kukabiliana na kila kitu Ninachofanya. Hamuwezi kuelewa Ninachomaanisha, hivyo basi acheni Niwatolee maelezo rahisi: Mnachohitaji si ukweli na maisha; si kanuni za jinsi ya kutenda, na hasa siyo kazi Yangu yenye kujitahidi. Yote mnayohitaji ni yale ambayo mnamiliki katika mwili—mali, hadhi, familia, ndoa, nk. Ninyi mnatupilia mbali kabisa maneno na kazi Yangu, hivyo Naweza kujumlisha imani yako kwa neno moja: shingo upande. Mtafanya lolote ili kutimiza mambo ambayo bila shaka mmejitolea, lakini Nimegundua kwamba hampuuzi kila kitu kwa ajili ya mambo ya imani yenu katika Mungu. Badala yake, nyinyi ni waaminifu tu kiasi, na kiasi. Hiyo ndiyo sababu Nasema kwamba wale wanaokosa moyo wa usafi mkubwa ni washinde katika imani yao katika Mungu. Fikiria kwa uangalifu—je, kunao wengi washinde miongoni mwenu?

Mnapaswa kujua kwamba mafanikio katika kumwamini Mungu yanatimizwa kwa sababu ya matendo ya watu wenyewe; wakati watu hawafanikiwi lakini badala yake wanashindwa, hiyo pia ni kwa sababu ya matendo yao wenyewe, sio matokeo ya vipengele vingine. Ninaamini kwamba mngefanya kitu chochote kitachukua ili kupata kitu kufanyika ambacho ni kigumu zaidi na kinachohitaji mateso zaidi kuliko kumwamini Mungu, na kwamba mngekichukulia kwa makini sana. Hamngetaka hata kufanya makosa yoyote; hizi ni aina za juhudi zisizolegea ambazo nyote mmeweka katika maisha yenu wenyewe. Nyinyi hata mna uwezo wa kunidanganya Mimi katika mwili chini ya hali ambazo hamuwezi kudanganya yeyote wa familia yenu wenyewe. Hii ni tabia yenu thabiti na kanuni ambayo mnatumia katika maisha yenu. Je, si bado mnaendeleza picha ya uongo ili kunidanganya Mimi, kwa ajili ya hatima yenu, na kuwa na hatima nzuri na ya furaha? Nafahamu kwamba ibada yenu na unyofu wenu ni wa muda tu; je, matamanio yenu na gharama mnayolipa ni ya sasa tu na si ya baadaye? Mnataka tu kutumia nguvu moja ya mwisho ili kupata hatima nzuri. Azma yenu ni kubadilisha tu; siyo ili msiwe wenye deni kwa ukweli, na ni hasa msinilipe kwa ajili ya gharama Niliyolipa. Kwa neno, mko tu tayari kutumia ujanja wenu, lakini hamtaki kuipigania. Je, si haya ni matakwa yenu ya dhati? Sio lazima mjifiche, na hata zaidi, sio lazima mpige mbongo zenu juu ya hatima yenu hadi pale ambapo hamuwezi kula au kulala. Je, si ni kweli kwamba matokeo yenu yatakuwa yameamuliwa mwishowe? Mnapaswa kufanya wajibu wenu wenyewe kwa kadri ya uwezo wenu kwa mioyo iliyo wazi na wima, na muwe tayari kufanya chochote kitakachohitajika. Kama mlivyosema, wakati siku itakuja, Mungu hatakosa kumjali mtu yeyote ambaye aliteseka au kulipa gharama kwa ajili Yake. Aina hii ya imani ni yenye thamani kuishikilia, na hampaswi kuisahau kamwe. Ni tu kwa njia hii Ninaweza kutuliza akili Yangu kuwahusu. Vinginevyo, Sitakuwa na uwezo wa kutuliza akili Yangu kuwahusu, na milele mtakuwa malengo ya chuki Yangu. Kama nyote mnaweza kufuata dhamiri zenu na kutoa yote kwa ajili Yangu, msiwache jitihada zozote kwa ajili ya kazi Yangu, na kutenga maisha ya jitihada za kazi ya injili Yangu, basi si moyo Wangu mara kwa mara utaruka kwa furaha kwa ajili yenu? Si Mimi Nitakuwa na uwezo wa kutuliza akili Yangu kuwahusu? Ni aibu kwamba kile mnaweza kufanya ni cha kusikitisha sana na sehemu ndogo sana ya kile Ninachotarajia; hivi sasa, ni jinsi gani mna nyongo ya kutafuta kutoka Kwangu kile mnatumainia?

Hatima yenu na majaliwa yenu ni muhimu sana kwenu—ni za matatizo makubwa. Mnaamini kuwa msipofanya mambo kwa uangalifu sana, itakuwa sawa na kutokuwa na hatima, na uharibifu wa majaliwa yenu. Lakini mmewahi kufikiri kwamba kama juhudi mtu hutumia ni kwa ajili ya hatima zao tu, hizo ni kazi tu zisizo na matunda? Juhudi za aina hiyo si halisi—ni bandia na danganyifu. Kama ni hivyo, wale ambao wanafanya kazi kwa ajili ya hatima yao watapokea maangamizo yao ya mwisho, kwa sababu kushindwa katika imani ya watu katika Mungu hutendeka kwa sababu ya udanganyifu. Hapo awali Nilisema kuwa Mimi Sipendi kusifiwa mno au kupendekezwa, au kuchukuliwa kwa shauku. Ninapenda watu waaminifu kukubali hali ilivyo kuhusu ukweli na matarajio Yangu. Hata zaidi, Ninapenda wakati watu wanaweza kuonyesha uangalifu mkubwa na kufikiria kwa ajili ya moyo Wangu, na wakati wanaweza hata salimisha kila kitu kwa ajili Yangu. Ni kwa njia hii tu ndipo Moyo wangu unaweza kuliwazwa. Sasa hivi, ni mambo mangapi yapo yanayowahusu ambayo Mimi Nachukia? Ni mambo mangapi yapo yanayowahusu ambayo Napenda? Je, hakuna kati yenu ambaye ametambua ubaya wote ambao mmeonyesha kwa ajili ya hatima zenu?

Katika moyo Wangu, Sitaki kuwa Mwenye kudhuru moyo wowote ambao ni chanya na wa motisha, na Mimi hasa Sitaki kupunguza bidii ya mtu yeyote ambaye anafanya wajibu wake kwa uaminifu; hata hivyo, ni lazima Niwakumbushe kila mmoja wenu juu ya upungufu wenu na roho chafu sana ndani ya mioyo yenu. Azma ya kufanya hivyo ni kutarajia kwamba mtaweza kutoa mioyo yenu ya kweli katika kukabiliana na maneno Yangu, kwa sababu kile Nachukia zaidi ni udanganyifu wa watu kuelekezwa Kwangu. Natarajia tu kuwa katika hatua ya mwisho ya kazi Yangu, mnaweza kutekeleza kwa kujitokeza, kujitoa kikamilifu, na wala sio shingo upande tena. Bila shaka, Natarajia pia kuwa nyote muwe na hatima nzuri. Hata hivyo, bado Nina mahitaji Yangu ambayo ni kwenu nyinyi mfanye uamuzi bora kabisa katika kujitoa Kwangu pekee na moyo wa ibada ya mwisho. Kama mtu hana moyo huo wa ibada pekee, mtu huyo hakika atakwenda kuwa thamani ya Shetani, na Mimi Sitaendelea kumtumia. Nitamtuma nyumbani akatunzwe na wazazi wake. Kazi yangu imekuwa ya msaada sana kwa ajili yenu; kile Natarajia kupata kutoka kwenu ni moyo ulio mwaminifu na unaotia msukumo kwenda juu, lakini hadi sasa mikono Yangu bado ni tupu. Fikiria kulihusu: Wakati siku moja bado Nitakuwa na kukwazika kusikoelezeka, mtazamo Wangu kuwaelekea utakuwa upi? Je, Mimi bado Nitakuwa mwema? Je, Moyo wangu utakuwa bado mtulivu? Je, mnaelewa hisia za mtu ambaye kwa kujitahidi amelima lakini hakuvuna hata nafaka moja? Je, mnaelewa ukubwa wa jeraha la mtu ambaye amepigwa kipigo kikubwa? Je, mnaweza kuonja uchungu wa mtu aliyejawa na matumaini ambaye anafaa kuachana na mtu kwa uhusiano mbaya? Je, mmeona hasira ya mtu ambaye amekasirishwa? Je, mnaweza kujua hisia ya kulipiza kisasi kwa haraka ya mtu ambaye amekuwa akichukuliwa kwa uadui na udanganyifu? Kama mnaelewa fikira za watu hawa, Nadhani haipaswi kuwa vigumu kwenu kuwaza mtazamo Mungu Atakuwa nao wakati ule wa adhabu Yake. Hatimaye, Natarajia nyote mnaweka jitihada kali kwa ajili ya hatima yenu wenyewe; hata hivyo, ni bora msitumie njia za udanganyifu katika juhudi zenu, au bado Nitasikitishwa nanyi katika moyo Wangu. Je, kusikitishwa kwa aina hii huelekea wapi? Je, hamjidanganyi wenyewe? Wale ambao hufikiria kuhusu hatima yao na bado wanaiharibu ni watu wenye uwezekano mdogo zaidi wa kuokolewa. Hata kama watu hawa watakerwa, ni nani atawahurumia? Kwa jumla, bado Niko tayari Kuwatakia muwe na hatima inayofaa na nzuri. Hata zaidi, Natarajia kwamba hakuna kati yenu atakayeanguka katika maafa.

Iliyotangulia: Wewe U Mwaminifu kwa Nani?

Inayofuata: Maonyo Matatu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp