Fumbo la Kupata Mwili (1)

Katika Enzi ya Neema, Yohana alimwandalia Yesu njia. Hangeweza kufanya kazi ya Mungu Mwenyewe ila alitimiza tu kazi ya mwanadamu. Ingawa Yohana alikuwa mtangulizi wa Bwana; hangeweza kumwakilisha Mungu; alikuwa tu binadamu aliyetumiwa na Roho Mtakatifu. Kufuatia ubatizo wa Yesu, “Roho Mtakatifu alimshukia Yeye kwa mfano wa njiwa.” Kisha Akaanza kazi Yake, hivyo, Alianza kufanya huduma ya Kristo. Hiyo ndiyo maana Alichukua utambulisho wa Mungu, kwa sababu Alitoka Kwa Mungu. Haijalishi jinsi imani Yake ilivyokuwa kabla ya hii—labda wakati mwingine ilikuwa dhaifu, au wakati mwingine ilikuwa na nguvu—hayo ndiyo yalikuwa maisha Yake ya kawaida ya binadamu kabla Afanye huduma Yake. Baada ya kubatizwa (kuteuliwa), mara moja Alikuwa na nguvu na utukufu wa Mungu pamoja Naye, na hivyo Akaanza Kufanya huduma Yake. Angetenda ishara na maajabu, Atende miujiza, Alikuwa na nguvu na mamlaka, kwani Alifanya kazi kwa niaba ya Mungu Mwenyewe; Alifanya kazi ya Roho badala Yake na kuonyesha sauti ya Roho Mtakatifu; kwa hivyo Alikuwa Mungu Mwenyewe. Hili halina pingamizi. Yohana alitumiwa na Roho Mtakatifu. Hangemwakilisha Mungu, na hakungekuwa na uwezekano wa yeye kumwakilisha Mungu. Kama angetaka kufanya hivyo, Roho Mtakatifu hangelikubali, kwani hangeweza kufanya kazi ambayo Mungu Mwenyewe alinuia kukamilisha. Labda kulikuwa na mengi ndani yake yaliyokuwa ya mapenzi ya mwanadamu, ama kitu kilichokuwa cha mwacha maadili; hakuna hali yoyote ambapo angemwakilisha Mungu moja kwa moja. Makosa Yake na mambo yasiyo sahihi yalimwakilisha yeye pekee, lakini kazi Yake ilikuwa uwakilishi wa Roho Mtakatifu. Ilhali, huwezi kusema kuwa yeye mzima alimwakilisha Mungu. Je upotovu na kuwa kwake na makosa kungemwakilisha Mungu pia? Kuwa na makosa katika kumwakilisha mwanadamu ni kawaida, lakini kama alikuwa na upotovu katika kumwakilisha Mungu, basi si hiyo ingekuwa kutomheshimu Mungu? Je hilo halingekuwa kufuru dhidi ya Roho Mtakatifu? Roho Mtakatifu hawezi kumruhusu mwanadamu asimame mahali pa Mungu anavyotaka, hata kama anasifiwa na wengine. Kama yeye si Mungu, basi hataweza kubaki akiwa amesimama mwishowe. Roho Mtakatifu hamkubali mwanadamu amwakilishe Mungu vile mwanadamu atakavyo! Kwa mfano, Roho Mtakatifu alimshuhudia Yohana na pia kumtambulisha kuwa mmoja wa wale watakaomwandalia Yesu njia, lakini kazi iliyofanywa ndani Yake na Roho Mtakatifu ilikuwa imepimwa vizuri. Kilichotakiwa kwa Yohana ilikuwa awe wa kutayarisha njia ya Yesu tu, kumtayarishia Yesu njia. Hiyo ni kusema, Roho Mtakatifu Aliiunga mkono kazi yake katika kutengeneza njia na kumruhusu afanye kazi ya aina hiyo pekee, hakuna mwingine. Yohana alimwakilisha Eliya, na alimwakilisha nabii aliyetengeneza njia. Hili liliungwa mkono na Roho Mtakatifu; bora kazi yake iwe kutengeneza njia, Roho Mtakatifu aliiunga mkono. Hata hivyo, kama angeweka madai kwamba yeye ni Mungu Mwenyewe na amekuja kumaliza kazi ya ukombozi, Roho Mtakatifu lazima amwadhibu. Haijalishi ukuu wa kazi ya Yohana, na ingawa iliungwa mkono na Roho Mtakatifu, kazi Yake ilibaki katika mipaka. Ni ukweli hakika kuwa kazi yake iliungwa mkono na Roho Mtakatifu, lakini nguvu aliyopewa katika wakati huo iliwekewa mipaka tu katika kutengeneza njia. Hangeweza, hata kidogo, kufanya kazi nyingine, kwani alikuwa tu Yohana aliyetengeneza njia, ila si Yesu. Kwa hivyo ushuhuda wa Roho Mtakatifu ni muhimu, lakini kazi ambayo mwanadamu anaruhusiwa kufanya na Roho Mtakatifu ni muhimu zaidi. Je, Yohana hakushuhudiwa sana? Kazi yake haikuwa kuu pia? Lakini kazi aliyofanya haingeshinda ile ya Yesu, kwani alikuwa mwanadamu tu aliyetumiwa na Roho Mtakatifu na hangeweza kumwakilisha Mungu moja kwa moja, na kwa hiyo kazi aliyofanya ilikuwa yenye mipaka. Baada ya yeye kuimaliza kazi ya kuandaa njia, Roho Mtakatifu hakuthibitisha ushuhuda wake tena, hakuna kazi mpya iliyomfuata yeye tena, na aliondoka kazi ya Mungu Mwenyewe ilipoanza.

Kuna wengine ambao wamepagawa na roho wachafu na wanalia kwa kusisitiza wakisema, “Mimi ni Mungu!” Lakini mwishowe, hufichuliwa, kwani wanafanya kazi kwa niaba ya kiumbe asiyefaa. Wanawakilisha Shetani na Roho Mtakatifu hajali kuwahusu hata kidogo. Hata ujiinue vipi, ama kwa nguvu kivipi, wewe bado ni kiumbe aliyeumbwa na wewe unamilikiwa na Shetani. Mimi sipigi mayowe Nikisema, “Mimi ni Mungu, Mimi ni Mwana Mpendwa wa Mungu!” Lakini kazi Nifanyayo ni ya Mungu. Kuna haja Nipige mayowe? Hakuna haja ya kujiinua. Mungu hufanya kazi Yake Mwenyewe na hahitaji mwanadamu kumpa ruhusa ama cheo kubwa, na kazi Yake inatosha kuwakilisha utambulisho Wake na cheo. Kabla ya ubatizo Wake, si Yesu alikuwa Mungu Mwenyewe? Je, Yeye hakuwa mwili wa Mungu? Hakika haiwezi kusemekana kuwa Alikuwa Mwana wa pekee wa Mungu baada ya kushuhudiwa? Je, hakukuwa na mwanadamu jina lake Yesu kitambo kabla Aanze kazi Yake? Huwezi kuleta njia mpya ama kumwakilisha Roho. Huwezi kueleza kazi ya Roho ama maneno Anenayo. Huwezi kufanya kazi ya Mungu Mwenyewe ama ile ya Roho. Huwezi kuelezea hekima, ajabu na mambo ya Mungu yasiyoeleweka, ama tabia yote ambayo Mungu humwadibu mwanadamu kupitia kwayo. Kwa hivyo madai yako ya kila mara ya kusema kuwa wewe ni Mungu hayajalishi; unalo tu jina lakini huna dutu. Mungu Mwenyewe Amekuja, lakini hakuna anayemtambua, ilhali Anaendelea na kazi Yake na Anafanya hivyo kwa uwakilishi wa Roho. Haijalishi unamwita mwanadamu ama Mungu, Bwana ama Kristo, ama umwite dada, yote ni sawa. Lakini kazi Afanyayo ni ile ya Roho na Anawakilisha kazi ya Mungu Mwenyewe. Hajali ni jina gani mwanadamu anamwita. Je, jina hilo linaweza kuamua kazi Yake? Bila kujali unachomwita, kutoka kwa mtazamo wa Mungu, Yeye ni kupata mwili kwa Roho wa Mungu; Anawakilisha Roho na amekubaliwa na Yeye. Huwezi kutengeneza njia ya enzi mpya, na huwezi kuhitimisha enzi nzee na huwezi kukaribisha enzi mpya ama kufanya kazi mpya. Kwa hivyo, huwezi kuitwa Mungu!

Hata mwanadamu anayetumiwa na Roho Mtakatifu hawezi kumwakilisha Mungu Mwenyewe. Na mwanadamu huyu hawezi tu kumwakilisha Mungu bali pia kazi yake haiwezi kumwakilisha Mungu moja kwa moja. Hivyo ni kusema uzoefu wa mwanadamu hauwezi kuwekwa moja kwa moja katika usimamizi wa Mungu, na hauwezi kuwakilisha usimamizi wa Mungu. Kazi yote ambayo Mungu Mwenyewe hufanya ni kazi Anayolenga Kufanya katika mpango Wake wa usimamizi na inahusiana na usimamizi mkuu. Kazi ifanywayo na mwanadamu (mwanadamu anayetumiwa na Roho Mtakatifu) hukidhi uzoefu wake binafsi. Anapata njia mpya ya uzoefu mbali na ile iliyotembelewa na wale waliomtangulia na anawaongoza ndugu zake chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu. Kinachotolewa na watu hawa ni uzoefu wao ama maandishi ya kiroho ya watu wa kiroho. Ingawa wanatumiwa na Roho Mtakatifu, kazi ya watu kama hao haina uhusiano na kazi ya usimamizi mkuu katika mpango wa miaka elfu sita. Wamesimamishwa na Roho Mtakatifu katika wakati tofauti kuongoza watu katika mkondo wa Roho Mtakatifu hadi wakamilishe kazi yao ama maisha yao yafike mwisho. Kazi wanayofanya ni kutayarisha njia ifaayo kwa ajili ya Mungu Mwenyewe ama kuendeleza kitu kimoja kwa usimamizi wa Mungu Mwenyewe katika dunia. Watu hao hawawezi kufanya kazi kuu katika usimamizi Wake, na hawawezi kufungua njia mpya, ama kumaliza kazi yote ya Mungu kutoka enzi ya kitambo. Kwa hivyo, kazi wafanyayo inawakilisha kiumbe aliyeumbwa pekee akifanya kazi Yake na hawezi kuwakilisha Mungu Mwenyewe Akifanya huduma Yake. Hii ni kwa sababu kazi wanayofanya haifanani na ile inayofanywa na Mungu Mwenyewe. Kazi ya kukaribisha enzi mpya haiwezi kufanywa na mwanadamu kwa niaba ya Mungu. Haiwezi kufanywa na mwingine ila Mungu Mwenyewe. Kazi yote inayofanywa na mwanadamu ni kufanya wajibu wake kama mmoja wa viumbe na inafanywa akiguswa au kupewa nuru na Roho Mtakatifu. Uongozi ambao watu hao hupeana ni jinsi ya kuzoea katika kila siku ya maisha ya mwanadamu na jinsi mwanadamu anapaswa kutenda kwa maelewano na mapenzi ya Mungu. Kazi ya mwanadamu haihusishi usimamizi wa Mungu ama kuwakilisha kazi ya Roho. Kama mfano, kazi ya Witness Lee na Watchman Nee ilikuwa ni kuongoza njia. Njia iwe mpya au nzee, kazi ilifanywa kwa misingi ya kanuni ya kutozidi Biblia. Haijalishi kama makanisa ya mitaa yalirejeshwa yalivyokuwa awali au yalijengwa, kazi yao ilikuwa ni kuanzisha makanisa. Kazi waliyofanya iliendeleza kazi ambayo Yesu Kristo na mitume Wake walikuwa hawajamaliza au kuendeleza zaidi kwenye Enzi ya Neema. Kile walichofanya katika kazi yao kilikuwa ni kurejesha kile ambacho Yesu Kristo Alikuwa Ameomba katika kazi Yake ya vizazi vitakavyokuja baada Yake Yeye, kama vile kuhakikisha kwamba vichwa vyao vimefunikwa, ubatizo, umegaji mkate, au unywaji wa mvinyo. Inaweza kusemekana kwamba kazi yao ilikuwa kubakia tu kwenye Biblia na kutafuta njia zinazotokana tu na Biblia. Hawakupiga hatua yoyote mpya kamwe. Hivyo basi, mtu anaweza kuona tu ugunduzi wa njia mpya ndani ya Biblia, pamoja na mazoea bora zaidi na yenye uhalisia zaidi. Lakini mtu hawezi kupata katika kazi yao mapenzi ya sasa ya Mungu, isitoshe hawezi kupata kazi mpya ambayo Mungu Atafanya kwenye siku za mwisho. Hii ni kwa sababu njia ambayo walitembelea ilikuwa bado ile nzee; hakukuwa na maendeleo yoyote na kitu chochote kipya. Waliendelea kuufuata ukweli wa “kule kusulubishwa kwa Yesu,” mazoea ya “kuwaomba watu kutubu na kukiri dhambi zao,” msemo kwamba “yule atakayevumilia hata mwisho ataokoka,” na msemo kwamba “mwanamume ndiye kichwa cha mwanamke, na mwanamke lazima amtii mume wake.” Aidha, waliendeleza dhana ya kitamaduni kwamba “akina dada hawawezi kuhubiri, na wanaweza tu kutii.” Ikiwa njia kama hiyo ya uongozi ingeendelea, basi Roho Mtakatifu asingewahi kuweza kutekeleza kazi mpya, kuwaweka binadamu huru kutokana na mafundisho, au kuwaongoza binadamu kwenye himaya ya uhuru na urembo. Hivyo basi, hatua hii ya kazi ya mabadiliko ya enzi lazima ifanywe na kuzungumzwa na Mungu Mwenyewe, la sivyo hakuna mwanadamu anayeweza kufanya hivyo badala Yake. Mpaka hapa, kazi yote ya Roho Mtakatifu iliyo nje ya mfululizo huu imesimama, na wale waliotumiwa na Roho Mtakatifu wamepoteza mwelekeo wao. Kwa hivyo, kwa sababu kazi ya wanadamu wanaotumiwa na Roho Mtakatifu si sawa na kazi ifanywayo na Mungu Mwenyewe, utambulisho wao na wanayefanya kazi kwa niaba yake ni tofauti. Hii ni kwa sababu kazi ambayo Roho Mtakatifu Analenga Kufanya ni tofauti, na hapo kutoa utambulisho tofauti na hadhi kwa wale wote wafanyao kazi. Wanadamu wanaotumiwa na Roho Mtakatifu wanaweza kufanya kazi mpya na wanaweza kutoa kazi iliyofanywa katika enzi iliyopita, lakini kazi yao haiwezi kueleza tabia na mapenzi ya Mungu kwa enzi mpya. Wanafanya kazi ili kuondoa kazi ya enzi iliyopita tu, sio kufanya kazi mpya kuwakilisha moja kwa moja tabia ya Mungu Mwenyewe. Hivyo, haijalishi matendo mangapi yaliyopitwa na wakati wanakomesha ama matendo mapya wanaanzisha, bado wanawakilisha mwanadamu na viumbe vilivyoumbwa. Mungu Mwenyewe Akifanya kazi, hata hivyo, Hatangazi wazi kukomeshwa kwa matendo ya enzi ya zamani au kutangaza moja kwa moja kuanzishwa kwa enzi mpya. Yeye hufanya kazi Yake moja kwa moja na kwa njia ya moja kwa moja. Yeye hufanya kazi Anayolenga kufanya moja kwa moja; hivyo, yeye hueleza moja kwa moja kazi Aliyoleta, Anafanya kazi Yake moja kwa moja Alivyolenga hapo awali, Akieleza uwepo Wake na tabia Yake. Mwanadamu anavyoona, tabia Yake na kazi Yake pia hazifanani na zile ya kitambo. Hata hivyo, kutoka kwa mtazamo wa Mungu Mwenyewe, huku ni kuendelea na ujenzi zaidi wa kazi Yake. Mungu Mwenyewe Akifanya kazi, Anaeleza neno Lake na Analeta kazi mpya moja kwa moja. Tofauti ni, mwanadamu akifanya kazi, ni kwa ukombozi na kusoma, ama ni kwa maendeleo ya maarifa na mpangilio wa mazoezi iliyojengwa juu ya msingi wa kazi za wengine. Hiyo ni kusema, umuhimu wa kazi inayofanywa na mwanadamu ni ya kuweka mkataba na “kutembea njia za kitambo kwa vitu mpya.” Hii inamanisha kuwa hata njia ambayo inatembelewa na watu wanaotumiwa na Roho Mtakatifu imejengwa juu ya yale yalifunguliwa na Mungu Mwenyewe. Kwa hivyo mwanadamu ni baada ya yote mwanadamu, na Mungu ni Mungu.

Yohana alizaliwa kwa ahadi, kama vile Isaka alivyozaliwa kwa Abrahamu. Alimwandalia Yesu njia na alifanya kazi nyingi, lakini hakuwa Mungu. Badala yake, anafikiriwa kuwa ni nabii kwa sababu alimwandalia tu Yesu njia. Kazi yake ilikuwa kuu pia, na ni baada ya yeye kuandaa njia tu ndipo Yesu akaanza kazi Yake kwa urasimu. Kimsingi, yeye alimfanyia tu Yesu kazi, na kazi yake ilikuwa katika huduma ya kazi ya Yesu. Baada ya yeye kuiandaa njia, Yesu akaanza kazi Yake, kazi iliyokuwa mpya zaidi, dhahiri zaidi, na katika utondoti mkubwa zaidi. Yohana alifanya tu kazi ya mwanzo; nyingi ya kazi mpya ilifanywa na Yesu. Yohana alifanya kazi mpya pia, lakini sio yeye aliyeianzisha enzi mpya. Yohana alizaliwa kwa ahadi, na jina lake kupewa na malaika. Katika wakati huo wengine walitaka kumpa jina la baba yake Zakaria, lakini mama yake alinena akisema, “Mtoto huyu hawezi kuitwa kwa jina hilo. Anapaswa kuitwa Yohana.” Haya yote yalielekezwa na Roho Mtakatifu. Jina la Yesu pia lilikuwa limeelekezwa na Roho Mtakatifu, na Alizaliwa wa Roho Mtakatifu, na kwa ahadi ya Roho Mtakatifu. Yesu Alikuwa Mungu, Kristo, na Mwana wa mtu. Kazi ya Yohana ilikuwa kuu pia, lakini mbona hakuitwa Mungu? Ni nini tofauti kati ya kazi iliyofanywa na Yesu na ile iliyofanywa na Yohana? Je, sababu pekee ni kwa kuwa Yohana ndiye aliyetengeneza njia ya Yesu? Au ni kwa sababu ilikuwa imepangwa na Mungu? Ingawa Yohana alisema kuwa, “Ninyi tubuni: kwa kuwa ufalme wa mbinguni uko karibu,” na kuhubiri pia injili ya ufalme wa mbinguni, kazi yake haikuwa yenye kina na ilijumuisha tu mwanzo. Kinyume, Yesu Alikaribisha enzi mpya na kuikamilisha enzi ya kitambo, lakini pia Alitimiza sheria ya Agano la Kale pia. Kazi Aliyofanya ni kubwa kuliko ile ya Yohana, na Alikuja kuwakomboa wanadamu wote—Alifanya hatua hii ya kazi. Yohana alitayarisha tu njia. Ingawa kazi yake ilikuwa kubwa, maneno yake mengi, na wale wafuasi waliomfuata wengi, kazi yake haikufanya kitu kingine ila kuletea mwanadamu mwanzo mpya. Mwanadamu hakupokea maisha, njia, ama ukweli wa ndani kutoka kwake, wala mwanadamu hakupata kupitia kwake ufahamu wa mapenzi ya Mungu. Yohana alikuwa nabii mkuu (Eliya) aliyeanza msingi mpya wa kazi ya Yesu na kutayarisha aliyeteuliwa; alikuwa mtangulizi wa Enzi ya Neema. Mambo kama haya hayawezi kutambuliwa kirahisi kwa kuchunguza kuonekana kwao kwa kawaida. Hasa sana, Yohana alifanya kazi kubwa; zaidi ya hayo, alizaliwa kutoka kwa ahadi ya Roho Mtakatifu, na kazi yake ikashikiliwa na Roho Mtakatifu. Hivyo, kutofautisha kati ya utambulisho wao inaweza kufanywa tu kupitia kazi yao, kwa kuwa sura tu ya nje ya mwanadamu haiwezi kuonyesha dutu yake, na mwanadamu hawezi kuhakikisha ushuhuda wa kweli wa Roho Mtakatifu. Kazi iliyofanywa na Yohana na ile iliyofanywa na Yesu si sawa na ilikuwa ya asili tofauti. Hii ndiyo inafaa kuonyesha kama yeye ni Mungu ama sio Mungu. Kazi ya Yesu ilikuwa kuanza, kuendelea, kuhitimisha na kukamilisha. Kila moja ya hatua hizi zilichukuliwa na Yesu, ilhali kazi ya Yohana haikuwa zaidi ya kuanzisha. Hapo mwanzo, Yesu Alieneza injili na kuhubiri njia ya kutubu, na Akaendelea mpaka kumbatiza mwanadamu, kuponya magonjwa, na kukemea mapepo. Mwishowe, Alimkomboa mwanadamu kutoka kwa dhambi na kukamilisha kazi Yake ya enzi yote. Alimhubiria mwanadamu na kueneza injili ya ufalme wa mbinguni katika sehemu zote. Hii ilikuwa sawa na Yohana, tofauti ikiwa kwamba Yesu Alikaribisha enzi mpya na kuleta Enzi ya Neema kwa mwanadamu. Kutoka kwa Mdomo Wake lilitoka neno jinsi mwanadamu anavyopaswa kutenda na njia mwanadamu anayopaswa kufuata Enzi ya Neema, na mwishowe, Akamaliza kazi ya Wokovu. Kazi kama hiyo haingeweza kutekelezwa na Yohana. Kwa hivyo, ni Yesu ndiye Aliyefanya Kazi Ya Mungu Mwenyewe, na ni Yeye ndiye Mungu Mwenyewe na Anamwakilisha Mungu moja kwa moja. Dhana za mwanadamu zinasema kwamba wale wote waliozaliwa kwa ahadi, waliozaliwa kwa Roho, waliothibitishwa na Roho Mtakatifu, na waliozifungua njia mpya ni Mungu. Kwa kadri ya fikira hii, Yohana pia angekuwa Mungu, na Musa, Abrahamu, na Daudi…, wao pia wangekuwa Mungu. Je, huu sio mzaha mkubwa? 

Kabla ya kutekeleza huduma Yake, Yesu pia alikuwa mtu wa kawaida tu Aliyefuata kazi yoyote ile ya Roho Mtakatifu. Haijalishi kama Alifahamu utambulisho Wake mwenyewe wakati huo, Alitii yote yaliyotoka kwa Mungu. Roho Mtakatifu hakufichua kamwe utambulisho Wake kabla ya kuanza kwa huduma Yake. Ni baada ya Yeye kuanza huduma Yake ndipo Alitangua amri hizo na sheria hizo, na ni baada tu ya Yeye kuanza kwa urasimu kutekeleza huduma Yake ndipo maneno Yake yakajaa mamlaka na nguvu. Ni baada tu ya kuanza huduma Yake ndipo kazi Yake ya kuleta enzi mpya ilianza. Kabla ya hili, Roho Mtakatifu aliendelea kujificha ndani Yake kwa miaka 29, wakati ambapo Alimwakilisha mwanadamu tu na hakuwa na utambulisho wa Mungu. Kazi ya Mungu ilianza na Yeye kufanya kazi na kutekeleza huduma Yake, Aliifanya kazi Yake kama ilivyopangwa ndani, bila kujali mwanadamu alijua kiasi gani kumhusu, na kazi Yake ilikuwa uwakilishi wa moja kwa moja wa Mungu Mwenyewe. Wakati huo, Yesu aliwauliza waliokuwa karibu na Yeye, “Mnasema Mimi ni nani?” Nao wakajibu, “Wewe ni mkuu zaidi kati ya manabii na tabibu wetu mwema.” Na wengine wakajibu, “Wewe ni kuhani mkuu wetu.” … Majibu mbalimbali yalitolewa; wengine walisema kwamba Alikuwa Yohana, kwamba Alikuwa Eliya. Kisha Yesu akamgeukia Simoni Petro na kuuliza, “Wewe unasema Mimi ni nani?” Petro akajibu, “Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aishiye.” Tangu wakati huo kuendelea watu wakafahamu kwamba Yeye alikuwa Mungu. Hili lilipofahamishwa, ni Petro ndiye aliyekuwa wa kwanza kupata utambuzi huu na kutoka kinywani mwake hayo yalisemwa. Kisha Yesu akanena, “Ulichosema hakikufichuliwa na mwili na damu, bali na Baba Yangu.” Baada ya ubatizo Wake, kama ilijulikana kwa wengine au la, kazi Yake ilikuwa kwa niaba ya Mungu. Alikuja kuitekeleza kazi Yake, sio kufichua utambulisho Wake. Ni baada tu ya maneno hayo kusemwa na Petro ndipo utambulisho Wake ukajulikana na mwanadamu kwa dhahiri. Kama ulifahamu kwamba Alikuwa Mungu Mwenyewe au la, Alianza kazi Yake wakati ambapo muda ulifika. Aliendelea na kazi Yake kama ulifahamu au la. Hata kama ungeikana, Angeitekeleza kazi Yake na angeimaliza ulipokuwa wakati wa kufanya hivyo. Alikuja kufanya kazi na kutekeleza huduma Yake, sio kwa mwanadamu kuujua mwili Wake, bali kwa mwanadamu kuipokea kazi Yake. Iwapo hutambui kwamba hatua ya kazi siku hii ni ile ya Mungu Mwenyewe, ni kwa sababu huna maono. Hata hivyo, huwezi kukataa hatua hii ya kazi; kukosa kwako kuitambua hakumaanishi kuwa Roho Mtakatifu hafanyi kazi ama ya kwamba kazi Yake si sawa. Wengine hata hulinganisha kazi ya wakati huu dhidi ya ile ya Yesu katika Biblia, na kutumia tofauti zilizopo kati ya kazi hizi kukataa hatua hii ya kazi. Je haya si matendo ya aliyepofushwa? Yote yaliyoandikwa katika Biblia ni machache na hayawezi kuwakilisha kazi yote ya Mungu. Injili Nne zina chini ya sura mia moja zote pamoja ambamo mliandikwa mambo yale yaliotendeka yanayohesabika, kwa mfano Yesu Akilaani mti wa mkuyu, Petro akimkana Bwana mara tatu, Yesu Akiwaonekania wanafunzi Wake baada ya kusulubiwa na ufufuo Wake, Akifunza kuhusu kufunga, kufunza kuhusu maombi, kufunza kuhusu talaka, kuzaliwa na kizazi cha Yesu, uteuzi wa Yesu wa wanafunzi, na mengine mengi. Hata hivyo, mwanadamu anayathamini kama hazina, hata kuthibitisha kazi ya leo kulingana nayo. Hata wanaamini kuwa Yesu Alitenda kiasi tu katika muda baada ya kuzaliwa Kwake. Ni kana kwamba wanaamini kuwa Mungu anaweza kufanya hayo tu, kwamba hakuna kazi nyingine. Je huu si upumbavu? 

Kipindi ambacho Yesu alikuwa nacho duniani kilikuwa miaka thelathini na mitatu na nusu, yaani, Aliishi duniani miaka thelathini na mitatu na nusu. Ni miaka mitatu na nusu pekee ya kipindi hiki ndiyo iliyotumiwa kutekeleza huduma Yake, na, ile iliyobaki, Aliishi tu maisha ya binadamu ya kawaida. Hapo mwanzo, Alihudhuria ibada katika sinagogi na hapo Alisikiliza mahubiri ya makuhani, na ujumbe wa wengine; Alipata ufahamu mwingi wa Biblia. Hakuzaliwa na ufahamu kama huo, na aliupata tu kupitia kusoma na kusikiliza. Imerekodiwa kwa dhahiri ndani ya Biblia kwamba Aliwauliza waalimu maswali ndani ya sinagogi alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili: Unabii wa manabii wa zamani ulikuwa upi? Na kuhusu sheria za Musa? Maandiko? Na kuhusu mwanadamu kumhudumia Mungu katika mavazi ya kikuhani ndani ya hekalu? … Aliuliza maswali mengi, kwani Hakuwa na maarifa au ufahamu. Ingawa mimba Yake ilitungwa na Roho Mtakatifu, Alizaliwa kama mwanadamu wa kawaida kamili. Licha ya sifa nyingine maalumu, Yeye hata hivyo alikuwa mwanadamu wa kawaida. Hekima Yake ilikua kwa kuendelea kwa kukubaliana na kimo na umri Wake, na maisha Yake yaliendelea kama yale ya mwanadamu wa kawaida. Katika mawazo ya mwanadamu, Yesu hakupitia utoto na wala ujana; mwanadamu ana fikira kwamba Alizaliwa katika maisha ya mwanadamu mwenye umri wa miaka thelathini na mitatu, na Akasulubiwa baada ya kuimaliza kazi Yake. Wao huamini kwamba labda maisha Yake hayakupitia maendeleo kama ya mwanadamu wa kawaida; labda Hakula wala kushirikiana na mwanadamu, na Hakutazamwa kwa urahisi na mwanadamu. Labda Alikuwa mkengeuko ambaye angewatisha wale waliomwona Yeye, kwani Yeye ni Mungu. Watu huamini kuwa Mungu mwenye Mwili lakini haishi jinsi mwanadamu wa kawaida anavyoishi; wanaamini kuwa ni msafi hata hawezi kusugua meno Yake ama kuosha uso Wake, kwani ni mtu mtakatifu. Je hizi kikamilifu si dhana ya mwanadamu? Biblia haina rekodi yoyote kuhusu maisha ya Yesu kama mwanadamu, kazi Yake pekee, lakini hili halithibitishi kuwa hakuwa na ubinadamu wa kawaida ama hakuishi maisha ya mwanadamu wa kawaida kabla ya umri wa miaka thelathini. Alianza kazi Yake rasmi Akiwa na miaka 29, lakini huwezi kukana maisha Yake yote kama mwanadamu kabla ya umri huo. Biblia iliacha hatua hiyo katika maandishi Yake; kwani yalikuwa maisha Yake kama mwanadamu wa kawaida na si hatua ya kazi Yake takatifu, hakukuwa na haja ya maneno hayo kuandikwa chini. Kwani kabla ya ubatizo wa Yesu, Roho Mtakatifu hakufanya kazi Yake moja kwa moja, lakini akadumisha maisha Yake kama mwanadamu wa kawaida tu hadi siku ambayo Yesu Alikuwa Anapaswa kuanza huduma Yake. Ingawa Alikuwa Mungu katika mwili, Alipitia mchakato wa kukomaa kama jinsi mwanadamu wa kawaida afanyavyo. Hatua hii iliwachwa nje ya Biblia, kwani haingeleta usaidizi mkubwa kwa kukuwa kwa maisha ya mwanadamu. Kabla ya ubatizo Wake ulikuwa wakati ambapo hakujulikana, na wala Hakutenda ishara na miujiza. Baada tu ya ubatizo wa Yesu ndipo Alipoanza kazi ya ukombozi wa mwanadamu, kazi ambayo imejaa sana neema, ukweli, na upendo na huruma. Mwanzo wa kazi hii ndio ulikuwa pia mwanzo wa Enzi ya Neema; kwa sababu hii, matukio haya yaliandikwa chini na kupitishwa kwa vizazi mpaka wakati huu. Ilifungua njia na kuyafanya yote kupata mafanikio kwa wale walio katika Enzi ya Neema kuitembea njia ya enzi hiyo na kuitembea njia ya msalaba. Ingawa rekodi za hayo ziliandikwa na mwanadamu, zote ni maelezo ya ukweli, zenye makosa madogo tu katika mambo fulani. Hata hivyo, mtu hawezi kukana ukweli wa mambo hayo. Hayo yote ni ya ukweli, ingawa makosa yalionekana yalipoandikwa na mwanadamu. Kuna wengine atakaosema kwamba, kama Yesu alikuwa sawa na binadamu kawaida, kwa hiyo ingekuwaje kwamba Alikuwa mwenye uwezo wa kufanya ishara na maajabu? Siku arobaini za majaribu ambayo Yesu alipitia ni ishara ya muujiza, ambayo mwanadamu wa kawaida hangekuwa na uwezo wa kutimiza. Siku Zake arobaini za majaribu ilikuwa kazi ya Roho Mtakatifu; basi ni vipi ambavyo mtu anaweza kusema kwamba hakuna ya rohoni hata kidogo ndani Yake? Kufanya Kwake ishara na maajabu hakuonyeshi kwamba Hakuwa mwanadamu wa kawaida bali mwanadamu anayezidi uwezo wa binadamu; ni kwamba tu Roho Mtakatifu alifanya kazi ndani ya mwanadamu wa kawaida kama Yeye, na hivyo kumwezesha Yeye kutekeleza miujiza na kufanya kazi kuu zaidi. Kabla ya Yesu kufanya huduma Yake, ama isemwavyo katika Biblia, kabla ya Roho Mtakatifu kushuka juu Yake, Yesu Alikuwa mwanadamu wa kawaida na bila kuwa na chochote kisicho cha kawaida. Roho Mtakatifu Aliposhuka, hiyo ni, Alipoanza kazi ya huduma Yake, Alijazwa na vitu vya kimiujiza. Kwa njia hii, mwanadamu anaanza kuamini kwamba mwili wa Mungu hauna ubinadamu wa kawaida; aidha anafikiri kimakosa kwamba Mungu mwenye mwili ana uungu tu, sio ubinadamu. Hakika, Mungu akujapo duniani kufanya kazi Yake, yote aonayo mwanadamu ni matukio yasiyo ya kawaida. Chote anachoona kwa macho yake na anachosikia kwa masikio yake si cha kawaida, kwani kazi Yake na maneno Yake hayaeleweki na kufikiwa naye. Kitu cha mbinguni kikiletwa duniani, itakuwa vipi kiwe kitu cha kawaida? Mafumbo ya ufalme wa mbinguni yanapoletwa duniani, mafumbo yasiyoweza kufikiriwa na kueleweka na mwanadamu, ambayo ni ya ajabu na yenye hekima—yote si yasiyo ya kawaida? Hata hivyo, unapaswa kujua kuwa, haijalishi jinsi kisicho cha kawaida, mambo yote yanatekelezwa katika ubinadamu Wake wa kawaida. Mwili wa Mungu umejaa ubinadamu, la sivyo, haungekuwa Mwili wa Mungu katika mwili. Katika wakati huo, Yesu alitenda miujiza mingi sana. Kile ambacho Waisraeli wa wakati huo waliona kilijaa mambo yasiyo ya kawaida; walitazama malaika na wajumbe, na walisikia sauti ya Yehova. Je, haya yote hayakuwa yasiyo ya kawaida? Bila shaka, leo kunao baadhi ya pepo wabaya wanaomdanganya mwanadamu kutumia mambo yasiyo ya kawaida; hilo si chochote bali ni uigaji kwa upande wao, kumpotosha mwanadamu kupitia kwa kazi ambayo kwa sasa haifanywi na Roho Mtakatifu. Watu wengi hufanya miujiza na kuwaponya wagonjwa na kufukuza mapepo; hizi ni kazi za pepo wabaya tu, kwani Roho Mtakatifu hafanyi tena kazi kama hiyo leo na wale wote ambao wameiga kazi ya Roho Mtakatifu kutoka wakati huo kuendelea—wao ni pepo wabaya kweli. Kazi yote iliyotekelezwa Israeli wakati huo ilikuwa ile ya miujiza, ingawa Roho Mtakatifu sasa hafanyi kazi kwa njia hiyo, na kazi yoyotekama hiyo sasa ni kuiga na kujificha kwa Shetani na usumbufu wake. Lakini huwezi kusema kwamba mambo yote ya rohoni ni shughuli ya pepo waovu. Hili linategemea enzi ya kazi ya Mungu. Ni kazi gani inayofanywa na Mungu aliyepata mwili siku hii si ya rohoni? Maneno Yake ni yasiyoeleweka na yasiyofikika kwako, na kazi Yake haiwezi kufanywa na mwanadamu. Kile kilicho katika ufahamu Wake hakiwezi kueleweka na mwanadamu, na wala mwanadamu hawezi kujua maarifa Yake yanatoka wapi. Wengine husema, mimi pia ni wa kawaida kama Wewe, ni kwa nini mimi sijui unachojua Wewe? Mimi ni mzee zaidi na mwingi zaidi wa uzoefu, ilhali Wewe unawezaje kujua kile nisichojua mimi? Haya yote ni yasiyofikika kwa mwanadamu. Kisha kuna wale ambao husema, “Hakuna anayejua kazi iliyotekelezwa Israeli, na hata wafasiri wa Biblia hawawezi kutoa ufafanuzi; mbona Wewe unajua?” Haya yote siyo mambo ya miujiza? Hajawahi kupitia maajabu yoyote, ilhali Anayajua yote; Anazungumza na kuonyesha ukweli kwa urahisi sana. Je, hili sio jambo la kimuijiza? Kazi Yake inazidi ile inayofikika kwa mwili. Kazi hiyo haiwezi hasa kutimizwa kwa fikira zozote za mwili na ni isiyowazika kabisa kwa mawazo na fikira ya mwanadamu. Ingawa hajasoma Biblia asilani, Yeye huelewa kazi ya Mungu katika Israeli. Na ingawa Yeye husimama duniani Anapozungumza, Yeye huzungumza kuhusu mafumbo ya mbingu ya tatu. Mwanadamu atazamapo maneno haya, hisia humlemea mwanadamu, “Je, hii siyo lugha ya mbingu ya tatu?” Haya yote siyo mambo yanayozidi kile ambacho mwanadamu wa kawaida anaweza kukifikia? Wakati huo, Yesu alipofanya mfungo wa siku arobaini, hilo halikuwa la rohoni? Ukisema kwamba mfungo wa siku arobaini ni la rohoni na kitendo cha pepo waovu, basi hujamshutumu Yesu? Kabla ya Yesu kutekeleza huduma Yake, Alikuwa kama wanadamu wote wa kawaida. Yeye pia alisoma shuleni; ni vipi vinginevyo ambavyo angejifunza kusoma na kuandika? Mungu alipopata mwili, Roho alijificha ndani ya mwili. Hata hivyo, kama wanadamu wote wa kawaida, ilikuwa lazima Yeye apitie mchakato wa ukuaji, na ni baada tu ya akili na fikira Zake kukomaa na Yeye kuweza kutambua mambo, ndipo Alifikiriwa kuwa mwanadamu wa kawaida. Ni baada tu ya ubinadamu Wake kukomaa ndipo Angeweza kutekeleza huduma Yake. Angewezaje kutekeleza huduma Yake ilhali ubinadamu Wake ulikuwa bado haujakomaa na fikira Zake zikiwa pungufu? Kwa hakika Hangetarajiwa kutekeleza huduma Yake akiwa na umri wa miaka sita au saba! Mbona Mungu hakujidhihirisha Mwenyewe wazi wakati ambapo Mungu alipata mwili kwanza? Kwa sababu ubinadamu wa mwili Wake ulikuwa bado haujakomaa; mawazo na akili, pamoja na ubinadamu wa kawaida wa mwili huo, havikuwa vimemilikiwa kwa ukamilifu. Kwa sababu hii, ilikuwa lazima bila shaka kwa Yeye kumilikiwa na ubinadamu wa kawaida na maarifa ya kawaida ya mwanadamu wa kawaida mpaka viweze kutosha kufanya kazi Yake katika mwili. Ni wakati huo tu ndipo Angeanza kazi Yake, la sivyo ingekuwa lazima Yeye aendelee kukua. Kama Yesu angeanza kazi Yake akiwa na umri wa miaka saba au minane, mwanadamu hangemchukulia Yeye kuwa kioja? Wanadamu wote hawangemfikiria Yeye kuwa mtoto tu? Ni nani angemwona Yeye kuwa wa kuridhisha? Mtoto wa umri wa miaka saba au minane hakuwa mrefu kuliko mimbari aliyosimamia nyuma yake—alifaa kuhubiri? Kabla ya ubinadamu Wake wa kawaida kukomaa, Hangeweza kufanya kazi. Kuhusu ubinadamu Wake ambao bado haukuwa umekomaa, sehemu kubwa ya kazi Yake haikuweza kutimizwa kabisa. Kazi ya Roho wa Mungu katika mwili pia inaongozwa na kanuni zake. Ni wakati tu Anapojitayarisha na ubinadamu wa kawaida ndipo Anapoweza kufanya kazi na kumwongoza Baba. Hapo tu ndipo Angeanza kazi Yake. Utotoni Mwake, Yesu hangeelewa mengi ya yale yaliyotendeka katika wakati wa kale, na ni kwa kuuliza waalimu ndani ya sinagogi tu ndipo Alipata kuelewa. Iwapo Angeanza kazi Yake pindi Alipojua kuzungumza, Angewezaje kutofanya makosa yoyote? Mungu Angewezaje kufanya makosa? Kwa hivyo, ilikuwa tu baada ya kuweza ndipo Alianza kazi Yake; Hakufanya kazi yoyote hadi Alipokuwa na uwezo wa kuyatekeleza. Akiwa na miaka 29, Yesu Alikuwa Amekomaa vya kutosha na ubinadamu Wake kutosha kutekeleza kazi Aliyopaswa kutekeleza. Ilikuwa hapo tu ndipo Roho wa Mungu Akaanza kirasmi kufanya kazi ndani Yake. Katika wakati huo, Yohana alikuwa ametenda kazi kwa miaka saba kwa kutayarisha njia Yake, na baada ya kumaliza kazi Yake, Yohana alitupwa gerezani. Mzigo wote basi ukamwangukia Yesu. Kama Angetekeleza kazi hii Akiwa na miaka 21 ama 22, Alipokuwa bado hana ubinadamu wa kutosha na Ameingia tu utu uzima, Akiwa bado haelewi mambo mengi, hangeweza kuchukua udhibiti. Katika wakati huo, Yohana alikuwa ameshafanya kazi yake kwa muda kabla Yesu kuanza kazi Yake katika miaka Yake ya katikati. Katika miaka hiyo, ubinadamu Wake wa kawaida ulikuwa unatosha kufanya kazi Aliyopaswa kufanya. Sasa, Mungu aliyepata mwili pia ana ubinadamu wa kawaida naingawa sio uliokomaa ukilinganishwa na wale walio wazee miongoni mwenu, ubinadamu huu tayari unatosha jinsi ulivyo kufanya kazi Yake; hali ya kazi Anayofanya leo siyo sawa kabisa na ile ya Yesu. Kwa nini Yesu aliwachagua mitume kumi na wawili? Yote ilikuwa ni kwa usaidizi wa kazi Yake na pamoja na hiyo. Kwa upande mmoja, ilikuwa ni kuweka msingi wa kazi Yake wakati huo, na vilevile pia kufanya hivyo kwa ajili ya kazi Yake iliyofuata. Kwa mujibu wa kazi wakati huo, uchaguzi wa wanafunzi kumi na wawili ulikuwa kusudi la Yesu, na vilevile la Mungu Mwenyewe. Aliamini wanafunzi kumi na wawili walipaswa kuchaguliwa kisha waongozwe kuhubiri mahali kote. Lakini hakuna haja ya hili miongoni mwenu siku hii! Kazi ya Mungu mwenye mwili katika mwili na kanuni nyingi. Kuna mengi ambayo mwanadamu haelewi, ilhali mwanadamu anatumia mara kwa mara fikira zake kuipima au kuwa na matarajio mengi kutoka Kwake. Hata wakati huu kunao wengi wasiofahamu kabisa kuwa maarifa yao ni ya fikira zao tu. Haijalishi enzi ama mahali ambapo Mungu anapata mwili, kanuni za kazi Yake katika mwili Wake hazibadiliki. Hawezi kuwa Mwili kisha Avuke mwili kwa kufanya kazi; zaidi, hawezi kuwa mwili kisha Akose kufanya kazi katika mwili wa kawaida wa binadamu. Vinginevyo, umuhimu wa Mungu kupata mwili utapotea na kuwa bure, na Neno kuwa mwili itakuwa haina maana. Zaidi ya hayo, Baba tu Aliye mbinguni (Roho) Anajua kuhusu Mungu katika mwili wa Mungu, na sio mwingine, sio hata mwili Mwenyewe ama wajumbe wa mbinguni. Hivyo, kazi ya Mungu katika mwili ni ya kawaida zaidi na bora kueleza Neno kuwa mwili; mwili unamaanisha mwanadamu wa kawaida. 

Wengine wanaweza kushangaa, mbona enzi ikaribishwe na Mungu Mwenyewe? Kiumbe kilichoumbwa hakiwezi kusimama kwa niaba Yake? Nyote mnafahamu kuwa Mungu Anakuwa mwili hasa kwa ajili ya kuikaribisha enzi mpya, na, kwa hakika, Anapoikaribisha enzi mpya, Atakuwa Ameikamilisha enzi ya kale wakati uo huo. Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho; ni Yeye Mwenyewe ndiye Anayeanzisha kazi Yake na hivyo lazima iwe ni Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani na huishinda dunia. Kila wakati Yeye Mwenyewe Anapofanya kazi miongoni mwa mwanadamu, ni mwanzo wa mapigano mapya. Bila mwanzo wa kazi mpya, kwa kawaida hakutakuwa na kikomo kwa enzi ya kale. Na bila kikomo kwa enzi ya kale ina maana kuwa vita na Shetani havijafika mwisho. Ni kama tu Mungu Mwenyewe Anakuja miongoni mwa mwanadamu na kutenda kazi mpya ndipo mwanadamu atakapoweza kujitoa kutoka katika umiliki wa Shetani na kupata maisha na mwanzo mpya. Vinginevyo, mwanadamu ataishi milele katika wakati wa kale na milele kuishi katika ushawishi wa kale wa Shetani. Katika kila enzi inayoongozwa na Mungu, sehemu ya mwanadamu huwekwa huru, na hivyo, mwanadamu huendelea na kazi ya Mungu kuelekea enzi mpya. Ushindi wa Mungu ni ushindi kwa wale ambao humfuata Yeye. Kama binadamu wa kuumbwa angepewa usukani wa kutimiza enzi, basi iwe kutoka kwa mtazamo wa mwanadamu ama Shetani, hii ni kama kupinga au kusaliti Mungu, na hivyo kazi ya mwanadamu ingegeuka kuwa chombo kwa Shetani. Mwanadamu anapotii na kumfuata Mungu katika enzi iliyokaribishwa na Mungu Mwenyewe tu ndipo Shetani angeshawishiwa kabisa, kwani hiyo ndiyo kazi ya kiumbe aliyeumbwa. Kwa hivyo Nasema kuwa mnafaa tu kufuata na kutii, na hakuna kingine kitakachoulizwa kutoka kwenu. Hiyo ndiyo maana ya kusema kila mmoja kuendeleza kazi na kufanya kazi Yake. Mungu hufanya kazi Yake Mwenyewe na Yeye hahitaji mwanadamu kufanya kazi Yake kwa niaba Yake, na wala hajishughulishi katika kazi ya viumbe. Mwanadamu anafanya kazi yake na haingilii kati kazi ya Mungu, na huo ndio utii wa kweli na ushahidi kuwa Shetani ameshindwa. Baada ya Mungu Mwenyewe kukaribisha enzi mpya, Yeye Mwenyewe hafanyi kazi tena kati ya mwanadamu. Ni wakati huo tu ndipo mwanadamu anaingia rasmi katika enzi mpya kufanya kazi yake na kutekeleza misheni yake kama kiumbe aliyeumbwa. Hivyo ndivyo zilivyo kanuni za kazi zisizowezwa kukiukwa na yeyote. Kufanya kazi katika njia hii pekee ndio yenye busara. Kazi ya Mungu hufanywa na Mungu Mwenyewe. Ni Yeye ndiye Anayeweka kazi katika mwendo, na pia Yeye ndiye Anayemaliza. Ni Yeye ndiye hupanga kazi, na pia Yeye ndiye Anayesimamia, na zaidi ya hayo, ni Yeye ndiye Anayeleta kazi kuzaa matunda. Ni ilivyoandikwa katika Biblia, “Mimi ndiye Mwanzo na Mwisho: Mimi ndiye Mpanzi na Mvunaji.” Yote yanayohusiana na usimamizi wa kazi Yake yanafanywa na mkono Wake. Yeye ndiye Mtawala wa mpango wa miaka elfu sita; hakuna anayeweza kufanya kazi Yake kwa niaba Yake ama kuleta kazi Yake hadi mwisho, kwani Yeye ndiye Aliye katika uongozi wa yote. Kwa kuwa Aliumba dunia, Ataongoza ulimwengu mzima kuishi katika nuru Yake, na Atamaliza enzi yote na kuleta mpango Wake wote kwa mafanikio!

Iliyotangulia: Utendaji (2)

Inayofuata: Fumbo la Kupata Mwili (2)

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp