Matukio Aliyopitia Petro: Ufahamu Wake wa Adabu na Hukumu

Alipokuwa akiadibiwa na Mungu, Petro aliomba, “Ee Mungu! Mwili wangu ni mkaidi, na unaniadibu na kunihukumu mimi. Nafurahi katika adabu Yako na hukumu, na hata kama Hunitaki mimi, katika hukumu Yako mimi ninaona tabia Yako takatifu na tabia Yako ya haki. Unaponihukumu, ili wengine wapate kuiona hali Yako ya haki katika hukumu Yako, ninaridhika. Ikiwa inaweza kuionyesha tabia Yako na kuiruhusu tabia Yako ya haki iweze kuonekana na viumbe wote, na kama inaweza kuufanya upendo wangu Kwako uwe safi zaidi, kwamba naweza kufikia mfano wa yule ambaye ni mwenye haki, basi hukumu Yako ni nzuri, kwa maana hivyo ndivyo mapenzi Yako ya neema yalivyo. Najua kwamba bado kuna mengi ndani yangu yaliyo ya uasi, na kwamba mimi bado sifai kuja mbele Yako. Ningependa unihukumu hata zaidi, iwe ni kupitia mazingira ya uhasama au mateso makubwa; haijalishi ni nini Utakayofanya, kwangu ni ya thamani. Upendo Wako ni mkuu, na mimi niko tayari kujiweka katika huruma Yako bila malalamiko hata kidogo.” Huu ni ufahamu wa Petro baada ya yeye kuiona kazi ya Mungu, na pia ni ushahidi wa upendo wake kwa Mungu. Leo hii, nyinyi tayari mmeshashindwa—lakini ni jinsi gani ushindi huu unaonekana ndani yenu? Baadhi ya watu wanasema, “Ushindi Wangu ni neema kuu na kuinuliwa kwa Mungu. Ni sasa tu ndipo ninapotambua kwamba maisha ya mwanadamu ni bure na yasiyo na maana. Mwanadamu hutumia maisha yake kukimbia huku na kule, kuzalisha na kuongeza kizazi baada ya kizazi cha watoto, na hatimaye huwachwa bila chochote. Leo, baada tu ya kushindwa na Mungu ndio nimeona kwamba hakuna thamani ya kuishi kwa njia hii; kwa kweli ni maisha yasiyo na maana. Afadhali nife na kuyasahau haya!” Je, watu kama hao ambao wameshindwa wanaweza kukombolewa na Mungu? Je, wanaweza kuwa vielelezo na mifano? Watu kama hao ni somo katika kutoshughulika, hawana matarajio, na wala kujitahidi kujiboresha wenyewe! Ingawa wao huhesabiwa kama walioshindwa na Mungu, watu kama hao wasioshughulika hawawezi kufanywa wakamilifu. Karibu mwishoni mwa maisha yake, baada ya yeye kufanywa kuwa mkamilifu, Petro akasema, “Ee Mungu! Kama ningeweza kuishi miaka michache zaidi ya hapa, ningependa kufikia usafi zaidi na upendo wa ndani Kwako.” Alipokuwa karibu kusulubiwa, katika moyo wake akaomba, “Ee Mungu! Wakati Wako umewadia, wakati ulionitayarishia umefika. Mimi lazima nisulubiwe kwa ajili Yako, lazima niwe na ushuhuda huu Kwako, na ninatumai kwamba upendo wangu utaweza kukidhi mahitaji Yako, na kwamba unaweza kuwa safi zaidi. Leo, kuwa na uwezo wa kufa kwa ajili Yako, na kusulubiwa kwa ajili Yako, ni faraja na ya kutia moyo kwangu, kwa maana hakuna kinachonifurahisha kuliko kuweza kusulubiwa kwa ajili Yako na kukidhi matakwa Yako, na kuweza kujitoa Kwako, kutoa maisha yangu Kwako. Ee Mungu! Wewe ni wa kupendeza kweli! Kama Ungeniruhusu niishi, ningenuia kukupenda zaidi. Mradi tu ninaishi, mimi nitakupenda. Natamani kukupenda kwa undani zaidi. Unanihukumu, Unaniadibu, na kunijaribu kwa sababu mimi si mwenye haki, kwa sababu nimetenda dhambi. Na tabia Yako ya haki inakuwa dhahiri zaidi kwangu. Hii ni baraka kwangu, kwa maana ninapata uwezo wa kukupenda kwa undani zaidi, na mimi niko tayari kukupenda kwa njia hii hata kama Hunipendi. Mimi niko tayari kutazama tabia Yako ya haki, kwa maana inafanya niweze kuishi maisha ya maana zaidi. Mimi ninahisi kwamba maisha yangu sasa ni ya maana zaidi, kwa maana nimesulubiwa kwa ajili Yako, na ni jambo la maana kufa kwa ajili Yako. Hata hivyo bado mimi sijaridhika, kwa maana najua kidogo sana kukuhusu, najua kwamba siwezi kutimiza matakwa Yako kikamilifu, na kuwa nimekulipa kidogo mno. Katika maisha yangu, sijaweza kurudisha nafsi yangu Kwako kikamilifu; Niko mbali sana na hili. Nikitazama nyuma kwa wakati huu, mimi huhisi kuwa nina mzigo mkubwa wa madeni kwako, na sina muda mwingine ila huu kwa ajili ya kurekebisha makosa yangu na upendo wote ambao sijakulipa Wewe.”

Mwanadamu lazima azingatie kuishi kwa kudhihirisha maisha ya maana, na hapaswi kuridhika na hali yake ya sasa. Kuishi kama mfano wa Petro, lazima awe na maarifa na uzoefu wa Petro. Mtu lazima ashikilie mambo ambayo ni ya juu na zaidi ya yaliyo makuu. Ni lazima yeye afuatilie kwa ndani zaidi, usafi zaidi wa upendo wa Mungu, na maisha ambayo yana thamani na umuhimu. Haya tu ndiyo maisha; hivi tu ndivyo mwanadamu atakuwa sawa na Petro. Lazima kuzingatia kuwa makini kwa kuingia kwako kwa upande mwema, na lazima uhakikishe kwamba haurudi nyuma kwa ajili ya urahisi wa kitambo na kupuuza mambo mengine makubwa, zaidi maalum, na zaidi kwa ukweli wa vitendo. Upendo wako lazima uwe wa vitendo, na lazima utafute njia ya kujitoa katika upotovu huu, maisha yasiyo na kujali ambayo hayana tofauti na ya mnyama. Lazima uishi maisha ya maana, maisha ya thamani, na usijipumbaze, au kufanya maisha yako kama kitu cha kuchezea. Kwa kila mtu ambaye anatumai kumpenda Mungu, hakuna ukweli usioweza kupatikana, na hakuna haki wasioweza kusimama imara nayo. Unafaa kuishije maisha Yako? Unapaswa kumpenda Mungu vipi na kutumia upendo huu ili kukidhi hamu Yake? Hakuna kubwa zaidi katika maisha Yako. Zaidi ya yote, lazima uwe na matarajio hayo na uvumilivu, na hupaswi kuwa kama wanyonge wasio na nia. Lazima ujifunze jinsi ya kupitia maisha ya maana, na kuuona ukweli wa maana, na hupaswi kujichukua kipurukushani katika njia hiyo. Bila wewe kujua, maisha Yako yatakupita tu; na baada ya hapo, je utakuwa una fursa nyingine ya kumpenda Mungu? Je, mwanadamu anaweza kumpenda Mungu baada ya kufa? Lazima uwe na matarajio na dhamiri sawa na ya Petro; maisha Yako ni lazima yawe na maana, na usifanye mchezo na nafsi yako. Kama mwanadamu, na kama mtu ambaye anamfuata Mungu, ni lazima uweze kufikiria kwa makini jinsi unavyoendesha maisha yako, jinsi unapaswa kujitoa mwenyewe kwa Mungu, jinsi unapaswa kuwa na imani yenye maana zaidi katika Mungu, na jinsi, kwa kuwa wewe unampenda Mungu, unapaswa kumpenda Yeye kwa njia ambayo ni safi zaidi, nzuri zaidi, na bora zaidi. Leo hii, huwezi tu kuridhika na jinsi wewe umeshindwa, lakini lazima pia uzingatie njia ambayo utatembelea siku zijazo. Lazima uwe na matarajio na ujasiri wa kufanywa mkamilifu, na hupaswi daima kufikiria kwamba huwezi. Je, ukweli una maonevu? Je, ukweli huwapinga watu kwa makusudi? Kama wewe utaufuata ukweli, je unaweza kukushinda? Kama wewe utasimama imara kwa ajili ya haki, je utakuangusha chini? Kama ni hamu yako kwa kweli kufuata maisha, je, maisha yanaweza kukuhepa? Kama wewe huna ukweli, si kwamba ukweli unakupuuza, lakini ni kwa sababu wewe unakaa mbali na ukweli; kama huwezi kusimama imara kwa ajili ya haki, hiyo si kwa sababu kuna kitu kibaya na haki, lakini ni kwa sababu unaamini kuwa ni kinyume na ukweli; kama hujapata maisha baada ya kuyatafuta kwa miaka mingi, si kwa sababu maisha hayana dhamira kwako, bali ni kwa sababu wewe huna dhamira kwa maisha, na kuwa umeyafukuzilia mbali maisha; Iwapo unaishi katika mwanga, na hujaweza kuupata mwanga, hiyo siyo kwa sababu mwanga hauwezi kukuangazia, lakini kwa sababu wewe hujaweka makini kwa kuwepo kwa mwanga, na hivyo mwanga umeondoka kwa kimya. Kama huwezi kufuata, basi inaweza kusemwa kwamba wewe ni taka usiye na maana, na huna ujasiri katika maisha yako, na huna roho ya kupinga nguvu za giza. Wewe ni mdhaifu mno! Huwezi kutoroka nguvu za Shetani ambazo zimekuzingira, na kuwa uko tayari tu kuishi haya maisha ya usalama na kufa katika ujinga. Kile unachopaswa kufanya ni kutekeleza azma yako ya kuwa mshinde; huu ni wajibu wako uliokushikilia. Kama wewe umeridhika na kushindwa, basi unafukuza kuwepo kwa mwanga. Lazima uvumilie mateso kwa ajili ya ukweli, lazima ujitoe kwa ajili ya ukweli, lazima uvumilie udhalilishaji kwa ajili ya ukweli, na kupata ukweli zaidi lazima upate mateso zaidi. Hili ndilo unalopaswa kufanya. Msitupilie mbali ukweli kwa ajili ya maisha ya amani ya familia, na lazima msiipoteze heshima na uadilifu wa maisha kwa ajili ya starehe ya muda mfupi. Unapaswa kufuata yote ambayo ni ya kupendeza na mema, na unapaswa kufuatilia njia katika maisha ambayo ni ya maana zaidi. Kama wewe unaishi maisha ya kishenzi, na wala hufuati malengo yoyote, je, si huko ni kupoteza maisha Yako? Ni nini unachoweza kupata kutoka kwa maisha ya aina hii? Unapaswa kuziacha starehe zote za mwili kwa ajili ya ukweli mmoja, na hupaswi kutupilia mbali ukweli wote kwa ajili ya starehe ya muda mfupi. Watu kama hawa hawana uadilifu au heshima; hakuna maana ya kuwepo kwao!

Mungu humuadibu na kumhukumu mwanadamu kwa sababu inatakiwa vile na kazi Yake, na zaidi ya hayo, kwa sababu yanahitajika na mwanadamu. Mwanadamu anahitaji kuadibiwa na kuhukumiwa, na ni vile tu ndivyo anaweza kufikia upendo wa Mungu. Leo, mmeshawishiwa kikamilifu, lakini wakati mnapokutana na kizingiti kidogo mtakuwa mashakani; kimo chenu bado ni kidogo mno, na nyinyi bado mnahitaji kupata adabu na hukumu hiyo zaidi ili mfikie ufahamu zaidi. Leo, mna heshima kidogo kwa Mungu, na mnamcha Mungu, na mnajua Yeye ni Mungu wa kweli, lakini hamna upendo mkubwa wa Kwake, na bado hamjafikia upendo safi; maarifa yenu ni ya juujuu, na kimo chenu bado hakitoshi. Wakati nyinyi mnapatana na mazingira, bado hamjashuhudia, sehemu ndogo ya kuingia kwenu ndiyo makini, na nyinyi hamjui jinsi ya kufanya mazoezi. Watu wengi ni watazamaji tu na si watendaji; wao humpenda Mungu tu kwa siri katika nyoyo zao, lakini hawana njia ya mazoezi, wala hawafahamu vizuri malengo yao ni nini. Wale ambao wamefanywa wakamilifu hawana tu ubinadamu wa kawaida, lakini wanao ukweli unaozidi vipimo vya dhamiri, na kwamba ni kuu zaidi kuliko viwango ya dhamiri; wao hawatumii tu dhamiri yao kulipia upendo wa Mungu, lakini, zaidi ya hayo, wanajua Mungu, na wameona kwamba Mungu ni mzuri, na Anastahili upendo wa mtu, na kwamba kuna mambo mengi ya upendo katika Mungu ambayo mtu hana budi ila kumpenda Mungu. Upendo kwa Mungu wa wale ambao wamekuwa wakamilifu ni kwa ajili ya kutimiza matarajio yao binafsi. Upendo wao ni wa papo hapo, upendo usiouliza chochote, na usio wa kubadilisha na kitu. Wanampenda Mungu kwa sababu ya ufahamu wao Kwake, na sio kwa sababu nyingine. Watu kama hawa hawajali kama Mungu anawapa neema au la, wanaridhishwa na kumridhisha Mungu. Hawabishani na Mungu wapate kitu kwa badala yake, wala kupima upendo wao kwa Mungu na dhamiri: Umenipa, kwa hivyo nitakupenda kwa badala yake; kama Wewe Hunipi, basi sina chochote cha kukupa kwa badala yake. Wale ambao wamekuwa wakamilifu daima huamini kwamba: Mungu ni Muumba, na Yeye hufanya kazi Yake juu yetu. Kwa vile nina fursa hii, hali, na uwezo wa kufanywa kamili, azma yangu inafaa kuwa kuishi kwa kudhihirisha maisha yaliyo na maana, na ninapaswa kumridhisha Yeye. Ni kama yale aliyopitia Petro: Alipokuwa katika hatua ya udhaifu, alisali kwa Mungu na kusema, “Ee Mungu! Bila kujali wakati au mahali, Unajua kuwa mimi daima hukukumbuka. Haijalishi wakati au mahali, Unajua kuwa mimi nataka kukupenda, lakini kimo changu ni kidogo mno, mimi ni mdhaifu mno na sina nguvu, upendo wangu ni mdogo sana, na uaminifu wangu kwako pia mdogo. Ikilinganishwa na upendo Wako, mimi sifai kuishi. Natamani tu kwamba maisha yangu yasiwe bure, na kwamba nisiweze tu kulipa upendo wako, lakini, kwamba niweze kukukabidhi vyote nilivyo navyo. Kama naweza kukuridhisha, basi kama kiumbe, mimi nitakuwa na amani moyoni, na sitauliza chochote zaidi. Ingawa mimi ni mdhaifu na asiye na nguvu sasa, siwezi kusahau ushauri Wako, na siwezi kusahau upendo Wako. Sasa sifanyi kitu chochote zaidi ya kulipa upendo wako. Ee Mungu, ninahisi kuwa mbaya! Ninawezaje kukupa upendo ulio moyoni mwangu, nitafanyaje yote ninayoweza, na niwe na uwezo wa kutimiza matakwa Yako, na kuwa na uwezo wa kukupa kila nilicho nacho? Unajua udhaifu wa mwanadamu; ninawezaje kuustahili upendo wako? Ee Mungu! Unajua mimi ni wa kimo kidogo, kwamba upendo wangu pia ni mdogo. Jinsi gani niweze kufanya jinsi niwezavyo katika aina hii ya mazingira? Ninajua napaswa kuulipa upendo Wako, najua kwamba napaswa kutoa yote niliyo nayo Kwako, lakini leo kimo changu ni kidogo mno. Naomba kwamba Wewe Unipe nguvu, na kunipa ujasiri, ili niweze kuwa na upendo safi zaidi na kujitoa kwa ajili Yako, na niweze kutoa yote niliyo nayo Kwako; sitaweza kuulipa upendo Wako tu, lakini zaidi nitaweza kupitia adabu Yako, hukumu na majaribu, na hata laana kali zaidi. Umeniruhusu kutazama upendo wako, na sina uwezo wa kutokukupenda Wewe, na ingawa mimi ni mdhaifu na asiye na nguvu leo, inawezekanaje nikusahau Wewe? Upendo wako, adabu na hukumu imenisababisha mimi kujua Wewe, lakini nahisi sina uwezo wa kutimiza upendo Wako kwa hakika, kwa maana Wewe ni Mkuu zaidi. Nitawezaje kutoa yote niliyo nayo kwa Muumba?” Hilo ndilo lilikuwa ombi la Petro, ilhali kimo chake kilikuwa duni. Wakati huu, alijisikia kama kisu kilikuwa kinasukumwa katika moyo wake na alikuwa katika maumivu makali; hakujua cha kufanya katika hali hiyo. Hata hivyo bado aliendelea kuomba: “Ee Mungu! Mwanadamu ni wa kimo cha kitoto, dhamiri yake ni dhaifu, na kitu tu naweza kufikia ni kurejesha upendo Wako. Leo, mimi sijui jinsi ya kukidhi matamanio Yako, na ningependa tu kufanya yote ninayoweza, kutoa yote niliyo nayo, na kukukabidhi Wewe yote niliyo nayo. Licha ya Hukumu Yako, licha ya adabu Yako, licha ya yote uliyonipa, licha ya yale Unachukua kutoka kwangu, Niokoe kutokana na aina yoyote ya lalamiko Kwako kutoka kwangu. Mara nyingi, wakati uliniadibu na kunihukumu, nilijinung’unikia, na sikuwa na uwezo wa kufikia usafi, au wa kutimiza matakwa Yako. Ulipaji wangu wa upendo Wako ulizaliwa kutokana na lazima, na katika wakati huu najichukia hata zaidi.” Ilikuwa ni kwa sababu yeye alitaka upendo safi zaidi wa Mungu kwamba Petro aliomba kwa njia hii. Alikuwa akitafuta, na kumwomba, na, zaidi ya hayo, alikuwa akiishtaki nafsi yake, na kukiri dhambi zake kwa Mungu. Alijisikia mdeni kwa Mungu, na aliichukia nafsi yake, ilhali alikuwa pia kwa kiasi fulani mwenye huzuni na asiyeshughulika. Yeye daima aliona hivyo, kama kwamba hakuwa mzuri wa kutosha kwa ajili ya matakwa ya Mungu, na kuwa hakuweza kufanya bora zaidi. Katika hali kama hiyo, Petro bado alifuata imani ya Ayubu. Aliona jinsi imani ya Ayubu ilivyokuwa kubwa, kwa maana Ayubu aliona kwamba yote yalifanywa na Mungu, na ilikuwa ni ya asili ya Mungu kuchukua kila kitu kutoka kwake, na kwamba Mungu angempa yeyote ambaye Angependa kumpa—hivyo ndivyo ilivyokuwa tabia ya haki ya Mungu. Ayubu hakuwa na malalamiko, na bado aliweza kumtukuza Mungu. Petro pia alijua mwenyewe, na katika moyo wake akaomba, “Leo mimi siwezi kuridhika na kulipa upendo Wako kwa kutumia dhamiri yangu na kwa upendo wowote ninaokupa, kwa sababu mawazo yangu yamepotoshwa sana, na kwa sababu mimi sina uwezo wa kukuona Wewe kama Muumba. Kwa sababu mimi bado sifai kukupenda, lazima kukamilisha uwezo wa kutoa yote niliyonayo Kwako, na hivyo nitafanya kwa hiari. Ni lazima nijue yote Uliyofanya, na sina budi, na mimi lazima nitazame upendo Wako, na kuwa na uwezo wa kusema sifa Zako, na kutaja jina lako takatifu, ili Uweze kupata utukufu mwingi kupitia kwangu. Mimi niko tayari kusimama imara katika ushuhuda huu Kwako. Ee Mungu! Upendo wako ni wenye thamani na wa kupendeza; jinsi gani mimi ningetaka kuishi katika mikono ya yule mwovu? Je, mimi sikuumbwa na Wewe? Ningewezaje kuishi chini ya miliki ya Shetani? Ningependa nafsi yangu nzima iishi chini ya adabu Yako. Sitaki kuishi chini ya miliki ya yule mwovu. Kama mimi ninaweza kutakaswa, na ninaweza kutoa yote niliyonayo Kwako, mimi niko tayari kutoa mwili wangu na akili kwa hukumu na adabu Yako, kwa maana mimi nachukizwa na Shetani, na sina nia ya kuishi chini ya uwanja wake. Kupitia hukumu Yako kwangu, umenionyesha tabia Yako ya haki; Nina furaha, na sina malalamiko hata kidogo. Kama mimi nina uwezo wa kutekeleza jukumu la kiumbe, mimi niko tayari kuwa maisha yangu yote yaambatane na hukumu Yako, kwa njia ambayo mimi nitapata kujua tabia Yako ya haki, na kujiondolea ushawishi wa yule mwovu.” Petro aliomba hivyo kila mara, na daima alitafuta hivyo, na aliufikia ulimwengu wa juu, kwa ulinganisho. Hakuweza tu kuulipa upendo wa Mungu, lakini, la muhimu zaidi, yeye alitimiza wajibu wake kama kiumbe. Hakutuhumiwa tu na dhamiri yake, lakini alikuwa pia na uwezo wa kuvuka viwango vya dhamiri. Maombi yake yaliendelea kwenda mbele za Mungu, hivyo kwamba matarajio yake yalikuwa milele juu, na upendo wake kwa Mungu ulikuwa milele mkuu. Ingawa yeye alipitia maumivu makali, bado hakusahau kumpenda Mungu, na bado alitaka kufikia uwezo wa kuelewa mapenzi ya Mungu. Kwa maombi yake yalitamkwa maneno yafuatayo: Sijatimiza chochote zaidi ya ulipaji wa upendo wako. Sijatoa ushuhuda Kwako mbele ya Shetani, sijajiweka huru mwenyewe kutokana na ushawishi wa Shetani, na bado naishi miongoni mwa umbo la mwili. Ningependa kutumia upendo wangu kumshinda shetani, na kumwaibisha, na hivyo kuridhisha hamu Yako. Ningependa kujitoa mzima Kwako, nisijitoe hata kidogo kwa Shetani, kwani Shetani ni adui Wako. Zaidi ya alivyoendelea kwa njia hii, ndivyo alivyozidi kusongeshwa, na ndivyo ujuzi wake wa mambo haya ulivyozidi kukua. Bila kujua, alitambua kwamba anapaswa kujikwamua kutokana na ushawishi wa Shetani, na kujirudisha mwenyewe kabisa kwa Mungu. Huo ndio ulimwengu alioufikia. Alikuwa anauzidi kwa mbali ushawishi wa Shetani, na kujitoa mwenyewe kwenye raha na starehe za mwili, na alikuwa tayari kupitia kwa kina zaidi adabu zote na hukumu ya Mungu. Alisema, “Hata ingawa ninaishi katika adabu Yako, na huku kukiwa na hukumu Yako, bila kujali ugumu unaohusiana na maisha, bado mimi sina nia ya kuishi chini ya miliki ya Shetani, sina nia ya kuteseka na hila za Shetani. Mimi nina furaha kuishi kwenye laana Yako, na ninapata uchungu kwa kuishi katika baraka za shetani. Nakupenda kwa kuishi katika hukumu Yako, na hii huniletea furaha kuu. Adabu Yako na hukumu ni yenye uadilifu na takatifu; ni vyema ukinitakasa, na hata zaidi kuniokoa. Ninapenda niishi maisha yangu yote katika hukumu Yako na kuwa chini ya uchungaji Wako. Sina nia ya kuishi chini ya mamlaka ya Shetani hata kwa dakika moja; Napenda kutakaswa na Wewe; hata kama ninapitia taabu, sina nia ya kutumiwa na kuhadaiwa na shetani. Mimi, kiumbe hiki, nafaa nitumike na Wewe, nijazwe na Wewe, nihukumiwe na Wewe, na kuadibiwa na Wewe. Nafaa hata nipokee laana kutoka Kwako. Moyo wangu hufurahi wakati Uko tayari kunibariki, kwa maana nimeona upendo Wako. Wewe ni Muumba, na mimi ni kiumbe: Sifai kukusaliti Wewe na kuishi chini ya himaya ya Shetani, wala sifai kutumiwa na Shetani. Mimi nafaa kuwa farasi wako, au ng’ombe, badala ya kuishi kwa ajili ya Shetani. Afadhali niishi katika adabu Yako, bila neema ya kimwili, na hii itanipa raha na starehe hata kama ningepoteza neema Yako. Ingawa neema Yako haiko nami, mimi nafurahia kuadibiwa na kuhukumiwa na Wewe; Hii ndiyo baraka Yako nzuri zaidi, neema Yako kuu. Ingawa Wewe daima ni Mkuu na mwenye ghadhabu kwangu, bado mimi siwezi kukuacha, bado sina uwezo wa kukupenda vya kutosha. Ningependelea kuishi katika nyumba Yako, Ningependa kulaaniwa, kuadibiwa, na kuchapwa na Wewe, na sina nia ya kuishi chini ya himaya ya Shetani, wala mimi sina nia ya kukimbilia na kushughulika kwa ajili ya mwili tu, zaidi ya hayo siko tayari kuishi kwa ajili ya mwili.” Upendo wa Petro ulikuwa upendo safi. Huu ni ujuzi wa kufanywa mkamilifu, na ni ulimwengu wa juu wa kufanywa mkamilifu, na hakuna maisha yaliyo na maana zaidi ya haya. Alikubali adabu ya Mungu na hukumu, aliipenda tabia ya Mungu ya haki, na hakuna jambo kuhusu Petro lililokuwa la thamani zaidi ya hili. Alisema, “Shetani ananipa starehe za mwili, lakini mimi sithamini hayo. Adabu ya Mungu na hukumu inakuja juu yangu—na katika hili mimi nimeneemeka, katika hili mimi ninapata starehe, na katika hili mimi nimebarikiwa. Kama si kwa hukumu Yake, mimi singeweza kumpenda Mungu, bado ningeishi chini ya himaya ya Shetani, bado ningedhibitiwa nayo, na ningekuwa naamuriwa nayo. Kama ingekuwa vile, singewahi kuwa binadamu wa kweli, kwa maana singeweza kumtosheleza Mungu, na singejitoa kikamilifu kwa Mungu. Japokuwa Mungu Hanibariki, na kuniacha bila faraja ndani yangu, kana kwamba moto mkuu unachoma ndani yangu, na hakuna amani au furaha, na hata ingawa adabu na nidhamu ya Mungu kamwe iko na mimi, katika adabu ya Mungu na hukumu ninao uwezo wa kuona tabia Yake ya haki. Mimi hupata furaha katika hili; hakuna kitu cha thamani zaidi au cha maana zaidi ya hili katika maisha. Ingawa ulinzi Wake na huduma vimekuwa adabu kali, hukumu, laana na mipigo, bado mimi hupata starehe katika mambo haya, kwani yanaweza kunitakasa bora zaidi na kunibadilisha, yanaweza kunileta karibu na Mungu zaidi, yanaweza kufanya niweze kumpenda Mungu zaidi, na yanaweza kufanya upendo wangu kwa Mungu uwe safi zaidi. Hii inanifanya niwe na uwezo wa kutimiza wajibu wangu kama kiumbe, na inanichukua mbele za Mungu na kuniweka mbali na ushawishi wa Shetani, ili nisije tena nikamtumikia Shetani. Wakati siishi chini ya himaya ya Shetani, na ninaweza kutoa kila kitu nilicho nacho na kile ninachoweza kwa ajili ya Mungu, bila kubakisha chochote—hapo ndipo nitakuwa nimeridhika kikamilifu. Ni adabu ya Mungu na hukumu Yake ndiyo iliyoniokoa, na maisha yangu hayawezi kutengwa kutoka kwenye adabu na hukumu ya Mungu. Maisha yangu hapa duniani yamo chini ya himaya ya Shetani, na isingekuwa huduma na ulinzi na adabu ya Mungu na hukumu Yake, ningeliishi daima chini ya himaya ya Shetani, na, zaidi ya hayo, singekuwa na nafasi au njia ya kuishi kwa kudhihirisha maisha yenye maana. Ni wakati tu ambapo adabu ya Mungu na hukumu kamwe hainiachi, ndio nitakapokuwa na uwezo wa kutakaswa na Mungu. Ni kwa maneno makali na tabia ya haki ya Mungu, na hukumu kuu ya Mungu, ndipo nimepata ulinzi mkuu, na kuishi katika mwanga, na kupokea baraka za Mungu. Kuwa na uwezo wa kutakaswa, na kujiweka huru kutokana na Shetani, na kuishi chini ya utawala wa Mungu—hii ndiyo baraka kubwa zaidi katika maisha yangu leo.” Huu ndio ulimwengu wa juu zaidi aliopitia Petro.

Hizi ndizo hali ambazo mwanadamu lazima afikie baada ya kufanywa mkamilifu. Kama huwezi kufikia kiasi hiki, basi huwezi kuishi kwa kudhihirisha maisha yenye maana. Mwanadamu anaishi katika mwili, ambayo ina maana anaishi katika kuzimu ya binadamu, na bila hukumu na adabu ya Mungu, mwanadamu ni mchafu kama Shetani. Mwanadamu atawezaje kuwa mtakatifu? Petro aliamini kwamba adabu na hukumu ya Mungu ndio uliokuwa ulinzi bora zaidi wa mwanadamu na neema kubwa. Ni kwa njia ya adabu na hukumu ya Mungu ndipo mwanadamu angeweza kugutuka, na kuchukia mwili, na kumchukia Shetani. Nidhamu kali ya Mungu inamweka huru kutokana na ushawishi wa Shetani, inamweka huru kutokana na dunia yake ndogo, na inamruhusu kuishi katika mwanga wa uwepo wa Mungu. Hakuna wokovu bora zaidi kuliko adabu na hukumu! Petro aliomba, “Ee Mungu! Mradi tu Wewe unaniadibu na kunihukumu, nitajua kwamba Wewe hujaniacha. Hata kama Huwezi kunipa furaha au amani, na kufanya niishi katika mateso, na kunirudi mara nyingi, bora tu Hutaniacha moyo wangu utakuwa na amani. Leo hii, adabu Yako na hukumu umekuwa ulinzi wangu bora na baraka yangu kubwa. Neema unayonipa inanilinda. Neema unayoweka juu yangu leo ni kielelezo cha tabia Yako ya haki, na ni adabu na hukumu; zaidi ya hayo, ni majaribu, na, zaidi ya hapo, ni maisha ya mateso.” Petro alikuwa na uwezo wa kuweka kando raha ya mwili na kutafuta mapenzi zaidi na ulinzi zaidi, kwa sababu alikuwa amepata neema nyingi kutoka kwa adabu na hukumu ya Mungu. Katika maisha yake, kama mwanadamu anatamani kutakaswa na kufikia mabadiliko katika tabia yake, kama anatamani kuishi kwa kudhihirisha maisha yenye maana, na kutimiza wajibu wake kama kiumbe, basi lazima akubali adabu na hukumu ya Mungu, na lazima asiruhusu nidhamu ya Mungu na kipigo cha Mungu kiondoke kwake, ili aweze kujiweka huru kutokana na kutawalwa na ushawishi wa Shetani na kuishi katika mwanga wa Mungu. Ujue kwamba adabu ya Mungu na hukumu ni mwanga, na mwanga wa wokovu wa mwanadamu, na kwamba hakuna baraka bora zaidi, neema au ulinzi bora kwa ajili ya mwanadamu. Mwanadamu anaishi chini ya ushawishi wa Shetani, na yupo katika mwili; kama yeye hatatakaswa na kupokea ulinzi wa Mungu, basi mwanadamu atakuwa milele mpotovu zaidi. Kama yeye anataka kumpenda Mungu, basi lazima atakaswe na kuokolewa. Petro aliomba, “Mungu, wakati Unanitendea wema ninapata furaha, na kuhisi faraja; wakati unaniadibu, najisikia faraja kubwa zaidi na furaha. Ingawa mimi ni mdhaifu, na kuvumilia mateso yasiyotajika, ingawa kuna machozi na huzuni, Unajua kwamba huzuni huu ni kwa sababu ya kutotii kwangu, na kwa sababu ya udhaifu wangu. Mimi ninalia kwa sababu siwezi kukidhi hamu Yako, nahisi huzuni na majuto kwa sababu mimi sitoshi kwa mahitaji Yako, lakini niko tayari kufikia ulimwengu huu, niko tayari kufanya yote niwezayo ili nikuridhishe. Adabu Yako imeniletea ulinzi, na kunipa wokovu bora; hukumu Yako inazidi ustahimili Wako na uvumilivu Wako. Bila adabu Yako na hukumu, singefurahia huruma Yako na rehema. Leo, naona zaidi kwamba upendo wako umepita mipaka ya mbinguni na kuwa bora ya yote. Upendo wako sio tu huruma na fadhili; hata zaidi ya hayo, ni adabu na hukumu. Adabu Yako na hukumu imenipa mengi. Bila adabu Yako na hukumu, hakuna hata mmoja angetakaswa, na hakuna hata mmoja angeweza kupata upendo wa Muumba. Ingawa nimevumilia mamia ya majaribio na mateso, na hata nimekuwa karibu na kifo, haya yameniruhusu kukujua Wewe kwa kweli na kupata wokovu mkuu. Kama adabu Yako, hukumu na nidhamu vingeondoka kutoka kwangu, basi ningeishi gizani, chini ya himaya ya Shetani. Mwili wa binadamu una faida gani? Kama adabu Yako na hukumu ingeniwacha, ingekuwa kana kwamba Roho Wako alikuwa ameniacha, ni kama Wewe Haukuwa tena pamoja nami. Kama ingekuwa vile, ni jinsi gani ningeendelea kuishi? Kama Wewe utanipa ugonjwa, na kuchukua uhuru wangu, naweza kuendelea kuishi, lakini adabu Yako na hukumu vikiondoka kutoka kwangu, sitakuwa na njia ya kuendelea kuishi. Kama ningekuwa bila adabu Yako na hukumu, ningepoteza upendo Wako, upendo ambao ni mkuu sana mpaka sina maneno ya kuueleza. Bila Upendo wako, ningeishi chini ya miliki ya Shetani, na singeweza kuuona uso wako mtukufu. Ningewezaje kuendelea kuishi? Giza kama hili, maisha kama haya, singeweza kuvumilia. Mimi kuwa na wewe ni kama kukuona Wewe, hivyo ni jinsi gani ningeweza kukuacha? Ninakusihi, nakuomba usichukue faraja yangu kubwa kutoka kwangu, hata kama ni maneno machache tu ya uhakikisho. Nimefurahia upendo wako, na leo hii siwezi kuwa mbali na Wewe; ningewezaje kutokupenda Wewe? Nimemwaga machozi mengi ya huzuni kwa sababu ya upendo Wako, ilhali daima nimehisi kuwa maisha kama haya ni ya maana zaidi, yenye uwezo mwingi wa kuniimarisha, yenye uwezo zaidi wa kunibadilisha, na yenye uwezo zaidi wa kunifanya nifikie ukweli ambao lazima viumbe wawe nao.”

Maisha yote ya mwanadamu yamekuwa chini ya himaya ya Shetani, na hakuna mtu yeyote anayeweza kujitoa kutoka katika ushawishi wa Shetani yeye mwenyewe. Wote wanaishi katika dunia chafu, kwa upotovu na utupu, bila maana yoyote au thamani; wanaishi maisha ya kutojali kwa ajili ya mwili, tamaa, na kwa ajili ya Shetani. Hakuna maana yoyote kwa kuwepo kwao. Mwanadamu hana uwezo wa kupata ukweli utakaomweka huru kutoka kwa ushawishi wa Shetani. Ingawa mwanadamu anaamini katika Mungu na anasoma Biblia haelewi jinsi ya kujitoa kutoka kwa ushawishi wa Shetani. Kutoka kitambo, watu wachache sana wametambua siri hii, wachache sana wameielewa. Hivyo, hata kama mwanadamu anamchukia Shetani, na anachukia mwili, hajui jinsi ya kujitoa kutoka kwa ushawishi mkuu wa Shetani. Je, leo bado hamjamilikiwa na Shetani? Hamjuti juu ya matendo yenu ya uasi, zaidi ya hayo, hamhisi kama wachafu na waasi. Baada ya kumpinga Mungu, bado mna amani ya moyo na mnahisi utulivu mwingi. Je, utulivu wako si kwa sababu wewe ni mpotovu? Je, hii amani ya mawazo haitokani na kuasi kwako? Mwanadamu anaishi katika jehanamu ya binadamu, anaishi katika ushawishi wa giza la Shetani; mkabala katika ardhi, mapepo yanaishi na mwanadamu, yakienea katika mwili wa mwanadamu. Duniani, hauishi katika Paradiso ya kupendeza. Mahali ambapo ulipo ni ulimwengu wa Shetani, jehanamu ya binadamu, dunia ya chini. Mwanadamu asipotakaswa, basi yeye ni wa uchafu; asipolindwa na kutunzwa na Mungu, basi yeye bado ni mfungwa wa Shetani; asipohukumiwa na kuadibiwa, basi hatakuwa na njia ya kuepuka ukandamizaji na ushawishi mbaya wa Shetani. Tabia potovu unayoonyesha, na tabia ya uasi unayoishi kwa kudhihirisha inatosha kuonyesha kwamba bado unaishi katika himaya ya Shetani. Kama akili na mawazo yako hayajatakaswa, na tabia yako haijahukumiwa na kuadibiwa, basi nafsi yako yote bado inadhibitiwa na himaya ya Shetani, akili yako bado inadhibitiwa na Shetani, mawazo yako yanatawaliwa na Shetani, na nafsi yako yote inadhibitiwa na mikono ya Shetani. Je, unajua uko umbali gani, sasa, na viwango alivyokuwa navyo Petro? Je, wewe unamiliki kiwango hicho? Ni kiasi gani unajua kuhusu adabu na hukumu ya wakati wa leo? Unacho kiasi gani cha yale Petro alipata kujua? Iwapo, leo, huna uwezo wa kutambua, je utaweza kupata maarifa haya baadaye? Mtu mzembe na mwoga kama wewe hawezi kujua kuhusu adhabu na hukumu. Ukifuata amani ya kimwili, na raha za kimwili, basi hutakuwa na njia yoyote ya kutakaswa, na mwishowe utarudishwa kwa Shetani, kwa sababu hali unayoishi kwa kudhihirisha ni ya Shetani, na ya mwili. Vitu vilivyo sasa, watu wengi hawayafuati maisha, kwa hivyo inamaanisha kuwa hawajali kuhusu kutakaswa, ama kuingia katika uzoefu wa ndani ya maisha. Je, watawezaje kufanywa kuwa wakamilifu? Wale wasiofuata maisha hawana fursa ya kufanywa wakamilifu, na wale wasiofuata maarifa ya Mungu, na hawafuati mabadiliko katika tabia zao, hawataweza kuepuka ushawishi wa giza wa Shetani. Kwa kuashiria maarifa yao kuhusu Mungu na kuingia kwao katika mabadiliko ya tabia zao, hawana umakini kuzihusu, kama wale wanaoamini katika dini pekee, na wale wanaofuata tu sherehe na kuhudhuria huduma za kawaida. Je, hiyo si kupoteza wakati? Kama, kwa imani yake kwa Mungu, mwanadamu hayuko makini katika mambo ya maisha, hafuati kuingia katika ukweli, hazingatii mabadiliko katika tabia yake, ama kufuata maarifa ya kazi ya Mungu, basi hawezi kufanywa mkamilifu. Kama unatamani kufanywa mkamilifu, lazima uelewe kazi ya Mungu. Hasa, lazima uelewe umuhimu wa adabu na hukumu Yake, na kwa nini kazi hii inafanywa juu ya mwanadamu. Je, unaweza kukubali? Wakati wa adabu ya aina hii, unaweza kupata uzoefu na maarifa kama Petro? Ukifuata maarifa ya Mungu na ya kazi ya Roho Mtakatifu, na kuzingatia mabadiliko katika tabia yako, basi una fursa ya kufanywa mkamilifu.

Kwa wale ambao wanatakiwa kufanywa wakamilifu, hatua hii ya kazi ya kushinda ni ya lazima; Ni baada ya kushindwa tu ndipo mwanadamu anaweza kuiona kazi ya kufanywa mkamilifu. Hakuna maana kubwa ya kufanya kazi ya kushindwa, ambayo itakufanya usiwe mwenye kufaa kufanya kazi yoyote ya Mungu. Hutakuwa na uwezo wowote wa kufanya kazi yako ya kueneza injili, kwa sababu hufuati maisha, na hujibadilishi na kujifanya mpya, na hivyo basi huna uzoefu kamili wa maisha. Katika kazi hii ya hatua kwa hatua, uliwahi kuwa na nafasi ya mtendaji-huduma, na foili[a], lakini kwa hakika usipofuata kuwa kama Petro, na ufuasi wako sio kama wenye njia ambayo Petro alifanywa mkamilifu, basi, kiasili hutapata mabadiliko katika tabia yako. Kama wewe ni mtu anayefuata kuwa mkamilifu, basi utakuwa na ushuhuda, na utasema: “Katika hii kazi ya hatua kwa hatua ya Mungu, nimekubali kazi ya Mungu ya adabu na hukumu, na hata kama nimepitia mateso mengi, nimepata kujua jinsi Mungu hufanya mwanadamu kuwa mkamilifu, nimepata kazi iliyofanywa na Mungu, nimekuwa na maarifa ya haki ya Mungu, na adabu Yake imeniokoa. Tabia Yake ya haki imekuja juu yangu, na ikaniletea baraka na neema; ni hukumu Yake na adabu ambazo zimenilinda na kunitakasa. Kama singeadibiwa na kuhukumiwa na Mungu, na kama maneno makali ya Mungu hayangekuja juu yangu, singalimjua Mungu, ama kuokolewa. Leo, naona, kama kiumbe, kwamba mtu hafurahii tu vitu vilivyoumbwa na Muumba, lakini pia, la maana sana ni kwamba viumbe vyote watafurahia haki ya tabia ya Mungu, na kufurahia hukumu Yake ya haki, kwa sababu tabia ya Mungu ina umuhimu katika furaha ya Mwanadamu. Kama kiumbe ambaye amepotoshwa na Shetani, kila mmoja anafaa kufurahia tabia ya haki ya Mungu. Katika tabia Yake ya haki, kuna adabu na hukumu, na pia, kuna upendo mkuu. Ingawa sina uwezo wa kupata kwa kikamilifu upendo wote wa Mungu leo, nimekuwa na bahati nzuri ya kuuona, na katika haya, nimebarikiwa.” Hii ndio njia ambayo wale waliofanywa wakamilifu hutembea na maarifa wanayoongelea. Watu hao wanafanana na Petro; wanao uzoefu sawa na wa Petro. Watu kama hao pia ndio wale ambao wamepokea maisha, na walio na ukweli. Wanapokuwa na uzoefu mpaka mwisho kabisa, wakati wa hukumu ya Mungu kwa hakika wataweza kikamilifu kujitoa katika ushawishi wa Shetani, na atakuwa wa Mungu.

Baada ya kushindwa, watu hawana ushuhuda wa kusikia. Kwa hakika wameaibisha tu Shetani, lakini hawajaishi kwa kudhihirisha ukweli wa neno la Mungu. Haujapata wokovu wa pili; umepata tu sadaka ya dhambi, ilhali haujafanywa mkamilifu—hii ni hasara kubwa. Lazima muelewe yale mnafaa kuingia ndani yake, na yale mnafaa kuishi kwa kudhihirisha, na lazima muingie ndani mwao. Kama mwishowe, hautafaulu kufanywa mkamilifu, basi hautakuwa binadamu wa kweli, na utajawa na majuto. Adamu na Hawa waliumbwa na Mungu hapo mwanzo wakiwa watu watakatifu, ni kama kusema, katika bustani ya Edeni, walikuwa watakatifu, wasiokuwa na uchafu. Walikuwa watiifu kwa Yehova, na hawakujua chochote kuhusu kuasi Yehova. Hii ni kwa sababu hawakuwa na kusumbuliwa na ushawishi wa Shetani, hawakuwa na sumu ya Shetani, na walikuwa watu wasafi kati ya binadamu wote. Waliishi katika bustani ya Edeni, bila kutiwa najisi na uchafu wowote, bila kuingiliwa na mwili, na heshima kwa Yehova. Baadaye, walipojaribiwa na Shetani, wakawa na sumu ya nyoka, na tamaa ya kuasi Yehova, na wakaishi chini ya ushawishi wa Shetani. Hapo mwanzo, walikuwa watakatifu na wenye kuheshimu sana Yehova; hivyo tu ndivyo walikuwa binadamu. Baadaye, baada ya kujaribiwa na Shetani, wakala tunda la maarifa ya kujua mazuri na mabaya, na wakaishi chini ya ushawishi wa Shetani. Waliendelea kupotoshwa na Shetani, na wakapoteza sura asili ya mwanadamu. Hapo mwanzo, mwanadamu alikuwa na pumzi ya Yehova, na hakuwa muasi hata kidogo, na hakuwa na uovu wowote katika moyo wake. Wakati huo, mwanadamu alikuwa binadamu wa kweli. Baada ya kupotoshwa na Shetani, mwanadamu akawa mnyama. Fikra zake zikajawa na uovu na uchafu, bila mazuri ama utakatifu. Je, huyu si Shetani? Umepata kujua mengi kuhusu kazi ya Mungu, ilhali haujabadilika wala kutakaswa. Bado unaishi katika himaya ya Shetani, na bado hujajitoa na kunyenyekea kwa Mungu. Huyu ni mtu ambaye ameshindwa lakini hajafanywa mkamilifu. Na mbona inasemekana kuwa mtu kama huyu hajafanywa mkamilifu? Kwa sababu mtu huyu hafuati maisha ama maarifa ya kazi ya Mungu, na hutamani tu raha za kimwili na starehe ya muda mfupi. Na kwa hivyo hakuna mabadiliko katika tabia zao, na hawajapata sura asili ya mwanadamu ilivyoumbwa na Mungu. Watu hao ni maiti zinazotembea, ni waliokufa na hawana roho! Wale wasiofuata maarifa ya mambo katika Roho, wasiofuata utakatifu, na wasiofuata kuishi kulingana na maisha ya ukweli, wanaotosheka na kushindwa kwa upande wa kanusho, na wasioweza kuishi kwa kufuata maneno ya Mungu na kuwa binadamu watakatifu—hawa ni watu ambao hawajaokolewa. Kwani, kama hana ukweli, mwanadamu hataweza kusimama imara katika majaribu ya Mungu; wale watakaoweza kusimama imara katika majaribu ya Mungu pekee ndio wale ambao wameokolewa. Ninalotaka Mimi ni watu kama Petro, watu wanaofuata kufanywa wakamilifu. Ukweli wa leo unatolewa kwa wale ambao wanautamani na kuutafuta. Wokovu huu unapewa wale ambao wanatamani kuokolewa na Mungu, na haujakusudiwa kuwafaidi tu, lakini ili pia ili mpatwe na Mungu. Mnampata Mungu ili Mungu pia awapate. Leo nimenena hayo maneno kwenu, na mmeyasikia, na mnafaa kutenda kulingana na maneno haya. Mwishowe, mkiweka maneno haya katika matendo ndipo nitakapowapata nyinyi kupitia katika maneno haya; na pia, mtakuwa mmepata maneno haya, kumaanisha, mtakuwa mmepata wokovu mkuu. Punde mtakapofanywa wasafi, mtakuwa wanadamu halisi. Kama huwezi kuishi kulingana na ukweli, ama kuishi kulingana na aliyefanywa mkamilifu, basi inaweza kusemwa kuwa wewe si binadamu, ila wewe ni mfu anayetembea, mnyama, kwa sababu huna ukweli, ni kusema huna pumzi ya Yehova, na basi wewe ni mtu aliyekufa ambaye hana roho! Ingawa unaweza kuwa na ushuhuda baada ya kushindwa, unachopata ni wokovu kidogo, na hujakuwa kiumbe chenye roho. Ingawa umepata adabu na hukumu, tabia yako haijafanywa upya ama kubadilishwa kama matokeo; umebaki tu ulivyokuwa, bado wewe ni wa Shetani, na wewe si mtu aliyetakaswa. Wale tu waliofanywa wakamilifu ndio wenye thamani, na watu tu kama hao ndio wamepata maisha ya kweli. Siku moja, mtu atakuambia, “Umeishuhudia kazi ya Mungu, basi zungumzia kidogo jinsi kazi Yake ilivyo. Daudi aliishuhudia kazi ya Mungu, na kuona kazi ya Yehova, Musa pia alishuhudia matendo ya Yehova, na wawili hao waliweza kuelezea juu ya matendo ya Yehova, na wangeweza kuongelea maajabu ya Yehova. Mmeona kazi iliyofanywa na Mungu mwenye mwili siku za mwisho; unaweza kuongea kuhusu hekima Yake? Unaweza kuongelea maajabu ya kazi Yake? Ni nini Mungu alihitaji kutoka kwenu, na mliyaona vipi? Mmeiona kazi ya Mungu katika siku za mwisho; maono yenu makuu ni yapi? Mnaweza kuzungumza kuhusu haya? Mnaweza kuongea juu ya tabia ya haki ya Mungu?” Utajibu nini utakapokabiliana na maswali hayo? Ukisema, “Mungu ni mwenye haki sana, Anaadibu na kutuhukumu, na kutuonyesha kwa wazi. Tabia ya Mungu kwa hakika haistahimili makosa ya mwanadamu. Baada ya kuiona kazi ya Mungu, nimejua unyama wetu, na kwa hakika nimeona tabia ya haki ya Mungu,” halafu yule mtu mwingine ataendelea kukuuliza, “Ni nini kingine unachojua kumhusu Mungu? Mtu anaingiaje katika uzima? Je, una matarajio yoyote ya kibinafsi?” Utajibu, “Baada ya kupotoshwa na Shetani, viumbe wa Mungu walikuwa wanyama, na hawakuwa na tofauti na punda. Leo, ninaishi katika mikono ya Mungu, kwa hivyo lazima nikidhi matakwa na matamanio ya Muumba, na kutii kile Anachofunza. Sina chaguo lingine.” Kama unaongea kwa ujumla kama huo pekee, mtu yule hataelewa kile unachokisema. Wakikuuliza ni maarifa gani unayo juu ya kazi ya Mungu, wanazungumzia kazi uliyofanya na mambo uliyopitia binafsi. Wanataka kujua juu ya ufahamu ulionao juu ya adabu na hukumu ya Mungu baada ya kuipitia, na kwa hiyo wanaongelea kuhusu matukio yako ya binafsi, na kuuliza uongelee ufahamu wako juu ya ukweli. Kama huwezi kuongelea mambo haya, hii inadhihirisha kwamba hujui lolote kuhusu kazi ya leo. Wewe huzungumza kuhusu maneno ya kupotosha, au yale yanayojulikana na kila mtu; hujapitia matukio yoyote halisi, wala huna dutu katika maarifa yako, na huna ushuhuda wa ukweli, na hivyo wengine hawatashawishiwa na mambo yako. Usiwe mfuasi tu wa kumtazama Mungu, na usifuate kile kinachokufanya utake kuchunguza. Kwa kutokuwa moto ama baridi utajiangamiza na kuchelewesha maisha yako. Lazima ujitoe kutoka kwa utazamaji na kutofanya chochote na uwe wa kufuata vitu vyema na kuushinda udhaifu wako, ili uweze kupata ukweli na kuishi kwa kudhihirisha maisha ya ukweli. Hakuna kitu cha kuogopesha kuhusu udhaifu wako, na kasoro zako sio shida yako kubwa. Shida yako kubwa, na kasoro yako kubwa, ni kutokuwa baridi ama moto na kutokuwa na hamu ya kuutafuta ukweli. Shida kubwa na nyinyi wote ni hali ya uoga ambapo mnaridhika na hali ilivyo, na kungoja mkitazama tu. Hiki ndicho kizuizi chenu kikuu, na adui mkubwa kwa harakati yenu ya kutafuta ukweli. Kama unatii tu kwa sababu maneno Ninayosema ni makubwa, basi huna maarifa kwa kweli, wala huuthamini ukweli. Kutii kama kwako si ushuhuda, na Siukubali utiifu wa aina hii. Mtu anaweza kukuuliza, “Mungu wako anatoka wapi hasa? Huyu Mungu wako ana kiini gani hasa?” Utajibu, “Dutu yake ni adabu na hukumu.” Kisha anaendelea, “Je, Mungu si wa huruma na upendo kwa mwanadamu? Je, hujui hivyo?” Utasema, “Huyo ni Mungu wa wengine. Ni Mungu ambaye watu wa dini wanaamini, si Mungu wetu.” Wakati watu kama wewe wanaeneza injili, ukweli unapotoshwa na wewe, basi una maana gani? Watu wengine watawezaje kuupata ukweli kutoka kwako? Huna ukweli, na huwezi kuongea chochote cha ukweli, ama, zaidi ya hayo, huwezi kuishi kwa kudhihirisha ukweli. Ni nini kinakuhitimisha kuishi mbele ya Mungu? Unapoeneza injili kwa wengine, na unaposhiriki kuhusu ukweli, na kuwa na ushuhuda kuhusu Mungu, kama huwezi kuwatwaa kuja kwa Mungu, watayakataa maneno yako. Je, hutakuwa mpotezaji wa nafasi? Umeona mengi kuhusu kazi ya Mungu, ilhali ukiongelea ukweli, haueleweki. Je, wewe si bure tu? Wewe una maana gani? Mngewezaje kuwa mmeshuhudia kazi nyingi ya Mungu vile, ilhali hamna ufahamu kuhusu Mungu? Wakiuliza ni maarifa gani hasa uliyonayo ya Mungu, huna la kusema, au unajibu na kitu kisichoambatana na swali—ukisema kuwa Mungu ni mkuu, kuwa baraka ambayo umepokea ni uadhimisho wa Mungu, na kwamba hakuna bahati kuu kushinda kumwona Mungu kibinafsi. Kuna thamani gani ndani ya kusema hivyo? Ni maneno matupu yasiyo na maana! Kwa kuwa umeshuhudia kazi nyingi ya Mungu, je, unajua kuwa uadhimisho wa Mungu ni ukweli? Lazima ujue kazi ya Mungu, na hapo tu ndipo utakuwa na ushuhuda wa kweli kwa Mungu. Watu ambao hawajaupata ukweli watawezaje kumshuhudia Mungu?

Ikiwa kazi nyingi, na maneno mengi, hayajakuwa na mabadiliko kwako, basi wakati utakapofika wa kueneza kazi ya Mungu hutaweza kufanya kazi yako, na utaaibika na kufedheheshwa. Wakati huo utajisikia kuwa una deni kubwa kwa Mungu, kwamba maarifa yako juu ya Mungu ni juujuu. Usipofuata maarifa ya Mungu leo, Akiwa bado Anafanya kazi, basi baadaye itakuwa umechelewa. Mwishowe hutakuwa na maarifa yoyote ya kuongelea—utawachwa tupu, bila chochote. Ni nini utakachotumia kupeana uwajibikaji wako kwa Mungu? Je, una uchungu kuangalia Mungu? Unafaa kujitahidi katika shughuli yako sasa, ili mwishowe uweze, kama, Petro, kujua jinsi adabu na hukumu ya Mungu ina manufaa kwa binadamu, na bila adabu na hukumu Yake mwanadamu hawezi kuokolewa, na atazidi kuzama kwenye ardhi chafu, ndani zaidi kwenye tope. Wanadamu wamepotoshwa na Shetani, wamefitini wenyewe kwa wenyewe, wamekuliana njama wenyewe kwa wenyewe, wamepoteza heshima yao kwa Mungu, na uasi wao ni mkubwa sana, fikira zao ni nyingi, na wote ni wa Shetani. Bila adabu na hukumu ya Mungu, tabia potovu ya mwanadamu haiwezi kutakaswa na hangeweza kuokolewa. Kinachoelezwa na Mungu anayefanya kazi katika mwili hasa ndicho kile kinachoelezwa na Roho, na kazi afanyayo inafanyika kulingana na ile ifanywayo na Roho. Leo, kama huna maarifa yoyote juu ya hii kazi, basi wewe ni mpumbavu sana, na umepoteza mengi! Kama hujapata wokovu wa Mungu, basi imani yako ni ya kidini, na wewe ni Mkristo wa dini. Kwa sababu umeshikilia mafundisho yaliyokufa, umepoteza kazi mpya ya Roho Mtakatifu; wengine, wanaofuata upendo wa Mungu, wanaweza kupata ukweli na uhai, ambapo imani yako haiwezi kupata idhini ya Mungu. Badala yake, umekuwa mtenda maovu, mtu afanyaye vitendo vyenye kuharibu na vya chuki, umekuwa kilele cha utani wa Shetani, na mfungwa wa Shetani. Mungu si wa kuaminiwa na mwanadamu, lakini wa kupendwa na yeye, na kufuatwa na kuabudiwa na yeye. Usipomfuata leo, basi siku itakuja ambapo utasema, “Hapo zamani mbona sikumfuata Mungu vizuri sikumridhisha vizuri, sikufuatilia mabadiliko katika tabia yangu ya maisha? Najuta kutojiwasilisha kwa Mungu kwa wakati ufaao, na kutotafuta maarifa ya neno la Mungu. Mungu alisema mengi wakati ule; nilikosa vipi kufuata? Nilikuwa mjinga!” Utajichukia mpaka kiwango fulani. Leo, huamini maneno ninayosema, na huyatilii maanani; wakati utakapofika kwa hii kazi kuenezwa, na unaona ukamilifu wake, utajuta, na wakati huo utakuwa bubu. Kuna baraka, ilhali hujui kuzifurahia, na kuna ukweli, ilhali hujui kuufuata. Je, hujiletei dharau? Leo ingawa hatua inayofuata kwa kazi ya Mungu haijaanza, hakuna kitu cha kipekee juu ya mahitaji yanayohitajika kwako na unachoulizwa kuishi kwa kudhihirisha. Kuna kazi nyingi, na ukweli mwingi; Je, hazina maana kujulikana na wewe? Je, adabu na hukumu ya Mungu haitoshi kuamsha roho yako? Je, adabu na hukumu ya Mungu haitoshi kukufanya ujichukie? Umetosheka kuishi katika ushawishi wa Shetani, kwa amani na furaha, na raha kidogo ya kimwili? Je, wewe si mtu wa chini zaidi kati ya watu wote? Hakuna aliye mpumbavu kuliko wale ambao wameona wokovu lakini hawaufuati ili kuupata; hawa ni watu ambao wanalafua mwili na kufurahia Shetani. Unatumai kwamba imani yako kwa Mungu haitakuwa na changamoto ama dhiki, ama mateso yoyote. Unafuata vile vitu ambavyo havina maana, na huambatanishi faida yoyote kwa maisha, badala yake kuweka mawazo ya fujo kabla ya ukweli. Huna maana! Unaishi kama nguruwe—kuna tofauti gani kati yako, nguruwe na mbwa? Je, hao wasiofuata ukweli na badala yake wanafuata mapenzi ya kimwili, si wote ni wanyama? Hao waliokufa na bila roho si wafu wanaotembea? Maneno mangapi yamenenwa kati yenu? Je, kazi kidogo imefanywa kati yenu? Ni kiasi gani nimetoa kati yenu? Na mbona hujapata chochote? Una nini cha kulalamikia? Je, si ni kweli kuwa hujapata chochote kwa sababu unapenda mwili sana? Na ni kwa sababu mawazo yako ni ya fujo sana? Je, si kwa sababu wewe ni mpumbavu sana? Kama huna uwezo wa kupata baraka hizi, unaweza kumlaumu Mungu kwa kutokukuokoa? Unachofuata ni cha kukuwezesha kupata amani baada ya kumwamini Mungu—watoto wako wawe huru kutokana na magonjwa, ili mme wako apate kazi nzuri, ili mwana wako apate mke mwema, binti wako apate mme anayeheshimika, ili ndume na farasi wako walime shamba vizuri, kwa mwaka wa hali ya anga nzuri kwa mimea yako. Hili ndilo unalolitafuta. Harakati yako ni kuishi kwa starehe, ili ajali isipate familia yako, ili upepo ukupite, ili uso wako usiguswe na changarawe, ili mazao ya familia yako yasipate mafuriko, ili usiguswe na majanga yoyote, kuishi katika mikono ya Mungu, kuishi kwenye kiota chenye joto. Mwoga kama wewe, anafuata mwili kila wakati—je, una moyo, una roho? Si wewe ni mnyama? Nakupa njia ya ukweli bila kukuuliza chochote, ilhali hauifuati. Je, wewe ni wale wamwaminio Mungu? Nahifadhi uhai wa ukweli wa binadamu juu yako, ila hauufuati. Je, una tofauti kati ya nguruwe na mbwa? Nguruwe hawafuati maisha ya binadamu, hawafuati kutakaswa, na hawaelewi maana ya maisha. Kila siku wanapokula na kushiba, wanalala. Nimekupa njia ya ukweli, ila hujaipata: Wewe u mkono mtupu. Je, unakubali kuendelea na maisha haya, maisha ya nguruwe? Umuhimu wa watu hao kuwa hai ni nini? Maisha yako ni ya kudharauliwa na kutoheshimika, unaishi huku ukiwa na uchafu na uzinzi, na hufuati lengo lolote; je, si maisha yako ni ya kutoheshimika kwa yote? Je, una ujasiri wa kumtazamia Mungu? Ukiendelea kuwa na uzoefu wa haya, je, si utakosa kupata chochote? Umepewa njia ya ukweli, lakini kama utaipata ama hapana inategemea na kutafuta kwako. Watu husema Mungu ni Mungu wa haki, na kwamba mradi tu mwanadamu atamfuata mpaka mwisho, basi Hatakuwa na upendeleo kwa mwanadamu, kwani Yeye ni mwenye haki. Je, mwanadamu akimfuata mpaka mwisho kabisa, Mungu anaweza kumtupa mwanadamu nje? Sina upendeleo kwa mwanadamu yeyote, na Huwahukumu wanadamu wote kwa tabia Yangu ya haki, ilhali kuna mahitaji yanayofaa Ninayohitaji kutoka kwa mwanadamu, na Ninahitaji yakamilishwe na wanadamu wote, bila kujali ni nani. Sijali kiwango cha kufuzu kwako au kuheshimiwa kwako; najali tu kama utatembea kwa njia Yangu, na kama unapenda na una kiu ya ukweli. Kama huna ukweli, na unaleta aibu katika jina Langu, na matendo yako ni kinyume cha njia Yangu, kufuata tu bila kujali, basi wakati huo nitakupiga na kukuadhibu kwa uovu wako, na utakuwa na nini la kusema? Utaweza kusema Mungu si mwenye haki? Leo kama umezingatia maneno ambayo nimenena, basi wewe ni mtu ambaye Namkubali. Unasema umeumia ukifuata Mungu, kwamba umemfuata kwa marefu na mapana, na umeshiriki na yeye katika wakati mzuri na mbaya, lakini hujaishi kulingana na maneno yaliyosemwa na Mungu; unataka tu kukimbia huku na kule kwa ajili ya Mungu na kujitumia kwa ajili ya Mungu kila siku, na hujafikiria kuishi kwa kudhihirisha maisha yenye maana. Unasema pia, “Kwa vyovyote, naamini Mungu ni mwenye haki. Nimeteseka kwa ajili Yake, nikashughulika kwa ajili Yake, kujitoa kikamilifu Kwake, na nimefanya bidii ingawa sijapata kutambuliwa; Yeye hakika atanikumbuka.” Ni ukweli kwamba Mungu ni mwenye haki, na haki hii haijatiwa doa na uchafu wowote: Haina mapenzi ya binadamu, na haijatiwa doa na mwili, ama kitendo chochote cha binadamu. Wale wote ambao ni waasi na wako kwa upinzani, na hawazingatii njia Zake wataadhibiwa; hakuna atakayesamehewa, na hakuna atakayeepuka! Watu wengine husema, “Leo nakimbia juu yako; mwisho ukifika, utanipa baraka kidogo?” Sasa Nakuuliza, “Umezingatia maneno Yangu?” Haki unayoongelea inategemea matendo. Unafikiria kwamba Mimi ni mwenye haki, na asiye na mapendeleo kwa binadamu wote, na kwamba wale wanifuatao hadi mwisho wataokolewa na kupata baraka Yangu. Kuna maana ya ndani kwa maneno Yangu kwamba “wale wote wanifuatao hadi mwisho wataokolewa”: Wale wanifuatao mpaka mwisho ndio Nitakaowapata, ni wale, baada ya kushindwa Nami, watautafuta ukweli na kufanywa wakamilifu. Ni hali gani umepata? Umepata kunifuata hadi mwisho, lakini nini kingine? Je, umezingatia maneno Yangu? Umekamilisha moja kati ya tano ya mahitaji Yangu, ilhali huna mpango wa kumaliza manne yaliyobaki. Umepata ile njia rahisi, na ukafuata ukifikiria umebahatika. Kwa mtu kama wewe, haki Yangu ni adabu na hukumu, ni adhabu ya haki, na ni adhabu ya haki kwa watenda maovu wote; wale wote wasiotembea kwa njia Yangu wataadhibiwa, hata kama watafuata mpaka mwisho. Hii ndio haki ya Mungu. Wakati tabia hii ya haki inapodhihirishwa katika adhabu ya mwanadamu, mwanadamu atakosa la kusema, na kujuta kwamba, alipokuwa akimfuata Mungu hakutembea katika njia Yake. “Wakati huo niliteseka kidogo tu nikimfuata Mungu, lakini sikutembea katika njia ya Mungu. Kuna udhuru gani? Hakuna namna ila kuadibiwa!” Ila kwa akili yake anafikiria, “Nimefuata hadi mwisho, hata Ukiniadibu haitakuwa adabu kali, na baada ya kuadibu kwa kuchosha, bado Utanihitaji. Najua Wewe ni mwenye haki, na Hutanifanyia hivyo milele. Mimi si kama wale watakaofagiliwa nje; wale watakaofagiliwa watapokea adabu kuu, na adabu Yangu itakuwa kidogo.” Adabu ya Mungu ya tabia ya haki si unavyosema. Sio kwamba wale ambao wanatubu dhambi zao kila wakati wataadibiwa kwa huruma. Haki ni utakatifu, na ni tabia ambayo haivumilii makosa ya mwanadamu, na yale yote ambayo ni machafu na hayajabadilika ndiyo shabaha ya chukizo kwa Mungu. Haki ya Mungu si sheria, lakini amri ya utawala: Ni amri ya utawala katika ufalme, na hii amri ya utawala ni adhabu ya haki kwa yeyote asiye na ukweli na hajabadilika, na hakuna kiwango cha wokovu. Mwanadamu akiwekwa kulingana na aina, wazuri watazawadiwa na wabaya kuadhibiwa. Ndio wakati hatima ya mwanadamu itawekwa wazi, na ndio ni wakati ambao kazi ya wokovu itafika mwisho, baada ya hapo, kazi ya kuokoa binadamu haitafanyika tena, na adabu italetwa kwa wale waliotenda maovu. Watu wengine husema, “Mungu hukumbuka kila mmoja ambaye huwa kando Yake kila wakati. Hatasahau hata mmoja wetu. Tumehakikishiwa kufanywa wakamilifu na Mungu. Hatawakumbuka wowote walio chini, wale kati yao watakaofanywa wakamilifu wana uhakika kuwa watakuwa duni kutuliko sisi, tunaokutana na Mungu kila wakati; kati yetu hakuna ambaye amesahaulika na Mungu, wote tumeshakubaliwa na Mungu, na tunalo hakikisho la kufanywa wakamilifu na Mungu.” Nyote mna mawazo ya aina hii. Je, hii ni haki? Je, umeweka ukweli katika vitendo au la? Kwa hakika unaeneza uvumi kama huu—huna aibu!

Leo, watu wengine wanatafuta kutumiwa na Mungu, lakini baada ya kushindwa hawawezi kutumika moja kwa moja. Kwa maneno yaliyonenwa leo, kama, wakati Mungu anapotumia watu, bado huwezi kuyakamilisha, basi hujafanywa mkamilifu. Kwa maneno mengine, kufika kwa mwisho wa wakati ambao mwanadamu anafanywa mkamilifu kutabaini iwapo mwanadamu atatupwa ama atatumiwa na Mungu. Wale walioshindwa ni mifano wa kutojihusisha na uhasi tu; ni sampuli na mifano, lakini si chochote ila ni ujazio wa wimbo. Ni wakati tabia ya maisha ya mwanadamu imebadilika, na amepata mabadiliko ndani na nje, ndipo atakapokuwa amefanywa mkamilifu. Leo, ni nini utakacho, kushindwa ama kufanywa mkamilifu? Ni nini unachotamani kupata? Umetimiza masharti ya kufanywa mkamilifu? Ni yapi ambayo bado unakosa? Unapaswa kujihami vipi, na utaweka mikakati ipi ili kuondoa upungufu wako? Utaingia vipi katika njia ya kufanywa mkamilifu? Utajiwasilisha vipi kikamilifu? Unataka kufanywa mkamilifu, je, unafuata utakatifu? Je, wewe ni mtu anayetaka kupitia hukumu na kuadibu ili uweze kutakaswa? Unatafuta kutakaswa, kwa hivyo una nia ya kukubali adabu na hukumu? Unataka kujua Mungu, lakini je, una maarifa ya adabu na hukumu Yake? Leo, kazi nyingi Anayofanya kwenu ni adabu na hukumu; ufahamu wako wa kazi hii ni upi, ambayo imetekelezwa juu yako? Je, adabu na hukumu ambayo umepitia imekutakasa? Imekubadilisha? Imekuwa na mabadiliko yoyote kwako? Umechoka sana na kazi hii nyingi ya leo—laana, hukumu na ufichuzi—ama unaona mambo haya yakiwa ya manufaa kwako? Unapenda Mungu, lakini kwa nini unampenda Yeye? Je, unampenda Mungu kwa sababu umepokea neema kidogo? Ama unapenda Mungu baada ya kupata amani na furaha? Ama unampenda Mungu baada ya kutakaswa na adabu na hukumu yake? Ni nini hasa kinachokufanya umpende Mungu? Ni masharti yapi ndiyo Petro alikamilisha ili afanywe mkamilifu? Baada ya kufanywa mkamilifu, ni njia gani muhimu ndiyo ilitumiwa kudhihirisha? Je, alimpenda Bwana Yesu kwa sababu alitamani kuwa na Yeye, ama kwa sababu hangeweza kumuona, ama ni kwa sababu alikuwa ameshutumiwa? Ama alimpenda Bwana Yesu zaidi kwa sababu alikubali mateso ya shida, na alikuwa amejua uchafu wake na kuasi, alikuwa amepata kujua utakatifu wa Bwana? Je, mapenzi yake kwa Mungu yalikuwa safi kwa sababu ya adabu na hukumu ya Mungu, ama kwa sababu ya kitu kingine? Ni nini hasa? Unampenda Mungu kwa sababu ya neema ya Mungu, na kwa sababu leo amekupa baraka kidogo. Je, huu ni upendo wa ukweli? Unapaswa kumpenda Mungu vipi? Je, unapaswa kukubali kuadibu na hukumu Yake, na, baada ya kuona tabia Yake yenye haki, uweze kumpenda kwa kweli, hivi kwamba umeshawishika kabisa, na kuwa na maarifa Yake? Kama Petro, unaweza kusema kwamba huwezi kumpenda Mungu vya kutosha? Je, unachofuata kishindwe baada ya adabu na hukumu, ama kutakaswa, kimelindwa na kushughulikiwa baada ya adabu na hukumu? Ni gani kati ya haya unayofuata? Je, maisha yako yana maana ama hayana maana wala dhamani? Unataka mwili ama ukweli? Unataka hukumu, ama faraja? Baada ya kupitia na kuiona kazi nyingi ya Mungu, na baada ya kuuona utakatifu na haki ya Mungu, unafaa kumfuata vipi? Unapaswa kutembea vipi katika njia hii? Utahitajika kuweka mapenzi ya Mungu katika matendo kivipi? Je, adabu na hukumu ya Mungu zimekuwa na athari yoyote kwako? Kama una maarifa ya adabu na hukumu ya Mungu itategemea jinsi unavyoishi kwa kudhihirisha, na kiwango gani unapenda Mungu! Kinywa chako kinasema unampenda Mungu, ilhali unachoishi kwa kudhihirisha ni tabia nzee, zilizo potovu; humchi Mungu, na sembuse kuwa na dhamiri. Je, watu wa aina hii wanampenda Mungu? Je, watu wa aina hii ni waaminifu kwa Mungu? Je, wao ni wale wanaokubali adabu na hukumu ya Mungu? Unasema unampenda na kumwamini Mungu, ilhali huachi hisia zako. Katika kazi yako, kuingia kwako, maneno uzungumzayo, na katika maisha yako, hakuna udhihirisho wa mapenzi yako kwa Mungu, na hakuna heshima kwa Mungu. Je, huyu ni mtu ambaye amepata adabu na hukumu? Mtu kama huyu anaweza kuwa Petro? Wale walio kama Petro wana maarifa, lakini je, wanaishi kulingana nayo? Leo, ni hali gani inahitaji mwanadamu aishi kwa kudhihirisha maisha ya ukweli? Maombi ya Petro hayakuwa maneno matupu yaliyotoka mdomoni mwake? Hayakuwa maneno kutoka moyoni mwake? Petro aliomba tu, na hakuweka ukweli katika matendo? Kufuata kwako ni kwa niaba ya nani? Utajiwezeshaje kupokea ulinzi na utakaso wakati wa hukumu na kuadibu kwa Mungu? Je, adabu na hukumu ya Mungu haina faida yoyote kwa mwanadamu? Je, hukumu yote ni adhabu? Je, amani na furaha, baraka ya vitu vya dunia na faraja, ni muhimu kwa maisha ya mwanadamu? Mwanadamu akiishi katika mazingira mazuri ya raha, bila maisha ya hukumu, anaweza kutakaswa? Iwapo mwanadamu anataka kubadilika na kutakaswa, anafaa kukubali vipi kufanywa mkamilifu? Ni njia gani unayopaswa kuchagua leo?

Tanbihi:

a. “Foili” inahusu mtu au kitu kinachodhihirisha uzuri/ubora wa kingine kwa kuvilinganisha.

Iliyotangulia: Umuhimu wa Kuukoa Uzao wa Moabu

Inayofuata: Ni Lazima Muielewe Kazi—Msifuate kwa Rabsha!

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp