13. Sauti Hii Yatoka Wapi?

Na Shiyin, China

Nilizaliwa katika familia ya Kikristo, na jamaa wangu wengi ni wahubiri. Nilimwamini Bwana pamoja na wazazi wangu tangu nilipokuwa mdogo. Baada ya kukua, nilitoa ombi hili kwa Bwana: Kama ningepata mume ambaye pia ni mwumini, ningejitolea pamoja naye katika huduma kwa Bwana. Baada ya kuolewa, mume wangu kweli alikuja kuamini katika Bwana, na kwa kweli akawa mhubiri wa wakati wote mwenye kujitolea. Ili mume wangu aweke mawazo yake juu ya kazi yake kwa ajili ya Bwana na kutimiza ahadi aliyokuwa ameweka mbele ya Bwana, nilichukua hatua ya kuchukua kazi ngumu ya kusimamia mambo ya nyumba yetu. Ingawa ilikuwa ngumu kidogo na ya kuchosha, moyo wangu ulijawa na furaha na amani bila kujali mambo yalivyokuwa magumu kwa sababu nilikuwa na Bwana kama msaada wangu.

Mwaka wa 1997 ulikuja na ukapita, na wakati fulani niligundua kuwa mahubiri ya mume wangu hayakuwa na nuru ambayo yalikuwa nayo zamani. Wakati wowote nilipomwuliza afanye jambo nyumbani angetoa vijisababu vya kushughulika na kazi yake ya kuhubiri. Hata kama angefanya kazi kiasi ya nyumbani, hangeifanya kwa shauku kabisa, na mara nyingi angenikasirikia kwa sababu ya mambo madogo madogo. Ingawa kwa nje nilidumisha uvumilivu na sikubishana naye, moyoni mwangu nilihisi kutoridhika sana na tabia ya mume wangu. Mzigo mzito wa nyumba yetu na giza ndani ya roho yangu viliniacha katika uchungu. Nilichoweza kufanya kilikuwa tu kuja mbele ya Bwana kuomba na kusema kila kitu kilichokuwa moyoni mwangu usiku wa manane wakati kila mtu alikuwa amelala, na kumwomba Anipe imani na nguvu zaidi. Wakati huo huo, nilitamani sana Bwana arudi hivi karibuni na kuniokoa kutoka katika maisha yangu ya huzuni.

Siku moja mnamo Aprili 2000 nilipokuwa nikiweka nguo kadhaa nilipata mkoba wa mume wangu na nikaona kuwa ulikuwa umejaa kabisa. Niliufungua kwa udadisi na nikaona Biblia na kitabu cha nyimbo na vile vile kitabu kipya kilichokuwa na kifuniko cha nje. Nikajiwazia: “Ni vipi kwamba sijawahi kuona kitabu hiki hapo awali? Lazima kiwe ni aina fulani ya kitabu cha marejeleo kwa kuhubiri au uzoefu wa mtu fulani wa kiroho. Lazima nikisome—labda naweza kupata ruzuku kutoka kwacho.” Nilikifungua kwa udadisi na nikaona kichwa ambacho kilichosema, “Wale Wanaopaswa Kukamilishwa Lazima Wapitie Usafishaji.” “Kicha kizuri namna gani!” Niliwaza, “Kwa kuzingatia mada hii, uzoefu wa usafishaji si jambo baya! Sasa ninapitia usafishaji ambao siwezi kuupita, kwa hivyo nahitaji kusoma hili kwa uangalifu ili nione uzoefu wake wa usafishaji. Kisha nitaweza kupata njia ya utendaji kutoka ndani ya hilo.” Wakati huo, nilianza kusoma: “Hapo zamani, watu wote walikuja mbele za Mungu kufanya maazimio yao na walisema: ‘Hata kama hakuna mtu mwingine anayempenda Mungu, ni lazima mimi nimpende.’ Lakini sasa, usafishaji unakujia, na kwa sababu hili halilingani na fikira zako, hivyo unapoteza imani katika Mungu. Je, huu ni upendo wa kweli? Umesoma mara nyingi kuhusu matendo ya Ayubu—Je, umesahau kuyahusu? Upendo wa kweli unaweza tu kukua kutoka ndani ya imani. … Unapokabiliwa na mateso ni lazima uweze kuweka kando masilahi ya mwili na usifanye malalamiko dhidi ya Mungu. Wakati Mungu anajificha kutoka kwako, ni lazima uweze kuwa na imani ya kumfuata Yeye, kudumisha upendo wako wa awali bila kuuruhusu ufifie au kutoweka. Haijalishi anachofanya Mungu, ni lazima utii mpango Wake na uwe tayari kuulaani mwili wako mwenyewe badala ya kulalamika dhidi Yake. Wakati unakabiliwa na majaribu, lazima umridhishe Mungu, ingawa unaweza kulia kwa uchungu au uhisi kusita kuhusu kuacha kitu unachopenda. Huu tu ndio upendo wa kweli na imani. Haijalishi kimo chako halisi ni kipi, ni lazima kwanza umiliki nia ya kupitia ugumu na imani ya kweli, na ni pia lazima uwe na nia ya kuutelekeza mwili. Unapaswa kuwa tayari kuvumilia ugumu wa kibinafasi na kupata hasara kwa maslahi yako binafsi ili kuridhisha mapenzi ya Mungu. Lazima pia uwe na uwezo wa kuhusi majuto kujihusu moyoni mwako: Hapo zamani, hukuweza kumridhisha Mungu, na sasa unaweza kujuta mwenyewe. Ni lazima usipungukiwe katika yoyote ya hali hizi—Ni kupitia katika vitu hivi ndiyo Mungu atakukamilisha. Usipoweza kufikia viwango hivi, basi huwezi kukamilishwa(Neno Laonekana katika Mwili). Maneno haya yaliugusa moyo wangu sana. Nililia huku nikisoma haya—si hili ndilo nililokuwa nikipitia hasa? Zamani nilikuwa nimeamua kujitolea mwenyewe na mume wangu kwa Bwana. Nilifurahia kabisa kuchukua mzigo wote wa kuendesha kaya ili nimsaidie mume wangu katika kazi aliyokuwa akimfanyia Bwana nje ya nyumba, haijalishi ilivyokuwa ngumu au ya kuchosha. Lakini wakati huo, kwa sababu ya ugumu nyumbani na kutojali masilahi yangu kwa mume wangu, niliishi na hisia za kudumu za kuwa nimekosewa; Nilikuwa naishi katikati ya usafishaji na kupoteza imani na upendo ambao zamani nilikuwa nao. Nilikuwa nimeshindwa kushikilia kwa uthabiti azimio nililokuwa nimefanya mbele ya Mungu, na mara nyingi ningelia peke yangu kwa siri. Nilifikiria juu ya jinsi Ayubu aliweza kuwa shahidi kwa Mungu katikati ya jaribio kubwa na ngumu hivyo na hakupoteza imani katika Mungu. Hata alisema, “Yehova alinipa, na Yehova amechukua; jina la Yehova libarikiwe” (Ayubu 1:21). Ningewezaje kusahau hata hilo? Kisha nilihisi majuto sana kwa yote niliyoyafanya mbele ya Bwana. Ayubu afadhali ateseke na kuacha masilahi yake mwenyewe kuliko kushindwa kumridhisha Mungu. Licha ya miaka mingi ya imani katika Bwana, nilikuwa nimepoteza imani Kwake. Nilimlalamikia Bwana huku nikivumilia usafishaji na sikuwa nikionyesha upendo wangu Kwake hata kidogo! Nilipogundua hili niliamua kwa siri kwamba singeweza tena kuwa kama vile nilivyokuwa hapo awali, kwamba nilipaswa kumuunga mkono mume wangu katika kazi yake kwa Bwana, na kwamba ilikuwa sahihi kwangu kupitia shida kidogo.

Mara mawazo yangu yalipofikia hatua hiyo hali yangu ilibadilika sana na kuwa bora. Nilihisi maneno haya yalisemwa vizuri sana na kweli yalifikia kina cha hali yangu halisi. Yalinionyesha njia ya kutenda na kabla ya mimi kugundua, nguvu na imani viliibuka ndani yangu. Nikajiuliza, “Nani alisema maneno haya? Angewezaje kuwa na ufahamu wa hali ya juu sana? Nimesoma vitabu vilivyoandikwa na watu mashuhuri wa kiroho, na ingawa ni vya kujenga maadili kwa kiasi fulani, havijaandikwa kwa njia iliyo wazi na inayofafanua kama kitabu hiki, wala havina ukweli. Maneno haya yalitoka kwa nani kweli?” Nilivutiwa na maneno katika kitabu hiki na nilitaka kuendelea kusoma; kadiri nilivyosoma zaidi ndivyo nilivyohisi jinsi maneno hayo yalivyokuwa mazuri. Kila mstari uliongea moja kwa moja na moyo wangu. Yaliniruhusu kuelewa kuwa haijalishi mateso ya mtu ni makubwa jinsi gani, lazima tumfuate Mungu hadi mwisho kabisa na kumtii Mungu kwa furaha katika mateso. Hata mtu akiwa dhaifu katikati ya jaribio, anapaswa kuwa na imani katika Bwana na kumtegemea Mungu ili asimame imara. Kadiri nilivyosoma, ndivyo nilivyohisi mwangaza ndani ya moyo wangu na ndivyo nilivyohisi kuwa na njia ya kutenda. Mume wangu alifika nyumbani wakati huo tu, na nikamuuliza mara moja, “Ulipata wapi kitabu hiki?” Alitabasamu na kusema, “Nimekiazima kutoka kwa mtu, na lazima nikirudishe hivi karibuni.” Sikusema kitu kingine chochote.

Siku moja nilipokuwa nikipika, niliweza kusikia sehemu fulani za wimbo ambao mume wangu alikuwa anaucheza. “Nani asiyeshangazwa na haya? Ni nani asiye na hamu ya kumwona Mungu? … Mungu wakati mmoja alishiriki furaha na dhiki na mwanadamu, na leo Amepatanishwa tena na binadamu kufanya upya upendo Wake wa zamani na wao. Baada ya Yeye kuondoka Uyahudi, Mungu alipotea bila kuonekana. Watu wana hamu ya kumwona tena, lakini kwamwe hawajawahi kutarajia kuungana na Yeye hapa na leo. Hii itakosa vipi kuleta kumbukumbu za kitambo? Miaka elfu mbili iliyopita, Simoni mwana wa Yohana alikutana na Bwana Yesu, na akala na Bwana katika meza moja. Miaka ya kufuatia iliongeza upendo wake Kwake. Alimpenda Yesu kwa dhati. Mungu ameishi kwa miaka mingi kati ya binadamu, lakini binadamu hafahamu. Leo, Mungu Mwenyewe ameonekana ili kufanya upya upendo Wake wa kitambo na mwanadamu(“Miaka Elfu Mbili ya Kungoja” katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Maneno ya wimbo huu yaliyapa mawazo yangu ya ndani kabisa sauti na yakaiamsha hisia yangu ya kutamani sana kurudi kwa Bwana. Nililia sana nilipokuwa nikisikiliza, na nikajiwazia: “Tangu nianze kuwa mwumini hadi sasa, nimefikiria kumhusu Bwana Yesu kila siku, nikitumaini kuwa Angeweza kurudi hivi karibuni ili tuweze kukusanyika na kukumbuka tena nyakati zilizopita.” Maneno ya wimbo yalikuwa ya kweli na ya kugusa sana, na hasa yakiweza kuonyesha hisia za kutamani ambazo watu wanazo kwa Bwana. Kisha niliweka kando chakula nilichokuwa nikitayarisha na nikasikiliza kwa makini kabisa. Wimbo mwingine ulianza kucheza baada ya hapo, unaoitwa “Moyo Mwaminifu kwa Mungu”: “Siombi chochote katika maisha yangu ila fikira zangu za upendo kwa Mungu na tamanio la moyo wangu kuweza kukubaliwa na Mungu(Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Niliwaza, “Ni nani aliyeandika wimbo huu? Azimio lake linawezaje kuwa kubwa sana?” Mstari huu hasa ulikuwa wa kutia moyo kwangu: “Siombi chochote katika maisha yangu ila fikira zangu za upendo kwa Mungu na tamanio la moyo wangu kuweza kukubaliwa na Mungu.” Upendo wa aina hiyo kwa Mungu ni safi sana! Katika imani yangu hapo zamani, sikujua jinsi ya kumpenda Bwana, lakini nilitaka tu kufurahia neema Yake, na kufuatilia amani na furaha. Wimbo huu ulifunua mtazamo wangu wa ulimwengu kweli siku hiyo, na nikaona kwamba wale wanaomwamini Mungu lazima wampende Mungu, na wasijitafutie chochote—ni upendo wa aina hii tu ndio unaoweza kuwa safi. Wimbo huu uliandikwa vizuri sana. Kisha nilifanya uamuzi kwa siri ndani ya moyo wangu kuwa mimi pia nilitaka kufuatilia lengo hili, na kwamba ningempenda Bwana hata kama mtu mwingine angempenda au la.

Baada ya kusoma maneno katika kitabu hicho na kusikiliza nyimbo hizo, nilianza kutenda kulingana na yalivyosema. Mume wangu alipoenda kazini tena na hakuwa na wakati wa kusaidia na kazi ya nyumbani, sikuhisi kuwa na mfadhaiko kama hapo awali. Ikiwa ndugu wengine wangeteleza katika kile walichosema, niliweza kuwa mwenye uvumilivu kwa sababu nilitaka kumridhisha Mungu. Nilitafuta tu kumpenda Mungu kama wimbo ulioelezea kwa moyo wangu wote.

Kufumba na kufmbua ulikuwa umewadia wakati wa kupanda mazao yetu. Jioni moja, nilipokuwa nikipanga vitu, mume wangu aliniambia, “Nahitaji kwenda katika kanisa lingine nje ya mji kesho.” Jibu langu la haraka lilikuwa, “Je, utarudi ndani ya siku chache?” “Sijui,” Alisema. “Nitajaribu sana kurudi hivi karibuni. Usijifadhaishe juu ya kazi za hapa nyumbani.” Nilikunja uso mara moja na nikawaza, “Unasema nisifadhaike juu yake, lakini nawezaje kukosa kufadhaika? Unaondoka bila kujua utarudi lini, na shamba la kila mtu mwingine tayari limepandwa. Letu hata hatujalima, na mbegu zikipandwa zikiwa zimechelewa, hatutakuwa na mavuno mazuri katika msimu wa kupukutika kwa majani. Na kisha tutafanya nini? Laiti ungemaliza kupanda mbegu shambani halafu uende kuwasaidia ndugu!” Jioni hiyo nililala kitandani, nisiweze kabisa kulala. Nilikuwa na msukosuko mwingi, nikiwaza: “Mara ya mwisho mume wangu alipoondoka, alienda kwa zaidi ya wiki mbili, lakini hatukuwa na kazi yoyote shambani wakati huo. Huu ni wakati muhimu wa kupanda, kwa hivyo akienda kwa muda wa wiki mbili tena, nitafanyaje? Labda napaswa kumwambia atafute mfanyakazi mwenza afanye kazi hiyo na amalizane nayo.” Lakini niliwaza zaidi kulihusu: “Hapana, hilo halitafaa. Ndugu wanangojea msaada wake. Asipoenda, hilo halitakuwa kosa dhidi ya Bwana?” Katikati ya usafishaji huu nilikuja mbele za Bwana na nikaomba: “Bwana! Sio kwamba siko tayari mume wangu kwenda kuwasaidia ndugu, ni kwamba tu tunahitaji kupanda mashamba sasa. Ninahisi kabisa matokeo ya usafishaji huu na sijui la kufanya. Bwana! Naomba msaada Wako, ili kuulinda moyo wangu na kunizuia nisisumbuliwe na mambo haya.” Baada ya kuomba, maneno haya yalinijia akilini mwangu kwa wazi sana: “Haijalishi kimo chako halisi ni kipi, ni lazima kwanza umiliki nia ya kupitia ugumu na imani ya kweli, na ni pia lazima uwe na nia ya kuutelekeza mwili. Unapaswa kuwa tayari kuvumilia ugumu wa kibinafasi na kupata hasara kwa maslahi yako binafsi ili kuridhisha mapenzi ya Mungu …(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Wale Wanaopaswa Kukamilishwa Lazima Wapitie Usafishaji). Maneno haya yaliushika moyo wangu mara moja na kuuangaza kwa kiasi kikubwa. “Hiyo ni kweli,” Niliwaza, “Mtu akitaka kumridhisha Bwana, anahitaji azimio la kuvumilia shida, na anapaswa kuwa na furaha ya kuteseka katika mwili na masilahi yake ya kibinafsi kutiwa hatarini mradi ni kuhusu kuridhisha mapenzi ya Mungu!” Maneno haya yalinipa imani, na nikawaza: “Mashamba yakipandwa muda ukiwa umepita kidogo, basi iwe hivyo! Kiasi tunachovuna ni uamuzi wa Mungu, na mume wangu kumfanyia Bwana kazi ndilo jambo la muhimu zaidi.” Nikiwa na hili mawazoni, nilihisi hisia ya utulivu na kuachiliwa moyoni mwangu, na kabla ya kujua nilikuwa nimelala. Asubuhi iliyofuata nilimwambia mume wangu: “Nenda ukafanye kazi yako kwa ajili ya Bwana na usijali kuhusu jambo lolote. Wakati wowote utarudi itakuwa sawa. Nitatii kile ambacho Bwana anapanga.” Nikifikiria kuhusu ukweli kwamba matendo yangu yalikuwa yanamridhisha Bwana, nilihisi furaha na uthabiti moyoni mwangu.

Mume wangu alirudi siku chache baadaye, na alinionekania kuwa mtu tofauti kabisa. Alinisaidia na kazi ya nyumbani, na hata akaniambia: “Unafanya kazi kwa bidii kupita kiasi! Miaka michache iliyopita imekuwa migumu kwako vya kutosha, ukishughulikia mambo yetu yote, ndani na nje ya nyumba. Ninajua hili. Nimekuwa nikienda kazini bila kusaidia kushiriki mzigo wa kazi ya nyumbani na wewe. Kuanzia sasa na kuendelea nitasaidia zaidi wakati wowote ninapokuwa na wakati.” Kumsikia akisema jambo hili kulinigusa sana, kwa sababu mume wangu alikuwa hajawahi kuongea namna hii hapo awali. Nilijiwazia: “Tangu asome kitabu hicho nimeona mabadiliko makubwa sana kwake. Sio tu kwamba mahubiri yake yamejawa na mwanga, lakini mtazamo wake kwangu ni tofauti. Kusoma Biblia miaka yote hii hakujambadilisha, lakini sasa amebadilika sana katika muda mfupi sana. Inaonekana maneno katika kitabu hicho yana nguvu ya kuwabadilisha watu!” Wakati huo huo nilihisi kwamba kile kilicho katika kitabu hicho kilikuwa na faida kubwa kwangu pia. Kukisoma kulinitia moyoni imani na nguvu, na nilipotenda kulingana na kile kilichosema, kutoridhika nilikohisi kwa mume wangu kulitoweka tu. Na baada ya kukisoma mtazamo wake kwangu ulikuwa umebadilika pia; alielewa jinsi ya kunijali na kunitunza. Mabadiliko haya yote yaliimarisha hisia zangu kuwa yaliyomo kwenye kitabu hicho ni ya nguvu na yenye mamlaka kweli. Lakini nilishangaa, ni nani aliyekuwa ameandika maneno yaliyo katika kitabu hiki? Sikuwa nimepata jibu.

Siku moja, miezi miwili baadaye, mume wangu alisema alitaka niandamane naye kwenda kuhudhuria mkutano. Nilikuwa na hisia kwamba mkutano huu ungekuwa jambo la kipekee sana, la sivyo hangeenda nami. Nilijawa na matarajio na nikatazamia kuona kitabu hicho tena. Siku iliyofuata, mimi na mume wangu pamoja na dada wawili kwa furaha tulikuwa katika gari njiani kuelekea nyumbani kwa dada mmoja. Kulikuwa na ndugu wengine kadhaa wakishiriki, kati yao dada mmoja katika miaka yake ya thelathini ambaye alijumuisha Maandiko katika ushirika alishiriki nasi ukweli mwingi juu ya kazi ya Mungu katika siku za mwisho. Moyo wangu uling’aa kweli nilipokuwa nikimsikiliza, na nilipata ufahamu wa wazi wa vifungu vingi vya Biblia ambavyo sikuwahi kuelewa hapo awali na vya kuhusu Mungu kurudi kufanya kazi ya hukumu. Nilijiwazia, “Je, ni vipi kwamba ushirika wake ni mzuri sana, kwamba anaweza kuieleza Biblia kwa uwazi sana? Anaelewaje mengi hivyo?” Wakati huo tu, dada huyu alituambia kwa sauti kubwa, tabasamu likiujaza uso wake, “Ningependa kuwaambia, ndugu, habari njema ambayo ni ya kufurahisha sana. Bwana Yesu ambaye tumekuwa tukimtamani sana kwa muda mrefu sasa amerudi akiwa katika mwili miongoni mwetu kutekeleza kazi Yake mpya; kutamka maneno na kufunua ukweli na siri zote; kuweka wazi siri za hatua tatu za kazi ya Mungu, mpango Wake wa usimamizi wa miaka elfu sita, kupata mwili kwa Mungu, na Biblia. Kila kitu nilichoshiriki katika ushirika leo kilitoka katika maneno ambayo yametamkwa na Mungu.” Mimi na ndugu wote waliohudhuria tulisikia habari hii nzuri na mwishowe niligundua: Ilitukia kuwa dada huyu alielewa mengi sana kwa sababu Bwana, aliyekuwa amerejea, alikuwa ameshiriki yote na wanadamu. Sasa sisi pia tulikuwa tunaisikia sauti ya Bwana. Sisi sote tulikumbatiana kwa furaha na tukatoa machozi ya shangwe—mahali pote palianza kutetemeka kwa ajili ya uchangamfu. Nilifurahi sana kiasi kwamba nilitaka kuruka kwa shangwe, na niliwaza: “Siku zote nimetumainia Bwana Yesu arudi hivi karibuni, na sasa Amerudi kweli! Nimebarikiwa sana kwamba ninaweza kukaribisha kurudi kwa Bwana Yesu wakati wa maisha yangu!”

Mkutano ulipokuwa unakaribia kumalizika, dada huyo alimpa kila mmoja wetu kitabu kinachoitwa Hukumu Yaanza na Nyumba ya Mungu. Kwa uangalifu nikishikilia kitabu cha maneno ya Mungu kwa mikono yote miwili, kitabu hicho nilichokuwa nimekisoma hapo awali ghafla kilinijia mawazoni. Kinaweza kuwa kitabu hicho hicho? Baada ya kurudi nyumbani nilimuuliza mume wangu mara moja, “Kitabu nilichoona siku hiyo—kilikuwa kitabu kile kile cha maneno ya Mungu ambacho dada huyo alitupa leo?” Alitabasamu na kusema, “Ndicho.” Wakati huo nilihisi kama niliye kuwa naamka kutoka ndotoni. Sauti hiyo ilitoka kwa Mungu hata hivyo—hiyo ni sauti ya Bwana Yesu aliyerejea, sauti ya Mungu! Si ajabu maneno haya yalikuwa yanayonigusa sana, yakinipa imani na nguvu, yakinibadilisha, na yakaniondoa kutoka katika mateso yangu. Kisha nikamsuta mume wangu, “Kwa nini ulinificha kwamba umekubali kazi mpya ya Mungu?” Alisema, “Wakati huo nilikuwa nataka sana kukuambia, lakini watu wengi katika familia yako ni wahubiri katika jamii za dini, na wanapinga na kuishutumu kazi ya Mungu katika siku za mwisho. Wamekuwa wakituzuia kuichunguza njia ya kweli wakati huu wote. Niliogopa kwamba kama singeweza kueleza wazi vya kutosha na kisha jamaa zako wagundue kulihusu, punde tu ambapo wangeanza kujitokeza kukukatiza na kukuzuia, hili halingeharibu tu nafasi yako ya wokovu, lakini pia ingenifanya kuwa mtenda maovu! Kwa hivyo, niliamua kukuambia baada ya kulichunguza na kupata uwazi juu yake.” Kusikia maelezo haya kuliondoa kumwelewa visivyo mume wangu, na nilishukuru zaidi kwa wokovu wa Mungu kwangu. Niliamua kusoma kitabu hiki cha maneno ya Mungu kwa uangalifu.

Kusoma maneno ya Mwenyezi Mungu kuliiletea lishe na ruzuku roho yangu iliyokuwa na kiu. Sikuwahi kufikiria kwamba ningeweza kusikia maneno ya Bwana aliyerejea kwa masikio yangu mwenyewe, kuinuliwa mbele za Mungu, au kuwa na uso wa uso na Mungu. Nilihisi mwenye shukrani hasa kwa Mungu kwa ajili ya upendo na wokovu Wake. Takribani siku kumi baadaye, mimi na mume wangu tulifanya kazi na dada ambao walieneza injili kuwaleta wale ndugu wengine wenye imani ya kweli katika Bwana kanisani kwetu mbele za Mungu Mwenyezi.

Iliyotangulia: 12. Fumbo la Utatu Linafichuliwa

Inayofuata: 14. Bwana Ameonekana Mashariki

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

4. Mwamko wa Roho Aliyedanganywa

Na Yuanzhi, BraziliNilizaliwa katika mji mdogo huko Kaskazini mwa China na mnamo 2010, nikafuata jamaa kwenda Brazili. Hapa nchini Brazili,...

3. Kufichua Fumbo la Hukumu

Na Enhui, MalasiaJina langu ni Enhui; nina umri wa miaka 46. Ninaishi Malaysia, nami nimekuwa mwumini katika Bwana kwa miaka 27. Mnamo...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp