244 Wokovu wa Mungu kwa Mwanadamu Ni Halisi Sana

1 Baada ya kupitia hukumu ya maneno ya Kristo, moyo wangu hatimaye umeamka. Naona jinsi upotovu wangu ulivyo wa kina, kwamba mimi ni ukoo wa Shetani. Nisingeshindwa na maneno ya Mungu, ingekuwa vigumu sana kukubali hukumu ya Mungu. Natafakari jinsi matendo na mawazo yangu yalivyojaa mawazo ya kishetani. Nilifuatilia tu umaarufu na hadhi, nilitaka kushikilia mamlaka ya mfalme. Niliishi kwa dhana na mawazo, lakini bado nilifikiria kwamba nilikuwa na ukweli. Nilifikiria kuwa ningepokea baraka za Mungu kama malipo ya kufanya kazi kwa bidii na kuteseka. Bahati iliyoje kwamba hukumu ya Mungu ilinijia; hapo tu ndipo nilitubu kweli.

2 Maneno makali ya Mungu huchoma vina vya roho yangu. Ingawa napata maumivu, moyoni mwangu naelewa kuwa maneno ya Mungu ni ukweli. Kuwa mtu mwaminifu, lazima nikubali ukweli na nijifunze kumtii Mungu. Nisipokubali hukumu ya ukweli, sistahili kuwa binadamu. Nikithubutu bado kutotii, basi nitakuwa naikosea tabia ya Mungu. Nampinga Mungu kwa makusudi na kupoteza dhamiri na busara yangu, mimi kweli ni mtu duni. Hukumu ya Mungu inanifanya nitubu na kusujudu mbele za Mungu. Hukumu na kuadibu ni wokovu wa Mungu, na moyo wangu wamsifu Mungu.

3 Baada ya kupata hukumu ya maneno ya Mungu, nimeelewa ukweli mwingi. Naona kuwa giza na uovu wa dunia ni kwa sababu Shetani anashikilia mamlaka. Tabia ya kishetani huwaongoza watu kutenda maovu, kutenda dhambi, na kumpinga Mungu. Binadamu amejaa tabia za kishetani, ameshapoteza sura ya binadamu. Ni hukumu na kuadibu kwa Mungu tu vinavyoweza kumtakasa na kuomwokoa binadamu. Kwamba naweza kukubali hukumu ya Mungu ni kwa ajili ya neema na uinuaji Wake. Kula, kunywa, na kufurahia maneno ya Mungu ndiyo baraka yangu kubwa zaidi ya maisha. Naona kuwa Mungu ni mzuri sana, na nitamsifu na kumshukuru Mungu milele.

Iliyotangulia: 243 Moyo Wangu Hauhitaji Chochote Kingine

Inayofuata: 245 Naomba tu Nimpende Mungu Maisha Yangu Yote

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp