Filamu za Injili | "Njia ya Kwenda katika Ufalme wa Mbinguni ni Yenye Hatari"

12/06/2018

Zhong Xin ni mhubiri kutoka katika kanisa moja la nyumbani katika bara China. Amekuwa muumini katika Mungu kwa miaka mingi na kila mara amepitia kukamatwa na mateso ya CCP. Chuki yake ya CCP ni ya kina sana, na ameona wazi kwa muda mrefu sasa kwamba CCP ni utawala wa kishetani ambao unajiweka katika upinzani na Mungu. Kwa miaka ya hivi majuzi, ameona shutuma, kukamatwa na kuteswa kinyama kwa kanisa la Umeme wa Mashariki na serikali ya CCP na dunia ya kidini. Alichoona kuwa cha ajabu, hata hivyo, kilikuwa kwamba Umeme wa Mashariki halikukosa tu kushindwa, lakini kwa kinyume lilikuwa limenawiri zaidi na zaidi, na hivyo Zhong Xin alianza kutafakari tena: Je, hili Umeme wa Mashariki ni dhihirisho la kuonekana na kazi ya Bwana? Aligundua pia kwamba maneno yaliyotumiwa na CCP na dunia ya kidini kulishutumu Umeme wa Mashariki yote yalikuwa uvumi na uongo na kadhalika, hivyo ili kupata ukweli wa mambo, aliwaongoza ndugu zake kuchunguza Umeme wa Mashariki. Kupitia kusikiliza ushirika wa wale waliotoa ushuhuda katika Kanisa la Mwenyezi Mungu, wengi wao walithibitisha kwamba maneno yaliyoonyeshwa na Mwenyezi Mungu ni ukweli, kwamba maneno haya ni sauti ya Mungu na kwamba Mwenyezi Mungu ni Bwana Yesu aliyerudi. Lakini lilikabiliwa na ukandamizaji na utesaji wa kikatili wa Kanisa la Mwenyezi Mungu na serikali ya CCP, na vilevile uasi na shutuma za wazi kutoka kwa wachungaji na wazee wa dunia ya kidni, watu wengine walishangazwa: Kazi ya Mwenyezi Mungu ni njia ya kweli, hivyo ni kwa nini inakumbana na uasi na shutuma za wazi za nguvu za kisiasa na dunia ya dini? Kwa kusoma maneno ya Mwenyezi Mungu, na kwa kusikiliza ushirika wa wale wanaotoa ushuhuda katika Kanisa la Mwenyezi Mungu, ndugu wanaelewa sababu ya msingi ya uasi wa wanadamu kwa Mungu, wanaona wazi kwa nini njia ya kwenda mbinguni ni yenye hatari sana, na wanapata kuwa na utambuzi kuhusu kiini kipinga Mungu, cha kuchukia ukweli cha utawala ya kishetani ya CCP na viongozi wa dunia ya kidini. Watu kama Zhong Xin kwa uamuzi wametupa vifungo na minyororo ya ushawishi wa Shetani, wamekubali kazi ya siku za mwisho ya Mwenyezi Mungu, na kwa kweli wamerejea mbele ya kiti cha enzi cha Mungu.

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp