Kupitia kwa Majonzi Makuu, Nimevuna Faida Kubwa

16/01/2018

Rongguang Mji wa Zhengzhou, Mkoa wa Henan

Baada ya kumfuata Mwenyezi Mungu, niliwekwa katika jela kwa sababu mimi niliamini katika Mungu. Wakati huo nilikuwa muumini mpya na Mungu alikuwa amenipa nguvu ili niweze shikilia msimamo katika ushahidi wangu. Hata hivyo, niliamini kimakosa kuwa nilikuwa na kimo; nilidhani kwamba nilikuwa na kiasi kikubwa cha imani, upendo na uaminifu kwa Mungu, kwa hiyo sikuzingatia hasa kula na kunywa maneno ya Mungu ya hukumu na kuadibu. Ingawa nilisoma, nililinganisha neno ambalo kwalo Mungu humfichua mtu na watu wengine na kujitenga mwenyewe kutoka kwa maneno ya kuhukumu ya Mungu. Nilikuwa tu na nia ya kusoma kuyahusu mafumbo ambayo Mungu ameyafichua na unabii pamoja na maneno kuhusu kupata baraka; haya ndiyo maneno niliyokuwa na haja nayo sana. Nilisoma maneno ya Mungu: “Kwa misingi ya kazi zao na shuhuda zao tofauti, washindi katika ufalme watatumika kama makuhani au wafuasi, na wale wote watakaoshinda taabu watakuwa mwili wa makuhani katika ufalme. … Katika baraza la makuhani, patakuwepo makuhani wakuu na makuhani, na watakaosalia watakuwa wana na watu wa Mungu. Haya yote huamuliwa na ushuhuda wao kwa Mungu wakati wa majaribu; sio nyadhifa zinazopeanwa kwa wazo la ghafla(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kazi ya Mungu na Utendaji wa Mwanadamu). “Wakati wa dhiki hautarefushwa sana; kwa kweli, utadumu kwa chini ya mwaka mmoja. Ukidumu kwa mwaka mzima, hatua inayofuata ya kazi itacheleweshwa, na kimo cha watu hakitakuwa cha kutosha. Ukiwa mrefu sana, basi watu hatawaweza kuistahimili. Hata hivyo, kimo cha watu kina mapungufu yake(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Jinsi Unavyopaswa Kuitembea Sehemu ya Mwisho ya Njia). Niliwaza: Nafasi katika ufalme itaamuliwa kulingana na jinsi watu hushuhudia wakati wa majonzi; shuhuda hizi zinaweza kuathiri majaliwa ya mtu. Majonzi yakinijia, itabidi nijikaze kisabuni na kutoa nguvu ya kutosha, na bila shaka nitatoa ushahidi mzuri. Kwa njia hiyo nitaweza kupata baraka kubwa; aidha, majonzi hayatadumu kwa muda mrefu sana–yatakuwa chini ya mwaka mmoja. Bila kujali kitakachotokea, nitaweza kustahamili kipindi hiki cha shida. Kwa kuwa nikiongozwa na mawazo ya kupata baraka niliamua kujiweka tayari kwa vita; nilidhani kwamba kwa kuitegemea “imani” na “mapenzi” yangu, ningeweza kuwa mshindi wakati wa majonzi.

Kazi ya Mungu ya kuwaokoa watu ni ya ajabu sana na ya busara sana. Katika mwaka wa 1996, sisi wote tuliingia katika majonzi makuu kupitia mpangilio wa Mungu. Lakini wakati majonzi yalipotujia, hakuna yeyote aliyejua juu yake; kila kitu kilitokea kwa njia ya kawaida sana, mtindo wangu wa kweli na hali ya kuwa mfuata upepo vilifichuka wakati wa majonzi hayo.

Miezi ya Juni na Julai ya mwaka wa 1996, nilikuwa katika sehemu nyingine ya nchi kutimiza wajibu wangu ulioshirikisha kuandika. Siku moja, kiongozi wa eneo hili alikuja na kutuambia kuwa hali ya hivi karibuni haikuwa nzuri sana na kwamba Dada fulani alikuwa amekamatwa na joka kubwa jekundu. Tuliposikia haya, tulitaka kumwombea huyu dada na hatukufikiria jambo jingine zaidi, kwa sababu sisi sote tulijua kwamba lilikuwa jambo la kawaida kwa watu kukamatwa kwa sababu ya imani yao katika Mungu nchini China, nchi ambayo ilimtesa Mungu kwa njia hii. Lakini, hazikupita siku nyingi kabla ya kusikia kwamba ndugu wengine kadhaa wa kiume na wa kike walikamatwa. Baada ya siku kadhaa, tukasikia kwamba watu takribani dazeni moja walikamatwa, na waumini wengi mashuhuri waliokuwa wakitumikia kama viongozi katika familia ya Mungu walikuwa wameorodheshwa kwa siri kama waliotakiwa. Pia kulikuwa na baadhi ya watu ambao walikuwa na zawadi kwa kukamatwa kwao. Viongozi wa mahali pale pia walikuwa kwenye orodha ya watu wanaodhaniwa kuwa wabaya ya joka kubwa jekundu. Nilihisi kuwa mambo hayakuwa mazuri: Ilionekana kama joka kubwa jekundu lilikuwa linajaribu kuangamiza waumini kwa dharuba moja. Tulihisi aina ya hofu kuu katika anga iliyotuzingira; hatukujua cha kufanya katika hali ya aina hii; tulitaka kuwasiliana na aliye juu na kumwuliza jinsi ya kuendelea, lakini hatukuweza kuwasiliana naye. Baadaye niligundua kwamba majonzi yalikuwa yameanza mwezi mmoja kabla. Lakini wakati huo tulikuwa w enye ganzi katika roho na hatukuthubutu kukisia na kufafanua kazi ya Mungu. Kwa sababu hiyo hatukujua kwamba haya yalikuwa ni majonzi makuu. Yote tuliyoweza kuhisi ulikuwa ni mkono mweusi wa joka kubwa jekundu ukigandamiza karibu nasi na hatungeweza kuendelea katika kazi yetu kwa sababu binafsi. Katika kukabili aina hii ya taabu, kwa uhafifu tukatambua kuwa kazi ilikuwa imezuiwa na mkono wa Mungu; Mungu alikuwa akituongoza kuacha kazi na kujificha na kutopoteza muda kurejea kwa nchi yetu ya asili. Kwa njia hiyo tungekuwa salama. Kwa hiyo, tulilazimika kutawanyika na kurudi kwa nchi yetu ya asili.

Nilikuwa nyumbani kwa wiki moja tu wakati dada mmoja alikuja na kunipa barua ikisema kuwa ndugu mmoja katika kanisa letu alikamatwa, na nilihitajika kuondoka nyumbani mara moja. Wakati huu nilishtuka; sikuwa na imani yoyote na nilikuwa na wazo moja tu katika moyo wangu: Kujificha kwa haraka na kutoruhusu joka kubwa jekundu kunikamata; joka kubwa jekundu ni la kusikitisha mno na katili, mbinu mbovu inazotumia kuwaangamiza waumini ni katili. Nikianguka katika mikono ya pepo, matokeo yatakuwa yasiyofikirika. Kufuatia hili, dada fulani alinileta milimani ili kuwapikia wachimba madini. Nilikuwa hapo na dada wawili na tukatumia nyakati hizo kwa manufaa yetu wakati hakukuwa mtu yeyote karibu kula na kunywa maneno ya Mungu, kufanya ushirika na kuimba nyimbo. Kwa sababu tulikuwa na ugavi wa maneno ya Mungu, kila siku ilikuwa ya kusitawisha sana. Hata hivyo, katika chini ya mwezi mmoja, polisi walikuja katika eneo hilo na sikuwa na jingine la kufanya ila kuondoka kwa haraka. Baadaye nilikuja kwa mkahawa mwingine kufanya kazi. Kila mtu niliyekutana naye alikuwa asiyemwamini Mungu na sikuwa na lugha yoyote ya pamoja nao; zaidi ya hayo, sikuwa na neno la Mungu katika mazingira ya aina hii, na hakukuwa na yeyote wa kufanya ushirika naye kiasi kwamba ilikuwa ni vigumu hata kutoa sala sahihi. Nilihisi upweke na mwenye ukiwa na moyo wangu haukuwa na budi ila kuanza kulalamika. Hata nilitaka kumsaliti Mungu: “Kuamini katika Mungu kweli si rahisi na nilikuwa mwenye wahaka mchana kutwa; Ninatangatanga katika duniani ambayo haina haki; siku hizi zitakwisha lini? Kama sikuamini katika Mungu, nikiishi maisha ya raha na imara kama makafiri, si hivyo vingekuwa vizuri sana?” Hata kama moyo wangu ulifikiri kwa njia hii, nilihisi woga na sikuthubutu kumwacha Mungu; pia nilihisi singemwacha Mungu, wazo la kumwacha Mungu lilinisababishia maumivu. Lakini kwa vile sikupenda kusoma maneno ya Mungu katika siku za nyuma, sikutafuta ukweli, na nilitimiza wajibu wangu tu ili kupata baraka, kwa hiyo, wakati nilipoviacha vitabu vya neno la Mungu, moyo wangu haukuwa na msitari wa neno la Mungu uliobaki ndani yake. Bila maneno ya Mungu ya uzima kunisaidia, nilikuwa tu kama mjinga aliyerukwa na akili. Sikujua cha kufanya ama cha kufuatilia baadaye. Nilijitahidi tu bila tumaini kila siku. Mapenzi ya Mungu yalikuwa yapi? Kwa nini Yeye alinipangia hili? Ningetendaje na kumtosheleza Mungu? Sikuwa na nguvu ya kutafakari hili, yote niliyoyafikiria yalikuwa kuhusu taabu zangu. Wakati huo imani yangu katika kudura na maarifa ya Mungu na imani yangu katika utawala wa Mungu wa mahali pote yote yalikuwa yamepotea. Ilifikia kiwango kwamba wakati dada fulani alikuja kunialika kwenda kutembelea baadhi ya ndugu wa kike na wa kiume, nilikataa, kwa sababu moyo wangu ulikuwa unaogopa na wenye woga. Sikuwa na imani au nguvu, nilitegemewa tu mawazo na fikira zangu, nikifikiri kwamba mazingira hayatakuwa mazuri kabla ya Hong Kong kurudi China. Katika kipindi hiki cha wakati, joka kubwa jekundu kwa wayowayo litamkandamiza na kumkomesha kila mtu ambaye kwa dhati huamini katika Mungu. Sasa itakuwa muda mrefu kabla ya kurudi kwa Hong Kong, hakika ni lazima nijilinde mwenyewe vizuri. Wakati wa miezi miwili na nusu ambayo nilifanya kazi katika mkahawa, moyo wangu ukawa mbali na Mungu zaidi na zaidi, karibu kufikia mahali ambapo nilikubali tu jina la Mungu, lakini sikuwa na Mungu katika moyo wangu. Moyo wangu ulikuwa mara nyingi ukivutiwa kwa kupenda anasa; nilitaka kumtoroka Mungu na kuishi maisha ya wasiosadiki. Hata hivyo, katika siku chache zilizofuata hasa nilimkosa Mungu na ndugu wa kiume na wa kike; niliyakosa maisha yangu ya zamani ya kanisa. Wakati nikiwa peke yangu, daima sikujizuia kulia. Moyo wangu ulikuwa wa kusononeka: Ewe Mungu, siku nzima niko na watu wasioamini; kama sifanyi kazi, basi nala au kuwa na mazungumzo ya uchoshi. Ni Wewe tu unayejua utupu na maumivu katika moyo wangu. Ee Mungu, ni lini usiku huu mrefu utapita? Ni lini tutafanywa huru kuamini katika Mungu, kama katika siku za nyuma wakati tulipoishi katika familia Yako njema? Moyo wangu uliteseka kana kwamba ulikuwa ukienewa na magugu na singebaki tena. Ilielekea kwamba ilikuwa inakaribia Tamasha la Majira ya Kuchipua na nikajinufaisha kwa fursa hii na kuacha kazi yangu na kwa haraka kurejea kwa ndugu zangu wa kiume na wa kike. Baadaye nikagundua kuwa haikuwa mimi tu niliyekuwa na mawazo haya; kulikuwa na ndugu wengi wa kiume na wa kiume waliokuwa wameepuka kukamatwa na joka kubwa jekundu kwa kutorokea maeneo mengine ambao walikuwa wamepitia jambo hilo hilo. Wote wakarudi nyumbani kwa sababu walikuwa wakifikiri kitu kimoja. Huu ulikuwa ni mwongozo wa kimiujiza wa Roho Mtakatifu.

Siku chache tu baada ya mimi kurudi nyumbani, dada mmoja alikuja kuniarifu juu ya mkusanyiko wa kanisa. Niliposikia dada huyu akisema kwamba majonzi yalikuwa yameisha, na kwamba kila kitu kilikuwa kimerejea tena katika hali ya kawaida, na kwamba ningeweza kwenda na kutimiza wajibu wangu wa zamani, nilichukua muda kabla ya kutambua: “Unasemaje? Majonzi yameisha? Haya yalikuwa ndiyo majonzi? Bado itakuwa miezi michache kabla ya Hong Kong kurudi China. Inawezekanaje kuwa majonzi yamekwisha? Hili silo nililolitarajia! Wakati wote huu mambo haya tuliyokuwa tukiyapitia yalikuwa ni majonzi, sasa nimekwisha! Ni lipi nililolidhihirisha wakati wa majonzi? Licha ya kuwa mwenye woga na hofu, nililalamika, nikatoroka, na nikasaliti. Sikuwa na vipengele vyovyote vya imani, sembuse uaminifu na upendo. Wakati huu Mungu ameijaribu kazi yangu na mimi nilifeli kabisa.” Nilitahayari katika kukata tamaa nikiwa na kila aina ya hisia katika moyo wangu. Wakati huu niliweza kuelewa kile Mungu alichokisema kabla ya majonzi kuanza: “Baada ya kazi Yangu mwenyewe kukamilika, hatua inayofuata itakuwa kwa watu kuitembea njia wanayopaswa kuitembea. Kila mtu lazima aelewe ni njia gani anayopaswa kuitembea—ni njia na mchakato wa kuteseka, na pia ni njia ya kusafisha dhamira yako ya kumpenda Mungu. Unapaswa kuingia katika ukweli upi, ni ukweli gani unaopaswa kujazilia, jinsi unavyopaswa kupitia na unapaswa kuingia kutoka katika kipengele kipi—sharti uelewe mambo haya yote. Lazima ujiandae sasa. Dhiki itakapokujia, utakuwa umechelewa mno(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Jinsi Unavyopaswa Kuitembea Sehemu ya Mwisho ya Njia). Somo hili la huzuni huniambia: Watu hawawezi kuwa na shahidi katika majonzi kama hawana ukweli na kama wanategemea tamaa zao wenyewe. Watu wanaoishi bila ukweli katika kazi ya Mungu bila shaka watafichuliwa kikamilifu; hawataweza kujificha hata kidogo ama kuweza kuigiza kwa udanganyifu tena. Bila ukweli, umejengwa juu ya msingi wa mchanga, ambao hautahimili jaribio hata dogo. Ni kwa ukweli tu unapoweza kuona mambo kwa dhahiri, kuwa na imani na nguvu, kuweza kupata ushindi juu ya Shetani na kuweza kuweka ukweli katika vitendo ili kumtosheleza Mungu na kutoa ushahidi kwa ajili ya Mungu. Kwa kweli nilijichukia: Mungu tayari kwa uvumilivu ametuambia mambo haya zamani sana, na mbona sikuamini, mbona sikuchukulia hilo kwa uzito kabisa! Hakuna kinachoweza kufutwa; hakuna uchaguzi mwingine ila kutafuta ukweli kwa bidii katika njia iliyo mbele.

Tulipomaliza kukutana, nikasikia dada mmoja akifichua baadhi ya taarifa za ndani za CCP: Joka kubwa jekundu bado linaendeleza kwa ujeuri kuwakamata waumini na jambo hili linazidi kuwa kali hata zaidi. Niliposikia hili, moyo wangu wa imani kidogo ulinong’oneza tena: Mazingira ni kaze hivi na ndugu wa kiume na wa kike wote wanatimiza wajibu wao. Hili ni sawa? Lakini ukweli uliniruhusu kuona kwamba: Hata kama hali ni kaze, hatuogopi kama tulivyokuwa wakati wa majonzi; wakati tunapotimiza wajibu wetu, mioyo yetu hasa ni imara na yenye amani kana kwamba kila mtu alisahau kile kipande cha taarifa za ndani tulizoambiwa na yule dada. Roho Mtakatifu pia anafanya kazi kubwa sana katika kanisa; haitakuwa muda mrefu kabla ya tukio kuu wakati injili itasambazwa katika kila nchi. Kazi yetu inaendelea kuwa na shughuli nyingi na kila wajibu unatekelezwa kwa urahisi. Karibu ndugu wote wa kiume na kike wanatimiza wajibu wao kwa juhudi zao bora katika nafasi zao mtawaliwa. Mandhari yanaendelea kupamba moto mbele tu ya joka kubwa nyekundu, lakini jinsi kazi inavyopanuka kwa nguvu hivi, hakujakuwa na ukamatwaji wowote kama huo katikati ya majonzi makuu. Ukweli huu uliniruhusu kuona ukweli kwa dhahiri: Kwa kweli, joka kubwa jekundu hufanya kazi daima kumpinga Mungu, kumtesa Mungu na kuwashurutisha watu wateule wa Mungu; halijaacha na linataka kumuua Mungu na watu Wake wateule. Wakati mwingine kisu cha bucha mkononi mwake hakituangukii, na huyo ni Mungu akituangalia na kutulinda. Wakati mwingine hata hatutambui nia yake ya kuua, na huyo ni Mungu anayetumia nguvu Yake kubwa kutuhifadhi, si kwamba joka kubwa jekundu liliweka kisu chake chini na kusimamisha mateso yake. Joka kubwa jekundu halijawahi kuweka kisu chake cha bucha chini; halitakiweka chini kamwe; linataka kumpinga Mungu hadi mwisho na kadiri linavyokaribia mwisho, ndivyo linavyozidi kuwa lenye wayowayo, kwa sababu joka kubwa jekundu ni Shetani, pepo mbaya. Linajua kwamba siku ile tukufu Mungu atakapokamilisha kazi Yake ya wokovu ndiyo siku yake ya mwisho. Kwa hiyo, jinsi kifo kinavyozidi kukaribia, ndivyo linavyozidi kupambana. Hata hivyo, bila kujali kitakachotokea, kazi ya Mungu hutumia joka kubwa jekundu kama foili[a], ni chombo cha hudumu katika mikono ya Mungu, ni kitu cha kuwajaribu wateule wa Mungu. Ukatili wake hauwezi kuzuia kazi ya Mungu, bila idhini ya Mungu, halina nguvu juu ya wateule wa Mungu. Wakati Mungu haliruhusu kuwinda, wateule wa Mungu watakuwa mbele yake na halitaweza kuwashika. Halina uchaguzi mwingine ila kuwa chini ya Mungu. Kama tu neno la Mungu linavyosema: “Ninapoanza kirasmi Kazi Yangu, watu wote wanatembea kama Mimi hatua kwa hatua, kiasi kwamba watu katika ulimwengu wote wanakuwa katika hatua na Mimi, kuna ‘shangwe’ ulimwengu mzima, na mwanadamu anaendelezwa mbele na Mimi. Kwa sababu hii, joka kubwa jekundu mwenyewe anachapwa na Mimi mpaka anakuwa katika hali ya kuchanganyikiwa na wazimu, na anahudumia Kazi Yangu, na, licha ya kutokuwa na nia, anashindwa kufuata tamaa zake mwenyewe, na kukosa njia nyingine ila kujiwasilisha kwa udhibiti Wangu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima, Sura ya 29). Katika majonzi makuu, Mungu aliruhusu joka kubwa jekundu kuwatesa wateule wa Mungu, kwa sababu Alitaka kulitumia joka kubwa jekundu na kulitumia kunufaisha wateule wa Mungu waliochaguliwa ili kuona wazi kiini cha upinzani wa joka kubwa jekundu dhidi ya Mungu. Kama Mungu Hakuruhusu tupitie mateso, basi hatungeweza kuamini kwa hakika maneno yaliyofichuliwa na Mungu juu ya kiini cha upotovu wa joka kubwa jekundu; na hatungeweza kuwa na ufahamu wa uaminifu wa Mungu. Kwa hiyo, Mungu huturuhusu kuona ukweli wa mambo ya hakika wakati unaofaa. Ni kwa njia hii tu tunapoweza kuona kwamba kila kitu anachokisema Mungu ni kweli na kwamba joka kubwa jekundu kweli ni adui wa Mungu, kwamba ni pepo mbaya, na kwamba huwaua watu na huzimeza roho za watu. Kama mambo haya ya hakika hayangekufichuliwa, bado ningechezewa na kudanganywa nalo; bado ningeliamini liliposema, “uhuru wa dini” na “haki za kisheria za wananchi.” Leo, mimi binafsi nimepitia ufukuziaji na mateso ya joka kubwa jekundu, nimeona uso wa kikatili wa mauaji ya joka kubwa jekundu ya wateule wa Mungu na macho yangu mwenyewe. Na ninajua sasa kuwa uhuru na demokrasia linazozitangaza zote ni hila kuwadanganya na kuwalaghai watu. Sasa ninaona kwa dhahiri kiini cha uovu na kusikitisha cha kishetani cha joka kubwa jekundu, na moyo wangu kwa kweli unalidharau. Nimeamua kulisaliti na kumfuata Mungu hadi mwisho.

Majonzi huja kutoka kwa Mungu, na mpangilio wa kuisha kwao bila shaka uko katika mikono ya Mungu. Wakati kazi ya Mungu hutoa matokeo, Mungu bila shaka hataahiri wakati. Kama tu Mungu alivyosema: “Wakati wa dhiki hautarefushwa sana; kwa kweli, utadumu kwa chini ya mwaka mmoja. Ukidumu kwa mwaka mzima, hatua inayofuata ya kazi itacheleweshwa, na kimo cha watu hakitakuwa cha kutosha. Ukiwa mrefu sana, basi watu hatawaweza kuistahimili. Hata hivyo, kimo cha watu kina mapungufu yake.” Mungu ana ufahamu wa kina kutuhusu, Yeye anajua vimo vyetu, Yeye anajua hali zetu, na Yeye hayuko radhi kuyaruhusu maisha yetu kuwa na hasara. Kwa hivyo, Mungu hataairisha hata kwa sekunde moja, na tunaweza kustahimili yote haya. Mungu amefanya mipango kamili kwetu katika kazi Yake, Yeye amefikiria maisha yetu kwa kila njia; lakini katika majonzi yangu, yote niliyowaza ni kuhusu usalama wangu mwenyewe na kama nilikuwa nikisumbuliwa na matatizo au la; sikumfikiria Mungu hata kidogo. Mimi kwa kweli nina ubinafsi na ninasikitisha; sina dhamiri razini na sistahili kuishi katika uwepo wa Mungu. Katika majonzi yangu, Mungu alifichua kimo changu halisi, jambo lililonisababisha mimi kuwa na uelewa halisi wangu mwenyewe. Niliona jinsi nilivyokuwa duni, wa kudharaulika na kipofu; nikaona kwamba sikuwa na imani au upendo kwa Mungu, lakini nilikuwa tu na uasi na upinzani kiasi kwamba ningesaliti wakati wowote na mahali popote. Kwa wakati huu, niliweza kuona hatari yangu, na nikaona umuhimu wa kuwa nimejiandaa na ukweli; tangu hapo nimekuwa na kiu ya ukweli. Kwa wakati huu nilisoma maneno ambayo Mungu aliifichua kuhusu asili potovu ya mtu na nikahisi neno la Mungu likiwa hai ndani yangu kama upanga wenye makali kuwili ukichoma viungo vyangu na uboho na kufichua uchafu na udhalimu katika kina cha moyo wangu. Lilinisababishia kuona kwamba nilikuwa wa kusikitisha na mbaya na kuona kwamba nilikuwa nimepotoshwa kwa kina na Shetani. Nililianza kujidharau mwenyewe na nikawa na hamu ya kujibadilisha mwenyewe; nilikuwa na kiu ya kuwa mtu halisi. Nilihisi kuwa kazi ya Mungu ya hukumu na kuadibu ilikuwa kwa kweli inawatakasa watu na mradi nilitafuta ukweli kwa moyo safi, bila shaka ningetakaswa na kuokolewa. Mara ya kwanza nilihisi thamani ya maneno ya Mungu na umuhimu wa ukweli, moyo wangu ulifurahishwa kwa ndani: hatimaye nimeingia katika imani yangu kwa Mungu, ninapiga hatua ndefu kuelekea mwanzo mpya na ninaweza kuona matumaini ya kupata wokovu. Kwa hiyo, niliweka azimio: Bila kujali jinsi njia iliyo mbele yangu ilivyo na mgongano, siku zote nitakuwa dhabiti na nisiyetingisika katika kumfuata Mungu na kutembea katika njia sahihi ya maisha.

Mipango ya ajabu ya Mungu ilituruhusu kuingia katika majonzi bila kujua na kuinuka kutoka kwa majonzi bila kujua. Mavuno tuliyoyapata kutoka kwa hili yalikuwa wazi na rahisi kuona. Kupitia majonzi haya, tunaweza kuona kuwa Mungu ni mwenye uweza na mwenye busara; tunaona kwamba joka kubwa jekundu haliwezi na ni jinga. Ni jeuri na shenzi, na halina uchaguzi mwingine ila kurushwa huku na huko na kazi ya Mungu pasipo kutaka; litashindwa milele katika mikono ya Mungu. Joka kubwa jekundu hujaribu bila mafanikio kuwaogofya wateule wa Mungu kwa njia ya mateso ya kikatili na kuvuruga na kuvunja kazi ya Mungu. Halitambui kwamba Mungu anatumia hili ili kuwakamilisha watu wa Mungu. Hata kama kwa nje inaonekana kama kwamba mateso ya joka kubwa jekundu yamewajia watu, katika hali halisi, yote yamepangwa na mkono wa Mungu Mwenyezi. Yeye huwatawanya watu na kuwakusanya watu, Yeye huwaongoza watu katika majonzi na kuwaongoza watu kutoka katika majonzi; Yeye huwaruhusu watu kuvumilia mpaka wanapotaka kuondoka, lakini Yeye daima amewaauni watu, amewavuta watu, na kuwasababisha watu kutokuwa na uwezo wa kuondoka. Ni katikati ya mipango hii ya ajabu ya Mungu ambapo watu wanaweza kuona wazi sura mbovu ya joka kubwa jekundu na kwa kweli kulidharau joka kubwa jekundu kutoka kwa kina cha mioyo yao. Watu pia waweza kuiona nguvu kubwa ya Mungu na kupitia upendo wa Mungu, uenye enzi na hekima. Wako dhabiti zaidi na hawasiti katika kumfuata Mungu, na wanaweza kuona vimo vyao vya kweli na uchechefu; mioyo yao ina kiu zaidi ya Mungu na ukweli. Kuna umuhimu sana katika Mungu kusababisha majonzi makuu; kuna hekima nyingi sana katika kazi ya Mungu. Hakuna mtu anayeweza kuielewa. Niliweza kushiriki katika majonzi makuu yaliyopangwa na Mungu; ilikuwa kwa hakika ni sifa ya Mungu na upendo mwingi na heshima yangu katika maisha haya. Kila wakati ninapotafakari juu ya hili ninazidiwa na hisia na kutaka kutoa shukrani zangu za dhati na sifa kwa Mungu. Kama singepitia majonzi, singekuwa na uchaguzi mwingine ila kufuata kwa upofu na mwishowe, ningeanguka na kuangamia kwa kutopata ukweli na kwa kutobadilishwa tabia yangu potovu. Kama singepitia majonzi, singekuwa na imani ya kweli katika Mungu na singeelewa ugumu wa kazi ya Mungu, na kwamba kuwaokoa watu hakukuwa rahisi. Kama singepitia majonzi, singekuwa na uwezo wa kuona uso wa kweli wa joka kubwa jekundu na mimi bado ningekuwa na madanganyo kuhusu jamii hii ovu, bado ningekuwa na upendo kwa ulimwengu huu na singeweza kumfuata Mungu kwa moyo wa chuma. Ni kazi ajabu na hekima ya Mungu ambayo imenishinda mimi; ni kudura ya Mungu na upendo mkubwa ambao umenifanya niwe mahali nilipo leo! Kuanzia sasa kwendelea, bila kujali majaribu na majonzi ninayoyakabili, nitakuwa tayari kutegemea imani na upendo wangu kwa Mungu ili kuwa shahidi kwa Mungu na kuufariji moyo wa Mungu.

Tanbihi:

a. Mtu/kitu kinachodhihirisha uzuri/ubora wa kingine kwa kuvilinganisha.

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Baada ya Kupoteza Hadhi Yangu

Huimin Mji wa Jiaozuo, Mkoa wa Henan Kila wakati nilipoona au kusikia kuhusu mtu aliyekuwa amebadilishwa kama kiongozi naye kujisikia...

Ukombozi wa Moyo

Na Zheng Xin, Marekani Mnamo Oktoba ya 2016, mimi na mume wangu tulikubali kazi ya Mungu katika siku za mwisho wakati tulikuwa ughaibuni....

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp