172 Tunakamilisha Misheni Yetu

1

Tunaishi duniani, Mungu anatawala maisha na mauti, majanga na mali yetu, na hakuna aliye nje ya amri ya Mungu.

Mafanikio au kutofaulu, uhafifu au utajiri na umaarufu, furaha au huzuni, vyote ni tupu.

Kristo wa siku za mwisho Anaonekana na kufanya kazi, Yeye anatoa ukweli na kuleta uzima wa milele.

Neno la Mungu linatunyunyizia nasi tunaielewa dunia, tunamfuata Mungu na kutembea katika njia sahihi maishani.

Ni kwa kupitia neno la Mungu na kuuelewa ukweli tu ndiyo twajua kuwa kumpenda Mungu ni muhimu zaidi.

Tunafurahia upendo wa Mungu kwa hivyo tunapaswa kumlipa na kueneza neno la wokovu wa Mungu wa siku za mwisho.

Tunayafikiria mapenzi Yake nasi tunatimiza misheni yetu, neno la Mungu linatuongoza na tu waaminifu mpaka kifo.

Sisi ni wa rangi tofauti, mataifa tofauti, upendo wa Mungu unatuunganisha katika kupendana.

Ndugu wanafanya kazi kwa pamoja, tukitekeleza wajibu wetu ili kuuridhisha moyo wa Mungu.

Kwa uwiano, tunalipiza upendo wa Mungu na kushuhudia matendo ya Muumba.

Tunatumia nguvu zetu zote bila kujali kule tuliko ulimwenguni, tunatimiza misheni yetu na tumejitolea kabisa kwa Mungu.

2

Nchini China, nchi ya pepo, hakuna haki za binadamu, tunateswa kwa sababu ya kumshuhudia Kristo.

Tunafadhaika kutokana na mateso na maumivu makali, na tunaiona sura mbaya ya kweli ya ibilisi.

Tunamdharau Shetani, astahiliye dharau na mkatili sana, mioyoni mwetu tunamtamani Kristo achukue mamlaka.

Barabara kwenda katika ufalme ni yenye milima na mabonde, tukitegemea neno la Mungu imara tunasonga mbele.

Tuliokejeliwa na kukashifiwa, kukataliwa na kutengwa, mioyo yetu imeridhika alimradi tumfariji Mungu.

Tukiushuhudia upendo wa Mungu, tukijawa imani, tunakamilisha kazi yetu na kukamilisha misheni yetu.

Kutoka katika mataifa yote kote ulimwenguni, tunakusanyika pamoja, injili ya ufalme inaenea ulimwenguni kote.

Dini zote zinakuwa moja bila kujali mipaka ya kitaifa, wampendao Mungu wanarejea mbele Yake.

Tunamshuhudia Kristo na kulitukuza jina la Mungu, tunatoa shukrani na sifa zetu kwa Mungu.

Maafa na dhiki zote zimepita, alfajiri ya haki imeonekana.

Tunatoa sifa na tunaimba, Kristo wa siku za mwisho anatawala kama Mfalme!

Iliyotangulia: 171 Wito wa Nafsi

Inayofuata: 173 Azimio Langu Huimarishwa Kupitia Mateso

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp