Siri ya “Ufufuo wa Mfu”

19/05/2021

Li Cheng

Ndugu zangu, amani iwe kwenu! Mshukuruni Bwana kwa maandalizi Yake ambayo yameturuhusu kuwasiliana ukweli wa Maandiko hapa. Bwana atuongoze. Leo, nataka kuzungumza na kila mtu kuhusu mada “ufufuo wa mfu.”

Siri ya “Ufufuo wa Mfu”

Kama watu wamwaminio Bwana wote wanavyojua, “ufufuo wa mfu” hurejelea wakati ambapo Yesu anarudi. Hii pia ni hali ambayo sisi kama Wakristo tunatarajia kuona. Sasa, “mtu aliyekufa” anaweza kufufuliwaje? Watu wengi wangefikiria sura ya 37, mistari ya 5 hadi 6 katika Kitabu cha Ezekieli: “Hivi ndivyo Yehova Mungu alivyoiambia mifupa hii; Tazama, nitafanya pumzi iingie ndani yenu, nanyi mtaishi: Nami nitalaza mishipa juu yenu, naminitaweka nyama juu yenu, na kuwafunika kwa ngozi, na kuweka pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi: nanyi mtafahamu kwamba mimi ndiye Yehova.” Katika Injili ya Yohana sura ya 6, mstari wa 39, Yesu alisema: “Na haya ni mapenzi ya Baba ambaye amenituma, ya kuwa sipaswi kumpoteza hata mmoja kati ya wale wote ambao amenipa, lakini napaswa kumfufua katika siku ya mwisho.” Katika sura ya 15, mistari ya 52 hadi 53 katika Kitabu cha 1 Wakorintho, wanasoma: “lakini sote tutabadilishwa, ghafla, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho: kwani parapanda italia, na wafu watafufuliwa bila uharibifu, na sisi tutabadilishwa. Kwa kuwa hili lipotoshwalo lazima livae kutopotoshwa, na hili la kufariki lazima livae kutofariki.” Aidha, watu wakisoma maana halisi ya Biblia, wataamini: Katika siku za mwisho, Bwana atakapokaribia kushuka, kutakuwa na mambo mengi makubwa na ya ajabu ambayo yatatokea. Kwa uweza Wake, ataifufua miili ya watakatifu ambao wamekuwa wakilala kwa vizazi. Atawafufua kutoka kwa makaburi yao, kutoka chini ya ardhi au chini ya bahari. Maelfu ya mifupa mitupu ambayo tayari imeoza chini ya ardhi au chini ya bahari itapewa uzima mpya mara moja. Uozo utatokomea kimiujiza na itaingia katika utukufu. Ni onyesho lililoje la kustaajabisha! … Hii pia ni mitazamo yetu na mawazo kuhusu “ufufuo wa mfu.” Unabii huu utatimizwa vipi hasa? Je, kweli utakuwa wa kimiujiza kama tunavyofikiria utakuwa? Je, Bwana atafanikisha jambo hili kulingana na mawazo yetu?

Sote tunajua, hekima ya Mungu ni ya juu kuliko mbingu. Kile Mungu afanyacho hupita mawazo na fikira zetu. Katika Biblia, imeandikwa: “Kwa kuwa fikira zangu si fikira zenu, wala namna zenu sio namna zangu, alisema Yehova. Kwa kuwa jinsi mbingu zilivyo juu zaidi kuliko dunia, ndivyo namna zangu zilivyo juu zaidi kuliko namna zenu, na fikira zangu kuliko fikira zenu(Isaya 55: 8-9). Kama viumbe mbele ya Mungu, sisi hatuna thamani na ni duni kama vumbi. Hatutaweza kamwe kuielewa kazi ya Mungu. Hili ni sawa na rekodi katika Biblia ya Yesu akizungumza na Nikodemo kuhusu ukweli wa kuzaliwa upya: “Ila mwanadamu azaliwe tena, hawezi kuuona ufalme wa Mungu(Yoh 3:3). Nikodemo alielewa maneno ya Yesu kwa maana halisi. Aliamini "kuzaliwa upya" kulimaanisha kutokeza tena kutoka tumboni mwa mama ya mtu. Akitumia ubongo wake na mawazo yake, alielewa jambo la kiroho kana kwamba lilikuwa jambo la ulimwengu. Ridhaa ya aina hii ni mbaya sana. Aidha, Yesu alipokuwa akizungumza na mwanamke kutoka Samaria, Alisema, “Ila yeyote akunywaye maji ambaye nitampa hatawahi kuwa na kiu(Yohana 4:14). Wakati huo, yule mwanamke kutoka Samaria hakuelewa kile Bwana alichokuwa akisema. Alidhani kuwa maji ambayo Bwana alikuwa akiyatoa yalikuwa sawa na maji yanayonywewa na wanadamu. Kwa sababu hiyo, akasema, “Bwana, nipe maji haya, ili nisihisi kiu, wala kuja hapa kuchota” (Yohana 4: 15). Kwa kweli, “maji” ambayo Yesu alikuwa akimaanisha lilikuwa neno la Bwana. Alikuwa akimaanisha maji ya uzima. Yule mwanamke kutoka Samaria alielewa tu maana halisi ya kile Yesu alichokisema na hivyo, kuelewa visivyo maana yake. Kutoka kwa hili tunaweza kuona kwamba neno la Mungu ni ukweli. Huwa linaficha fumbo la kazi ya Mungu. Kama Mungu hafichui mafumbo haya, ufahamu wetu ungekuwa mdogo sana. Vivyo hivyo, kama tunaelewa tu maana halisi ya unabii “ufufuo wa mfu,” si tungekuwa tukifanya makosa sawa na yaliyofanywa na Nikodemo na yule mwanamke kutoka Samaria? Kwa hiyo, linapohusu unabii, tunapaswa kudumisha uchaji, kutafuta zaidi, sio kufasiri maandishi kwa maana halisi, sio kutegemea mawazo na fikira zetu kuamua na zaidi ya hayo, kutotegemea maana yetu wenyewe binafsi kuuelezea.

Sasa, “ufufuo wa mfu” unamaanisha nini hasa? Je, “Mfu” na “mtu aliye hai” humaanisha nini? Kwa maelfu ya miaka, hakuna mtu hata mmoja aliyeweza kujibu swali hili kwa dhahiri. Ni Mungu pekee anayeweza kufichua mafumbo haya. Sasa, Mungu tayari amerejea katika umbo la Mwenyezi Mungu mwenye mwili. Ameonyesha milioni nyingi za maneno na kufunua mafumbo yote yaliyo katika Biblia. Hebu tuangalie pamoja maneno ya Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu anasema: “Mungu alimuumba mwanadamu, baada ya hapo mwanadamu akaharibiwa na Shetani, na uharibifu huu umewafanya watu wawe maiti—na hivyo, baada ya kuwa umebadilika, utakuwa tofauti na maiti hizi. Ni maneno ya Mungu ndiyo yanatoa uzima kwa roho za watu na kuwasababisha kuzaliwa upya, na roho za watu zinapozaliwa upya, watakuwa hai tena. Neno ‘wafu’ linarejelea maiti ambazo hazina roho, kwa watu ambao roho zao zimekufa. Roho za watu zinapowekewa uhai, wanakuwa hai tena. Watakatifu waliozungumziwa awali huashiria watu ambao wamekuwa hai, wale ambao walikuwa chini ya ushawishi wa Shetani lakini wakamshinda Shetani. … Mwanadamu wa asili aliyeumbwa na Mungu alikuwa hai, lakini kwa sababu ya uharibifu wa Shetani mwanadamu anaishi katikati ya kifo, na anaishi chini ya ushawishi wa Shetani, na hivyo watu hawa wamekuwa wafu ambao hawana roho, wamekuwa ni maadui ambao wanampinga Mungu, wamekuwa nyenzo ya Shetani, na wamekuwa mateka wa Shetani. … Wafu ni wale ambao hawana roho, wale ambao ni mbumbumbu kupita kiasi, na wale ambao wanampinga Mungu. Aidha, ni wale ambao hawamjui Mungu. Watu hawa hawana nia hata ndogo ya kumtii Mungu, kazi yao ni kumpinga na kuasi dhidi Yake, na hawana hata chembe ya utii. Walio hai ni wale ambao roho zao zimezaliwa upya, wale wanaojua kumtii Mungu, na ambao ni watii kwa Mungu. Wanao ukweli, na ushuhuda, na ni watu wa aina hii tu ndio wanaompendeza Mungu katika nyumba Yake. Mungu anawaokoa wale ambao wanaweza kuwa hai tena, ambao wanaweza kuuona wokovu wa Mungu, ambao wanaweza kuwa watii kwa Mungu, na wapo tayari kumtafuta Mungu. Anawaokoa wanaomwamini Mungu aliyepata mwili, na wanaamini katika kuonekana Kwake” (“Je, Wewe ni Mtu Ambaye Amepata Uzima?” katika Neno Laonekana katika Mwili).

Maneno ya Mwenyezi Mungu yametuelezea maana ya “mfu” na “mtu aliye hai”. Mwanzoni, Mungu aliwaumba mababu za wanadamu, Adamu na Hawa. Walikuwa wanadamu hai wenye roho. Walikuwa watu ambao walikuwa waangalifu sana na wenye akili na waliweza kumdhihirisha Mungu na kumheshimu Mungu. Baadaye, walijaribiwa na Shetani kula tunda kutoka kwa mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Kwa sababu hiyo, walijazwa sumu ya Shetani. Hawakuwa waaminifu tena kwa Mungu wala hawakumtii Mungu. Walikuwa wamepoteza mfano wa mtu ambaye Mungu alikuwa amemuumba hapo mwanzo. Ingawa miili yao bado ilikuwa hai, kwa mawazo ya Mungu, tayari walikuwa wamekuwa wafu wasio na roho. Hivi sasa, tunapopotoshwa zaidi na zaidi na Shetani. Tumejaa tabia potovu za kishetani kama vile kiburi, ubinafsi, udanganyifu, uovu na uroho. Imefikia kiwango ambapo tunapokabiliwa na kitu ambacho hakilingani na fikira zetu, tunalalamika kwa Mungu, kumhukumu Mungu, tunampinga Mungu na kumsaliti Mungu. Kwa mawazo ya Mungu, sisi ni wafu ambao hawana roho. Kutoka kwa hili, tunaweza kuona kwamba “mfu” inamaanisha wale wanaoishi chini ya ushawishi wa Shetani, wale walio na asili potovu ambazo humpinga Mungu na wale ambao ni maadui wa Mungu. Vinginevyo, “mtu aliye hai” inamaanisha wale ambao wameitupa tabia potovu ya shetani, wale ambao wamerejesha dhamiri zao na hisi, wale wanaomfahamu Mungu, wale ambao humtii Mungu na wale wanaompenda Mungu. Watu hawa wana nafasi ya Mungu ndani ya mioyo yao. Katika mambo yote wanaweza kutafuta ukweli, kuelewa makusudi ya Mungu, kuweka ukweli wa maneno ya Mungu katika vitendo na sio kutegemea tena sheria za Shetani za maisha. Wao ni watu ambao wameshinda ushawishi wa Shetani na wamerejea kwa Mungu. Hawa ni watu hai walio na roho na kwa kweli wamefufuliwa kutoka kwa wafu.

Baada ya kuelewa tofauti kati ya “mfu” na “mtu aliye hai,” baadhi ya ndugu wa kiume na wa kike wanaweza kuuliza, utabiri wa “ufufuo wa mfu” utatimizwaje? Kabla ya kujibu swali hili, hebu tuangalie mfano mmoja. Ingawa dhambi zetu zimelipiwa na Yesu na kusamehewa, kiini cha kutenda dhambi kwetu hakijatatuliwa. Bado tunaishi ndani ya tabia potovu ya shetani. Sisi hufanya dhambi na kuzikubali siku baada ya siku. Kwa mfano: tunashindwa kuzishika amri za Mungu na hatuwezi kuweka maneno ya Bwana katika vitendo. Sisi ni kama wale katika ulimwengu wa kidunia ambao hufuata mielekeo ya ulimwengu, wakitamani utajiri na furaha za kimwili. Sisi ni wenye kiburi na majivuno, wasio waaminifu na wadanganyifu na wenye ubinafsi na wabaya. Tunatawaliwa na asili yetu ya kishetani. Mara kwa mara sisi humkanusha Mungu na kumpinga Mungu. Sisi hupenda kujidhihirisha miongoni mwa halaiki. Sisi hujishuhudia ili wengine watuheshimu sana na tunashindania hadhi na Mungu. Kwa manufaa yetu wenyewe, tunaweza kufanya mambo ya udanganyifu, kusema uongo ili kuwadanganya watu na kupigana waziwazi na kufanya hila kwa siri na wengine. Tunaweza hata kuahidi viapo vya uongo na kutoa ahadi tupu mbele ya Bwana. Wakati midomo yetu inasema kwamba tunampenda Bwana, kimsingi, tunajadiliana na Bwana. Kwa nje, tunafanya kazi kwa bidii, tukiondoa na kutumia, lakini tunafanya mambo haya kwa matumaini ya kubadilishana na riziki ya Mungu na baraka. Sisi humwamini Mungu, lakini hatumheshimu Mungu kama mkuu. Hatuna nafasi ya Bwana katika mioyo yetu. Badala yake, sisi huwaabudu watu maarufu, watu wakuu, wachungaji na wazee wa kanisa n.k. Kama hatuwezi kutakasa tabia zetu potovu, tunawezaje kuwa watu walio hai na tunawezaje kupata idhini ya Mungu na kuingia katika ufalme wa mbinguni? Kwa sababu hiyo, bado tunamhitaji Mungu kutoa hatua moja zaidi ya wokovu.

Yesu alisema: “Bado ningali nayo mengi ya kuwaambieni, lakini hivi sasa hamwezi kuyavumilia. Hata hivyo, wakati yeye, Roho wa ukweli, atakapokuja, atawaongoza hadi kwenye ukweli wote: kwa maana hatazungumza juu yake mwenyewe; bali chochote atakachosikia, atakinena: na atawaonyesha mambo yajayo(Yohana 16:12-13). K wa dhahiri, Mungu atarudi katika siku za mwisho kuonyesha ukweli na kufanya hatua ya mwisho ya kazi Yake ya kuruzuku maisha kwa mwanadamu. Maneno ya Mwenyezi Mungu yanasema: “Ikiwa watu wanatamani kuwa viumbe hai, na kuwa na ushuhuda wa Mungu, na kuthibitishwa na Mungu, wanapaswa kukubali wokovu wa Mungu, wanapaswa kuwa watiifu katika hukumu na kuadibu Kwake, na wanapaswa kukubali kwa furaha kushughulikiwa na kupogolewa na Mungu. Ni hapo tu ndipo wataweza kuweka katika matendo ukweli wote unaohitajika na Mungu, na baada ya hapo ndipo wataweza kupata wokovu wa Mungu, na kuwa viumbe hai kabisa(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Je, Wewe ni Mtu Ambaye Amepata Uzima?). Katika siku za mwisho, ili kutuokoa kutoka kwa ushawishi wa Shetani, Mungu amepata mwili tena. Yeye hutumia jina la Mwenyezi Mungu kuonyesha kazi Yake ya hukumu ambayo huanza kutoka kwa nyumba Yake. Tumepitia hukumu na kuadibiwa, kushughulikiwa na kupogolewa na majaribu na kusafishwa na maneno ya Mungu. Kwa kweli tunaelewa ukweli wa upinzani wetu wenyewe na kupingana na Mungu na asili na kiini chetu cha kishetani. Wakati huo huo, tuna ufahamu kiasi wa tabia ya haki na takatifu ya Mungu. Tunaona kwamba wokovu wa Mungu ni wa utendaji sana. Aidha, tunachukia na kuisaliti tabia yetu wenyewe ya kishetani. Tuko tayari kuweka ukweli katika vitendo, kuyategemea maneno ya Mungu ili kuishi kama wanadamu, kutupa tabia yetu potovu na kuyaridhisha makusudi ya Mungu. Tumepokea ukweli ambao Mungu ameuonyesha na kuugeuza kuwa maisha yetu. Tumepata utii wa kweli kwa Mungu, upendo kwa Mungu na tunaishi kwa kudhihirisha sura kweli ya binadamu. Hivi ndivyo “mfu” anavyoweza kubadilika kuwa “mtu aliye hai.” Huu ni ufufuo kutoka kwa wafu. Hili pia linatimiza maneno ya Yesu: “Na haya ni mapenzi ya Baba ambaye amenituma, ya kuwa sipaswi kumpoteza hata mmoja kati ya wale wote ambao amenipa, lakini napaswa kumfufua katika siku ya mwisho(Yohana 6:39). Kwa dhahiri, “ufufuo” unafanikishwa kupitia kazi ya hukumu ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na sio wa kimiujiza kama watu wanavyoufikiri kuwa. Ndugu zangu, kile ambacho Mungu anataka ni watu walio hai na si wafu. Ni watu wanaoishi tu wanaoweza kumheshimu Mungu na kumshuhudia Mungu. Ni watu wanaoishi tu wanaostahili kuirithi ahadi ya Mungu—kuingia katika ufalme wa mbinguni. Alimradi tunaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho, tupitie maneno ya Mungu ya hukumu na kuadibu na kuukubali ukweli kama maisha yetu, tunaweza kufufuliwa kutoka kwa wafu!

Mshukuru Mungu! Utukufu wote ni kwa Mungu!

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp