Mafanikio au Kushindwa Kunategemea Njia Ambayo Mwanadamu Hutembea

Watu wengi wanamwamini Mungu kwa ajili ya hatima yao ya baadaye au kwa ajili ya starehe ya muda mfupi. Kwa wale ambao hawajapitia ushughulikiaji wowote, imani kwa Mungu ni kwa ajili ya kuingia mbinguni, ili kupata tuzo. Sio ili kufanywa wawe na ukamilifu, au kutekeleza wajibu wa kiumbe wa Mungu. Ambayo ni kusema kwamba watu wengi hawamwamini Mungu ili watimize majukumu yao, au kukamilisha wajibu wao. Mara chache watu humwamini Mungu ili waishi maisha ya maana, wala hamna wale ambao wanaamini kwamba kwa kuwa mwanadamu yu hai, anapaswa ampende Mungu kwa kuwa ni sheria ya Mbinguni na kanuni ya dunia kufanya hivyo, na ni wito wa asili wa mwanadamu. Kwa njia hii, ingawa watu tofauti kila mmoja hufuatilia malengo yao binafsi, lengo la harakati zao na motisha yao yote ni sawa, na, zaidi ya hayo, kwa wengi wao, malengo yao ya ibada kwa kiasi kikubwa ni sawa. Katika kipindi cha elfu kadhaa za miaka iliyopita, waumini wengi wamekufa, na wengi wamekufa na kuzaliwa tena. Sio mtu mmoja au wawili ambao humtafuta Mungu, wala hata watu elfu moja au mbili, ilhali harakati ya wengi wa watu hawa ni kwa ajili ya matarajio yao wenyewe ama matumaini yao tukufu ya siku zijazo. Wale ambao ni waaminifu kwa Kristo ni wachache na nadra. Waumini wengi wanaomcha Mungu bado wamekufa wakiwa wametegwa na nyavu zao wenyewe, na zaidi ya hayo, idadi ya watu ambao wamekuwa washindi, ni ndogo mno. Hadi siku ya leo, sababu za watu kushindwa, au siri ya ushindi wao, bado haijulikani kwao. Wale ambao wamejawa na hamu ya kumtafuta Kristo bado hawajapata wakati wao wa ufahamu wa ghafla, hawajafikia kina cha mafumbo haya, kwa sababu hawajui. Ingawa wao wanafanya juhudi za mchwa katika harakati zao, njia ambayo wanatembelea ni njia ya kushindwa ambayo ilitembelewa na watangulizi wao, na si njia ya mafanikio. Kwa njia hii, bila kujali jinsi wanavyotafuta, je, si wao wanatembea katika njia ambayo inaelekea gizani? Je, si wanachopata ni matunda machungu? Ni vigumu vya kutosha kutabiri ikiwa watu ambao huiga wale waliofaulu katika nyakati za zamani hatimaye watapata utajiri au msiba. Uwezekano ni mbaya kiasi gani, basi, kwa watu ambao hutafuta kwa kufuata nyayo za wale ambao hawakufaulu? Je, si wao wana uwezekano mkubwa zaidi wa kutofaulu? Ni thamani gani iliyoko katika njia wanayoipitia? Je, wao si wanapoteza wakati wao? Bila kujali iwapo mtu hufaulu ama hufeli katika harakati yake, kuna, kwa kifupi, sababu kwa nini wao wanafanya hivyo, na si kweli kuwa kufaulu kwao ama kushindwa kwao kunaamuliwa na kutafuta vyovyote watakavyo.

Mahitaji ya msingi ya imani ya mtu kwa Mungu ni kuwa ni sharti awe na moyo mwaminifu, na kwamba ajitolee mwenyewe, na kutii kwa kweli. Kile kigumu sana kwa mwanadamu ni kupeana mwili wake ili abadilishe na imani ya kweli, ambapo kupitia hii anaweza kupata ukweli mzima, na kutimiza wajibu wake kama kiumbe wa Mungu. Hili haliwezi kupatikana na wale ambao wanafeli, na halipatikani hata zaidi na wale ambao hawawezi kumpata Yesu. Kwa sababu mwanadamu si hodari kwa kujitolea mwenyewe kwa Mungu kabisa, kwa sababu mwanadamu hayuko tayari kutekeleza wajibu wake kwa Muumba, kwa sababu mwanadamu ameona ukweli lakini anauepuka na kutembea katika njia yake mwenyewe, kwa sababu mwanadamu daima anatafuta kwa kufuata njia ya wale walioshindwa, kwa sababu mwanadamu daima anaasi Mbingu, hivyo, mwanadamu daima hushindwa, huchukuliwa na hila za Shetani, na anakamatwa kwa hila na wavu wake. Kwa sababu mwanadamu hamjui Kristo, kwa sababu mwanadamu hana ustadi katika kuelewa na kushuhudia ukweli, kwa sababu mwanadamu ni wa kuabudu Paulo sana na mwenye tamaa nyingi ya mbinguni, kwa sababu mwanadamu daima anadai kuwa Kristo awe akimtii yeye na kuagiza kuhusu Mungu, hivyo mashujaa hao wakuu na wale ambao wamepitia mabadiliko mabaya ya dunia bado wamo na ubinaadamu, na bado hufa kwa kuadibu kwa Mungu. Yote Ninayoweza kusema kuhusu watu kama hawa ni kuwa wanakufa kifo cha kutisha, na athari yao—kifo chao—si bila haki. Je, si kushindwa kwao hakuvumiliki hata zaidi kwa sheria ya Mbinguni? Ukweli unatoka katika ulimwengu wa mwanadamu, na bado ukweli katika mwanadamu unapitishwa na Kristo. Unaanzia kwa Kristo, yaani, kutoka kwa Mungu mwenyewe, na hiki si kitu ambacho mwanadamu anaweza kufanya. Ilhali Kristo hutoa ukweli tu; Yeye haji kuamua ikiwa mwanadamu atafanikiwa katika harakati yake ya kufuata ukweli. Hivyo, kinachofuata ni kuwa mafanikio au kushindwa kwa kweli yote yanategemea harakati ya mwanadamu. Mafanikio au kushindwa kwa mwanadamu kwa kweli kamwe hakuna uhusiano na Kristo, lakini kwa mbadala kunategemea harakati yake. Hatima ya mwanadamu na mafanikio yake ama kushindwa haiwezi kurundikwa kichwani pa Mungu, ili Mungu mwenyewe afanywe wa kuibeba, kwa sababu sio jambo la Mungu mwenyewe, lakini linahusiana moja kwa moja na wajibu ambao viumbe wa Mungu wanapaswa kutekeleza. Watu wengi wana maarifa madogo ya harakati na hatima za Paulo na Petro, lakini watu hawajui lolote ila matokeo ya Petro na Paulo, na hawajui kuhusu siri ya mafanikio ya Petro, au mapungufu yaliyosababisha kushindwa kwa Paulo. Na kwa hivyo, kama ninyi hamwezi kabisa kuelewa kiini cha harakati zao basi harakati ya wengi wenu bila shaka haitafaulu, na hata kama wachache wenu watafaulu, bado hawatakuwa sawa na Petro. Ikiwa njia unayopitia katika kutafuta ni ya kweli, basi una matumaini ya mafanikio. Kama njia unayopitia katika kufuatilia ukweli ni mbaya, basi wewe milele hutaweza kufanikiwa, na utakuwa na hatima sawa na Paulo.

Petro alikuwa mtu aliyefanywa mkamilifu. Ni baada tu ya kupitia kuadibu na hukumu, na hivyo kupata upendo safi kwa Mungu, ndipo alifanywa mkamilifu kabisa; njia ambayo alipitia ilikuwa ni njia ya kukamilishwa. Ambayo ni kusema kuwa, tangu hapo mwanzo kabisa, njia ambayo Petro alipitia ilikuwa ya haki, na motisha ya kumwamini Mungu ilikuwa sahihi, na kwa hivyo akawa mtu aliyekuwa amefanywa kamili na alifuata njia mpya ambayo mwanadamu kamwe hajawahi kuitembelea hapo awali. Hata hivyo, njia ambayo Paulo alitembea tangu mwanzo ilikuwa njia ya upinzani kwa Kristo, na ni kwa sababu tu Roho Mtakatifu alitaka kumtumia, na kufaidika na vipaji vyake na ustahili wake wote kwa kazi yake, kwamba alifanya kazi kwa ajili ya Kristo kwa miongo mingi. Alikuwa mtu tu ambaye alitumiwa na Roho Mtakatifu, na hakutumika kwa sababu Yesu alitazama ubinadamu wake kwa mapendeleo, lakini ni kwa sababu ya vipaji vyake. Aliweza kufanya kazi ya Yesu kwa sababu alipigwa, na sio kwa sababu alifurahia kufanya hivyo. Aliweza kufanya kazi kama hiyo kwa sababu ya kupata nuru na uongozi wa Roho Mtakatifu, na kazi aliyoifanya haikuwakilisha ufuatiliaji wake kwa njia yeyote, au ubinadamu wake. Kazi ya Paulo iliwakilisha kazi ya mtumishi, ambayo ni kusema kuwa yeye alifanya kazi ya mtume. Petro, hata hivyo, alikuwa tofauti: Yeye pia alifanya baadhi ya kazi; haikuwa kuu kama kazi ya Paulo, lakini alifanya kazi huku akiwa na harakati ya kuingia kwake mwenyewe, na kazi yake ilikuwa tofauti na kazi ya Paulo. Kazi ya Petro ilikuwa utekelezaji wa wajibu wa kiumbe wa Mungu. Yeye hakufanya kazi katika nafasi ya mtume, lakini alifanya kazi huku akifuatilia upendo kwa Mungu. Mwendo wa kazi ya Paulo pia ulikuwa na harakati yake binafsi. Ufuatiliaji wake ulikuwa tu kwa ajili ya matumaini yake ya siku za baadaye, na shauku yake ya hatima nzuri. Yeye hakukubali usafishaji wakati wa kazi yake, wala hakukubali upogoaji na ushughulikaji. Yeye aliamini kuwa alimradi kazi aliyoifanya iliridhisha mapenzi ya Mungu, na yote aliyofanya yalimpendeza Mungu, basi tuzo hatimaye ilikuwa inamsubiri. Hakukuwa na matukio ya kibinafsi katika kazi yake—yote yalikuwa kwa ajili yake mwenyewe, na hayakufanyika huku kukiwa na harakati ya mabadiliko. Kila kitu katika kazi yake kilikuwa shughuli, na hakukuwa na wajibu wowote au kujisalimisha kwa kiumbe cha Mungu. Wakati wa safari ya kazi yake, hakuna mabadiliko yaliyotokea katika tabia ya zamani ya Paulo. Kazi yake ilikuwa tu ya kufanya huduma kwa ajili ya wengine, na haikuwa na uwezo wa kuleta mabadiliko katika tabia yake. Paulo alifanya kazi yake moja kwa moja, bila ya kufanywa mkamilifu ama kushughulikiwa, na alivutiwa na thawabu. Petro alikuwa tofauti: alikuwa mtu ambaye alikuwa amepitia upogoaji na ushughulikiaji na alikuwa amepitia usafishaji. Lengo na motisha za kazi ya Petro zilikuwa tofauti kimsingi na zile za Paulo. Ingawa Petro hakufanya sehemu kubwa ya kazi, tabia yake ilipitia mabadiliko mengi, na alichotafuta ni ukweli, na mabadiliko ya kweli. Kazi yake haikufanyika tu kwa ajili ya kazi yenyewe. Ingawa Paulo alifanya kazi nyingi, yote ilikuwa kazi ya Roho Mtakatifu, na ingawa Paulo alishirikiana katika kazi hii, yeye, hakuipitia. Kwamba Petro alifanya kazi ndogo ilikuwa tu kwa ajili Roho Mtakatifu hakufanya kazi kubwa kupitia yeye. Wingi wa kazi zao haukuamua iwapo walikuwa wamefanywa wakamilifu; harakati ya mmoja ilikuwa ili kupokea tuzo, na ile ya mwingine ilikuwa ili kufikia upendo wa mwisho kwa Mungu na kutimiza wajibu wake kama kiumbe cha Mungu, kwa kiasi kwamba angeweza kuishi kwa kudhihirisha picha inayopendeza ili kukidhi mapenzi ya Mungu. Nje walikuwa tofauti, na pia vile vile viini vyao vilikuwa tofauti. Huwezi kuamua ni nani kati yao alifanywa mkamilifu kwa msingi wa kazi waliyofanya. Petro alitafuta kuishi kwa kudhihirisha picha ya yule ambaye hupenda Mungu, kuwa mtu ambaye alimtii Mungu, kuwa mtu ambaye alikubali ushughulikaji na upogoaji, na kuwa mtu aliyetekeleza wajibu wake kama kiumbe wa Mungu. Aliweza kujitolea kwa Mungu, kuweka nafsi yake kamilifu katika mikono ya Mungu, na kumtii hadi kifo. Hilo ndilo alilokuwa ameamua kufanya na, zaidi ya hayo, hilo ndilo alilotimiza. Hii ndiyo sababu ya msingi ya kwani hatima yake ilikuwa tofauti na ile ya Paulo. Kazi ambayo Roho Mtakatifu alifanya ndani ya Petro ilikuwa kumfanya mkamilifu, na kazi ambayo Roho Mtakatifu alifanya ndani ya Paulo ilikuwa kumtumia. Hii ni kwa sababu asili zao na mitazamo yao kuhusu harakati hazikuwa sawa. Wote walikuwa na kazi ya Roho Mtakatifu. Petro alitumia kazi hii kwake mwenyewe, na pia akawapa watu wengine; Paulo, kwa upande mwingine, aliwapa wengine kazi nzima ya Roho Mtakatifu, na mwenyewe hakufaidika na chochote kutoka kwa kazi hiyo. Kwa njia hii, baada ya yeye kushuhudia kazi ya Roho Mtakatifu kwa miaka mingi, mabadiliko ndani ya Paulo yalikuwa karibu na kutokuwepo. Yeye bado alibaki karibu katika hali yake ya asili, na bado yeye alikuwa yule Paulo wa awali. Ni baada tu ya kuvumilia ugumu wa miaka mingi ya kazi, ndivyo alikuwa amejifunza jinsi ya kufanya “kazi” na kujifunza uvumilivu, lakini asili yake ya zamani—ushindani wake mkuu na asili wa kimamluki—bado ilibaki. Baada ya kufanya kazi kwa miaka mingi, hakufahamu asili yake potovu, wala hakuwa amejiondoa mwenyewe kutoka kwa asili yake ya zamani, na bado ilikuwa inaonekana katika kazi yake. Kwake, kulikuwepo tu na uzoefu wa kazi zaidi, lakini uzoefu mdogo kiasi hicho pekee haukuwa na uwezo wa kumbadilisha na hukuweza kubadilisha maoni yake kuhusu kuwepo au umuhimu wa harakati yake. Ingawa alimfanyia Kristo kazi kwa miaka mingi, na hakumtesa tena Bwana Yesu, ndani ya Moyo wake hakukuwa na mabadiliko katika elimu kuhusu Mungu. Hii ina maana kuwa hakufanya kazi ili awe mwaminifu kwa Mungu, lakini badala yake, alilazimika kufanya kazi kwa ajili ya hatima yake ya siku zijazo. Kwa kuwa, hapo mwanzo, alimtesa Kristo, na hakumtii Kristo; kiasili yeye alikuwa mwasi ambaye alimpinga Kristo kimakusudi, na mtu ambaye hakuwa na elimu kuhusu kazi ya Roho Mtakatifu. Kazi yake ilipokuwa inakaribia kukamilika, yeye bado hakujua kazi ya Roho Mtakatifu, na yeye tu alitenda kwa hiari yake mwenyewe kwa mujibu wa hulka yake mwenyewe, bila hata kidogo kutilia maanani mapenzi ya Roho Mtakatifu. Na hivyo asili yake ilikuwa katika uhasama na Kristo na haikutii ukweli. Mtu kama huyu, ambaye alikuwa ameachwa na kazi ya Roho Mtakatifu, ambaye hakujua kazi ya Roho Mtakatifu, na ambaye pia alimpinga Kristo—je, ni jinsi gani mtu kama huyu angeokolewa? Iwapo mtu ataweza kuokolewa au la haitegemei kiasi cha kazi anayoifanya, au ni kiasi gani anajitolea, lakini badala yake kuamuliwa na iwapo anajua au hajui kazi ya Roho Mtakatifu, iwapo anaweza kuweka ukweli kwenye vitendo au la, na iwapo maoni yake kuhusu harakati yanalingana na ukweli au la.

Ingawa ufunuo wa asilia ulitokea baada ya Petro kuanza kumfuata Yesu, katika asili alikuwa, tangu mwanzo kabisa, mtu ambaye alikuwa tayari kujiwasilisha kwa Roho Mtakatifu na kumtafuta Kristo. Utiifu wake kwa Roho Mtakatifu ulikuwa safi: hakutafuta umaarufu na mali, lakini badala yake alikuwa amepewa motisha na utii wa ukweli. Ingawa kuna nyakati tatu ambapo Petro alikana kumjua Kristo, na ingawa alimjaribu Bwana Yesu, udhaifu kidogo kama huu wa kibinadamu haukubeba uhusiano wa asilia yake, na haukuathiri harakati zake za mbeleni, na huwezi kuthibitisha kikamilifu ya kuwa majaribu yake yalikuwa kitendo cha mpinga Kristo. Udhaifu wa kawaida wa kibinadamu ni kitu ambacho kimo kwa watu wote duniani—je, unatarajia Petro kuwa tofauti vyovyote vile? Je, si watu wana mtazamo fulani kuhusu Petro kwa sababu alifanya makosa mengi ya kijinga? Na je, si watu wanampenda Paulo kwa sababu ya kazi yote aliyoifanya, na nyaraka zote alizoandika? Itakuwaje mtu kuwa na uwezo wa kuona kupitia kiini cha mwanadamu? Hakika, je, wale ambao kwa kweli wana hisia wanaweza kuona kitu chenye thamani ndogo kama hiyo? Ingawa miaka mingi ya matukio ya uchungu ya Petro hayajanakiliwa katika Biblia, hii haithibitishi kuwa Petro hakuwa na matukio halisi, au kwamba Petro hakufanywa mkamilifu. Ni jinsi gani kazi ya Mungu inaweza kueleweka na mwanadamu? Kumbukumbu kwenye Biblia hazikuchaguliwa binafsi na Yesu, lakini zilikusanywa na vizazi vya baadaye. Kwa njia hii, si yote ambayo yaliandikwa katika Biblia yalichaguliwa kulingana na mawazo na mwanadamu? Zaidi ya hayo, hatima ya Petro na Paulo hazijaelezwa kwa dhati katika nyaraka, kwa hivyo mwanadamu anawahukumu Petro na Paulo kulingana na mtazamo wake mwenyewe, na kulingana na matakwa yake mwenyewe. Na kwa kuwa Paulo alifanya kazi kubwa sana, kwa sababu “michango” yake ilikuwa mikuu sana, yeye alipata imani ya umma. Je, si mwanadamu anamakinika tu na vitu vya juu juu tu. Inakuwaje mwanadamu kuwa na uwezo wa kuona kupitia kwa kiini cha mwanadamu? Bila kutaja, kwa kuwa Paulo amekuwa mlengwa wa ibada kwa maelfu ya miaka, ni nani ambaye atathubutu kukana kazi yake kwa haraka? Petro alikuwa mvuvi tu, hivyo ni jinsi gani mchango wake ungekuwa mkubwa kama ule wa Paulo? Kwa msingi wa mchango, Paulo angepaswa kuzawadiwa kabla ya Petro, na inapaswa kuwa yeye ndiye angekuwa amehitimu vyema zaidi kupata kibali cha Mungu. Nani angeweza kufikiri kuwa, katika kumtendea Paulo, Mungu alimfanya tu afanye kazi kupitia vipawa vyake, ilhali Mungu alimfanya Petro kuwa mkamilifu. Si kwa njia yoyote kweli ya kwamba Bwana Yesu alikuwa amefanya mpango kwa ajili ya Petro na Paulo tangu mwanzo kabisa: Badala yake, walifanywa wakamilifu au kuwekwa kazini kulingana na tabia zao za kiasili. Na kwa hivyo, kitu ambacho wanadamu wanachoona kama michango ya nje ya mwanadamu tu, ilhali anachoona Mungu ni kiini cha mtu, na vile vile kama njia ambayo mwanadamu hufuatilia tangu mwanzo, na motisha inayosukuma harakati ya mwanadamu. Watu hupima mwanadamu kulingana na dhana zao, na kulingana na mitazamo yao wenyewe, na bado hatima ya mwisho ya mwanadamu haiamuliwi kulingana na mambo ya nje ya mwanadamu. Na kwa hivyo Mimi ninasema kwamba kama njia unayochukua tangu mwanzo ni njia ya mafanikio, na mtazamo wako kuhusu harakati ni sahihi tangu mwanzo, basi wewe ni kama ya Petro; kama njia ambayo unatembea ni njia ya kushindwa, basi gharama yoyote ambayo unalipa, hatima yako itakuwa sawa na ile ya Paulo. Yawayo yoyote, hatima yako, na kama utafaulu ama hautafaulu, yote yanaamuliwa na kama njia unayotafuta ni sahihi ama si sahihi, badala ya kujitolea kwenu, au gharama ambayo wewe hulipa. Kiini cha Petro na kiini cha Paulo, na malengo ambayo walifuatilia, yalikuwa tofauti; mwanadamu hana uwezo wa kugundua vitu hivi, na Mungu pekee anaweza kuyajua kwa ujumla wao. Kwa kuwa kitu ambacho Mungu huona ni kiini cha mwanadamu, ilhali mwanadamu hajui chochote kuhusu kiini chake mwenyewe. Mwanadamu hana uwezo wa kukitazama kiini ndani ya mwanadamu ama kimo chake halisi, na hivyo hana uwezo wa kutambua sababu za kutofaulu ama kufaulu kwa Paulo na Petro. Sababu ya wanadamu wengi kumuabudu Paulo na wala si Petro ni kuwa Paulo alitumika katika kazi ya umma, na mwanadamu anaweza kutambua kazi hii, na hivyo watu wanakiri “mafanikio” ya Paulo. Matukio ya Petro, wakati huo huo, hayaonekani na mwanadamu, na kwamba kile alichotafuta hakipatikani na mwanadamu, na hivyo mwanadamu hana moyo wa kutaka kumjua Petro.

Petro alifanywa mkamilifu kwa kupitia ushughulishaji na usafishaji. Alisema, “Mimi ni lazima nikidhi mapenzi ya Mungu wakati wote. Kwa yote nifanyayo mimi natafuta tu kukidhi mapenzi ya Mungu, na kama mimi ninaadibiwa, au kuhukumiwa, bado nina furaha kufanya hivyo.” Petro alimpa Mungu kila kitu chake, na kazi yake, maneno, na maisha yote yalikuwa yote kwa ajili ya kumpenda Mungu. Alikuwa mtu ambaye alitafuta utakatifu, na alipopitia zaidi, ndivyo upendo wake wa Mungu ndani ya moyo wake ulikuwa mkubwa zaidi. Paulo, wakati huo huo, alifanya tu kazi ya nje, na ingawa alitia bidii katika kazi yake, juhudi zake zilikuwa kwa ajili ya kufanya kazi yake vizuri na hivyo kupata tuzo. Angalijua kuwa hatapokea tuzo, yeye angalikata tamaa katika kazi yake. Kitu ambacho Petro alijali mno ni upendo wa kweli moyoni mwake, na ule ambao ulikuwa wa vitendo na ungeweza kutimizika. Yeye hakujali kuhusu iwapo angepokea tuzo, lakini kuhusu iwapo tabia yake ingebadilishwa. Paulo alijali kuhusu kufanya kazi kwa bidii hata zaidi, yeye alijali kuhusu kazi ya nje na kujitolea, na kuhusu mafundisho ambayo hayashuhudiwi na watu wa kawaida. Yeye hakujali chochote kuhusu mabadiliko ndani yake wala kwa ajili ya upendo wa kweli kwa Mungu. Uzoefu wa Petro ulikuwa kwa ajili ya kupata upendo wa kweli na maarifa ya kweli kuhusu Mungu. Uzoefu wake ulikuwa ili kupata uhusiano wa karibu na Mungu, na kwa kuishi kwa kudhihirisha kwa vitendo. Kazi ya Paulo ilifanywa kwa sababu ya kile alichoaminiwa na Yesu, na ili apate vitu ambavyo alitamani, lakini haya hayakuwa na uhusiano na elimu yake mwenyewe na ya Mungu. Kazi yake ilikuwa tu kwa ajili ya kuepuka kuadibu na hukumu. Kitu ambacho Petro alitafuta kilikuwa ni upendo safi, na Paulo alitafuta taji ya hali ya kuwa mwenye haki. Petro alishuhudia miaka mingi ya kazi ya Roho Mtakatifu, na alikuwa na elimu ya vitendo kuhusu Kristo, na vile vile elimu ya kina kujihusu yeye mwenyewe. Na hivyo, upendo wake wa Mungu ulikuwa safi. Miaka mingi ya usafishaji ilikuwa imeinua elimu yake kuhusu Yesu na maisha, na upendo wake ulikuwa upendo usio na masharti, ulikuwa upendo wa hiari, na hakuagiza chochote akitarajia malipo, na wala hakutumainia kuwa na faida yeyote. Paulo alifanya kazi kwa miaka mingi, ilhali hakumiliki elimu kubwa ya Yesu, na elimu yake ya kibinafsi ilikuwa ndogo mno. Yeye kwa kifupi hakuwa na upendo kwa Kristo, na kazi yake na mwendo ambao alikimbia ilikuwa ili apate heshima na taji la mwisho. Kitu ambacho alitafuta kilikuwa taji zuri kabisa, wala si upendo safi. Yeye hakutafuta kikamilifu, lakini kwa kutoonyesha hisia; hakuwa anatekeleza majukumu yake, lakini alilazimika katika harakati yake baada ya kukamatwa na kazi ya Roho Mtakatifu. Kwa hivyo, harakati yake haithibitishi kuwa yeye alikuwa kiumbe wa Mungu kilichokuwa na sifa zinazostahili; ilikuwa ni Petro ambaye alikuwa kiumbe wa Mungu aliyekuwa na sifa zilizostahili na ambaye alitekeleza wajibu wake. Mwanadamu anafikiri kuwa wale wote wanaotoa mchango kwa Mungu wanapaswa kupokea tuzo, na kwamba mchango unavyokuwa mkubwa zaidi, ndivyo mwanadamu anavyosadiki zaidi kuwa atapokea fadhila za Mungu. Kiini cha mtazamo wa mwanadamu ni wa shughuli, na hatafuti kikamilifu kutekeleza wajibu wake kama kiumbe wa Mungu. Kwa Mungu, watu wanavyozidi kutafuta upendo kwa Mungu wa kweli na utii mkamilifu kwa Mungu, ambayo pia ina maana kutafuta kutekeleza wajibu wao kama viumbe wa Mungu, ndivyo zaidi wanaweza kupata kibali cha Mungu. Mtazamo wa Mungu ni kudai kwamba mwanadamu arejeshe hadhi na wajibu wake wa awali. Mwanadamu ni kiumbe wa Mungu, na kwa hivyo mwanadamu hapaswi kuvuka mpaka mwenyewe kwa kutoa madai yoyote kwa Mungu, na anapaswa asifanye lolote zaidi ya kutekeleza wajibu wake kama kiumbe wa Mungu. Hatima ya Paulo na hatima ya Petro ilipimwa kulingana na iwapo wangeweza kutekeleza wajibu wao kama viumbe wa Mungu, na wala si kulingana na ukubwa wa michango yao; hatima zao ziliamuliwa kulingana na kile ambacho walitafuta tangu mwanzo, wala si kulingana na kiasi cha kazi waliyofanya, au makadirio ya watu wengine kuwahusu. Kwa hivyo, kutafuta kutekeleza kikamilifu wajibu wa mtu kama kiumbe wa Mungu ndiyo njia ya mafanikio; kutafuta njia ya upendo wa kweli kwa Mungu ndiyo njia sahihi kabisa; kutafuta mabadiliko katika tabia ya zamani ya mtu, na kutafuta upendo safi kwa Mungu, ndiyo njia ya mafanikio. Njia kama hii ya mafanikio ndiyo njia ya kurejeshwa kwa wajibu wa awali na vile vile pia kuonekana kwanza kwa kiumbe wa Mungu. Hiyo ndiyo njia ya kurejeshwa, na pia ni lengo la kazi yote ya Mungu kuanzia mwanzo hadi mwisho. Kama harakati ya mwanadamu inatiwa doa na madai badhirifu ya kibinafsi na tamaa isiyo ya akili, basi athari ambayo inatimizwa haitakuwa mabadiliko katika tabia ya mwanadamu. Hii ni kinyume na kazi ya kurejeshwa. Bila shaka siyo kazi inayofanywa na Roho Mtakatifu, na hivyo hii inathibitisha kuwa harakati ya aina hii haikubaliki na Mungu. Harakati ambayo haijakubalika na Mungu ina umuhimu gani?

Kazi iliyofanywa na Paulo ilionyeshwa mbele ya mwanadamu, lakini upendo wake wa Mungu ulikuwa safi kiasi gani, upendo wake kwa Mungu ulikuwa ndani ya moyo wake kiasi gani—haya hayaonekani na mwanadamu. Mwanadamu anaweza tu kutazama kazi ambayo aliifanya, ambapo mwanadamu hujua kuwa kwa hakika alitumika na Roho Mtakatifu, na hivyo mwanadamu hudhani kwamba Paulo alikuwa bora kuliko Petro, ya kwamba kazi yake ilikuwa kubwa zaidi, kwa kuwa alikuwa na uwezo wa kutoa kwa makanisa. Petro alitazama tu matukio yake binafsi, na akapata watu wachache wakati wa kazi yake ya mara kwa mara. Kutoka kwake kunazo lakini nyaraka chache zinazojulikana, lakini ni nani anayejua jinsi upendo wa Mungu ulivyokuwa mkubwa kiasi gani moyoni mwake? Siku zote, usiku na mchana, Paulo alimfanyia Mungu kazi: alimradi kulikuwepo na kazi ya kufanywa, yeye aliifanya. Yeye alihisi kuwa kwa njia hii angeweza kulipata taji, na angemridhisha Mungu, lakini hakutafuta njia za kujibadilisha mwenyewe kupitia kazi hii. Chochote katika maisha ya Petro ambacho hakikukimu mapenzi ya Mungu kilimfanya kuhisi wasiwasi. Kama hakikukidhi mapenzi ya Mungu, basi angehisi kujuta, na angetafuta njia mwafaka ambayo angejitahidi kuridhisha moyo wa Mungu. Hata katika masuala madogo kabisa maishani mwake yasiyokuwa na maana, bado alijishurutisha mwenyewe kukidhi mapenzi ya Mungu. Alikuwa pia mkali ilipofikia tabia yake ya asili na alikuwa daima mkali katika masharti yake mwenyewe ili kuelekea ndani zaidi kwa ukweli. Paulo alitafuta tu sifa na hadhi ya kijuu juu. Alitafuta kuringa mwenyewe mbele za mwanadamu, na hakutafuta kufanya maendeleo zaidi katika kuingia kwa maisha. Kile alichojali kuhusu ni mafundisho ya kidini, si uhalisi. Baadhi ya watu husema, “Paulo alimfanyia Mungu kazi nyingi, kwa nini yeye hakukumbukwa na Mungu? Petro alimfanyia Mungu kazi kidogo, na hakufanya mchango mkubwa katika makanisa, je, kwa nini yeye alifanywa mkamilifu?” Petro alimpenda Mungu hadi kiwango fulani, ambacho kilitakiwa na Mungu; ni watu kama hawa pekee wana ushuhuda. Na kuhusu Paulo? Ni kiwango gani ambacho Paulo alimpenda Mungu, je, wewe wajua? Kazi ya Paulo ilikuwa kwa ajili ya nini? Na kazi ya Petro ilikuwa kwa ajili ya nini? Petro hakufanya kazi kubwa, lakini, je, wafahamu ni nini kilikuwa moyoni mwake? Kazi ya Paulo inahusiana na utoaji makanisani, na msaada wa makanisa. Kile ambacho Petro alishuhudia ni mabadiliko ya tabia ya maisha yake; alishuhudia upendo kwa Mungu. Kwa kuwa sasa unajua tofauti katika kiini cha kila mmoja wao, unaweza kuona ni nani, hatimaye, kwa kweli alimwamini Mungu, na ni nani ambaye kwa kweli hakumwamini Mungu. Mmoja wao alimpenda Mungu kwa kweli, na mwingine hakumpenda Mungu kwa kweli; mmoja alipitia mabadiliko katika tabia yake, na mwingine hakupitia; mmoja alihudumu kwa unyenyekevu, na hakuonekana na watu kwa urahisi na mwingine aliabudiwa na watu, na alikuwa na picha nzuri; mmoja alitafuta utakatifu, na mwingine hakuutafuta, na ingawa hakuwa najisi, hakuwa amemilikiwa na upendo safi; mmoja alimilikiwa na ubinadamu wa kweli, na mwingine hakuwa nao; mmoja alikuwa na hisia ya kiumbe wa Mungu, na mwingine hakuwa na hisia hiyo. Tofauti kama hizi ndizo zilizo katika kiini cha Paulo sawa na Petro. Njia ambayo Petro alitembea ni njia ya mafanikio, ambayo pia ni njia ya kutimiza kupatwa tena kwa ubinadamu wa kawaida na wajibu wa kiumbe wa Mungu. Petro anawakilisha wote hao waliofaulu. Njia ambayo Paulo aliitembea ni njia ya kushindwa, na anawakilisha wale wote ambao wanajisalimisha na kujipa matarajio yao wenyewe ya kijuu juu, na hawampendi Mungu kwa dhati. Paulo anawakilisha wote ambao hawana ukweli. Katika imani yake kwa Mungu, Petro alitafuta kumridhisha Mungu katika kila kitu, na alitafuta kutii yote yaliyotoka kwa Mungu. Bila malalamiko hata kidogo, aliweza kukubali kuadibu na hukumu, na vile vile usafishaji, dhiki na kuwa bila kitu maishani, yote ambayo hayangeweza kubadilisha upendo wake kwa Mungu. Je, huu haukuwa upendo mkamilifu kwa Mungu? Je, huku hakukuwa ni kutimiza wajibu wa kiumbe wa Mungu? Kuadibu, hukumu, dhiki—una uwezo wa kufikia utii hadi kifo, na hili ndilo linafaa kutimizwa na kiumbe wa Mungu, huu ni usafi wa upendo kwa Mungu. Kama mwanadamu anaweza kutimiza kiasi hiki, basi yeye ni kiumbe wa Mungu mwenye sifa inayostahili, na hakuna kitu kinachokidhi mapenzi ya Muumba bora zaidi ya hiki. Fikiria kwamba wewe unaweza kumfanyia Mungu kazi, ilhali wewe humtii Mungu, na huna uwezo wa kumpenda Mungu kwa kweli. Kwa njia hii, wewe hutakuwa tu umekosa kutimiza wajibu wa kiumbe cha Mungu, lakini pia utalaaniwa na Mungu, kwa kuwa wewe ni mtu ambaye hana ukweli, ambaye hana uwezo wa kumtii Mungu, na ambaye si mtiifu kwa Mungu. Wewe unajali tu kuhusu kumfanyia Mungu kazi, na hujali kuhusu kuweka ukweli katika vitendo, ama kujifahamu. Wewe humfahamu ama kumjua Muumba, na humtii ama kumpenda Muumba. Wewe ni mtu ambaye asilia si mtiifu kwa Mungu, na hivyo watu kama hawa hawapendwi na Muumba.

Baadhi ya watu husema, “Paulo alifanya kazi kubwa kiasi cha ajabu, na alibeba mizigo mikubwa ya makanisa na aliwachangia mno. Nyaraka kumi na tatu ya Paulo zilizingatia miaka 2,000 ya Enzi ya Neema, na ni za pili tu baada ya Injili Nne. Nani anaweza kulinganishwa naye? Hakuna ambaye anaweza kufumbua maandiko ya Ufunuo wa Yohana, ilhali nyaraka za Paulo zinatoa maisha, na kazi ambayo alifanya ilikuwa na manufaa kwa makanisa. Ni nani mwingine angeweza kutimiza mambo kama haya? Na kipi ambacho Petro alikifanya?” Mwanadamu anapowapima wengine, ni kwa mujibu wa michango yao. Mungu anapompima mwanadamu, ni kwa mujibu wa asili yake. Miongoni mwa wale ambao hutafuta uzima, Paulo alikuwa mtu ambaye hakujua kiini chake mwenyewe. Hakuwa kwa njia yoyote mnyenyekevu ama mtiifu, wala kujua kiini chake, ambacho kilikinzana na Mungu. Na kwa hivyo, alikuwa mtu ambaye hakuwa amepitia matukio ya kina, na alikuwa mtu ambaye hakuweka ukweli katika vitendo. Petro alikuwa tofauti. Yeye alijua kutokamilika kwake, udhaifu, na tabia yake potovu kama kiumbe wa Mungu, na hivyo alikuwa na njia ya vitendo ambayo angebadilishia tabia yake; hakuwa mmoja wa wale ambao walikuwa tu na mafundisho ya kidini lakini hawakuwa na uhalisi. Wale ambao hubadilika ni watu wapya ambao wameokolewa, ni wale ambao wana sifa zinazostahili katika kufuatilia ukweli. Watu ambao hawabadiliki ni wa wale ambao hawafai kwa sasa kiasili; ni wale ambao hawajaokolewa, yaani, ni wale ambao wamechukiwa na kukataliwa na Mungu. Hawatakumbukwa na Mungu bila kujali jinsi kazi zao ni kubwa. Wakati unapolinganisha haya na harakati yako mwenyewe, kama wewe hatimaye ni mtu wa aina sawa na Petro au Paulo inapaswa kuwa dhahiri kibinafsi. Kama bado hakuna ukweli kwa yale unayotafuta, na kama hata leo bado wewe ni mwenye kiburi na jeuri kama Paulo, na bado wewe ni mwepesi wa kusema maneno matupu na mwenye kujisifu kama yeye, basi bila shaka wewe ni aliyeharibika tabia na ambaye hushindwa. Kama wewe hutafuta jinsi sawa na Petro, kama unatafuta vitendo na mabadiliko ya kweli, na usiwe mwenye kiburi au mkaidi, bali utafute kutekeleza majukumu yako, basi utakuwa kiumbe wa Mungu ambaye anaweza kufikia ushindi. Paulo hakujua kiini chake mwenyewe ama upotovu, vile vile hakujua kutotii kwake. Hakuwahi kutaja uasi wake kwa Kristo unaostahili dharau, wala yeye hakuwa mwenye kujuta kupindukia. Yeye tu alipeana maelezo mafupi, na, ndani katika moyo wake, hakujiwasilisha kwa Mungu kikamilifu. Ingawa alianguka barabarani akielekea Dameski, yeye hakuangalia nafsi yake kwa kina. Aliridhika tu kwa kuendelea kufanya kazi, na hakuzingatia kujijua mwenyewe na kubadilisha tabia yake ya zamani kuwa jambo la muhimu zaidi ya masuala yote. Yeye aliridhika tu kwa kusema ukweli, na kukimu wengine kama dawa ya dhamiri yake mwenyewe, na kwa kutowatesa tena wanafunzi wa Yesu kujifariji na kujisamehe kwa dhambi zake za zamani. Lengo ambalo yeye alifuatilia tu lilikuwa taji ya wakati ujao na kazi ya muda pekee, lengo ambalo alifuatilia lilikuwa neema tele. Yeye hakutafuta ukweli wa kutosha, wala hakutafuta kuendelea ndani katika kiini cha ukweli ambao hakuwa hapo awali ameufahamu. Na kwa hivyo elimu yake ya nafsi yake inaweza semwa kuwa ya uwongo, na hakukubali kuadibu au hukumu. Kwamba aliweza kufanya kazi haina maana alikuwa na elimu ya asili yake au kiini; lengo lake lilikuwa la vitendo vya nje pekee. Lile ambalo daima alijitahidi kwalo, zaidi ya hayo, halikuwa mabadiliko, laikini elimu. Kazi yake kwa ujumla ilikuwa matokeo ya kuonekana kwa Yesu njiani kuelekea Dameski. Hakikuwa kitu ambacho alikuwa ameamua kukifanya hapo awali, wala haikuwa kazi ambayo ilikuwa imetokea baada ya yeye kukubali upogoaji wa tabia yake ya zamani. Bila kujali jinsi ambavyo alifanya kazi, tabia yake ya zamani haikubadilika, na hivyo kazi yake haikulipia dhambi yake ya zamani lakini ilikuwa tu na wajibu fulani kwenye makanisa ya wakati huo. Kwa mtu kama huyu, ambaye tabia yake ya zamani haikubadilika—hivyo ni kusema, ambaye hakupata wokovu, na hata zaidi alikuwa bila ukweli—alikuwa hawezi kabisa kukuwa mmoja wa wale waliokubaliwa na Bwana Yesu. Hakuwa mtu ambaye alikuwa amejazwa na upendo na heshima kwa Yesu Kristo, wala hakuwa mtu ambaye alikuwa na ustadi katika kutafuta ukweli, na wala hakuwa mtu ambaye alitafuta fumbo la kupata mwili kwa Yesu Kristo. Alikuwa tu mtu ambaye alikuwa na ujuzi katika utata, na ambaye hangeweza kusalimu amri kwa yeyote ambaye alikuwa mkuu kwake au aliyekuwa na ukweli. Aliwaonea kijicho watu ama ukweli ambao ulikuwa tofauti naye, ama wenye uadui naye, na kupendelea watu wenye vipawa ambao walionyesha picha nzuri na kumiliki maarifa makubwa. Hakupenda kuingiliana na watu maskini ambao walitafuta njia ya ukweli na waliojali kuhusu ukweli pekee, na badala yake alijihusisha na viongozi mashuhuri kutoka mashirika ya kidini ambao walizungumza kuhusu mafundisho ya dini pekee, na walikuwa na elimu tele. Hakuwa na upendo wa kazi mpya ya Roho Mtakatifu, na hakujali kuhusu harakati za kazi mpya ya Roho Mtakatifu. Badala yake, yeye alipendelea kanuni hizo na mafundisho ya dini ambayo yalikuwa juu kuliko ukweli wa ujumla. Katika kiini chake cha kiasilia na uzima wa kile alichotafuta, hastahili kuitwa Mkristo ambaye alifuatilia ukweli, wala mtumishi mwaminifu katika nyumba ya Mungu, kwa kuwa unafiki wake ulikuwa mwingi sana, na kutotii kwake kulikuwa kukubwa sana. Ingawa anajulikana kama mtumishi wa Bwana Yesu, hakustahili kamwe kuingia kwenye lango la ufalme wa mbinguni, kwa kuwa matendo yake tangu mwanzo hadi mwisho hayawezi kuitwa yenye haki. Anaweza tu kuonekana kama mtu ambaye alikuwa mnafiki, na aliyefanya udhalimu, ilhali ambaye alimfanyia Yesu kazi. Ingawa hawezi kuitwa mwovu, yeye anaweza ipasavyo kuitwa mtu ambaye alifanya udhalimu. Alifanya kazi nyingi, ilhali ni lazima asihukumiwe juu ya wingi wa kazi aliyofanya, lakini tu kwa ubora na umuhimu wa kazi hiyo. Ni kwa njia hii tu ndiyo inawezekana kufikia kwenye kiini cha suala hili. Yeye siku zote aliamini: “Mimi nina uwezo wa kufanya kazi, mimi ni bora kuliko watu wengi; mimi ni mwenye kujali kuhusu mzigo wa Bwana kuliko mtu yeyote, na hakuna anayetubu sana kama ninavyotubu, kwa kuwa mwanga mkuu uling’aa kwangu, na nimeuona mwanga mkuu, na hivyo toba yangu ni kuu kuliko ya yeyote mwingine.” Wakati huo, hivi ndivyo alivyofikiria moyoni mwake. Mwishoni mwa kazi yake, Paulo alisema: “Nimefanya bidii katika mashindano, nimemaliza safari yote na sasa imebakia tu kupewa tuzo la ushindi kwa maisha ya uadilifu.” Mapambano yake, kazi, na safari zilikuwa kwa ajili ya taji la haki, na yeye hakusonga mbele; ingawa yeye hakuwa wa juu juu tu katika kazi yake, inaweza kusemwa kuwa kazi yake ilikuwa kwa ajili tu ya kusahihisha makosa yake, na kusahihisha shutuma za dhamiri yake. Yeye tu alitumaini kukamilisha kazi yake, kumaliza safari yake, na kupigana vita vyake haraka iwezekanavyo, ili kwamba aweze kupata tuzo lake la haki alilotamani kwa haraka. Alilotamani halikuwa kukutana na Bwana Yesu na uzoefu wake na elimu ya kweli, lakini kukamilisha kazi yake haraka iwezekanavyo, ili kwamba aweze kupokea tuzo ambayo kazi yake ilikuwa imemwezesha kupata wakati alipokutana na Bwana Yesu. Alitumia kazi yake kujifariji, na kufanya makubaliano kwa ajili ya kupewa taji siku zijazo. Alichotafuta sio ukweli ama Mungu, lakini taji tu. Harakati kama hii inawezekanaje kuwa ya kiwangogezi? Motisha yake, kazi yake, gharama aliyolipa, na juhudi zake zote—ndoto zake za ajabu zilienea kote, na alifanya kazi kabisa kulingana na mapenzi yake. Katika ukamilifu wa kazi yake, hapakuwa na hiari kidogo ya gharama aliyolipa; alikuwa anashiriki kwenye mapatano tu. Juhudi zake hazikufanywa kwa hiari ili kutimiza wajibu wake, bali zilifanywa kwa hiari ili kutekeleza lengo la mapatano. Je, kuna thamani yoyote kwa jitihada kama hizo? Nani ambaye anaweza kusifu juhudi zake chafu? Nani ambaye ana moyo wa kujua juhudi kama hizi? Kazi yake ilijawa na ndoto za mbeleni, zilijawa na mipango ya ajabu, na hazikuwa na njia ya kubadilishia tabia ya kibinadamu. Ukarimu wake mwingi ulikuwa wa unafiki; kazi yake haikuleta maisha, lakini ilikuwa unyenyekevu bandia; lilikuwa tendo la maafikiano. Jinsi gani kazi kama hii kumwongoza mwanadamu kwenye njia ya kupata tena wajibu wake wa awali?

Yote ambayo Petro alitafuta yalikuwa kufuata Moyo wa Mungu. Alitaka kutimiza mapenzi ya Mungu, na licha ya taabu na mashaka, bado yeye alikuwa tayari kutimiza mapenzi ya Mungu. Hakuna ukimbizaji mkuu zaidi wa muumini katika Mungu. Kile ambacho Paulo alitafuta kilitiwa doa na mwili wake, na dhana zake mwenyewe, na mipango na mipangilio yake mwenyewe. Hakuwa kwa njia yeyote kiumbe wa Mungu aliyehitimu, hakuwa mtu ambaye alitaka kutimiza mapenzi ya Mungu. Petro alitaka kujiwasilisha kwenye mipango ya Mungu, na ingawa kazi aliyofanya haikuwa kuu, motisha ya harakati yake na njia ambayo alitembea zilikuwa sahihi; ingawa hakuweza kupata watu wengi, aliweza kufuata njia ya ukweli. Kwa hivyo inaweza kusemwa kwamba alikuwa kiumbe wa Mungu aliyehitimu. Leo, hata kama wewe si mfanyikazi, unapaswa kuwa na uwezo wa kutekeleza wajibu wa kiumbe wa Mungu, na kutafuta kujiwasilisha kwa mipango yote ya Mungu. Unapaswa kuwa na uwezo wa kutii chochote Mungu anachosema, na upitie kila aina ya madhila na usafishaji, na ingawa wewe ni dhaifu, moyoni mwako unapaswa bado uwe na uwezo wa kumpenda Mungu. Wale ambao huchukua jukumu katika maisha yao wako tayari kutekeleza wajibu wa kiumbe wa Mungu, na mtazamo wa watu kama hawa kuhusu harakati ni ule sahihi. Hawa ndio watu ambao Mungu anahitaji. Iwapo ulifanya kazi nyingi, na watu wengine walipata mafundisho yako, lakini wewe mwenyewe hukubadilika, na hukuwa na ushuhuda wowote, au kuwa na uzoefu wowote wa kweli, kwa namna kuwa katika hatima ya maisha yako, bado hakuna yoyote uliyofanya iliyo na ushuhuda, basi je, wewe ni mtu aliyebadilika? Je, wewe ni mtu ambaye hufuatilia ukweli? Wakati huo, Roho Mtakatifu alikutumia, lakini alipokutumia, alitumia sehemu yako ambayo ingeweza kutumika kufanya kazi, na wala hakutumia sehemu yako ambayo haingeweza kutumika kufanya kazi. Kama wewe ulitafuta kubadilika, basi ungeweza kufanywa mkamilifu hatua kwa hatua wakati wa mchakato wa kutumika. Hata hivyo Roho Mtakatifu hakubali jukumu la kama au la wewe mwishowe utapatwa, na hii inategemea na namna ya ukimbizaji wako. Iwapo hakuna mabadiliko katika tabia yako binafsi, basi hiyo ni kwa sababu mtazamo wako kuelekea kufuatilia ni mbaya. Kama hutatunukiwa tuzo, basi hilo ni tatizo lako, na kwa sababu wewe mwenyewe hujaweka ukweli katika vitendo, na huwezi kutimiza mapenzi ya Mungu. Na kwa hivyo, hakuna kitu cha umuhimu kama uzoefu wako wa kibinafsi, na hakuna kilicho cha maana kuliko kuingia kwako kibinafsi. Baadhi ya watu wataishia kusema, “Mimi nimefanya kazi nyingi kwa ajili yako, na ingawa kuna uwezekano kuwa hazikuwa na mafanikio ya kusherehekewa, bado nimekuwa mwenye jitihada kwenye juhudi zangu. Huwezi tu kuniruhusu niingie mbinguni ili nile tunda la uzima?” Ni lazima ujue aina ya watu ambao Ninataka; wale walio najisi hawakubaliki kuingia katika ufalme, wale walio najisi hawakubaliki kuchafua nchi takatifu. Ingawa unaweza kuwa umefanya kazi nyingi, na umefanya kazi kwa miaka mingi, mwishowe kama bado wewe ni mwovu kupindukia—hakuvumiliki kwa sheria ya Mbinguni kwamba wewe unataka kuingia katika ufalme wangu! Tangu mwanzo wa dunia hadi leo, kamwe Sijatoa njia rahisi ya kuingilia ufalme Wangu kwa wale wenye neema Yangu. Hii ni sheria ya Mbinguni, na hakuna awezaye kuivunja. Ni lazima utafute uzima. Leo, wale watakaofanywa wakamilifu ni wa aina sawa na Petro: ni wale ambao hutafuta mabadiliko katika tabia yao wenyewe, na wako tayari kuwa na ushuhuda kwa Mungu na kutekeleza wajibu wao kama kiumbe wa Mungu. Ni watu kama hawa pekee watakaofanywa wakamilifu. Kama wewe tu unatazamia tuzo, na hutafuti kubadilisha tabia ya maisha yako mwenyewe, basi juhudi zako zote zitakuwa za bure—na huu ni ukweli usiobadilika!

Kutoka kwa tofauti katika kiini cha Paulo na kiini cha Petro unapaswa kufahamu kuwa wale wote ambao hawafuati uzima wanafanya kazi ya bure! Unamwamini Mungu na unafuata Mungu, na kwa hivyo moyoni mwako ni lazima umpende Mungu. Ni lazima uache tabia yako potovu, lazima utafute kutimiza mapenzi ya Mungu, na ni lazima utekeleze wajibu wako kama kiumbe wa Mungu. Kwa kuwa unamwamini na kumfuata Mungu, unapaswa kutoa kila kitu kwake, na hupaswi kufanya uamuzi au madai ya kibinafsi, na unapaswa kutimiza ukamilishaji wa mapenzi ya Mungu. Kwa kuwa uliumbwa, unapaswa kumtii Bwana aliyekuumba, kwa kuwa wewe huna mamlaka kiasili juu yako mwenyewe, na huna uwezo wa kudhibiti hatima yako. Kwa kuwa wewe ni mtu ambaye anamwamini Mungu, inapaswa utafute utakatifu na mabadiliko. Kwa kuwa wewe ni kiumbe wa Mungu, unapaswa kushika wajibu wako, na kuhifadhi nafasi yako, na ni lazima usivuke mpaka wa wajibu wako. Hii si kwa ajili ya kukuzuia, ama kukukandamiza kupitia mafundisho, bali ndiyo njia ambayo utaweza kutekelezea wajibu wako, na inaweza kufikiwa—na inapaswa kufikiwa—na wote wanaotenda haki. Ukilinganisha kiini cha Petro na kiini cha Paulo, basi utajua jinsi unapaswa kutafuta. Kati ya njia ambazo Petro na Paulo walitembea, njia moja ni ya kufanywa mkamilifu, na nyingine ni njia ya kutolewa katika mashindano; Petro na Paulo wanawakilisha njia mbili tofauti. Ingawa kila moja wao alipokea kazi ya Roho Mtakatifu, na kila mmoja alipata nuru na mwangaza wa Roho Mtakatifu, na kila mmoja alikubali kile alichokuwa ameaminiwa na Bwana Yesu, tunda lililozaliwa katika kila mmoja wao halikuwa sawa. Mmoja kwa kweli alizaa tunda, na mwingine hukuzaa tunda. Kutokana na kiini cha kila mmoja wao, kazi waliyofanya, hiyo walioonyesha kwa upande wa nje, na hatima yao ya mwisho, unapaswa kuelewa ni njia gani unayopaswa kuchukua, njia ambayo unapaswa kuchagua kuitembea. Walitembelea njia mbili ambazo dhahiri ni tofauti. Paulo na Petro, walikuwa mifano ya kila njia, na kwa hivyo tangu mwanzo walionekana kuwakilisha njia hizi mbili. Je, ni mawazo gani muhimu katika uzoefu wa Paulo, na ni kwa nini yeye hakufaulu? Je, ni pointi gani muhimu katika matukio ya Petro, na ni jinsi gani yeye alishuhudia kufanywa mkalifu? Ukilinganisha kile ambacho kila alijali kuhusu, basi utajua aina hasa ya mtu ambaye Mungu anamtaka, mapenzi ya Mungu ni gani, na tabia ya Mungu, ni mtu wa aina gani ambaye hatimaye atafanywa mkamilifu, na pia aina gani ya mtu hawezi kufanywa mkamilifu, nini tabia ya wale ambao watafanywa wakamilifu, na nini tabia ya wale ambao hawatafanywa wakamilifu—masuala haya ya kiini yanaweza kuonekana katika uzoefu wa Petro na Paulo. Mungu aliumba kila kitu, na hivyo yeye hufanya viumbe wote kuwa chini ya utawala wake, na kujiwasilisha kwenye utawala wake; Yeye ataamuru kila kitu, ili kila kitu kiwe mikononi mwake. Vitu vyote vilivyoumbwa na Mungu, pamoja na wanyama, mimea, mwanadamu, milima na mito, na maziwa—vyote ni lazima vije chini ya utawala Wake. Vitu vyote mbinguni na ardhini lazima zije chini ya utawala Wake. Haviwezi kuwa na hiari yoyote na vyote ni lazima vitii mipango Yake. Hii iliagizwa na Mungu, na ni mamlaka ya Mungu. Mungu huamuru kila kitu, na huagiza na kuainisha kila kitu, ambapo kila kimoja huainishwa kulingana na aina, na kutengewa nafasi zao zenyewe, kulingana na mapenzi ya Mungu. Bila kujali kitu ni kikubwa namna gani, hakuna kitu kinachoweza kumpita Mungu, na vitu vyote ambavyo vinamtumikia mwanadamu aliyeumbwa na Mungu, na hakuna kitu kinachothubutu kumuasi Mungu ama kumdai Mungu. Na kwa hivyo mwanadamu, kama kiumbe wa Mungu, ni lazima atekeleze wajibu wa mwanadamu. Bila kujali iwapo yeye ni bwana au mlindaji wa vitu vyote, bila kujali jinsi hadhi ya mwanadamu ni kuu miongoni mwa vitu vyote, bado yeye ni binadamu mdogo anayetawaliwa na Mungu, na si zaidi ya binadamu asiye na umuhimu, kiumbe wa Mungu, na kamwe hatawahi kuwa juu ya Mungu. Kama kiumbe wa Mungu, mwanadamu anapaswa kutafuta kutekeleza wajibu wa kiumbe wa Mungu, na kutafuta kumpenda Mungu bila kufanya chaguo lingine kwa kuwa Mungu anastahiki upendo wa mwanadamu. Wale ambao wanatafuta kumpenda Mungu hawapaswi kutafuta faida zozote za kibinafsi au lile ambalo wanatamani binafsi; hii ndiyo njia sahihi kabisa ya ufuatiliaji. Kama kile ambacho unatafuta ni ukweli, kile ambacho unatenda ni ukweli, na kile ambacho unafikia ni badiliko katika tabia yako, basi njia unayopitia ni sahihi. Iwapo utafutacho ni baraka za mwili, na kile unachoweka katika vitendo ni ukweli wa dhana zako mwenyewe, na iwapo hakuna mabadiliko katika tabia yako, na wewe si mtiifu kabisa kwa Mungu katika mwili, na bado unaishi kwenye mashaka, basi unachotafuta bila shaka kitakupeleka kuzimu, kwa kuwa njia ambayo unatembea ni njia ya kushindwa. Iwapo utafanywa mkamilifu ama utatolewa katika mashindano inategemea na harakati yako mwenyewe, ambayo pia ni kusema kuwa mafanikio au kushindwa kunategemea njia ambayo mwanadamu anapitia.

Iliyotangulia: Msimamo Wako Kuhusu Nyaraka Kumi na Tatu ni Upi?

Inayofuata: Kazi ya Mungu na Kazi ya Mwanadamu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp