Sura ya 119

Ni lazima nyote muelewe nia Zangu, nyote mnapaswa kuelewa hali Yangu ya moyo. Sasa ni wakati wa kujiandaa kurudi Sayuni, sina mawazo ya lolote isipokuwa hili. Mimi Ninatumaini tu kwamba Ninaweza kukutana nanyi siku moja hivi karibuni, na kutumia kila dakika na kila sekunde pamoja nanyi katika Sayuni. Mimi Naichukia kabisa dunia, Nauchukia kabisa mwili, na Mimi Namchukia kabisa hata zaidi kila binadamu duniani; Sina nia ya kuwaona, kwa sababu wote ni kama mapepo, bila hata chembe ya asili ya binadamu; Sina nia ya kuishi duniani, Mimi Nawachukia kabisa viumbe wote, Mimi Nawachukia kabisa wote ambao ni wa mwili na damu. Nchi yote inavunda maiti; Mimi Nataka kurudi Sayuni mara moja, ili kuiondoa harufu yote mbaya ya maiti kutoka dunia, na kufanya dunia yote ijae sifa kwa ajili Yangu. Mimi Nitarejea Sayuni, Mimi Nitajiondoa kutoka kwa mwili na ulimwengu, hakuna yeyote anayepaswa kuweka kizuizi mbele Yangu; Mkono wangu ambao huua mwanadamu hauna hata chembe ya hisia! Kuanzia sasa na kuendelea, hakuna yeyote anayepaswa kunena juu ya ujenzi wa kanisa, vinginevyo Mimi sitamsamehe. (Hii ni kwa sababu sasa ni wakati wa kushuhudia wanangu wa kiume wazaliwa wa kwanza, wakati wa kujenga ufalme; yeyote anenaye juu ya ujenzi wa kanisa anaubomoa ujenzi wa ufalme na kuukatiza usimamizi Wangu.) Lote liko tayari, lote limetayarishwa, lote libakilo ni kwa wana wazaliwa wa kiume wa kwanza kutukuzwa, kushuhudiwa, na wakati hayo yanapofanyika Mimi, bila kuchelewa kwa muda na bila kuzingatia mtindo, lazima Nirudi Sayuni mara moja—mahali mnapashikilia mawazoni mwenu usiku na mchana. Msiangalie tu jinsi dunia ilivyo laini na thabiti sasa; lakini kazi hii yote ni kuhusu hali ya kurudi Sayuni; msijali kuhusu mambo hayo sasa, na wakati siku ya kurudi Sayuni inapowadia yote yatakuwa kamili. Ni nani asiyetaka kurudi Sayuni hivi punde? Ni nani asiyetaka Baba na wana wa kiume kupatana hivi karibuni? Bila kujali jinsi anasa za duniani zinavyofurahisha, haziwezi kuweka mshiko juu ya miili yetu; tutavuka mipaka ya miili yetu na kwa pamoja kurudi Sayuni. Ni nani huthubutu kuzuia? Ni nani huthubutu kuweka vikwazo? Mimi bila ya shaka Sitamsamehe! Mimi Nitaviondoa vikwazo vyote. (Sababu Ninasema siwezi kurejea Sayuni mara moja ni kwa sababu ya hili. Mimi Natekeleza kazi hii ya utakasaji sawia na Ninavyoshuhudia wanangu wazaliwa wa kiume wa kwanza; kazi hizi mbili zinaendelea kwa wakati mmoja. Kazi ya utakasaji inapokamilika, utakuwa ni wakati wa Mimi kuwafichua wana wa kiume wazaliwa wa kwanza. Vikwazo ambavyo Nimezungumzia vinarejelea idadi kubwa ya watenda huduma, hivyo Ninasema kwamba kazi hizi mbili zinafanyika sawia.) Nitawafanya wanangu wa kiume wazaliwa wa kwanza wazunguke pamoja na Mimi kote ulimwenguni na kufika miisho ya dunia, kuvuka milima na mito na vitu vyote; ni nani huthubutu kukwamisha? Ni nani huthubutu kuzuia? Mkono Wangu haumuachilii kwa urahisi mtu yeyote; mbali na wanangu wa kiume wazaliwa wa kwanza, Mimi hughadhibika dhidi ya na kuwalaani wote. Kuvuka nchi nzima hakuna mwenye kufa hata mmoja ambaye hupata baraka Zangu; wote hukumbana na laana Yangu. Tangu mwanzo wa uumbaji wa dunia, Mimi Sijambariki yeyote; hata wakati Mimi Nimepeana baraka imekuwa maneno tu, haijawahi kamwe kuwa uhalisi, kwa sababu Mimi Ninamchukia Shetani kwa hali ya juu, na Mimi Sitawahi kamwe kumbariki, ila kumwadhibu tu. Ni mwishowe tu, baada ya Mimi kumshinda Shetani kikamilifu, baada ya ushindi kamili kuwa Wangu, Nitakapowapa baraka za yakinifu wahudumu wote waaminifu, Niwaache wanisifu Mimi kama starehe, kwa sababu kazi Yangu itakuwa imekamilika.

Kwa kweli muda Wangu hautakuwa mrefu zaidi, mpango wa usimamizi wa miaka elfu sita unafikia ukamilisho mbele ya macho yako. (Hakika ni mbele ya macho yako; siyo kuonyesha kabla, unaweza kuona kutoka kwa hali Yangu ya moyo.) Mimi Nitawachukua wanangu wa kiume wazaliwa wa kwanza mara moja hadi nyumbani Sayuni. Baadhi ya watu watasema, “Kwa kuwa ni kwa ajili ya wazaliwa wa kwanza tu, kwa nini Utumie miaka elfu sita yenye thamani ya wakati? Na kwa nini Ufanye watu wengi?” Nimesema kabla kuwa kila kitu Changu ni cha thamani. Ni jinsi gani wanangu wa kiume wazaliwa wa kwanza wasiwe hivyo hata zaidi? Mimi Nitawahamasisha wote kunitumikia Mimi, na zaidi ya hayo, Mimi Nitafichua nguvu Yangu, ili kila mtu aweze kuona kwamba katika ulimwengu dunia wote hakuna kitu hata kimoja ambacho hakimo mikononi mwetu, hakuna mtu hata mmoja ambaye hayuko katika huduma Yetu, na hakuna ufanikishaji hata mmoja ambao haujatekelezwa kwa ajili yetu. Mimi nitafanikisha kila kitu. Kwangu Mimi hakuna wazo la muda; ingawa Mimi nadhamiria kuukamilisha mpango na kuikamilisha kazi Yangu kwa miaka elfu sita, kwangu Mimi yote yamekombolewa na huru. Hata kama ni chini ya miaka elfu sita, mradi kwa maoni Yangu wakati umefika, ni nani angethubutu kutamka neno la upinzani? Ni nani angethubutu kusimama na kuhukumu apendavyo? Kazi Yangu, Mimi hufanya Mwenyewe; Muda wangu, Mimi hupanga Mwenyewe. Hakuna mtu, hakuna jambo, hakuna kitu huthubutu kutenda kimakusudi; Mimi nitavifanya vyote vinifuate. Kwangu Mimi hakuna jema au bovu; Mimi Nikisema ni jema, ni jema kabisa; Mimi Nikisema ni bovu, hilo ni kweli pia. Hupaswi daima kutumia dhana za binadamu kunipima Mimi! Mimi Ninasema wana wa kiume wazaliwa wa kwanza pamoja na Mimi tumebarikiwa—ni nani huthubutu kukataa kunyenyekea? Mimi Nitakuangamiza papo hapo! Wakataa kunyenyekea! Wewe ni muasi! Mimi sina huruma kabisa kwa ajili ya wanadamu wote, Mimi nimewachukia kwa kiasi fulani; Mimi siwezi kabisa kuwa mvumilivu zaidi. Kulingana na Mimi, ulimwengu dunia wote ni lazima uangamizwe mara moja, ni hapo tu ndipo kazi Yangu kubwa itakapokamilishwa, ni hapo tu ndipo usimamizi wa mpango Wangu wa usimamizi utakapokamilishwa, ni hapo tu ndipo chuki iliyo moyoni Mwangu itakapoondoka. Sasa Mimi Ninajali tu kuhusu kushuhudia wanangu wa kiume wazaliwa wa kwanza, masuala mengine yote Mimi Nitayaweka kando na kutojali kwa sasa; kwanza fanya jambo lililo kuu, kisha fanya jambo la kufuata. Hizi ndizo hatua za kazi Yangu, hakuna yeyote anayepaswa kuenda kinyume na hili, wote lazima wafuate Ninayosema Mimi, ili wasiwe malengo ya laana Yangu.

Sasa kazi yangu imekamilishwa, Mimi Ninaweza kupumzika. Kuanzia sasa na kuendelea, Mimi Sitafanya kazi tena, Mimi Nitawaambia wanangu wa kiume wazaliwa wa kwanza wafanye yote ambayo Mimi Ninataka yafanywe kwa ajili Yangu, kwa sababu wanangu wa kiume wazaliwa wa kwanza ni Mimi, wanangu wa kiume wazaliwa wa kwanza ni nafsi Yangu; hivi si vibaya hata kidogo; msifuate dhana na kuhukumu. Kuwaona wana wa kiume wazaliwa wa kwanza ni kuniona Mimi, kwa sababu sisi ni kitu kimoja; yeyote ambaye hututenganisha sisi kwa hivyo ananipinga Mimi, na Mimi sitamsamehe. Kwa maneno Yangu, kuna mafumbo yasiyoeleweka kwa mwanadamu. Wale tu Ninaowapenda Mimi wanaoweza kunionyesha Mimi, na hakuna wengine wanaoweza kulifanya; hili huamuliwa na Mimi, na hakuna anayeweza kulibadilisha. Maneno Yangu ni ya thamani, maneno Yangu ni yenye maarifa na ya kina kirefu. Wote ni lazima watumie juhudi kubwa kwa maneno Yangu, jaribuni kuyatafakari maneno Yangu mara kwa mara, msikose neno hata moja au sentensi, vinginevyo watachukua maana yenye makosa, na kutoyaelewa maneno Yangu. Mimi Nimesema tabia Yangu haivumilii kosa, ikimaanisha kuwa wanangu wa kiume wazaliwa wa kwanza walioshuhudiwa hawawezi kupingwa. Wanangu wa kiume wazaliwa wa kwanza huwakilisha kila kipengele cha tabia Yangu, kwa hivyo tarumbeta takatifu inapopigwa, hapo ndipo Mimi Ninapoanza kuwashuhudia wana wa kiume wazaliwa wa kwanza; na hivyo baadaye tarumbeta takatifu itakuja baadaye kuwa tangazo taratibu la tabia Yangu kwa halaiki. Kwa maneno mengine, wakati wana wa kiume wazaliwa wa kwanza wanapofichuliwa, huo ndio utakuwa wakati ampapo tabia Yangu inafichuliwa. Ni nani anayeweza kulielewa hili? Mimi nasema hayo hata katika mafumbo niliyoyafichua Mimi, hapo yanabaki mafumbo ambayo watu hawawezi kufumbua. Ni nani kati yenu ambaye kwa kweli amejaribu kuelewa maana ya kweli ya maneno haya? Tabia Yangu ni nafsi ya mtu kama vile ambavyo mmefikiria? Ni kosa la kijinga lililoje! Leo yeyote ambaye huona wanangu wa kiume wazaliwa wa kwanza ni kitu cha baraka na huona tabia Yangu, hili ni kweli kabisa. Wanangu wazaliwa wa kwanza huniwakilisha Mimi mzima, bila shaka yoyote ni nafsi Yangu. Hakuna yeyote anayepaswa kutilia hili shaka! Walio watiifu wanabarikiwa na neema, na waasi wanalaaniwa. Hili ndilo Ninaloamrisha Mimi, na hakuna yeyote anayeweza kulibadilisha!

Iliyotangulia: Sura ya 118

Inayofuata: Sura ya 120

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp