2. Katikati ya Jaribu la Kifo

Na Xingdao, Korea ya Kusini

Mwenyezi Mungu anasema, “Mungu amekuja kufanya kazi ulimwenguni ili kumwokoa mwanadamu aliyepotoka—hakuna uongo katika haya; kama upo, Asingefanya kazi Yake yeye Mwenyewe. Kitambo, mbinu Zake za wokovu zilikuwa kuonyesha upendo na huruma mkuu, kiasi cha kwamba Alijitolea Yake yote kwa Shetani ili naye aweze kuwapata wanadamu wote. Leo haifanani kamwe na kitambo: Wokovu uliopewa leo unatokea wakati wa siku za mwisho, wakati wa uainishaji wa kila mmoja kulingana na aina yake; mbinu za wokovu wako si upendo wala huruma, lakini kuadibu na hukumu ili mwanadamu aweze kuokolewa kabisa. Hivyo basi, kila kitu unachopokea ni kuadibu, hukumu, na kupiga bila huruma, lakini jua kwamba katika kupiga huku kusiko na huruma hakuna hata adhabu ndogo zaidi, jua kwamba licha ya namna ambavyo maneno haya yanavyoweza kuwa makali, kile kinachokupata ni maneno machache yanayoonekana kutokuwa na huruma kabisa kwako, na jua kwamba, licha ya namna ambavyo hasira Yangu itakavyokuwa, kile kitakachokujia bado ni maneno ya mafunzo, na sinuii kukudhuru, au kukuua. Je, haya yote ni ukweli, sivyo? Jua kwamba leo, iwe hukumu ya haki au usafishaji na adhabu visivyo na huruma, yote haya ni kwa minajili ya wokovu. Haijalishi kama leo kila anaainishwa kulingana na aina yake, ama makundi ya wanadamu yanafichuliwa, matamko yote ya Mungu na kazi ni kwa ajili ya kuwaokoa wale wanaompenda Mungu kwa dhati. Kuhukumu kwa haki ni kwa ajili ya kumtakasa mwanadamu, utakasaji usio na huruma ni kwa ajili ya kumsafisha mwanadamu, maneno makali au kuadibu yote ni kwa ajili ya kutakasa, na kwa minajili ya wokovu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mnapaswa Kuweka Pembeni Baraka za Hadhi na Kuelewa Mapenzi ya Mungu ya Kumletea Mwanadamu Wokovu). Maneno ya Mungu hunigusa sana na hunifanya nilifikirie tukio lisilosahaulika nililopitia zaidi ya miaka 20 iliyopita wakati wa jaribu la kifo. Kwa kweli nilikuja kufahamu kuwa hukumu na kuadibu kwa Mungu ni upendo na wokovu Wake kwa mwanadamu. Haijalishi maneno ya Mungu yanaweza kuwa makali au ya kukasirisha vipi, yananuiwa tu kututakasa na kutubadilisha.

Ilikuwa mnamo Februari 1992. Baada ya jaribu la watendaji huduma, Mungu alituinua tuwe watu wa Enzi ya Ufalme na Alitupa mahitaji Yake: Tuzingatie kusoma maneno Yake na kuyatia katika vitendo, tutafute kumjua Mungu, tumshuhudie Mungu kupitia katika majaribu na kufikia kiwango cha watu wa ufalme haraka iwezekanavyo. Wakati huo, maneno ya Mungu yalitaja mara nyingi “watu wa nyumbani Mwangu,” na “watu wa ufalme Wangu” Maneno haya kila wakati yalinifanya nihisi kama Mungu alituona kama familia Yake mwenyewe. Nilikuwa na ukunjufu na kutia moyo, kwa hivyo nilianza kufuatilia kiwango cha kuwa mmoja wa watu wa Mungu. Ninaomba nikisoma maneno ya Mungu na kutafakari mapenzi Yake kutoka katika maneno Yake. Nilifanya wajibu wangu kadiri ya uwezo wangu na nikaazimia kumfuata Mungu maisha yangu yote. Nilikuwa na umri wa miaka 22. Watu wengi wa rika langu walikuwa wameoa na kupata watoto wakati huo. Familia yangu isiyoamini iliendelea kunitafutia mke, lakini niliwakataa wote.

Nilipenda sana kuimba “Wimbo wa Ufalme,” hasa sehemu hii: “Kwa sauti ya saluti ya ufalme, ufalme wa Shetani unaanguka, ukiangamizwa katika mngurumo wa wimbo wa ufalme, usiinuke tena kamwe!” “Nani duniani anathubutu kuinuka na kupinga? Ninaposhuka duniani Naleta moto, Naleta ghadhabu, Naleta maafa ya aina yote. Falme za dunia sasa ni ufalme Wangu!(Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Nilifikiria jinsi ufalme wa Mungu utakavyodhihirika hapa duniani, na wakati kazi ya Mungu imekamilika, maafa makubwa yatakuja na kila mtu anayempinga Mungu ataangamizwa. Sisi tunaomfuata Mungu, hata hivyo, tutaokoka na Mungu atuongoza kuingia katika ufalme kufurahia baraka za milele. Lilikuwa jambo zuri sana kufikiria yote haya. Wakati huo, nilifikiri kwamba kukubali jina la Mwenyezi Mungu na kuinuliwa ili kujiunga na watu wa ufalme kulimaanisha kwamba kuingia katika ufalme wa Mungu katika maisha haya lilikuwa jambo la hakika ambalo hakuna ambaye angeninyang’anya. Nilifurahi sana. Roho zetu zilisisimshwa na tukajawa na furaha. Tulijitumia kwa ajili ya Mungu bila kuchoka.

Lakini Mungu ni Mwenyezi Mungu na mtakatifu, Yeye huona ndani ya mioyo yetu. na Anajua mawazo, fikira, na tamaa nyingi tulizo nazo. Wakati tu tulijawa na tumaini kwamba tutaingia katika ufalme na kufurahia baraka zake, mwishoni mwa mwezi wa Aprili, Mungu alitamka maneno mapya, akituingiza sote katika jaribu la kifo.

Siku moja, kiongozi wa kanisa alifanya mkutano na akasoma maneno ya Mungu: “Huku watu wanapoota, Nasafiri katika nchi za dunia Nikinyunyizia ‘harufu ya kifo’ iliyo mikononi Mwangu miongoni mwa binadamu. Watu wote ghafula huacha uchangamfu na kuingia katika daraja inayofuata ya maisha ya binadamu. Miongoni mwa wanadamu, viumbe vinavyoishi haviwezi kuonekana tena, maiti imetapakaa kila mahali, vitu vinavyojawa na uchangamfu hutoweka mara moja bila dalili, na harufu ya kusonga ya maiti huenea kote ardhini. … Leo, hapa, maiti ya watu wote imelala hapa na pale katika mchafukoge. Bila watu kujua, Naachilia ndwele yoyote yenye kufisha iliyo mikononi Mwangu, na miili ya binadamu huoza, bila kuacha dalili yoyote ya mwili kutoka utosini hadi kidoleni, na Naenda mbali sana kutoka kwa mwanadamu. Kamwe Sitakusanyika na mwanadamu tena, kamwe Sitakuja miongoni mwa binadamu, kwani hatua ya mwisho ya usimamizi Wangu wote imefika mwisho, na Sitawaumba wanadamu tena, Sitatilia maanani mwanadamu tena. Baada ya kusoma maneno kutoka kinywani Mwangu, watu wote hukosa tumaini, kwani hawataki kufa—lakini ni nani ‘hafi’ kwa ajili ya ‘kuwa hai’? Ninapowaambia watu Nakosa mazingaombwe ya kuwafanya kuwa hai, wao huangua kilio kwa uchungu; kweli, ingawa Mimi ndiye Muumba, Ninayo tu nguvu ya kuwafanya watu wafe, na Nakosa uwezo wa kuwafanya wawe hai. Kwa hili, Naomba msamaha kwa mwanadamu. Hivyo, Nilimwambia mwanadamu kabla kwamba ‘Nina deni lake lisilolipika’—lakini alidhani Nilikuwa nakuwa mpole. Leo, na majilio ya ukweli, bado Nasema hili. Sitausaliti ukweli Ninenapo. Katika dhana zao, watu huamini kwamba kuna njia nyingi ambazo kwazo Mimi huzungumza, kwa hiyo wao kila mara hukamata imara maneno Ninayowapa huku wakitumaini kitu kingine. Je, hizi sizo motisha zenye kosa za mwanadamu? Ni chini ya hali hizi ndiyo Nathubutu kusema ‘kwa ujasiri’ kwamba mwanadamu hanipendi kweli. Singekana dhamiri na kupotosha ukweli, kwa kuwa Singewapeleka watu katika nchi yao iliyo bora; mwishowe, wakati ambapo kazi Yangu itaisha, Nitawaongoza katika nchi ya kifo(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima, Sura ya 40). Niliposoma “Ingawa Mimi ndiye Muumba, Ninayo tu nguvu ya kuwafanya watu wafe, na Nakosa uwezo wa kuwafanya wawe hai.” Nilichanganyikiwa sana. “Kwa nini Mungu aseme hivyo?” Niliwaza. “Maisha na kifo cha mwanadamu vimo mikononi mwa Mungu. Kwa nini Aseme kwamba hana ‘uwezo’ wa kumfanya mwanadamu kuwa hai? Je, sisi waumini kweli tutakufa mwishowe? Sisi ni watu wa ufalme, kwa hivyo tunawezaje kufa? Haiwezekani! Lakini Mungu asingetufanyia utani. Maneno Yake yanasema wazi, ‘Wakati ambapo kazi Yangu itaisha, Nitawaongoza katika nchi ya kifo.’ Je, hiyo haimaanishi kuwa tutaishia kukutana na mauti? Je, hili linahusu nini?” Sikuweza kuelewa tu kwa nini Mungu alisema kitu kama hicho. Kina ndugu wengine karibu na mimi walionekana kana kwamba hawakujua la kusema pia. Kiongozi wa kanisa kisha alitupa ushirika: “Miili yetu imepotoshwa sana na Shetani. Imejawa na tabia za kishetani kama vile kiburi, udanganyifu, ubinafsi, na ulafi, na bado tunasema uwongo na kudanganya wakati wote. Tunaweza kumwamini Mungu na kujitumia kwa ajili yake, lakini hatuwezi kuyatia maneno Yake katika vitendo. Bado tunamhukumu na kumlaumu wakati dhiki na majaribu yanatujia. Hii inaonyesha kuwa mwili wetu ni wa Shetani na unampinga Mungu. Tabia ya Mungu ni yenye haki, takatifu na isiyokosewa. Anawezaje kuwaruhusu watu wa Shetani waingie katika ufalme Wake? Kwa hivyo kazi Yake itakapomalizika, maafa makubwa yatakuja na ikiwa sisi kama waumini hatujapata ukweli, ikiwa tabia zetu za maisha hazijabadilika, basi bado tutakufa.”

Niliposikia ushirika huu kutoka kwa kiongozi, nilizidiwa na hisia na sikujua jinsi nilivyopasa kuhisi. Nilihisi kama kwamba mbingu zilianguka ghafla—nilishtuka. Kuchanganyikiwa na chuki zilijaa akilini mwangu, na nikawaza, “Kama kizazi cha mwisho, je, si sisi ndio tuliobarikiwa zaidi? Mungu ametuinua kuwa watu wa Enzi ya Ufalme. Sisi ndio nguzo za ufalme wa Mungu. Je, tunawezaje kufa mwishowe? Niliacha ujana wangu na matarajio ya ndoa ili nimfuate Mungu. Nimekimbia huku na kule, nimejitumia kwa ajili ya Mungu, na kuteseka sana. Nimekamatwa na kuteswa na CCP, nilidhihakiwa na kukashifiwa na wasioamini. Je, kwa nini bado lazima nife mwishowe? Je, mateso yangu yote yamekuwa bure?” Kufikiria hili kuliniumiza sana. Nilihisi uzito mkubwa ukinigandamiza na nilikuwa na shida kupumua. Niligundua kwamba kila mtu karibu na mimi alikuwa akihisi vivyo hivyo. Wengine walikuwa wakilia kimya kimya, huku wengine wakiweka nyuso zao mikononi mwao na kulia. Baada ya mkutano, mama yangu alisema kwa kushusha pumzi, “Nina zaidi ya miaka 60, na nimekubali kifo. Lakini wewe ni mchanga sana, maisha yako yameanza tu….” Nilipomsikia akisema haya kulinisikitisha hata zaidi na sikuweza kuzuia machozi. Nipinduka na kugeuka kitandani usiku huo, nisiweze kupata hata chembe ya usingizi. Sikuweza kulielewa jambo hilo. Nilikuwa nimejitolea kwa bidii kwa ajili ya Mungu na nikaacha kila kitu ili nimfuate, kwa hivyo kwa nini ilikuwa lazima nife katika maafa makubwa? Sikuweza kukubali jambo hilo, kwa hivyo nilianza kupitia pitia maneno ya Mungu nikitumaini kupata kidokezo, kuona ikiwa matokeo yetu yataweza kubadilishwa. Lakini sikupata majibu niliyotaka. Nikiwa nimepigwa na bumbuazi, niliwaza, “Inaonekana kana kwamba Mungu ametushutumu na vifo vyetu vipo bila shaka. Hakuna anayeweza kubadilisha jambo hilo. Ndicho ambacho Mbingu ameamuru.”

Katika siku chache zilizofuata, nilihisi dhaifu sana. Nilizungumza kwa sauti ya chini sana na sikutaka kufanya chochote. Siku zote nilikuwa nikifanya kazi kwa masaa mengi ya ziada nikiandika maneno ya Mungu hadi mkono wangu ukaumia, lakini jambo hilo kamwe halikunisumbua. Nilitaka tu kina ndugu wasome matamko mapya ya Mungu haraka iwezekanavyo, lakini hali hiyo ya uwajibikaji ilikuwa imekwisha. Ari yangu kuu ilikuwa imeshuka ghafla. Nilipoandika maneno ya Mungu sasa, niliwaza, “Mimi bado mdogo na bado sijafurahia baraka za ufalme wa mbinguni. Kweli sitaki kufa namna hii!” Nilianza kulia nilipoyafikiria hayo yote tena. Moyo wangu ulikuwa mzito wakati huo, na uliuma kama kwamba ulikuwa umedungwa kisu. Kwangu, ulimwengu ulikuwa umepoteza ladha. Nilihisi kana kwamba maafa makubwa yangeweza kuja dakika yoyote, na sikujua ni lini nitakufa. Nilihisi kana kwamba dunia ilikuwa imekwisha.

Nilisoma maneno ya Mungu na nikapata ujuzi fulani wa kibinafsi, kisha polepole, baada ya muda, nilihisi huru. Nilisoma haya katika maneno ya Mungu: “Leo, wakati wa kusonga mbele kuelekea kwa lango la ufalme, watu wote wanaanza kuendelea mbele—lakini wanapofika mbele ya lango, Nafunga lango, Nawafungia watu nje, na kuwataka waonyeshe pasi zao za kuingia. Kitendo cha ajabu kama hiki hakifanani na kile ambacho watu walikuwa wanatarajia, na wote wanastaajabu. Mbona lango—ambalo kila mara limekuwa wazi kabisa—leo limefungwa ghafla kwa kubanwa? Watu wanakanyaga miguu yao kwa nguvu na kutembea hapa na pale. Wanafikiri kwamba wanaweza kuingia ndani kwa hila, lakini wanaponipa pasi zao za kuingia zisizo halisi, Nazitupa ndani ya shimo la moto papo hapo—na, wanapoona ‘juhudi zao za kujitahidi’ zikiteketea moto, wanakata tamaa. Wanashika vichwa vyao, wakilia, wakitazama mandhari mazuri ndani ya ufalme lakini wasiweze kuingia. Lakini Siwaruhusu kuingia kwa sababu ya hali yao ya kusikitisha—ni nani awezaye kuuvuruga mpango Wangu apendavyo? Je, baraka za siku za baadaye hutolewa kwa kubadilishana na ari ya watu? Je, maana ya kuweko kwa mwanadamu inategemea kuingia katika ufalme Wangu apendavyo mtu? … Nilipoteza imani kwa mwanadamu kitambo sana, Nilipoteza tumaini kwa watu kitambo sana, kwani wanakosa lengo, hawajawahi kuweza kunipa moyo unaompenda Mungu, na wao kila mara hunipa misukumo yao badala yake. Nimesema mengi kwa mwanadamu, na kwa kuwa bado watu wanapuuza ushauri Wangu leo, Mimi huwaambia kuhusu maoni Yangu ili kuwazuia kuuelewa vibaya moyo Wangu katika siku za baadaye; kama wataishi au kufa katika nyakati zijazo ni shauri yao, Sina mamlaka juu ya jambo hili. Natumaini watapata njia yao wenyewe ya kuendelea kuishi, nami Sina mamlaka katika hili(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima, Sura ya 46). “Watu wanapokuwa tayari kuyatoa maisha yao, kila kitu huwa hafifu, na hakuna anayeweza kuwashinda. Ni nini kingekuwa muhimu zaidi kuliko uzima? Hivyo, Shetani anakuwa hawezi kufanya chochote zaidi ndani ya watu, hakuna anachoweza kufanya na mwanadamu. Ingawa, katika ufafanuzi wa ‘mwili’ inasemekana kwamba mwili hupotoshwa na Shetani, kama watu watajitoa kweli, na wasiendeshwe na Shetani, basi hakuna anayeweza kuwashinda—na wakati huu, mwili utatekeleza kazi yake nyingine, na kuanza kupokea rasmi mwongozo wa Roho wa Mungu. Huu ni mchakato wa lazima, lazima ufanyike hatua kwa hatua; la sivyo, Mungu hangekuwa na njia ya kufanya kazi ndani ya mwili mkaidi. Hiyo ndiyo hekima ya Mungu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ufafanuzi wa Mafumbo ya “Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima”, Sura ya 36). Nilifadhaika sana nilipokuwa nikitafakari maneno ya Mungu. Sikuwa najisikia hasi na mwenye uchungu kwa sababu niliogopa kifo na nilitamani baraka nyingi? Katika siku za kwanza, nilikuwa nimemwamini Mungu kwa ajili ya baraka na ili niingiea katika ufalme wa mbinguni. Ingawa nilikuwa nimepitia katika jaribu la watendaji huduma, na niliweza kuacha tamaa yangu ya baraka kidogo na niliazimia kumtumikia Mungu, asili yangu danganyifu na ovu ya kishetani ilikuwa imekita mizizi. Mara tu Mungu alipotufanya tuwe watu Wake, moyo wangu tena ulirukaruka kwa matarajio. Nilidhani hakika nitaweza kuingia katika ufalme wa mbinguni wakati huu. Nilidhani kwamba kwa kukubali jina la Mungu, kuinuliwa na Mungu kuwa mmoja wa watu wa ufalme, kuacha kila kitu, na kujitumia, basi bila shaka ningeingia katika ufalme wa mbinguni. Lilikuwa jambo la hakika. Kazi ya Mungu ilipoyavunja mawazo yangu na kuchukua matarajio na hatima yangu, nilikuwa dhaifu na hasi na nikamlalamikia Mungu. Hata nilijuta kujitolea ambako nilijitolea zamani. Niliona kwamba juhudi zangu zote zilikuwa kupata baraka za ufalme wa mbinguni. Sikuwa nikifanya mabadilishano na Mungu, nikimdanganya na kumtumia? Nilifichua tu uasi na malalamiko nilipokumbwa na kila jaribu. Nilitaka kumtii lakini sikuweza, na sikuweza kutenda ukweli niliojua vizuri. Niligundua kuwa nilikuwa mpinzani kwa Mungu kiasili, kwamba nilikuwa wa Shetani. Mtu kama mimi, aliyejaa hisia za kishetani kabisa, anapaswa kufa na kuangamizwa. Sikustahili kabisa kuingia katika ufalme wa Mungu. Hili liliamuliwa na tabia Yake ya haki. Kuweza kupata fursa ya kumfuata Mungu na kujua tabia Yake ya haki kulimaanisha kwamba maisha yangu hayakuwa yamepotea! Kisha nilimwomba Mungu: “Sitaki kuishi kwa ajili ya mwili wangu tena, lakini nilitamani kutii sheria na mipango Yako. Haijalishi mwisho wangu utakuwa upi, hata nikifa, nitaisifu haki Yako.” Nilipoacha kufikiria mwisho na hatima yangu na nilitamani kutii mipango ya Mungu hata kwa gharama ya maisha yangu, nilihisi hisia nzuri ya kuachiliwa.

Lakini wakati huo, ingawa tuliweza kutii na kumfuata Mungu bila kujali matokeo yetu, hatukuwa na lengo la kufuatilia. Lakini mnamo Mei 1992, Mungu alionyesha maneno zaidi, Akituambia tutafute kumpenda Mungu tukiwa hai na tuishi kwa kudhihirsha maisha yenye maana. Mungu alikuwa ametukaribisha katika wakati wa kumpenda Mungu, na jaribu la kifo lilikuwa limeisha. Kupitia kusoma maneno ya Mungu, kukutana na kufanya ushirika, niligundua kwamba ingawa hatima ya mwanadamu iko mikononi mwa Mungu na hakuna mtu anayeweza kuepuka kifo, mapenzi ya Mungu si kwamba sisi tukutane na mauti kwa njia hasi. Anataka tutafute kumpenda kama tungali hai, tuwe na uwezo wa kutenda ukweli, tutupilie mbali tabia zetu potovu, na tuokolewe kabisa. Hapo tu ndipo tutakapostahili kuingia katika ufalme Wake. Mwishowe nilielewa kwamba kwa kutuongoza kuingia katika jaribu la kifo, Mungu hakuwa akituongoza kuelekea kwa mauti yetu, lakini kutufichulia tabia Yake ya haki. Alifanya hili ili tuweze kuelewa Anamwokoa nani, na Anamwangamiza nani, na ni nani anayestahili kuingia katika ufalme Wake. Niliona pia jinsi nilivyokuwa nimepotoshwa na Shetani na niliweza kuyaacha mawazo, fikira, na tamaa yangu ya baraka. Niliweza kutii utawala na mipango ya Mungu na kweli nilianza kufuatilia ukweli. Huu ulikuwa wokovu wa Mungu kwangu! Niliona hata zaidi kwamba Mungu hawahukumu na kuwaadibu watu kwa sababu Anatuchukia au anataka kututesa, bali ili kutuongoza kwenda kwenye njia sahihi ya kufuatilia ukweli na kuokolewa! Kila kitu ambacho Mungu hufanya ndani yetu si kwa ujio wa ukweli. Yeye hupata matokeo kwa kuonyesha tu maneno yanayotuhukumu, kutuadibu, kutujaribu na kutusafisha. Kazi ya Mungu ni yenye busara sana na upendo na wokovu Wake kwa mwanadamu ni halisi sana!

Iliyotangulia: 1. Nimebahatika Kumhudumia Mungu

Inayofuata: 3. Jaribu la Foili

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp