Maonyo Matatu

Kama muumini katika Mungu, hupaswi kuwa mtiifu kwa mwingine yeyote isipokuwa Yeye katika mambo yote, na uweze kupatana na mapenzi Yake katika mambo yote. Hata hivyo, ingawa kila mmoja anaelewa ujumbe huu, kwa sababu ya matatizo mengi ya mwanadamu—kwa sababu ya ujinga wake, upuuzi, na upotovu, kwa mfano—kweli hizi, ambazo ni za wazi zaidi na za msingi kuliko zote, hazionekani kabisa kwake. Kwa hivyo, kabla ya kuamua mwisho wenu, Ninapaswa kuwaambia kwanza baadhi ya mambo, ambayo yana umuhimu mkubwa sana kwenu. Kabla Sijaendelea, mnapaswa kwanza kuelewa yafuatayo: Maneno Ninayozungumza ni ukweli unaoelekezwa kwa wanadamu wote, na wala hayajaelekezwa kwa mtu mahususi au aina fulani ya mtu. Kwa hiyo, mnapaswa kuzingatia kuyaelewa maneno Yangu kutoka katika mtazamo wa ukweli, na vile vile mdumishe mtazamo wa uangalifu na uaminifu kamili. Msipuuze hata neno moja au ukweli Ninaozungumza, na wala usiyachukulie maneno Yangu kwa dharau. Katika maisha yenu, Naona mengi ambayo mnafanya ambayo hayana uhusiano na ukweli, kwa hivyo Nawaambia kwa uwazi kwamba muwe watumishi wa ukweli, ili msiwe watumwa wa uovu na ubaya, na kwamba msiukanyage ukweli na kuchafua sehemu yoyote ya nyumba ya Mungu. Hili ndilo onyo Langu kwenu. Sasa Nitaanza kuzungumza kuhusu mada tuliyo nayo:

Kwanza, kwa ajili ya majaliwa yenu, mnapaswa kutafuta kuidhinishwa na Mungu. Hii ni kusema kwamba, kwa sababu mnatambua kwamba nyinyi mmehesabiwa miongoni mwa wale walio katika nyumba ya Mungu, basi mnapaswa kumletea Mungu utulivu wa akili katika mambo yote na kumtosheleza katika kila jambo. Kwa maneno mengine, ni lazima muwe na kanuni katika matendo yenu na mlingane na ukweli katika mambo kama hayo. Kama jambo hili linazidi uwezo wako, basi utachukiwa na kukataliwa na Mungu na vilevile kukataliwa kwa dharau na kila mwanadamu. Pale tu utakapokuwa katika hali mbaya kama hii, basi hauwezi kuhesabiwa miongoni mwa wale walio kwenye nyumba ya Mungu. Hii ndiyo maana ya kutoidhinishwa na Mungu.

Pili, mnapaswa kujua kwamba Mungu anampenda binadamu mwaminifu. Mungu ana kiini cha uaminifu, na kwa hivyo neno Lake siku zote linaweza kuaminika. Aidha, matendo Yake hayana dosari wala hayatiliwi. Hii ndiyo maana Mungu anawapenda wale walio waaminifu kabisa Kwake. Uaminifu unamaanisha kumpa Mungu moyo wako; kutomdanganya kamwe katika kitu chochote; kuwa wazi Kwake katika mambo yote, kutowahi kuficha ukweli; kutowahi kufanya kile kinachowadanganya wale walio juu na kuwafumba macho wale walio chini; na kutowahi kufanya kile ambacho unajipendekeza tu mwenyewe kwa Mungu. Kwa ufupi, kuwa waaminifu ni kujizuia dhidi ya uchafu katika matendo na maneno yenu, na kutomdanganya Mungu wala binadamu. Kile Ninachoongea ni rahisi sana lakini ni kigumu maradufu kwenu. Watu wengi wanaona ni afadhali wahukumiwe kwenda kuzimu kuliko kunena na kutenda kwa uaminifu. Si ajabu kwamba Nina utendaji mwingine kwa wale ambao si waaminifu. Bila shaka, Ninaelewa ugumu mkubwa mnaokumbana nao kwa kuwa binadamu waaminifu. Ninyi nyote ni werevu sana na wastadi katika kuwapima watu kwa kipimo chenu kidogo; hii inafanya kazi Yangu iwe rahisi zaidi. Na kwa sababu nyinyi mnaficha siri katika mioyo yenu, basi, Nitawapeleka, mmoja baada ya mwingine, katika janga ili “mfundishwe” kwa moto, ili kwamba baada ya hapo mjitoe kikamilifu katika kuamini maneno Yangu. Hatimaye, Nitaondoa vinywani mwenu maneno “Mungu ni Mungu mwaminifu,” kisha ndipo mtakapojipiga vifua na kuomboleza, “Moyo wa mwanadamu ni mdanganyifu!” Je, hali za akili zenu zitakuwa vipi kwa wakati huu? Ninafikiri hamtakuwa na majivuno kama mlivyo sasa. Na hata hamtakuwa “wa kina sana kiasi cha kushindwa kueleweka” kama mlivyo sasa. Baadhi ya watu hutenda kwa ustaarabu na wanaonekana hasa “wana tabia nzuri” mbele za Mungu, lakini bado wanakuwa waasi na wasiojizuia mbele ya Roho Mtakatifu. Je, mnaweza kumhesabu binadamu kama huyu miongoni mwa wale walio waaminifu? Kama wewe ni mnafiki, mtu ambaye ni stadi katika “mahusiano baina ya watu,” basi Nasema kwamba bila shaka wewe ni mtu ambaye unajaribu kumchezea Mungu. Kama maneno yako yamejaa visingizio na uthibitisho usio na maana, basi Nasema kwamba wewe ni mtu ambaye unachukia kabisa kuuweka ukweli katika vitendo. Kama wewe una siri nyingi usizotaka kuzitoa, na kama hauko tayari kabisa kuziweka wazi siri zako—yaani, magumu yako—kwa wengine ili uweze kutafuta njia yenye mwanga, basi Ninasema kwamba wewe ni mtu ambaye hutapokea wokovu kwa urahisi na ambaye hutaweza kuibuka kutoka gizani kwa urahisi. Kama kutafuta njia ya kweli kunakupendeza sana, basi wewe ni mtu ambaye unakaa daima katika nuru. Kama wewe unafurahia kuwa mtenda-huduma katika nyumba ya Mungu, ukifanya kazi kwa bidii na kwa uangalifu bila kuonekana, daima ukitoa na kamwe usipokee, basi Nasema kwamba wewe ni mtakatifu mwaminifu, kwani hutafuti tuzo na unakuwa tu binadamu mwaminifu. Kama uko radhi kuwa wazi, kama uko radhi kutoa kila kitu ulichonacho, kama una uwezo wa kujitolea maisha yako kwa ajili ya Mungu na kuwa shahidi, kama wewe ni mwaminifu hadi kwa kiwango ambacho unajua tu kumridhisha Mungu na si kujifikiria au kuchukua chochote kwa ajili yako, basi Nasema kwamba watu kama hao ndio wanaostawishwa na mwangaza na wataishi milele katika ufalme. Unapaswa kujua kama una imani ya kweli na uaminifu wa kweli ndani yako, kama una rekodi ya kuteseka kwa ajili ya Mungu, na kama umemtii Mungu kikamilifu. Kama unakosa hivi Nilivyotaja, basi ndani yako kunasalia uasi, udanganyifu, ulafi, na malalamiko. Kwa vile moyo wako uko mbali na uaminifu, hujawahi kupokea idhinisho kutoka kwa Mungu na hujawahi kuishi katika nuru. Jinsi ambavyo hatima ya mtu itakuwa mwishoni inategemea kama wana moyo wenye uaminifu na wa kweli, na ikiwa wana nafsi safi. Kama wewe ni mtu ambaye si mwaminifu kabisa, ni mtu mwenye moyo muovu, mwenye nafsi isiyo safi, basi una uhakika wa kuishia mahali ambapo mwanadamu anaadhibiwa, kama ilivyoandikwa katika rekodi ya majaliwa yako. Kama unadai kwamba wewe ni mwaminifu sana, na bado kamwe hutendi kulingana na ukweli au kuongea neno la kweli, hivyo je, bado unatarajia Mungu akupe thawabu? Je, bado unatumaini kwamba Mungu atakuchukulia kama mboni ya jicho Lake? Je, mawazo kama hayo si ya kipumbavu? Unamdanganya Mungu katika mambo yote, hivyo nyumba ya Mungu inawezaje kumpa nafasi mtu kama wewe, ambaye mikono yake si safi?

Jambo la tatu Ninalotaka kuwaambia ni hili: Kila mwanadamu, katika kuishi maisha yake ya imani katika Mungu, amefanya mambo ambayo yanampinga na kumdanganya Mungu. Baadhi ya matendo mabaya hayahitaji kurekodiwa kama kosa, lakini mengine hayasameheki; kwani mengi ni yale yanayokiuka amri za utawala, ambapo ni kusema, yanaikosea tabia ya Mungu. Wengi ambao wanajali kuhusu hatima zao wenyewewanaweza kuuliza matendo haya ni yapi. Lazima mjue kwamba nyinyi mna kiburi na mna majivuno kiasili, na hamko tayari kuutii ukweli. Kwa sababu hii, Nitawaambia kidogo kidogo baada ya ninyi kuwa mmejitafakari wenyewe. Ninawasihi muwe na ufahamu bora zaidi wa yaliyomo katika amri za utawala, na mfanye bidii kuijua tabia ya Mungu. Vinginevyo, mtapata ugumu sana wa kufunga vinywa vyenu, ndimi zenu zitaropoka kwa uhuru kwa maneno ya kujigamba, na bila kujua mtaikosea tabia ya Mungu na kujipata kwenye giza, mkipoteza uwepo wa Roho Mtakatifu na mwangaza. Kwa sababu ninyi hamna kanuni katika matendo yenu, kwa sababu mnafanya na kusema yale msiyopaswa, basi mtapata adhabu inayowafaa. Lazima ujue kwamba ingawa wewe ni mpotovu katika maneno yako na matendo yako, Mungu ana kanuni katika hayo yote. Sababu ya wewe kupokea adhabu ni kwa sababu umemkosea Mungu na wala si binadamu. Kama, katika maisha yako, unatenda makosa mengi dhidi ya tabia ya Mungu, basi utalazimika kuwa mtoto wa kuzimu. Kwa binadamu inaweza kuonekana kwamba umetenda matendo machache tu yasiyolingana na ukweli na si chochote zaidi. Je, una habari, hata hivyo, kwamba machoni pa Mungu, tayari wewe ni mmoja ambaye kwako hakuna tena sadaka ya dhambi? Kwani umevunja amri za utawala za Mungu zaidi ya mara moja na hujaonyesha ishara yoyote ya kutubu, kwa hivyo huna chaguo lolote ila kutumbukia kuzimu mahali ambapo Mungu anamwadhibu mwanadamu. Idadi ndogo ya watu, wakati wanamfuata Mungu, walifanya baadhi ya matendo ambayo yalikiuka kanuni, lakini baada ya kupogolewa na kupewa mwongozo, waligundua upotovu wao wenyewe hatua kwa hatua, kisha wakaingia kwenye njia sahihi ya ukweli, na wamebaki na msingi mzuri leo. Watu kama hao ndio watakaobaki mwishoni. Hata hivyo, ni wale walio waaminifu ndio Ninaowatafuta; ikiwa wewe ni mtu mwaminifu na ni mtu ambaye unatenda kulingana na kanuni, basi unaweza kuwa msiri wa Mungu. Kama katika matendo yako huikosei tabia ya Mungu, na unatafuta mapenzi ya Mungu na una moyo wa kumcha Mungu, basi imani yako iko kwenye kiwango kinachotakiwa. Yeyote asiyemcha Mungu na asiye na moyo unaotetemeka kwa hofu kuna uwezekano wa kukiuka kwa urahisi amri za utawala za Mungu. Wengi wanamtumikia Mungu kwa nguvu ya shauku zao, lakini hawana ufahamu wa amri za utawala za Mungu, sembuse hata ufahamu wowote wa maana ya maneno Yake. Na kwa hivyo, kwa nia zao nzuri, mara nyingi wanaishia kufanya mambo ambayo yanatatiza usimamizi wa Mungu. Katika hali mbaya zaidi, wanafukuzwa kutoka kwenye nyumba ya Mungu, wakinyimwa nafasi yoyote zaidi ya kumfuata, na watatupwa kuzimu, hatimaye hawatakuwa na uhusiano mwingine wowote na nyumba ya Mungu. Watu hawa wanafanya kazi katika nyumba ya Mungu kwa nguvu ya nia zao nzuri zisizojua wanaishia kuikasirisha tabia ya Mungu. Watu huleta njia zao za kuwahudumia wakuu na mabwana katika nyumba ya Mungu na kujaribu kuzifanya zitumike, wakidhania kwa kiburi kwamba njia kama hizo zinaweza kutumika hapa kiurahisi. Hawakuwahi kufikiria kwamba Mungu hana ile tabia ya mwanakondoo bali ile ya simba. Kwa hiyo, wale wanaojihusisha na Mungu kwa mara ya kwanza wanashindwa kuwasiliana na Yeye, kwani moyo wa Mungu ni tofauti na ule wa binadamu. Ni baada tu ya kuelewa ukweli mwingi ndipo utakapoweza kuendelea kumjua Mungu. Maarifa haya si tu maneno wala mafundisho, lakini yanaweza kutumika kama hazina ya kuingia katika matumaini ya kumkaribia Mungu, na uthibitisho kwamba Anafurahishwa na wewe. Kama unakosa uhalisia wa maarifa, na haujajiandaa na ukweli, basi huduma yako ya dhati itakuletea tu kuchukiwa na kudharauliwa na Mungu. Sasa unapaswa kuelewa kwamba imani katika Mungu si masomo tu ya theolojia.

Ingawa maneno Ninayotumia kuwaonya ni mafupi, vyote Nilivyovifafanua hapa ndivyo vinavyokosekana zaidi ndani yenu. Lazima mjue kwamba kile Ninachozungumzia sasa ni kwa ajili ya kazi Yangu ya mwisho miongoni mwa binadamu, kwa ajili ya kuamua hatima ya binadamu. Sipendelei kufanya kazi nyingi zaidi isiyo na maana, na wala Sipendelei kuendelea kuwaongoza wale binadamu wasio na matumaini kama mti uliooza, sembuse wale walio na nia mbaya kwa siri. Pengine siku moja mtaelewa nia za dhati zinazoyasukuma maneno Yangu na michango ambayo Nimemfanyia mwanadamu. Pengine siku moja mtafahamu kanuni inayowawezesha kuamua hatima yenu wenyewe.

Iliyotangulia: Juu ya Hatima

Inayofuata: Dhambi Zitamwongoza Mwanadamu Jahanamu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp