37 Kazi Kuu ya Mungu Imekamilishwa

Kiambata: Sisi tunaomfuta Kristo wa siku za mwisho tunashuhudia kwa ulimwengu mzima: Kazi kuu ya Mungu imekamilika!

1 Mwenyezi Mungu ameonekana katika mwili, akionyesha ukweli ili kuwaokoa binadamu. Tumesikia sauti ya bwana arusi, tumeinuliwa mbele ya Mungu. Hatimaye tumehudhuria karamu ya harusi ya Mwanakondoo, tumeingia katika mafunzo ya ufalme. Hukumu imeanza na nyumba ya Mungu, tabia Yake imefichuliwa kabisa. Ukweli wa maneno ya Mungu hutushinda, tunaanguka mbele za Mungu na kumwabudu. Mioyo yetu na akili zetu zimewekwa wazi kabisa na maneno ya Mungu. Tunapopitia majaribu na usafishaji wa Mungu, tabia zetu potovu zinatakaswa. Kupitia hukumu ya Mungu tunaona haki na utakatifu Wake. Watu wa Mungu ni watiifu mbele Yake, na ni waaminifu kwa Mungu hadi kifo. Mungu amemshinda kabisa Shetani, akiunda kundi la washindi. Sisi tunaomfuta Kristo wa siku za mwisho tunashuhudia kwa ulimwengu mzima: Kazi kuu ya Mungu imekamilika, Amepata utukufu wote!

2 Mwenyezi Mungu amefunua hukumu ya siku za mwisho, akizindua Enzi ya Ufalme. Madhehebu yote yanapitia njaa kuu, watu wote wanalazimishwa kutafuta njia ya kweli. Wanawali wenye busara wanasikia sauti ya Mungu na wanainuliwa mbele ya Mungu kabla ya maafa. Wote wanaokataa kumkubali Kristo wa siku za mwisho watazama katika maafa. Mungu ni Mwenye uweza na hekima katika kazi Yake, Yeye huwapanga watu wote kulingana na aina zao. Mataifa yote na watu wote huja kwenye mwanga, wakinyenyekea mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Matarajio ya ufalme ni yenye kung’aa bila kikomo, yakionyesha mandhari yenye ari. Maafa yataondoa binadamu waovu wa binadamu, yakifichua haki na uadhama wa Mungu. Kila neno la Mungu linatimizwa, maneno ya Mungu yatakamilisha vitu vyote. Ufalme wa Kristo umeonekana duniani, Mungu anaishi pamoja na watu Wake. Sisi tunaomfuta Kristo wa siku za mwisho tunashuhudia kwa ulimwengu mzima: Kazi kuu ya Mungu imekamilika, Amepata utukufu wote!

Iliyotangulia: 36 Mtukuze Mwenyezi Mungu Kwa Sauti Kubwa

Inayofuata: 38 Msifuni Mungu kwa Kupata Utukufu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp