34. Uzinduzi wa Kiroho wa Mkristo

Na Lingwu, Japani

Mimi ni mtoto wa miaka ya themanini, na nilizaliwa katika kaya ya kawaida ya mkulima. Kakangu mkubwa alikuwa mgonjwa na asiyejiweza daima tangu alipokuwa mdogo. Babangu alijeruhiwa katika ajali nilipokuwa na umri wa miaka 10; alipoozwa miaka miwili baada ya hiyo. Hali ya fedha ya familia yetu ilikuwa fukara kuanzia, na tukaingia katika deni kubwa kumtibu babangu. Marafiki na jamaa zetu waliogopa kwamba hatungeweza kulipa deni hilo, na hawakuwa tayari kutupokesha pesa. Nikiwa sijiwezi, nililazimika kuacha shule nikiwa na miaka 16 kufanya kazi mbali na nyumbani. Katika usiku wa manane na mtulivu, ningefikiri mara nyingi: Walipokuwa wadogo, watoto wenye umri sawa na mimi wangecheza kwa uhuru baada ya shule, wakati ningelazimika kuwa mashambani nikifanya kazi ya ukulima; sasa wamekuwa wakubwa kama mimi, na bado wanaenda shuleni, wakitenda kama watoto waliodekezwa na wazazi wao lakini ninalazimika kuanza kazi kwa umri mdogo na kuteseka aina zote za taabu kusaidia familia yangu. … Wakati huo, nililalamika kwa wazazi wangu kuhusu kwa nini walinizaa, na kuuliza ni kwa nini nilikuja duniani kuteseka na kufanya kazi kwa bidii tu. Lakini hakukuwa na chochote ambacho ningeweza kufanya kuhusu hilo, na ningekubali tu uhalisi huu. Wakati huo, matakwa yangu makubwa zaidi yalikuwa kufanya kazi kwa bidii, kupata pesa, na kuwaruhusu wazazi wangu kuishi kwa kustareheka, na kutoangaliwa na dharau na wengine.

Mwanzoni nilifanya kazi katika kiwanda cha binafsi cha alumini. Kwa kuwa nilikuwa mfanyakazi mtoto, bosi alinitunza vizuri na chakula na nyumba yangu daima. Baada ya mwaka mmoja, nilihisi kwamba mishahara yangu ilikuwa ndogo sana, na kuchagua kufanya kazi ya kunyunyiza vanishi katika kiwanda cha fanicha ambayo watu wengine hawakutaka kuifanya. Wakati huo, bila kujali ni aina gani ya kazi gani niliyokuwa nikifanya, alimradi sikuvunja sheria, ningeenda kuifanya kama ningeweza kuchuma pesa zaidi. Lengo langu la pekee lilikuwa kwamba nilitaka kuwa mtu aliye na pesa, ili nisilazimike kuishi maisha ya mtu maskini tena. Baada ya hilo, jamaa zangu walinijulisha kwa kampuni iliyonipa fursa ya kuondoka nchini kwa ajili ya kazi. Sikuwahi kufikiria kwamba baada ya miaka michache ningeenda ng’ambo.

Katika majira ya kuchipua ya mwaka wa 2012, matakwa yangu yalitimizwa nilipokuja Japani na kuanza maisha yangu mapya. Nilihusika katika tasnia ya ujenzi wa meli, na kupitia uanagenzi niliweka saini mkataba wa miaka mitatu na kampuni hiyo. Nilipoanza kufanya kazi, kwa sababu sikujua jinsi ya kupika, nilikula nudo za haraka kwa mwezi mmoja, hadi singeweza kuzila bila hisia kwamba ningetapika na nikalazimika kujifunza kupika. Sikumbuki ni siku ngapi nilikula wali ambao haujaiva vizuri. Huko Japani, tulikuwa wageni, kwa hivyo hakungeepukika kwamba waajiri wa eneo hilo hawakututendea kwa haki sana. Walitufanya tufanye kazi nyingi chafu, ya kuchosha, na hatari. Hasa nilipokuwa nikinyunyiza vanishi, nilikuwa na woga kiasi, kwa sababu ikiwa gesi ingepatana na moto ingewaka, na ikiwa ningeacha kuwa makini kwa muda ingehatarisha maisha yangu. Lakini bila kujali kama ilikuwa kuteseka katika maisha yangu au hatari katika kazi yangu, alimradi nilifikiri kuhusu kuchuma pesa zaidi kutuma kwa familia yangu, na kuweza kununua gari na nyumba baada ya kurudi nyumbani na kujiinua juu ya wengine na kutoishi tena maisha ya mtu maskini na kuangaliwa na dharau na wengine, nilihisi kwamba kuteseka kwangu wakati huo hakukuwa kubaya sana kwa kweli. Miaka mitatu ya maisha yangu ilipita kufumba kufumbua nikifanya kazi hapo, na muda wa viza yangu ulikuwa karibu kuisha. Kampuni ilikuwa na sera ya kufanya upya mikataba, kwa hiyo ili kuchuma pesa zaidi, nilichagua kufanya upya mkataba wangu na kuendelea kufanya kazi Japani. Kilichonishangaza kwa kufurahisha kilikuwa kwamba muda mfupi baada ya kufanya upya mkataba wangu, nilikutana na injili ya ufalme wa Mwenyezi Mungu.

Mnamo Septemba mwaka wa 2015, rafiki niliyekuwa nimekutana naye Japani aliniambia kuhusu kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho. Alipokuwa akiniambia kuhusu kumwamini Mungu, sikudhani kulipendeza na kufikiri kwamba hili lilikuwa aina ya imani tu. Nilihisi kwamba kumwamini Mungu hakungeweza kubadili kudura yangu. Punde baada ya hilo, nilimwambia rafiki yangu kuhusu ninavyofikiria mwenyewe, kisha nikamwuliza, “Kumwamini Mungu kunaweza kubadili kudura yangu? Mimi ni mtu mwenye kisirani tu, nimeteseka sana tangu nilipokuwa mdogo. Ningekuwa na pesa singekuwa nikiteseka. Nafikiri sasa hivi jambo halisi zaidi kwangu ni kutengeneza pesa. Kwangu, kumwamini Mungu ni jambo la mbali.” Rafiki yangu aliposikia nikizungumza hivi, alinisomea sehemu ya neno la Mungu: “Pale utakapoenda kila siku, kile utakachofanya, yule au kile utakachokumbana nacho, kile utakachosema, kile kitakachokufanyikia—je, kati ya vyote hivi kipo kinachoweza kutabirika? Watu hawawezi kutabiri matukio haya yote, sikutajii kudhibiti namna ambavyo yanavyoendelea. Katika maisha, matukio haya yasiyotabirika hufanyika kila wakati, na ni tukio la kila siku. Mabadiliko haya ya kila siku na njia ambazo yanajitokeza, au ruwaza ambazo yanajitokeza, ni vikumbusho vya kila wakati kwa binadamu kwamba hakuna kinachofanyika bila mpango, kwamba njia ya maendeleo inayochukuliwa na mambo haya, na kutoepukika kwa mambo haya, haviwezi kubadilishwa na mapenzi ya binadamu. Kila tukio linaonyesha onyo kutoka kwa Muumba kwa mwanadamu, na pia linatuma ujumbe kwamba, binadamu hawawezi kudhibiti hatima zao wenyewe; na wakati uo huo kila tukio ni upingaji wa malengo yasiyo na mwelekeo, yasiyo na maana ya binadamu na tamanio la kuchukua hatima yake na kutaka kuidhibiti mwenyewe. … Kutokana na mabadiliko haya ya kila siku katika hatima za maisha yote ya binadamu, hakuna kitu ambacho hakifichui mipango ya Muumba na ukuu Wake; hakuna kile ambacho hakiutumi ujumbe huu kwamba ‘yale mamlaka ya Muumba hayawezi kupitwa,’ ambacho hakionyeshi ukweli wa milele kwamba ‘mamlaka ya Muumba ni ya juu zaidi’(Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III). Baada ya kusikia hili, nilihisi kwamba maneno haya yalikuwa na maana sana, na singeweza kujizuia kufikiri kwamba kuweza kufanya upya mkataba wangu pia kulionekana kama jambo ambalo lilikuwa limepangwa na Mbingu. Lilinifanya pia kufikiri kuhusu nyumbani nilimozaliwa, maisha yangu na familia yangu na kila kitu kilichofanyika karibu na mimi yalikuwa mambo ambayo sikuwa na chaguo kuyahusu na singetarajia. Nilikuwa na hisia kwamba mahali fulani kule nje kuna Mkuu aliye mamlakani.

Rafiki yangu pia alinifanya nisome sehemu hii ya neno la Mungu Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III ambayo inazungumza kuhusu awamu sita ambayo mtu lazima apitie katika maisha: Kuzaliwa: Awamu ya Kwanza; Kukua: Awamu ya Pili; Kujitegemea: Awamu ya tatu; Ndoa: Awamu ya Nne; Uzao: Awamu ya Tano; Kifo: Awamu ya Sita. Nilipokuwa nimesoma neno la Mungu, Nilishangazwa. Sikuwahi kufikiri kwamba Mungu alikuwa amezungumza wazi sana kuhusu kudura ya mwanadamu, na ukweli kwa kweli ni kama Alivyoelezea. Familia ambayo mtu anazaliwa kwayo sio chaguo lake kabisa, na hawezi kuchagua ni aina gani ya wazazi anakuwa nao. Baada ya yeye kukua, hachagui aina ya mume au mke ambaye atakuwa naye. … Kadiri nilivyotafakari kuyahusu, ndivyo nilivyohisi zaidi kwamba maneno haya yalikuwa ya busara kweli, na kisha moyoni mwangu nikaanza kuamini kile ambacho Mwenyezi Mungu alikuwa amesema. Kudura si jambo ambalo linaweza kubadilishwa na mtu mwenyewe. Kutoka wakati huo, nilianza kuvutiwa na kumwamini Mungu zaidi na zaidi, na niliamini kwamba Mungu yuko, na kuamini kwamba kudura ya mtu haiko katika udhibiti wake. Lakini kwa sababu sikujua mengi kumhusu Mungu, nilihisi kwamba Mungu alikuwa mbali sana kutoka kwangu. Hata hivyo, katika uzoefu uliotokea muda mfupi baada ya hilo, nilihisi kwa kweli: Mungu yuko kando yangu, akinichunga na kunilinda.

Kulikuwa kukinyesha siku hiyo, na nilifika kazini kwa wakati uliofaa kama kawaida. Mnamo saa nne asubuhi, nilikuwa mahali pa kazi nikifanya kazi, wakati ghafla nilisikia ngurumo. Sikujua ni nini kilikuwa kimeanguka na kugonga sakafu, na nilikuwa na hofu kuu kwa ajili ya hilo. Nilipogeuza kichwa changu kuangalia, nilishangaa, niliona bomba la chuma la kipenyo cha sentimita 40 na urefu wa mita 4 lililokuwa na uzito wa takriban nusu tani ambalo lilikuwa limeanguka kutoka kwa winchi. Lilianguka na kugonga sakafu chini ya nusu mita kutoka mahali nilipokuwa nikisimama. Niliogopa sana wakati huo kiasi kwamba sikuzungumza kabisa, na ilinichukua muda kupata tena utulivu kutoka kwa mshtuko huo. Moyoni mwangu nilikuwa nikipiga yowe bila kukoma. “Asante Mungu! Asante Mungu!” Kama Mungu hangekuwa hapo akinichunga na kunilinda, basi bomba la chuma lingeniangukia kwa kishindo moja kwa moja, na maisha yangu yasiyo na maana yangekuwa yameisha.

Baada ya kutoka kazini, nilipokuwa nikiongea na ndugu kuhusu kile kilichokuwa kimetokea siku hiyo, walishiriki kwangu kwamba ulikuwa ulinzi wa Mungu. Pia walinisomea kutoka katika neno la Mwenyezi Mungu: “Katika miaka yenu mirefu yote, kimsingi kila mtu amekutana na hali nyingi hatari na kupitia majaribu mengi. Hii ni kwa sababu Shetani yupo kando yako, macho yake yakikutazama kila wakati. Anapenda janga linapokupata, wakati maafa yanakupata, wakati hakuna chochote kinaenda sawa kwako, na anapendelea unaponaswa na wavu wa Shetani. Kuhusu Mungu, anakulinda kila wakati, kukuweka mbali na bahati moja mbaya baada ya nyingine na kutokana na janga moja baada ya jingine. Hii ndiyo maana Nasema kwamba kila kitu ambacho mwanadamu anacho—amani na furaha, baraka na usalama wa kibinafsi—yote hakika yanadhibitiwa na Mungu, na Anaongoza na kuamua hatima ya kila mtu(Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VI). Baada ya kusoma neno la Mungu, nilielewa kwamba watu wanaishi kila siku ndani ya wavu wa Shetani. Wakati wowote, wanaweza kukabiliwa na kila aina ya majaribio hatari kutoka kwa Shetani, na wanaweza kupatana na maafa, balaa na idadi yoyote ya mambo ya kusikitisha. Bila Mungu kuwachunga na kuwalinda, watu wangekuwa wamemezwa na Shetani kitambo. Kufikiria kuhusu hatari niliyokumbana nayo katika kazi yangu mwenyewe, na bomba la chuma la nusu tani likianguka na kupiga sakafu nusu mita tu kutoka kwangu, najua kwamba hii haikuwa tu bahati. Kulikuwa Mungu kunichunga na kunilinda ambako kuliniokoa kutoka kwa bahati hii mbaya. Miaka hii yote, sijui ni mara ngapi nilifurahia Mungu kunichunga na kunilinda, lakini wakati huu wote sikumjua Mungu au kumwabudu; kweli sikuwa na dhamiri. Kuanzia kwa wakati huo, nilielewa neema ya Mungu ya wokovu vyema zaidi. Kwamba niliweza kuishi hadi sasa yote ni kwa sababu ya mkono wa upendo wa Mungu kunilinda, na nilimshukuru Mungu kwa dhati. Niliamua pia kwamba katika siku za baadaye ningefanya yote niliyoweza kumfuata Mungu. Katika siku zilizofuata, nilihudhuria mikutano na ndugu mara nyingi, tukasoma neno la Mungu pamoja, na kuwasiliana na kushiriki uzoefu na ufahamu wetu wa maneno ya Mungu, na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu. Tulikuwa huru na tuliokombolewa mioyoni mwetu, kusaidiana na kuauniana katika maisha ya kiroho. Hakuna hata mmoja wao aliyeniangalia kwa dharau, wala hakukuwa na yeyote aliyewatweza maskini na kujipendekeza kwa matajiri, na nilihisi niliweza kuishi kwa heshima. Nilipoishi miongoni mwa kaya hii kubwa, kunjufu, na iliyobarikiwa ya Kanisa la Mwenyezi Mungu, kulikuwa na mabadiliko katika maisha yangu polepole. Sikuwa tena na wasiwasi, mateso na utupu niliokuwa nao awali. Nilihisi mwenye furaha na kuridhishwa zaidi kuliko zamani.

Siku moja, kitu kilifanyika kwa mwajiriwa wa muda mrefu katika kampuni yetu. Alikuwa Mjapani na tayari alikuwa na zaidi ya miaka kumi ya uzoefu katika kampuni. Alikuwa hodari bila kujali kama ilikuwa katika ufahamu wa usalama au teknolojia. Siku hiyo, alipokuwa kazini, alikuwa akiendesha lori la kuinua na alikuwa akifanya kazi fulani huku akiwa ameinuliwa mita 20 hewani. Katika harakati ya kuliendesha, kutokana na kutokuwa makini alisababisha gesi iliyoyeyuka ya lori kuvuja. Kulikuwa na mfanyakazi mwingine wakati huo huo juu yake akifanya uunganishaji fulani, na ghafla kimota kikaanguka na kuishia kwa mavazi yake. Wakati gesi ambayo ilivuja ilipatana na kimota, ililipuka mwale haraka, na moto ukazuka. Watu wengi hapo walimkodolea macho bila kufanya kingine huyu mfanyikazi mzee ambaye alikuwa akimezwa na miako ya moto, lakini hawakujiweza kabisa na hawakuweza kufanya chochote. Hakukuwa na wakati wa kuenda kumtafuta mtu kumwokoa, na katika dakika chache, alikuwa amechomeka hadi kufa. Tulipoona msiba huu ukitokea, watu wengi walimwonea huruma, na hawakuweza kujizuia kufikiri kuhusu maisha yetu wenyewe: Hata hivyo, watu wanaishi kwa ajili ya nini? Kwa sababu ya jambo kama hili likifanyika kando tu na mimi, kweli nilitambua kwamba kama mtu ameondoka kwa Mungu na hana Mungu akimchunga na kumlinda, basi maisha yake hayalindwi nyakati zote. Maisha ya binadamu ni dhaifu sana na si salama yakikabiliwa na balaa. Nilihisi sana kwamba bila kujali jinsi ubingwa wa mtu ulivyo juu kiasi gani au ni kiasi gani cha pesa mtu anacho zaidi, hawezi kudhibiti kudura yake mwenyewe, sembuse kuweza kujiokoa kutoka kwa maafa na kifo.

Baadaye, nilisoma fungu la neno la Mungu: “Kwa sababu ya ukuu na kuamuliwa kabla kwa Muumba, nafsi pweke iliyoanza bila chochote kwa jina lake huweza kupata wazazi na familia, fursa ya kuwa mwanachama wa kizazi cha binadamu, fursa ya kupitia maisha ya binadamu na kuona ulimwengu; na pia inafaidi fursa ya kupitia ukuu wa Muumba, kujua uzuri wa uumbaji wa Muumba, na zaidi kuliko vyote, kujua na kutii mamlaka ya Muumba. Lakini watu wengi zaidi huwa hawatumii vizuri fursa hii nadra na ya kipekee. Mtu hutumia nguvu zake zote maishani akipigana dhidi ya hatima yake, akatumia muda wake wote akihangaika na akijaribu kulisha familia yake na akisafiri huku na kule kati ya kutafuta utajiri na hadhi katika jamii. Mambo ambayo watu huthamini ni familia, pesa, na umaarufu; wanaona mambo haya kuwa mambo yenye thamani zaidi katika maisha. Kila mtu hulalamikia hatima yake, ilhali bado wanazisukuma hatima hizi nyuma ya akili zao na wanabaki na maswali ambayo ni lazima zaidi kuchunguza na kuelewa: kwa nini binadamu yuko hai, namna ambavyo binadamu anafaa kuishi, ni nini maana na thamani ya maisha. Katika maisha yao yote, hata hivyo iwe miaka mingapi, wanakimbilia tu kuhusu kutafuta umaarufu na utajiri, mpaka ujana wao ukawaacha, mpaka wakawa na nywele za kijivu na makunyanzi kwenye uso wao; mpaka wakagundua utajiri na umaarufu ni vitu visivyoweza kusitisha mtu kuelekea katika udhaifu unaotokana na uzee, kwamba pesa haiwezi kujaza utupu wa moyo: mpaka wanapoelewa kwamba hakuna mtu ambaye anaachwa nje kutoka kwenye sheria ya kuzaliwa, kuwa mzee, magonjwa, na kifo, kwamba hakuna mtu anayeweza kutoroka hatima ile inayomsubiri. Mpaka tu pale ambapo anapolazimishwa kukabiliana na awamu ya mwisho maishani ndipo anapong’amua kwa kweli kwamba hata kama mtu anamiliki mamilioni ya mali, hata kama mtu anayo heshima na cheo kikubwa, hakuna anayeweza kutoroka kifo, kwamba kila mtu atarudi kwenye sehemu yake asilia: nafsi pweke, bila chochote kwa jina lake(Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III). Baada ya kumaliza kusoma maneno ya Mungu, nilihisi kusisimuliwa sana: Roho za watu hutoka kwa Mungu, na zinakusudiwa na Mungu kuja miongoni mwa dunia ya wanadamu. Lakini watu bado hawataki kumwamini na kumwabudu Mungu, na hawathamini fursa ya kupitia mamlaka ya Muumba, lakini wanajua tu kuishi kwa ajili ya pesa, umaarufu na uhusiano wa damu. Wote wanashughulika kuharakisha huku na kule kwa bidii sana kujaribu kujikomboa kutoka kwa mpango wa kudura yao, lakini watu wanaweza kupata nini kwa kutafuta mambo haya? Ni gani kati ya mambo haya—jamaa, umaarufu, au utajiri—linaweza kuokoa maisha yao wakati kifo kinakaribia sana? Angalia kifo cha mfanyakazi mwenzangu mzee—huo si ushahidi mzuri kabisa wa ukweli huu? Nikifikiria kuhusu mambo ambayo nimetafuta zamani, si sawa? Nilipoenda ng’ambo kufanya kazi, ningechukua kazi yoyote chafu, ya kuchosha au hatari, ili tu kupata pesa zaidi, kuwafanya watu waniheshimu, na ili nisipate aibu ya umaskini. Hata ingawa nilipitia kila aina ya mateso, sikuwahi kufikiri kubadili njia hii ya kuishi. Nilifuata tu njia iyo hiyo wakati huo wote. Moyoni mwangu, sikujua kama kuna Mungu, wala sikujua kwamba kudura ya mwanadamu iko mikononi mwa Mungu. Nilijitegemea kubadili kudura yangu, na nilijitahidi kutoroka kutoka kwa utaratibu na mpango wa Mungu yaliyopangwa katika maisha yangu. Sikuwa nikifuata njia ya maangamizi? Kama haungekuwa wokovu wa Mungu, au Mungu kunichunga na kunilinda, nahofia kwamba maisha yangu madogo yangekuwa yamenyakuliwa na Shetani kitambo. Hata zaidi, maisha yangu yangewezaje kukamilishwa na kuwa ya maana kama nilivyo sasa? Wakati huo, hatimaye niliona kwamba maana ya maisha si kutafuta utajiri au umaarufu, si kutafuta kuwa mbele ya wengine ili waweze kutuheshimu, lakini badala yake ni kuja katika uwepo wa Mungu, na kupokea wokovu Wake. Ni kwa kuabudu na kumtii Mungu tu ndiyo tunaweza kujiweka huru dhidi ya madhara ya Mungu na kuishi kwa imani na furaha. Kadiri ninavyofikiria hivi, ndivyo ninavyoguswa zaidi. Naona kwamba naweza kumwamini Mungu, na huku ni Mungu kunitendea kwa neema ya pekee. Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniokoa!

Iliyotangulia: 33. Bahati na Bahati Mbaya

Inayofuata: 35. Baada ya Kukubali Wokovu wa Mungu katika Siku za Mwisho, Tunapokea Uzima Mpya

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

13. Sauti Hii Yatoka Wapi?

Na Shiyin, ChinaNilizaliwa katika familia ya Kikristo, na jamaa wangu wengi ni wahubiri. Nilimwamini Bwana pamoja na wazazi wangu tangu...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp