21. Nimejifunza Jinsi ya Kuwatendea Watu Vizuri

Na Siyuan, Ufaransa

Miaka michache iliyopita, nilikuwa nikifanya wajibu wa kiongozi wa kanisa. Kulikuwa na ndugu mmoja kanisani aliyekuwa na jina la ukoo la Chen na ambaye alikuwa mwenye ubora mzuri wa tabia. Lakini tabia yake ilikuwa ya kiburi sana, na alielekea kuwazuia wengine. Alipenda kujionyesha, kwa hivyo nilianza kuwa na chuki kwake na kubuni maoni juu yake. Siku moja, Ndugu Chen alinijia na kusema kwamba alitaka kuwanyunyizia waumini wapya. Hakuwa amemwamini Mungu kwa muda mrefu na alikuwa na ufahamu wa juujuu kuhusu ukweli, kwa hivyo nilikataa. Alipoona kwamba sikutoa idhini yangu, alisema, “Nina ubora mzuri sana wa tabia, kwa nini nisifanye wajibu wa kunyunyizia? Nisipoenda kuufanya, talanta haitakuwa ikitumiwa kikamilifu.” Sikufurahia jambo hili, na niliwaza, “Unafikiri kwamba wajibu wa kunyunyizia ni rahisi sana? Je, unaweza kufanya wajibu huu vizuri ukitumia tu vipaji vyako na ubora mzuri wa tabia, bila kuelewa ukweli? Usijivune!” Nilikataa ombi la Ndugu Chen na niliwaambia ndugu wengine jinsi alivyokuwa mwenye kiburi, nikiwapa mifano ya njia nyingi ambazo alionyesha upotovu. Wengine wao walikubaliana nami.

Wiki mbili baadaye, kanisa lilifanya mipango ili katika mikutano ya baadaye, tuweze kutazama filamu za kanisa na vilevile kusoma maneno ya Mwenyezi Mungu. Filamu hizi zote zilishiriki juu ya ukweli na zilimshuhudia Mungu, kwa hivyo kuzitazama kungetusaidia kuelewa ukweli. Katika mkutano uliofuata, Ndugu Chen alisema, “Huu ni mpango mzuri. Viongozi na wafanyakazi wengine hushiriki tu mambo ya kawaida mikutanoni, kwa hivyo ni bora kutazama filamu. Niliona mwanzoni kwamba wajibu wangu ulikuwa mgumu sana kwa sababu sikuelewa ukweli. Lakini baadaye niliomba, nilimtegemea Mungu, na nikasoma maneno ya Mungu zaidi, na filamu hizi za kanisa zimenisaidia sana pia. Nimeelewa ukweli kidogo kutokana nazo. Sasa nina ujuzi mwingi katika wajibu wangu na nina ufahamu wa msingi juu ya kanuni. Mimi hufanikisha mengi katika wajibu wangu.” Niliona ushirika wake ukiwa wa kuchukiza na uliovuka mipaka, na niliwaza, “Hakika wewe hutumia kila nafasi kujionyesha, siyo? Una kiburi sana!” Baadaye tuliratibu masuala machache ya kushughulikiwa kwenye mkutano wetu uliofuata na Ndugu Chen alichukua kwa pupa masuala matatu kati ya maswala yote. Pia aliwagawia wengine masuala yaliyobaki ili wafanye ushirika kuyahusu. Nilipokuwa tu nikimteua kiongozi wa kikundi atakayeandaa mkutano huo, Ndugu Chen alimuuliza kwa sauti ya mashaka, “Una hakika kwamba unaweza kufanya jambo hili?” Nilipomsikia akisema hivi kana kwamba ni yeye pekee ambaye angeandaa mkutano huo, nilighadhabika, na nikawaza, “Huna mantiki kabisa. Unajionyesha tu ili kuwafanya wengine wakuheshimu. Kama hilo ndilo unalofuata, basi lisahau.” Kwa hivyo nilipanga upya kila kitu na sikumruhusu aandae mkutano huo. Katika kipindi hicho cha muda, nilimchukia sana Ndugu Chen kila nilipofikiri juu ya tabia yake, nilihisi kwamba alikuwa na kiburi mno, na kwamba kiburi chake kilipita kiasi. Kwa hivyo nilimbainisha kama mtu ambaye hakuweza kubadilika na niliamua kwamba mtu mwenye kiburi kama yeye hakufaa kabisa kufanya wajibu wake. Nilidhani kwamba nilihitaji tu kumbadilisha na huo ungekuwa mwisho wa tatizo hilo.

Mkutano ulipofika kikomo, nilifikiria hali yangu na tabia yangu mwenyewe, na nilihisi vibaya kidogo. Nilihisi kwamba nilikuwa mkali sana kwa Ndugu Chen, kwa hivyo nilimwomba Mungu, nikisema, “Ee Mungu, najua kwamba hali yangu ni mbaya, lakini sijui tatizo langu ni lipi au napaswa kuingia katika kanuni zipi za ukweli. Tafadhali nitie nuru na Uniongoze.” Siku iliyofuata wakati wa ibada, nilisoma maneno haya ya Mungu: “Unapaswa kuwatendea washiriki wa familia ya Mungu kulingana na kanuni gani? (Mtendee kila ndugu kwa haki.) Unawatendeaje kwa haki? Kila mtu ana makosa na upungufu mdogo mdogo, pamoja na upekepeke fulani; watu wote wana kujidai, udhaifu, na sehemu ambazo wana upungufu. Unapaswa kuwasaidia kwa moyo wenye upendo, uwe mvumilivu na mstahimilivu, na usiwe mkali sana au kufuatilia kila jambo dogo. Kwa watu ambao ni vijana au ambao hawajamwamini Mungu kwa muda mrefu sana, au ambao wameanza hivi karibuni kutekeleza wajibu wao na walio na maombi fulani maalum, ukishika tu vitu hivi kwanguvu na uvitumie dhidi yao, basi huku ndiko kunakojulikana kama kuwa mkali. Unapuuza maovu yanayofanywa na wale viongozi wa uwongo na wapinga Kristo, lakini unapoona mapungufu na makosa madogo katika ndugu zako, unakataa kuwasaidia, badala yake ukichagua kuhangaikia vitu hivyo na kuwahukumu bila wao kujua, na hivyo kuwasababisha watu hata zaidi wawapinge, kuwaacha, na kuwatenga. Hii ni tabia ya aina gani? Huku ni kufanya mambo kulingana na upendeleo wako wa kibinafsi tu, na kutoweza kuwatendea watu kwa haki; hii inaonyesha tabia potovu ya kishetani! Haya ni makosa! Watu wafanyapo mambo, Mungu anatazama; kila ufanyacho na bila kujali unavyofikiria, Yeye huona!(“Ili Kupata Ukweli, Lazima Ujifunze Kutoka kwa Watu, Mambo, na Vitu Vinavyokuzunguka” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). Maneno ya Mungu yalinionyesha hali yangu na nilihisi aibu. Niliona kwamba nilikuwa nikimshughulikia Ndugu Chen kupitia tabia yangu potovu. Nilipokumbuka tangu nilipokutana naye, niliona kwamba mara nyingi alifichua kiburi chake katika maneno na vitendo vyake, na kwa hivyo nilihisi kwamba alikuwa mchanga na fidhuli, na hakujijua. Alipotajwa tu kidogo, nilikumbuka tu dosari zake. Nilishikilia maonyesho yake ya upotovu, nikiamua kuwa alikuwa na kiburi kupita kiasi, na kwamba watu kama hao kamwe hawawezi kubadilika. Sikuwahi kumtendea kwa haki. Nilipinga na kuchukia maoni yoyote ambayo alionyesha. Nilimhukumu na kumdunisha mbele ya wengine, nilieneza chuki zangu kwake, na kuwashawishi wengine wamtenge pamoja nami. Nilitaka hata kumwachisha wajibu wake. Je, sikuwa nikitumia cheo changu kama kiongozi kumkandamiza na kumvunja moyo? Nilipotoshwa sana na Shetani, sikuwa na kanuni za ukweli, nilikuwa na maoni ya upuuzi wakati mwingi, lakini bado niliwahukumu na kuwashutumu wengine bila msingi. Sikuwa na busara hata kidogo! Sikumcha Mungu hata kidogo. Niliwatendea kina ndugu jinsi nilivyopenda na kuishi kwa kudhihirisha asili ya pepo. Nilimchukiza sana Mungu, na kumkirihi sana. Nilijawa na hatia nilipofikiria hayo.

Baadaye, nilitafuta kanuni za jinsi ya kuwatendea watu haki katika maneno ya Mungu. Nilipata vifungu viwili vya maneno ya Mungu. “Jinsi unavyopaswa kuwatendea wengine imeonyeshwa au kudokezwa katika maneno ya Mungu; mtazamo ambao Mungu huchukua katika kuwatendea binadamu ndio mtazamo ambao watu wanapaswa kuwa nao katika kutendeana wao kwa wao. Je, Mungu humtendeaje kila mmoja? Watu wengine ni wenye kimo kisicho komavu, au ni wachanga, au wamemwamini Mungu kwa muda mfupi tu. Mungu anaweza kuwaona watu hawa kama wasio wabaya wala waovu kiasili na katika kiini; ni kwamba tu ni wajinga au wanaopungukiwa katika ubora wa tabia, au kwamba wamechafuliwa sana na jamii. Hawajaingia katika uhalisi wa ukweli, kwa hivyo ni vigumu kwao kujiepusha kufanya mambo mengine ya kijinga au kufanya vitendo kadhaa vya ujinga. Hata hivyo, kutoka katika mtazamo wa Mungu, mambo kama haya siyo muhimu; Yeye huangalia tu mioyo ya watu. Kama wameazimia kuingia katika uhalisi wa ukweli, wanaelekea katika njia sahihi, na hili ndilo kusudi lao, basi Mungu anawaangalia, kuwangojea, na kuwapa muda na fursa zinazowaruhusu kuingia. Siyo kwamba Mungu anawaangusha kwa pigo moja, wala siyo kwamba Anashikilia kosa walilotenda wakati mmoja na kukataa kuliachilia; Yeye hajawahi kuwatendea watu kwa namna hii. Licha ya hayo, watu wakitendeana kwa namna hiyo, basi hili halionyeshi tabia yao potovu? Hii hasa ndiyo tabia yao potovu. Lazima uangalie jinsi Mungu anavyowatendea watu wasiojua na wapumbavu, jinsi Anavyowatendea wale wasio na kimo komavu, jinsi Anavyochukulia udhihirisho wa kawaida wa tabia potovu ya binadamu, na jinsi Anavyowatendea wale ambao ni waovu. Mungu ana njia mbali mbali za kuwatendea watu tofauti, na pia Ana njia mbali mbali za kusimamia hali nyingi tofauti za watu. Lazima uelewe ukweli wa mambo haya. Mara unapoelewa ukweli huu, unaweza basi kujua jinsi ya kuyapitia(“Ili Kupata Ukweli, Lazima Ujifunze Kutoka kwa Watu, Mambo, na Vitu Vinavyokuzunguka” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). “Unaweza kuwa usiyepatana na tabia ya mtu, na unaweza kutompenda, lakini unapofanya kazi pamoja naye, unasalia mwadilifu na hutaeleza kufadhaika kwako unapofanya wajibu wako, hutaathiri wajibu wako, au kufanya mifadhaiko yako iathiri masilahi ya familia ya Mungu. Unaweza kufanya vitu kulingana na kanuni; hivyo, unakuwa na uchaji wa kimsingi kwa Mungu. Ukiwa na zaidi kidogo ya hayo, basi unapoona kwamba mtu fulani ana makosa au udhaifu fulani—hata ikiwa amekukosea au kuyadhuru masilahi yako mwenyewe—bado utakuwa na moyo wa kumsaidia. Kufanya hivyo kutakuwa hata bora zaidi; kutamaanisha kwamba wewe ni mtu aliye na ubinadamu, uhalisi wa ukweli, na uchaji kwa Mungu(“Masharti Matano Ambayo Watu Wanayo Kabla ya Kuingia Kwenye Njia Sahihi ya Kumwamini Mungu” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo).

Maneno ya Mungu yanaeleza waziwazi kanuni na njia ya kuwatendea watu kwa haki, na vilevile mtazamo Wake kwa watu. Mtazamo Wake kwa wapinga Kristo na watu waovu ni wa chuki, laana, na adhabu. Kuhusiana na wale wenye kimo kidogo, wenye ubora duni wa tabia, na ambao wana dosari na tabia mbalimbali potovu, almradi wamwamini Mungu kwa kweli, wawe na hamu ya kufuatilia ukweli, na waweze kukubali ukweli, mtazamo wa Mungu ni wa upendo, huruma, na wokovu. Tunaona kuwa Mungu ana kanuni za jinsi Anavyomtendea kila mtu, na Anataka kwamba tuwatendee wengine kulingana na kanuni za ukweli. Kwa mfano, lazima tuwe wavumilivu na kuwasamehe wale wanaomwamini Mungu kwa kweli. Lazima tuwasaidie kutokana na upendo na tuwape nafasi ya kutubu na kubadilika. Hatuwezi kuwavunja watu moyo kwa sababu tu wanaonyesha upotovu fulani. Haya si mapenzi ya Mungu. Mchukulie Ndugu Chen kwa mfano—alikuwa na ubora mzuri wa tabia na alikuwa mwaminifu katika wajibu wake. Alikuwa tayari pia kutia bidii katika kufuatilia ukweli. Alikuwa muumini mgeni, uzoefu wake ulikuwa wa juu juu, na alikuwa upande wa kiburi, lakini nilipaswa kuwa nikimtendea kwa haki kulingana na kanuni za ukweli na kufanya ushirika naye juu ya ukweli kwa upendo ili kumsaidia. Mbali na kutomsaidia, kukataa kuona uwezo wake na maoni yake mazuri, pia nilimchukia, nilimhukumu na kumtenga, na nilitaka aondoke. Nilikuwa na asili mbovu sana! Nilikumbuka jinsi nilivyokuwa kama kiongozi. Nilidhani kila wakati kwamba nilikuwa bora kuwaliko wengine, nilitaka kuwa kauli ya mwisho, kufanya chochote nilichotaka, na sikusikiliza maoni ya wengine. Matokeo yake ni kwamba, nilifanya mambo mengine ambayo yaliivuruga kazi ya kanisa. Na bado Mungu hakuniondoa, lakini badala yake Alitumia maneno yake kunihukumu, kunifundisha nidhamu na kunishughulikia, kunifanya nitafakari juu yangu mwenyewe, Akinipa nafasi ya kutubu na kubadilika. Niliona kuwa Mungu haachani nasi kamwe au kutuondoa kwa sababu tu ya kuonyesha upotovu kidogo, lakini Yeye hufanya juu chini kutuokoa. Mungu ana moyo mzuri sana! Kisha, kuzingatia tabia yangu mwenyewe na jinsi nilivyokuwa nikimtendea Ndugu Chen kulinifanya nione haya na nilitaka ardhi inimeze. Kisha nilimwomba Mungu na kutubu Kwake, nikitaka kutenda kanuni za ukweli na kumsaidia Ndugu Chen kwa moyo wenye upendo.

Kwa hivyo nilikwenda kwa Ndugu Chen na kufanya ushirika naye kuhusu vifungu fulani vya maneno ya Mungu na kumwonyesha makosa yake. Alianza kuelewa tabia yake mwenyewe ya kiburi na alitambua hatari ya kuiacha bila kuitatua. Alisema kwamba ushirika wangu na onyo langu vilimsaidia sana, na alitaka kutafakari juu yake mwenyewe na kutafuta ukweli ili atatue tabia yake potovu. Niliguswa sana nilipomsikia akisema hivi, lakini pia nilihisi vibaya. Alikuwa na uwezo wa kubadilika kinyume na jinsi nilivyokuwa nimedhani. Ni mimi ndiye sikuwa nimefanya wajibu wangu vizuri. Sikuwa nimewahi kabisa kujaribu kumsaidia kweli kwa moyo wenye upendo lakini nilikuwa nimeshikilia upotovu na makosa yake, na hata kumhukumu na kumtenga. Nilikuwa mwenye kiburi sana na asiye na ubinadamu!

Baadaye katika mkutano, nilimsikia ndugu kutoka juu akitoa mahubiri haya: “Wanadamu wote wapotovu wana tabia ya kiburi. Hata wale wanaopenda ukweli na wanaofuatilia kukamilishwa wote wana tabia ya kiburi na ya kujidai, ingawa hii haiathiri uwezo wao wa kupata wokovu na kukamilishwa. Almradi watu wanaweza kukubali ukweli na kukubali kupogolewa na kushughulikiwa, na wanaweza kutii ukweli kabisa bila kujali hali, basi wanaweza kabisa kupata wokovu na kukamilishwa. Kwa kweli, kati ya wale ambao kwa kweli wana ubora mzuri wa tabia na wana maazimio, hakuna ambao hawana kiburi. Huu ni ukweli. Watu wateule wa Mungu lazima wawatendee wengine kwa njia inayofaa. Hawana budi kutomwekea mtu mipaka kama ambaye si mzuri na ambaye hawezi kuokolewa na kukamilishwa kwa sababu tu mtu huyo ana kiburi na hujidai kupita kiasi. … Kuhusiana na hoja hii, mtu anahitaji kuelewa mapenzi ya Mungu. Hakuna mtu ambaye ana ubora mzuri wa tabia na aliye na azimio, ambaye si mwenye kiburi au asiyejidai hata kidogo; kama kungekuwapo naye, basi bila shaka huyo angekuwa mtu ambaye anajifanya au mnafiki. Ni lazima mtu ajue kwamba wanadamu wote wapotovu wana asili ya kiburi na majivuno. Huu ni ukweli usiokanika.” Kimetoholewa kutoka katika Ushirika kutoka kwa Aliye Juu Hii ilinisaidia kuelewa vizuri jinsi ya kuwatendea watu wenye tabia ya kiburi. Si kwamba hawawezi kubadilika. Jambo la muhimu ni kuona ikiwa wanaweza kufuatilia na kukubali ukweli. Ikiwa wanaweza kukubali ukweli, na kukubali hukumu, kuadibu, upogoaji na ushughulikiaji wa Mungu, basi hamna sababu ya wao kutobadilika na kukamilishwa na Mungu. Kwa kweli, watu wote ambao wana vipaji, uwezo na ubora wa tabia wana kiburi mno. Lakini kwa sababu ubora wao wa tabia ni mzuri, wanaelewa ukweli haraka na ni hodari katika wajibu wao. Watu kama hawa wanapoelewa ukweli na kutenda kwa kanuni, hiyo hunufaisha sana kazi ya nyumba ya Mungu. Ndugu Chen alikuwa na ubora mzuri wa tabia, kwa hivyo nilipaswa kumsaidia zaidi kutokana na upendo, na kufanya ushirika zaidi ili kumsaidia. Huko pekee ndiko kunaweza kuwa kuzingatia mapenzi ya Mungu.

Tukio hili lilinifanya nifahamu kwamba kuwatendea watu kulingana na tabia zetu potovu na za kishetani bila ukweli kunaweza tu kuwadhuru sana kina ndugu, na kuchelewesha kuingia kwao katika uzima na kazi ya kanisa. Hiyo ni dhambi, ni kufanya uovu. Niliona jinsi kuwatendea wengine kulingana na kanuni za ukweli kulivyo muhimu. Nimepata ufahamu huu mdogo kutokana na mwongozo wa maneno ya Mungu.

Iliyotangulia: 20. Kwa Nini Nimetembea Njia ya Mafarisayo

Inayofuata: 23. Hatimaye Naelewa Maana ya Kutimiza Wajibu Wangu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

4. Jaribu la Uzao wa Moabu

Na Zhuanyi, UchinaMwenyezi Mungu anasema, “Kazi yote ifanywayo siku hii ya leo ni ili mwanadamu afanywe msafi na kubadilika; kupitia hukumu...

45. Kuishi Mbele za Mungu

Na Yongsui, Korea ya KusiniMwenyezi Mungu anasema, “Ili kuingia katika uhalisi, mtu lazima apindue vitu vyote kuelekea maisha halisi. Iwapo...

57. Kuripoti Au Kutoripoti

Na Yang Yi, UchinaMwenyezi Mungu anasema, “Kwa minajili ya majaliwa yenu, mnastahili kutafuta kuidhinishwa na Mungu. Hii ni kusema kwamba,...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp