182 Watakatifu Ni Washindi

1

Kristo wa siku za mwisho anaonyesha ukweli, Akihukumu na kuwatakasa binadamu.

Tumesikia sauti ya Mungu na tukarudi mbele Yake.

Maneno ya Mungu yanaonyesha uweza Wake, yakituamsha na kutushinda.

Bila kujali vurugu, vizuizi, au mashambulio ya nguvu za uovu za Shetani,

tumeamua kuwa Kristo ndiye ukweli na uzima, tunamfuata Mungu kwa uthabiti!

2

Katika pango la giza la pepo, mioyo yetu na miili yetu inateswa, damu na machozi yanatiririka.

Wakati wa mapambano ya kufa kupona, tunamwita Mungu, na maneno ya Mungu yanatuongoza kupitia shida zetu.

Ninapoona jinsi nguvu ya uzima wa Mungu ulivyo mkuu na wa ajabu, nampenda kwa uthabiti zaidi.

Tunaweza kutoa maisha yetu kuwa waaminifu kwa Mungu, na kamwe kutokubali kushindwa na Shetani kama Yuda.

Kupata majaribio na usafishaji, tunatoa ushuhuda mzuri na mkuu sana kwa Mungu.

3

Mungu amefanyiza kundi la washindi, Amemshinda Shetani na kupata utukufu kamili.

Kazi kubwa ya Mungu imekamilika, na Anaanza kushusha maafa na kuharibu joka kubwa jekundu.

Mungu mwenye haki hulipa wema na kuwaadhibu waovu, tabia Yake imefunuliwa kabisa.

Watakatifu wameshinda, ufalme wa Kristo umekuja ulimwenguni, na ukweli unashikilia utawala.

Tunasifu haki ya Mungu na uweza Wake. Sifa yetu kwa jina takatifu la Mwenyezi Mungu ni ya milele!

Iliyotangulia: 181 Nimeamua Mumfuata Mungu

Inayofuata: 183 Ninatamani Kuona Siku ya Utukufu wa Mungu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp