240 Upendo wa Mungu Waniruhusu Kupata Wokovu

1

Nilimwamini Bwana kwa miaka,

niliishi tu ndani ya mafundisho,

Niliishi ndani ya dhana na mawazo.

Nilimwamini Bwana kwa miaka,

lakini sikujua kutenda

au kupitia neno Lake,

wala sikujua jinsi ya kumtii.

Niliamini kuwa nilijua ukweli,

daima nikitamani baraka za Mungu.

Nilijadiliana na Mungu wakati ninajitumia,

Nilikuwa mdanganyifu na mwovu.

Sikuwahi kuupenda ukweli,

sikuwa na ujasiri wa kutupilia mbali ushawishi wa giza.

Uso wangu mbaya umefichuliwa.

2

Ni kwa Mungu mwenye mwili,

ni kwa ukweli Wake mkubwa,

kwamba nimeokolewa kutoka kwa upotovu wangu.

Upendo wa Mungu waniruhusu kupata wokovu.

Ni Mwenyezi Mungu aniongozaye

kila hatua ya njia.

Kwa sababu ya kuadibu na hukumu Yake,

Nimebadilishwa kama nilivyo leo.

Ni maneno ya Mungu yanayouamsha moyo wangu,

sasa naichukia asili yangu ya kishetani.

Naamua kuutenda ukweli,

na sasa mwili ninajitahidi kuunyima.

Katika siku za mwisho tunaokolewa na Mungu,

tunaokolewa katika siku za mwisho.

Tutaepuka majanga

na kuiona siku ya utukufu wa Mungu;

tutapokea ahadi ya Mungu

na tufurahie baraka za ufalme.

Huu ni upendo wa Mungu ukitujia,

huu ni upendo wa Mungu unaotujia.

3

Leo nimepitia

tabia ya Mungu yenye haki.

Leo nimepitia

upendo wa Mungu na kupata wokovu mkuu wa Mungu.

Leo nimepitia

upendo wa Mungu na nimepokea utakaso Wake.

Kwa mtu mpotovu kama mimi,

kwa mtu mpotovu kama mimi,

kwa mtu mpotovu kama mimi

kuinuliwa, nitakosaje kumshukuru?

Ni kwa Mungu mwenye mwili,

ni kwa ukweli Wake mkubwa,

kwamba nimeokolewa kutoka kwa upotovu wangu.

Upendo wa Mungu waniruhusu kupata wokovu.

Toeni shukrani na sifa kwa Mwenyezi Mungu,

kwa maana upendo wa Mungu pekee ndio safi kabisa.

Nawezaje kutomshukuru Mungu kwa upendo Wake?

Nawezaje kutomshukuru Mungu kwa upendo Wake?

Iliyotangulia: 239 Ni Mungu Ambaye Ameniokoa

Inayofuata: 241 Upendo wa Mungu Daima Unabaki Moyoni Mwangu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp