2 Mwana wa Adamu Ameonekana

Kutoka Mashariki ya ulimwengu, mwale wa mwanga unatokea,

ukiangaza njia yote kwenda magharibi.

Mwana wa Adamu ameshuka duniani.

1

Mwokozi amerejea, Yeye ni Mwenyezi Mungu.

Akionyesha ukweli, Ameanzisha enzi mpya.

Mwana wa Adamu ameonekana. (Siyo?)

Mungu amekuja. (Eh!)

Yeye huwaletea binadamu njia ya uzima wa milele.

Mbingu mpya, dunia mpya, enzi mpya,

binadamu wapya, njia mpya, maisha mapya.

Yerusalemu mpya umeshuka duniani.

Mwenyezi Mungu, Kristo wa siku za mwisho, mpendwa wetu apendezaye.

Kila mstari Anenao ni ukweli, utunyinyiziao.

Anatufundisha jinsi ya kutenda, jinsi ya kuwa waaminifu.

Tukiishi kati ya baraka za Mungu, tunampenda Mungu kwa moyo wetu wote.

2

Tumerudi kwa familia ya Mungu na tunaishi maisha ya kanisa,

kila siku tukila na kunywa neno la Mungu, tukikua katika upendo Wake.

Wewe kuja na uimbe! (Sawa!)

Nitacheza ngoma! (Ngoma!)

Tuna baraka za Mungu, tuko katika uwepo wa Mungu.

(Tunaufurahia kweli.)

Maisha yetu ni ya furaha kweli. Ufalme wa Kristo ni nyumba kunjufu.

(Tuna furaha sana.)

Mwenyezi Mungu, Kristo wa siku za mwisho, mpendwa wetu apendezaye.

Kila mstari Anenao ni ukweli, utunyinyiziao.

Anatufundisha jinsi ya kutenda, jinsi ya kuwa waaminifu.

Tukiishi kati ya baraka za Mungu, tunampenda Mungu kwa moyo wetu wote.

3

Hukumu ya neno la Mungu inaishinda mioyo ya watu wote.

Wakiwa wametakaswa, watu wa Mungu humtolea ushuhuda.

Hebu tuwe wenye akili moja (tukitimiza wajibu wetu),

tukilipiza upendo wa Mungu,

tukieneza injili ya Ufalme wa Mungu.

(kuwa na ushuhuda kwa Mungu).

Jina takatifu la Mungu linasifiwa na wote.

Neno la Mungu linaenea duniani kote.

Ufalme wa Kristo unafanyika duniani.

Mwenyezi Mungu, Kristo wa siku za mwisho, mpendwa wetu apendezaye.

Kila mstari Anenao ni ukweli, utunyinyiziao.

Anatufundisha jinsi ya kutenda, jinsi ya kuwa waaminifu.

Tukiishi kati ya baraka za Mungu, tunampenda Mungu kwa moyo wetu wote.

Iliyotangulia: 1 Mwana wa Adamu Ashuka Duniani

Inayofuata: 3 Mwenyezi Mungu, wa Kwanza na wa Mwisho

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp