29. Toba ya Afisa

Na Zhenxin, Uchina

Mwenyezi Mungu anasema, “Tangu uumbaji wa dunia hadi sasa, yote ambayo Mungu amefanya katika kazi Yake ni upendo, bila chuki yoyote kwa mwanadamu. Hata kuadibu na hukumu uliyoiona ni mapenzi pia, upendo wa kweli na wa dhati zaidi; upendo huu huwaongoza wanadamu kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu. … Kazi yote Aliyoifanya ni kumwongoza mwanadamu kwenye njia sahihi ya maisha ya wanadamu, ili kwamba wawe na maisha ya kawaida ya wanadamu, kwani mwanadamu hajui jinsi ya kuishi. Bila uongozi kama huo, utaishi maisha tupu yasiyo na maana wala thamani, na kamwe hutajua jinsi ya kuwa mwanadamu wa kawaida(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ukweli wa Ndani wa Kazi ya Ushindi (4)).

Nilizaliwa mashambani. Wazazi wangu walikuwa wakulima waaminifu na wenye bidii. Wanakijiji wengine walitudharau kila wakati na walituonea kwa sababu tulikuwa maskini. Niliwaza, “Siku moja nitawaonyesha. Siku moja wataniangalia kwa njia tofauti.” Nilijiunga na jeshi nilipokuwa katika ujana wangu. Ningechukua kazi yoyote, bila kujali jinsi ilivyokuwa chafu au ya kuchosha, nikitumai kupandishwa cheo. Lakini kwa miaka mingi nilisalia kuwa askari asiye na cheo. Kisha nikagundua, kutoa zawadi ndiko kulileta tathmini nzuri na vyeo wala si juhudi. Hilo lilikuwa jambo la kukera kwangu, lakini nilitaka kupandishwa cheo, kwa hiyo nilijikakamua na kuwanunulia wakubwa wangu zawadi kwa kutumia akiba yangu yote. Kwa hakika, karibuni nilipata “sifa” ya kujiunga na chuo cha jeshi. Kwenye kitengo changu baada ya kuhitimu, nilitumwa kufanya kazi kama mpishi kwa kuwa sikuwa na pesa za kununua zawadi. Nilijua vizuri kwamba “Viongozi hawafanyi mambo kuwa magumu kwa wale wanaobeba zawadi" "Mtu hafanikishi chochote bila kubembeleza na kujipendekeza” Ikiwa nilitaka kufanikiwa, ningelazimika kufanya juu chini ili kupata pesa za kununua zawadi, vinginevyo singefanikiwa bila kujali nilikuwa stadi jinsi gani. Nilitaka kufaulu, kwa hiyo nilifanya kila nililoweza kupata pesa, na nilijipendekeza kwa wakuu wangu na kuwapa vitu nilivyojua kuwa walivipenda. Nilijua kuwa kile nilichokuwa nikifanya kilikuwa haramu, na niliogopa kukamatwa na kupelekwa gerezani. Nilijawa na wasiwasi moyoni wakati wote, lakini wazo la kuwa afisa lilinifanya niendelee. Baada ya kitambo kidogo, nilifanywa kuwa kamanda wa batalioni hatimaye. Kila niliporudi nyumbani, wanakijiji walikusanyika karibu yangu, wakinisifu mno na kujipendekeza. Hii ilizidisha kiburi changu sana, huku malengo na tamaa zangu pia zikiongezeka. Kama wasemavyo: “Kuwa na madaraka rasmi ni kwa ajili ya chakula na nguo nzuri" "Tumia nguvu wakati unayo, kwa sababu itowekapo, huwezi kuitumia” Nilianza kufurahia faida za kuwa afisa, nikipata tu chochote nilichotaka bila gharama. Yeyote ambaye alihitaji kitu fulani kutoka kwangu alilazimika kuninunulia chakula au kunipa zawadi. Nilitumia hata wadhifa wangu kama mpendwa wa kamanda na wa afisa wa chama kuwafanya wasaidizi wanipe hiki au kile. Niliacha kuwa mwana wa mkulima wa kawaida na kuwa mtu mlafi, mjanja na mdanganyifu.

Sikutenda kama mwonevu pekee katika kazi yangu bali pia nilimtendea mke wangu vibaya kule nyumbani. Nilimshutumu kwa kutokuwa mwaminifu katika ndoa bila sababu, nikizidisha ugomvi kati yetu. Mwishowe, alikuwa amechoshwa na akaniambia kuwa alitaka nimpe talaka. Familia yangu yenye furaha ilikuwa karibu kuvunjika, na mtoto wetu angeteseka pia. Nilihisi vibaya sana na nikarejelea mara kwa mara maisha yangu ya kale: Nilikuwa nimeazimia kujitokeza tangu nilipokuwa mtoto, na kuwa bora kuliko wengine. Mimi na mke wangu tulikuwa na kazi nzuri, na tuliishi maisha ya starehe. Kila mtu alitustahi, kwa hiyo nilipaswa kuwa na furaha na kuridhika. Kwa nini bado nilihisi mtupu sana na kuishi kwa maumivu kama haya? Je, haya ndiyo maisha niliyotaka? Tunapaswa kuishije, kwa kweli? Nilihisi kuchanganyikiwa na kupotea, lakini sikuweza kupata majibu yoyote. Baadaye mke wangu alikubali injili ya ufalme wa Mwenyezi Mungu na alikusanyika na kushiriki pamoja na ndugu wakati wote. Baada ya muda mfupi alikua mtu mwenye kusaidia sana. Hakubishana nami tena, na akaacha kuzungumza juu ya talaka. Nilipoona mabadiliko ya mke wangu, nilifikiri imani katika Mungu hakika ni nzuri. Pia nilipata imani katika Mwenyezi Mungu kwa kusoma maneno Yake.

Nilianza kuishi maisha ya kanisa, na nikagundua kuwa Kanisa la Mwenyezi Mungu lilikuwa tofauti kabisa na ulimwengu. Ndugu husoma maneno ya Mungu na hufanya ushirika juu ya ukweli. Wao hutafuta kutenda kulingana na maneno ya Mungu na ukweli, kuwa waaminifu na wanyofu, na kuwa wenye mioyo safi. Nilihisi kana kwamba nilikuwa nimekuja mahali pa utakatifu, na nilihisi uhuru na uachiliwaji ambao sikuwahi kuhisi hapo awali. Kwa kuhudhuria mikutano na kusoma maneno ya Mungu, nilijifunza kuwa Mungu ni mtakatifu na mwenye haki, na kwamba Anachukia uchafu na upotovu wa binadamu zaidi ya yote. Nilikuwa nimeingia katika tabia nyingi mbaya katika jeshi na iwapo singekutubu, nilijua Mungu angenidharau na kuniondoa. Kisha nikasoma maneno haya ya Mungu: “Kwa sababu ya kuzaliwa katika nchi ya uchafu vile, mwanadamu ameangamizwa kabisa na jamii, amekuwa akishawishiwa na maadili ya kikabaila, na amefundisha katika ‘taasisi za elimu ya juu.’ Fikra zilizo nyuma kimaendeleo, maadili potovu, mtazamo mbaya juu ya maisha, falsafa za kudharauliwa za kuishi, uwepo usio na thamani, na hali potovu za maisha na desturi—mambo yote haya yameuingilia moyo wa mwanadamu, na kudhoofisha na kushambuliwa dhamiri yake pakubwa. Matokeo yake, mwanadamu kamwe yuko mbali kutoka kwa Mungu, na kila mara anampinga. Tabia ya mwanadamu inakuwa matata zaidi kila siku, na hakuna hata mmoja ambaye kwa hiari yake atatoa chochote kwa ajili ya Mungu, hakuna hata mmoja ambaye kwa hiari atamtii Mungu, wala, zaidi ya hayo, mwanadamu mmoja ambaye kwa hiari yake atatafuta uso wa Mungu. Badala yake, chini ya umiliki wa shetani, mwanadamu hafanyi kitu ila kukimbiza anasa, kujitoa mwenyewe kwa upotovu wa mwili katika nchi ya matope(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kuwa na Tabia Isiyobadilika Ni Kuwa katika Uadui na Mungu). Kusoma maneno haya kulinionyesha ni kwa nini nilikuwa nimepotoka sana. Nilifikiri juu ya wakati nilipokuwa kwenye jeshi. Nilikuwa nimefuata sheria za mila na desturi za ulimwengu ili kufanikiwa, nikifanya mambo mengi mabaya na kupata faida kwa njia ya magendo. Nilikuwa nimepotoshwa na kukengeushwa sana, nikiishi katika dhambi bila aibu. Maneno ya Mungu yalinionyesha tofauti kati ya mema na mabaya, na yalinifanya nione chanzo cha upotovu na mkengeuko wangu. Imetukia kuwa Shetani ndiye chanzo cha yote hayo. Shetani, mfalme wa pepo, ametumia kila aina ya elimu na ushawishi kuipotosha jamii yetu na kuifanya iwe pipa kubwa la dhambi. Watu wenye mamlaka wameenea pote, wakiwapuuza kabisa watu wa kawaida, huku watu wa kawaida na waaminifu wakionewa tu na hawafaulu maishani. Jamii yetu imejaa dhana za uwongo na uzushi, “Mbingu huwaangamiza wale ambao hawajiwakilishi” “Wenye ubongo hutawala wenye misulo,” “Kujipatia sifa na kuleta heshima kwa mababu zake” “Mtu hujitahidi kwenda juu; maji hububujika kwenda chini” “Viongozi hawafanyi mambo kuwa magumu kwa wale wanaobeba zawadi” “Mtu hafanikishi chochote bila kubembeleza na kujipendekeza” “Kuwa na madaraka rasmi ni kwa ajili ya chakula na nguo nzuri” “Tumia nguvu wakati unayo, kwa sababu itowekapo, huwezi kuitumia” Kutawaliwa na vitu hivi na shinikizo iliyokuwa pote vilinifanya nipoteze njia yangu bila hata kujua. Nilikuwa nimefanya juu chini ili niwe afisa, nikitumia mamlaka yangu vibaya kwa manufaa yangu binafsi. Nilikuwa mtu mpotovu kabisa, mwenye shauku ya kulangua. Nilijutia sana matendo yangu maovu. Shukrani kwa Mungu kwa kuniokoa, kwa kuwa Alinipa nafasi ya kuanza tena. Vinginevyo, ningelaaniwa na kuadhibiwa kwa sababu ya tabia yangu. Nilihisi mwenye shukrani sana kwa Mungu, niliamua kubadili njia zangu, kuondoka katika jeshi, na kutafuta kazi mpya. Lakini mkuu wangu aliendelea kujaribu kunifanya nisalie, akisema kwamba angenipandisha cheo niwe naibu kamanda wa rejimenti. Nilisita, nikifikiri, “Naibu wa kamanda wa rejimenti? Huko kutakuwa kutimia kwa ndoto!” Kwa muda mfupi nilijitahidi kuacha cheo hicho, na sikujua la kufanya, kwa hiyo nilikuja mbele za Mungu kuomba na kutafuta. Kisha nikasoma maneno haya ya Mungu: “Kama wewe ni wa daraja la juu, wa sifa ya heshima, aliyemiliki maarifa mengi, mmiliki wa mali nyingi, na kuungwa mkono na watu wengi, lakini mambo haya hayakuzuii kuja mbele za Mungu kuukubali wito Wake na agizo Lake, kufanya kile Mungu anachokuambia ufanye, basi yote unayoyafanya yatakuwa yenye umuhimu zaidi duniani na yenye haki zaidi ya binadamu. Ukiukataa wito wa Mungu kwa sababu ya hadhi yako na malengo yako mwenyewe, yote utakayoyafanya yatalaaniwa na hata kudharauliwa na Mungu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kiambatisho 2: Mungu Anaongoza Majaliwa ya Wanadamu Wote). “Watu huja duniani na ni nadra kupatana na Mimi, na pia ni nadra kuwa na fursa ya kutafuta na kupata ukweli. Kwa nini msithamini wakati huu mzuri kama njia sahihi ya kutafuta katika maisha haya? Na ni kwa nini daima nyinyi hupuuza sana ukweli na haki? Kwa nini daima nyinyi hujikanyaga na kujiangamiza kwa ajili ya ule udhalimu na uchafu ambao huchezea watu?(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maneno kwa Vijana na kwa Wazee). Kila neno lililenga dhamiri yangu. Niliamshwa. “Naam,” niliwaza. “Bahati yangu nzuri ya kukutana na Mungu mwenye mwili, Ambaye amekuja duniani kuonyesha ukweli na kumwokoa mwanadamu, na kuwa na nafasi ya kufuatilia ukweli na kujitolea kwa ajili ya Mungu ni ukuzwaji na neema kubwa ya Mungu!” Ni nini kinachoweza kuwa cha maana zaidi kuliko kujitumia kwa ajili ya Muumba? Bila kujali ningepanda cheo cha juu kiasi gani, je, ningekuwa na furaha kweli? Watu wengi wenye mamlaka hufanya kama wanavyopenda na kufanya kila aina ya uovu lakini wote hupata kile wanachostahili mwishowe. Na viongozi wengi sana wangazi za juu wamekuwa matajiri na wenye kusifika kwa muda, lakini pindi wanapoteza pambano la mamlaka, wengine huishia gerezani bila chochote, na wengine hujiua … Vitu vya aina hii hufanyika kila wakati. Kwa mintarafu yangu, nilikuwa nikipanda cheo kwa bidii, lakini nilianza tu kuwa mwenye majivuno, mbinafsi na mdanganyifu sana! Sasa, Mungu amenipa ukweli mwingi na amenionyesha njia sahihi maishani. Ninawezaje kuendelea kuishi kama zamani? Nilikuwa nimeumizwa na kudanganywa na Shetani kwa muda mwingi wa maisha yangu hadi sikufanana na mwanadamu hata kidogo. Nilitaka kuishi kwa namna tofauti kuanzia wakati huo na kuendelea, kumfuata Mungu, kutenda ukweli, na kutenda kulingana na maneno ya Mungu. Kwa hivyo niliamua kubadilisha kazi na kuondoa uhusiano wote na jeshi. Lakini kwa kuwa Shetani alikuwa amenipotosha sana, sumu yake ya “Kujitofautisha na kuleta heshima kwa mababu zake” ilikuwa maisha yangu. Kanisani, nilikuwa daima nashindania cheo, na ni ufunuo na hukumu ya Mungu pekee ndiyo iliyorekebisha ufuatiliaji wangu.

Baada ya kufanya wajibu wangu kanisani kwa muda mfupi, niliona kulikuwa na kiongozi mdogo sana wa kanisa na mwingine ambaye tulikuwa marafikiri hapo awali. Nilikuwa na wasiwasi, nikifikiri, “Nyote mlikuwa chini yangu ulimwenguni, lakini hapa kanisani ninyi ni wakubwa wangu. Naweza kuwa kiongozi bora kuwaliko!” Nilianza kujaribu kupata cheo hicho kwa udi na ambari. Kwanza, nilifanya mpango: Niliamka saa 11 asubuhi kila siku kusoma maneno ya Mungu, kisha nikasikiliza mahubiri kwa saa mbili, na kujifunza nyimbo tatu za maneno ya Mungu kila wiki. nilijihusisha zaidi katika wajibu wangu, na kuongoza katika jambo lolote nilloweza kufanya kanisani, bila kujali lilikuwa gumu au la kuchosha kiasi gani. Katika mikusanyiko, nilizungumza juu ya uzoefu wangu katika jeshi, nilishaua uwezo wangu, na kuonyesha dharau kwenye ushirika wa viongozi wa kanisa. Wakati mwingine, nilishushia hadhi fikira na matendo yao kana kwamba ningeweza kufanya kazi nzuri zaidi. Hivi ndivyo nilivyoishi ndani ya mapambano ya umaarufu na hadhi, kila wakati nikitumai kuwa kiongozi wa kanisa. Wakati mmoja, niligundua kiongozi mmoja hakuwa ameshughulikia jambo fulani vizuri. Nilimkaripia kwa kutokuwa na uwezo wa kushughulikia mambo, na nikadokeza kwamba anapaswa kujiuzulu. Nilitumai kuteuliwa kuwa kiongozi katika uchaguzi uliofuata. Ndugu walipogundua tukio hilo, walichunguza tabia yangu, wakisema nilikuwa mdanganyifu, mwenye tamaa, na nilitaka kulidhibiti kanisa. Niliachishwa wajibu wangu kama kiongozi wa kikundi. Tukio hili liliniudhi sana, na nikafikiri, “Nilikuwa kamanda wa batalioni mwenye heshima, lakini sasa siwezi hata kuwa kiongozi wa kikundi kanisani.” Baada ya miezi kadhaa, sikukubaliana na hayo, na sikuweza kuvumilia kuwaona ndugu zangu. Nilinyamaza mikutanoni. Nafsi yangu ilianza kufififa na sikuweza kumhisi Mungu tena. Ni wakati huo tu ndipo nilianza kuhofia, kwa hiyo nilifanya hima kuomba na kumtaka Mungu aniongoze kutoka kwenye giza hili.

Baadaye nilisoma maneno haya ya Mungu: “Katika kutafuta kwenu, mna dhana, matumaini, na siku za baadaye nyingi sana za kibinafsi. Kazi ya sasa ni ili kushughulikia tamaa yenu ya hadhi na tamaa zenu badhirifu. Matumaini, hadhi, na dhana yote ni mifano bora kabisa ya tabia ya kishetani. … Sasa nyinyi ni wafuasi, na mmepata ufahamu fulani wa hatua hii ya kazi. Hata hivyo, bado hamjaweka kando tamaa yenu ya hadhi. Wakati hadhi yenu iko juu mnatafuta vizuri, lakini wakati hadhi yenu iko chini hamtafuti tena. Baraka za hadhi daima ziko katika fikira zenu. … Kadiri unavyotafuta zaidi kwa njia hii, ndivyo utakavyovuna kidogo zaidi. Kadiri ilivyo kubwa zaidi tamaa ya mtu ya hadhi, ndivyo itabidi washughulikiwe kwa uzito zaidi na ndivyo watakavyozalimika kupitia usafishaji mkubwa. Watu kama hao hawana thamani kabisa! Lazima wshughulikiwe na wahukumiwe vya kutosha ili waachane na mambo haya kabisa. Mkifuatilia kwa njia hii mpaka mwisho, hamtavuna chochote. Wale ambao hawafuatilii uzima hawawezi kubadilishwa, na wale ambao hawana kiu ya ukweli hawawezi kupata ukweli. Hulengi kufuatilia mabadiliko ya kibinafsi na uingiaji, lakini badala yake unalenga tamaa badhirifu na vitu vinavyozuia upendo wako kwa Mungu na kukuzuia kumkaribia Yeye. Je, vitu hivyo vinaweza kukubadili? Je, vinaweza kukuleta katika ufalme?(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mbona Huna Hiari ya Kuwa Foili?). Maneno ya Mungu yaliuchoma moyo wangu na nilihisi aibu sana. Nilikuwa nikipigania cheo, kisha nikafunuliwa na kushughulikiwa na ndugu, na kuachishwa wajibu wangu. Si kile nilichotaka, lakini haikuwa kwa sababu mtu fulani alikuwa na kisasi nami. Badala yake, ilikuwa hukumu ya haki na wokovu wa Mungu wa wakati ufaao. Kazi ya Mungu katika siku za mwisho ni ya kubadilisha fikira na mawazo yetu ya zamani, kutuokoa kutoka kwa ushawishi wa Shetani, ili tuweze kupata ukweli na uzima kutoka kwa Mungu, na kuishi katika nuru. Sikuwa nikitembea kwenye njia sahihi, wala sikuwa nimelenga kufuatilia ukweli, lakini nilifuatilia cheo na sifa. Nilikuwa nimetumia hila na nikatumia njia za hila kupata cheo. Je, si hiyo ilikuwa kinyume kabisa na mapenzi ya Mungu ya kuwaokoa wanadamu? Kuendelea kwa njia hiyo kungemaanisha kuwa singepata ukweli na ningeondolewa. Ili kunizuia nisipotoke na kunirudisha kwenye njia, Mungu alinipogoa na kunishughulikia kupitia kwa ndugu, Akifunua malengo na tamaa zangu, na kuondoa cheo changu. ili nitafakari kujihusu na kubadili njia zangu. Niliona kwamba Mungu kwa kweli huona ndani kabisa ya mioyo yetu. Pia nilikuja kupata ufahamu kiasi wa kweli kuhusu haki, utakatifu, nguvu na hekima ya Mungu. Sikuwa tena hasi au mwenye huzuni juu ya kupoteza cheo changu, lakini badala yake nilitaka kufuatilia ukweli na kutii utaratibu na mipango ya Mungu.

Miezi sita baadaye, nilienda kuishi maisha ya kanisa katika kanisa lingine, ambapo walikuwa karibu kuchagua viongozi. Nilifurahi nilipopata habari kwamba kule hakukuwa mtu ambaye alikuwa amewamini Mungu kwa muda mrefu kama mimi, kwa hiyo nilifikiri kuwa ningekuwa na nafasi. Katika uzoefu wa maisha na miaka ya imani, niliwapiku. Ninapaswa bila shaka kuchaguliwa kuwa kiongozi wa kanisa, nilidhani. Nilipokuwa tu nikijiandaa kujionesha vizuri, dada fulani kutoka kanisa langu la zamani alikimbilia katika kanisa hili kwa kuwa alikuwa akisakwa na CCP. Nilifikiri, “Anajua jinsi nilivyokuwa nikishindania cheo kwenye kanisa langu la zamani. Akiniona nikishindania kuwa kiongozi wa kanisa tena, je, atafichua tabia yangu ya zamani yenye kashfa? Sifa yangu itaathirika sana akifanya hivyo.” Kwa kuwa sikuwa na chaguo, niliacha mipango yangu na kuhakiki hali hiyo: “Kwanza nitakuwa kiongozi wa kikundi na kisha nitapanda ngazi kuanzia hapo.” Hata hivyo, kwa mshangao wangu, sikuchaguliwa hata kuwa kiongozi wa kikundi. Kanisa halikuwa na watu wa kutosha wa kufanya wajibu mwingine wa kawaida, kwa hiyo viongozi wa kanisa waliuliza ikiwa nilitaka kusaidia. Nikiogopa kuonekana mwasi, nilikubali shingo upande. Nilikuwa nimekuwa kamanda wa batalioni mwenye heshima lakini nilikuwa nikifanya wajibu wa chini sana. Nilihisi jambo hilo halikuwa sawa kwangu. Muda si muda, polisi walianza kuvizia mahali tulipokusanyikia, kwa hivyo hatukuweza kukusanyika pale tena. Kiongozi wa kanisa aliniweka kwenye kikundi kingine ili nikusanyike na ndugu waliofanya wajibu wa mwenyeji. Jambo hili lilikuwa zito sana kwangu. Sikuwa nikifanya tu wajibu duni, lakini pia sasa ilibidi nikusanyike na ndugu waliofanya wajibu wa wenyeji. Nilihisi kama kwamba hili lilinishushia hadhi kabisa. Niliwezaje kushuka sana vile? Ikiwa mambo yangeendelea hivyo, ningekuwa na matarajio ya aina gani? Nilizidi kufadhaika, na yote niliyoweza kufanya ni kumwomba Mungu upesi, nikimwomba Anipe nuru na kunielekeza.

Kisha, nikasoma maneno haya ya Mungu: “Kwa miaka mingi, mawazo ambayo watu wametegemea kwa ajili ya kuendelea kuishi kwao yamekuwa yakiharibu mioyo yao hadi kiwango ambapo wamekuwa wadanganyifu, waoga, na wenye kustahili dharau. Hawakosi tu ushupavu na uamuzi, lakini pia wamekuwa walafi, wenye kiburi, na wa kudhamiria. Kabisa wanakosa uamuzi wowote upitao sana ubinafsi, na hata zaidi, hawana ujasiri hata kidogo wa kuondoa shutuma za ushawishi huu wa giza. Fikira na maisha ya watu ni mabovu sana kiasi kwamba mitazamo yao juu ya kuamini katika Mungu bado ni miovu kwa namna isiyovumilika, na hata watu wanaponena kuhusu mitazamo yao juu ya imani katika Mungu haivumiliki kabisa kusikia. Watu wote ni waoga, wasiojimudu, wenye kustahili dharau, na dhaifu. Hawahisi maudhi kwa nguvu za giza, na hawahisi upendo kwa nuru na ukweli; badala yake, wanafanya kila wanaloweza kuvifukuza. Je, si fikira na mitazamo yenu ya sasa iko hivi tu? ‘Kwa kuwa ninaamini katika Mungu ninapaswa tu kumiminiwa baraka na inapaswa kuhakikishwa kwamba hadhi yangu kamwe haitelezi na kwamba inabaki kuwa juu kuliko ile ya wasioamini.’ Hamjakuwa mkihodhi mtazamo wa aina hiyo ndani yenu kwa mwaka mmoja au miaka miwili tu, lakini kwa miaka mingi. Kufikiria kwenu kwa kibiashara kumekua sana. Ingawa mmewasili kwenye hatua hii leo, bado hamjaacha hadhi lakini mnapambana bila kukoma kuuliza kuihusu, na mnaichunguza kila siku, kwa hofu kubwa kwamba siku moja hadhi yenu itapotea na jina lenu litaharibiwa. Watu hawajawahi kuweka kando tamaa yao ya starehe(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mbona Huna Hiari ya Kuwa Foili?). “Unapoitembea njia ya leo, ufuatiliaji unaofaa zaidi ni wa aina gani? Katika ufuatiliaji wako, unapaswa kujiona kama mtu wa aina gani? Unafaa kujua jinsi unavyopaswa kukabili yote yanayokukumba leo, yawe majaribu ama taabu, ama kuadibu na laana isiyo ya huruma. Unapaswa kuyazingatia kwa uangalifu katika hali zote(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Wale Wasiojifunza na Wanaosalia Wajinga: Je, Wao Sio Wanyama?). Nilipokuwa nikitafakari maneno ya Mungu, nilitafakari kujihusu. “Naam,” nilifikiri. “Je, napaswa kujiona kama mtu wa aina gani, katika ufuatiliaji wangu?” Siku zote nilikuwa nikijifikiria kama kamanda wa batalioni, mtu mwenye cheo. Ni wajibu wenye cheo fulani pekee ndio ulinifaa, na watu wenye hadhi ya juu pekee ndio walistahili kukusanyika nami. Niliwadharau ndugu ambao walifanya wajibu wa maandalizi, nikifikiri kwamba kuwa nao kulionyesha kwamba sikuwa na cheo. Bila hadhi, nilianza kuwa hasi na mwenye upinzani, na hata nilihisi kuwa maisha hayakuwa na maana. Hadhi, sifa na faida vilikuwa vimekanganya ubongo wangu na nikapoteza ubinadamu wangu. Nilikuwa mtu mwenye kustahili dharau na mbaya sana! Mtu kama mimi angestahili vipi kuwa kiongozi wa kanisa? Kanisa si kama jamii. Kanisani, ukweli hutawala. Kiongozi lazima awe mwenye ubinadamu mzuri na afuatilie ukweli. Lakini nilichofanya ni kufuatilia hadhi na kushindania kuwa kiongozi. Niliwezaje kuwa mtu asiye na busara na aibu?

Baadaye nilisoma maneno haya ya Mungu: “Ninaamua hatima ya kila mtu si kwa kuzingatia umri, ukubwa, kiwango cha mateso, sembuse kiwango ambacho kwacho anataka huruma, bali kulingana na ikiwa anao ukweli. Hakuna chaguo lingine ila hili. Sharti mtambue kwamba wale wote ambao hawafuati mapenzi ya Mungu wataadhibiwa pia. Huu ni ukweli usiobadilika(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Tayarisha Matendo Mema ya Kutosha kwa ajili ya Hatima Yako). Nilielewa kutoka kwa maneno ya Mungu kuwa Yeye haamui hatima yetu kulingana na hadhi yetu au kulingana na kiasi ambacho tunafanya kazi. Kilicho muhimu ni ikiwa tumepata ukweli, na ikiwa tunamtii Mungu. Niliona kwamba tabia ya Mungu ni ya haki kwa wote, na bila kujali ni wajibu upi tunaofanya, lazima tufuatilie ukweli siku zote. Mtu akiwa na ukweli, bado anaweza kuokolewa hata asipokuwa na hadhi yoyote. Lakini bila kufuatilia ukweli, hakuna anayeweza kuokolewa bila kujali hadhi yake ni ya juu kiasi gani. Nilifikiri jinsi nilivyokuwa mpumbavu kwa kufuatilia hadhi sana. Nilikuwa nimewachukia wale maafisa wapotovu wa jeshi, lakini nilipokuwa nikipanda vyeo, mimi mwenyewe nilizidi kuwa mbaya zaidi, mwishowe nikawa afisa mpotovu kama tu wao. Watu wengine wenye mamlaka wanaweza kufanya wajibu wao kwa uaminifu sana kabla ya kuwa na hadhi, lakini mara tu wanapopata mamlaka wanaanza kuyatumia vibaya, na dhambi zao huongezeka zaidi na zaidi. Nilifikiri juu ya wapinga Kristo ambao walikuwa wamefukuzwa kanisani. Wakati ambapo hawakuwa na hadhi, walionekana kutofanya chochote kiovu, lakini mara tu hilo lilipobadilika, walianza kuwakandamiza na kuwadhalilisha wengine kwa lengo la kujionyesha kuwa woa ni bora, wakisema na kufanya mambo ili kulinda nyadhifa zao, wakitenda maovu, na kuvuruga kazi ya nyumba ya Mungu. Hii ilinionyesha kuwa bila ukweli, sisi daima hutegemea tabia zetu potovu. Mara tunapopata mamlaka na hadhi, tunakuwa wapotovu na kufanya maovu, hiyo mwishowe inamaanisha adhabu! Nilipokuwa nikijitahidi na kupania kupanda ngazi katika jeshi miaka hiyo yote, nilijawa na tabia ya kishetani. Nilikuwa mwenye kiburi, mdanganyifu, mbinafsi na mlafi kabisa. Ikiwa ningejikuta katika wadhifa wa juu, tamaa yangu ya makuu yangekua kwa kasi, kama tu nilipotumia vibaya mamlaka yangu kama afisa wa jeshi. Ningeishia kutenda maovu, kuikosea tabia ya Mungu, na kuadhibiwa. Nilipofikiria mambo haya, nilihisi mwenye hofu na mwenye shukurani. Mungu alikuwa amesababisha vipingamizi na ushinde tena na tena, Akizuia malengo na tamaa zangu zisitimizwe. Huo ulikuwa wokovu na ulinzi Wake kwangu! Shukrani kwa Mungu kwa nuru Yake iliyonifanya nione kiini na matokeo ya kufuatilia umaarufu na hadhi. Aidha, niliona mwishowe jinsi ambavyo kufuatilia ukweli kulivyo muhimu.

Tangu wakati huo, nimelenga kufuatilia ukweli ili kutatua upotovu wangu. Bila kujali kanisa lilinipa wajibu gani, cheo hakikuwa tena lengo langu. Badala yake, nililenga kutafuta kanuni za ukweli na kufanya wajibu wangu vizuri. Niliweza kuhisi uwepo na mwongozo wa Mungu nilipoanza kutenda kwa njia hii, na nilihisi amani na furaha isiyoelezeka Baada ya muda kiasi, niligundua kuwa nilikuwa mnyenyekevu zaidi nilipokuwa na watu wengine, na sikujishaua tena kwa kuwa ofisa wa jeshi. Ndugu walipoonyesha makosa yangu, nilimwomba Mungu kwa uzingatifu na kunyenyekea, kisha nikatafakari na kujaribu kujijua. Niliweza kupatana na wengine kwa usawa, na sikufikiri tena kuwa nilikuwa bora zaidi. Muda si muda, maoni yangu juu ya ufuatiliaji yalibadilika. Hadhi, umaarufu na faida vilikuwa vimefifia sana kwangu. Havikunizuia tena. Nilipowaona watu wakiwa viongozi wa kanisa ambao walikuwa na imani kwa muda mfupi kuniliko, bado nilihisi wivu kidogo, lakini kwa kuomba na kutafuta ukweli, niliweza kuacha kuhisi hivyo haraka. Sasa mimi hufanya wajibu wangu nyumbani pamoja na mke wangu. Huenda ikawa si kitu chochote cha kujivunia, lakini nimeridhika kabisa. Katika maisha yetu, sisi hujizoeza kuruhusu maneno ya Mungu kutawala, Na sisi humsikiza mtu yeyote azungumzaye kwa usahihi na anayefuata ukweli. Kwa kweli nimepata uozefu kwamba Mwenyezi Mungu amenibadilisha. Aliokoa ndoa yangu, familia yangu, na Aliniokoa, mimi mtu mpotovu sana. Nilikuwa mwenye kiburi, mdanganyifu, mwenye tamaa ya hadhi na faida, mwovu na mlafi sana. Bila wokovu wa Mungu, singeweza kamwe kutembea kwenye njia sahihi maishani. Ningekuwa tu mpotovu na mwovu zaidi, na mwishowe ningetenda maovu mengi sana kiasi kwamba Mungu angenilaani na kuniadhibu. Kwa kweli nimehisi wokovu na upendo wa Mungu kupitia matukio haya. Kuwa na uwezo wa kutenda ukweli kiasi na kuishi kwa kudhihirisha sehemu ya mfano wa binadamu ni kwa usaidizi tu wa hukumu ya Mungu na kuadibu Kwake! Shukrani ziwe kwa Mungu!

Iliyotangulia: 28. Jinsi ya Kuuchukulia Wajibu Wako

Inayofuata: 31. Kushikilia Wajibu Wangu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

1. Nimebahatika Kumhudumia Mungu

Na Gensui, Korea ya KusiniMwenyezi Mungu anasema, “Ni kupitia nini ndiyo ukamilishaji wa Mungu kwa mwanadamu hutimizwa? Kupitia tabia Yake...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp