243 Moyo Wangu Hauhitaji Chochote Kingine

1 Mungu amekuwa mwili na ameonyesha ukweli, akimtolea mwanadamu uzima. Amevumilia udhalilishaji na mateso yote ili kumwokoa wanadamu, Amekataliwa na enzi hii. Upendo wa Mungu ni mkubwa sana na ni halisi, umekita mizizi moyoni mwangu. Kwa moyo na roho, ninawezaje tena kuwa hasi na mwasi, nikimwumiza Mungu? Nilikuwa mchanga, mpumbavu, na mjinga, sikujali mapenzi ya Mungu. Ingawa nilitimiza wajibu wangu, bila ukweli singeweza kumshuhudia Mungu hata kidogo. Sasa nimeona kuwa Mungu amelipa gharama kubwa sana kuwaokoa wanadamu. Natamani kutoa nguvu zangu zote kufuatilia ukweli na kutekeleza wajibu wangu wa kumridhisha Mungu.

2 Hukumu na kuadibu ni baraka za Mungu, Amenitolea mengi sana. Mara nyingi sana nilikuwa dhaifu na hasi, ni maneno ya Mungu ambayo yalinielekeza na kunifariji. Mara nyingi sana nilijikwaa na kuanguka, ni maneno ya Mungu ambayo yalinisaidia kuinuka tena. Kwa miaka ya usafishaji upendo wote ambao Mungu alinipa ni mkubwa na hauwezi kusahaulika. Kukubali hukumu ya Mungu, nimeijua tabia yangu potovu. Katikati ya ugumu nimejifunza kutii, tabia yangu imebadilika. Nimeonja jinsi karamu ambayo Mungu ameniandalia ni nzuri. Kuweza kuishi kwa kudhihirisha mfano kiasi wa binadamu leo ni kwa sababu ya wokovu wa Mungu.

3 Hukumu na kuadibu kwa Mungu vimenitakasa, nimeazimia kulipa upendo Wake. Nina bahati nzuri kumjua Mungu, kwa kweli ni baraka kubwa zaidi katika maisha haya. Mungu amenielekeza hatua kwa hatua kwenye njia sahihi ya maisha angavu. Kuwa na bahati ya kupokea hukumu na kuadibu kwa Mungu ndilo jambo la maana zaidi. Haki na utakatifu wa Mungu vinastahili sifa, siwezi kumpenda vya kutosha. Natamani kufurahia haki ya Mungu zaidi, naomba iwe pamoja nami ninapomtumikia Mungu maisha yangu yote. Hukumu ya Mungu imeniruhusu kupata wokovu na kuwa mtu mwenye ubinadamu. Naishi kwa kudhihirisha maisha halisi ya binadamu, nitashukuru kila wakati kwa ajili ya upendo wa Mungu.

Iliyotangulia: 242 Nimefurahia Upendo Mwingi wa Mungu

Inayofuata: 244 Wokovu wa Mungu kwa Mwanadamu Ni Halisi Sana

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp