205 Pingu

1

Najali sana hadhi yangu katika mioyo ya wengine.

Napenda kuheshimiwa na wengine na nafurahia kuonwa mkuu.

Nastahimili aibu na nafanya kazi kwa bidii kujiendeleza mbele na kuwatawala wengine.

Na hili limekuwa pingu zangu, zikinifunga kila wakati.

2

Nimemwamini Mungu kwa miaka mingi lakini bado natafuta kuwatala wengine na napenda kujionyesha.

Niliyejaa majivuno, nahubiri nadharia za kiroho kuwatega na kuwadanganya wengine.

Mnafiki sana, niliikosea tabia ya Mungu zamani na Mungu alinichukia na kunikataa.

Nilianguka gizani na kuonja kwa kina uchungu wa kufungwa na umaarufu na utajiri.

3

Maneno ya Mungu huuchoma moyo wangu kama upanga wenye makali kuwili,

yakiweka asili yangu wazi na kufunua ubaya katika roho yangu.

Naona kuwa kiburi na kujidai, na tamaa ya mamlaka, imekuwa asili yangu.

Kung’ang’ania nafasi kwa njia yoyote iwezekanayo, nilipoteza dhamiri na mantiki yangu.

4

Kristo ni mkuu na mheshimiwa, lakini Yeye ni mnyenyekevu na kamwe hajidai.

Mimi ni mavumbi, duni na nisiye muhimu, na bado najistahi na mwenye kujidai.

Kujua kwamba tabia ya Mungu ni ya haki, takatifu na ya kupendeka, sina popote pa kuficha aibu yangu.

Nahisi kwa kina jinsi nilivyo mpotovu, na sifanani kabisa na mwanadamu.

5

Nikipitia hukumu ya maneno ya Mungu, naanguka mbele za Mungu.

Nimekusudia kufuatilia ukweli, kuwa mtu mpya na kuufariji moyo wa Mungu.

Kwa kuunyima mwili wangu na kutenda ukweli, tabia yangu ya kishetani inasafishwa.

Hukumu na kuadibu kwa Mungu vimeniokoa, namshukuru na kumsifu Mungu!

Iliyotangulia: 204 Kuzinduka kwa Barakala

Inayofuata: 206 Sitawahi Tena Kujitenga na Mungu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp