7. Jinsi ya kuelewa kwamba Kristo ndiye ukweli, njia, na uzima?

Aya za Biblia za Kurejelea:

“Mwanzoni kulikuwa na Neno, na Neno alikuwa na Mungu, na Neno alikuwa Mungu. Hivyo ndivyo alivyokuwa mwanzoni na Mungu” (Yohana 1:1-2).

“Na Neno alifanywa kuwa mwili, na akakaa kati yetu … aliyejawa neema na ukweli” (Yohana 1:14).

“Mimi ndiye njia, ukweli, na uzima: hakuna mwanadamu ayaje kwa Baba, bali kwa njia yangu” (Yohana 14:6).

“Maneno ninayoongea kwenu ni roho, na ni uhai” (Yohana 6:63).

Maneno Husika ya Mungu:

Njia ya uzima si kitu ambacho mtu yeyote anaweza kumiliki, wala si kitu ambacho kila mtu anaweza kufikia kwa urahisi. Hii ni kwa sababu uzima unaweza kutoka tu kwa Mungu, ambayo ni kusema, ni Mungu Mwenyewe pekee ndiye Anayemiliki kiini cha uzima, na ni Mungu Mwenyewe pekee aliye na njia ya uzima. Na hivyo Mungu tu ndiye chanzo cha uzima, na kijito cha maji ya uzima kinachotiririka nyakati zote. Tangu uumbaji wa dunia, Mungu amefanya kazi kubwa sana inayobeba pamoja nayo uzima uhai wa uzima, Amefanya kazi nyingi ambayo inamletea mwanadamu uzima, na Amelipa gharama kubwa inayomwezesha mwanadamu apate uzima. Hii ni kwa sababu Mungu Mwenyewe ni uzima wa milele, na Mungu Mwenyewe ndiye njia ambayo kwayo mwanadamu anaweza kufufuliwa. Mungu kamwe hajawahi kosa kuwepo moyoni mwa mwanadamu, na Anaishi miongoni mwa wanadamu wakati wote. Yeye ndiye nguvu ya kuendesha maisha ya mwanadamu, chanzo cha kuendelea kuishi kwa mwanadamu, na rasilmali kubwa ya kuwepo kwa mwanadamu baada ya kuzaliwa. Yeye huwasababisha watu kuzaliwa upya, na kuwawezesha kuishi kwa ushupavu katika jukumu lao binafsi. Akitegemea uwezo Wake, na nguvu Yake ya uzima isiyozima, mwanadamu ameishi kwa kizazi baada ya kizazi, huku nguvu ya uzima wa Mungu imekuwa ikitoa utegemezi miongoni mwa binadamu, na Mungu amelipa gharama ambayo hakuna mtu wa kawaida amewahi kulipa. Nguvu za Mungu za maisha zinaweza kutawala juu ya nguvu zozote; hata zaidi ya hayo, zinapita mamlaka yoyote. Uzima Wake ni wa milele, nguvu Zake ni za ajabu, na nguvu Zake za uzima haziwezi kuzidiwa na kiumbe yeyote au nguvu za adui. Nguvu za uzima wa Mungu zipo na hung’aa kwa mwangaza ulio mzuri sana, bila kujali muda au mahali. Mbingu na dunia zinaweza kupitia mabadiliko ya ajabu, lakini uzima wa Mungu ni ule ule daima. Mambo yote yanaweza kupita, lakini uzima wa Mungu bado utakuwepo. Hii ni kwa sababu Mungu ndiye chanzo cha kuwepo kwa vitu vyote, na mzizi unaotegemewa na kila kitu ili kiendelee kuishi. Asili ya maisha ya mwanadamu hutoka kwa Mungu, kuwepo kwa mbingu ni kwa sababu ya Mungu, na kuwepo kwa ardhi kunatokana na nguvu ya uhai wa Mungu. Hakuna kitu kinachomiliki nguvu kinachoweza kuzidi ukuu wa Mungu, na hakuna kitu chenye nguvu kinachoweza kuvunja mipaka ya mamlaka ya Mungu. Kwa njia hii, bila kujali wao ni nani, kila mtu lazima ajiwasilishe kwa utawala wa Mungu, kila mtu lazima aishi chini ya amri za Mungu, na hakuna mtu anayeweza kutoroka kutoka katika utawala Wake.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ni Kristo wa Siku za Mwisho Pekee Ndiye Anayeweza Kumpa Mwanadamu Njia ya Uzima wa Milele

Mungu Mwenyewe ni uzima, na ukweli, na uzima Wake na ukweli vipo pamoja. Wale ambao hawana uwezo wa kupata ukweli hawatapata uzima kamwe. Bila mwongozo, usaidizi, na utoaji wa ukweli, utapata tu barua, mafundisho, na, zaidi ya hayo, kifo. Maisha ya Mungu ni ya milele, na ukweli wake na maisha hupatana. Kama huwezi kupata chanzo cha ukweli, basi huwezi kupata lishe ya maisha; kama huwezi kupata starehe ya maisha, basi utakuwa hakika huna ukweli, na hivyo mbali na mawazo na dhana, ukamilifu wa mwili wako hautakuwa chochote ila mwili, mwili wako unaonuka. Ujue kwamba maneno ya vitabu hayahesabiki kama maisha, kumbukumbu za historia haziwezi kupokelewa kama ukweli, na mafundisho ya siku za nyuma hayawezi kutumika kama sababu ya maneno ya sasa anayosema Mungu. Kinachoonyeshwa tu na Mungu anapokuja duniani na kuishi miongoni mwa binadamu ni ukweli, maisha, mapenzi ya Mungu, na njia Yake ya sasa ya kufanya kazi.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ni Kristo wa Siku za Mwisho Pekee Ndiye Anayeweza Kumpa Mwanadamu Njia ya Uzima wa Milele

Kristo wa siku za mwisho huleta uzima, na huleta njia ya kweli ya kudumu na ya milele. Ukweli huu ndiyo njia ambayo kwayo binadamu anapata uzima, na ndiyo njia pekee ambayo mwanadamu atamjua Mungu na kukubaliwa na Mungu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ni Kristo wa Siku za Mwisho Pekee Ndiye Anayeweza Kumpa Mwanadamu Njia ya Uzima wa Milele

Wakati huu, Mungu haji kufanya kazi kwa mwili wa kiroho, ila kwa ule wa kawaida sana. Zaidi ya hayo, ni mwili wa kupata mwili kwa Mungu mara ya pili, na pia ni mwili ambao Mungu anarudi kupitia kwao tena. Ni mwili wa kawaida sana. Ukimwangalia, huwezi kuona chochote kinachomfanya aonekane tofauti na wengine, lakini unaweza kupata kutoka Kwake ukweli ambao haujawahi kusikika hapo awali. Mwili huu tu usio na umuhimu ni mfano halisi wa maneno yote ya Mungu ya ukweli, uletao kazi ya Mungu katika siku za mwisho, na maonyesho ambayo kwayo mwanadamu anaielewa tabia nzima ya Mungu. Je, hukutamani sana kumwona Mungu aliye mbinguni? Je, hutamani sana kumwelewa Mungu aliye mbinguni? Je, hutamani sana kuona hatima ya mwanadamu? Atakwambia hizi siri zote—siri ambazo hakuna mwanadamu yeyote amewahi kuweza kukuambia—na pia Atakwambia ukweli ambao huelewi. Yeye ndiye lango la kuingia katika ufalme, na mwongozo wako katika enzi mpya. Mwili wa kawaida kama huu una siri nyingi zisizoeleweka. Matendo Yake labda hayaeleweki kwako, lakini lengo la kazi yote Anayoifanya limekutosha kuona kuwa Yeye si mwili wa kawaida anavyoamini mwanadamu. Kwani Anawakilisha mapenzi ya Mungu na pia utunzaji anaoonyesha Mungu kwa mwanadamu siku za mwisho. Ingawa huwezi kuyasikia maneno Anayozungumza yanayoonekana kutingisha mbingu na dunia wala kuona macho Yake kama moto mkali, na ingawa huwezi kuhisi nidhamu ya fimbo Yake ya chuma, unaweza kusikia kupitia maneno Yake ghadhabu ya Mungu na kujua kwamba Mungu Anaonyesha huruma kwa mwanadamu; unaweza kuona tabia ya haki ya Mungu na hekima Yake, na zaidi ya hayo, kutambua wasiwasi na utunzaji anao Mungu kwa wanadamu wote. Kazi ya Mungu ya siku za mwisho ni kuruhusu mwanadamu kumwona Mungu aliye mbinguni Akiishi miongoni mwa wanadamu duniani, na kumwezesha mwanadamu kuja kumjua, kumtii, kumheshimu, na kumpenda Mungu. Hii ndiyo maana Amerudi kwa mwili kwa mara ya pili. …

… Ukweli kwamba mmefika siku ya leo ni kwa sababu ya huu mwili. Ni kwa sababu Mungu huishi ndani ya mwili ndiyo mna nafasi ya kuishi. Hii bahati yote nzuri imepatwa kwa sababu ya huyu mwanadamu wa kawaida. Siyo haya tu, lakini mwishowe kila taifa litamwabudu huyu mwanadamu wa kawaida, na pia kumpa shukrani na kumtii huyu mwanadamu asiye muhimu, kwa sababu ni ukweli, uzima, na njia Aliyoleta ndivyo vilivyowaokoa wanadamu wote, kutuliza migogoro kati ya mwanadamu na Mungu, ikafupisha umbali kati yao, na kufungua kiungo kati ya mawazo ya Mungu na mwanadamu. Pia ni Yeye ambaye Ameleta hata utukufu zaidi kwa Mungu. Mwanadamu wa kawaida kama huyu hastahili uaminifu na ibada yako? Mwili wa kawaida kama huu haufai kuitwa Kristo? Mwanadamu wa kawaida kama huyu hawezi kuwa maonyesho ya Mungu miongoni mwa wanadamu? Mwanadamu kama huyu anayesaidia wanadamu kuepuka maafa hastahili mapenzi upendo wenu na nyinyi kumshikilia? Mkiukataa ukweli unaotamkwa kutoka mdomo Wake na pia kuchukia kuwepo Kwake miongoni mwenu, basi nini itakuwa majaliwa yenu?

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Je, Ulikuwa Unajua? Mungu Amefanya Jambo Kubwa Miongoni Mwa Wanadamu

Na bado ni mtu huyu wa kawaida, Aliyejificha kati ya watu, ndiye anayefanya kazi hii mpya ya kutuokoa. Yeye hatupi maelezo yoyote, wala Hatuambii kwa nini amerudi, lakini Yeye anafanya tu kazi Anayokusudia kufanya kulingana na mpango Wake na utaratibu Wake. Maneno Yake na matamshi Yake yanazidi kuwa ya mara kwa mara. Kuanzia kufariji, kuhimiza, kukumbusha, na kuonya mpaka kukaripia na kutia adabu; kuanzia kutumia toni ya upole na laini mpaka kutumia maneno makali na ya adhama—yote hayo humfanya mwanadamu ahisi rehema kuu na hofu kabisa. Kila kitu Anachosema kinalenga siri zilizofichwa ndani yetu; maneno Yake huchoma mioyo yetu, huchoma nafsi zetu, na kutuacha tukiwa tumejaa aibu isiyovumilika, tusijue pa kujificha. …

Bila sisi kujua, mtu huyu asiye na umuhimu Ametuelekeza katika hatua moja baada ya nyingine ya kazi ya Mungu. Tunapitia majaribu mengi, na kuadibu kusikohesabika, na tunajaribiwa na kifo. Tunapata kujua kuhusu tabia ya Mungu ya haki na uadhama, kufurahia pia, upendo na huruma Zake, tunakuja kufahamu nguvu za Mungu ambazo ni kubwa na hekima Yake, tunashuhudia uzuri wa Mungu, na kutazama shauku Yake ya kumwokoa mwanadamu. Kwa maneno ya huyu mtu wa kawaida, tunakuja kujua tabia na kiini cha Mungu, kufahamu mapenzi ya Mungu, kujua asili ya mwanadamu na kiini cha mwanadamu, na tunapata kuona njia ya wokovu na ukamilifu. Maneno Yake yanafanya sisi “tufe,” na yanatufanya “tuzaliwe upya”; maneno Yake hutufariji, lakini pia yanatuacha tukiwa tumejawa na hatia na hisia ya kuwa wadeni; maneno Yake hutuletea furaha na amani, lakini pia maumivu makubwa sana. Wakati mwingine sisi ni kama wanakondoo wa kuchinjwa mikononi Mwake; wakati mwingine sisi ni kama vipenzi vya roho Yake na tunafurahia upendo Wake wenye upole; wakati mwingine sisi ni kama maadui Wake, na chini ya macho Yake tunageuzwa kuwa majivu kwa ghadhabu Yake. Sisi ni jamii ya wanadamu waliookolewa Naye, sisi ni funza machoni Pake, na sisi ni wanakondoo waliopotea ambao, usiku na mchana, Yeye hunuia kuwapata. Yeye ni mwenye huruma kwetu, Anatudharau, Anatuinua, Anatufariji na kutuhimiza, Anatuongoza, Anatupa nuru, Anaturudi na kutufundisha nidhamu, na Yeye hata hutulaani. Usiku na mchana, Yeye haachi kamwe kuwa na wasiwasi juu yetu, na Anatulinda na kututunza usiku na mchana, Haondoki kamwe upande wetu. Anamwaga damu yote ya moyo Wake kwa ajili yetu na kulipa gharama zozote kwa ajili yetu. Ndani ya matamshi ya mwili huu usio na maana na wa kawaida, tumefurahia ukamilifu wa Mungu na kuona hatima ambayo Mungu ametupa. …

Mungu huendelea na matamshi Yake, akitumia mbinu mbalimbali na mitazamo kutuonya kuhusu kile tunachopaswa kufanya, wakati huo huo Anaeleza sauti ya moyo Wake. Maneno Yake yanabeba nguvu za maisha, yanatuonyesha njia tunayopaswa kuitembea, na kutuwezesha kufahamu ukweli ni nini. Tunaanza kuvutiwa na maneno Yake, tunaanza kuzingatia sauti Yake na jinsi Anavyoongea, na bila hiari tunaanza kuvutiwa na hisia za ndani kabisa za mwanadamu huyu asiye wa ajabu. Anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yetu, Anapoteza usingizi na hamu ya kula kwa ajili yetu, Analia kwa ajili yetu, Anashusha pumzi kwa ajili yetu, Anaugulia katika ugonjwa kwa ajili yetu, Anadhalilishwa kwa ajili ya wokovu na hatima zetu; na uasi wetu na kufa ganzi kwetu kunatoa machozi na damu kutoka moyoni Mwake. Hakuna mtu wa kawaida mweye nafsi hii au miliki hizi, wala haiwezi kumilikiwa au kufikiwa na mtu yeyote aliyepotoka. Anaonyesha uvumilivu na subira isiyomilikiwa na mtu wa kawaida, na upendo Wake si kitu ambacho kiumbe chochote kimepewa. Hakuna mtu mbali na Yeye anayeweza kujua mawazo yetu yote, au kufahamu asili yetu na kiini chetu kwa uwazi na kwa ukamilifu, ama kuhukumu uasi na upotovu wa binadamu, ama kusema nasi na kufanya kazi kati yetu kama hivi kwa niaba ya Mungu aliye mbinguni. Hakuna mtu isipokuwa Yeye ambaye amepewa mamlaka, hekima, na heshima ya Mungu; tabia ya Mungu na kile ambacho Mungu anacho na alicho vinatoka, kwa ukamilifu wao, ndani Yake. Hakuna mtu mbali na Yeye ambaye anaweza kutuonyesha njia na kutuletea mwangaza. Hakuna yeyote ila Yeye anayeweza kutufichulia siri ambazo Mungu hajatufunulia tangu uumbaji hadi leo. Hakuna yeyote isipokuwa Yeye ambaye anaweza kutuokoa kutoka kwenye utumwa wa Shetani na tabia zetu potovu. Anamwakilisha Mungu; Anaonyesha sauti ya moyo wa Mungu, ushawishi wa Mungu, na maneno ya hukumu ya Mungu kwa wanadamu wote. Ameifungua enzi mpya, nyakati mpya, na kuleta mbingu na nchi mpya na kazi mpya, Ametuletea matumaini na kukomesha maisha yaliyosababisha hali isiyo dhahiri, na Amewezesha nafsi zetu zote kuiona njia ya wokovu kikamilifu. Ameshinda nafsi zetu zote na kupata mioyo yetu. Tangu wakati huo na kuendelea, mioyo yetu imepata kutambua, na roho zetu zinaonekana kuhuishwa: Mtu huyu wa kawaida, asiyekuwa mwenye umuhimu, mtu huyu anayeishi miongoni mwetu na Aliyekataliwa na sisi kwa muda mrefu sana—je, huyu si Bwana Yesu, ambaye daima yupo katika mawazo yetu, tunapoamka au tunapoota, na ambaye tunamtamani usiku na mchana? Ni Yeye! Ni Yeye kweli! Yeye ni Mungu wetu! Yeye ndiye ukweli, njia, na uzima! Yeye ametuwezesha kuishi tena na kuona nuru na Amekomesha mioyo yetu kuhangaika. Tumerudi nyumbani mwa Mungu, tumerejea mbele ya kiti Chake cha enzi, tuko uso kwa uso pamoja na Yeye, tumeshuhudia uso Wake, na tumeona njia iliyo mbele.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kiambatisho 4: Kutazama Kuonekana kwa Mungu katika Hukumu na Kuadibu Kwake

Katika Enzi ya Ufalme, Mungu hutumia maneno kuikaribisha enzi mpya, kubadilisha njia ambayo kwayo Yeye hufanya kazi, na kufanya kazi ya enzi nzima. Hii ndiyo kanuni ambayo kwayo Mungu hufanya kazi katika Enzi ya Neno. Alikuwa mwili ili Anene kutoka katika mitazamo tofauti, ili mwanadamu aweze kumwona Mungu kweli, ambaye ni Neno kuonekana katika mwili, na angeweza kuona hekima na ajabu Yake. Kazi kama hiyo inafanywa ili kufikia malengo ya kumshinda mwanadamu, kumkamilisha mwanadamu na kumuondoa mwanadamu. Hii ndiyo maana halisi ya kutumia Neno kufanya kazi katika Enzi ya Neno. Kupitia kwa Neno, mwanadamu anakuja kuijua kazi ya Mungu, tabia ya Mungu, kiini cha mwanadamu, na kile ambacho mwanadamu anafaa kuingia ndani. Kupitia kwa Neno, kazi ambayo Mungu anataka kufanya katika Enzi ya Neno inatimizwa kwa ukamilifu. Kupitia kwa Neno, mwanadamu anafichuliwa, anaondolewa, na kujaribiwa. Mwanadamu ameliona Neno, amelisikia Neno, na kuwa na ufahamu wa kuwepo kwa Neno. Kwa sababu hiyo, anaamini katika kuwepo kwa Mungu, katika uweza na hekima ya Mungu, na vilevile katika upendo wa Mungu kwa mwanadamu na hamu Yake ya kumwokoa mwanadamu. Ingawa neno “Neno” ni rahisi na la kawaida, Neno kutoka katika kinywa cha Mungu mwenye mwili hutikisa ulimwengu mzima; linabadilisha moyo wa mwanadamu, mawazo, na tabia ya zamani, na jinsi ulimwengu wote ulivyokuwa ukionekana. Katika enzi zote, ni Mungu wa leo tu ndiye Anayefanya kazi kwa njia hii, na ni Yeye Anayezungumza kwa namna hii na kuja kumwokoa mwanadamu hivi. Kuanzia wakati huu na kuendelea, mwanadamu anaishi chini ya mwongozo wa maneno ya Mungu, akichungwa na kuruzukiwa na maneno Yake. Watu wanaishi katika ulimwengu wa maneno ya Mungu, kati ya laana na baraka za maneno ya Mungu, na kuna hata watu wengi zaidi ambao wamekuja kuishi chini ya hukumu na kuadibu kwa maneno Yake. Maneno haya na kazi hii vyote ni kwa sababu ya wokovu wa mwanadamu, kwa sababu ya kutimiza mapenzi ya Mungu, na kwa sababu ya kubadilisha kuonekana kwa asili kwa ulimwengu wa uumbaji wa zamani. Mungu aliuumba ulimwengu kwa kutumia maneno, Anawaongoza watu ulimwenguni kote kutumia maneno, na Anawashinda na kuwaokoa kutumia maneno. Hatimaye, Atatumia maneno kuutamatisha ulimwengu mzima wa zamani, hivyo kuukamilisha mpango Wake mzima wa usimamizi.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Enzi ya Ufalme Ni Enzi ya Neno

Neno limepata mwili na Roho wa kweli amepatikana katika mwili—ukweli wote, njia, na uzima umekuja katika mwili, na Roho wa Mungu hakika amewasili duniani na Roho amekuja katika mwili kwa kweli. Ingawa, kijuujuu, hili linaonekana kuwa tofauti na utungaji mimba kwa Roho Mtakatifu, katika kazi hii mnaweza kuona dhahiri zaidi kwamba Roho tayari amedhihirika katika mwili, na, zaidi ya hayo, kwamba Neno limepata mwili, na Neno limeonekana katika mwili. Unaweza kufahamu maana ya kweli ya maneno haya: “Mwanzoni kulikuwa na Neno, na Neno alikuwa na Mungu, na Neno alikuwa Mungu.” Zaidi ya hayo, lazima ufahamu kwamba Neno la leo ni Mungu, na utazame Neno likiwa mwili. Huu ni ushuhuda bora zaidi unaoweza kuwa nao. Hili linathibitisha kwamba una ufahamu wa kweli wa Mungu kupata mwili—mbali na kumjua Yeye, lakini pia unajua kwamba njia unayoifuata leo ni njia ya uzima, na njia ya ukweli. Hatua ya kazi ambayo Yesu alitekeleza ilitimiza tu kiini cha “Neno alikuwako kwa Mungu”: Ukweli wa Mungu ulikuwako kwa Mungu, na Roho wa Mungu alikuwa na mwili na alikuwa asiyetenganishwa kutoka katika mwili huo. Yaani, mwili wa Mungu mwenye mwili ulikuwa na Roho wa Mungu, ambalo ni thibitisho kuu zaidi kwamba Yesu mwenye mwili alikuwa kupata mwili wa kwanza wa Mungu. Hatua hii ya kazi hasa inatimiza maana ya ndani ya “Neno lakuwa mwili,” ilichangia kwenye maana ya kina zaidi ya “naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu,” na inakuruhusu wewe uamini kwa uthabiti maneno “Hapo mwanzo kulikuwako na Neno.” Ambalo ni kusema, wakati wa uumbaji Mungu alikuwa na maneno, Maneno Yake yalikuwa na Yeye na yasiyotenganishwa kutoka Kwake, na katika enzi ya mwisho, Yeye anafanya nguvu na mamlaka ya maneno Yake yawe hata wazi zaidi, na kumruhusu mwanadamu kuziona njia Zake zote—kuyasikia maneno Yake yote. Hiyo ndiyo kazi ya enzi ya mwisho. Lazima uelewe mambo haya yote kabisa. Si suala la kuujua mwili, bali la jinsi unavyouelewa mwili na Neno. Huu ndio ushuhuda unaopaswa kuwa nao, kile ambacho kila mtu lazima akijue.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Utendaji (4)

Maneno yangu ndio ukweli usiobadilika milele. Mimi Ndiye mtoaji wa maisha kwa mwanadamu na mwongozo wa pekee kwa wanadamu. Thamani na maana ya maneno Yangu haibainishwi na kama yanakubaliwa au kutambuliwa na mwanadamu, ila ni kwa kiini cha maneno yenyewe. Hata kama hakuna mtu hata mmoja duniani anaweza kupokea maneno Yangu, thamani ya maneno Yangu na usaidizi wake kwa mwanadamu hayapimiki na mwanadamu yeyote. Kwa hivyo, Ninapokumbwa na wanadamu wengi wanaoasi, kukataa au kudharau kabisa maneno Yangu, msimamo Wangu ni huu tu: Acha wakati na ukweli uwe shahidi Wangu na uonyeshe kuwa maneno Yangu ndiyo ukweli, njia na uhai. Wacha vionyeshe kuwa yote Niliyosema ni sawa, na ni yale ambayo mwanadamu anapaswa kuwa nayo, na, zaidi ya hayo, yale ambayo mwanadamu anapaswa kukubali. Nitawajulisha wote wanaonifuata ukweli huu: Wale ambao hawawezi kuyakubali maneno Yangu kikamilifu, wale ambao hawawezi kutenda maneno Yangu, wale ambao hawawezi kupata kusudi katika maneno Yangu, na wale ambao hawawezi kupokea wokovu kwa sababu ya maneno Yangu, ni wale ambao wamehukumiwa na maneno Yangu na, zaidi ya hayo, wamepoteza wokovu Wangu, na fimbo Yangu haitaondoka kamwe miongoni mwao.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mnapaswa Kuzingatia Matendo Yenu

Iliyotangulia: 6. Kwa nini husemwa kuwa kupata mwili kwili kwa Mungu hukamilish umuhimu wa kupata mwili?

Inayofuata: 8. Ni jinsi gani Mungu anayepata mwili ili kufanya kazi ya hukumu huimaliza imani ya wanadamu katika Mungu asiye yakini na enzi ya giza ya utawala wa Shetani?

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp