Sura ya 57

Je, umechunguza kila fikira na mawazo yako, na kila tendo lako? Uko wazi kuhusu gani kati ya haya yanalingana na mapenzi Yangu na gani hayalingani? Huna uwezo wa kutambua haya! Mbona hujaja mbele Yangu? Je, ni kwa sababu Sitakuambia, au ni kwa ajili ya sababu nyingine? Unapaswa kujua hili! Kujua kwamba wale walio wazembe hawawezi kuyaelewa mapenzi Yangu kabisa au kupokea mwangaza na ufunuo mkuu.

Je, umegundua sababu kanisa haliwezi kupata lishe na linakosa ushirika wa kweli? Unajua ni vipengele vigapi ambavyo vimesababisha haya vinahusiana na wewe? Nilikuagiza kutoa uhai na kuachilia sauti Yangu. Umefanya haya? Unaweza kuwajibikia kuchelewesha maendeleo ya ndugu zako katika maisha? Unapokabiliwa na masuala umekuwa mwenye wasiwasi badala ya kuwa mtulivu na makini. Kweli wewe ni mjinga! Sauti Yangu inapaswa kuachiliwa kwa watakatifu. Usizuie kazi ya Roho Mtakatifu na usinicheleweshee muda; hakuna kati ya hayo inayofaidi yeyote. Nataka ujitolee kikamilifu kwa ajili Yangu, kimwili na kiakili, ili kwamba kila wazo na fikira yako iwe kwa ajili Yangu, ili uweze kushiriki mawazo Yangu na wasiwasi Wangu, na kwamba kila kitu unachofanya kitakuwa kwa ajili ya ufalme wa leo na usimamizi Wangu, na si kwa ajili yako. Hilo pekee ndilo litauridhisha moyo Wangu.

Chochote ambacho Nimefanya hakikosi ithibati. Mbona hujaniiga? Mbona hujatafuta ithibati kwa ajili ya kile unachofanya? Unataka Niseme nini zaidi? Nilikuchukua kwa mkono kukufundisha, lakini umeshindwa kujifunza—wewe ni mjinga sana! Unataka kuanza tena? Usivunjike moyo. Ni lazima ujikaze tena na kujitoa kikamilifu kwa niaba ya matumaini yaliyoshirikiwa na matakwa yaliyoshirikiwa ya watakatifu. Kumbuka maneno hayo: “Kwa wale wanaotumia rasilmali kwa dhati kwa ajili Yangu, hakika Nitakubariki sana.”

Chochote unachofanya lazima ukifanye kwa mpango, sio ovyoovyo. Kweli unathubutu kusema unajua hali ya watakatifu kama unavyojua kiganja cha mkono wako mwenyewe? Hilo linaonyesha unakosa hekima, kwamba hujachukulia suala hili kwa uzito hata kidogo, na hujatumia muda wowote kwalo. Ikiwa kweli ungeweza kutumia muda wako wote kwa hilo, ona vile hali yako ya ndani ingekuwa. Hutafuti kutoa juhudi za nafsi ila unatafuta tu sababu zisizopendelea na huonyeshi fikira hata kidogo kwa mapenzi Yangu—hilo limenihuzunisha sana! Usiendelee hivi! Inaweza kuwa kwamba hukubali baraka ambazo Nimekupa?

Ee, Mungu! Mwana Wako ni mdeni Wako. Sijachukulia kazi Yako kwa uzito, au kufikiria mapenzi Yako, wala sijakuwa mwaminifu kwa ushawishi Wako. Mwana Wako anataka kugeuza haya yote. Naomba Usiniache, na naomba Uendelee kutekeleza kazi yako kunipitia. Ee, Mungu! Usimwache mwana Wako yeye peke yake, ila andamana nami kila wakati. Ee, Mungu! Mwana Wako anajua Unanipenda, lakini siwezi kuyaelewa mapenzi Yako, sijui jinsi ya kufikiria mzigo Wako, na sijui jinsi ya kutimiza kile ambacho Umeniaminia, sembuse kujua jinsi ya kuliongoza kanisa. Unajua kwamba mimi ni mwenye huzuni na majonzi juu ya hili. Ee, Mungu! Tafadhali Niongoze nyakati zote. Ni sasa tu ninapohisi jinsi ninavyokosa, nahisi vyema sana! Siwezi kulieleza kabisa. Acha mkono Wako wenye enzi uonyeshe neema kwa mwana Wako, msaidie mwana Wako nyakati zote, na mfanye mwana Wako aweze kujihusudu kabisa mbele Yako, asifanye uamuzi wake tena, asiwe na fikira na mawazo yake tena. Ee, Mungu! Unajua kwamba mwana Wako anataka kufanya kila kitu kwa ajili Yako kabisa, kwa ajili ya ufalme leo kabisa. Unajua ninachofikiri na ninachofanya wakati huu. Ee, Mungu! Nichunguze Wewe mwenyewe. Naomba tu kwamba Utembee nami na kubaki nami katika maisha haya nyakati zote, ili nguvu Yako iandamane na matendo yangu.

Iliyotangulia: Sura ya 56

Inayofuata: Sura ya 58

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp