Kusudi la Kuwasimamia Binadamu

Ikiwa watu wanaweza kweli kuiona vizuri njia sahihi ya maisha ya binadamu na vilevile kusudi la usimamizi wa Mungu wa binadamu, wasingeshikilia mategemeo yao ya baadaye na majaliwa yao binafsi kama hazina mioyoni mwao. Kisha wasingetataka tena kuwatumikia wazazi wao, ambao ni wabaya zaidi kuliko nguruwe na mbwa. Je, mustakabali na majaliwa ya mwanadamu si hasa wale wanaodaiwa kuwa “wazazi” wa Petro wa wakati wa sasa? Yamekuwa tu kama mwili na damu ya mwanadamu. Je, hatima na mustakabali wa mwili utakuwa upi hasa? Je, utakuwa kumwona Mungu wakati ukiwa ungali hai, au kwa roho kukutana na Mungu baada ya kifo? Je, kesho mwili utaishia katika tanuu kuu ya taabu, au katika moto mkubwa? Je, si maswali kama haya yanahusu iwapo mwili wa mwanadamu utahimili taabu au utavumilia habari kubwa sana ambayo kila mtu aliye katika mkondo huu wa sasa ambaye ana akili na ni mwenye busara anayahangaika? (Hapa, kuteseka kunarejelea kupokea baraka; kunamaanisha kwamba majaribu ya siku zijazo ni yenye manufaa kwa hatima ya mwanadamu. Taabu hurejelea kushindwa kusimama imara, au kudanganywa; au, kunamaanisha kwamba mtu atakumbana na hali za bahati mbaya na kupoteza maisha ya mtu katikati ya majanga, na kwamba hakuna hatima nzuri kwa roho wa mtu.) Ingawa wanadamu wana mantiki timamu, pengine kile wanachofikiri hakifanani kabisa na kile ambacho mantiki yao yanapaswa kuwa nacho. Hii ni kwa sababu wote ni waliochanganyikiwa na wao hufuata vitu bila kufikiri. Wote wanapaswa kuwa na ufahamu wa kina wa kile ambacho wanapaswa kuingia kwacho, na kwa mahususi wanapaswa kutatua kile wanachopaswa kuingia kwacho wakati wa mateso (yaani, wakati wa utakasaji katika tanuu), na vile vile kile wanachopaswa kujiandaa nacho wakati wa majaribu ya moto. Usiwatumikie wazazi wako siku zote (kumaanisha mwili) ambao ni sawa na nguruwe na mbwa na hata ni wabaya zaidi kuliko chungu na wadudu. Kuna haja gani ya kuteseka juu ya hilo, kufikiri sana, na kupiga bongo zako? Mwili si wako, bali upo katika mikono ya Mungu, ambaye kando na kukudhibiti wewe, pia Anamwamuru Shetani. (Hili linamaanisha kuwa kiasili mwili ni wa Shetani. Kwa kuwa Shetani pia yumo mikononi mwa Mungu, inaweza tu kusemwa hivi. Hii ni kwa sababu inashawishi zaidi kusema namna hiyo; inamaanisha kuwa wanadamu hawamilikiwi na Shetani kabisa, bali wamo mikononi mwa Mungu.) Unaishi chini ya mateso ya mwili, lakini, je, mwili ni wako? Uko chini ya udhibiti wako? Kwa nini upige bongo sana juu ya hilo? Kwa nini usumbuke sana kumsihi Mungu kwa ajili ya mwili wako uliooza ambao umeshahukumiwa zamani sana, kulaaniwa na vilevile kutiwa najisi na roho wachafu? Kuna haja gani ya kuwaweka washirika wa Shetani karibu sana na moyo wako? Huna wasiwasi kwamba mwili unaweza kuuharibu mustakabali wako halisi, matumaini yako mazuri, na hatima ya kweli ya maisha yako?

Njia ya leo si rahisi kuitembea. Inaweza kusemekana kwamba ni vigumu kuipata, na katika enzi zote imekuwa adimu sana. Hata hivyo, nani angeweza kufikiria kuwa mwili wa mwanadamu pekee ungetosha kumwangamiza? Kazi ya leo hakika ni ya thamani kama vile mvua ya majira ya kuchipua na ni ya thamani kama wema wa Mungu kwa mwanadamu. Hata hivyo, ikiwa mwanadamu hajui kusudi la kazi Yake ya sasa au kuelewa kiini cha mwanadamu, basi inawezekanaje tunu na thamani yake vizungumziwe? Mwili si wa wanadamu wenyewe, hivyo kwa kweli hakuna mtu anayeweza kuona waziwazi hatima yake itakuwa wapi. Hata hivyo, unapaswa kujua vizuri kwamba Mungu wa uumbaji Atawarudisha binadamu, ambao waliumbwa, katika nafasi yao ya asili, na kurejesha sura yao ya asili kutoka wakati wa kuumbwa kwao. Atachukua tena kikamilifu pumzi Aliyoipuliza ndani ya binadamu, na kuchukua tena mifupa na mwili wake na kurudisha vyote kwa Bwana wa viumbe. Atabadilisha na kufanya upya binadamu kikamilifu, na kuchukua tena kutoka kwa binadamu urithi wote wa Mungu ambao si wa binadamu, bali ni wa Mungu, na kamwe hatampa tena binadamu urithi huo. Hii ni kwa sababu kiasili, hakuna hata kitu kimoja kati ya hivyo kilichokuwa cha binadamu. Atavichukua vyote tena—huu si uporaji usio wa haki; lakini badala yake, unakusudiwa kuirejesha mbingu na dunia katika hali zake za asili, na vile vile kubadilisha na kumfanya upya binadamu. Hii ndiyo hatima inayofaa kwa mwanadamu, ingawa pengine haitakuwa kutwaa tena kwa mwili baada ya kuadibiwa, kama watu wanavyoweza kufikiri. Mungu hataki mifupa ya mwili baada ya maangamizi yake; Anataka vitu vya asili katika mwanadamu ambavyo mwanzo vilikuwa vya Mungu. Hivyo, Hatawaangamiza binadamu au kuuondoa kabisa mwili wa mwanadamu, kwa kuwa mwili wa mwanadamu si mali yake binafsi. Badala yake, ni kiungo cha Mungu, ambaye anasimamia binadamu. Angewezaje kuuangamiza mwili wa mwanadamu kwa ajili ya “furaha” Yake? Kufikia sasa, je, umeachana kwa kweli na ukamilifu wa huo mwili wako ambao hauna thamani hata ya senti moja? Kama ungeweza kuelewa asilimia thelathini ya kazi ya siku za mwisho (hii asilimia ndogo thelathini inamaanisha kuifahamu kazi ya Roho Mtakatifu leo na vile vile kazi ya Mungu ya neno katika siku za mwisho), basi usingeweza kuendelea “kuutumikia” au “kuwa” na upendo kwa mwili wako—mwili ambao umepotoka kwa miaka mingi—kama ilivyo leo. Unapaswa kuona wazi wazi kwamba binadamu sasa wameendelea hadi kufikia hali ambayo haijawahi kufikiwa na hawataendelea tena kusonga mbele kama magurudumu ya historia. Mwili wako ulioota kuvu umeshafunikwa na nzi tangu zamani, hivyo unawezaje kuwa na nguvu ya kurudisha nyuma magurudumu ya historia ambayo Mungu ameyawezesha kuendelea hadi siku hii ya leo? Unawezaje kufanya saa ipigayo kimya kimya ya siku za mwisho ipige tena, na iendelee kusogeza mikono yake kwa upande wa kulia? Unawezaje kuubadilisha upya ulimwengu ambao unaonekana kama umefunikwa na ukungu mzito? Je, mwili wako unaweza kuifufua milima na mito? Je, mwili wako, ambao una kazi kidogo tu, unaweza kweli kurejesha aina ya ulimwengu wa binadamu ambao umekuwa ukiutamani sana? Unaweza kweli kuwaelimisha wazawa wako wawe “binadamu”? Je, unaelewa sasa? Mwili wako unamilikiwa na nini hasa? Makusudi asili ya Mungu ya kumwokoa mwanadamu, ya kumkamilisha mwanadamu, na ya kumbadilisha mwanadamu hayakuwa kukupatia nchi nzuri ya asili au kuleta pumziko la amani kwa mwili wa mwanadamu; ilikuwa ni kwa ajili ya utukufu Wake na ushuhuda Wake, kwa furaha bora ya binadamu hapo baadaye, na ili kwamba hivi karibuni waweze kupumzika. Bado, ilikuwa kwa ajili ya mwili wako, maana mwanadamu ni mtaji wa usimamizi wa Mungu, na mwili wa mwanadamu ni kiungo tu. (Mwanadamu ni kitu chenye roho na mwili, ilhali mwili ni chombo kiozacho tu. Hii humaanisha kwamba mwili ni chombo cha kutumiwa katika mpango wa usimamizi.) Unapaswa kujua kwamba Mungu kuwakamilisha, kuwatimiza, na kuwapata wanadamu hakuleti kitu chochote ila panga na maangamizi juu ya miili wao, na na vile vile mateso yasiyokoma, moto mkali, hukumu zisizokuwa na huruma, kuadibu, laana, na majaribu yasiyokuwa na mipaka. Hicho ni kisa cha ndani na ukweli wa kazi ya kumsimamia binadamu. Hata hivyo, vitu hivi vyote vinalengwa kwa mwili wa mwanadamu, na mishale yote ya uhasama bila huruma inaelekezwa kwenye mwili wa mwanadamu (kwa maana mwanadamu hana hatia). Haya yote ni kwa ajili ya utukufu na ushuhuda Wake, na kwa ajili ya usimamizi Wake. Hii ni kwa sababu kazi Yake si kwa ajili ya binadamu tu, bali pia kwa ajili ya mpango wote, na vile vile kutimiza mapenzi Yake ya asili Alipomuumba binadamu. Kwa hiyo, pengine asilimia tisini ya kile ambacho mwanadamu hupitia kinajumuisha mateso na majaribu ya moto, na kuna siku chache sana ambazo ni tamu na zenye furaha au hata hakuna kabisa, ambazo mwili wa mwanadamu umekuwa ukitamani sana. Sembuse mwanadamu kuweza kufurahia nyakati za furaha katika mwili, akishinda nyakati nzuri pamoja na Mungu. Mwili ni mchafu, hivyo kile ambacho mwili wa mwanadamu unakiona au unakifurahia ni kuadibu kwa Mungu tu ambako mwanadamu huona kukiwa kusiko kuzuri, na ni kana kwamba hakuna mantiki ya kawaida. Hii ni kwa sababu Mungu atadhihirisha tabia Yake ya haki, ambayo haipendwi na mwanadamu, haivumilii makosa ya mwanadamu, na huchukia kabisa maadui. Mungu hufichua waziwazi tabia Yake yote kwa njia yoyote inayolazimu, na hivyo Akihitimisha kazi ya vita Vyake na Shetani vya miaka elfu sita—kazi ya wokovu wa binadamu wote na maangamizo ya Shetani wa zamani!

Iliyotangulia: Unapaswa Kushughulikiaje Wito Wako wa Baadaye?

Inayofuata: Asili na Utambulisho wa Mwanadamu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp