Kuhusu Kila Mmoja Kutekeleza Wajibu Wake

Katika mkondo wa sasa, kila mtu anayempenda Mungu kwa kweli ana fursa ya kukamilishwa na Yeye. Bila kujali kama yeye ni kijana au mzee, mradi tu anatazamia kwa hamu kumtii Mungu na kumheshimu Yeye, wataweza kukamilishwa na Yeye. Mungu huwakamilisha watu kulingana na kazi zao tofauti. Mradi tu umefanya yote kwa nguvu yako na kuitii kazi ya Mungu utakuwa na uwezo wa kukamilishwa na Yeye. Kwa sasa hakuna hata mmoja wenu aliye mkamilifu. Wakati mwingine mnaweza kutekeleza aina moja ya kazi na wakati mwingine mnaweza kutekeleza mbili; mradi tu mnatoa nguvu zenu zote kujitumia kwa ajili ya Mungu, hatimaye mtafanywa wakamilifu na Mungu.

Vijana wana falsafa chache za maisha, na hawana hekima na ufahamu. Mungu amekuja hapa kukamilisha hekima na ufahamu wa mwanadamu, na neno la Mungu huyafidia mambo haya ambayo hawana. Hata hivyo, tabia za vijana si thabiti na hii inahitaji mbadiliko na Mungu. Vijana wana mawazo machache ya kidini na falsafa chache za maisha Wanafikiri kwa maneno rahisi, na fikira zao sio ngumu kufahamika. Hiki ni kipengele ambacho ubinadamu wao bado haujachukua umbo na ni kipengele cha kupendeza, lakini vijana hawajui na hawana hekima, na hii ni sehemu ambayo inahitaji kukamilishwa na Mungu. Kupitia kukamilishwa na Mungu, mnaweza kukuza utambuzi na kuweza kuelewa mambo mengi ya kiroho, na hatua kwa hatua mgeuke kuwa watu wanaostahili kutumiwa na Mungu. Ndugu na dada wakubwa pia wanaweza kutekeleza kazi fulani na hawajaachwa na Mungu. Na ndugu na dada wakubwa, wao pia wana mambo yanayofaa na baadhi ya mambo yasiyofaa. Ndugu na dada wakubwa wana falsafa zaidi za maisha, wana mawazo zaidi ya kidini, vitendo vyao vimekwama katika mfumo usiopindika, hufuata sheria kama roboti, wao huvitumia bila kufikiri, na hawawezi kubadilika. Hiki sicho kipengele kinachofaa. Hata hivyo, ndugu na dada wakubwa ni watulivu na wenye kijidhibiti nafsi kuelekea chochote kinachojitokeza; tabia zao ni imara, na hawana hisia kali zisizoweza kutabiriwa. Wanaweza kuwa wapole katika kukubali mambo, lakini hii siyo kasoro kubwa. Mradi mnaweza kutii; mradi mnaweza kuyakubali maneno ya sasa ya Mungu, ikiwa hamchunguzi maneno ya Mungu, ikiwa hamsiti kutii na kufuata, ikiwa hakika hutoi hukumu au kuwa na mawazo mengine mabaya, na ikiwa mnakubali maneno Yake na kuyaweka katika matendo—ikiwa mnakidhi hali hizi—mtaweza kukamilishwa.

Bila kujali kama ninyi ni ndugu au dada wadogo au wakubwa, mnajua kazi mnayopaswa kutekeleza. Wale walio katika ujana wao sio wenye kiburi; wale walio wakubwa zaidi sio wasioonyesha hisia na hawarudi nyuma. Nao wanaweza kutumia nguvu za kila mmoja kufidia upungufu wao, na wanaweza kuhudumiana bila ubaguzi wowote. Daraja la urafiki linajengwa kati ya ndugu na dada wadogo na wakubwa. Kwa sababu ya upendo wa Mungu mnaweza kuelewana vizuri zaidi. Ndugu wadogo hawawadharau ndugu wakubwa, na ndugu wakubwa sio wa kujidai. Je! Huu si ushirikiano patanifu? Ikiwa ninyi nyote mna uamuzi huu, basi mapenzi ya Mungu hakika yatatimizwa katika kizazi chenu.

Katika siku zijazo, ikiwa wewe unabarikiwa au kulaaniwa kutaamuliwa kulingana na matendo unayotekeleza leo. Ikiwa unafaa kukamilishwa na Mungu itakuwa ni sasa hivi katika enzi hii; hakutakuwa na fursa nyingine katika siku zijazo. Mungu kwa kweli Anataka kukukamilisha sasa, na hii sio njia ya kuzungumza. Katika siku zijazo, bila kujali majaribio gani yanayokufikia, matukio gani yanayofanyika, au maafa gani yanayokupata, Mungu anataka kukukamilisha—huu ni ukweli wa hakika na usio na shaka. Je, jambo hili inaweza kuonekana kutoka wapi? Kutokana na ukweli kwamba neno la Mungu katika enzi zote na vizazi halijawahi kufikia kiwango kikubwa kama lilivyo leo—limeingia katika ulimwengu wa juu, na kazi ya Roho Mtakatifu miongoni mwa wanadamu leo ni ya kipekee. Ni wachache sana kutoka vizazi vilivyopita wameonja hili. Hata katika enzi ya Yesu hapakuwa na ufunuo wa leo; viwango vikubwa vimefikiwa katika maneno yaliyosemwa kwenu, mambo mnayoyaelewa, na mambo mnayoyapitia. Hamuondoki katikati ya majaribu na kuadibiwa, na hii ni inatosha kuthibitisha kwamba kazi ya Mungu imefikia uzuri ambao haujawahi kutokea. Hiki si kitu ambacho mwanadamu anaweza kufanya na sio kitu ambacho mwanadamu anadumisha, lakini badala yake ni kazi ya Mungu Mwenyewe. Kwa hivyo, kutokana na ukweli mwingi wa kazi ya Mungu inaweza kuonekana kwamba Mungu anataka kumkamilisha mwanadamu, na Yeye hakika Anaweza kukufanya uwe mkamilifu. Ikiwa mnaweza kuona jambo hili, ikiwa unaweza kupata ugunduzi huu mpya, basi hutangoja kuja kwa pili kwa Yesu lakini badala yake, utamruhusu Mungu akufanye mkamilifu katika enzi ya sasa. Hivyo, kila mmoja wenu anapaswa kufanya kila linalowezekana na kujitahidi sana ili aweze kukamilishwa na Mungu.

Siku hizi hupaswi kuzingatia mambo hasi. Lazima kwanza uweke kando na kutojali kila kitu ambacho kinaweza kukufanya usihisi hasi. Unaposhughulikia mambo lazima udumishe moyo wa kutafuta na kupapasa papasa, na lazima udumishe moyo wa utii kwa Mungu. Wakati wowote mnapogundua udhaifu wowote ndani yenu, lakini hamko chini ya udhibiti wake na mnatenda kazi ambayo mnapaswa kutenda, hii ni hatua ya hakika kwenda mbele. Kwa mfano: Ndugu wana mawazo ya kidini, lakini unaweza kuomba, na unaweza kutii, kula na kunywa neno la Mungu, na kuimba nyimbo.... Kwa neno moja, chochote unachoweza kufanya, kazi yoyote unayoweza kutenda, jitolee kikamilifu kwa nguvu zote unazoweza kuzitumia. Usisubiri kwa kukaa tu. Kuweza kutimiza wajibu wako kwa ridhaa ya Mungu ni hatua ya kwanza. Kisha unapoweza kuuelewa ukweli na kuingia katika ukweli wa neno la Mungu, utakuwa umekamilishwa na Mungu.

Iliyotangulia: Kujadili Maisha ya Kanisa na Maisha Halisi

Inayofuata: Kuhusu Mungu Kumtumia Mwanadamu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp