Kuulewa Moyo wa Mungu Kunaweza Kuondoa Kuelewa Visivyo

18/10/2019

Na Chen Gang, Mkoa wa Hebei

Maneno ya Mungu yanasema, “Mamlaka ya juu, ukubwa, utakatifu, uvumilivu, upendo, wa Mungu na kadhalika—kila utondoti wa kila mojawapo ya vipengele vya tabia ya Mungu na kiini Chake unapata maonyesho ya vitendo kila wakati Anapoanza kazi Yake, zikiwa katika mapenzi Yake kwa binadamu, na pia zikitimizwa na kuonyeshwa kwa kila mtu. Licha ya kama umewahi kuzihisi awali, Mungu anamtunza kila mtu katika kila njia inayowezekana, kwa kutumia moyo Wake wa dhati, hekima, na mbinu mbalimbali ili kupashana mioyo ya kila mtu, na kuzindua roho ya kila mmoja. Huu ni ukweli usiopingika(Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I). Baada ya kusoma maneno ya Mungu, niliona kwamba kila kitu Anachofanya kimejaa upendo na rehema Yake na vile vile kutujali Kwake. Matendo yote ya Mungu ni ya faida sana kwetu, na ndiyo tunayohitaji sana; almradi tuyatafute na kuyapitia kwa bidii, tutahisi upendo huu Wake. Hata hivyo, kwa sababu ya kutojua kwangu kuhusu tabia na kiini cha Mungu, mara nyingi nilikuwa nikiishi katika hali ya kuelewa vibaya, tuhuma, na kujitetea dhidi ya Mungu, na sikuweza kumpa moyo wangu. Wakati wowote ambao kulikuwa na wajibu wa kutekelezwa, kila wakati nilijaribu kuukwepa au kukataa kuufanya, na hivyo kupoteza fursa nyingi za kupata ukweli. Wakati fulani uliopita, nikiwa nimekabiliwa na hali halisi na hukumu na kuadibiwa kutoka kwa maneno ya Mungu kulinisababisha nipate ufahamu fulani wa asili yangu mwenyewe ya kishetani na vile vile ufahamu fulani wa kweli wa kiini kizuri na cha kupendeza cha Mungu; ni hapo tu ndipo nilijiondolea baadhi ya kuelewa kwangu visivyo kumhusu Yeye.

Baada ya kuanza kumwamini Mungu, kila wakati nilipoona au kusikia kuhusu mtu yeyote kutimuliwa kutoka katika wajibu wa uongozi na kubadilishwa—wakati mwingine hata kutimuliwa kwa sababu ya kutenda uovu mwingi sana—kila mara ningekuwa nikipata hisia ambayo ni ngumu kueleza, na singeweza kujizuia kufikiria, “Kutimiza wajibu wa mtu katika nafasi ya uongozi ni jukumu kubwa; mtu anaweza kufutwa kazi na kubadilishwa kwa sababu ta kutoshughulikia jambo vizuri ipasavyo, na anaweza hata kuwa katika hatari ya kutimuliwa na kuondolewa. Inaonekana kwamba kadiri nafasi ya mtu ilivyo ya juu zaidi, ndivyo ilivyo hatarini zaidi. Kuna ukweli fulani katika misemo, ‘kuna upweke kule juu’ na ‘kadiri walivyo wakubwa, ndivyo waangukavyo kwa kishindo.’ Nadhani kutimiza wajibu ambao hauambatani na nafasi ya juu ni salama kidogo; almradi nisipandishwe cheo au kushushwa, nitakuwa sawa. Kwa njia hiyo naweza kuzuia kufanya matendo mengi maovu na kuwekwa wazi na kuondolewa kwa ajili yake, na kuwa na imani hadi mwisho lakini kuishia bila chochote.” Muda mfupi baada ya hapo, wakati wowote kanisa lilitaka kunipandisha cheo au kunipangia nishiriki katika uchaguzi, nilitoa kila aina ya vijisababu kujiondoa na kukataa. Polepole, ufa mkubwa wa kina ulijiunda kati yangu na Mungu. Wakati wa mkutano mwezi Aprili mwaka huu, kiongozi wangu aliniuliza, “Ndugu, uchaguzi wa kila mwaka wa wilaya yetu ndogo utafanyika hivi karibuni. Je, maoni yako ni yapi kuhusu jambo hilo?” Baada ya kusikia kuwa uchaguzi ungefanyika hivi karibuni, nilihisi mwenye wasiwasi na sikuwa na uhakika jinsi ya kujibu. Nilifikiria kuhusu jinsi ndugu wengine hapo zamani walivyokuwa wametimuliwa kazi na kubadilishwa kwa kutoweza kufanya kazi halisi, na hadi wa leo hawakuwa wameweza kutekeleza wajibu wao. Niliogopa kwamba kama ningechaguliwa, ningepatwa na jaala kama hiyo kama, wakati utakapofika, mimi pia singeweza kumaliza kazi yoyote halisi. Kwa wakati huo mambo yalikuwa mazuri; sikuwa tu na wajibu wa kutimiza, lakini pia sikuhitaji kuwa na wasiwasi juu ya kupoteza nafasi yangu na kubadilishwa. Nikiwa na mawazo haya akilini, nilimjibu kiongozi wangu kwa haraka, “Nina upungufu mwingi sana katika kila kipengele. Mimi pia huwa mwenye wahaka sana wakati wa mikutano na ndugu zetu. Pengine itafaa zaidi kwangu kuendelea kupata mazoezi zaidi katika wajibu wangu wa sasa, kwa hivyo sitagombea katika uchaguzi huu.” Kuona kwamba sikulipendelea sana wazo la kuchaguliwa, kiongozi wangu aliwasiliana nami mara kadhaa zaidi juu ya hoja hiyo kwa matumaini kwamba ningeshiriki katika uchaguzi uliokuwa unakaribia, lakini kila mara nilikataa kwa heshima.

Jioni moja siku chache baadaye, niliwatafuta viongozi wangu kwa sababu nilikuwa na jambo la kujadili nao. Walikuwa katikati ya kusoma barua kutoka kwa uongozi wa ngazi ya juu kuhusu uchaguzi. Nikiwa na woga mwingi sana, nilifikiria kimoyomoyo, “Nahitaji kukimbia nijifiche, la sivyo watataka kuwasiliana nami tena juu ya uchaguzi.” Kwa hivyo nilijificha bafuni na kupitisha wakati, lakini matokeo yake, nilipokuwa nikijikuna pahali pa mwasho, kwa bahati mbaya nikapasua uvimbe, na nikawa na damu kwenye mkono wangu wote. Niliipanguza haraka kwa kitambaa cha karatasi na kuweka shinikizo kwenye jeraha, lakini baada ya muda, kitambaa cha karatasi kilikuwa kimelowa chepe chepe. Ghafla, nilipigwa na bumbuazi: Nitafanyaje nisipoweza kuizuia damu kutoka? Huku nikiweka shinikizo kwenye kidonda kwa mkono mmoja, nilichukua hatua za haraka na nikaharakisha kurudi ndani ya chumba ili viongozi wangu waangalie na waone ni nini kinachoweza kufanywa ili kuzuia utokaji wa damu. Ndugu mmoja alilitazama na kusema, “Unavuja damu nyingi sana; haitakoma. Kadiri unavyolipanguza zaidi, ndivyo litakavyovuja damu zaidi!” Kusikia hili, nilihisi kutokuwa na uhakika hata zaidi: Je, lilikuwa jambo zito hivi? Je, uvimbe mdogo ungewezaje kuvuja damu nyingi vile? Kama singekomesha kuvuja damu huko, kungeendelea hadi siku inayofuata hadi niwe mkavu kwa kuishiwa na damu? Wimbi la woga, wasiwasi, na unyonge liliniingia ghafla, na sikujua la kufanya. Nilihisi kana kwamba hewa ilikuwa karibu kuganda. Wakati huo tu, nilianza kufahamu uwezekano kwamba tukio la ghafla la siku hiyo halikuwa la nasibu hata kidogo, na kwamba lazima niharakishe na kutafakari juu ya matendo yangu ili niweze kujijua vema zaidi! Kisha nikatulia na kutafakari kama nilikuwa nimemkosea Mungu kwa njia yoyote hivi karibuni, lakini haijalishi nilivyojaribu kutafakari, sikuweza kufikiria chochote. Kisha nikakumbuka kifungu cha matamko ya Mungu: “Watu wanapomkosea Mungu, inaweza isiwe kwa tukio moja, au kitu kimoja walichokisema, bali ni kwa sababu ya mtazamo walionao na hali waliyomo. Hili ni jambo la kutisha sana(Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VII). Mwongozo wa maneno ya Mungu ulinileta mbele Yake kutafuta ukweli: “Mungu! Nimekuwa kipofu na mpumbavu sana. Siwezi kuelewa nilichofanya kukukosea. Tafadhali, nionyeshe njia; nifichulie mapenzi Yako, ili niweze kugundua ukaidi na upinzani wangu. Ningependa kutubu mbele Yako.” Baada ya kumaliza kuomba, nilihisi nikiwa mwenye amani zaidi, na nikaanza kutafakari juu ya matendo na mawazo yangu ya zamani, nikishangaa ni wapi ambapo huenda nilipotea kutoka kwa mapenzi ya Mungu. Wakati huo tu, ghafla nilikumbuka jinsi nilivyokuwa nimetenda na mtazamo niliokuwa nao kuhusu uchaguzi: Viongozi wangu walikuwa wamenitafuta mara kwa mara ili kuwasiliana maoni yao kwamba nilipaswa kushiriki katika uchaguzi, lakini siku zote nilikuwa nikidumisha fikira zangu mwenyewe; nikiogopa kuwa ningefichuliwa kama ningefanya kazi duni ya kutimiza wajibu wangu, nilikuwa nimebuni sababu na visingizio vya kila aina tena na tena ili nikatae kushiriki. Mtazamo wangu haukuwa ule wa kukubali na kutii, hata kidogo. Nilijua vizuri kuwa uchaguzi wa kidemokrasia uliofanywa na kanisa ulihitajika ili kutekeleza mipangilio ya kazi; hii ilikuwa sehemu muhimu ya kazi ya familia ya Mungu, na ilikuwa na mapenzi ya Mungu. Hata hivyo, sikuwa nimetafuta ukweli hata kidogo; ili kujilinda, nilikuwa nimeukwepa uchaguzi mara kwa mara na kukataa kugombea uchaguzi. Mtazamo wa aina hii ambao nilikuwa nao kwa kina—wa kuwa adui wa Mungu—ulinifanya niwe mwenye kuchukiza na kukirihiwa machoni Pake, na hata zaidi, ulikuwa umemfanya Ahuzunike na kuvunjika moyo. Kukumbana kwangu ghafla na shida ya aina hii ilikuwa njia ya Mungu kunifundisha nidhamu. Nilipogundua hili, niliona kuwa tabia ya haki ya Mungu haiwezi kustahimili kukosewa na wanadamu, kwa hivyo nilitaka kuigeuza hali hii yangu mbaya na kutubu mbele ya Mungu. Kwa hivyo niliwapa viongozi wangu maelezo yote ya kila kitu ambacho nilikuwa nimetafakari kuhusu, kuanzia mwanzo hadi mwisho. Baada ya kunisikiliza, ndugu huyo alishiriki nami juu ya mtazamo na ufunuo aliokuwa nao aliposhiriki katika uchaguzi. Mshukuru Mungu! Tukio hili lilikuwa limenipa funzo, na saa moja baadaye, uvimbe wangu uliacha kutokwa na damu. Hili lilinifanya nigundue kuwa wakati nilikuwa nikiishi katika hali ya upotovu na ukaidi, Mungu alinionyeshea tabia Yake ya haki, isiyoweza kukosewa; na wakati nilikuwa nimemrudia kwa hamu ya kutafuta ukweli, Alikuwa amenifichulia uso Wake wenye tabasamu, na nilikuwa nimeonja kuwa tabia ya Mungu ni wazi kabisa na ya uhai.

Baadaye, sikuwa na budi ila kutafakari kuwa kila wakati kanisa lilifanya uchaguzi, kila wakati nilikuwa nimetafuta kuuepuka na kutoa visingizio ili nijiondoe. Sikutaka kugombea, nikihofia kwamba kama ningalichaguliwa katika nafasi ya uongozi na nifanye jambo dhidi ya Mungu, ningetimuliwa na kuondolewa. Kwa nini mawazo haya yalikuwa daima yakipita kichwani mwangu? Wakati wa ibada zangu za kiroho, kwa kufahamu nilitafuta maneno ya Mungu juu ya mada hii, ili nipate kuyala na kuyanywa. Siku moja nilisoma tamko hili la Mungu: “Wengine husema, ‘Kumwamini Mungu mbele Yake—unapaswa kuwa mwangalifu sana! Ni kama kuishi ukingoni!’ Wengine husema, ‘Kumwamini Mungu ni kama huo msemo wa wasioamini, “Kuwa karibu na mfalme ni kama kuwa karibu na chui.” Ni jambo baya sana! Ukisema au kufanya kitu kimoja kibaya, basi utaondolewa; utatupwa kuzimu na kuangamizwa!’ Je, misemo kama hiyo ni sahihi? Je, msemo unaosema, ‘Kuwa karibu na mfalme ni kama kuwa karibu na chui,’ hutumiwa zaidi wakati gani? Na ‘lazima uwe mwangalifu sana mbele ya Mungu’ kunamaanisha nini? Je, ‘kuishi ukingoni’ kunamaanisha nini? Nyote mnapaswa kujua maana halisi ya misemo hii; yote inaashiria hatari kubwa. Ni kama mtu kumfuga simba au chui: Kila siku ni lazima uwe mwangalifu sana au kuishi ukingoni; maneno hayo yanaashiria hali ya aina hii. Asili hiyo kali ya chui na simba inaweza kujitokeza wakati wowote. Wao ni wanyama wakatili wasio na upendo kwa wanadamu, bila kujali ni miaka mingapi wanayoweza kuwa wameshirikianaa nao. Ikiwa wanataka kukula wewe, watakula; wakitaka kukudhuru, watakudhuru. Kwa hivyo, ni sawa kutumia misemo kama hiyo kuelezea kumwamini Mungu ni kuko vipi? Je, wakati mwingine hamfikirii kwa njia ifuatayo? ‘Kumwamini Mungu kweli ni lazima uwe mwangalifu sana; hasira hiyo Yake inaweza kuibuka mara moja. Anaweza kukasirishwa wakati wowote, na Anaweza kumwondoa mtu kutoka katika nafasi yake wakati wowote. Yeyote asiyependwa na Mungu atafunuliwa na kuondolewa.’ Je, hivi ndivyo ilivyo? (La.) Inaonekana kwamba mmekuwa na uzoefu na hili na mnalielewa, kwa hivyo hampaswi kudanganywa. Huu ni uongo; ni jambo la upuuzi kabisa kusema(“Mpe Mungu Moyo Wako wa Kweli, Na Unaweza Kupata Ukweli” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). “Watu wengine husema, ‘Usiwe kiongozi, na usiwe na hadhi. Watu wamo hatarini punde wanapopata hadhi, na Mungu atawafunua! Mara tu watakapofunuliwa, hata hawatastahili kuwa waumini wa kawaida, na hawatakuwa tena na nafasi ya kuokolewa. Mungu siye mwenye haki!’ Hili ni jambo la aina gani kusema? Kwa kujaribu sana, linawakilisha kumwelewa Mungu visivyo; mbaya zaidi, ni kumkufuru Mungu(“Ili Kutatua Tabia Potovu ya Mtu, Mtu Lazima Awe na Njia Maalum ya Kutenda” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). Mstari kwa mstari, maneno ya Mungu yaliniacha nikiwa nimeguswa sana, kwa kuwa yaliielezea hali yangu kwa usahihi. Kwa kweli sikuwa nimesema wazi kuwa kumwamini Mungu kulikuwa “like being near a tiger” au “living on a knife’s edge,” lakini nikiangalia mtazamo wangu kwa uchaguzi wa kanisa, nilikuwa mwenye kujitetea kabisa na nilijawa na kutoelewa. Hii ilionyesha kuwa hiyo ndiyo iliyokuwa hali niliyokuwa nikiishi kwayo hasa. Baada ya kuona maisha ya mateso na dhiki ya baadhi ya ndugu ambao walikuwa wametimuliwa kutoka katika nafasi za uongozi, baadhi ambao walikuwa hata wametimuliwa kwa sababu ya kufanya maovu mengi, siku zote nilikuwa nimekwepa kutoka kwa wazo la kutimiza wajibu wangu kama kiongozi, nikitamani badala yake kuweka umbali wa heshima, kwa sababu kutoka kwa mtazamo wangu, uongozi ulikuja pamoja na hadhi, na pamoja na hilo ilikuja hatari ya kuwekwa wazi na kuondolewa. Hata nilifika kiwango cha kuwa mwangalifu na mwenye woga sana na mwenye kusita ninapokamilisha wajibu wangu mwenyewe, na sikuwa nimewahi kuwa na haja na uchaguzi, nikiogopa sana kuwa kama ningechaguliwa kuwa kiongozi na nifanye kosa, ningetimuliwa kazi na kuondolewa kama matokeo. Katika mawazo yangu, nilikuwa nikimwona Mungu kwa njia ile ile niliyowaona maafisa wa Chama cha Kikomunisti cha China walioshika madaraka; sikuthubutu kumkaribia sana au kumkasirisha. Nilikuwa nimedhani kwamba mtu yeyote aliyemkosea lazima angepata msiba mkubwa, na hata nilikuwa nimedhani kuwa wale ndugu ambao walikuwa wametimuliwa na kuondolewa walijiletea shida kwa kutumikia katika nafasi za uongozi. Nilikuwa nimeona “viongozi”, nafasi iliyowekwa katika muundo wa utawala wa familia ya Mungu, kama njia ya kuwafunua na kuwaondoa watu. Ni sasa tu, kupitia ufunuo wa neno la Mungu, ndipo niligundua kuwa fikira hizi ambazo nilikuwa nikishikilia zilifunua ukosefu kamili wa ufahamu wa kiini kitakatifu cha Mungu. Kisio hizi ambazo nilikuwa nazo juu ya Mungu zilikuwa zenye kukufuru sana! Nilipogundua hili, nilihisi hofu ikinizunguka, na sikuwa na budi ila kupiga magoti mbele ya Mungu katika sala: “Mungu! Ingawa nimekufuata kwa miaka mingi, sikujui Wewe. Hayo mawasiliano kutoka kwa ndugu zangu ya kunifanya nishiriki katika uchaguzi yalikuwa fursa ambazo Ulikuwa umenifadili ili kunifundisha, na kunitakasa na kunibadilisha—lakini sikukosa tu kuelewa mapenzi Yako, kwa kweli nilikataa na kujaribu kuyaepa, nikiwa mwenye kujitetea kabisa na mwenye kutokuelewa. Sikukutendea kama Mungu hata kidogo. Huo mtazamo wangu ulikuwa tu wa mtu asiyeamini—aina ya kishetani kweli! Mungu! Usingenifunua kwa njia hii, nisingewahi kutafakari juu ya maswala yangu mwenyewe, na bado ningekuwa naishi katika hali ya uhasama na kutoelewa. Kama hilo lingeendelea, mimi ningechukiwa, kukirihiwa na kudharauliwa na Wewe. Mungu! Sasa niko tayari kutubu. Tafadhali, nielekeze kwa ufahamu wa ukweli na wa mapenzi Yako.…”

Baada ya hayo, nilisoma maneno zaidi ya Mungu: “Punde watu wanapopata hadhi—bila kujali wao ni akina nani—basi wanakuwa wapinga Kristo? (Ikiwa hawafuatilii ukweli, basi watakuwa wapinga Kristo, lakini ikiwa wanafuata ukweli, basi hawatakuwa wapinga Kristo.) Kwa hivyo, siyo dhahiri. Kwa hivyo, je, wale ambao huitembea njia ya wapinga Kristo hatimaye wameshikwa na hadhi? Hilo hufanyika wakati watu hawachukui njia sahihi. Wana njia nzuri ya kufuata, lakini hawaifuati; badala yake, wao hufuata njia ovu. Hii ni sawa na jinsi watu wanavyokula: Wengine hawali chakula kinachoweza kuipa miili yao afya na kudumisha maisha yao ya kawaida, na hutumia dawa badala yake. Mwishowe, kutumia dawa huwafanya wazizoee na mwoshowe zinawaua. Je, hili si chaguo ambalo watu hufanya wenyewea?(“Ili Kutatua Tabia Potovu ya Mtu, Mtu Lazima Awe na Njia Maalum ya Kutenda” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). Kisha nikasoma ushirika mwingine ambao ulisema, “Kwa nini watu wengi sana huwekwa wazi wakifanya kila aina ya uovu kutumia nafasi na mamlaka yao? Sio kwa sababu nafasi yao inawaumiza. Shida ya msingi ni kiini cha asili ya mwanadamu. Nafasi kwa hakika inaweza kuwafunua watu, lakini kama mtu mwenye moyo mzuri ana nafasi ya juu, hatatenda maovu kadhaa” (“Unapaswa Kupata Uzoefu na Kuingia kwa Uhalisi wa Ukweli wa Neno la Mungu Ili Uweze Kupata Ukamilifu wa Mungu” katika Mkusanyiko wa Mahubiri—Ruzuku ya Maisha). Maneno ya Mungu na ushirika huu uliniruhusu nitambue mambo fulani. Kama ilivyotokea, wale wafanya kazi wenza na viongozi ambao walikuwa wametimuliwa na kuondolewa hawakutimuliwa nyadhifani kwa sababu ya nafasi zao za uongozi, lakini kwa sababu wakati wa kutekeleza wajibu wao, walikuwa wameshindwa kufuatilia ukweli bila kukoma au kutembea kwenye njia sahihi; kwa hivyo walikuwa wamewekwa wazi na kuondolewa. Sikuwa na budi ila kufikiria juu ya viongozi na wafanyakazi wenza karibu nami ambao walikuwa wamewekwa wazi. Ndugu mmoja alikuwa hasa mwenye kujidai, na hakuwa ametimiza wajibu wake kulingana na kanuni. Alikuwa amewapandisha vyeo watu ambao walikuwa na vipaji na sifa lakini hawakuwa na uhalisi wa ukweli kwa uhuru ili watekeleze wajibu wa uongozi. Hakuwa amekubali ukumbusho na msaada wa mara kwa mara kutoka kwa ndugu, na kwa sababu hiyo, alikuwa ameleta usumbufu katika maisha ya kanisa, akiwazuia ndugu kupata uingiaji katika maisha. Ndugu huyu alikuwa ametegemea sana maoni yake mwenyewe, hata kufikia hatua ya kupuuza ushauri wa wafanyakazi wenzake. Alisisitiza kuweka pesa na mali ya thamani ya kanisa ndani ya nyumba ambayo ilikuwa na hatari za kiusalama, jambo ambalo lilisababisha yote kukamatwa na Chama cha Kikomunisti cha China. Kulikuwa pia na dada ambaye alikuwa akihangaikia hadhi sana, na alipokuwa akitimiza wajibu wake kama mfanyakazi mwenza, hakuweza kukubali ukosolewaji unaojenga kutoka kwa kila mtu. Alikuwa hata amewasingizia na kulipiza kisasi dhidi ya wale ndugu ambao walikuwa wamempa ushauri, na alikuwa amekataa kukubali ushirika na msaada kutoka kwa wakubwa wake mara nyingi. Mwishowe, alikuwa amepewa onyo, lakini bado hakutafakati juu ya matendo yake ili ajijue, sembuse kukubali ukweli; alikuwa hajawahi kutubu au kubadilika, na badala yake alitembea katika njia ya mpinga Kristo kwa ukaidi.… Mifano hii ya kutofaulu ilinifanya nione kuwa kanisa halikuwa limemfukuza au kumwondoa mtu yeyote bila sababu nzuri. Ni baada tu ya kuchambua kwa uangalifu jinsi watu hawa waliotimuliwa na kuondolewa walivyokuwa wametenda muda huo wote ndipo niliona kwamba wengi wao walikuwa na ukaidi mzito mno katika tabia zao na hawakuwa wamewahi kuendesha kazi ya kanisa kulingana na kanuni za ukweli. Wote walikuwa wamefanya tu jinsi walivyopenda, na waliiishia kusababisha katizo na usumbufu katika kazi ya kanisa, wakiwazuia kwa uzito sana ndugu wengine kufikia kuingia katika maisha. Hatimaye, ilibidi wafutwe kazi na kubadilishwa. Ni wazi kuwa, kabla ya mtu yeyote kutimuliwa kazini, Mungu alikuwa amempa nafasi za kutosha za kutubu, na ndugu walikuwa wamewasaidia na kuwaungwa mkono mara nyingi; ilikuwa tu kwamba viongozi hao walikuwa hawajawahi kuonyesha nia yoyote ya kubadilika, na walikuwa wameingilia kati, kusumbua, na kuzuia kazi ya kanisa kwa uzito kabla ya kutimuliwa na kubadilishwa hatimaye. Lawama yote ya kushindwa kwao ilikuwa juu yao, sivyo? Je, haya hayakuwa matunda machungu ya matendo yao ya hatua kwa hatua? Hata hivyo, kutokana na kutofaulu na kuanguka kwao, sikuwa nimetambua njia ya makosa ambayo watu hawa walikuwa wakiifuata au kuona wazi chanzo cha upinzano wao dhidi ya Mungu, na baadaye sikuwa nimetafakari juu ya vitendo vyangu mwenyewe na kutumia mfano wao kama onyo kwangu. Pia sikuwa nimejua kwamba tabia ya Mungu ni isiyokosewa, kwa hivyo sikuwa nimekuza uchaji Mungu ambao ungenizuia kufuata nyayo zao; badala yake, nilikuwa nimeibua hali ya kutoelewa na kujitetea dhidi ya Mungu. Nilikuwa nimeuchukua uovu wote na kumwekea Mungu. Niliweza kuona kwamba kwa kweli nilikuwa mjinga na kipofu, mwenye kudharauliwa na mwenye kusikitisha, na kweli nilikuwa nimemwumiza Mungu kwa kina. Pia nilikumbuka kwamba sasa kulikuwa na kikundi cha watu kanisani ambao, licha ya kuwa hawakuwahi kushikilia nyadhifa zozote za juu, walikuwa wameendelea kushindwa kufuata ukweli na kusababisha katizo na usumbufu kanisani na hawakutimiza malengo yao vizuri; vivyo hivyo, wao, pia, walikuwa wamewekwa wazi na kuondolewa na Mungu. Utambuzi huu ulinipa ufahamu dhahiri zaidi kwamba wakati tunamfuata Mungu, ikiwa tunawekwa wazi au kuondolewa au la hakuhusiani na wajibu upi tunaotimiza au ni nafasi gani tunayoshikilia. Tusipofuatilia ukweli au kutembea kwenye njia ya mabadiliko katika tabia zetu, basi bila kujali ni nafasi gani tunazoweza kuwa tunashikilia au la, sote tunaweza kudhibitiwa na tabia ya Shetani, na wakati wowote tunaweza kufanya vitu ambavyo vinamkosea au kumpinga Mungu na kwa hivyo tuwekwe wazi na kuondolewa. Hili lilikuwa thibitisho sahihi la maneno ya Mungu: “Kuwa na Tabia Isiyobadilika Ni Kuwa katika Uadui na Mungu.” Nashukuru nuru na mwongozo wa Mungu, ambao uliniruhusu nipate ufahamu na utambuzi fulani wa maoni mabaya ambayo nilikuwa nimeshikilia, na vile vile kufahamu umuhimu wa kufuatilia ukweli wakati namwamini Mungu na kujitahidi kwa ajili ya mabadiliko katika tabia. Wakati huo huo, nilikuwa na ufahamu wa jinsi nilivyokuwa mpuuzi na mjinga kuishi ndani ya mawazo na fikira zangu potovu.

Baadaye, nilisoma kifungu kingine katika ushirika ambacho kilienda hivi: “Nilimuuliza ndugu, ‘Je, umepiga hatua yoyote katika miaka michache iliyopita?’ Akasema, ‘Maendeleo makubwa zaidi niliyoyafanya yalitokana na kutimuliwa huko kutoka kazini ambako nilipitia.’ Kwa nini alifanya maendeleo makubwa zaidi kutokana na kutimuliwa? Bila shaka alikuwa ameomba kwa dharura mbele za Mungu, na hakika alikuwa ametumia wakati mwingi kutafakari juu ya matendo yake na kujijua mwenyewe. Pia alikuwa tayari kutubu, na hakutaka kutupiliwa mbali na Mungu. Kuomba kwa dhati kwa Mungu kulileta nuru na mwangaza mwingi, na vile vile kujijua; alipata kugundua jinsi alivyokuwa ametenda na kufanya kwa miaka, na ni njia gani ambayo alikuwa akichukua. Kwa njia ya matukio haya hasi ya kujifunza, aligundua hasa jinsi anavyopaswa kuwa akimwamini Mungu na jinsi anavyopaswa kufuatilia ukweli. Baada ya hapo, alifanya toba ya kweli mbele za Mungu, na alikuwa tayari kufanya kazi kwa bidii katika ufuatiliaji wake wa ukweli, kutii hukumu na kuadibu kwa Mungu, na kustsahi mipangilio Yake. Kwa njia hii, safari yake ya kumwamini Mungu ilifanywa upya, na akaenenda rasmi kwenye njia ya imani. Kwa hivyo, unaweza kuuliza ikiwa kutimuliwa kama huko kuna faida yoyote au la, na ikiwa kwa kweli ni njia ya kuwaletea watu wokovu au la” (Ushirika kutoka kwa Aliye Juu). Kutoka kwa ushirika huu, niliweza kuona rehema na wokovu mkuu ambao Mungu alileta kwa watu. Wengine walikuwa wametimuliwa na kanisa kwa sababu ya matendo maovu waliyokuwa wamefanya, lakini almradi walitubu kwa dhati na walikuwa tayari kukubali na kutii ufunzaji nidhamu na kuadibu kwa Mungu, watafakari kujihusu ili wajijue vema, na kuanza kufuatilia ukweli, basi bado kulikuwa na tumaini la wokovu wao. Wakati huo huo, nilikuja kuelewa kwamba hukumu kali ya Mungu, njia za kuwashughulikia watu, kuadibu, na kufunza nidhamu pia zilikuwa ni aina za wokovu kwa watu ambao walitubu kwa kweli; kusudi lao lilikuwa kuwawezesha watu kujitafakari vema zaidi na kuelewa asili yao ya kishetani ambayo iliwasababisha wamkatae Mungu na kumwona kama adui. Ilikuwa kuwawezesha wajichukie kwa kweli na kuinyima miili yao ili waweze kusababisha uchaji wa kuogofya kwa Mungu na kuenenda katika njia ya kufuatilia ukweli. Kwa watu ambao wana imani katika Mungu kwa dhati na hufuatilia ukweli, bila kujali kile ambacho wamepitia—iwe walifutwa na kubadilishwa, au walitimuliwa, au nini—hakuna chochote kati ya hivi ambacho kilikuwa kuwekwa wazi au kuondolewa, lakini badala yake zilikuwa hatua muhimu katika njia zao kuelekea kumwamini Mungu! Bila kujua, nilikumbushwa kuhusu kifungu cha maneno ya Mungu: “Kutofaulu na kuanguka mara nyingi si jambo baya; na kufunuliwa pia si jambo baya. Iwe umeshughulikiwa, kupogolewa, au kufunuliwa, lazima ukumbuke hili wakati wote: Kufunuliwa hakumaanishi kuwa unashutumiwa. Kufunuliwa ni jambo zuri; ni fursa bora zaidi kwako kupata kujijua. Kunaweza kuuletea uzoefu wako wa maisha mabadiliko ya mwendo. Bila hilo, hutamiliki fursa, hali, wala muktadha wa kuweza kufikia ufahamu wa ukweli wa upotovu wako. Kama unaweza kujua vitu vilivyo ndani yako, vipengele hivyo vyote vilivyofichika ndani yako ambavyo ni vigumu kutambua na ni vigumu kufukua, basi hili ni jambo zuri. Kuweza kujijua mwenyewe kweli ndiyo fursa bora zaidi kwako kurekebisha njia zako na kuwa mtu mpya; ni fursa bora kwako kupata maisha mapya. Mara tu unapojijua mwenyewe kweli, utaweza kuona kwamba ukweli unapokuwa maisha ya mtu, ni jambo la thamani kweli, na utakuwa na kiu ya ukweli na kuingia katika uhalisi. Hili ni jambo zuri sana! Kama unaweza kunyakua fursa hii na ujitafakari mwenyewe kwa bidii na kupata ufahamu wa kweli kujihusu kila unaposhindwa au kuanguka, basi katikati ya uhasi na udhaifu, utaweza kusimama tena. Mara tu unapovuka kilele hiki, basi utaweza kuchukua hatua kubwa mbele na kuingia katika uhalisi wa ukweli(“Ili Kupata Ukweli, Lazima Ujifunze Kutoka kwa Watu, Mambo, na Vitu Vinavyokuzunguka” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). Nilipofikiria kuhusu hili, nilipata ufahamu wa kina hata zaidi kuhusu mapenzi ya Mungu: Iwe Anatupiga, kutufundisha nidhamu, au kutufukuza na kututimua, kila kitu Anachofanya kwetu huamuliwa kwa kutegemea tabia yetu wenyewe na kiini cha potovu. Kila kitu ambacho Mungu hufanya kinanuiwa kuwatakasa na kuwabadilisha watu; kwetu sisi, vitu hivi vyote ni wokovu, na vyenye manufaa makubwa zaidi. Wakati wote huo, nilikuwa nimeuangalia wajibu wa uongozi kwa woga kwa sababu watu hao walikuwa wamewekwa wazi, kutimuliwa, na kuondolewa, na nilikuwa nimejionya mwenyewe kutowahi kukubali kutekeleza wajibu uliokuja na cheo, kwa sababu kwa namna hiyo singeanguka chini au kushindwa, wala singeishi katika usafishaji wenye uchungu. Tabia ya haki ya Mungu inajumuisha hukumu, kuadibu, kurudi, na ufunzaji nidhamu wetu, lakini pia inajumuisha uvumilivu na ustahimilivu na upendo mkubwa zaidi kwa ajili yetu. Sikuwa nimewahi kuyaona mambo haya hapo awali, badala yake niliishi katika hali ya kuelewa vibaya na kisio kwa Mungu ambayo ilitegemezwa kwa msingi wa mawazo na fikira zangu mwenyewe. Sikuwa radhi kushiriki katika uchaguzi, sembuse kuwa na hamu yoyote ya kutimiza wajibu wa uongozi, na kwa sababu hiyo, nilikuwa nimepoteza fursa nyingi za kupata ukweli na kumjua Mungu. Ni sasa tu ndipo nilipoona wazi kwamba fikira zangu za awali”, “kuna upweke kule juu” na “kadiri walivyo wakubwa, ndivyo waangukavyo kwa kishindo.” yalikuwa maoni ya ujinga ya Shetani ambayo yalikuwa yakizuia sana ufuatiliaji wangu wa ukweli na kutafuta kwangu kumjua Mungu. Nilimshukuru Mungu kwa nuru na mwongozo Wake, ambao ulikuwa umeniruhusu nijiondolee dhana fulani potovu ambazo nilikuwa nazo Kwake. Wakati huo huo, nilihisi jinsi kweli nilivyokuwa mbaya, mwenye kuchukiza, mkaidi, na mjinga kweli!

Baadaye, sikuweza kujizuia ila kuwaza kwa kujifikiria kwa nini nilikuwa nikijilinda sana dhidi ya Mungu na ni asili ipi iliyonidhibiti kufanya hivyo. Nilisoma kifungu cha maneno ya Mungu, ambacho kilisema, “Na ikiwa unaweza kumshuku Mungu na kumkisia utakavyo, basi wewe bila shaka ni mdanganyifu zaidi kati ya wanadamu wengine. Mnakisia iwapo Mungu anaweza kuwa kama mwanadamu: mwenye dhambi isiyosameheka, mwenye tabia ndogondogo, anayependelea na asiye na mantiki, aliyekosa hisia ya haki, mwenye mbinu ovu, mdanganyifu na mjanja, na pia anayefurahishwa na uovu na giza, na kadhalika. Si sababu ambayo mwanadamu ana mawazo kama haya kwamba hana hata ufahamu mdogo wa Mungu?(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Jinsi ya Kumjua Mungu Duniani). Pia nilisoma ushirika uliosema, “Wale wote ambao wanajitetea dhidi ya Mungu wanapokabiliwa na majaribu ni wadanganyifu, wabinafsi, na wachoyo, na wanajifikiria wenyewe tu na hawamshikilii Mungu mioyoni mwao. Watu kama hao ndio wanaopambana dhidi ya Mungu. Mara tu wanapokumbana na shida, wao hujitetea dhidi ya Mungu na kumchunguza, wakijiuliza, ‘Mungu alimaanisha nini na hili? Kwa nini aliruhusu hili linitendekee?’ Kisha wao hujaribu kujadiliana na Mungu. Je, watu kama hao si wasio na haki katika nia zao? Je, kufuatilia ukweli ni rahisi kwa watu kama hao? La, sio. Hawa sio watu wa kawaida; wao wana asili ya mapepo, na hawawezi kabisa kushirikiana na mtu yeyote” (“Maswali na Majibu” katika Mahubiri na Ushirika Kuhusu Kuingia Katika Maisha XIII). Maneno ya Mungu na ushirika huu vilifichua kiini cha shida yangu ya kujitetea dhidi ya Mungu na kisio kumhusu Mungu. Kwa sababu kiasili nilikuwa mjanja kupindukia, kila wakati kanisa lilipotaka kunikuza na kunipandisha cheo, sikushindwa tu kuelewa mapenzi ambayo Mungu alikuwa nayo kwangu au kuelewa nia Yake yenye uchungu, lakini, kinyume na hilo, nilidhani kwamba kutekeleza wajibu wa uongozi kungekuwa hatari sana na kwamba mara tu ningekuwa na wadhifa na nitende uovu, ningekuwa katika hatari ya kutimuliwa kazini na kuondolewa kila wakati. Nilifikiria kuhusu jinsi nilivyokuwa nikifurahia mbingu na dunia na vitu vyote ambavyo Mungu alikuwa ameumba—hadi jua na mvua—pamoja na unyunyizaji na ruzuku yote kutoka kwa matamko mengi ya Mungu, lakini sikuwa nimejaribu angalau kuuthamini upendo na wokovu Aliokuwa nao kwa watu. Kila wakati nilikuwa nikijitetea dhidi Yake na kumwumiza, nikishuku kuwa Mungu alikuwa mdogo kama wanadamu na asiye na huruma au upendo kwetu. Kwa kweli nilikuwa mdanganyafu na mwenye kustahili dharau sana, na sikuwa nimeonyesha hata mfano mdogo kabisa wa mwanadamu maishani mwangu. Wakati huo tu, nilihisi kuwa mwenye hatia sana, na mara nyingine tena nikakumbuka maneno ya Mungu: “Mungu anafanya kimyakimya kila kitu kwa ajili ya binadamu, akifanya kimyakimya kupitia ukweli, uaminifu, na upendo Wake. Lakini siku zote Hana hofu au majuto yoyote kwa yale yote Anayofanya, wala hahitaji mtu yeyote kumlipa Yeye kwa njia yoyote au kuwa na nia za kuwahi kupokea kitu kutoka kwa wanadamu. Kusudio tu la kila kitu Alichowahi kufanya ni ili Aweze kupokea imani na upendo wa kweli kutoka kwa wanadamu(Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I). “Mungu aliwaumba wanadamu; licha ya kama wamepotoka au kama wanamfuata Yeye, Mungu hushughulikia binadamu kama wapendwa Wake wanaothaminiwa zaidi—au kama vile binadamu wangesema, watu walio wapenzi Wake sana—na wala si kama vikaragosi Wake(Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I). “Kuanzia mwanzo hadi leo, ni binadamu tu ambaye ameweza kuzungumza na Mungu. Yaani, miongoni mwa viumbe wote walio hai na viumbe wa Mungu, hakuna yeyote isipokuwa binadamu ameweza kuzungumza na Mungu. Binadamu anayo masikio yanayomwezesha kusikia, na macho yanayomwezesha kuona; anayo lugha na fikira zake binafsi, na pia anao uhuru wa kuamua chochote. Anamiliki kila kitu kinachohitajika kusikia Mungu akiongea, na kuelewa mapenzi ya Mungu, na kukubali agizo la Mungu, na hivyo basi Mungu anayaweka matamanio yake yote kwake binadamu, Akitaka kumfanya binadamu kuwa mwandani Wake ambaye anayo akili sawa na Yeye na ambaye anaweza kutembea na Yeye. Tangu Alipoanza kusimamia, Mungu amekuwa akisubiria binadamu kumpa moyo wake, kumwacha Mungu kuutakasa na kuufaa ipaswavyo, kumfanya yeye kumtosheleza Mungu na kupendwa na Mungu, kumfanya yeye kumstahi Mungu na kujiepusha na maovu. Mungu amewahi kutazamia mbele na kusubiria matokeo haya(Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II). Kati ya mistari na maneno ya matamko ya Mungu mlifichuliwa upendo na utunzaji kwa binadamu, na vile vile tumaini na matarajio. Mungu huwatendea wanadamu kama mama mwenye huruma anavyowatendea watoto wake, Akitupenda kwa dhati na kumtunza kila mmoja wetu vizuri. Ili kulipata kundi la wanadamu ambao wanalingana na mapenzi Yake, Mungu amepata mwili mara mbili, akivumilia fedheha kubwa na kulipa gharama kubwa zaidi kwa sababu ya kuleta ukombozi na wokovu kwa binadamu. Licha ya ukaidi, suitafahamu, na kulalamika ambako tumeonyesha kwa Mungu, Ameendelea, kwa uvumilivu na ustahimilivu mwingi, kufanya kazi ya wokovu kwa wanadamu kwa kimya. Mungu amekuja kati yetu kuonyesha ukweli, akitunyunyizia na kuturuzuku na kutuongoza, kwa matumaini kwamba siku moja tunaweza kuelewa nia Zake nzuri katika kuwaokoa watu na kumpa Mungu mioyo yetu, kutii hukumu na kuadibu Kwake, kutupilia mbali tabia zetu potovu, na kubadilika kuwa watu ambao Mungu amewaokoa ambao wanamcha Yeye na kuepukana na maovu. Niliweza kuona kwamba kiini cha Mungu ni kizuri na cha kupendeza sana, na upendo Wake kwa binadamu ni wa kweli kabisa! Mimi, kwa upande mwingine, nilikuwa kipofu na mpumbavu, nikikosa hata chembe ya ufahamu kumhusu Mungu; sembuse kuelewa nia Zake nzuri. Nilikuwa mwenye kujitetea na kumwelewa Mungu visivyo, nikikataa wokovu Wake bila huruma kila wakati, nikimwepa na kujitenga na Mungu kana kwamba Yeye ni adui, na kumpa tu uchungu na mateso. Hata hivyo, Mungu hakuwa amelenga ukaidi, upumbavu, na ujinga wangu, lakini badala yake Alikuwa ameweka mazingira ambayo yangenirudi na kunidundisha nidhamu. Alikuwa pia Amenipa nuru na kunielekeza kwa njia ya maneno Yake, na hivyo kuniondolea ujinga na suitafahamu yangu kuelekea Kwake na kuniwezesha kumpa moyo wangu. Upendo wa Mungu ulinifanya nihisi aibu, na sikuwa na budi ila kujitupa chini mbele Yake katika kusujudu na kusema, “Mungu! Nimedai kuwa na imani Kwako, lakini sijakujua Wewe hata kidogo. Katika kila njia, nimekuwa mwenye kujitetea dhidi yako na kukuelewa visivyo. Kwa kweli mimi ni mdanganyifu sana; nimekuumiza tena na tena, na sistahili kuja mbele Yako. Mungu! Leo hukumu na kuadibu Kwako vimenifanya nigundue kusudi Lako la kuwaletea watu wokovu, na vimeniondolea kutoelewa kwangu kukuhusu Wewe kidogo kidogo. Mungu! Singependa kukosa fursa nyingine zaidi za kupata ukweli na kukamilishwa. Ningependa tu kufuatilia ukweli na kutimiza wajibu wangu ili nilipize mapenzi Yako!” Baada ya kumaliza kuomba, moyoni mwangu nilihisi nikiwa karibu sana na Mungu, na sasa nilikuwa na azimio la kutafuta njia ya kumridhisha.

Siku chache baadaye, viongozi wangu walishiriki nami tena kuhusu uchaguzi uliokuwa unakaribia kwa matumaini kwamba ningeshiriki. Nilijua kuwa hii ilikuwa fursa aliyoitoa Mungu ya toba, na nilitamani kufanya kila niwezalo ili kuithamini, kwa hivyo niliwaambia kwa furaha “ndiyo.” Siku chache baada ya kugeuza dhana zangu potovu na kutupa kujilinda nilikokuwa nako dhidi ya Mungu, na kugombea katika uchaguzi, ndugu zangu walinichagua kutimiza wajibu wa uongozi. Katika wakati huo nilihisi kuguswa sana, na macho yangu yalijaa machozi ya shukrani. Nilijua kwa kina kwamba huu ulikuwa ni upendo wa Mungu niliopewa, na kwamba kile nilichotaka kufanya kilikuwa kufanya kazi kwa bidii katika kufuatilia ukweli na kutimiza wajibu wangu na kutumia vitendo halisi kulipiza upendo wa Mungu.

Nikitazama nyuma kwenye uzoefu huu, najua kuwa ilikuwa ni nuru na mwongozo wa maneno ya Mungu ambavyo, kidogo kidogo, viliniondolea dhana zangu potovu kumhusu Mungu na kunifanya nithamini ukuu na heshima ya tabia Yake. Wakati Mungu anafanya kazi ya wokovu, bila kujali ni ukaidi, upotovu, au hata upinzani kiasi gani unaofichuliwa ndani yetu, almradi tu tunayo hamu ndogo ya kubadilika, Mungu hatatuacha. Badala yake, Ataleta wokovu wa kiwango cha juu kabisa kwa kila mmoja wetu. Hata ingawa maneno ya Mungu yana hukumu na shutuma, Yeye daima hutupa upendo na wokovu wa kweli zaidi; hii ndiyo njia ya pekee tunayoweza kuchukia upotovu na uovu wetu kwa kina hata zaidi, na kufanya bidii kufuatilia ukweli na kufikia mabadiliko ya tabia. Maneno ya Mungu yanasema, “Kiini cha Mungu sio tu kwa mwanadamu kuamini; vilevile ni, kwa mwanadamu kupenda. Lakini wengi wa wale wanaomwamini Mungu hawana uwezo wa kugundua hii ‘siri.’ Watu hawathubutu kumpenda Mungu, wala hawajaribu kumpenda Yeye. Hawajawahi kugundua kuwa kuna mengi sana ya kupendeza kuhusu Mungu, hawajawahi kugundua kwamba Mungu ni Mungu anayempenda mwanadamu, na kwamba ni Mungu ambaye mwanadamu anapaswa kumpenda(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Wanaompenda Mungu Wataishi Milele Katika Mwangaza Wake). Kiini cha Mungu ni kizuri na cha kupendeza, na kuna mambo mengi sana ya kupenda kumhusu Yeye. Tunahitaji kufahamu na kutambua hili kupitia uzoefu. Kuanzia sasa kuendelea, katika mazingira ambayo Mungu ameniandalia, ningependa kutumia wakati zaidi kutafuta ukweli, nikijaribu kuyaelewa mapenzi ya Mungu, kugundua hata sifa zaidi za kupendeza za Mungu, na kujitahidi kumjua Mungu ili niweze kuondoa tabia yangu potovu haraka iwezekanavyo na kuwa anayelingana na Mungu.

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wokovu wa Mungu

Na Yichen, Uchina Mwenyezi Mungu anasema: “Kila hatua ya kazi ya Mungu—kama ni maneno makali, au hukumu, au kuadibu—humfanya mwanadamu kuwa...

Nimebahatika Kumhudumia Mungu

Na Gensui, Korea ya Kusini Mwenyezi Mungu anasema, “Ni kupitia nini ndiyo ukamilishaji wa Mungu kwa mwanadamu hutimizwa? Kupitia tabia Yake...

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp