Furahini, Enyi Watu Wote!

Katika nuru Yangu, watu wanaiona nuru tena. Katika neno Langu, watu wanapata mambo ambayo wanafurahia. Nimekuja kutoka Mashariki, Ninatoka Mashariki. Utukufu Wangu unapoangaza, mataifa yote yanatiwa nuru, vitu vyote vinaletwa kwenye mwanga, hakuna kitu hata kimoja kinachobaki gizani. Katika ufalme, maisha ambayo watu wa Mungu wanaishi pamoja na Mungu ni yenye furaha kupita kiasi. Maji yanacheza kwa furaha katika maisha ya watu yenye baraka, milima inafurahia pamoja na watu katika wingi Wangu. Wanadamu wote wanajitahidi, wakifanya bidii, wakionyesha uaminifu wao katika ufalme Wangu. Katika ufalme, uasi haupo tena, upinzani haupo tena; mbingu na dunia zinategemeana, Mimi na mwanadamu tunakaribiana katika hisia ya kina, katika furaha kuu tamu ya maisha, tukiegemeana…. Wakati huu, Ninayaanza rasmi maisha Yangu mbinguni. Usumbufu wa Shetani haupo tena, na watu wanaingia katika pumziko. Ulimwenguni kote, watu Wangu wateule wanaishi ndani ya utukufu Wangu, wakiwa wamebarikiwa sana, si kama watu wanaoishi kati ya watu, lakini kama watu wanaoishi na Mungu. Binadamu wote wamepitia upotovu wa Shetani, na kuishi maisha ya mateso makubwa. Sasa, mtu anawezaje kutofurahia akiishi katika nuru Yangu? Mtu anawezaje kuuachilia wakati huu mzuri umponyoke? Enyi watu! Imbeni wimbo ulio mioyoni mwenu na mnichezee kwa furaha! Iinueni na mnitolee mioyo yenu ya dhati! Pigeni ngoma zenu na mnichezee kwa furaha! Ninaangaza furaha Yangu ulimwenguni kote! Naufichua uso Wangu mtukufu kwa watu! Nitaita kwa sauti kubwa! Nitaupita ulimwengu wote! Tayari Ninatawala kati ya watu! Ninatukuzwa na watu! Ninapeperuka kwenye mbingu zenye rangi ya samawati na watu wanakwenda wakitembea pamoja nami. Ninatembea kati ya watu na watu Wangu wananizunguka! Mioyo ya watu ni yenye furaha, nyimbo zao zinautikisa ulimwengu, zikiipasua mbingu! Ulimwengu haujafunikwa kwa ukungu tena; hakuna matope tena, hakuna mkusanyiko wa maji machafu tena. Watu watakatifu wa ulimwengu! Mnaonyesha nyuso zenu za kweli chini ya ukaguzi Wangu. Ninyi sio watu mliofunikwa na uchafu, lakini ni watakatifu walio safi kama jiwe la thamani lenye rangi ya kijani kibichi, ninyi nyote ni wapendwa Wangu, ninyi nyote ni furaha Yangu! Vitu vyote vinafufuka! Watakatifu wote wamerejea ili kunitumikia mbinguni, wakiingia katika kumbatio Langu lililo changamfu, hawalii tena, hawana wasiwasi tena, wakijitoa Kwangu, wakirudi nyumbani Kwangu, nao watanipenda bila kukoma katika nchi yao! Wasibadilike kamwe milele! Huzuni iko wapi! Machozi yako wapi! Mwili uko wapi! Dunia inapita, lakini mbingu ni za milele. Ninawaonekania watu wote, na watu wote wananisifu. Maisha haya, uzuri huu, tangu zama za kale hadi mwisho wa dahari, havitabadilika. Haya ndiyo maisha ya ufalme.

Iliyotangulia: Sura ya 25

Inayofuata: Sura ya 26

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp